Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali Wizara ya Maji na Umwagiliaji 2018/2019

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali Wizara ya Maji na Umwagiliaji 2018/2019

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kutumia muda huu kuchangia kwenye hotuba iliyoko mbele yetu ambayo ni Wizara ya Maji na Umwagiliaji.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba nikitaarifu kiti chako kwa sababu Mheshimiwa Nsanzugwanko hapa ametoka kumalizia anasema kwamba kuna uwezekano mkubwa DAWASA na DAWASCO sasa hivi wanakwenda kuunganishwa, hii ni kwa ajili ya wakazi wa Dar es Salaam lakini naomba tu tuwasaidie jambo moja na kiti chako kifahamu kwamba kuna ubadhirifu mkubwa sana umefanyika ndani ya DAWASCO na wanapokwenda sasa hivi kuunganisha DAWASCO na DAWASA madeni haya yote yatarudi kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, zaidi ya shilingi bilioni 800 na kuna madeni makubwa sana pale ndani, kwa hiyo tunaomba tufahamu, kuna madeni ya umeme ambayo ni shilingi bilioni 3.5; kuna madeni ya NSSF pamoja na PSPF karibu shilingi bilioni 12; kuna madeni pale ya TRA na madeni mengine mengi kiasi wale wafanyakazi wa DAWASCO na wafanyakazi wa DAWASA wao hawaelewi wanasimama upande gani kwenye kulikamilisha hili jambo lao. Kwa hiyo, tunamuomba Waziri na ikiwezekana uagize kiti chake kifanye Special Audit kabla ya hizi taasisi mbili hazijaunganishwa kutokana na madeni yaliyoko kule ndani, otherwise tunakwenda kuwasababishia matatizo makubwa sana watumishi wanaobaki na wale wengine watakaohama pale.

Mheshimiwa Spika, kama tulivyosema toka mwanzo Wizara hii ni Wizara nyeti sana inagusa maeneo yote ya Tanzania na kilio kimekuwa kikubwa sana kwa Wabunge wote na wewe mwenyewe pia umeshuhudia kinachotokea hapa. Naomba nitumie nafasi yangu kuwakumbusha pia Wabunge wenzangu majukumu yetu kimsingi.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa niseme tunatakiwa tuwe wazalendo kwa ajili ya Taifa letu. Jambo la pili tuhakikishe tunasimama mguu mmoja na wapiga kura wetu lazima tuone maslahi ya wapiga kura wetu yanasimamiwa na jambo la tatu lazima tuwe na uhakika kwamba tunavitetea na kuvilinda vyama vyetu kwa uchache wake lakini ni jambo la tatu; na mwisho kabisa tuangalie nafsi zetu wenyewe.

Mheshimiwa Spika, Bunge lako na ninavyoona mimi nilivyojifunza kwa hizi siku chache nilizoko hapa ndani kwamba sasa hivi linaanza kuegemea upande mmoja tu, tunaangalia sana maslahi ya chama, tunasahau wapiga kura wetu, tunasahau uzalendo juu ya nchi yetu, lakini pia tunasahau kuhusu nafsi zetu wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumepokea hizi taarifa zote mbili kutoka kwa Kamati, lakini pia tumepokea taarifa ya Waziri mwenyewe kwenye kitabu chake. Vitabu hivi ukiviangalia kwa pamoja vinatofautiana sana kwenye baadhi ya maeneo. Tukianza moja kwa moja kwenye suala la umwagiliaji. Ukienda kwenye kitabu cha Waziri, suala la umwagiliaji ukurasa wa 11 wanasema hivi; “Mheshimiwa Spika, nchi yetu ina eneo la hekta 29.4 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji, ambapo hekta 2.3 zina uwezekano mkubwa wa kumwagiliwa, hekta 4.8 uwezekano wa kati na hekta 22.3 zina uwezekano mdogo wa kumwagiliwa.” Anaendelea kusema kwamba; “Serikali ina nia ya kujenga miundombinu yenye jumla ya hekta milioni moja kwa ajili ya kuwasaidia wakulima wadogo wadogo. Hadi mwezi Machi, 2018 jumla ya hekta 475,000 zinamwagiliwa sawa na asilimia 47.44 ya lengo la asilimia 1.6 eneo linalofaa kumwagiliwa”

Mheshimiwa Spika, wasiwasi wangu taarifa hizi zote walizotupatia huku juu zilikuwa irrelevant. Taarifa hapa ya muhimu walikuwa watuonyeshe namna hii heka milioni moja ambavyo wao wanakwenda kuitumia, matokeo yake wanatuletea taarifa zenye kuvutia, zinazoongea habari za heka milioni 29.4 mwisho kabisa wanakwenda kumalizia kwa kuongelea tu hekta milioni moja ambazo nazo hatujafanikiwa wanakwenda kusema tunakwenda kufanya asilimia 47.44.

Mheshimiwa Spika, tunasema tunataka kwenda kuwa nchi ya viwanda. Sasa tujiulize tunakwenda kwenye viwanda vya aina gani, kwa sababu tunapoenda kung’ang’ana bila kuwasaidia wakulima wa nchi hii maeneo mengi yanafaa kabisa kwa kilimo na yapo yanaonekana tunakwenda kuoanisha vipi kati ya viwanda hivi na sekta ya kilimo. Kwa nini tusitumie nguvu nyingi kuwaongezea nguvu wakulima, tukawaongeza asilimia kidogo pale kwenye suala la umwagiliaji tukaenda kuwasaidia badala ya sasa hivi kujikita kwenye viwanda vya uzalishaji mali. Kwa mfano, tunasema tunakwenda kutengeneza nondo na vitu vingine. Tunawasaidiaje wakulima ambao ni asilimia 85 ya wananchi wetu hapa Tanzania ili wao waweze kujikwamua kiuchumi tuweze kusogea mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wameongelea hapa kwenye Fungu Na. 49 kwenye suala la pesa za maendeleo. Ukienda kwenye kitabu cha Kamati wanasema wenyewe hapa kwamba So far…kwenye Kitabu hiki cha Waziri wanasema wamepata pesa walizozipokea mpaka sasa hivi walizokuwa wametengewa ni shilingi bilioni 648 lakini wao mpaka sasa wamepokea shilingi bilioni 347. Kamati inatuambia wamepokea shilingi bilioni 135 sasa tumuelewe nani? Ndiyo maana Wabunge wengine wamependekeza hili sasa suala la kuwakalisha Kamati na Wizara watuambie pesa walizozipata mpaka sasa hivi kiasi gani ili tuweze kuwaeleza Watanzania kwamba Mheshimiwa Waziri wa Maji pamoja na juhudi zake zote anashindwa kutekeleza majukumu yake kwa sababu hana ushirikiano mzuri au watu wa Wizara ya Fedha wanataka kumuangusha kwa makusudi. Haiwezekani watengewe bajeti yote hii halafu waende kupata tu pesa kiasi kidogo wakati wenyewe tunasema tuna nia ya kutaka kumtua Mama ndoo kichwani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukienda hata kwenye hiki kitabu chao labda ndiyo maana iko hivi, Mheshimiwa hapa anaonekana Mheshimiwa Makamu wa Rais akimtwisha Mama ndoo kichwani. Kwa hiyo, tafsiri yake ni kwamba Serikali haitaki kuwatua ndoo akina mama halafu tunakuja kuitetea hii Wizara kwamba ipate pesa ya kutosha kwa ajili ya kwenda kuwatua ndoo akina mama na ndiyo maana basi utakuta Wizara ya Fedha haipeleki pesa ya kutosha kuhakikisha miradi ya maji maeneo mbalimbali inakamilika. Kwa hiyo, kwa namna ya pekee kabisa tuwaombe Wizara ya Fedha wahakikishe pesa za maji kila mara zinafika pale kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, kuna mradi hapa umetajwa sana wa Stiglers’ Gorge.

Tunaongelea hapa kuhusu mradi wa Stiglers’ Gorge. Huu mradi nia yake ilikuwa ni kuongeza uzalishaji wa umeme ili twende kwenye nchi ya viwanda. Sasa tunasema kufikia mwaka 2025 Tanzania itakuwa ni nchi ya viwanda, lakini tukumbuke Bunge hili liliazimia kwamba miradi hii ya kimkakati na ndiyo kisa cha kwenda kuwekeza kwenye miradi ya gesi. Inakuwaje tunakwenda kwenye gesi, gesi inayosemwa inatumika kwa asilimia saba tu, leo tunaacha hii pesa ingekwenda kutumika kuwasaidia akina mama kupata maji tunakwenda kuwekeza Stiglers’ Gorge wakati Mto Rufiji sasa hivi hata yale makingio yake ya maji yameanza kupungua. Mwanzoni Mto Rufiji ulikuwa unapokea maji kutoka mito midogo midogo 29. Sasa hivi Mto Rufiji unapokea maji kutoka kwenye mito mitano tu, kwa hiyo kwa vyovyote huu mto baada ya muda fulani unaweza ukashangaa unakauka.

T A A R I F A . . .

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, naomba nikuambie kwamba kutokana na haya mambo yanayotokea kama hivi unavyoona hii michango na vitu vingine tunashindwa hasa kusimamia uzalendo ule tunaouhitaji wa kuweza kwenda kumtua mama sasa ndoo kichwani. Tumebakisha tu kwenda kusifia tunafikiri hii ndiyo sifa ya msingi ya Ubunge badala ya kuisimamia na kuishauri Serikali. Tumebakisha kupongeza badala ya kwenda kutoa michango yetu ili iweze ku-improve hizi ripoti zilizoko pale.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo yanayohusiana na Taifa kwa ujumla sasa nirudi Jimboni kwangu. Tuna vijiji kule kwetu vingi sana, ukienda Kata ya Mlingura, ukienda Kata ya Namajani, ukienda Kata ya Msikisi pamoja na Malembo, Chingulungulu, Nanganga pamoja na Liputo haya maeneo yote ndiko ambako linapita bomba la Mbwinji linalopeleka maji Wilaya ya Nachingwea, lakini pia linapeleka maji Wilaya ya Ruangwa.

Mheshimiwa Spika, Serikali hapa mwaka jana ilituambia vijiji vyote ambavyo viko kwenye radius ya kilometa kumi kutoka kwenye bomba kubwa vitapatiwa maji. Mimi nilisema hapa na nikatoa ushauri mnataka tusichimbe visima virefu kwa sababu tunafahamu lile bomba liko mita tano tu toka usawa wa ardhi, tutakwenda sasa kutoboa ili wananchi wapate yale maji kirahisi kama Serikali haitaamua kuyapeleka yale maji vijijini moja kwa moja.

Mheshimiwa Spika, kule kwetu kuna chombo kinaitwa MANAWASA ndiyo kinachotusababishia maji watu wa Masasi pamoja na watu wa Nachingwea. Mara nyingi wamekuwa wakiahidiwa kupata pesa, ukiongea na Mkurugenzi wa MANAWASA anasema chombo kile kikiongezewa nguvu kina uwezo wa kutatua tatizo la maji Kanda ya Kusini kuanzia Nachingwea mpaka Kilwa, wanahitaji tu kupewa pesa kidogo. Lakini kuna sintofahamu inayoendelea, kuna miradi ya mabwawa inaendelea kwenye maeneo haya na mtakumbuka hapa Waziri wa TAMISEMI alituambia kwamba wanataka kwenda kutengeneza Bwawa Lukuledi kwa kutumia pesa shilingi milioni 60 kufanya upembuzi yakinifu. Wakati tayari tulifanikiwa kupeleka maji Kijiji cha Chikunja kwa kutumia shilingi milioni 70, sasa hatuoni faida kubwa sana ya mabwawa haya badala ya kuwekeza kwenda kupata maji safi na salama. Muwashirikishe wenyeji wa maeneo husika ili kuweza kujua miradi ya kipaumbele kwenye maeneo yao, vinginevyo tutakuwa tunatumia nguvu kubwa kwenye eneo lisilohusika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna mradi wa maji unaoanzia Kata ya Mwena, Chikundi, Chigugu, Chikukwe na Vijiji vya Maparagwe pamoja na Mbemba. Mradi huu tunashukuru unaendelea vizuri lakini kuna tatizo moja, mkandarasi analalamika halipwi pesa zake kwa wakati mradi unasuasua.