Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Munde Abdallah Tambwe (1 total)

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, mimi binafsi na Watanzania wote wana imani na Rais Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Waziri Mkuu wetu na tuna imani haya yote aliyoyasema hapa kwa Serikali hii ya Awamu ya Tano yatatekelezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimuulize swali dogo tu la nyongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu. Atakuwa tayari sasa kuzifuatilia Halmashauri zote ziwe zinapokea pesa kwa kutumia mashine za kielektroniki?
yote, tumeendelea kuwaagiza Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na watendaji wa Halmashauri wakiwemo Wakurugenzi kuhakikisha kwamba moja ya majukumu yao waliyonayo ni kuhakikisha na kujiridhisha kwamba kila eneo la makusanyo, vifaa vya kielektroniki vinatumika na kwa hiyo, wajibu wangu ni kusimamia kuona kwamba matumizi ya vifaa hivi yanafanyika na yanaendelea. Ahsante sana.