Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi sana kwa Waziri Mheshimiwa Jafo pamoja na Manaibu wake, Katibu Mkuu na Naibu Makatibu Wakuu kwa kazi kubwa wanayoifanya kwa ujumla.

Nashukuru kwa fedha ya Kituo cha Afya cha Mkoli na kuwekwa kwenye bajeti kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Nyasa kwa kutengewa bilioni 1.5. Naamini zitatolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupatiwa Madaktari kwenye Wilaya yangu. Naomba nimpongeze sana Dkt. Aron Hyera, Ag. DMO kwa kazi nzuri ambayo mimi binafsi naridhika nayo pamoja na wenzake ambao wapo katika Wilaya ya Nyasa. Naamini kuna siku atapitishwa kuwa kamili, mnyonge mnyongeni haki yake apewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Nyasa kupitia Kituo cha Afya cha Mbamba bay wameweza kuokoa maisha ya mama na mtoto; upasuaji 231 mpaka last week, operation nyinginezo 87 kuanza tarehe 19 Mei, 2017. Si kawaida sana lakini imewezekana, ubunifu unaofanyika ni mkubwa tumepoteza mama mmoja tu na sababu ni kuwa alicheleweshwa nyumbani hivyo kwa niaba ya wananchi wa Nyasa, nawashukuru sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazidi kuomba uboreshaji kituo cha Afya cha Lipelambo kipo mbali sana takribani 130 kilometres (isolated); Kukamilishwa kwa jengo la utawala Kituo cha Afya cha Kuhagara pamoja na kupata wodi; na Kukamilisha majengo ya Kituo cha Afya cha Chiwanda na Ntipwili ambayo yalijengwa na wananchi angalau yaweze kutumika kama zahanati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumalizika jengo la utawala la mbamba bay secondary school; kuweka kwenye mpango ujenzi wa Kituo cha Afya Kingerikiti ili kuendelea kupunguza umbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mchango wangu hauwezi kukamilika kama sitawashukuru na kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Makamu wa Rais pamoja na Mheshimiwa Kassim Majaliwa Mbunge, Waziri wetu Mkuu, kwa kazi kubwa na nzuri kwa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naomba pia kukumbusha ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja jimboni kwangu, kama nilivyomnakilisha Naibu Waziri Mheshimiwa Josephat Kakunda aliyeongozana naye na kutoa maagizo kwa Mkuu wa Mkoa kuhusu wodi Grade A.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.