Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali Wizara ya Maji na Umwagiliaji 2018/2019

Hon. Susanne Peter Maselle

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali Wizara ya Maji na Umwagiliaji 2018/2019

MHE. SUSANNE P. MASELLE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia Wizara hii ya Maji.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Mwanza umezungukwa na Ziwa Victoria lakini maeneo mengi ya mkoa huu hayana maji. Maeneo kama ya Misungwi, Magu na Buchosa; maeneo haya yako karibu sana na Ziwa Victoria lakini hayana maji. Ni aibu sana kwa Taifa kama hili ambalo lina miaka 57 toka limepata uhuru halafu bado wananchi wana-share maji na viumbe.

Mheshimiwa Spika, ningeomba Waziri anapokuja ku- wind up atueleze wananchi wa Mwanza ni lini tutafaidika na hili ziwa kwa sababu haya maeneo sioni sababu kwanini mama zangu wa kule ninakotoka Misungwi wahangaike kuchota maji na ku-share na wanyama maji machafu wakati wako karibu kabisa na ziwa.

Mheshimiwa Spika, ziwa hili limewasaidia watu wa Misri ambao wanatumia Mto Nile lakini wameweza kupata maji ambayo yanawasaidia hata katika viwanda kwa sababu wameweza ku-utilize hili ziwa vizuri. Sasa kwa nini sisi tunashindwa hata kupata maji ya kunywa tu ambapo ziwa kwa kiwango kikubwa liko katika nchi yetu?

Mheshimiwa Spika, nizungumzie miradi ambayo haijakamilika, Mradi wa Lumea Kalebezo. Mradi huu ulianza mwaka 2012 katika Halmashauri ya Buchosa na ulitakiwa kutumia miezi sita tu, lakini mpaka sasa hivi miaka sita mradi huu haujakamilika. Mradi huu ulikuwa wa kiwango cha shilingi bilioni 1.69 na mkandarasi ameshapewa shilingi bilioni 1.3 na maji hayajatoka. (Makofi)

Sasa Waziri nataka uje utuambie hii hela imeenda wapi, huu ni ubadhirifu wa hali ya juu sana. Hela za walipa kodi zinaliwa tu na tunaangalia tu. Nataka uje utuambie hawa watendaji waliyofanya haya mambo, waliolipa hela nyingi kwa mkandarasi wakati hajamaliza kazi watachukuliwa hatua gani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie kuhusu Taasisi za Serikali ambazo hazilipi bill. Kwa nini Serikali hawalipi bill katika taasisi zao matokeo yake wanakatiwa maji, wanakatiwa na umeme? Hii inasumbua watu wetu, mnawapa adhabu watu wetu ambao wanalipa bill kwa wakati. Tunaomba hili tatizo liishe; ni aibu sana kwa Serikali kukatiwa maji au umeme kwa sababu ya kutokulipa bill wakati ninyi mmekuwa mbele sana kuwakatia watu. Sasa tunaomba muoneshe mfano katika taasisi zenu.

Mheshimiwa Spika, ni aibu kwa hospitali kukatiwa maji, yaani mnategemea sasa watu wetu wafanye nini, kama sisi wenyewe tunashindwa kujisimamia? Ninaomba unapokuja ku-wind up utuambie kwamba ni lini sasa mama zetu wataacha kubeba ndoo? Kwa sababu hili limezungumzwa sana na wabunge tumekuwa tukilisemea sana na tunaenda kupitisha bajeti kama kawaida. Tunaomba hii bajeti iende, pesa hizo ambazo tunazitenga naomba ziende kwenye hiyo miradi na miradi ikamilike.