Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. MAFTAH A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na nimshukuru Mwenyezi Mungu Subhanah wataala, naomba nichangie kwa dakika hizi tano kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza ni suala la fidia ya ardhi. Ndani ya Bunge hili hii ni mara yangu ya nne nasimama nikiwa nazungumza suala zima la eneo la Mjimwema pale Mtwara Mjini. Eneo ambalo lilichukuliwa na Serikali, Serikali iliyopita na Serikali hii ya Awamu ya Tano wakaahidi kulipa fidia, kuwalipa wananchi wa Mjimwema.

Tangu mwaka 2013 walipochukuliwa yale maeneo yao wale wananchi wamekatazwa kulima maeneo yale wala kuendeleza maeneo yale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikaleta swali mara mbili ndani ya Bunge hili na Serikali ikaahidi kwamba itaenda kulipa mwaka jana baada ya bajeti tu. Hata hivyo jambo la kusikitisha sana, baada ya kumalizika kwa bajeti naambiwa Serikali haiwezi kulipa. Sasa nashangaa sana, yaani Serikali hii inachukua maeneo ya wananchi zaidi ya miaka mitano sasa tangia mwaka 2013, halafu inaahidi kulipa na hatimaye inakuja inawaacha njiani, inasema haiwezi kulipa fidia Halmashauri wenyewe ndio waende wakalipe fidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo sana, wananchi wa Mjimwema, Mtwara Mikindani wanasikitika sana kwa sababu wamekosa kuendeleza yale maeneo kwa ahadi kwamba Serikali itawapa fidia, lakini mpaka leo Serikali inasema haiwezi kufidia wakati ilishaahidi hapa. Mimi nina Hansard mbili; ndani ya Bunge hili Wizara ya TAMISEMI na Wizara ya Ardhi ikisema inaenda kulipa fidia watu wa Mjimwema. Naomba safari hii Mheshimiwa Waziri atupe majibu ya uhakika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana nilimpongeza sana hapa Mheshimiwa Waziri kwa mpango kabambe wa Mtwara, lakini katika hili Mheshimiwa Waziri Lukuvi ametuangusha wananchi wa Jimbo la Mtwara Mjini. Naomba hizo pesa kama ni Waziri wa Fedha ampatie hizo pesa ili aweze kuwalipa wale wananchi. Wananchi wanalia sana, wananchi wa Mjimwema, Mtwara Mjini hawawezi kuchukuliwa kwa siku zote hayo maeneo yao halafu Serikali inawaacha njiani kwamba haiwezi kulipa, haiwezekani. Serikali hii haisemi uongo na hili ni Bunge, Hansard mbili zimezungumza hapa kwamba tunawalipa lakini wanasema hawawezi kulipa ni jambo la ajabu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, naomba kuzungumzia suala la urasimishaji, tunashukuru kweli mpango huu wa urasimishaji Mtwara ni Mji wa pili na urasimishaji unaendelea pale Mtwara. Hata hivyo, niseme Mheshimiwa Waziri kwamba vifaa hajatusaidia, kwamba wale wanaopima hawana vifaa vya kutosha, kwa hiyo kasi imekuwa ndogo sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi ya mwaka hivi sasa na maeneo waliyopima ni machache mno pale Mtwara mjini. Kwa hiyo nimwombe Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Lukuvi kwa sababu ni msikivu sana tunamwaminia, naomba atupe vifaa Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani ili urasimishaji uende kwa kasi katika maeneo ya Chipuputa, maeneo ya Kiholo, maeneo ya Komoro, maeneo ya Magomeni, Kata ya Ufukoni; tunataka urasimishaji kwa sababu wale wananchi walijenga kiholela holela. Kwa hiyo tunaomba vifaa ili kazi iweze kuendana na maagizo yake ambayo ameyatoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo naomba kuzungumza ni suala la migogoro ya ardhi. Ni kweli kwamba hata pale kwetu Mtwara bado lipo na mwaka jana Mheshimiwa Waziri nilimweleza suala la yule jamaa tapeli, anaitwa siju Azimio, sijui nani sijui, maeneo mengi amefuta hati zake, lakini Mtwara mjini eneo la Libya mpaka leo wale wananchi walinyang’anywa na bado Mheshimiwa Waziri Lukuvi pamoja na usikivu wake Mtwara Mjini amekaa kimya juu ya mgogoro huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yule tapeli naona kaenda mahakamani sasa hivi kwa sababu yale maeneo alichukua kinyume na taratibu. Yaani watu wamelala, wanaamka asubuhi wanakuta beacons zimewekwa pale; mwaka jana nilizungumza hapa. Kwa hiyo hili suala halihitaji mahakama, linahitaji yeye kama Waziri kwa mamlaka yake aliyopewa aende akachukue yale maeneo awarudishie wananchi wa Libya Mtwara Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa wananchi wanalia sana na yule ni tapeli na Mheshimiwa Waziri tumeshamsikia anazungumza katika maeneo mengi kwamba huyu tapeli lazima maeneo aliyochukua yarudishwe kwa wananchi. Kwa hiyo, hili suala la mgogoro wa Libya Mtwara Mjini Mheshimiwa Waziri mwaka huu aende akatusaidie wananchi wale wapate lile eneo lao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine kuna mgogoro ambao nao nilizungumza mwaka jana, naomba utusaidie Mtwara Mjini juu ya suala hili ili wananchi wapate haki zao, kwa sababu Serikali zilizopita huko nyuma zilikuwa ni Serikali za kudhulumu wananchi, ilikuwa ni udhulumati, wananchi wananyang’anywa maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nilikuwa nataka kuzungumza ni suala hili la mashamba ya walowezi. Tanzania hii kuna maeneo mengi ambayo yalikuwa ni mashamba ya walowezi. Hata pale Lindi ukija Kikwetu Estate pale lile shamba ni kubwa sana. Wananchi wanahitaji maeneo waweze kujenga nyumba, wanahitaji kuendeleza pale Kikwetu pale Lindi, lakini wanasema lile lilikuwa ni shamba la mlowezi mmoja kamuuzia Mohammed enterprises.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa haliendelezwi na Mheshimiwa Waziri ameshatamka kwamba kisheria kama mtu hajaendeleza kwa muda fulani basi yale maeneo yanarudishwa kwa wananchi. Kikwetu Estate wananchi wanahitaji kujenga pale, wanahitaji kulima pale. Niombe sana kwa sababu yalikuwa ni mashamba ya walowezi huko nyuma tunaomba yarudishwe kwa wananchi ili waweze kuyaendeleza.