Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa anayoifanya. Pili, nichukue nafasi ya kipekee kwa kumpongeza Waziri, Mheshimiwa Selemani Jafo kwa kazi kubwa anayoifanya kwa kuwatumikia Watanzania wote bila ubaguzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza miradi ya Sekta ya Afya hasa katika kufanikisha kunipatia fedha za Vituo vya Afya vya Karema, Mwese na Mishamo; zaidi ya hayo, ni kutenga fedha za Hospitali ya Wilaya ya Tanganyika. Pia nitoe shukrani kubwa kwa kunipatia gari ya ambulance.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo ambalo naomba sana Serikali itusaidie, ni kutupatia magari ya Sekta za Elimu katika Wilaya ya Tanganyika, Ujenzi na Afya. Kuna tatizo kubwa kwani Halmashauri ya Mpanda DC haina magari kutokana na halmashauri hii kuwa mama wa halmashauri zote zilizopo Mpanda, hivyo kupelekea kila halmashauri iliyogawanywa kuchukua magari kutoka halmashauri mama na matokeo yake halmashauri hii haina magari ya kufanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la uhaba wa Walimu; naomba tatizo hili liangaliwe sana hasa katika maeneo ya pembezoni ambako hakuna kabisa walimu hasa wa masomo ya sayansi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la barabara za vijijini ambazo zinahudumiwa na TARURA; tunaomba eneo la Mishamo lipewe budget ya kutosha, kwani eneo hili lina barabara kiasi cha kilometa 1008 ambazo TARURA pekee kwa bajeti inayotengwa haiwezi kutekeleza. Hivyo, tunaomba maombi maalum ya kutenga fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miradi ya maji, hasa katika shule na kwenye zahanati tunaomba iangaliwe na kusimamiwa ili iweze kuwasaidia wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.