Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, napongeza sana juhudi zinazofanywa na Mheshimiwa Waziri katika kuboresha na kutatua migogoro ya wafugaji na wakulima. Niiombe Wizara mambo yafuatayo:-
(1) Ije na mfumo mpya wa pembejeo ili kuondoa upotevu wa fedha na itasaidia kutathmini hali ya kilimo nchini.
(2) Mkoa wa Singida ni maarufu kwa kilimo cha alizeti na vitunguu, naiomba Wizara ituletee mbegu bora ili tukidhi bidhaa ghafi nchini.
(3) Cattle holding ground iliyoko Singida Mjini takribani kilomita tano toka centre, naiomba Wizara itupatie heka 21 ambayo ni sehemu ya eneo hilo ili tuweze kutengeneza Trading Area na kuboresha Mji wetu wa Singida, ukizingatia eneo limepitiwa barabara kuu.
(4) Naiomba Wizara iwasaidie wafanyabiashara wa ngozi kupata soko la uhakika la ndani na nje ya nchi, hasa Afrika Mashariki kwani sasa hivi soko hakuna na bei imeshuka kutoka 2000 kwa kilo mpaka 100 kilo. Wizara ije na mpango maalum wa kuboresha suala hili.