Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya njema pia naendelea kuwashukuru wapiga kura wangu wa Jimbo la Tanga kwa kunichagua na nawaahidi kuwatumikia kwa utumishi na uwakilishi uliotukuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, education is the most powerful weapon which we can use to change the World (By Nelson Mandela Madiba) education is the key of life.

Mheshimiwa Mwenyekiti, semi zote hizi zimetumiwa na Wahenga wetu zikiwa na maana kubwa sana. Katika miaka ya 1970, Tanzania ilikuwa katika level moja ya kiuchumi au hata sarafu yetu ilikuwa na thamani kuliko sarafu ya nchi za Singapore, Malaysia, Indonesia, China, Vietnam na Kenya lakini leo hii 2018, nchi zote hizi zimetuacha kiuchumi na kielimu na sababu kubwa wenzetu hawa waliwekeza katika elimu kuanzia nurseries, primaries, secondaries, colleges and universities.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika nchi za East African Communities tunaishinda Southern Sudan tu, nchi nyingine zilizobaki zimetuacha nyuma. Nchi nilizozitaja zimefikia uchumi wa dunia ya kwanza na dunia ya pili sababu waliwekeza katika elimu, hiyo ndio siri ya mafanikio. Kenya walipoamua elimu bure waliamua kwa dhati ya moyo wa Serikali yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri, Serikali iwekeze katika elimu ili tuepuke shida na matatizo yaliyopo katika elimu ya Tanzania kuanzia mitaala, chakula mashuleni, mikopo vyuo vikuu. Tanzania uchumi wake ukue practically badala theoretically kama nchi nilizozitaja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana 11 aprili 2018 Rais wa Kenya Uhuru Kenyata alisaini sheria kwa niaba ya Serikali kuwapatia huduma ya taulo za kike kwa wanafunzi wote wa kike nchini Kenya kupatiwa huduma hiyo bure (free of charge).

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu bure bado katika ngazi za chini haieleweki na Walimu wetu wamechanganyikiwa maji na umeme vinakatwa, walinzi hakuna na shule zinaibiwa vifaa mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, afya, naipongeza Serikali kwa kutoa katika halmshauri mbalimbali ikiwemo Halmashauri ya Jiji la Tanga kutupatia shilingi 1.4 bilioni kwa ajili ya Vituo vya Afya vifuatavyo:-

Makorora 500 milioni, Mikanjuni 400 milioni na Ngamiani 500 milioni na shughuli za ujenzi sasa hivi zinaendelea katika vituo hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanga hatuna hospitali ya Wilaya, katika bajeti ya halmashauri, Baraza la Madiwani tumetenga shilingi milioni300, regardless shilingi milioni 400 ambazo zimeshajenga administration block ambapo kwa sasa baadhi ya vyumba vinatumika kutoa huduma kwa wananchi kama zahanati. Naiomba Serikali itupatie shilingi bilioni 1.6 ili tuweze kujenga Out Patient Department (OPD). Kwa kufanya hivi tutaipunguzia mzigo mkubwa wa wagonjwa toka Wilaya zote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Bombo ni hospitali ya rufaa ambayo ina upungufu mkubwa wa vifaa tiba, Madaktari Bingwa lakini hata miundombinu, lift ina muda mrefu zaidi ya miaka mitatu ni mbovu na old model inahitajika lift mpya Bombo.

Mheshimiwa Mwenyekitim, nimefanya utafiti na ufuatiliaji katika kampuni maarufu ya lift ya OTIS- FRANCE zinahitajika euro 126,000 ambazo ni sawa na shilingi milioni 400 kuweza kupata lift mbili mpya kwa ukubwa wa jengo la lift lililopo. Naiomba Serikali itoe hizi euro 126,000 ili kutatua tatizo la lift na kuondoa adha ya mabaunsa kubeba wagonjwa na pia tunaomba Madaktari Bingwa wa mifupa, vichwa na magonjwa ya akinamama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo, nawapongeza wakulima wote Tanzania. Tanzania miaka 57 baada ya uhuru bado kilimo chetu ni cha jembe la mkono 80% na bado kilimo kipo katika propaganda za kisiasa na misamiati kibao. Kilimo cha ushirika, kilimo cha kufa na kupona, kilimo kwanza, kilimo cha bega kwa bega, lakini Serikali bado haipo serious na hata pale wakulima wanapofanya bidii ya kulima na kupata mazao ya kutosha kwa chakula na biashara wanakatazwa kuyauza kwa soko wanalotaka wenyewe. Mfano, zao la mahindi, Mbaazi na zao la Karafuu Zanzibar. Baada ya Bunge kuchachamaa mahindi ruksa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri, Tanga City Council, tunazalisha muhogo na matunda kwa wingi katika Kata za Kirare, Tongoni, Mabokweni, Pongwe, Mzizima na Chongoleani lakini hakuna soko la uhakika. Ni aibu kwa Tanzania kuagiza juice za orange, mango, guava, mastafeli tena tunaagiza kwa fedha za kigeni kutoka nchi za Saudi Arabia, South Africa na Kenya juice za Ceres na tropical. Serikali ijenge viwanda vya kusindika (processing) matunda Tanga kulingana na wingi wa matunda yaliyopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mifugo; ufugaji katika Tanzania imekuwa ni balaa wafugaji wanateseka wao na mifugo yao, hawaruhusiwi kuchunga mifugo yao katika mapori ya hifadhi wala ranchi za Serikali kwa kisingizio kuwa wanavamia hifadhi za Taifa. Mifugo ni uchumi na biashara, nchi kama Botswana, Swaziland na Ethiopia zinafaidika kiuchumi na kutumia fedha hizo katika miradi ya maendeleo. Tanzania wafugaji wetu wananyang’anywa mifugo yao na kutiwa umaskini hali inayosababisha wafugaji kukimbia familia zao kutokana na umaskini baada ya kunyanga’anywa mifugo yao. Wananyang’anywa mifugo ng’ombe 500, 700 hadi 2,000 habaki na hata ng’ombe mmoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuweka alama kwa moto, huu ni ukatili wa kupindukia kwa kuwa chuma cha moto ni maumivu makali kwao. Waziri wa Mifugo anazindua uwekaji alama kwa kumchoma mnyama kwa moto. Ushauri Serikali itoe elimu ya ufugaji wa kisasa kwa kuweka pin masikioni badala ya moto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uvuvi na zana za kisasa, wavuvi wamesahauliwa na kubwa kwao ni kulipishwa ushuru wa samaki, kunyang’anywa nyavu na boti zao. Hii sio haki inahitajika elimu na replacement za vifaa vinavyokubaliwa kisheria na sio kuchoma moto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TARURA (Tanzania Rural and Urban Road Agency); katika Bunge la mwaka jana bajeti tulipatiwa taarifa na kupitisha TARURA, tunajua nia njema ya Serikali lakini TARURA haijafahamika kwa Wabunge na Madiwani hata kidogo. Tuliomba Serikali itufanyie semina Wabunge, kisha Madiwani lakini hadi leo ni mwaka bado hakuna semina. Ushauri wangu, Wabunge tupatiwe semina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha za vijana na akinamama asilimia kumi; kila halmashauri inatakiwa kutenga 10% za vijana na akinamama, lakini kutokana na vyanzo vya mapato vya property tax na mabango kuporwa na Serikali Kuu (TRA), halmashauri kwa sasa zina hali mbaya kifedha. Hii ni moja ya sababu za kutotengwa kwa fedha hizi. Ushauri wangu ni kwamba, naomba Serikali irudishe vyanzo vya property tax na mabango ya biashara ili makusanyo haya yaweze kuziwezesha halmashauri kutenga fedha hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sekta ya Utumishi ni sehemu muhimu katika nchi yetu ambayo ina changamoto nyingi ikiwemo watumishi na wafanyakazi kucheleweshwa michango yao katika Mifuko ya kijamii kama vile NSSF, LAPF, GEPF na kadhalika. Miongoni mwa changamoto nyingine ni mtindo wa kuwahamasisha Walimu toka sekondari kuwarudisha kufundisha shule za msingi bila ya kuwalipa stahiki zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni tatizo na tunaona ni jambo jema kwa kisingizio cha kuboresha tatizo la upungufu wa Walimu katika shule za msingi, lakini hili ni tatizo ambalo Walimu hawa wanafanya mgomo wa kimya kimya na matokeo yake wanaoathirika ni wanafunzi kwa kuwa Walimu hawafundishi kwa moyo, wanafunzi wanafeli na ushahidi wa hili shule zinazoongoza kwa ufaulu ni za private.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vibali vya ajira kukosekana katika halmashauri, kufuatia zoezi la uhakiki wa vyeti feki watumishi waliokosa vyeti vya form four pamoja na Serikali kutangaza kuwa walioathirika na zoezi hili warudishwe kazini, lakini kuna tabia kule chini likitoka agizo la Serikali katika utekelezaji wanasema hatujapokea waraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kwamba, waraka huo ushushwe ngazi za chini immediately, wale ambao wamefariki kufuatia pressure na mshtuko ingawaje kufuatia zoezi hili pia athari zimepatikana katika sekta mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, afya, Madktari na wauguzi baadhi wamekosekana na vituo, zahanati zimekosa watumishi na ajira mpya vibali havitolewi bila ya kuelezwa sababu zenye kueleweka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu, bado kuna upungufu mkubwa sana katika sekta ya Walimu (shule za msingi, shule za sekondari na vyuo). Mfano, Mamlaka ya Maji Tanga wafanyakazi wengi wamefukuzwa katika Halmashauri ya Jiji la Tanga, tunazo kata 27 na mitaa 181; Watendaji wa Mtaa katika mitaa 181 waliopo 123 na pungufu ni 58. Watendaji Kata katika kata 27, waliopo ni watendaji 13, pungufu ni 14. Pia kuna mitaa ambayo kuna makaimu ni zaidi ya miaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu, vibali vya ajira vitolewe haraka ili kuondoa upungufu wa watumishi katika sekta mbalimbali ili kutoa huduma bora kwa wananchi.