Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye elimu bado nilisahau kuhusu msongamano wa wanafunzi na kwa makusudi kabisa wananchi wa Tarime pamoja na wadau mbalimbali tumeamua kujenga shule nyingi za msingi, mbili za sekondari, lakini cha kusikitisha Shule ya Msingi Rebu ilikuwa ikitumiwa na Shule ya Msingi Buguti pamoja na Shule ya Msingi Mturu, ambapo tumejenga shule Bufuti na imekamilika, tumejenga shule ya Mturu kwa ushirikiano wa Mitaa ya Uwanja wa Ndege na Mkuyuni ambapo tulijenga vyumba sita na ofisi hadi usawa wa renta, lakini Mkurugenzi amesimamisha ujenzi kwa sababu zisizo na msingi. Wakati Waziri Mkuu amekuja alisema DC ashughulikie hiyo shule, tunaomba sana tupate suluhisho ili wanafunzi wetu wasisome zaidi ya 120-200 kwa darasa au wengine kukaa chini ya mti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuondoa ukaimishaji wa idara zote zilizopo ndani ya Halmashauri ya Mji wa Tarime ili kuweza kuweka ufanisi wa kazi na kuleta maendeleo ndani ya halmashauri ya mji. Tupate rasilimali watu wenye uweledi na wanaomudu kazi zao. Tusibebane kwa maslahi ya watu wachache bali tuangalie Taifa. Halmashauri ndio wasimamizi wa miradi mbalimbali kutoka wizara zingine. Hivyo watendaji wazembe ni msiba kwa halmashauri na maendeleo hayatakuwepo. Mfano ni Idara ya Maji, miradi yote ya maji tulikosa kwa uzembe, Idara ya Mipango ndio ime-paralyze kabisa, idara zingine zimekwisha, si sawa. Tunaomba waajiriwe kama wanafaa au watafutwe wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nyingine ni fedha za jengo la utawala hatujapewa hata senti tano. Tunaomba review ifanyike ili na sisi tuweze kujenga jengo letu la kukamilika kuliko pale tulipo ili hata mandhari ya mji wetu yawe mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni mnada wa Magena, tunaomba sana Wizara hii ifanye follow up na Wizara ya Mifugo ili ule mnada ufunguliwe na kuwe chanzo cha mapato kuliko kupotea kwa kupeleka mnada wa mpakani kwa nchi ya Kenya (Mabara). Kwa nini sisi Magena isifunguliwe kwa makubaliano ya kikao cha 2016 kilichojumuisha Mheshimiwa Mwigulu, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi; Kamati ya Ulinzi na Usalama; wananchi na kuridhia kuwa minada yote ifanye kazi maana Magena ni wa mpakani na ule wa Kinimi Check point ni wa upili. Hii yote italeta tija ya mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.