Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. IKUPA S. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nampongeza sana Mheshimiwa Dkt. John Magufuli kwa miongozo yake ambayo imepelekea nchi yetu kuendelea kuwa na amani na utulivu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri Mwigulu Nchemba na Naibu Waziri wake Mheshimiwa Masauni kwa kazi kubwa wanazozifanya na jinsi wanavyojitoa kwa ajili ya Taifa letu. Baada ya pongezi hizo nina maombi au ushauri ufuatao kuhusu masuala ya watu wenye ulemavu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja; zoezi la ukamataji mtu mwenye ulemavu unapotenda kosa sambamba na uwekwaji ndani (mahabusu). Mikataba ya Kimataifa tuliyosaini kama nchi sambamba na sheria na sera ya watu wenye ulemavu inataka kuwe na utofauti wa ukamataji wa nguvu inayotumika kati ya mtu mwenye ulemavu na asiye na ulemavu. Pia mtu mwenye ulemavu awekwe kwenye mahabusu au magereza inayoendana na ulemavu wake, miundombinu iwe rafiki kwa watu wenye ulemavu, mahabusu na magereza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili; vibali vya mikutano ya hadhara vizingatie kundi la watu wenye ulemavu. Utolewaji wa vibali vya mikutano ya hadhara uzingatie uwepo wa ama matumizi ya lugha ya alama. Mwombaji kibali aoneshe kama kunakuwa na mkalimali ama wakalimali kwenye mkutano wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuwe na utaratibu pia wa kutenga maeneo maalum ambayo yatatumika ama yatakaliwa na watu wenye ulemavu kwenye mikutano hii, hii itawafanya watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu kwenye mikutano hii tofauti na ilivyo sasa ambapo ushiriki wao ni mdogo kwa kuhofia usalama wao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu; vitambulisho vya Taifa viwe na kipengele kinachoonesha ama kumtambua mtu mwenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha.