Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hali ya usalama nchini; kwa sasa hali ya usalama wa nchi yetu siyo salama sana, kumekuwa na matukio ambayo hatukuyazoea nchini kwetu, ambayo ni watu kupotea, watu kutekwa na kuuawa. Wananchi wameingia taharuki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kuhoji uraia wa watu wanapoipinga Serikali, jambo hili linaleta sintofahamu kabisa haijawahi kutokea toka tawala mbalimbali zilizopita, jambo hili halikubaliki kwani linajenga hofu miongoni mwa Watanzania ambao wanatumia haki yao ya Kikatiba kutoa maoni yao kulingana na mwenendo wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wasiojulikana jambo hili limekuwa kama kichaka cha wahalifu kujificha kwani kuna matukio yamejitokeza hivi karibuni ambayo wahusika hawajatambulika na ndiyo wanapewa majina hayo ya watu wasiojulikana, ni vema Wizara ya Mambo ya Ndani wakatueleza hawa ni watu gani, wako wapi na wanafadhiliwa na nani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa vituo vya Polisi katika Mkoa wa Rukwa; kuna ujenzi wa vituo vya Polisi katika Jimbo la Kwela, Wilaya ya Sumbawanga Vijijini. Kama Mbunge nimetembelea vituo hivyo, Serikali nayo itimize wajibu wake kwani wananchi wamechanga mpaka lenta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Polisi kubambikizia watu kesi ni jambo ambalo linaondoa weledi kwa Jeshi la Polisi na mambo hayo yanafanywa na baadhi ya askari wasio waaminifu; ni wajibu wa Wizara kulitazama jambo hili kwa maslahi ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuondolewa kwa kanuni ambazo ni kandamizi kwa Polisi hasa wadogo wasiokuwa na nafasi zozote katika Jeshi kwani wanafukuzwa hovyo jambo ambalo linaweza kuongeza wahalifu mitaani, kwani watu hawa wanakuwa hawana kazi mtaani.