Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naenda kuchangia hoja ya Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la migogoro ya ardhi katika Baraza la Ardhi kuchelewa kusikilizwa kutokana na tatizo la kukosa Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi. Tunduru hatuna Mwenyekiti na Baraza la Ardhi ili kusikiliza kesi za migogoro ya ardhi hivyo tunaomba tupatiwe Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi ili kuondoa kero hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la kuchelewa kupitishwa ramani/michoro ya Mji wa Tunduru kwa muda mrefu jambo ambalo linasababisha ucheleweshaji na wananchi kuendelea na mchakato wa kupata hati. Kwa mfano, Halmashauri ilitoa offer ya baadhi ya maeneo ya Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru (Nakayaya) tangu 2011 mpaka 2018, bado wananchi wanaambiwa mchoro haujarudi Wizarani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili linawakwaza wananchi wanaotaka kuendeleza maeneo yao kwa kutumia hati zao. Kukopa pesa benki tunaomba Wizara iangalie upya namna ya kutoa/kupitisha michoro ya Halmashauri mapema ili maeneo yaliyopimwa yapate hati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya vifaa vya kupimia ardhi pamoja na wafanyakazi wenye ujuzi katika kupima ardhi. Kumekuwa na tatizo la wafanyakazi katika Kitengo cha Ardhi jambo ambalo linachelewesha upimaji wa ardhi na utoaji wa hati kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kuna tatizo la baadhi ya wafanyakazi kuendelea na tabia za kupokea rushwa ili watekeleze majukumu yao ya kila siku. Vilevile Watumishi wa Halmashauri Kitengo cha Ardhi bado wanafanya kazi kwa mazoea bila kufuata maadili ya kazi. Vilevile kuna upungufu mkubwa wa Watumishi katika Kitengo cha Ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la fedha. Kitengo cha Ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru kinakumbwa kwa kiasi kikubwa na tatizo la fedha ili kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo linawalazimisha kuwachangisha wananchi wanaotaka huduma ya kupimiwa ardhi na hatimaye kupata hati ili kutekeleza majukumu yao. Hali hii inalazimisha wafanyakazi kutotekeleza majukumu yao na hatimaye kuingia kwenye mtego wa kuomba rushwa ili huduma itolewe kwa wananchi.