Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali na Watendaji wote wa Serikali kwa kazi nzuri ya kuwahudumia Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Jafo na Naibu Mawaziri wake na Watendaji wote wa Wizara ya TAMISEMI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia 10 ya vijana na wanawake; kauli ya Serikali kwamba kuanzia sasa fungu hili la vijana na wanawake halitatozwa riba ni jambo zuri. Ushauri wangu ni vizuri Serikali ijiridhishe suala la kodi ya mapato kwani TRA inatoza mapato Vyama vya Kuweka na Kukopa (SACCOS), hivyo ni vyema jambo hili likapewa ufafanuzi ni kwa namna gani pesa hizo zitapitia SACCOS bila kutozwa kodi ya mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TAMISEMI ndiyo inayosimamia shule za msingi na sekondari. Hali ya uanzishaji wa vyuo vya ufundi VETA hapa nchini si ya kuridhisha na tunatoa elimu ya nadharia zaidi. Nashauri Serikali kufanya maamuzi ya kuagiza kila halmashauri iongeze mchepuo wa ufundi katika shule moja au mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo lazima kuanzisha fani zaidi ya moja katika kila shule ili jambo hili liwezekane kwa urahisi ni vizuri kuanzisha fani zenye gharama nafuu ili vijana wakimaliza kidato cha nne wawe na ujuzi wa kuwawezesha kuwapatia ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Walimu wa shule ya msingi wenye cheti cha daraja la IIIA, hawana fursa ya kujiendeleza na daraja la IIIA siyo sifa ya kujiendeza katika chuo chochote hapa nchini. Nashauri Serikali, TAMISEMI wakae na Wizara ya Elimu ili kozi iliyozuiwa na Wizara ya Elimu iliyokuwa ikisimamiwa na NACTE na kuendeshwa na vyuo vya kati kwa kuwapa maarifa zaidi Walimu hawa pia kuwawezesha kupata madaraja mapya kwenye kada ya Walimu wa daraja IIIA hii pia itatia morali kwa Walimu hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.