Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii nami niweze kuchangia Mpango wa Serikali.

Kwanza kabisa ni pongeze Serikali ni mpongeze Rais wangu John Pombe Magufuli, kwa kazi kubwa anayoifanya, lakini kwa kweli kwa dhamira ya dhati kabisa nimpongeze Waziri Dkt. Mpango hakika Dkt. Mpango amekuwa mvumilivu, amekuwa kiongozi wa mfano, amevumialia mno matusi maneno lakini amefanya kazi kubwa ndani ya miaka mitatu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano Waziri Mpango amefanya kazi kubwa ya kuleta nidhamu ya kuleta pesa za umma, wote tunajua, mmejenga mfumo sahihi ya ukusanyaji wa kodi hakuna asiyejua, kila mwaka mapato yetu ya ndani ya kodi na yasiyo ya kodi yanakuwa yakiongezeka hii yote ni kazi ya Dkt. Mpango, Naibu wake, na Wizara nzima ya Fedha mimi binafsi kwa dhati yangu nawapongezeni sana. Maana kila siku tunawasema kwa mabaya yale mema wanayoyafanya tunashindwa hata kuwatia moyo. Kwa kweli Uwaziri wa Fedha ni kazi kubwa sana lazima tuwapokengeze. (Makofi)

Nimesikia wapinzani wanasema utekelezaji wa bajeti hauridhishi, lakini hawasemi bajeti hii imekuwa ikiongezeka kila mwaka, hawasemi wanasema tu kwamba hairidhishi, kwa sababu tulianza na asilimia arobaini na kidogo tukafata na asilimia hamsini na kidogo sasa hivi tupo na asilimia 57 lakini hivi asilimia 57 zinaonekana kazi inayofanyika inaonekana unaweza ukasema tumetekeleza kwa asilimia 80 lakini ukiangalia kazi haionekani hakika Serikali inafanya kazi kubwa na inastahili kupongezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Nimesikia kuna Mheshimiwa Mbunge amesema Mheshimiwa Rais atamaiza kumi hakuna kilichofanyika amenishangaza sana, mimi niwaambieni niwaombe mchukue kalamu na karatasi, niwaambie Rais Magufuli ikifika mwaka 2020/2025 ataacha legacy kubwa hata sahaulika katika nchi hii ya Tanzania, naomba niwaambie Rais Magufuli ataacha amejenga reli andikeni? Msinitizame Rais Magufuli atajenga Stiegler’s Gorge na umeme huo mtautumia kwa bei rahisi. Rais Magufuli ataacha amejenga zahanati za kutosha, amejenga vituo vya afya vya kutosha mpaka sasa hivi vituo vya afya ni zaidi 300 ndani ya mikaka mitatu, lakini toka tumepata Uhuru tumejenga vituo vya afya 500 Rais Magufuli miaka mitatu amejenga 300 leo unaniambia Rais Magufuli ataacha amefanya chochote ndani ya nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mimi nasema viongozi wetu labda akili zao zimezidi maana wanafanya mambo makubwa ambayo hatukuyategemea, hatukutegemea kabisa kwamba Rais anaweza kutujengea reli ya kisasa, hatukutegemea kama watoto wetu watasoma elimu bure, lakini leo watoto wetu pamoja na wakwenu wanasoma elimu bure.

Hatukutegemea kama mikopo ya vyuo vikuu kuongezeka kwa kiwango hiki, lakini leo watoto wetu wanapata mikopo na wanasoma. Hatukutegema upanuzi mkubwa unaoendelea wa viwanja ndege, upanuzi wa bandari, ujenzi wa flyover, ununuzi wa ndege ambao na wao wanapanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu anayesema mpango huu haufai mimi nasema mpango huu unafaa na unaendelea vizuri. Nimesikia Mheshimiwa Mbunge anaongelea kwamba hakuna ajira tangu Rais Magufuli ameingia, jamani tuone aibu, tumuongope Mwenyezi Mungu sisi wote tuna dini humu ndani, tumeapa kwa bible na wengine tumeapa kwa misahafu tumuongope Mwenyezi Mungu, tumeajiri walimu 13,000, tumeajiri watu wa afya 8,447 na tumeajiri watendaji wa kata, lakini kila siku ukifungua website ya Wizara ya Utumishi wanatangaza nafasi za kazi juzi tu nilifungua namtafutia mwanangu nimeona UTT wametangaza, nimeona SUMATRA wametangaza, nimeona TANESCO wametangaza, nimeona Bandari wametangaza, leo hii mnakuja mnasema hakuna ajira muogopeni Mwenyezi Mungu, pale tunapofanya kazi nzuri semeni mmefanya kazi nzuri, pale tunapokosea sio mseme jumla kwa chuki zenu binafsi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia wenzetu hawa sana wanaongea kuhusu swala zima la Katiba, kwamba Katiba imeachwa, Katiba imefanya nini mimi niwaambie ndugu zangu hawa waache kutafuta kiki za kisiasa, tulivyokuwa kwenye Bunge la Katiba walitoka nje, Katiba ilipitishwa na watu wachache kwa busara ya viongozi cha Chama cha Mapinduzi wakasema mapendekezo ya wachache yatachukuliwa na yatakwenda kuwaambia wananchi kupendekeza Katiba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mara ya kwanza walijiunga kama UKAWA wakatembea nchi nzimaya Tanzania kwamba Katiba isiungwe mkono iliyopendekezwa leo nawashangaa watu hawa yametoka wapi leo nawashangaa watu hawa wanaililia Katiba ninyi si mlikwenda nchi nzima kusema Katiba inayopendekezwa isichukuliwe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu hawa walienda nchi nzima wakajiunga UKAWA wakaanza kusema Katiba iliyopendekezwa isiungwe mkono leo nashangaa wanasema Rais anakataa Katiba Mpya, mimi naomba nimuombe Rais wangu asitoke kwenye reli, Rais Magufuli wakati anaomba kura aliwaahidi Watanzania maendeleo, hakuwaahidi Watanzania Katiba, wananchi wanataka maendeleo, wananchi wana taka reli, wanataka zahanati, wanataka maji wanataka dawa, wananchi awataki Katiba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kuna mkakati, wa kumtoa Rais Magufuli achukuwe mamilioni aweke kwenye Katiba tushindwe kutimiza malengo waje watuhoji, mimi niwaambie hatutakubali. Mhe.Rais usikubali ujinga huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Katiba limeeleweka naomba sasa kuhusu suala zima la usalama. Kumekuwa na masuala ya usalama yanaongelewa kwamba nchi hii haina usalama, nchi hii watu wanatekwa, nchi hii watu wanauwawa, suala la usalama ni suala la janga la dunia, Marekani wanalindwa kwa mitandao kwa mitambo kwa satellite lakini nikwambie kwa siku wanatekwa zaidi 240 kwa siku. Mimi nadhani imefika wakati sisi Wabunge tupige kelele tuiambie Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi iongeze pesa kwenye vyombo vyetu vya usalama, iongeze training za vijana wetu wa usalama, training za polisi, training za jeshi letu ili kukabiliana na janga kubwa lililopo la uwalifu katika nchi yetu linalotaka kuingia hili ni janga la dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumesikia juzi mwandishi wa habari kule ametekwa, ameuwawa mpaka leo wenzetu wale wamesonga mbele kiteknolojia bado hawajapata uhakika nani kafanya. Lakini leo likitokea Tanzania imefanya Serikali, mimi napata taabu Mwenyekiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natoka Tabora kutoka nikiwa mdogo kule kwetu mauwaji ya vikongwe yanaendelea, mauaji ya kimapenzi yanaendelea, wanauwaga polisi kila siku? Mbona yapo na Serikali zote zipo zimepita na Serikali zinapambana na hayo mambo.

Kwa hiyo, mimi nitoe rai yangu Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu unanisikia upo humu ndani, niombe sana Serikali iongeze pesa kwenye vyombo vya usalama, wakawasomeshi watu waweze kukabiliana na teknolojia za hawa watu wahalifu wao na teknolojia za kisasa na sisi tupate teknolojia za kisasa ili tuweze kukabiliana nao ili ndiyo naweza kulisema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kidogo Tume Huru ya Uchaguzi watu hawa wamekuwa wakiongea kwamba tunataka tume huru Katiba mpya ibadilike mimi naomba niwaulize humu ndani wapo zaidi ya asilimia 30 waliingiaje kama hakuna Tume Huru waliingiaje ndani watu hawa, wamezidi zaidi ya 100 tupo Wabunge 300 na kidogo wenzetu hawa wako zaidi ya 100 walifikaje humu ndani kama wako zaidi 100 kama hakuna Tume Huru ya Uchaguzi wasitake kututoa barabarani, wasitake kututoa kwenye reli tunataka maendeleo kama anavyosema Rais wetu John Pombe Magufuli. Tunamuombea kila heri Rais wetu amkinge na mapala na manuksi ya maneno yenu ya ajabu ajabu inshallah. Ahsante kwa kunipa nafasi hii.