Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Ajali Rashid Akibar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nichukue nafasi hii kukushukuru kunipa nafasi ili nitoe mchango kwa mpango huu ambao ndugu yangu, Mheshimiwa Dkt. Mpango, anaufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumsifu Mheshimiwa Dkt. Mpango, Waziri wa Fedha, kwa mipango yake, yeye ni mtaalam sana katika kuandaa mipango hasa ya kukusanya kodi. Ila tatizo la Mheshimiwa Dkt. Mpango ambalo mimi huwa naliona siku zote ni kwamba hafanyi coordination kati ya mpango mmoja kwa maana ya kwamba kushirikisha wale watu ambao wanazalisha, kwa mfano kushindanisha watu wa kilimo, watu wa uchumi na watu wa viwanda na kilimo kinaingiaje, yaani hao mahusiano hao watu anawezaje kuwaweka pamoja wakahusiana. Maana yake akishafanya coordination kati ya hivi vitu vyote basi Mheshimiwa Dkt. Mpango atakuwa mzuri sana katika bajeti. Kwa hiyo mimi naomba Mheshimiwa Dkt. Mpango nimshauri kwa mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Dkt. Mpango, kabla ya uhuru au baada ya uhuru mwaka 1961 na baada ya uhuru, Mheshimiwa Rais wetu mstaafu ambaye ni hayati sasa hivi, Baba wa Taifa alikuwa na Jeshi maalum ambalo baada ya kupata uhuru aliona kwamba nchi hii haiwezi kujiongoza peke yake mpaka nchi yote ya Afrika iwe huru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo baada ya kuona kwamba nchi yoyote haiwezi kuwa huru baada ya kuwa wameungana na Zanzibar kitu kilichofuata pale, Mheshimiwa Rais au Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilichofanya ni kuhakikisha Jeshi letu linakuwa Jeshi la Ukombozi la Afrika na Jeshi letu lilikuwa limepelekwa kila sehemu katika Afrika kwenda kufanya participation katika kuhakikisha kwamba zile nchi nyingine zinakuwa huru. Zile nchi huru zote leo zimekuwa huru lakini leo tulitarajia kwamba kwa kuwa kulitumia fedha zetu nyingi sana kwa kuweka makambi hapa nchini kwetu na sisi wenyewe tukabaki nyuma ndiyo hao hao ambao wametufikisha leo Tanzania tumekuwa nyuma wenzetu wamekuwa mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nini kifanyike Mheshimiwa Mpango ni coordination ile ile kama jeshi letu wakati ule lilikuwa la kupigania uhuru, sasa hivi jeshi letu liwe ni jeshi la kiuchumi, tutengeneze jeshi wakati ule wakati tulikuwa na watu milioni tisa leo tupo watu milioni 50, tuna rasilimali watu ambao ni wengi sana ambao tukitengeneza jeshi wale ambao tumeshawatafutia uhuru na bado wanaendelea kupigana kama ndugu wanashindwa kujiongoza sisi tunaenda kuwauliza eeh, bwana mmeshindwa kuelewana kujitawala si ndiyo, tunamgonga mmoja halafu wanatulipa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo ndivyo jeshi la kisasa lilivyo duniani kote yaani tuwe na nguvu tuwe na jeshi lenye nguvu kama watu wanapigana na tuliwasaidia kukomboa uhuru wao mbona hawakuturudishia hizo gharama tutapataje. Kwa hiyo, maana yake kwa kuwa masuala ya ulinzi mara nyingi hatuwezi kuyazungumza wazi. Niombe Kamati ya Ulinzi na Usalama ifanye coordination na Bwana Mpango tuangalie namna gani tunaweza tukatumia jeshi letu kulishirikisha kwa wale watu wanaofanya fujo wakati tuliwasaidia kukomboa uhuru ili tunaona kwamba wanashiriki vipi kutulipa zile gharama kama wao wataendelea na ugomvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huo mchango kwa upande wa participation kuangalia kuona nini jeshi linashiriki kiuchumi duniani kote na ndiyo maana jeshi watu wanalitumia kiuchumi kama ninyi tumewakomboa na bado mnaendelea kupigana siyo tunakwenda tunakuja hapa kila siku kuja kuwasuluhisha bila kutulipa haiwezekani kama unazalisha mafuta haya tupe meli 200 hapa halafu sisi tunaondoka zetu itakuwa ni moja ya uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nyingine Mheshimiwa Mpango ambalo nataka nikushauri ni kwamba leo umeanzisha mradi wa kimkakati uwe na miradi ya kimkakati kwa mfano ile ambayo umesema kwamba kutakuwa na reli, reli kuanzia Mtwara kwenda hadi Mbambabay ule ni mradi wa kimkakati kwa sababu pamoja na mazao ya kilimo ambayo yatakuwa yanapita, lakini kule unakokwenda kunakuwa na makaa yale Liganga ambayo na kwenyewe kule kuna madini ambayo ni ya kimkakati ambayo yanaweza kutumika kwa ajili ya kuzalisha katika viwanda vingine. Maana yake hapo moja kwa moja hiyo miradi kama hiyo wewe unakuwa umeishirikisha kiuchumi kuliko kupeleka ile miradi ambayo inakuwa ikienda inakuwa moja kwa moja inakuwa ni mwisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine Mheshimiwa Mpango ambalo mimi nataka kushauri nimeona jambo zuri sana wamefanya hawa watu wa Wizara na ambalo na wewe mwenyewe umeshiriki. Kuna center for excellence kwa mfano watu wa excellence kwa mfano hawa watu madini wamehakikisha kila kanda wanajenga mahala ambapo watu wenye fikra kuhusu utaalam wa madini unakuwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo na sisi tufanye tunafanyaje sasa. Tunahakikisha kwamba yale mazao yote ya kilimo ya kimkakati yale tunaweka center for excellence kwa mfano hapa Dodoma tukiona kwamba watu wanalima zabibu, tunaangalia ile kwamba center wale Makutupora na wao wanalima zabibu ili tuweze kuuza katika viwanda vyetu, kama Singida wanalima alizeti tunahakikisha kwamba pale tunaweka national service.

Kwa hiyo, maana yake vijana wetu tutakuwa tumewaajiri maana patakuwa nacenter for excellence, lakini wale watapata kuuza kwenye viwanda vyetu vya alizeti ambavyo vitakavyokuwepo Singida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaenda Pwani kuangalia je, Ukanda wetu wa Pwani una viwanda vya samaki, tunaweka vile tunaweka camps ambao tutahakikisha kwamba kutakuwa na uvuvi, lakini vilevile tutakuwa tunaweka viwanda ambavyo vya kuhakikisha kwamba vijana wetu wanakuwa wana participation. Kwa hiyo, maana yake Mikoa yote vijana wote watakuwa wanashirikishwa moja kwa moja kiuchumi na maana yake watakuwa wanafanya kazi kwa umoja wetu na utapata upinzani na utalisha na watu ambao watakuwa hawana kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hautashirika hivo maana yake unazalisha bomu ambalo baadae litakuwa ni mzigo kwetu sisi kitaifa maana yake wale vijana wote tutakuwa na center ambazo kila mahala kama ni Mbeya, kama ni Kigoma kama kuna mawese sehemu fulani tutaweka hayo tutangalia tusifanye mipango ya kukurupuka, tukisikia korosho leo imefikia shilingi 2000 basi tuna sambaza miche nchi nzima, haya leo imeshuka tunafanyaje yaani hiyo maana yake ni mipango ambayo hatushirikishi na tunashindwa kutumia nguvu zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo maana yake kwamba panapotokea jambo hata kama madini leo ni shilingi 5000 tusifikirie kuangalia madini yale peke yake, tuangalie nini ambacho kinafuata ili tukifanye ili tuhakikishe kwamba uchumi wetu unakuwa uchumi imara. Lakini tuweke uchumi ambao ni mfumo, tuweke mfumo ambao utakuwa ni endelevu, leo umetengeneza huu mpango je, huu mpango ni endelevu? Kama leo baada ya mwaka mmoja akija mtu mwingine anaweza akaubadilisha? Kamwe tusimpe loophole mtu mwingine kutokana na mpango wako ambao umeutengeneza leo akapata nafasi kuja kuuharibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie kama tumetengeneza mpango au watu wa Serikalini kwa mfano watumishi mimi nakumbuka wakati ule wakati tulipokuwa tunaajiriwa tulikuwa tunalipwa posho, kuna substance allowance mtu akishaajiriwa analipwa malundo ya posho kiasi kwamba yeye hawezi kuingia tena kwenye corruption.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo maana yake hawa watumishi wa Serikali lazima uangalie masilahi yao ili wao wanapoenda kufanya kazi miguu yaani watakuwa wanaishia huko. Lakini kama utakuwa unaangalia mpango tu wa kupata fedha Serikalini bila kuangalia hawa watumishi, Mpango utakuwa unajidanganya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jingine ambalo Mheshimiwa Mpango ambalo unatakiwa uliangalie ni kundi la wanasiasa, kundi ambalo ni kubwa sana Waheshimiwa. Mtu atakudanganya kwamba bwana okaywewe mpango wako angalia tu mambo ya kiuchumi. Lakini wanasiasa wapo na wao wana nafasi yao katika kufanya participation katika kufanya maamuzi sasa kama wao wanafanya maamuzi wamekaa humu ndani na wewe Mheshimiwa Mpango umesikia wanalalamika hapa watu kwamba wewe unatumia la STL, lakini hapa kuna Mbunge leo anaenda pale mpaka mnafika pale Kibaigwa unamkuta Mbunge gari yake ile aliyokopa ya milioni 60 hiyo mbovu imekufa, ameificha pembeni. Hivi wewe mtu kweli atakuunga mkono, kwa hiyo maana yake lazima uangalie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu watakuwa wanakudanganya, watakudanganya kwamba sisi hatutaki maslahi yetu. Lakini nawasifu kwamba mmetengeneza vitu ambavyo vya kimsingi unatengeneza kabisa kuna ndege, kuna viwanda, kuna participation lakini kubwa je, maslahi ya hayo maamuzi ya hao wanasiasa inakuaje. Nakushukuru sana...

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimkumbushe Mheshimiwa Mpango kwamba Mheshimiwa Karume wakati anaondoka pale alipojenga zile nyumba za Michenzani wale Mawaziri wake wake wote aliwajengea nyumba moja moja hawakuchukua rushwa, sasa leo wewe Wabunge badala ya kuwaona kwamba hawa Wabunge na wao wana nafasi unawaacha hivi hivi halafu unawaambia wasichukue rushwa kwa kuwa tu rushwa tu haipo, naomba uangalie wanasiasa uangalie watu binafsi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naunga mkono hoja.