Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kutoa mchango wangu katika Wizara hii ya Madini. Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetujalia afya na uzima wa kufikia siku ya leo na kutoa michango yetu katika Wizara hii muhimu kwa uchumi wa Taifa letu na tunafaidika na baraka hii aliyotupa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nichukue nafasi hii kuipongeza Wizara hii kwa ujumla, kuanzia Waziri wa Madini, Mheshimiwa Angellah Kairuki, Naibu Mawaziri, Mheshimiwa Nyongo na Mheshimiwa Biteko, pamoja na Katibu Mkuu na watendaji na wataalam wote wa Wizara kwa utendaji wao mzuri na weledi, hata kama Wizara hii ni mpya lakini wamefanya mambo makubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya shukrani na pongezi hizo, sasa nianze kutoa mchango wangu. Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa mikoa michache nchini yenye madini mengi na ya kila aina ikiwemo Wilaya ya Morogoro, hususan Morogoro Vijijini, lilipo Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki. Miongoni mwa madini yanayopatikana ni marble, ruby, dhahabu, graphite, manganese, garnet, emerald, corundum, ulanga, limestone, urani na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na wingi wa madini hayo katika maeneo yetu, lakini bado hayajatunufaisha ipasavyo wananchi wa maeneo hayo. Tumewahamasisha wachimbaji wadogo wadogo kujiunga pamoja ili kutambulika kisheria na kuweza kuaminika na kujipatia mtaji wa pamoja kutoka katika taasisi za fedha na mabenki na kuweza kujipatia vifaa vya kisasa na kuchimba kwa tija na faida kubwa na kujiongezea kipato chao na Taifa kwa ujumla. Hata hivyo mpaka sasa vikundi hivi havijapata vibali na leseni kutoka Wizarani kwa muda mrefu na kurushwa kama mpira mara waende wilayani, mkoani, Dodoma au Wizarani Dar-es-Salaam. Namuomba Mheshimiwa Waziri wakati anafunga hoja anieleze tatizo ni nini hata inachukua muda mrefu kuvipa vibali na leseni vikundi hivi?

Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ni kuhusu Sheria mpya ya Madini ya kutosafirisha nje ya nchi madini ghafi mpaka yawe yameongezwa thamani ndani ya nchi. Pamoja na nia hiyo nzuri kwa Serikali yenye lengo la kuongeza ajira kwa Watanzania, pato la fedha za kigeni, pamoja na kuitangaza nchi yetu nje ya Tanzania katika soko la kimataifa, nashauri Serikali ikaliangalie suala hili kwa upana zaidi kwa sababu, kuna madini mengine kama ruby na marble yanatumika kutengeneza bidhaa za mwisho tofautitofauti. Ruby ukiikata unapunguza thamani na inapatikana sehemu mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.