Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

MakadirioMakadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

MakadirioMakadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa uhakika Wizara hii inafanya kazi kama mchwa kutokana na hali iliyopo katika suala zima la matumizi bora ya ardhi kwa nchi yetu na kujikuta na migogoro kila upande na inayoendelea kupatiwa ufumbuzi. Utekelezaji huu unatokana na umahiri, weledi wa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na baadhi ya watumishi wazalendo wapendao maendeleo ya nchi yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchini mwetu tuna mtihani mkubwa wa matumizi bora ya ardhi na kupanga nchi yetu na kuiepusha na migogoro ya wananchi wetu. Hadi mwaka 2016/2017 tuliweza kuwa na wahitimu 559 tumejitahidi na kufikia 787 mwaka 2017/2018 kwa nyongeza ya watahiniwa 228.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara ichukue maamuzi ya makusudi ya kuomba majengo kadhaa UDOM na kuendesha mafunzo ya wataalam wa ardhi huku tukiendelea na kuboresha miundombinu ya vyuo vyetu. Upungufu ni mkubwa kwa mahitaji yake, ukiangalia nchi ni kubwa na wananchi wanaongezeka kwa kasi kubwa kimaendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kasi ya upimaji wa ardhi nchini imekuwa ya kusuasua kutokana na wataalam, pia vifaa husika. Pamoja na jitihada za Serikali na Wizara kuanzisha utaratibu wa kufungua ofisi husika kwa ngazi ya kanda, bado vifaa havijafika na wataalam wa kutumia vifaa hivyo bado hawajaandaliwa. Katika maonesho tumekutana na kampuni husika na upimaji ardhi wenye vifaa vya kisasa. Gharama ya ununuzi wa vifaa hivyo ni bei rafiki. Kwa chombo cha shilingi milioni 50 wao wanauza shilingi milioni 16. Je, Serikali haioni umuhimu wa kudhamini Halmashauri kupata vifaa hivyo kutoka kampuni hiyo waweze kuwa na vifaa vyao na kuongeza kasi ya upimaji wa ardhi yetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya fedha ni vema ikaona umuhimu wa kuwasilisha fedha zote zinazopitishwa kwenye Bajeti ya Wizara ya Ardhi ili nao wafahamu kuwa ni wadau wa kupiga vita migogoro ya ardhi na uimarishaji wa matumizi bora ya ardhi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ni vema ikaona namna ya kutoa maelekezo ya ulipaji wa gharama ya viwanja kwa wananchi wetu wa kawaida. Pamoja na kuchukua kwao viwanja vidogo, bado uwezo wa gharama anayotakiwa kulipa ni mtihani kwao kwa kipindi cha mwezi,

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wana kiu ya maendeleo, naomba tuwape muda watimize ndoto zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.