Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ili nami niweze kuchangia kwenye Wizara hizi mbili ambazo zimewasilisha hoja zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee kabisa naomba niwapongeze na hasa nimpongeze Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuendesha Serikali yake vizuri, lakini wakisaidiana na Makamu wa Rais na Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee kabisa nitoe pongezi kwa Ndugu yangu Mheshimiwa Waziri Jafo na Naibu Mawaziri wake wawili, Kandege na Kakunda lakini na Mzee wetu Mheshimiwa Mkuchika, hongereni kwa kazi nzuri sana. Vile vile tuwape pongezi Makatibu Wakuu wao wanaowasaidia kwenye shughuli zao, Mungu awape wepesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba nitumie nafasi hii kumpongeza Mkuu wangu wa Wilaya, Kanali Gaguti ambaye ameteuliwa jana kuwa Brigedia Jenerali; amefanya kazi nzuri sana kwenye Wilaya yetu, sasa Rais na Amiri Jeshi Mkuu amempandisha hadhi na ameambiwa aweze ku-report Makao Makuu ya Jeshi. Kwa hiyo Wilaya yetu itabaki bila kuwa na Mkuu wa Wilaya lakini tunamtakia mafanikio mema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishukuru TAMISEMI kwa kazi nzuri ambayo amefanya kwenye Jimbo la Buhigwe. Kazi nyingi zimefanyika katika muda mfupi na huku Wilaya yenyewe bado ni changa. Naomba niwapongeze kwamba tunajenga Ofisi ya Mkurugenzi na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya inaendelea vizuri, kwa hiyo hiyo ni complementary yao. Ujenzi wa hospitali ya Wilaya unaendelea ambapo wametupatia milioni mia nne hamsini, wametupatia milioni mia tano na sasa wametupangia bilioni 1.5, tunawashukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa kituo ch afya milioni mia nne, nashukuru sana Mheshimiwa Jafo kwa kutupatia kituo hiki. Pia nimpongeze Mheshimiwa Kandege kwa kwenda kukikagua na kukiona na niwashukuru sana kinaendelea vizuri na wananchi wanafurahia, wanabaki wanasubiri tu watendaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunacho Kituo kingine cha Afya cha Muyama ambacho tulisaidiana na World Vision ambacho sasa nacho kimeshaimarika na kinaendelea na upasuaji. Hiyo yote ni juhudi ya Serikali, tunaomba tuwapongeze sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, gari za wagonjwa kwenye Jimbo la Buhigwe zinatosha kwa sababu kila kituo kilichopo kina gari jipya, kwa hiyo tunawashukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo miradi ya maji inayoendelea ambayo ni juhudi zenu, lazima niziseme kama Mwana CCM. Tunayo miradi ya Nyamugari inaendelea, Nzeze, Kirungu, Mbanga, Myegela, Mgela, Kasumo, Nyanga hii yote ni miradi ya maji ambayo inaendelea kwenye Jimbo langu, kwa hiyo kwa kweli kwenye maji bado tuko vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunao mradi mmoja wa Mnanila unaokwenda Mkatanga na Kata ya Mwayaya; huu ni kati ya ndugu zetu Wabelgiji ambapo kwa kweli wa mradi huu bado hauja-take off, tungeomba Ofisi ya RAS-Mkoa ambayo ndiyo link na hawa Wabelgiji ili tuweze kuendelea na mradi huu kwa sababu watu wa Manyovu na Mnanila wanauhitaji huu mradi. Vile vile tunaendelea, kwa kibali chenu, tunaendeleza kupeleka maji Kilelema na Migongo, Wakandarasi bado wanaendelea kutafutwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunasambaza maji, tumepeleka andiko kwa Mheshimiwa Waziri na kupitia Waziri wa Maji, maji ya Mji wa Buhigwe ambao utaweza kusaidia Vijiji vya Songambele, Kavomo, Mlela, Buhigwe, Bwelanka na Kibande, hilo andika tunasubiri majibu tuweze kuona kwenye bajeti ya 2018/2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa afya ningependa kuomba yafuatayo:-

Tulikuwa na mkataba wa hospitali yetu ya Heri Mission ambayo iliingia mikataba na halmashauri kwa ajili ya kusaidia akinamama, watoto na wazee, kwa sababu yale
maeneo hatukuwa na kituo cha afya, lakini kwa maelezo yao walileta mkataba wa kusitisha ili huduma hii isiendelee. Sasa wananchi wanapata adha kwa sababu hakuna hopsitali ya karibu kwa sababu hospitali ya wilaya sasa ndiyo tunajenga. Tungeomba waturudishie hii huduma, ule mkataba ambao Katibu Mkuu aliandika ili akinamama hawa waendelee kupata huduma la sivyo, tutapata shida, lakini tutakapomaliza hospitali ya Wilaya wanaweza waka-cancel mkataba huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kuishukuru Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi, tumetengewa bilioni mbili na milioni mia nne kwa ajili ya kujenga soko zuri la Kimataifa pale Mnanila. Hili ni soko ambalo litakuwa na vyumba 300 vya kuuzia bidhaa, tutakuwa na vizimba vya kuuzia bidhaa 500, kutakuwa na vyumba vya Benki, kwa hiyo ni jambo kubwa. Tunachoomba, hiki kitakuwa ni chanzo cha mapato ya halmashauri lakini pia wafanyabiashara watapata eneo la kufanyia biashara. Tunaahidi kwamba tutautendea haki mradi huu, tunahitaji, tungependa tuone fedha hizi mapema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa elimu; naomba tu pamoja na changamoto zote zilizopo kwenye Wilaya yangu ya Buhigwe; Wilaya yangu ya Buhigwe kwenye ufaulu katika nchi hii ni ya 21 katika Halmashauri 189. Kwa hiyo ningependa tu niwapongeze Walimu kwa changamoto zilizopo lakini Buhigwe sisi kwenye ufaulu katika nchi hii ni watu wa 21 kati ya 189. Kwa hiyo nawapongeza na waendelee kuchapa kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kigoma, kwa wale ambao hamna taarifa ni Mkoa wa 10 katika mikoa ya Tanzania hii. Kwa hiyo msije mkafikiri tuko nyuma sana mkafikiri kwamba watu hawafanyi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna changamoto ya maboma ya madarasa kuezekwa; tungependa kuwe na special program. Wananchi wamejitolea, tunayo maboma karibu 17 kwenye Jimbo langu sasa tungependa kupata nguvu angalau tuweze kuezeka. Ilani ya Mheshimiwa Waziri ilisema kwamba tukiweza kufikisha kwenye lenta wao wanaweza wakatusaidia kuezeka. Kwa hiyo, nalo hilo tungeomba watusaidie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa elimu tunataka kupandisha shule nne ili ziwe kidato cha tano. Shule ya Myama, shule ya Buyenzi, shule ya Mkoza, pamoja na shule ya Munzeze tungepanda nazo zipande kuwa kidato cha tano kwa sababu sasa watu wanafaulu vizuri ili waweze kupata sehemu ya kwenda kusomea elimu ya juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TARURA miundombinu. Mheshimiwa Rais JPM alikubali kwamba kwa kuwa wilaya yetu tumehamisha makao makuu, vijiji namna ya kuungana imekuwa ni tatizo; alikubali kwamba ataweza kutupasulia barabara mpya ili ziweze kuunganisha vijiji na vijiji na Sheria ya TARURA inasema kwamba wao hawawezi kupasua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunapeleka ombi na ni ahadi ya Mheshimiwa Rais; tunayo ya kutoka Kijiji cha Nyakimwe kwenda Muhinda, Munzeze kwenda Kwitanga, Rusaba kwenda Nyarubanda, Myegera kwenda Songambele,
Kilelema kwenda…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niunge mkono hoja na hiyo ndiyo ilikuwa hoja yangu ya mwisho. Nakushukuru.