Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Mbarouk Salim Ali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wete

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. MBAROUK SALIM ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia leo hii kupata nafasi ya kuchangia katika Wizara hii. Niseme tuu kwamba this is a noble chance for me kwa sababu nimeomba Wizara karibu tano, lakini hii ni Wizara yangu ya mwisho ambayo niliomba na ndio mwanzo kupata leo. Nashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Waziri pamoja na Naibu wake pamoja na watendaji wote wa Wizara, kwa kweli wanafanya kazi nzuri sana. Niseme tu kwamba Wizara hii ina changamoto nyingi sana na ni Wizara ambayo ni ngumu sana kwa sababu ardhi ni rasilimali ya Watanzania wote na kila mtu anategemea ardhi kufanya shughuli zake. Sasa kama hatukupata watu, watendaji kama Waziri na Naibu waliopo hivi sasa, basi kwa kweli hayo malengo ambayo tunategemea kuyafikia tunaweza tusiyafikie kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napata mashaka makubwa sana, kwamba ule uchumi ambao malengo ya Serikali ya awamu hii tumekusudia kufikia, uchumi wa kati na uchumi wa viwanda, huenda hatutoufikia kutokana na matatizo ya ardhi. Matatizo ya ardhi bado ni makubwa mno na Serikali inashindwa kwa kweli Serikali inashindwa kutatua migogoro mingi ya ardhi ambayo ipo. Ukilinganisha labda Mheshimiwa Waziri atatuambia; hii migogoro kwa sisi watu wa nje tunavyoona ni kwamba badala ya kupungua, inazidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna migogoro mingi kati ya wakulima na wafugaji; kuna migogoro mingi kati ya wafugaji na watu wa hifadhi; kuna migogoro mingi hata katika taasisi za Serikali. Sasa, sitegemei au hatutegemei kwamba huko ambako tumelenga kufikia tunaweza tukafikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wasiwasi wangu ni kitu kimoja, kwamba kama ardhi ni tegemeo la watu wote nina wasiwasi kwamba kunakosekana coordination, coordination ya Taasisi za Serikali hakuna, kwamba kila taasisi inawania kipande hicho hicho cha ardhi lakini hakuna mtu ambaye ana-coordinate matumizi hayo ya ardhi. Sasa hili ni tatizo na inawezekana hili ndilo jambo ambalo linatusababishia migogoro mingi katika matumizi yetu ya ardhi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ingekuwa tunafuata utaratibu mzuri wa matumizi ya ardhi, kuna mbinu nyingi nyuma ambazo zimeweza kutumika/kuanzishwa ambazo zingeweza kutusaidia katika utatuzi wa migogoro ya ardhi. Kwa mfano, kuna mambo ya mbinu hizi za agro-forestry ambazo ni matumizi bora ya ardhi, tuliianzisha lakini utekelezaji wake unaonekana kama ni wa kusuasua. Pia kuna conservation agriculture ambacho ni kilimo kinachotumia ardhi vizuri, kinaonekana kwamba kimeanzishwa lakini uendelezaji wake ni wa kusuasua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mambo kama haya ambayo labda tungewaweka watumiaji wa ardhi kwenye eneo dogo tu wakaweza kutumia kwa pamoja, tukapunguza migogoro; sasa tunaanzisha halafu tunaacha. Tafiti zinaonesha kwamba haya mambo tukiyatumia vizuri kwa kweli tunaweza tukaenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningependa niligusie ni kuhusu bajeti. Bajeti ya Wizara hii inaonekana kwamba kila mwaka inashuka. Sasa bajeti inashuka; pamoja na kwamba bajeti ni ndogo lakini kile kima ambacho kinakisiwa pia hakitoki kikawaida. Kwa kweli ni jambo ambalo tunaifanya Wizara hii ishindwe kutekeleza kazi zake kama ambavyo imepanga kufanya. Napata mashaka makubwa kwamba utendaji wa Wizara hii unaweza ukawa mbovu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningependa nilizungumzie ni kuhusu Programu ya Land Tenure Support, ambayo ni nzuri na imeonekana kwamba inafanya vizuri. Hata hivyo, kwa sababu ya mfumo tu wa Serikali inaonekana kwamba hatuiendelezi. Ingawa Waziri ameigusia gusia katika kitabu chake lakini kuna technology inaitwa MAST…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.