Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niungane na wenzangu kujadili Mpango huu wa mwaka 2019/2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii ya kuishukuru Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais wetu mpendwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli pamoja na Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa, pamoja na Mheshimiwa Spika na Waheshimiwa Wabunge wote kwa kazi nzuri ambayo leo tunaijadili hapa ya Dkt. Mpango, kwa kupitisha bajeti ile ambayo tulikuwa tunakaa hapa na ndio sasa tunayaona yaliyokuwa yanafanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mpango tunakupongeza sana na timu yako na wataalam wako na Naibu Waziri kwa kazi nzuri ambayo ipo mbele yetu, kwa kweli lazima tuwe wakweli, nianze na Wizara ya Afya, Mheshimiwa Mpango imezungumzwa hapa kuna baadhi ya watu wanasema bajeti iliyoongezeka zaidi ya bilioni mia mbili na kitu bado hawaoni maana yake, mimi nimebaki nashangaa Waheshimiwa Wabunge. Hivi bajeti ile si baadhi ya vituo, zahanati na vituo vya afya ambavyo vimejengwa si lazima fedha ziongezeke? Kazi nzuri imefanywa sana na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti kazi nzuri iliyofanywa na Serikali ikiwepo kwenye jimbo langu vituo afya viwili vimeongezeka na hospitali ya Wilaya ya Halmshauri, lazima tuipongeze Serikali kwa kazi nzuri ambayo inafanywa hivi sasa kituo cha afya kwenye jimbo langu mwezi wa pili kinafunguliwa kwa fedha ambazo Serikali ya Awamu ya Tano kama walivyosema wenzangu vituo zaidi ya 300 na kila Jimbo nadhani vituo hivyo vipo. Kwa hiyo, naipongeza sana Serikali hata mwenzangu jirani ananiambia hata Tarime vipo, eeh kwa hiyo lazima tuipongeze sana Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile tukija kwenye upande wa maji, mwenye macho haambiwi tizama maji katika nchi nzima asilimia kubwa imepungua hata kwenye jimbo langu tu suala la maji ipo miradi inaendelea pale iko miradi mingi katika jimbo langu, ni fedha tu kwa hiyo Mheshimiwa Mpango tunakupongeza. Ipo miradi ile 26 ya maji katika nchi, katika miradi 26 mradi mmoja upo kwenye jimbo langu katika mpango huu wa wewe Mheshimiwa Mpango. Sasa tunaipongeza sasa Serikali ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija miundo mbinu ya barabara za kuunganisha mikoa kwa mikoa, leo mtu anatoka kule Mbinga kwa Mheshimiwa Mapuda, anatoka Mbinga asubuhi ikifika usiku anakuwa Mwanza, barabara zimetengezwa ni fedha hizi za Awamu ya Tano. Kwa hiyo tunaipongeza sana Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija barabara pale kwangu pia kwenye jimbo langu barabara za lami zinatengenezwa, ukitoka pale iko barabara ambayo barabara kuu ya kutoka Dar es Salaam - Zambia sasa hivi kwenye jimbo langu pale Makambako barabara na viunga vyake vinapendeza sana, kwa hiyo tunaipongeza sana Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzangu wamezungumzia hapa reli wenzetu wa kanda ya ziwa wamekuwa wakipata taabu sana juu ya reli hii ya kati, Serikali imechukua jukumu ya kuishughulikia reli hii, watu wanasema aaa mpango sio reli; kupanga ni kuchangua. Tunakupongeza sana Mheshimiwa Mpango kwa namna ambavyo umeelezea hapa kwamba reli hii lazima inakamilika songa mbele kama alivyosema mwenzangu Mheshimiwa Ndassa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ukija upande wa ndege, nimewahi kusema hapa Bunge la mwaka 2013 hapa na baadhi watu walikuwa wanazungumizia hapa duniani kokote kule hamuwezi kuwa mkawa hamna ndege za nchini kwenu, Rais amechukua jukumu la kununua ndege katika nchi yetu, tunaipondeza sana kwa taarifa hii ambayo kuna ndege zingine zinakuja mwakani mwezi Novemba, tunakupongeza Dkt. Mpango na Serikali ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kazi nzuri ambapo ndege hizi zitapunguza kero mbalimbali ambazo watu walikuwa wanapata tabu kusafiri lakini zitaongeza utalii wa ndani, Mheshimiwa Mpango songa mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipofanya ziara kwenye Jimbo langu mikutano 65 nimefanya kila siku nilifanya mikutano mitatu hakuna mwananchi hata mmoja aliporuhusiwa kuuliza maswali aliyezungumzia Katiba hayupo hata mmoja hayupo! Hata mmoja hayupo, watu walikuwa wanaauliza habari ya maji, barabara, pembejeo na kadhalika hakuna. Sasa leo tuanze kupoteza fedha kwa ajili ya Katiba, niombe sana Serikali na Rais na Waziri Mkuu upo hapa msijadili habari Katiba wananchi sio tatizo Katiba. Tatizo ni maendeleo katika maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa kazi iliyofanya Serikali ya Awamu ya Tano, tumuombe Mheshimiwa Spika na Wabunge wote baada ya kumaliza Bunge hili sijajua linaisha lini tufanye party ndogo ya kuipongea Serikali kwa kazi nzuri iliyofanywa, kwa hiyo, nikuombe Mwenyekiti jambo hili lipewe kipaumbele tufanye party ndogo ya kuipongeza Serikali kwa namna ambavyo inafanya kazi na leo narudia, kwa kazi iliyofanywa kwa miaka mitatu unadhani ni kazi ya miaka 20 huo ndio ukweli. (Makofi)

Sasa narudia kwa maneno haya niliwahi kusema Bungeni hapa, Rais wa China kwa kazi nzuri amekuwa akifanya na Marais wengine nchi mbalimbali wenzetu kule walisema awe Rais wa maisha. Narudia Rais huyu awe Rais wa maisha kutokana na kazi nzuri anayoifanya, lazima tuwe wa kweli, lazima tuwe wa kweli hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya maelezo hayo naunga mkono hoja, ya Mpango wa Dkt. Mpango kwa kazi nzuri, songa mbele na nakushuru sana.