Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Rukia Ahmed Kassim

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. RUKIA AHMED KASSIM: Mheshimiwa Naibu Spika, naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai na uzima nami nikaweza kuchangia katika hotuba hii ya Wizara ya Madini. Pili, napenda kuwapongeza Waziri Mheshimiwa Angellah Kairuki pamoja na Naibu Mawaziri wake, kwa utendaji wao mzuri wa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, madini ndicho chanzo kikubwa cha mapato katika nchi yetu. Tuna madini mengi sana katika nchi yetu lakini bado nchi yetu haijaongeza pato la Taifa kwa kiasi kikubwa kwa sababu Serikali haijajipanga kudhibiti madini haya. Bado tuna watu wasioitakia mema nchi yetu, wanayatorosha madini yetu na kuyapeleka nchi jirani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naishauri Serikali ijenge viwanda vya kuchakata madini ili watu wetu waweze kupata ajira. Tuna vijana wengi ambao hawana ajira, wamekaa vijiweni hawana shughuli ya kufanya. Hivyo, naishauri Serikali iwape mafunzo hawa wachimbaji wadogo wadogo ili na wenzao wakiona hawa vijana wamefanikiwa nao wataacha kukaa vijiweni watajishughulisha na huu uchimbaji na watajikwamua kimaisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho namalizia kwa kusema kwamba mikataba ya madini iangaliwe upya imepitwa na wakati haileti maslahi kwa Watanzania.