Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Naibu Spika, napongeza hotuba ya Kamati ya Madini, lakini pia naipongeza hotuba ya Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Rukwa hakuna shughuli za uchimbaji mdogo mdogo wa madini wala uchimbaji mkubwa. Hii ni kutokana na kutokufanyika kwa utafiti wa kujua aina ya madini yanayoweza kupatikana kule. Naamini kazi ya utafutaji ingefanyika wananchi wa Rukwa wangeweza kunufaika na rasilimali hii muhimu, tafadhali Wizara fanyeni hiyo kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Rais kwa usimamizi wake muhimu katika eneo hili. Leo tanzanite inaanza kulitangaza Taifa. Udhibiti uliowekwa kwa kujenga wigo utapandisha mapato ya nchi kwa tanzanite.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kujua, ni lini fedha za makinikia zitapatikana? Je, ndiyo mwisho? Kwa vile Serikali ilituambia hapa kuwa kutapatikana fedha ingetamkwa wananchi wajue ili waone juhudi za Serikali yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kuna mgodi wa makaa ya mawe jimboni kwangu unaitwa Mkomolo unaofanywa na mwekezaji Edenville. Naomba utaratibu ufanyike ili ikiwezekana waweze kufua umeme na uingie kwenye Gridi ya Taifa. Hii itasaidia kuwa na vyanzo tofauti tofauti vya nishati na huenda kwa kufanya hivyo bei ya nishati ya umeme inaweza kupungua na kuimarisha huduma ya upatikanaji wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, Rukwa Kusini kuna helium, Tanganyika kuna mafuta, tuanze basi kuchimba rasilimali hizi ili kukuza uchumi wa taifa na Mkoa kwa ujumla.