Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ya kuchangia Wizara ya Fedha na Mipango. Kwa lugha nyepesi kabisa adui namba moja wa maendeleo ya Taifa hili ni Wizara ya Fedha na Mipango. Adui namba moja na nina sababu, sababu namba moja Wizara ya Fedha inashindwa kutoa fedha ambazo zipo kisheria namba moja.

Mheshimiwa Spika, hili nalisema, nenda kwenye ripoti ya Mkaguzi, angalia fedha ambazo Wizara kwa kupitia TRA wamekusanya na ambazo wamepeleka na zile ambazo hawajapeleka, hawapeleki fedha. Leo ukienda kuangalia watu wa korosho wanalalamika, wamekuja watu wa Bodi ya Korosho kwetu wamelalamika juu ya Wizara ya Fedha wamekusanya bilioni 91, wamepelekewa bilioni 10, fedha yao halali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, railway development levy, hakuna hata senti iliyopelekwa kule, angalia kila kifungu Wizara ya Fedha wana sababu moja tu wanasema siku hizi uhakiki, yaani Serikali hiyo moja kigezo chao ni uhakiki na ndio kichaka cha kujifichia kutokupeleka fedha.

Mheshimiwa Spika, Mawaziri hapa wanakuja wanalia fedha hakuna na fedha zao ambazo zipo kisheria, wao jukumu lao ni kuchukua, kukusanya na kurudisha kule, hawafanyi wanalitakia mema Taifa hili, the answer is no, hawatakii mema Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, fedha za miradi ya maendeleo angalia kilimo chini ya asilimia 10, miradi ya maendeleo; viwanda ambavyo ndio tunahubiri, Wizara ya Viwanda na Biashara asilimia tisa, leo uchumi wa Taifa ambao tunalia kwamba tunakwenda kwenye uchumi wa viwanda
unapeleka asilimia tisa na Wizara hawawezi kuleta majibu hawa na tunawaona. Pia wana sababu za ajabu, maagizo kutoka juu, maagizo gani, yaani huko juu ni wapi mbinguni yaani ambako sisi kama Taifa hatuwezi kufika.

Mheshimiwa Spika, hivyo tuulizane swali dogo, unapoagizwa kutoka juu, hivyo mtu anayekuagiza kuvunja sheria you need to know one thing. Leo mpo ninyi, kesho utawala utakuja awamu nyingine, itakuja Awamu ya Sita atakayekuwa responsible ni ninyi Mawaziri kwa sababu sisi hatutamgusa Mheshimiwa Rais ana kinga Mheshimiwa Rais yoyote yule awe ni Mheshimiwa Dkt. Magufuli, afanye chochote kibaya ana kinga, ninyi hamna kinga tutawachukulia hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa haya ndio ambayo yanapelekea haya madudu kuendelea kufanyika na tumekuwa tukishuhudia kila wakati, sasa kuna maamuzi ambayo Wizara inayafanya ambayo sisi kama Taifa ndiyo tunaingia hasara, kwa mfano unajua unapojenga reli ya standard gauge ni jambo jema na sisi kama wananchi hatupingiki tunakubaliana na hilo jambo, lakini unapoamua kukopa mkopo wa kibiashara kwenda kuhudumia reli ambayo malipo yake ni baada ya miaka 20 ni kuliingizia Taifa hasara, yaani unatumia current asset to finance the long term liability, ni nini ninachokisema? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mikopo ya mabenki wanakupa muda wa grace period ya miezi sita, mradi wako hujakamilika unaanza kulipa fedha, lakini ukitumia concessional loan ni watu wanakwenda kwenye mradi, wanatekeleza mradi, mradi unakwisha, baada ya mradi kuisha unapewa muda fulani miaka mitatu, baada ya hapo ndio unaenda kuwalipa. Sasa leo hii miradi ni mema Kwa Taifa lakini tutaanza kulipa kabla miradi haijakamilika.

Mheshimiwa Spika, baada ya miaka 20 ndio mradi ile pay back period yake kuanza kutoa faida ndio unaanza kuiona, unajua matokeo yake ni nini? Hakuna maendeleo yatakayoendelea kufanyika, ndio maana leo tukija humu ndani kilimo wanalia, afya wanalia, elimu wanalia, maji wanalia, hakuna mradi unaofanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa haya wanaosimamia ni Wizara ya Fedha, sijawahi kuona Wizara ambayo inashindwa kuelewa kama Wizara ya Fedha na hii inabidi uwe mkali sana, bila kuisimamia Wizara ya Fedha kupeleka fedha hizi zote tunazosema hapa ni ngonjera, kwa sababu kila kilichoandikwa mwisho wa siku lazima kitafsiriwe na fedha iende pale. wanatamka mapato yameongezeka, sisi tunashangilia huko mtaani, haya tuonyesheni hela basi, hazionekani.

Mheshimiwa Spika, lLeo unakwenda angalia tu mfano mdogo tu deni la Taifa ndani ya miezi 12 wamekopa trilioni saba, hilo deni limeingia kwenye deni la Serikali, trilioni saba, haya waambieni hili deni la trilioni saba hela zake basi tuonyesheni na zile mlizokusanya ndani tuonyesheni vilevile tuone hii miradi na utekelezaji wake mnafanyaje wanakwambia tu hili ni himilivu kwa asilimia 34.4 ukomo wetu ni 56%, hawazungumzii tax to GDP yaani makusanyo ya kodi against pato la Taifa, tuko kwenye 14.5%, ndio ambayo tuko sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa duniani kote siku hizi watu walishaacha kutumia mfumo wa debt to GDP siku hizi watu wanatumia mfumo wa kodi kwa pato ghafi la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana umenielewa. Tunakumbushana, ni Mwalimu lakini ni mwananadharia. Mimi nayaishi haya maisha practically. Hii ndiyo changamoto inayo-face nchi. Maprofesa wengi wamefeli kwenye uongozi duaniani kote walipokabidhiwa. Kwa sababu hivi vitu, unajua kuzungumza na kutekeleza ni vitu viwili tofauti. Sasa hilo tumezungumza, tunaona hali halisi. Sasa kuna mambo mengi ambayo hawa wanasimamia, leo wanasimamia rufaa za kodi, angalia kule, kuna rufaa kibao; lakini wanasema ili tumsikilize mtu tupokee ombi lake lazima ulipe moja ya tatu ya kodi. Ndiyo kazi ya Wizara ya Fedha, yaani ni kukandamiza.

Mheshimiwa Spika, angalia mikakati yao Wizara ya Fedha. Mikakati yote ni kodi, kodi, ongezeko la kodi. Hakuna mahali popote wanayoweza kukuonesha namna watakavyozalisha ama namna ya watakavyotengeza mkakati wa wale watu wetu kwenda kulipa kodi. Hawa ndio wanaosimamia, sisi tunawahoji kila siku. Kuna majibu mengine tunayavumilia, lakini kiukweli wanataka kuvuna mahali ambapo hajawapanda, ndiyo kitu kibaya sana ambacho hawa watu wanacho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tatizo lingine ambalo wanalo, ni kutokutaka kuelewa. Kama walichokipanga wao wameshakipanga, maelezo yote tutakayotoa ndani ya Bunge hakuna jambo lolote watakalolisikia. Hilo ndilo tatizo. Wizara ya Fedha ina kiburi cha hali ya juu, sijawahi kuona katika nchi hii!

Mheshimiwa Spika, imezungumzwa hapa awali, wamejikita kwenye fedha, kwenye mipango ni kama hamna. Hiyo ndiyo imekuwa changamoto katika nchi hii kwa miaka mingi. Yaani inapofika suala la mipango, waulize hawa Mipango, ndiyo hii mipango inakuja mambo mapya. CAG ameshatoa mapendekezo mengine, wao wenyewe wanayakimbia. Haya yote ni kwa sababu wanashindwa kutusikiliza, wanashindwa kuelewa.

Mheshimiwa Spika, ubaya sana kwenye hizi nchi, inafika mahali watu wanawaachia haya nendeni basi tuwaone, mtafikia wapi? Mtashindwa! Sasa ninachofahamu, Mheshimiwa Rais anahitaji kushauriwa vizuri. Yeye ni binadamu, hata kama kuna wakati ana-push jambo ukimwelewesha usiku atalala peke yake, atasema lakini lile jambo Mheshimiwa Waziri Mpango alinimbia kweli. Sasa ile akikwambia tu “nimesema kuanzia leo, toa hela hizi peleka huku.” Unasema sawa mzee. Hakuna Taifa la namna hiyo! Lazima umwambie hapana Mheshimwa Rais. Nitatekeleza hilo jambo lako, lakini lazima tufuate utaratibu. Ni mambo ya kawaida. Hata Mbinguni kule kwa Mungu ili uende Mbinguni lazima ufuate utaratibu, hakuna dunia inaendeshwa bila utaratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haya ndiyo yaliyotufikisha leo hapa. Ni kwa sababu mambo mengi na fedha nyingi, zinakwenda bila utaratibu. Mwisho wa siku wanasema mali bila daftari huishia bila habari. Kwamba unaweza ukakusanya mali nyingi, lakini kama unashindwa kurekodi, kuwa na mipango, yaani hutafanya kitu chochote. Miaka mitano; imebaki miwili, itakwisha, mtakuja na the same story. Mtaishia kupiga kelele tu kwamba tumetekeleza; tuonesheni mlichokitekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, shilingi milioni 50 kila kijiji, ipo kwenye rekodi hapa; leo mwaka wa wangapi? Wa tatu huu, ndiyo bajeti ya tatu; tumebakiwa na bajeti mbili tu. Wanatenga, lakini hawajapeleka hata shilingi mia. Ipo kwenye taarifa yao. Walitenga shilingi bilioni 59, wakasema tunakwenda kwenye pilot study; hawajapeleka hata shilingi mia. Mwaka 2017 wakatenga shilingi bilioni 60, hawajapeleka hata shilingi mia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa tukija tukiwahoji tunaonekana tunakosea, lakini ni kweli hizi takwimu wameziandika wenyewe; wanaotudanganya ni wao wenyewe; lakini yote hii ni kwa sababu wanaamini sisi hatuelewi. Sisi tunajua, tunaweza kuwa katika ujinga wetu tunaelewa kidogo, lakini kwenye hiki cha ujinga kinatoka kwa wananchi. Wewe unafika Jimboni mtu anakuuliza, Mheshimiwa Mbunge shilingi milioni 50 hazijaja hapa kwa sababu wewe Mbunge ni mzembe, lakini unajua kabisa ni kwa sababu Mheshimiwa Waziri wa Fedha kasema hela itakuja. Namwuliza hela iko wapi? Anakwambia hela itakapopatikana. Si mmetuelezaa hela zipo nyingi huku! Sasa hilo ndiyo tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.