Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naomba nichukue fursa hii kuwapongeza sana Waheshimiwa Mawaziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo na Mzee wangu Mkuchika pia bila kuwasahau Naibu Mawaziri Mheshimiwa Kakunda, Kandege pamoja na Watendaji wote kwa kazi nzuri zinazofanyika katika Wizara zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu unajitokeza katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, afya; katika eneo hili kwanza naomba sana hospitali ya Mafinga Mjini iliyopo katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga, ipandishwe hadhi na iwe hospitali ya rufaa kwa ajili ya maslahi ya wananchi wa Wilaya nzima ya Mufindi pamoja na wakazi wengine wanaopata huduma kutoka wilaya nyingine na mkoa mwingine kama wakazi wa Madibila, Mapogoro kutoka Wilaya ya Rujewa, Mkoa wa Mbeya pia kumekua na ajali nyingi sana zinazotokea katika maeneo haya na zinakuwa zinahudumiwa na hospitali hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Mufindi Kaskazini lina Tarafa nne (4) lakini tuna vituo viwili tu vya afya na Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi haina hospitali. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI aliangalie jambo hili kwa macho mawili, kwa kuanzia tu hata tukiwa na kituo kimoja kwenye kila tarafa tutakuwa tumeanza nyema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ina watumishi asilimia 28 za watumishi. Kwenye Idara ya afya kuna upungufu wa asilimia 72. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri alione jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi tuna zahanati nne ambazo zimekamilika, zahanati hizo ni Mwitikila, Mufindi Kaskazini; Kiponda Nyigo na Igoda, Mufindi Kusini; lakini bado hazijafunguliwa sababu wataalam na vifaa, lini zahanati hizo zitafunguliwa ili kutokuvunja au kudhoofisha nguvu ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali iunge mkono juhudi za wananchi wanaojenga Zahanati kama vile Igomtwa na Wambi Mbelwa na Makongomi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara; kuna haja ya kuongeza pesa kwenye Taasisi ya TARURA ili iweze kufanya kazi zao vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna barabara muhimu sana katika Jimbo la Mufindi Kaskazini lakini wakati wa mvua haipitiki kabisa. Barabara hii ni kutoka Mtili – Ifwagi – Idaburo – Ihanu – Isipii – Mpangatazara - Mrimba. Barabara hii inaunganisha Mikoa miwili, Iringa na Morogoro, Wilaya ya Mufindi na Kilombero ina ukubwa wa zaidi ya kilomita 106.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Jafo anajua tatizo la barabara hii, naomba sana tupewe pesa ya kutosha kwa ajili ya matengenezo ya barabara hii yenye uchumi mkubwa kwani kuna kilimo cha chai, pareto, maharage, misitu mikubwa ya mbao pamoja na eneo la utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naunga mkono hoja ya bajeti zote mbili ya TAMISEMI pamoja na Utumishi na Utawala Bora.