Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali Wizara ya Maji na Umwagiliaji 2018/2019

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali Wizara ya Maji na Umwagiliaji 2018/2019

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kunipa afya siku hii ya leo niweze kuchangia kwenye Wizara hii. Ninakushukuru Mheshimiwa Spika, kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia Wizara ya Maji ukizigatia tunavyosema maji, maji ni kila kitu katika maisha yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tukizungumzia suala la maji kama ni uhai na ukiangalia kwa jinsi Serikali yetu haitaki kutekeleza ili sera hii ya kuwa maji ni uhai iweze kuwepo mimi nasikitika sana. Maji ni tatizo kwa nchi nzima hususan hata kwenye Mkoa wangu wa Iringa ukiangalia Nyakavangalala, Mkulula, Usolanga, Area Mgungwe, Luhota maji hatupati.

Mheshimiwa Spika, nimeona kwenye kitabu cha Waziri ukurasa 267 hadi 279 visima ambavyo vimechimbwa kwenye Mkoa wa Katavi, jumla kulikuwa na visima 225 kwa nchi nzima lakini Mkoa wa Katavi peke yake ni visima 79.

Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko hayo ukitoa unaona ni visima 146 vinavyobaki kugawanya Mikoa 29 na ukigawa kwenye mikoa 29 unaona kila Mkoa utapata visima
7.7 ukifanya estimation ni visima nane lakini Mkoa mmoja tu visima 79. Haya ni masikitiko kwa sababu Mkoa wa Katavi ndiko anakotoka Waziri wa Maji. Tukisema sisi watu wa…

T A A R I F A . . .

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Spika, taarifa hiyo siipokei kwa sababu Waziri wa Maji ndiye anayesimamia Mikoa yote ya Tanzania wapate maji, kwa msimamo huo yeye angelazimika kuhakikisha wataalam wanaenda kutoa elimu hiyo kwa Mikoa yote ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninaona upinzani tukisema tunataka Mawaziri wasitokane na mfumo wa Vyama vya Siasa ni kwenye tija kama hii, maana wakipatikana Mawaziri wenye taaluma unapoingia kwenye miradi kama hii hutapendelea huko unakotaka upate kura wewe. Sisi wote Wabunge tunataka turudi humu ndani. Namuomba Waziri wa Maji anapohitimisha hoja yake hii hebu aniambie vijiji nilivyosema atapeleka wataalamu lini wakatoe elimu hiyo kamaaliyoifanya kwake Katavi hatimaye wakapata hivyo visima 79 badala ya kupata visima 7.7. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa hii miradi mikubwa ya maji ambapo Serikali inawekeza ukiangalia bajeti ya mwaka jana 2017/2018 Bunge hili lilipitisha bajeti ya bilioni moja kwa ajili ya mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Kahama, Shinyanga hatimaye Tabora. Hadi 30 Machi, 2018 hakuna hata senti tano iliyoenda. Sasa tumebakiwa na miezi mitatu ili bajeti ya mwaka 2017 ifungwe, ninaomba Waziri wa Fedha anataka kuniambia katika miezi mitatu iliyobakia hiyo trilioni moja tuliyoipitisha hapa ndivyo ataitekeleza kwa kipindi kifupi hiki? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nafikiri ni vema tufikie wakati wa kupanga miradi yenye uwezo wa fedha ambazo tunazipata kwenye nchi yetu ili iweze kutekelezeka hatimaye Watanzania wote waweze kupata maji. Kwanza nina masikitiko makubwa ninapozungumza hapa katika Mkoa wa Iringa Wilaya ya Kilolo, Kijiji cha Nyanzu chenye wakazi wasiopungua 2,500 wenyewe kazi yao ni kilimo cha umwagiliaji ambapo takribani kama heka zisizopungua 2500 ni shamba la umwagiliaji. Hadi ninapozungumza hivi heka hizo zote vitunguu vimekauaka kwa sababu ya kukosa maji. Sasa mnaponiambia Mjumbe aliyepita anasema ni Halmashauri ambazo zinatakiwa zisimamie suala la maji wakati Waziri mwenye dhamana yupo, mwenye wataalam wake...

Mheshimiwa Spika, ninaomba maji watu wa Nyazwa wapate waweze kumwagilia mashamba yao.