Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 1966 Chinua Achebe aliandika kitabu cha A Man of the People na kwenye kile kitabu kuna character mmoja anaitwa Chief Nanga. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chief Nanga alikuwa mwalimu na baadae akawa Waziri. Na nikiangalia ile picha ambayo Chinua alikuwa anajaribu kui-portray kwenye uandishi wake na nikiiangalia Tanzania leo, namuona Chinua Achebe alikuwa anaandika kuhusu Tanzania. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri Mpango ameleta vitabu hapa, vingi sana anazungumza kuhusu mipango ya Taifa ya maendeleo ambayo kila mwaka tunaijadili hapa. Kwenye mipango yake Waziri Mpango, mwalimu hajazungumza kuhusu kuongeza mishahara ya watumishi ambao ndio anategemea wampe ufanisi kwenye utendaji kazi wake. Hajazungumza kuhusu ajira mpya, huyu Waziri Mpango na Serikali yenu, mmekuwa leo ni propaganda. Watu wakitaka kuzungumza mnageuza lile jambo, lionekane ni jambo baya kwenye society na watu waonekane wanatumiwa na mataifa ya nje. Kuna kauli imekuwa maarufu sana, wanatumiwa kuhujumu uchumi na watu wasiopenda Taifa letu. Hawa watu hamuwataji lakini wapo mnawajua ninyi.

Sasa Waziri Mpango wewe unaishi maisha mazuri kama uzalendo ni kuwa masikini kuishi vibaya, kuendesha gari mbaya tuoneshe wewe mfano huo wa uzalendo, kwa nini wewe huutaki huo uzalendo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huo uzalendo wa kutokukaa sehemu nzuri ambao mnataka muwaanimishe Watanzania kwamba uzalendo ni umasikini, kwa nini wewe huupendi huo uzalendo? Kwa nini unaendesha V8 ya Serikali, mafuta ya Serikali, una wasaidizi, nyumba nzuri wote humu Bungeni. Hampendi uzalendo ninyi, mnataka uzalendo huo kwa watumishi wa umma tu. Watoto wa watu wamemaliza

shule. Mwaka 2015 Serikali yenu hii inayokusanya mapato kuliko Serikali zote zilizopita haijaajiri mwaka 2015, hamjaajiri mwaka 2016, hamjaajiri mwaka 2017, hamjaajiri mwaka 2018. Na mnakunakusanya kuliko wote.

Sasa tuje kwenye takwimu zenu, Serikali tukufu mnaokusanya kuliko wote, mwaka 2016/2017…

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mwaka 2016/2017 Serikali hii inayokusanya kuliko zote ilitenga bajeti ya maendeleo shilingi trilioni 11.8 kwa mujibu wa kitabu cha Kamati. Pesa za maendeleo zilizokwenda ni shilingi trilioni 6.4 ambayo ni asilimia 55.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana ni nini, maana yake ni kwamba asilimia 45 ya miradi yote ya maendeleo iliyopangwa haitafanyika kwenye mwaka huo asilimia 45 ya miradi ya maendeleo. Ina maana shule asilimia 45 hazikujengwa, maji asilimia 45 hayakwenda kwa wananchi, barabara asilimia 45 hazikutengenezwa, miradi yote iliyoibuliwa kutoka kwa wananchi 45% haikutekelezwa, Serikali Tukufu inayokusanya kuliko zote ya akina Mpango. Mkikaa hapa mnaimba Stiegler’s Gorge, SGR, flyover kana kwamba mwananchi wa kijijini kwangu kule Nyamwaga au Nyanungu anajua SGR maana yake ni nini au mwananchi wa kijijini kwetu kule Sirari anajua flyover ya Dar es Salaam inamsaidiaje. Leo mmekuja hapa unatuambia kwenye kitabu chako Mpango kwamba kilimo kimekuwa 7.2; sasa mimi nakuuliza Mpango, kilimo kilichokuwa kwa asilimia 7.2 mmenunua mahindi kiasi gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inayokusanya kuliko zote mmeingia mmekuta gunia la mahindi shilingi 100,000, sasa hivi gunia la mahindi haliwezi kununua hata mfuko mmoja wa mbolea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili ununue mfuko mmoja wa mbolea, unahitaji kuuza mahindi gunia tatu, Serikali inayopigania wanyonge, wanyonge mnaojiita ni ninyi mnaoendesha V8. Lakini mnyonge wan chi hii hakuna mnyonge hata mmoja mnaempigania, na mimi nilitegemea Mheshimiwa Mpango muingie hapa, msijisifu Serikali ya wanyonge tuambieni mlikuta wanyonge milioni ngapi, na kwa miaka mitatu mmepunguza wanyonge milioni ngapi, mnataka ku- indoctrinate watu mambo ya ajabu, mnataka kuwaaminisha watu kwamba eti umasikini ni sifa, wakati nyie wenyewe mnaogelea kwenye maisha mazuri. Mnakuja hapa mwaka uliofuata mmetenga bajeti ya maendeleo shilingi trilioni 12 na bila aibu kila mwaka mnaongeza digit na namba hazidanganyi. Mwaka huu mmetenga shilingi trilioni 12 mkatoa ile ile shilingi trilioni sita asilimia 57, sasa mimi najiuliza hizo pesa Mheshimiwa Mpango mnazotuambia mmekusanya kuliko wote mnalia au ziko wapi? (Makofi/Kicheko)

Kwa sababu kwa wananchi hazipo, kwenye ajira hamna, kwenye barabara hatuoni, kwenye Halmashauri leo mnaondoa Capital Development Grant (Local Government Capital Development Grant) mmeiondoa kwa sababu kila siku inawaletea query hamjapeleka hata shilingi mia moja, Tarime mwaka 2016 hamkupeleka, mwaka 2017 hamkupeleka, mwaka 2018 hamkupeleka. Pesa zote tunazofanyia maendeleo tumejenga vituo, tumejenga barabara, own source ya wananchi wa Tarime hakuna shilingi mia moja mlioleta Mpango, pesa hizo ziko wapi? Ziko wapi hizo pesa ambazo mnakusanya?

Haya mmekuja hapa wewe Mpango unaesema unakusanya sana na mkasema mnaweza kununua kama mnanunua ndege mtanunua korosho na wakulima jana, wanunuzi wa korosho jana wametoa statement kwamba hawatanunua tena korosho na mimi namtaka Waziri Mpango wakati anajumuisha hapa atuambie wananunua korosho za wakulima zote ambazo ziko kwenye maghala, kwa sababu hili jambo mliambiwa hapa wananchi walipanga kufikia mwezi wa tisa huu, mwezi wa kumi, mwezi wa 11 wao wameuza korosho zao wapeleke watoto wao shule. Wawe wameuza korosho zao wanunue walau bodaboda, wengine walipe kodi za nyumba, wengine wafanye nini, tunataka Waziri Mpango unapokuja hapa jibu la kwanza utuambie kwa sababu mlisema mtanunua korosho, utuambie mnaanza lini kununua korosho na kwa bei ya shilingi 3,000 kwenda juu hakuna kushuka hata shilingi 100. (Makofi)

Ninyi msifikiri Watanzania hawawaoni haki za binadamu zina tolerate, watu wameuawa Waziri pale anasimama anasema aseme Waziri, aseme polisi aliyeua mtu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi mdogo wangu ameuawa kituo cha polisi halafu mnasimama hapa mnasema eti polisi hawaui watu! Mheshimiwa Zitto juzi ametoa taarifa polisi wameua watu wengi hamjaita kuhoji, mmeita kumtishia na yuko hapa na Zitto mimi nataka uendelee kusema humu Watanzania wajue hatusemi uongo. Mnatishia watu wanaowashauri, mnawawinda wengine tunaishi kwa kuhamahama kwa sababu mnatuwinda kila dakika.