Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza sana tena sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya na Mola ampe maisha mema na afya njema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Jafo ni Waziri wa kuigwa kutokana na jinsi anavyofanya kazi kwa kushirikisha zaidi na walengwa hadi ngazi ya awali, hafanyi kazi za mezani. Mola ampe nguvu na afya atimize azma yake. Pamoja na timu yake ya Wizara yake wanashirikiana vyema na waendelee hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mkuchika kwa kazi nzuri sana, ingawa bado ana jukumu kubwa kwa mazingira ya upungufu wa watumishi katika sekta mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mengi kufanyika vizuri, bado tunahitaji kazi ifanyike na hasa kwa mikoa ya pembezoni na kufuatiwa na miji kupanuka na wananchi kuibukia kujenga majengo yao kwa maendeleo yao na kuwaonesha kasi yao kubwa na kuacha Serikali nyuma. Mfano Rukwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba TAMISEMI ishirikiane na Wizara husika kupatikana kwa vyombo vya upimaji ardhi, ili miji ipangwe na tusiwe na maeneo yasiyo na mpangilio. Zoezi la matumizi bora ya ardhi kwenye mikoa yetu lifanyiwe kazi na kutathmininwa kila mwaka ili tuondokane na migogoro ya wakulima na wafugaji, pia na hifadhi zetu na miji yetu isivurugike kimpangilio.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba TAMISEMI kuona umuhimu wa kuongeza asilimia ya fungu la fedha za maendeleo ya ujenzi wa barabara za vijijini kwa TARURA. Barabara hizo ni nyingi na zinaongezeka siku hadi siku, kwa jinsi wananchi wanavyoongezeka kwenye maeneo na kuibuka vitongoji na vijiji kupanuka. Hivyo tunahitaji TARURA kuwa na nguvu kubwa kwa utekelezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukizingatia barabara za vijijini ni za muhimu sana kwa wakulima, kusafirisha mazao yao kuwapeleka sokoni na viwandani. Akinamama ndiyo wazalishaji hasa wanahitaji barabara kuwawezesha kufika sokoni, hospitali na kupunguza vifo vyao na watoto. Bora TARURA kupata asilimia 65 angalau kwa kuanzia kwani TANROADS hupata wao na wafadhili na marafiki wa nchi na mikopo ya nchi kuendeleza barabara husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana tena sana pamoja na kutokuwa na mapato ya kutosha na kutoa nguvu ya mwelekeo wa bajeti kuwa yenye matumaini makubwa kwa maendeleo. Bado tunaomba Wizara kuona uhitaji wa watumishi kwenye maeneo ya awali waliko wananchi wetu ambao wazalishaji wa mazao ya chakula na malighafi ya viwanda vyetu. Wanahitaji zahanati, vituo vya afya, majengo yapo na yanaendelea kujengwa lakini watumishi hawapo, wanahitajika wataalam husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu bure; inatuhitaji kujenga madarasa, tunaomba Serikali kuwaunga mkono wananchi kuyakamilisha madarasa haya na miundombinu yote ya shule. Maafisa Maendeleo wa Mitaa/Vijiji na Kata na Maafisa Ugani kuhakikisha wataalam hawa kuwepo katika maeneo hayo kwa nchi nzima kwa maendeleo ya wananchi wetu. Pia, wapewe usafiri kurahisisha kazi yao ya kuwatembelea walengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ongezeko la watoto kwenda shule kutokana na elimu bure, Wizara tunahitajika kuajiri Walimu wa shule za msingi na kuwapeleka Walimu kuwa na watoto (wafanyakazi) 45 kuliko ilivyo sasa zaidi ya 100 siyo vyema. Utaratibu wa ujenzi wa nyumba za Walimu ufanyike kwa kila mkoa kwa kuigwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado halmashauri zetu zinafanya vikao vya Mabaraza wakati wa ratiba ya Bunge na Kamati za Kudumu za Bunge. Hali hii inasababisha Wabunge kutohudhuria vikao hivyo, waskati mwingine inamgharimu pakubwa Mbunge kuhudhuria. Pia tunaomba posho ya Madiwani kuangaliwa upya na wasaidizi wao Wenyeviti wa Vijiji na Mitaa, kwani kazi yao ni kubwa kwa usimamizi wa ufuatiliaji wa miradi na maendeleo kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.