Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Neema William Mgaya (29 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, awali ya yote kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi tena ya kuweza kurudi ndani ya Bunge hili Tukufu. Lakini vilevile niwashukuru wapiga kura wangu akina mama wa Mkoa wa Njombe kwa kuniamini na kunichagua kuwa mwakilishi wao, ahsanteni sana akina mama. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumpongeza, Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwa taa ya ulimwengu. Hivi sasa Mataifa mbalimbali yamekuwa yakimzungumzia kwa utendaji wake wa kazi mzuri. Gazeti la New York Times nchini Marekani limemzungumzia na kumwelezea vizuri katika suala zima la uadilifu na utekelezaji wa sera aliokuwanao tangu alipokuwa Waziri kwa kipindi cha miaka 20. Pongezi sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna gazeti lingine nchini Uingereza linaitwa London Times, limeelezea jinsi wananchi wanavyomshauri Malkia Elizabeth kuwa siku ya yake ya kuzaliwa iwe siku ya usafi nchini Uingereza. Hii yote ni kwa sababu ya utendaji mzuri wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, ndiyo maana watu sasa hivi wanatamani ku-copy mambo yake. Hongera sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala la elimu. Naanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuweza kutukeleza ahadi yake katika suala zima la elimu, kwa maana ya kwamba ada kuanzia shule ya msingi hadi kidato cha nne imefutwa. Ni kweli sasa hivi wanafunzi wa shule ya msingi hadi kidato cha nne hawalipi ada tena. Vilevile ahadi yake ya kutoa vitabu kuanzia shule ya msingi mpaka kidato cha nne pia imetekelezeka. Hongera sana Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuishauri Serikali na kuijulisha kwamba dhana hii ya kufutwa kwa ada bado haijaeleweka kwa wananchi. Hivyo basi, naishauri Serikali ishuke chini kwa wananchi ili iwaeleweshe vizuri dhana nzima ya elimu bure, kwa maana ya ufutwaji wa ada kutokea shule ya msingi mpaka kidato cha nne, lakini vilevile na Serikali kuchangia vitabu kuanzia shule ya msingi mpaka kidato cha nne.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala la huduma ya afya. Nitakuwa mchoyo wa fadhila nisipoendelea kumpongeza Mheshimiwa Rais wangu kwa sababu hivi sasa tumeona ameweza kutatua kero mbalimbali katika Wizara ya Afya kwa muda mfupi sana aliokuwa madarakani. Kero kubwa ya CT-Scan katika hospitali ya Muhimbili imetekelezeka. Wananchi wanapata kipimo hiki cha CT-Scan ndani ya Hospitali ya Muhimbili ukilinganisha na zamani walikuwa wanaenda kupima kipimo hiki nje ya hospitali kwa gharama kubwa. Hongera sana Mheshimiwa Rais.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tumeona uanzishwaji wa maduka ya madawa ya MSD ndani ya hospitali ya Muhimbili na kule Mwanza. Hivi sasa wananchi wa Jiji la Dar es Salaam ambao wanakwenda kupata matibabu pale Muhimbili na wananchi wa Jiji la Mwanza wanapata dawa kwa bei nafuu. Hongera sana Mheshimiwa Rais kwa kutekeleza hilo ndani ya muda mfupi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeanza kuona mabadiliko ya wafanyakazi katika hospitali, lakini vilevile na vituo vya afya. Hii inapelekea zile ziara za kushtukiza katika hospitali hizi na vituo vya afya.
Rai yangu kwa Serikali, naomba sasa Serikali ishuke, iende kwenye mikoa mingine ili iweze kutatua kero ambazo zinawakabili wananchi wa mikoa mingine katika hospitali. Mfano kule kwetu Njombe, hospitali yetu ya Njombe sasa hivi imekuwa ni chakavu sana; haina dawa za kutosha, haina wahudumu wa kutosha wala hospitali hii haina vipimo, ukizingatia kwamba hospitali hii ya Njombe sasa hivi tunaitegemea kama hospitali ya Mkoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Halmashauri ya Njombe Mji wanatibiwa pale, wananchi wa Halmashauri ya Wanging‟ombe wote wanatibiwa pale. Namwomba Waziri, Dada yangu Mheshimiwa Ummy Mwalimu, tukitoka kwenye Bunge hapa mje kuona jinsi ilivyochakaa, dawa hakuna, hatuna Madaktari wa kutosha na vipimo hakuna. Nawaomba mje kuangalia changamoto hii ili muweze kututatulia, kwa sababu sisi mkoa wetu wa Njombe ni mkoa mpya, tunahitaji kupata, hospitali ya uhakika.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile napenda kumwomba Mheshimiwa Simbachawene kwamba katika mkoa wetu wa Njombe, tuna Wilaya mpya ya Wanging‟ombe, Wilaya hii haina hospitali ya Serikali. Wananchi wa Wanging‟ombe…
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti hii ya Wizara ya Maliasili na Utalii napende kuchangia mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya uhifadhi na utalii ni muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu. Sekta ya utalii inachangia takribani asilimia 17.5 ya uchumi wa Tanzania. Kuna umuhimu sasa Serikali itie mkazo katika kuhakikisha sekta hii ya utalii inafanya vizuri ili kuongeza mapato na kukuza uchumi wetu wa Tanzania. Serikali inatakiwa ifanye jitihada kuhakikisha ifikapo mwaka 2020 idadi ya watalii nchini iwe imeongezeka kufikia milioni mbili ambapo itaongezeka mpaka asilimia 20 - 25 katika uchumi wa Tanzania. Kuna umuhimu pia kuweka jitihada/mkazo kwenye utalii wa fukwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Wizara/Serikali iweke mikakati mizuri katika kuhamasisha utalii wa ndani kwa kuongeza matangazo katika sehemu muhimu ili wananchi watembelee maeneo ya utalii kama Ruaha National Park kule Iringa, wajulishwe uzuri wa kule, mfano kuna simba wanaotembea kwa makundi makubwa ambayo ni kivutio kikubwa. Mbuga ya Kitulo kule Mkoa wa Njombe, mbuga yenye maua mengi ya kila aina tuitangaze ili kuweza kupata watalii wengi, ni kivutio cha aina yake.

Mhesimiwa Mwenyekiti, Serikali pia iongeze mbinu za kupambana na ujangili ili tuweze kulinda wanyama wetu kama faru, tembo na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nashauri kwamba elimu ya uhifadhi itolewe kwa wananchi, waelewe faida ya uwepo wa mapori ya hifadhi. Kwa kufanya hivi tutaweza kuepusha migogoro ya wananchi na hifadhi kama kule Loliondo na maeneo mengine. Wahifadhi wa pori watoke kwa wananchi kutoa elimu ya uhifadhi, wasikae maofisini tu na Serikali iboreshe mikakati ya kuvutia watalii wengi zaidi nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Bodi ya Utalii, TANAPA pamoja na NCAA waendelee kutangaza vivutio vya utalii kwa kasi kubwa zaidi. Serikali/Wizara iweke mabango mengi na kuyasambaza kwenye maeneo muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, Serikali iwapatie budget/pesa za kutosha Wizara hii ili waweze kufanikisha shughuli zilizokusudiwa kufanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri ambayo ameanza kutekeleza, vilevile niwapongeze Mawaziri wetu wote wa Wizara zote. Kazi mnazozifanya tunaziona, tunazidi kuwatia nguvu ili muendelee kufanya kazi zaidi. Nimpongeze pia Waziri Mkuu kwa usimamizi mzuri na kazi nzuri anayoifanya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nijikite moja kwa moja kuzungumzia maendeleo ya Mkoa wa Njombe. Kwa kuwa hotuba tunayoijadili sasa hivi ni ya TAMISEMI, Mkoa wa Njombe ni Mkoa mpya na katika Mkoa huu mpya wa Njombe kuna Wilaya mpya ya Wanging‟ombe. Wilaya hii ya Wanging„ombe tuna uhaba wa hospitali hatuna hospitali ya Serikali tuna hospitali moja tu ya Ilembula ambayo ni ya binafisi, ya Kanisa hivyo basi wananchi wa Wilaya ya Wanging‟ombe wanatumia gharama kubwa sana katika matibabu. Naiomba Wizara hii ya TAMISEMI ione umuhimu wa kujenga hospitali ya Serikali ili kuweza kuwasaidia Wabena wenzangu wa kule Wanging‟ombe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, zahanati zetu katika Wilaya Wanging‟ombe hazina wahudumu wa kutosha, madaktari ni pungufu kabisa hakuna madaktari, utakuta nesi anafanya kazi ya daktari naomba pia Wizara hii ya TAMISEMI iangalie umuhumu wa kuongeza wauguzi kwa maana ya madaktari katika zahanati zetu za Wilaya ya Wanging‟ombe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kuzungumzia suala hili la afya nataka niguse Halmashauri zote za Mkoa wa Njombe. Halmashauri ya Mji wa Njombe ambayo ni Jimbo la Lupembe, pia kuna changamoto ya hospitali, hospitali hatuna kule katika ile Halmashauri. Kuna zahanati mbili tu, vituo vya afya viwili na vituo vya afya hivyo viwili havina huduma ya upasuaji. Naiomba Wizara iangalie umuhimu wa kuendelea kuboresha na kujenga zahanati zingine ndani ya Halmashauri ya Mji katika Jimbo la Lupembe. Najua wao wakiongeza zahanati nyingi basi Wizara Afya Mheshimiwa Waziri wa Afya Dada yangu Ummy Mwalimu ataleta dawa za kutosha na kuweza kuwahudumia Wabena wetu kule wa Lupembe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto pia hii ya afya ipo pia katika Halmashauri ya Makete, hospitali ni chakavu tunaomba hospitali ile ikarabatiwe, vilevile na waaguzi ni wachache katika hospitali ile ya Makete. Tunaomba sasa tuongezewe wauguzi ili wananchi wa kule Makete waweze kupata huduma vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende sasa Halmashauri ya Mji ya Njombe Mjini. Pale kuna Hospitali ya Kibena, hospitali ile ya Kibena sasa hivi inatumika kama hospitali ya Mkoa kwa sababu Wilaya zote zinategemea hospitali ile. Ninaiomba Serikali sasa ikarabati kwa haraka ile hospitali, iongeze wahudumu kwa sababu tuna changamoto bado za madaktari na baadhi ya manesi. Kwa kuwa hospitali ile inahudumia watu wengi sana tunaomba waongezeke madakitari pamoja na manesi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia miundombinu ya maji katika hospitali ile ya Kibena ni chakavu, umeme ni shida, naomba Serikali iangalie kwa karibu kwa sababu hospitali ile sasa hivi ndiyo inatumika kama Hospitali ya Mkoa ukizingatia kwamba Mkoa wetu wa Njombe ni mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, akina mama wanatoka umbali mrefu sana karibia kilometa 147, wale akina mama wanaotoka Lupembe kwenda kufuata huduma ya upasuaji. Ni vema basi tukaona sasa na madaktari wa upasuaji waongezeka wawe wengi ili akina mama wale wanapokwenda wasikae kwa muda mrefu pale hospitali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba niende kwenye suala la elimu; tunaishukuru Serikali kwa kutambua umuhimu wa elimu na kuweza kutoa elimu bure kuanzia chekechea mpaka elimu ya sekondari. (Mkofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nichukue nafasi hii kulipongeza Bunge kwa kutambua umuhimu wa elimu na kuweza kuchangia shilingi bilioni sita iende kununua madawati. Ina maana kila Jimbo litapata madawati 600; tunatambua umuhimu wa elimu na ndiyo maana tumeweza kufanya hivyo, nipongeze sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kule kwetu katika hizi Halmashauri zote nilizozitaja kwa maana ya Wanging‟ombe bado tuna tatizo la wafanyakazi katika shule, pia shule zilizokuwepo majengo yake ni chakavu sana yanatakiwa kukarabatiwa, miundombinu ya vyoo ni mibovu inatakiwa kukarabatiwa. Kwa mfano kule Wanging‟ombe kuna shule moja inaitwa shule ya msingi ya Mjenga ina walimu wawili tu. Kwa hiyo, bado uhaba wa walimu katika shule za msingi na sekondari bado ni changamoto kubwa sana katika Halmashauri ya Wanging‟ombe, vilevile ukienda kwenye Halmashuri ya Ludewa changamoto hii ipo katika shule 108 ni shule nne tu, ambazo zina walimu wa uhakika, lakini shule 104 zote hazina walimu wa kutosha katika Halmashauri ya Ludewa. Tunaomba pia Serikali iangalie na iweze kutatua tatizo hili. Tatizo hili vilevile liko Halmashauri ya Mji kule Jimbo la Lupembe pia kuna changamoto hiyo shule haziko za kutosha na zilizopo zipo katika hali mbaya, zinahitaji kukarabatiwa, hali kadhalika katika Wilaya ya Makete na Wilaya ya Njombe kwa ujumla. Natumaini Mawaziri wetu wa TAMISEMI watazichukua changamoto hizi kwa haraka zaidi ili kuweza kutatua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie barabara ambazo ziko katika Halmashauri zote za Mkoa wa Njombe. Zile barabara za Halmshauri, nilikuwa naiomba sasa Serikali iweze kutenga pesa nyingi ili ziweze kukarabatiwa katika kiwango kizuri ili ikifika msimu h wa mvua zile barabara zisiwe zinaharibika kwa urahisi. Kwa sababu Mkoa wetu wa Njombe ni Mkoa wenye neema kama jina langu, tunalima sana kule kwa hiyo, wananchi wa Mkoa wa Njombe wanashindwa kutoa yale mazao kutoka ndani kule vijijini kwa kutumia zile barabara za Halmashauri ili kukutana na zile barabara za TANROADS. Naomba Serikali izingatie hilo na iweze kutoa pesa ya kutosha katika suala zima la barabara za Halmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile wazungumzaji wengi waliopita wamezungumzia suala la asilimia kumi. Labda tu niwambie Wabunge wenzangu na wale waliokuwa kwenye Halmashauri Madiwani wenzetu ni kwamba asilimia kumi ni lazima iende kwa wanawake na vijana kwa sababu hiyo asilimia kumi inatokana na mapato ya Halmashauri, ina maana kama hiyo asilimia kumi haijaenda kwa wanawake na vijana hiyo Halmashauri haijakusanya mapato yoyote? Hili ni jipu, Mheshimiwa Waziri hili ni jipu lazima mliangaliye kama Halmashauri inaweza kukusanya mapato lazima ile ten percent ambayo asilimia tano inaenda kwa vijana na asilimia Tano inaenda kwa wanawake lazima zipelekwe ili ziweze kusaidia akina mama pamoja na vijana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo nashukuru kwa kunipa nafasi.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, nipo, nashukuru kwa kunipa nafasi naomba nami sasa nianze kuchangia Hotuba ya Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano. Nianze kwa kusema kwamba Mkoa wetu wa Njombe ni mkoa mpya, sitoacha kusema hivyo, kwa sababu tunahitaji maendeleo ili mkoa uweze kwenda. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kati ya barabara ambazo zimeshafanyiwa usanifu ndani ya Mkoa wa Njombe ni pamoja na barabara ya Njombe - Makete inayopita Mbunga ya Kitulo kwenda kutokezea Isonja, Mkoa wa Mbeya. Barabara hii iliwekwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi namba moja, lakini vilevile barabara hii iliwekwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi mwaka 2005 mpaka mwaka 2010 iliwekwa tena upya. Hiyo haitoshi, barabara hii Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli wakati anakuja kuomba kura za Urais kule Makete na Wilaya ya Wanging‟ombe alisema kwamba barabara hii ndiyo ya kwanza ambayo itajengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba Serikali itekeleze ahadi ya Mheshimiwa Rais, barabara hii ina umuhimu mkubwa sana kwa sababu, barabara hii kama itatengenezwa kwenye kiwango cha lami itainua uchumi wa Taifa, katika zao la Pareto, lakini vilevile katika masuala ya utalii. Sisi kule Makete kuna Mbuga ya Kitulo kwa sababu barabara hii imepita kwenye mbuga ya Kitulo, sasa hivi watalii wanashindwa kwenda kwa wingi kwenye ile mbuga ya Kitulo kwa sababu barabara ile haipitiki. Hasa kipindi cha mvua ndiyo haipitiki kabisa. Kwa hiyo, naiomba Serikali iweze kujenga kwa kiwango cha lami. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, vilevile kule katika barabara ile pia kuna mazao ambayo yanasafirishwa ya mbao, viazi mnavyokula Dar es Salaam vinatoka Makete. Barabara hii ina umuhimu mkubwa, naiomba Serikali iweze kujenga barabara hii. Vilevile ndani ya Mkoa wa Njombe bado kuna barabara nyingine ambayo imefanyiwa usanifu, barabara ya Njombe-Mdandu-Iyayi ambayo nayo inakwenda kukutana na Mkoa wa Mbeya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, barabara hii wakazi wa Wanging‟ombe wanaolima mazao ya alizeti pamoja na mbao wanashindwa kusafirisha kwa urahisi kupeleka Mbeya, lakini vilevile wanashindwa kusafirisha kwa urahisi kuja Njombe ili kwenda mikoa mingine kama Ruvuma. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tuna barabara nyingine ambayo imefanyiwa usanifu, barabara ya Njombe - Ludewa, Manda – Itoni. Barabara hii ni muhimu kwa sababu kule Ludewa kuna makaa ya mawe ya Liganga na Mchuchuma. Naiomba pia Serikali ikamilishe barabara hii kwa kuijenga kwa kiwango cha lami barabara yote ili kuweza kusafirisha makaa ya mawe kwa urahisi.
Mheshimwia Spika, pia tuna barabara ya kibena - Lupembe-Madete ambayo inaunganisha Mkoa wa Morogoro, tunaomba pia barabara hii ijengwe kwa kiwango cha lami. Nakumbuka asubuhi Mheshimiwa Hongoli aliuliza swali na Mheshimiwa Waziri alisema kwamba, barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami mwaka 2016 - 2017. Ukienda kwenye hotuba ukurasa wa 37 inasema kwamba Lupembe-Madete Kilometa 125 taratibu za kumpata Mhandisi Mshauri kwa ajili ya upembuzi yakinifu zinaendelea. Nimwambie tu Mheshimiwa Waziri, stage hii ilishapita, nilitegemea sasa hivi watatuambia kwamba labda tender inatangazwa kwa ajili ya kujenga barabara hii.
Mheshimiwa Spika, nina ombi moja kwa Serikali kuhusiana na Jimbo la Lupembe. Lupembe kuna barabara ambayo inatoka Lupembe-Lukalawa, inapita Ikonda kutokea Makambako. Barabara hii ni business road, kuna wakulima wanasafirisha sana mbao, maharage, pamoja na chai. Naomba sasa barabara hii itoke katika ngazi ya Halmashauri ipelekwe iwe barabara ya TANROAD, ili iweze kujengwa kwenye kiwango cha lami kwa uharaka. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nitoke kwenye barabara niende kwenye kiwanja cha ndege. Mkoa wetu wa Njombe kiwanja chetu cha ndege cha Njombe kina hali mbaya sana. Kwa nini naomba kiwanja hiki? Ruvuma hakuna kiwanja cha uhakika cha ndege, lakini kama tutakarabati kiwanja kile cha ndege cha Njombe na kuweka kwenye kiwango cha lami ina maana ndege nyingi sana zitakuja. Kwa hiyo, Mkoa jirani wa Ruvuma watafaidika na kiwanja kile. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, istoshe kule Njombe tunalima zao la maua haya, tunalima maua mazuri sana, kuna roses nyingi sana kule, tunashindwa kusafirisha kufikisha Dar es Salaam zikiwa fresh kwa sababu hatuna kiwanja cha ndege cha uhakika, hakuna ndege zinazokuja mkoani pale. Hivyo inasababisha kulega lega kwa kilimo hiki cha maua. Naiomba sasa Serikali ione umuhimu wa kiwanja hiki, wakarabati katika kiwango cha lami ili na sisi tuweze kusafirisha maua kwa wingi kuja Dar es Salaam na kwenda nchi za nje. (Makofi)
Mheshimiwa Spika nimalizie kwa kuipongeza Serikali kwa mradi wa DART, mabasi yaendayo haraka. Naipongeza Serikali kwa kuweza kutengeneza mradi mkubwa kama huu ambao umegharamia takribani bilioni 322. Hata hivyo, katika mradi huu bado kuna upungufu mwingi sana, kitu cha kwanza nilichokuwa naiomba Serikali ihakikishe kwanza lile suala la hisa. Suala la hisa halijakaa vizuri kwenye mradi huu, Serikali irudi iende ikaangalie kwa umakini jinsi gani ya utaratibu wa hisa. Vilevile nashangaa kwa nini mradi huu hauanzi? Mradi umetumia gharama kubwa sana, bilioni 322, uanze kufanya kazi ili wananchi waweze kunufaika. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, vilevile kuna vituo ambavyo havijakamilika katika mradi huu, kituo cha Kimara pale mwisho, kuna kituo cha Ubungo Terminal, kituo cha Morocco, kituo kule Posta ya zamani. Vituo hivi viko wazi, ni hatari kama mradi utaanza ina maana watu watakuwa wanaingia kwenye mabasi bure. Naiomba Serikali sasa iangalie umuhimu wa kukamilisha vituo hivi na Serikali iwape fedha huu mradi uweze kukamilika ili uweze kutumika.
Mheshimiwa Spika, baada ya hapo, naunga mkono hoja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia. Vilevile namshukuru Mungu kwa kuweza kunipa afya bora na kuweza kusimama mbele ya Bunge hili Tukufu kuchangia hotuba hii ya bajeti kuu ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuzungumzia suala la afya, nasikitika kusema kwamba sijaona mkakati mahsusi wa kujenga zahanati pamoja na vituo vya afya. Tuko katika mkakati wa kuhakikisha kwamba tunapunguza vifo vya akinamama wajawazito. Najiuliza tunawezaje kupambana na vita hii ilhali hatuna facilities za kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini nasema hivi? Katika bajeti hii nimeona Hospitali za Mikoa ndiyo ziko chini ya Wizara lakini kiuhalisia watu wengi wapo kwenye Kata na kwenye Halmashauri zetu. Watu waliokuwa kwenye Kata, kwenye vijiji vyetu macho yao yanakuwa yanatazama zahanati zao na vituo vyao vya afya ambavyo viko kwenye Kata na kwenye Halmashauri zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, natambua Kanuni ya 106 inasema kwamba Mbunge hataruhusiwa kupendekeza mabadiliko yoyote katika makadirio na mapato ya bajeti ya Serikali, lakini naiomba Serikali kwa bajeti inayokuja iweze kuliangalia vizuri suala la zahanati na vituo vya afya viwekwe katika Serikali Kuu ili tuweze kuviboresha na kuvijenga kwa ufanisi mkubwa ili kuweza kutatua tatizo lile la vifo vya akinamama wajawazito ambapo wengi wao wako kwenye Kata huko kwenye Halmashauri zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia niishauri Serikali, ni vyema kuweka pesa nyingi katika Mfuko wa Maji kwa sababu tatizo la maji ni kubwa sana Tanzania na anayeteseka katika matatizo ya maji ni sisi wanawake. Akinamama wa mkoani kwangu kule, akinamama wa Kata za Saja, Kijombe, Wanging‟ombe, Mkongobaki, Nkomang‟ombe, Ludewa Mjini, Ludewa Vijijini pamoja na Njombe Mjini kuna shida sana ya maji kwa muda wa miaka mingi. Ni vyema Serikali itambue umuhimu mkubwa wa kuweka pesa nyingi katika Mfuko wa Maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hapo, naomba nizungumzie suala la utalii. Wenzetu wa Kenya wametoa kodi katika suala la utalii lakini sisi Watanzania tumeamua kuweka kodi katika suala la utalii. Kiuhalisia sisi Tanzania mshindani wetu mkubwa katika suala la utalii ni Mkenya. Wenzetu Wakenya wana ndege ya moja kwa moja kutoka Europe na America kwenda Kenya na mtalii anapotumia ndege hiyo anapata ahueni ya pesa katika tiketi karibu asilimia 45 ya air ticket. Hiyo ni advantage kwa wenzetu wa Kenya kwa sababu watalii wengi watakuwa wanataka kwenda Kenya kwa ajili ya ku-save hizo costs za air ticket na mambo mengine. Kabla hatujaweka asilimia 18 bado utalii wetu wa Tanzania ulikuwa wa gharama kubwa ukilinganisha na wa Kenya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile mtalii kabla hajaamua kuja vocation huwa analipa in advance, mwaka mmoja kabla au miaka miwili kabla. Kwa kuweka kodi hii kutatokea usumbufu kwa wale watalii ambao tayari walishalipa hela zao kuja kutalii kwa mwaka huu wa fedha 2015/2016 na ikiwezekana 2017. Kwa mkanganyiko huo, kuna uwezekano mkubwa wa watalii wengi kuahirisha na kutaka pesa zao warudishiwe kwa sababu wanaona kwamba mimi nilishajipanga bajeti yangu ya vocation ni kiasi hiki na sasa hivi naambiwa kwamba niongeze asilimia 18 ya pesa ambayo ilikuwa haiko kwenye bajeti yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Wizara iangalie suala hili la utalii katika masuala mazima ya ushindani wa utalii baina yetu sisi na watu wa Kenya, huenda tukasababisha watalii wengi waache kuja Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna ile wanaita msafara wa nyumbu wanaokuwa wanazunguka Kenya na Tanzania, migration ya wanyama. Nina wasiwasi wanaweza watalii hawa wakawa wanasubiri wanyama wakifika Kenya ndio waende badala ya kuja kuangalia kwetu Tanzania wakati sisi tuna advantage kubwa wakati wanyama wanasafiri miezi ya saba ndiyo kipindi ambacho nchi nyingi za Ulaya wanakuwa wako kwenye holiday na wanatumia muda huo kuja kutalii Tanzania. Naomba Serikali iangalie ili tusiweze kupoteza mapato katika suala la utalii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika bajeti zilizopita imeonesha kabisa kwamba utalii unachangia asilimia 25 ya mapato ya Tanzania. Kwa nini leo tuisumbue sekta hii na twende katika kushusha mapato hayo? Naomba Serikali iangalie kwa umakini kwa sababu asilimia 25 ya kuchangia kwenye mapato ni asilimia kubwa sana, tuiangalie kwa umuhimu wa kipekee ikiwezekana hii kodi tuitoe ili tusiweze kukosa watalii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho nizungumzie suala la kiinua mgongo. Najua Serikali ina dhamira njema ya kuongeza mapato katika bajeti yetu, lakini nashangaa katika category ya watu tisa akiwemo Makamu wa Rais, Prime Minister, Chief Justice, High Court Judges, Maspika, Supreme Court Judges, Regional Commissioners na hawa Wakuu wa Wilaya, kwa nini wame-single out Mbunge tu ndiyo akatwe kodi ya kiinua mgongo ilhali katika hilo group hao watu wote nao wanatakiwa waingizwe kwenye kukatwa makato haya. Kama kweli Serikali ina nia ya dhati na hawa watu wengine wote wakatwe au labda kama kuna kitu kimejificha tunaomba Wabunge tukijue hicho kitu ni kitu gani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge tuna mzigo mkubwa, Wabunge tunahudumia watu wengi huko vijijini kwa hela hiyo hiyo, Wabunge tunapeleka watu hospitalini, tunahudumia misiba, harusi, wagonjwa, kwa kipindi hiki cha Ramadhani Wabunge ndiyo hao hao ambao wanasaidia kule watu wengine ambao hawajiwezi katika masuala mazima ya kuhakikisha kwamba wanafuturu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Serikali iwaangalie Wabunge kwa jicho la huruma na hatuna nia mbaya kwamba hatutaki kuchangia mapato kwa sababu katika mishahara yetu tunakatwa kodi. Naomba sasa watuangalie na sisi ili tujue ni jinsi gani ya kurudi humu ndani na tuendelee kuwahudumia wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi nami kuweza kuchangia Hotuba hii ya Waziri Mkuu. Kwanza nianze kwa kutoa pole kwa kifo cha mpendwa wetu Mheshimiwa Dkt. Elly Macha, Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi. Amina.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuanza mchango wangu kwa kuipongeza Serikali ya Chama cha Mapinduzi, Serikali ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Naipongeza kwa kuweza kujenga na kukarabati barabara urefu wa kilometa 430 ambayo ni 62% ya lengo alilojiwekea
katika kujenga barabara urefu wa kilometa 692 kuanzia Julai, 2016 hadi Februari, 2017. Naipongeza sana Serikali yangu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kwa masikitiko makubwa, pamoja na pongezi hizo, Mkoa wangu wa Njombe hauna barabara ya lami hata moja. Naishukuru Serikali imeweza kutenga bajeti katika barabara zote za Mkoa wa Njombe, lakini hakuna barabara hata moja iliyoanza kutengenezwa. Mfano, Barabara ya Itonyi – Ludewa – Manda; kuna Barabara ya Kibena – Lupembe – Madeke; kuna Barabara ya Njombe – Makete; Barabara ya Njombe – Mdandu – Iyai; zote hizo zimetengewa bajeti, lakini bado hazijaanza kutengenezwa. Naiomba Serikali yangu sikivu, ianze sasa mchakato wa kuweza kutengeneza barabara hizi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende kwenye suala la afya. Siku zote nimekuwa nikisimama ndani ya Bunge hili na kuiomba Serikali; Wilaya ya Wanging’ombe ni wilaya mpya, hatuna hospitali. Wananchi wa Wilaya ya Wanging’ombe wanakwenda kutibiwa Hospitali ya Ilembula
ambayo gharama zake ni kubwa. Wananchi wanashindwa kukidhi mahitaji ya afya kwa sababu gharama ni kubwa sana. Naiomba Serikali iangalie umuhimu wa kuweza kujenga Hopitali ya Wilaya ndani ya Wilaya ya Wanging’ombe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna pesa ambazo zilielekezwa zipelekwe kwenye Zahanati na Vituo vya Afya vilivyomo ndani ya Wilaya ya Wanging’ombe, lakini mpaka sasa hivi pesa zile hazijapelekwa ili kuweza kujenga Zahanati na Vituo vya Afya. Matokeo yake sasa wananchi
wamekusanya nguvu kubwa kuweza kujenga maboma kwa ajili ya Zahanati hizo na Vituo vya Afya, lakini pesa kwa ajili ya kuendeleza ujenzi hazijapelekwa. Hii inawavunja nguvu wananchi kwa sababu wanatumia nguvu kubwa kujenga maboma kwa ajili ya hizo Zahanati na hivyo Vituo vya Afya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naweza nikataja tu Vituo vya Afya na Zahanati chache ambazo ziko ndani ya Wilaya ya Wanging’ombe hazijapelekewa pesa ilhali pesa zilipangwa. Kuna Zahanati ya Itambo, Katenge, Igima, Mmerenge, Ivigo na kuna Vituo vya Afya, Mdandu, Igagala na Ilembula. Tunaomba sasa pesa zipelekwe ili Zahanati na Vituo vya Afya hivyo viweze kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tuna Hospitali ya Mkoa ya Kibena. Ile Hospitali ya Kibena ndiyo ambayo tunaitegemea sisi pale kwenye Mkoa wa Njombe, lakini hospitali ile majengo ni machakavu, vilevile wodi za wagonjwa ni chache. Kwa mfano, kuna wodi moja tu ya wanaume, wagonjwa wa Kifua Kikuu wanalala humo humo, wagonjwa wa ajali za bodaboda wanalala humo humo. Mtu anakwenda na ugonjwa mwingine, anakuja kupata ugonjwa mwingine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali iweze kuongeza wodi za wagonjwa katika Hospitali ya Kibena, vilevile na kukarabati yale majengo kwani yamekuwa machakavu sana. Tunaomba Serikali iweze kutatua tatizo hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda Jimbo la Lupembe, wananchi wamejitolea ekari 52 kwa ajili ya kuweza kujengewa hospitali katika Halmashauri ile ya Mji wa Njombe. Naiomba Serikali ifikirie sasa kwa kina na kuona umuhimu kwamba wananchi wa Jimbo la Lupembe nao wanahitaji hospitali ukizingatia kwamba Mkoa wetu wa Njombe ndiyo kwanza unaanza kukua na hivyo huduma nyingi za afya tunakuwa bado hatujapata vile inavyostahiki. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala la maji. Nimekuwa nikizungumzia suala la maji mara nyingi sana ndani ya Bunge hili na kuiomba Serikali iweze kutatua tatizo la maji katika Tarafa ya Wanging’ombe. Tatizo la maji Tarafa ya Wanging’ombe katika Jimbo la Wanging’ombe limekuwa ni tatizo sugu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulikwenda mwaka 2015 kuomba kura kwa ajili ya kumwombea Mbunge ambaye ni Waziri wa Maji, Mheshimiwa Lwenge, kwa kweli akinamama na akinababa tatizo lao kubwa sana kule ambalo walikuwa wakilitaja mara kwa mara ni tatizo la maji. Ukienda Kata ya Kijombe, Saja, Ilembula, Wanging’ombe yenyewe tatizo la maji ni kubwa sana. Tunaomba tatizo hilo liweze kutatuliwa mara moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia Mji wa Makambako wanapata maji kwa msimu. Kipindi cha kiangazi maji hakuna kabisa. Maji yanapatikana kipindi cha masika tu. Tunaomba Serikali iweze kuangalia tatizo hilo la maji katika Mji wa Makambako ili akina mama wa Makambako waweze
kujikwamua katika tatizo hilo la maji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Njombe Mjini hali ni hiyo hiyo, tatizo la maji bado lipo na inapunguza ufanisi mkubwa sana kwa akinamama kufanya kazi kwa sababu, muda mwingi wanakuwa wanatumia kwenda kutafuta maji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Lupembe katika vijiji 45, vijiji 31 vyote havina huduma ya maji. Hali ni mbaya. Tunaomba Serikali iweze kutatua tatizo hilo la maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende kwenye elimu. Shule zetu zilizopo ndani ya Mkoa wa Njombe, kwa maana ya Shule za Msingi na za Sekondari majengo yetu ni machakavu, lakini vilevile tuna uhaba wa madarasa na uhaba wa Walimu wa Sayansi katika Shule za Sekondari.
Mheshimiwa Naibu Spika, unaweza ukakuta Shule ya Sekondari haina Mwalimu hata mmoja wa sayansi na shule nyingine zina Mwalimu mmoja au wawili. Kwa kweli, naiomba Serikali sasa itambue umuhimu wa kuongeza Walimu wa sayansi katika shule zetu za sekondari ndani ya Mkoa wa Njombe na kuweza kukarabati madarasa hayo pamoja na kujenga madarasa mapya kwa ajili ya wanafunzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie kilimo. Kule kwetu Njombe tuna zao kubwa la chai, lakini hivi sasa bei ya chai imeshuka sana. Kilo moja wanauza 250/= wakati gharama za uzalishaji zinazidi kilo moja ya chai. Gharama za uzalishaji katika kilo moja ya chai ni shilingi 450/=, unaona kuna tofauti hapo ya karibu sh. 200/=. Tunaomba Serikali iangalie soko la chai katika kilimo chetu cha chai ndani ya Mkoa wetu wa Njombe ili wale wakulima ambao wanalima chai waweze kupata faida na wasiwe wanazalisha kwa hasara.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pembejeo. Mbegu zinachelewa kufika kwa wakati, lakini mbolea ya kukuzia inachelewa kufika. Hazifiki kwa wakati, lakini cha kusikitisha zaidi muda wa kupanda umeshapita, muda wa kuweka ile mbolea ya kukuzia umeshapita; wananchi wanalazimishwa wanunue zile mbolea, wanunue na zile mbegu, wakati huo muda unakuwa umeshakwisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli, hiyo siyo sawa na siyo jambo jema kwa wananchi wetu kuwafanyia hivyo. Tunaomba mbegu na mbolea za kupandia zifike kwa wakati ili zisije zikachelewa halafu tena bado mnawalazimisha wanunue hizo mbolea na hizo mbegu, inakuwa ni hasara
kwao.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo machache, nimalizie tu katika suala la umeme. Lupembe bado kuna changamoto kubwa sana ya umeme. Katika vijiji 45, vijiji 30 vizima havina umeme. Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.
Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi kuweza kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Afya. Nianze kwa kumpongeza Rais wangu, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa jitihada kubwa ya kuimarisha upatikanaji wa dawa.

Ukiangalia kwenye bajeti ya mwaka 2015/2016 pesa zilizopelekwa kwenye huduma ya upatikanaji wa dawa ilikuwa shilingi bilioni 24, hivi sasa ndani ya miezi tisa chini ya Dkt. John Pombe Magufuli, pesa zilizopelekwa za dawa ni shilingi bilioni 112. Kwa Mkoa wa Njombe mpaka dakika hii hospitali, zahanati, vituo vya afya tumeshapokea karibia asilimia 80 mpaka 90 ya pesa za dawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza Mawaziri kwa usimamizi mzuri, Mheshimiwa Ummy Mwalimu na Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla kwa kweli wanasimamia vizuri zoezi hili, pongezi sana kwao. Ombi langu moja kwa Serikali, Mheshimiwa Ummy ile hospitali yetu pale ya Makambako ni Hospitali ambayo ipo katikati inahudumia Mikoa ya karibu kama Iringa, wengine wanatoka Mbeya maeneo yale ya Mbarali kuja kupata huduma za matibabu pale Makambako. Hivyo basi, zile pesa mnazotupangia zinakuwa chache mno.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashukuru tumepata pesa karibu asilimia 90 za dawa lakini mnazo tupangia ni ndogo tunaomba muongeze bajeti katika pesa za dawa katika Hospitali ile ya Makambako.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee pia kuwapongeza tena Mheshimiwa Ummy na Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla kwa kusimamia kikamilifu huduma ya matibabu ya kibingwa. Kwa kweli katika hili mmefanya vizuri, tumeona katika hotuba yenu rufaa sasa hivi zimepungua za kwenda nje, hivyo naamini zile pesa ambazo zingetumika kwa ajili ya rufaa za wagonjwa kwenda nje zitatumika katika masuala mengine ya maendeleo kama maji, umeme, barabara na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sitochoka kuendelea kupongeza, nawapongeza pia Mheshimiwa Rais, Waziri Ummy, Naibu Waziri Kigwangalla kwa kuweza kufanikisha upatikanaji wa vifaa vya hospitali kama magodoro, vitanda, mashuka, tumeona kwamba Wilaya zote ndani ya nchi yetu ya Tanzania tumeweza kupata vifaa hivyo. Hongera sana kazi nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie suala la vifo vya mama wajawazito, kila mwanamke aliyesimama hapa amezungumzia tatizo hili la vifo vya akina mama wajawazito. Takwimu zinaonesha na kwenye hotuba yake Mheshimiwa Waziri ameonesha kabisa kwamba vifo vya akina mama wajawazito vimeongezeka kutoka 430 mpaka 556 katika vizazi hai 100,000, hali ni mbaya sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ummy wewe ndiye Waziri mwenye dhamana katika Wizara hii ya Afya, wewe ni mwanamke, wewe ni mzazi, wewe ni mama wa watoto. Mheshimiwa Ummy unatusaidiaje wanawake wenzio katika tatizo hili? Hakikisha unapambania tatizo hili kutusaidia wanawake wenzio ili uweze kuacha alama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Mheshimiwa Ummy katika Wizara hii unaye kaka yetu Naibu Waziri Dkt. Kigwangalla yeye ni daktari kwa taaluma na Balozi wa Wanawake, shirikianeni katika kuhakikisha kwamba tatizo hili la vifo vya wanawake linakwisha nchini kwetu Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie suala pia la huduma za afya kwa watoto wachanga. Nataka nijue ni lini Serikali itaweka utaratibu mzuri wa kuweza kusimamia afya ya mtoto mchanga kwa maana ya siku 30 mpaka siku moja. Nimesoma vijarida mbalimbali vya wataalam vinaonyesha kwamba tukiweza kudhibiti vifo vya watoto kuanzia siku 30 mpaka siku moja kwa maana ya kuboresha afya za watoto wao, tutaweza kupunguza vifo vya watoto wadogo chini ya miaka mitano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ulaya wenzetu watoto ambao wanazaliwa kwa gramu 500 mpaka gramu 600 wanaishi tofauti na hapa kwetu. Naiomba Serikali sasa ione umuhimu wa kuweza kuanzisha huduma ya afya za watoto hawa wachanga wa siku 30 mpaka siku moja, waanzishe wodi kwenye kila Wilaya ndani ya Tanzania kama ilivyopeleka vifaa vile kila Wilaya na hizi wodi za watoto wachanga zifunguliwe kila Wilaya ili kina mama wa Wilaya ya Wanging’ombe waweze kupata huduma hiyo, Ludewa, Makete, Njombe na Wilaya zingine ndani ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huduma ya matibabu ya saratani, katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri amezungumza kwamba sasa hivi wanakwenda kununua mitambo ya kutoa huduma ya tiba kwa ajili ya saratani. Mheshimiwa Waziri na dada yangu Ummy, kwa nini Serikali msiwekeze zaidi kwenye kinga, ukizingatia kwamba saratani ambayo inaua Watanzania wengi ni saratani ya shingo ya uzazi. Wanawake wengi wanakufa, hebu wekezeni zaidi kwenye kinga, kwenye Wilaya zetu kule tunakotoka ili mwanamke wa Ludewa kule aweze kupata huduma hiyo na kugundua hilo tatizo mapema. Kwa sababu inaonekana kwamba wagonjwa wa saratani wanakuja kugundulika wana matatizo hayo wakati imeshafika stage ya hali mbaya, matokeo yake Serikali inatumia gharama kubwa kuwatibia, kuwafanyia huduma na matibabu ya mionzi, chemotherapy wakati tungezigundua mapema tungeweza kuokoa maisha yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina experience Mama yangu amekufa kwa pancreatic cancer, na tumekuja kugundua muda umeshapita, kama kungekuwa na huduma hizi mapema hata akina mama wanapokwenda tu hospitali anaweza aka-check, akagundua mapema, mtu anaweza akakaa kwa muda mrefu zaidi ya miaka 15 mpaka 20, lakini wagonjwa wengi wa kansa wanagundulika wakati hali imeshakuwa mbaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ijikite zaidi kwenye kinga na kushusha kule kwenye Wilaya zetu ili kila Wilaya tuweze kupata huduma hii ya kinga ili tuweze kuokoa wanawake wengi, Kwa sababu kansa ya shingo ya uzazi ndiyo ambayo inaua wanawake wengi. Wengi wanaokufa na kansa ni wanawake ukiangalia katika takwimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie suala la uwezeshwaji wa wanawake kiuchumi. Mheshimiwa Waziri, Dada Ummy kwenye hotuba yako umejinasibu kwamba kule Dar es Salaam mmefungua Benki ya Wanawake, Pwani wamefaidika, Dar es Salaam wamefaidika na mikopo wamepatiwa viwanja. Mimi naomba kwenye majumuisho yako ukija kujumuisha hapa uniambie ni lini Benki ya Wanawake itafunguliwa Mkoa wa Njombe ili sisi wa kina mama wa Njombe tuweze kufaidika na sisi na mikopo hiyo, lakini vilevile tuweze kufaidika tupate viwanja kama walivyopata akina mama wa Dar es Salaam, kama walivyopata akina mama wa Pwani. Hivyo, katika majumuisho yako nitapenda unijibu kwamba ni lini benki hiyo itafunguliwa ndani ya Mkoa wa Njombe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nimalizie kwa kuzungumza suala la haki za watoto hasa watoto wa kike. Akina mama wenzangu Mheshimiwa Faida Bakar mpaka ametoa machozi hapa kuhusiana na suala la watoto, nakubali kabisa sisi kama walezi, wazazi tunajitahidi sana kuwasaidia watoto wetu wasiingie kwenye ndoa za utotoni, lakini Sheria ya Ndoa ni kichocheo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninajua kabisa kuwa suala hili ni la Katiba na Sheria, lakini Mheshimiwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dada Ummy wewe ndiye unayesimamia haki ya mtoto wa kike. Nakuomba sasa kushirikiana na Waziri wa Katiba na Sheria, mlilete suala hili mapema ndani ya Bunge ili tuweze kulifanyia maboresho na tusibaki tu tunalalamika hapa.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia hotuba hii ya Waziri Mkuu. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema ya kuweza kusimama ndani ya Bunge hili Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kumpongeza Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kazi nzuri anayoifanya katika kuhakikisha kwamba anaisimamia Serikali yetu vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naipongeza Serikali ya Awamu ya Tano, Serikali ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa mambo mengi, mazuri, makubwa yaliyofanywa ndani ya miaka miwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kufufua Shirika la ndege la Tanzania, lakini vile vile naipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuweza kuimarisha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba ndani ya nchi yetu. Tumeona bajeti ya dawa imeongezeka kutoka shilingi bilioni 252 hadi shilingi bilioni 269. Jamani hili siyo jambo dogo. (Makofi)


Mheshimiwa mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano imeanza ujenzi wa reli ya kisasa ya Kimataifa (standard gauge), naipongeza pia. Tumeona barabara za juu zikitengenezwa (flyovers). Vilevile Serikali hii ya Awamu ya Tano imeweza kuimarisha ulinzi wa rasilimali zetu zikiwemo madini pamoja na maliasili. Hivi kesho Mheshimiwa Rais anakwenda kuzindua ukuta ambao utakwenda kulinda Tanzanite yetu ili isiendelee kupotea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaona kwamba kuna elimu bure, tunaona takriban shilingi bilioni 20.8 kila mwezi zinakwenda kuhudumia Shule za Msingi na za Sekondari. Naipongeza sana Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi nzuri inayoifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo haya yote mazuri yanafanywa kwa sababu ya amani na utulivu tuliokuwa nao ndani ya Tanzania. Mambo haya yasingeweza kufanyika kama kuna vurugu na fujo na kama kunakuwa hakuna amani. Naamini amani ipo na utulivu na ndiyo maana mambo haya makubwa namazuri yanaweza kufanyika vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuhakikisha kwamba anasimamia amani ya nchi yetu; na yeyote anayethubutu kutaka kuharibu amani ya nchi hii ni lazima ata-deal naye perpendicularly. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mazuri na upungufu pia upo. Nataka nizungumzie sasa changamoto ambazo ziko ndani ya Mkoa wetu wa Njombe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la elimu sisi tuna changamoto ya madarasa. Madarasa mengi bado ni chakavu, lakini vilevile tuna uhaba wa Walimu wa Sayansi kwa Wilaya zote; Wanging’ombe, Makete, Njombe na Ludewa. Tunaomba Serikali itusaidie tuweze kupata Walimu wa sayansi kwa wingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika Wilaya ya Ludewa tuna changamoto ya Walimu wa Shule za Msingi. Tunahitaji Walimu 521 ili kuweza kukidhi idadi ya Walimu katika Wilaya yetu ya Ludewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nizungumzie suala la Afya. Nakiri kwamba Mkoa wetu wa Njombe tunapokea pesa za dawa zaidi ya asilimia 90, tunaishukuru Serikali, lakini kwenye ile hospitali yetu ya Makambako mnaichukulia kama Kituo cha Afya. Labda niikumbushe Serikali; hospitali yetu ya Makambako ilipandishwa hadhi kuwa hospitali tangu mwaka 2013, hivyo basi, tunaiomba Serikali irekebishe ili tuweze kuletewa dawa kwa kiwango cha hospitali na siyo Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunatambua kwamba Mkoa wa Njombe ni Mkoa mpya, Serikali sasa ione umuhimu wa kujenga Hospitali ya Wilaya katika Wilaya yetu ya Wanging’ombe, lakini vile vile tunaomba Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Njombe Vijijini Jimbo la Lupembe. Ile Hospitali ya Kibena ambayo sasa hivi inatumika kama Hospitali ya Mkoa, tunaomba ipatiwe ukarabati tujengewe fence kwa sababu mbwa wanasumbua sana wagonjwa nyakari za usiku na Wauguzi. Kule kwetu mbwa ni wengi, kwa hiyo, tunaomba mtusaidie katika ukarabati wa fence hiyo ya hospitali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie suala la kilimo. Kwa sasa Mkoa wetu wa Njombe nafikiri na Mikoa mingine ya Tanzania bado kuna changamoto kubwa sana za pembejeo za kilimo. Pembejeo za kilimo zimekuwa ghali na ilhali mazao bei imeshuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Serikali itazame suala hili la pembejeo za kilimo, wakulima wetu wapate pembejeo za kilimo kwa bei nafuu ili kuweza kuuza mazao yetu kwa bei nzuri, kwa sababu kama pembejeo za kilimo ziko juu, moja kwa moja itaathiri uzalishaji, lakini vilevile na bei za mazao zitaendelea kushuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2015 na 2016 kuna Mawakala wetu wa pembejeo za kilimo kutoka Mkoa wa Njombe bado hawajalipwa pesa zao. Naiomba Serikali itoe tamko ni lini Mawakala hawa watalipwa pesa zao hizo za pembejeo za kilimo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile napenda kwenda kuzungumzia suala la maji. Suala la maji bado ni sugu Makambako Mjini, Njombe Mjini; baadhi ya maeneo kama Makete na kule Lupembe zaidi ya vijiji asilimia 50 havina maji. Pale Makambako na Njombe kuna tatizo kubwa kipindi cha kiangazi, maji hayapatikani kabisa, ukizingatia kwamba Makambako Mjini na Njombe ni Miji ambayo inaendelea kukua na mahitaji ya maji yanazidi kuwa makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa tunaomba, kuna ule mradi wa fedha za India ambao uko kwenye bajeti, tunaomba sasa zile pesa zitoke ziende zikatumike ili kuweza kuimarisha huduma ya maji katika miradi ile ya maji. Kwa mfano, kama mradi wa Mbukwa wa maji kule Wanging’ombe ili wananchi wetu waweze kuondokana na tatizo hilo la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kuzungumza suala zima la barabara za Mkoa wa Njombe, nimekuwa nikisimama mara kwa mara ndani ya Bunge hili Tukufu nikiomba barabara za Mkoa wa Njombe. Kama nilivyosema kwamba Mkoa wa Njombe ni mpya, sisi lami yetu tunayo moja tu ambayo inatoka pale Makambako kupita inakwenda Songea. Kwa hiyo, kwa uhalisia, Mkoa wa Njombe bado hatuna barabara kabisa ambazo ziko kwenye kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, basi naiomba Serikali iweze kutujengea barabara zifuatazo: Barabara ya lami kutoka Kibena - Lupembe kutokea Makete ambayo inakwenda kuunganika na Mkoa wa Morogoro. Vilevile kuna barabara ya Njombe – Makete - Kitulo kwenda kutokea Mkoa wa Njombe. Pia kuna barabara ya Njombe - Iyai kwenda kutokea Mkoa wa Njombe; na tuna barabara nyingine ya Njombe – Itoni - Ludewa kwenda Manda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba mtujengee kwa viwango vya lami ili kuweza kufungua milango ya biashara. Sisi watu wa Njombe tunalima sana, kule Makete kuna mazao ya mbao na viazi. Viazi vyote vinavyoliwa Mjini Dar es Salaam huko vinatoka Njombe. Tunaomba sana Serikali ione umuhimu wa kutengeneza barabara hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi kuweza kuchangia hotuba hii ya Wizara ya TAMISEMI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, napenda niungane na Mheshimiwa Peter Msigwa, Mheshimiwa Joseph Selasini na Mheshimiwa Hamidu Bobali kumpongeza Mheshimiwa Selemani Jafo kwa kazi nzuri anayoifanya ndani ya Wizara yake. Hii inadhihirisha ni jinsi gani Waziri huyu kwa kushirikiana na Naibu Mawaziri wake wanavyoweza kuisimamia Ilani ya Chama cha Mapinduzi inavyotakiwa. Pongezi sana kwa Waziri huyu na Manaibu wake Josephat Kandege na Mheshimiwa Joseph Kakunda, bila kumsahau Mheshimiwa George Mkuchika, hongereni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa maombi ya jumla ndani ya Mkoa wetu wa Njombe. Mara kwa mara nimekuwa nikisimama ndani ya Bunge hili Tukufu nikiuliza maswali, nikichangia Mheshimiwa Selemani Jafo watu wa Njombe shida yetu katika Wilaya zetu zote nne kwa maana ya Wanging’ombe, Ludewa, Makete na Njombe tuna uhaba wa Walimu wa Sayansi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba watuongezee Walimu wa sayansi, tunaomba watuongezee Walimu wa shule za msingi, tunaomba watuongezee Wauguzi na wataalam wa afya. Mheshimiwa Jafo tunamtegemea sana katika hili ili tuendelee kumsifu kwa utendaji wake mzuri wa kazi na tuna imani na yeye, sisi watu wa Njombe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba ya Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Selemani Jafo ukurasa wa 112, ameainisha mikakati mahsusi ambayo ataifanya mwaka huu mwaka wa fedha 2018/2019 na katika malengo hayo mahsusi ambayo ameainisha ni pamoja na ujenzi wa hospitali 67 katika Halmashauri 67 za Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kwa Mheshimiwa Waziri Jafo nimekuwa nikiomba mara kwa mara hospitali ya Wilaya ndani ya Halmashauri ya Wanging’ombe, namwomba Mheshimiwa Jafo na watu wa Wanging’ombe tuwe wanufaika katika kuhakikisha kwamba mwaka huu tuanze kujengewa hospitali ya Wilaya ya Wanging’ombe ndani ya Halmashauri yetu ya Wanging’ombe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Wilaya ya Njombe katika Halmashauri ya Njombe Vijijini, wananchi wameshaandaa eneo square meter 52, wananchi wamejitolea ili kuiweza kujenga hospitali ya Wilaya. Tunaomba sasa kwa kuwa wananchi wameshajitolea eneo la square meter 52, Wizara sasa watusaidie tuingie katika malengo haya mahsusi ya kujengewa hospitali ya Wilaya ya Njombe ndani ya Halmashauri ya Njombe Vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la elimu ndani ya Wilaya ya Wanging’ombe. Tunaishukuru Serikali kwa kutupatia pesa na kushirikiana na wananchi pia katika kuhakikisha kwamba tumeweza kuboresha miundombinu ya shule ya Wanike Sekondari na miundombinu ya Makoga Sekondari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Naibu Katibu Mkuu alikuja pale Makoga na Wanike Sekondari akatoa maelekezo ya kufanya. Sisi watu wa Wanging’ombe tumefuata maelekezo yale, tumekamilisha, miundombinu iko vizuri, tunachokiomba kwa Serikali ni kuhakikisha kwamba wanatupa kibali hivi sasa tuweze kuchukua wanafunzi wa kidato cha tano kuanzia mwaka huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la vituo vya afya, Wanging’ombe tuna kituo cha afya cha miaka mingi sana cha Makoga. Kituo kile hatuna huduma ya upasuaji kwa sababu hatuna chumba cha upasuaji. Ikitokea mtu anahitaji huduma ya upasuaji, inabidi atembee kilomita zaidi ya hamsini (50) kwenda kufuata huduma ya upasuaji katika hospitali ya Kibena. Tunaiomba Serikali itujengee chumba cha upasuaji na vilevile tunaiomba Serikali itupatie ile ambulance na vitanda viwili ambavyo vilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna Kituo cha Afya cha Palangavano, tunaishukuru Serikali kutupatia milioni 100 kuweza kujenga kituo kile. Niitarifu tu Serikali kwamba zile milioni 100 tuna uwezo wa kujenga mpaka kufikia lenta, tunaiomba Serikali mtupatie pesa tuweze kumaliza kituo kile cha Palangavano kwa sababu kituo kile ni kituo cha kimkakati, kipo katikati ya Wilaya ya Wanging’ombe, wananchi kutoka Luduga, kutoka Malangali, Usuka, Ilembula, Igwachanya ni rahisi kutumia kituo kile cha afya, hivyo basi naiomba Serikali iweze kutupatia pesa kwa ajili ya kuweza kumalizia ujenzi wa Kituo cha Afya Palangavano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la barabara katika Halmashauri ya Wanging’ombe, tunaomba kilomita mbili tu Igwachanya na tunaomba kilomita mbili Ilembula, lakini vilevile tunaomba watujengee daraja letu la halali ambalo liko pale Kata ya Ilembula, kwani kipindi cha masika tunapata tabu kuvuka, tunaomba mtusaidie kwa sababu daraja lile ni muhimu, watu wanalitumia kwenda Makao Makuu ya Wilaya ya Wanging’ombe kwa sababu ile Tarafa nzima ya Wanging’ombe na baadhi ya Kata kutoka Tarafa ya Imalinyu wanatumia daraja lile kupita kwenda Igwachanya katika Makao Makuu ya Wilaya ya Wanging’ombe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niende Ludewa tuna shule yetu ya sekondari ya Manda, tunaiomba Serikali watusaidie tuweze kukamilisha kuboresha mabweni, hivi sasa tupo katika kuboresha miundombinu ya maji na umeme, watusaidie tuweze kukamilisha na baadaye watupe kibali cha kuweza kupandisha hadhi ya kuweza kuchukua watoto wa kidato cha tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la afya ndani ya Wilaya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa. Wananchi wa Ludewa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wameweza kujenga vituo vya afya 17, tuko kwenye mchakato wa kujenga vituo vya afya 17. Uwezo wetu ni kujenga kuanzia ngazi ya foundation mpaka kuezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachokiomba kwa Serikali watusaidie katika suala zima la finishing kwa sababu wananchi wa Ludewa kwa kushirikiana na wadau tunaweza kujenga kuanzia msingi mpaka kuezeka. Hivyo ombi letu kubwa kwa Serikali ni kutusaidia katika finishing ya vituo hivi vya afya 17 ndani ya Halmashauri ya Ludewa ili viweze kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la barabara za Halmashauri ndani ya Wilaya ya Ludewa, tunaomba watujengee barabara ya Lupingu kwenda Matema beach. Barabara hii ni muhimu katika suala zima la ulinzi na usalama kwa sababu barabara hii iko karibu na mpaka wa Malawi na Tanzania. Vilevile barabara hii itatusaidia katika masuala ya utalii na itasaidia kufungua uchumi wa wananchi wa Wilaya ya Ludewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendee kwenye Halmashauri ya Makete. Kama unavyojua jiografia ya Wilaya ya Makete iko vibaya sana siyo rafiki katika suala zima la kufikika. Hivyo basi, tunaomba ile Tarafa ya Ukwama ipatiwe kituo cha afya ili wananchi wale wa Tarafa ya Ukwama ambao wapo pembezoni sana Makete waweze kupata huduma ya afya kwa urahisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie katika suala zima la Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake na Vijana, naomba Serikali ilete sheria ndani ya Bunge tuweze kupitisha ili tuweze kuwabana Wakurugenzi ambao hawatoi pesa zile za mikopo ya akinamama na vijana katika Halmashauri zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba kuunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi kuweza kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuimarisha huduma ya matibabu ya kibingwa nchini Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona hivi sasa kumekuwa na uimarishwaji wa huduma ya matibabu ya kibingwa Tanzania ikiwemo kupandikiza figo na kupandikiza vifaa vya kuongeza usikivu. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri tumeona wagonjwa wa figo walikuwa wanatibiwa nje ya nchi kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 100, lakini hivi sasa tunaishukuru Serikali yetu hii ya Chama cha Mapinduzi sikivu kuleta huduma ndani ya nchi yetu kwa gharama nafuu ya shilingi milioni 20. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika shilingi milioni 100 sasa tunakwenda kutibu wagonjwa watano, hili nalo dogo? Tumeona ongezeko la wagonjwa wa sukari, pressure na magonjwa yote haya yanapelekea matatizo ya figo.

Naipongeza Serikali imeweza kuleta huduma hii wakati muafaka ambao Tanzania tunahitaji huduma hiyo kwa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nikwambie dada yangu Mheshimiwa Ummy, kwa kazi hii nzuri mnayoifanya, historia itakukumbuka. Profesa Mseru - Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, endelea kufanya kazi baba yangu, kazi yako nzuri, historia itakukumbuka. Vilevile natambua kabisa jitihada hizi ni msukumo mkubwa na jitihada kubwa anazozifanya Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie suala la Saratani ya shingo ya uzazi. Kwanza niipongeze Serikali yangu kwa kuwa sikivu. Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi ni sikivu. Ukifuatilia hotuba yangu ya bajeti iliyopita ya mwaka 2017/2018 niliishauri Serikali ijikite katika suala zima la kinga katika magonjwa ya saratani ya shingo ya kizazi. Naipongeza Serikali na ninaishukuru, hivi sasa imeanza kutoa chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, chanjo hii sasa hivi inatolewa kwa wasichana wenye umri wa miaka 14, lakini naendelea kuiomba Serikali yangu sasa, nawapa ushauri mwingine, mhakikishe kwamba chanjo hii ya saratani ya shingo ya kizazi, mtoe elimu kule vijijini ili wananchi waelewe umuhimu wa chanjo hii. Kwa sababu jambo lolote jipya linapoingia nchini kwetu, watu hujawa na hofu. Kwa hiyo, kwa kupeleka elimu kule vijijini wakajua umuhimu huu, sasa watajitokeza wasichana wengi na wazazi watapeleka wasichana wao kwenda kupata huduma hiyo ya chanjo ya saratani ya shingo ya uzazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwa wale wanawake ambao wameshazidi umri wa miaka 14, naishauri Serikali iongeze jitihada za kuwapima ili tuweze kujua wangapi wamepata matatizo hayo na wangapi hawajapata. Kwa wale ambao wameshapata, basi waanze kupata matibabu kwa haraka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye suala la Hospitali za Rufaa za Mikoa. Naishukuru Serikali ya Awamu ya Tano imeweza kutupatia fedha, hivi sasa tupo kwenye ujenzi wa Hospitali yetu ya Mkoa ya Njombe.

Mheshimiwa Ummy nataka ukija kutoa majumuisho yako hapa wakati unajibu hoja, nataka kujua Hospitali ya Mkoa wa Njombe, Serikali mmetupangia pesa shilingi ngapi ili kuweza kuikamilisha kwa sababu mkoa wetu ni mpya. Kila siku nasema mkoa wetu mpya bado mambo mengi tunahitaji. Kwa hiyo, naomba mtupe kipaumbele sisi watu Njombe, mtupe pesa za kutosha ili tuweze kukamilisha ujenzi wa hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napenda kuzungumzia suala la hali ya mapambano dhidi ya UKIMWI. Nimesoma taarifa ya hali ya maambukizi ya UKIMWI nchini (Tanzania HIV Impact Survey 2016/2017); napenda kuishukuru Serikali na wadau mbalimbali, hivi sasa Mkoa wetu wa Njombe maambukizi ya UKIMWI yanazidi kupungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa ya mwaka 2011/2012 inaonesha kwamba maambukizi ya UKIMWI yalikuwa asilimia
14.8 Mkoa wa Njombe, lakini taarifa ya mwaka 2016/2017 maambukizi ya UKIMWI yameshuka mpaka asilimia 11.4. Ninatambua hizi ni juhudi za Serikali pamoja na wadau mbalimbali wanaopambana na vita dhidi ya UKIMWI. Vilevile ushauri wangu kwa Serikali na wadau, ni muda muafaka sasa, mshuke kule chini kwa wananchi mkawasikilize maoni na ushauri wao ili kwa pamoja muweze kujua jinsi gani mtaweza kumaliza tatizo hili la UKIMWI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeze Wizara ya Afya kwa kazi nzuri iliyofanya katika kuhakikisha kwamba sasa hivi dawa za Kifua Kikuu (TB) kwa watoto wetu zinapatikana. Zamani watoto wadogo walikuwa hawana dozi kamili ya dawa za kifua kikuu. Utakuta kile kidonge kinakatwa robo tatu, robo mbili, mara mtu anakosea kukata, mtoto anaongezewa dozi, mara mwingine anapewa dozi haijakamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali kwamba sasa wameleta dawa za kifua kikuu kwa ajili ya watoto, dozi ambayo iko rafiki kwa watoto. Kama alivyosema Mheshimiwa Waziri, dawa ile ina flavor ya matunda, kwa hiyo, hata mtoto anakuwa anakunywa kwa urahisi na anaweza kupata matibabu vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa napenda niungane na Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli kumpongeza Profesa Mohamed Janabi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa kazi nzuri anayoifanya kuhakikisha utoaji wa matibabu ya moyo nchini kwetu Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia hotuba hii ya bajeti. Kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Mpango na Mheshimiwa Dkt. Ashantu kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wizara yao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze tu kwa kusema bajeti hii ni nzuri kwa sababu imejikita katika kuhakikisha kwamba inalinda viwanda vyetu vya ndani lakini vilevile imeweka urahisi wa kuanzisha viwanda vipya. Kwa mfano, tuna zero rate katika viwanda vinavyozalisha mafuta ya kula na mafuta haya ya kula yanatumia malighafi ambayo tunalima ndani ya nchi yetu ikiwemo michikichi, alizeti na parachichi kule Mikoa ya Njombe na Iringa. Naishauri Serikali iangalie upya Sera ya Viwanda na Uwekezaji ili tuweze kuwa na viwanda vidogo, viwanda vya katina viwanda vikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile naiomba Serikali iweke mkazo katika kuhakikisha kwamba tunajitosheleza kwa kuwekeza kwenye viwanda ambavyo vinazalisha malighafi ili iweze kutumika katika viwanda vikubwa. Kwa vile viwanda ambavyo vinazalisha malighafi vitumie malighafi ambayo zinatokana na mazao yetu humu nchini kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini nasema hivyo? Tunaweza tukatoa mfano tukawa na viwanda vinavyochambua mbegu na pamba, kiwanda hicho kinachochambua mbegu kinaenda kutumika kama malighafi kwenye kiwanda ambacho kinatengeneza mafuta. Hali kadhalika ile pamba inaenda kutumika kama malighafi kwenye viwanda ambavyo vinatengeneza majora ya nguo na majora ya nguo yanaenda kutumika kama malighafi kwenye viwanda ambavyo vinatengeneza suruali, sketi, mashati na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie mifumo ya upatikanaji wa mapato kwa kutumia teknolojia ya IT. Mheshimiwa Waziri katika kitabu chake cha bajeti amesema kwamba tutaendelea kuendeleza mifumo ya upatikanaji wa mapato kwa kutumia teknolojia ya IT. Ni jambo jema lakini nilitaka kumwambia Mheshimiwa Waziri ili kuendana na mifumo hiyo katika suala zima la ukaguzi ni vyema Serikali ikaweka mkazo kuhakikisha wakaguzi wetu wa ndani na wa nje wanaenda sambamba na teknolojia hiyo ili kuweza kuwasaidia kipindi cha ukaguzi. Kwa sababu kama ukaguzi hautaendana na mifumo hiyo, utatokea udanganyifu mkubwa kipindi cha ukaguzi. Hivyo basi, Serikali ione umuhimu kwa Internal na External Auditors wetu waweze kupata elimu hii ya teknolojia mpya katika mifumo ya ukusanyaji wa mapato. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini nasema hivyo? Nimepitia taarifa ya ukaguzi ambayo ilifanywa na Mkaguzi wa Nje, Eng. Maganga Machi, 2018, katika Halmashauri ya Misungwi. Katika mambo ambayo amegundua Mkaguzi huyu kulikuwa na baadhi ya mashine za kukusanyia ushuru ambazo hazikuunganishwa kwenye mfumo zaidi ya miaka miwili. Kutokana na kutokuunganishwa huko kwa mashine hizo za kukusanyia ushuru kwenye mifumo kumesababisha kupotea kwa pesa nyingi ndani ya halmashauri hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tujiulize, wale Wakaguzi wa Ndani wanafanya ukaguzi katika halmashauri kila baada ya miezi mitatu kwa mwaka (quarterly) na muda wa miaka miwili mashine hizo za POS hazikuunganishwa na mfumo na wao wamekuwa wakikagua ndani ya miaka miwili ina maana wamekagua zaidi ya mara nane ndani ya miaka miwili bila kugundua kwamba kuna pesa zinaibiwa mpaka alipokuja External Auditor kutoka Mwanza na kugundua kwamba kuna tatizo hilo na kuna pesa ambazo zimeibiwa kwa sababu tu ya hizo Point of Sale Machine hazijaunganishwa na mfumo ili kuweza kusaidia ukaguzi wa ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nizungumzie suala la gawio la asilimia 5 kwenye halmashauri zetu. Kwanza niipongeze Serikali kwa kuondoa riba katika gawio la asilimia tano kwa wanawake na vijana kwenye halmashauri zetu. Naiomba Serikali pesa hizo zitoke kwa wakati ili ziweze kwenda kuwasaidia wanawake pamoja na vijana kwenda kufanya maendeleo na vilevile kukuza uchumi wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niende kwenye sanitary pads, niwapongeze kwa kuondoa kodi katika suala zima la uingizwaji wa sanitary pads. Hata hivyo, nilitaka nimkumbushe Mheshimiwa Waziri tuna viwanda vya ndani ambavyo vinatengeneza sanitary pad na lengo letu ni kuvikuza viwanda vyetu vya ndani viweze kufanya kazi vizuri lakini ukiangalia hii kodi iliyoondolewa kwenye hizi sanitary pads imewa-favor wale watu wanao-import hizo sanitary pads. Hivyo basi, naishauri Serikali iangalie ni jinsi gani inaweza ikapunguza kodi kwenye malighafi ambayo inatumika kutengeneza sanitary pads ndani ya nchi yetu ili hivi viwanda vya ndani viweze ku-compete na zile sanitary pads zitakazokuwa zinaingia ndani ya nchi yetu, ziweze kushindana vizuri kwenye soko nao waweze kuuza kwa bei ya chini ili ile azma yetu ya kuwasaidia watoto wetu wa kike katika suala zima la kupata sanitary pads kwa bei nafuu tuweze kulifikia. (Makofi)

Mheshimia Naibu Spika, mwisho kabisa nipongeze kwa msamaha wa penalty na interest ambayo mmetoa kwa muda wa miezi sita. Mimi nashauri muongeze muda iwe mwaka mmoja ili kuweza kuwa-motivate wafanyabiashara wetu waweze kufanya biashara vizuri na kwa kujiamini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya na kuweza kusimama ndani ya Bunge hili Tukufu kuweza kuchangia mjadala huu wa bajeti ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri wanayoifanya na ambayo wanaendelea kuifanya ya usajili wa wakulima. Kwa sababu naamini kwa kufanya usajili wa wakulima kutatupelekea tuwe na takwimu sahihi ambayo itatusaidia kujua mahitaji sahihi ya wakulima katika masuala ya pembejeo, masuala ya masoko, lakini vilevile na miundombinu ya kilimo kwa maana ya maghala. Kwa kuwa tutakuwa na takwimu sahihi itatusaidia kupanga mipango sahihi ya kutatua changamoto mbalimbali za wakulima pamoja na wadau wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niwapongeze kwa kuanza kufanya tathmini ya afya ya udongo, kwa sababu kwa kufanya tathimini ya afya ya udongo itawasaidia wakulima wetu kulima mazao sahihi, sehemu sahihi na vilevile kutumia pembejeo sahihi katika maeneo yao ambayo itawezesha kuongeza uzalishaji na vilevile kuongezeka kwa kipato cha mkulima mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya pongezi hizo nilikuwa napenda sasa niishauri Serikali katika maeneo mbalimbali, nitaanza na kilimo cha biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuweze kubadilika ni lazima kabisa tuachane na kilimo cha jembe la mkono tujikite kwenye commercial farming. Niseme tu, isiwe large scale tuwekeze kwenye small scale ili kuweza kuwalenga kundi kubwa la wakulima wadogo nao waweze kutumia nyenzo za kisasa wakati wanafanya shughuli za kilimo kwa maana ya kutumia matrekta, lakini vilevile waweze kufanya kilimo cha umwagiliaji ambacho wataweza kuvuna na kulima zaidi ya mara mbili kwa mwaka. Hivyo basi Serikali ione umuhimu wa kuweza kuchimba malambo maeneo mbalimbali ya nchi yetu ili wakulima hawa waweze kupata fursa ya kuweza kufanya kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la kilimo chenye tija; na utakubaliana na mimi kabisa kwamba wakulima wetu wanatumia gharama kubwa sana katika uzalishaji kuliko kile kivuno wanachokipata. Wakulima wengi wanapata mavuno machache hivyo basi inawapelekea pia hata faida ile ya kilimo chao kuwa faida ndogo. Ningependa niishauri Serikali; kwanza kabisa muhakikishe kwamba hili zoezi la tathimini ya afya ya udongo linakamilika mapema ili kuweza kusaidia kilimo chetu kiweze kuleta tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niiombe Wizara hii ya Kilimo ikae na Wizara ya Viwanda ione namna bora ya kutengeneza vivutio kwa wawekezaji ambao wanawekeza katika viwanda vya pembejeo, kwa maana ya viwanda vya mbolea, ili kusudi wakiwekeza kwa wingi, wakifungua viwanda vingi vya mbolea ndani ya nchi yetu hii itapelekea wakulima wetu kupata mbolea kwa bei nafuu lakini vilevile itawasaidia wakulima wetu kuwa na uhakika wa mbolea pindi wanapokuwa wanahitaji na vilevile itakuwa kichocheo cha wakulima wengi kutumia mbolea na matokeo yake kilimo chetu kitaenda kuwa na tija, uzalishaji utaongezeka kipato cha mtu mmoja mmoja kitaongezeka na taifa kwa ujumla. Vilevile tukumbuke pia uanzishwaji wa viwanda hivyo vya mbolea italeta ajira kwa vijana wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende pia kuishauri Serikali katika suala zima la ushuru wa pembejeo za kilimo. Niishauri Serikali itoe ushuru katika pembejeo za kilimo, kwa maana ya mbolea na viuwadudu, ili kumpa nafuu mkulima aweze kununua pembejeo hizi kwa gharama nafuu na kuweza kuzalisha kwa gharama nafuu na kuweza kupata faida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la mbegu, naendelea kuishauri Serikali itumie vituo vya utafiti vya mbegu na kuviimarishavituo ili kuhakikisha kwamba wanazalisha mbegu bora ili wakulima wetu waweze kupata mbegu bora na kuweza kuzalisha mazao bora na kuweza kupata faida. Vilevile waangalie mbegu hizo zinaenda mahali gani, kwa mfano kwenye sehemu ambazo zina ukame wahakikishe kwamba mbegu wanazozipeleka kule ziwe zinakubaliana na hali halisi ya ukame. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kuzungumzia zao la parachichi ndani ya Mkoa wa Njombe. Kwanza kabisa nimpongeza Mheshimiwa Rais, alipokuja Mkoa wa Njombe kwenye ziara yake ailituhakikishia kwamba tutapata ndege ya mizigo ambayo itakuwa inatua Songwe na kuweza kubeba parachichi zetu sisi wakazi wa Mkoa wa Njombe, lakini vilevile na wa Songwe na wa Mbeya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii fursa ya zao la parachichi sisi wananchi wa Mkoa wa Njombe tumeipokea vizuri, tunalima kwa wingi, hivyo basi nilipenda kumshauri Mheshimiwa Waziri wa Kilimo akae pamoja na Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi waone namna bora ya kuweza kutumia reli ya TAZARA kwenye, yale mabehewa ya mizigo baadhi yao watengenezewe mfumo wa ubaridi na upoozwaji, kwa maana ya cold room, ili wakulima wengi watumie njia ya reli ya usafirishaji ambayo ni rahisi zaidi uki-compare na njia zingine. Hivyo basi nawashauri Wizara hii ikae na Wizara ya ujenzi ione namna bora ya kutumia ile reli ya TAZARA ili tuweze kusafirisha mazao yetu ya parachichi na yaweze kufika kwa mlaji wa ndani na wa nje yakiwa na ubora ili tuweze kuuza kwa bei nzuri na kuweza kulipa kodi na kuchangia Pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nilikuwa napenda kumwambia Mheshimiwa Waziri; hii fursa ya parachichi; maana kila mtu sasa hivi anajua kwamba parachichi sasa hivi ulimwenguni inaitwa green gold kwa sababu ina thamani kubwa sana na kila mtu sasa hivi amehamasika kulima parachichi. Lakini ningependa kumwambia Mheshimiwa Waziri, tukumbuke kwamba hii fursa ambayo sisi Watanzania hususani Mkoa wa Njombe tumeiona na Nyanda za Juu Kusini kwa maana ya Iringa na Mbeya tumeiona ya kulima parachichi na nchi zingine nayo wanaiona fursa hii, hivyo nilikuwa napenda kuishauri Serikali muhakikishe kwamba mnaingia mkataba mzuri na nchi walaji katika masuala ya masoko ili kuweza kulinda soko la mkulima wa parachichi ndani ya Tanzania yetu. Kwa sababu mnaona kwamba demand ya parachichi ni kubwa lakini kadri muda unavyozidi kuendelea kwa sababu fursa hii imeonwa na nchi nyingi baadaye supply ya parachichi itakuja kuwa kubwa na demand itakuwa iko pale pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi kumsaidia mkulima wa parachichi wa Mkoa wa Njombe na mikoa mingine ambayo inalima parachichi ndani ya Tanzania ni vyema basi mkaweka mikataba mizuri kwa nchi walaji ili kuweza kulinda soko la parachichi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Madini
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa kibali cha kuweza kusimama na kuweza kuchangia hotuba hii ya Wizara ya Madini.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa kazi nzuri ya kuamua kujenga ukuta Mererani. Nilipongeze Jeshi, nimpongeze Mkuu wa Majeshi, General Venance Mabeyo, kwa usimamizi mzuri wa ujenzi huu wa ukuta wa Mererani. Tumeona ndani ya miezi mitatu Jeshi limeweza kujenga kilometa 24.5 na kutumia gharama ndogo ya bilioni 5.2 ambazo kwa mkandarasi wa kawaida Serikali ingeweza kutumia zaidi ya bilioni nane na kutumia muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pongezi hizi si bure tu, tumeweza kuona matunda ya ukuta huu wa Mererani na tumeona kwamba mapato ya Tanzanite yameongezeka kutoka milioni 700 kwa mwaka, na katika taarifa ya Mheshimiwa Waziri amesema mpaka kufika Machi, mapato ya Tanzanite yameongezeka mpaka bilioni 1.43 na hivi sasa ninavyozungumza mapato ya Tanzanite yameongezeka mpaka bilioni 2.3. Hongera sana Wizara ya Madini kwa kazi nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niendelee pia kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Madini kwa kazi nzuri anayoifanya ya kusimamia uanzishwaji wa masoko ya madini. Ndani ya muda mchache wa miezi miwili tumeona kwamba wameshaweza kufungua masoko 13 ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuanzishwa kwa masoko haya, nilikuwa na ushauri katika Wizara hii ya Madini.

Mheshimiwa Spika, kwanza; Mheshimiwa Waziri na timu yako mhakikishe kwamba mnasimamia vizuri masoko haya ya madini ya kuhakikisha kwamba yanatimiza lengo lililokusudiwa na yasiende kugeuka kuwa kichaka cha wafanyabiashara haramu wa madini. Vile vile niwashauri Wizara hii muendelee kuwafanyia utafiti wa madini wachimbaji wadogo ili kuweza kuwapunguzia gharama ya uchimbaji. Vilevile endeleeni kuwatengea maeneo mengi wachimbaji hawa wadogo wa madini na ambayo yameshafanyiwa utafiti ili kuweza pia kuwapunguzia gharama za utafiti wachimbajia hawa wadogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia niiombe Serikali iwasaidie wachimbaji wadogo katika suala zima la environmental impact assessment kule kwenye maeneo yao ambayo wanachimba madini. Muhakikishe kwamba mnawaelekeza namna bora ya kuchimba madini lakini wakati huo huo wakiwa wanatunza mazingira.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie suaa la mradi wa Liganga na Mchuchuma. Mimi na Watanzania wengine hususan wakazi wa Mkoa wa Njombe Wilaya ya Ludewa tungependa sana kujua hatma ya mradi huu wa Liganga na Mchuchuma, kwani tumeweza kusikia mambo mengi mazuri yanayotokana na mradi huu lakini vilevile mradi huu umekuwa ni kichocheo kikubwa katika uchumi. Kwa sababu mradi huu endapo kama utamalizika utatoa ajira za moja kwa moja kwa watu 5,000 lakini ajira ambazo indirect kwa maana ya kwamba ya wakandarasi na jamii ambayo inazunguka mradi ule watu 30,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vile vile mradi huu kama utakamilika utaenda kuchangia Pato la Taifa (GDP) asilimia tatu mpaka asilimia nne. Hivyo basi na sisi wananchi wa Mkoa wa Njombe tuna hamu ya kuyaona mafanikio hayo na hivyo tunaiomba Seri kali iweze kutuambia status ya mradi huu iko vipi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimalizie tu kwa kusema, huu ni mradi wa kielelezo wa mpango wa miaka mitano kuanzia mwaka 2015 mpaka 2016 na 2020 mpaka 2021; lakini mpaka sasa ninavyozungumza hapa takriban miaka minne imeshapita na umebaki m wak ammoja tu hivyo basi kilio chetu wananchi wa Mkoa wa Njombe hususana Wilaya ya Ludewa tunaomba kujua status ya mradi huu Mheshimiwa Waziri ukija kufanya wind up, na kinyume cha hapo kwakweli utanisamehe Mheshimiwa naweza nikaja kushika shilingi.

SPIKA: Ahsante sana kwa kutumia muda wako vizuri sana.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimechangia kwa kuongea na malizia point yangu ya mwisho ambayo muda haukutosha. Naishauri Serikali kule bandarini iweke single receiving point ya mafuta, faida kubwa ya hii kwana hupunguza dermrage charges, ambayo humpunguzia mzigo muagizaji wa mafuta au mfanyabiashara wa mafuta.Vilevile itampunguzia gharama mlaji ikiwemo gharama za kuendesha viwanda zitaungua. Serikali pia itapata faida endapo tukipunguza dermrage change ambazo zinaingia kwenye gharama ya uendeshaji kwa mfanyabiashara wa mafuta ambayo inaathiri mapato ya Serikali kwa maana ya corporate tax.

Mheshimiwa Naibu Spika, single receiving point ya mafuta hii itaondoa utunzaji wa mafuta kwenye matanki ya makampuni binafsi kuwepo unafuu wa upotevu wa mafuta kwa 3% mpaka 5% kitu ambacho hupunguza mapato ya Serikali sababu wafanyabiashara wa mafuta wanaingiza kwenye gharama za uendeshaji ambazo zinaenda kuathiri corporate tax. Kwa kuwa hii ni sheria watu wanataka advantage kukwepa kodi.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuweza kuchangia hotuba hii ya Wizara ya fedha na Mipango.

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya ya kuweza kusimama ndani ya Bunge hili Tukufu na kuweza kuchangia hotuba hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli wka kazi kubwa anayoifanya ya kutekeleza miradi mikubwa ambayo itakuja kuleta tija na kujenga uchumi endelevu wa nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza pia Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na timu nzima ya Wizara hii ya Fedha kwa kuona umuhimu wa kutumia malighafi za kilimo, mifugo, uvuvi, madini katika kuzalisha bidhaa mbalimbali kwa ajili ya soko la ndani ya nchi yetu na ziada kwa ajili soko la nje na vilevile na kuongeza ajira kwa vijana.

Mheshimiwa Naibu Spika, dira yetu ni ya kujenga nchi ya viwanda; ni vyema basi tukajenga viwanda ambavyo vitatumia malighafi inayopatikana ndani ya nchi yetu kama hizo malighafi za kilimo, mifugo, uvuvi, madini n.k.

Mheshimiwa naibu Spika, nchi yetu imejaaliwa sana kuwa na malighafi hizi ndani ya maeneo mbalimbali ya nchi yetu. Ukiangalia kule Ludewa, nchi yetu imejaaliwa kuwa na madini ya chuma katika mradi wa Liganga na Mchuchuma. Kule kwenye mradi wa Liganga na Mchuchuma kuna takribani tani 128 za chuma ambazo zimechanganyika na madini mengine. Haya madini yanaweza kutusaidia kujenga uchumi wetu kama tukiamua kuyachimba na kuyatumia katika viwanda vya kutengeneza nondo, mabati, viwanda vya kutengeneza vifaa vya ujenzi wa madaraja na reli. Kwa kuweza kuzalisha chuma hiki tutaweza kuokoa pesa bilioni 640 kila mwaka kwa muda wa miaka 30 ya uhai wa mgodi huu wa Liganga na Mchuchuma, sambamba na kutengeneza ajira 35,000 zitakazotokana na mgodi huu wa Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie suala la malighafi ya misitu. Mkoa wa Njombe, Songwe, Mbeya, Iringa, Katavi, Rukwa, Tanga na mingineyo ndani ya nchi yetu ya Tanzania ina malighafi nyingi sana za misitu lakini vilevile misitu hii tuna kila aina ya mbao; tuna soft wood, tuna hard wood, tuna mianzi tuna mpaka nta ya kuweza kutengenezea furniture. Nilikuwa naiomba Serikali ihamasishe wawekezaji ambao watatumia malighafi hizi za mbao kuwekeza katika viwanda vya kutengeneza karatasi kwa wingi. Kwa kufanya hivi tutakwenda kutumia karatasi zetu za ndani ya Nchi bila kuagiza nje ya Nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile niishauri Serikali ihamasishe wawekezaji wa viwanda vya furniture ili waweze kuwekeza kwa wingi ndani ya nchi yetu na tuendelee kununua furniture ambazo zitakuwa zinatengenezwa ndani ya nchi yetu ambazo zina ubora zaidi ukilinganisha na zile ambazo zinatoka nje ya nchi. nyingi ambazo zinatoka nje ya nchi zinakuwani mavumbi tu ya mbao, siyo mbao halisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile ni wakati muafaka wa kujiuliza hivi kwa nini Serikali inaendelea kununua samani nje ya nchi ilhali tuna JKT, tuna Magareza, tuna viwanda vya watu binafsi ambavyo vinatengeneza mbao ndani ya nchi yetu. Na kwa hili niiombe sana Serikali iangalie namna bora ya kusaidia viwanda hivi vya furniture ambavyo viko ndani ya nchi yetu lakini vilevile na kuhamasiaha zaid wawekezaji wapya wa kuweza kuwekeza katika vianda hivi vya furniture na kuwatolea tozo na kodi ambazo si za lazima katika ufanisi wa viwanda hivi vya furniture. Vilevile wawaondolee kodi katika vile vifaa ambavyo vinatumika kurembea furniture zetu. Kwa mfano, vitasa, kuna vile vimishikio, msasa, vanish, vyote hivyo viondolewe kodi ili kuweza kuhamasisha ufunguaji wa viwanda vingi ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nilikuwa naiomba Serikali iongeze kodi kwa furniture zile ambazo zinatoka nje ya nchi ili kuweza kulinda viwanda vya furnitures ambavyo viko ndani ya nchi na ambavyo vitakavyoendelea kufunguliwa ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiwa bado katika suala zima la utengenezwaji wa samani bado kuna hii mlaighafi ya ngozi. Namini kabisa Tanzania tuna malighafi nyingi ya ngozi, tukiachilia mbali kutengeneza tu mikoba na viatu tuangalie namna bora ya kuweza kuwekeza zaidi katika viwanda vitakavyoweza kutumia malighafi ya ngozi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kule Ethiopia wenzetu wameingia mkataba na Kampuni ya Mercedes Benz. Nchi ya Ethiopia ina-supply ngozi ambayo inatengeneza viti ambavyo vinatumika katika magari ya Mercedes Benz. Nilikuwanaishauri Serikali ifanye utafiti na uwezekano wa kuingia mikataba kama hiyo ambayo Ethiopia wenzetu wameingia ili kuweza kutumia malighafi ya ngozi yetu lakini vilevile na kuweza kuongeza uchumi wa taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, sitoridhika kama nitamaliza kuchangia hotuba hii bila kuzungumzia malighafi ya mazao ya kilimo na hususani katika zao la parachichi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Njombe, Songwe, Rukwa, Mbeya, Iringa na Mikoa mingine ndani ya Tanzania inalima sana parachichi; na tunaishukuru Serikali kwa mikakati mbalimbali ambayo imefanya ya kuweza kuwasaidia wakulim wa parachichi kusafirisha nje ya nchi parachichi hiyo ikiwa ghafi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo bado, Serikali itafute namna ya kuhakikisha kwamba inahamasisha wawekezaji ambao watakuja kutumia malighafi hii ya parachichi ndani ya nchi yetu kuweza kufungua viwanda mbalimbali ambavyo vitatumia malighafi ya parachichi hii vikiwemo viwanda vya cosmetics kama mafuta ya nywele, lotion, conditioner kwa ajili ya nywele. Vile vile malighafi hii ya parachichi tunaweza kufungua viwanda vya kutengeneza asali pamoja na dawa ambazo zinatokana na majani ya parachichi. Kwa kufanya hivyo, tutaweza kukuza uchumi wa nchi yetu na kuweza kuendelea mbele. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwa kuishauri Serikali, kule bandarini nilikuwa naishauri Serikali iweze kuanzisha, iweke ile single receiving point ya mafuta. Kwa kuweka single receiving point ya mafuta, faida kubwa itasaidia katika kupunguza zile demurrage charges ambazo zinakwenda kumsaidia mfanyabiashara wa mafuta kumpunguzia mzigo. Halikadhalika itaenda ku...

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa, kengele ya pili ilishagonga.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia hotuba hii ya Wizara ya TAMISEMI.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa afya na kutuweka hai ndani ya miaka yote mitano hadi hivi leo tukishirikiana vizuri Wabunge wote pamoja na Mawaziri na Mheshimiwa Spika katika kutekeleza majukumu ambayo tulipewa na wananchi wetu ili tuje kuwawakilisha humu ndani ya Bunge. Nichukue nafasi hii kumwomba Mungu aturudishe wote kwa umoja wetu ili tuendelee kuwatumika wananchi wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kuipongeza Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi nzuri iliyofanya ndani ya miaka mitano. Nampongeza Rais, Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu. Vilevile, nampongeza Waziri, Mheshimiwa Jafo pamoja na Manaibu wake Mheshimiwa Kandege na Mheshimiwa Waitara kwa kazi nzuri waliyoifanya ndani ya Wizara hii. Nawaombea Mungu awarudishe tena na awarudishe kwenye nafasi zao ili waweze kukamilisha yale mambo mengine ambayo wamepanga kuwafanyia wananchi wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda pia kuwapongeza na kuwashukuru wananchi wa Mkoa wa Njombe hususani akina mama kwa kujitoa kwa moyo wote katika kuchangia masuala mbalimbali ya maendeleo ili kuhakikisha kwamba mipango yote na kazi zote zilizopangwa na Wizara hii zinatekelezeka kwa urahisi. Nawapongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sipongezi tu bila kuwa na sababu, nina sababu za msingi. Naipongeza Serikali ndani ya miaka mitano imejenga vituo vya afya 433. Ndani ya Mkoa wetu wa Njombe tunaishukuru Serikali tumepata vituo vya afya zaidi ya 10. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile niendelee kuipongeza Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi na Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Magufuli kwa kazi nzuri waliyoifanya kuhakikisha kwamba wamejenga zahanati 368. Ndani ya Mkoa wetu wa Njombe tumejengewa zahanati zaidi ya 10. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze Serikali pamoja na Rais wetu mpendwa kwa kazi nzuri waliyoifanya ndani ya miaka mitano ya kujenga Hospitali za Wilaya 98. Ndani ya Mkoa wetu wa Njombe tumepata hospitali tatu, Njombe DC, Makambako TC na Halimashauri ya Wanging’ombe. Vilevile, tumeona kwamba kuna hela zimetegwa kwa ajili ya wodi zetu, Halmashauri ya Wanging’ombe tunashukuru tumepata, Halmashauri ya Makambako TC tumepata lakini sijui mmetusahau kidogo kule Njombe DC muweze kufanya mambo yaweze kukaa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya kazi kubwa sana ndani ya miaka mitano. Kusema kweli kwa kazi nzuri aliyoifanya Mheshimiwa Rais naomba Watanzania wampe nafasi tena aweze kukamilisha mambo yale ambayo amekusudia kuyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imejenga madarasa 19,808, nina kila sababu ya kuipongeza Serikali. Serikali imejenga maabara 227 ndani ya miaka mitano na matundu ya vyoo 7,922. Hongera sana kwa Serikali, hongera sana kwa Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile shule zetu zimeweza kupata madawati 5,070,896, hongera kwa Serikali. Serikali haikuishia hapo imefanya kazi kubwa ya kukarabati shule kongwe 73 zikiwepo baadhi ya shule ndani ya Mkoa wangu wa Njombe. Sisi watu wa Njombe ni wa shukrani, tunaishukuru Serikali na tunaahidi hatutafanya makosa Oktoba, 25. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niipongeze pia Serikali imejitahidi, imejenga barabara kilometa 74,940. Hayo yote ni mambo mazuri ambayo yamefanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi chini ya Jemedari wetu, Rais wetu mpendwa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mpango mzuri ambao Serikali imeweka kwa ajili ya bajeti ya mwaka 2020/2021. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Jafo na Manaibu wake na timu nzima pale Wizarani kwa mkakati mzuri waliojiwekea wa kuhakikisha kwamba watakwenda kujenga maabara saba (7) na zahanati tatu (3) katika kila Halmashauri. Mimi sina cha kusema zaidi ya kuwatakia kheri Mawaziri hawa na Rais wetu na timu nzima, Mungu awape afya njema ili waje kutekeleza yale walioyokusudia kuyafanya. Kwa maana hiyo, namwombea Mheshimiwa Rais arudi, namuombea Mheshimiwa Waziri Jafo na Manaibu wake warudi Ubunge na kwenye nafasi zenu ili muweze kuifanya kazi hii vizuri na muikamilishe vizuri ndani ya miaka mitano mingine inayokuja.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nikutakie kheri wewe pamoja na Mheshimiwa Spika na Wabunge wote kila kheri turudi kukamilisha yale ambayo wananchi wetu wametutuma tuje kuukamilisha kwa umoja wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii kuwashukuru kina mama wa Mkoa wa Njombe kwa kuniamini na kwa kweli nimewatendea haki kama mnavyoniona na kila siku sichoki kuuzungumzia Mkoa wa Njombe. Kwa hiyo, nitumie pia nafasi hii kuwaomba ridhaa wanipe tena miaka mitano ili nije kukamilisha yale ambayo nilikuwa nimepanga kuja kuyazungumzia.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, nashukuru na naunga mkono hoja. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia mada hii. Awali ya yote, nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kunirudisha tena ndani ya Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia niwashukuru wapigakura wangu, akinamama wa Mkoa wa Njombe kwa kunichagua kwa kura nyingi za kishindo na kuweza kurudi tena ndani ya Bunge hili. Vilevile nikishukuru chama changu Chama Cha Mapinduzi kwa kuteua jina langu na kuniwezesha kuwa Mbunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri aliyoifanya ndani ya miaka mitano kuweza kutekeleza miradi mikubwa mbalimbali ndani ya nchi yetu, ukiwemo Mradi wa Stiegler’s, ukiwemo Mradi wa Standard Gauge. Miradi hii itakwenda kuufanya uchumi wetu wa Tanzania kuwa uchumi mkubwa lakini vilevile uchumi endelevu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, dira yetu ya Tanzania ni dira ya uchumi wa viwanda ambao utakuwa shindanishi lakini vilevile jumuishi kwa maisha bora ya Watanzania. Nimeona Wizara wana mipango mizuri ya kuhakikisha kwamba wanatumia malighafi mbalimbali zilizopo ndani ya Tanzania yetu ili kuweza kujenga uchumi imara na endelevu. Malighafi hizo zikiwa ni pamoja na malighafi ya uvuvi, malighafi zinazotokana na mazao, malighafi zinazotokana na madini na malighafi ambazo zinatokana na mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza kujielekeza kwenye malighafi ambazo zinatokana na madini. Kule kwetu Ludewa, Mkoa wa Njombe sisi tuna Mradi wa Liganga na Mchuchuma. Kwenye mradi ule kuna takribani madini ya chuma pamoja na mengine tani milioni 128. Kama Serikali itaamua sasa kutekeleza mradi ule, tutakuwa na chuma kingi ambacho kitasaidia kama malighafi katika viwanda vya kutengeneza nondo, mabati, vifaa vinavyotumika kwenye madaraja na vifaa ambavyo vinatumika kwenye reli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi huu wa Liganga na Mchuchuma, kama Serikali itaamua kuanza kuutekeleza tutakwenda kuokoa takribani bilioni 640 kwa mwaka ndani ya miaka 30 ya uhai wa mgodi huu wa Liganga na Mchuchuma, sambamba na kuweza kuzalisha ajira 35,000. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali, sisi wananchi wa Mkoa wa Njombe kwa muda wa miaka mingi tumekuwa tukiupigania, tumekuwa tukisimama, Wabunge mbalimbali wamekuwa wakisimama ndani ya Mkoa wa Njombe na Mikoa jirani kuiomba Serikali ianze kutekeleza Mradi huu wa Liganga na Mchuchuma. Kwa sababu kama nia yetu ni kukuza uchumi wa Tanzania, mradi huu kama utatekelezwa utakwenda kuchangia Pato la Taifa (GDP) asilimia tatu mpaka nne. Naomba Serikali itusikilize ili iweze kutekeleza mradi huu wa Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie malighafi ambazo zinatokana na mazao kama ya mbao. Mikoa ya Njombe, Songwe, Mbeya, Iringa, Rukwa, Katavi na Tanga ni wakulima wazuri sana wa mazao ya mbao. Naiomba sasa Serikali ihamasishe wawekezaji wa viwanda vya karatasi ili sisi Watanzania sasa twende kutumia karatasi zetu za hapa hapa Tanzania na kuhamasisha kufunguliwa kwa viwanda hivi vya karatasi. Hii itatusaidia pia kukuza ajira kwa watoto wa Kitanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nashangaa sana kama ikiwa mpaka sasa hivi Serikali na watu wengine tunaendelea kuagiza furniture kutoka nje ya nchi wakati tuna Magereza, JKT na wananchi ambao wana viwanda vya kutengeneza furniture, wanatengeneza furniture nzuri na zenye ubora kuzidi zile zinazoingizwa kutoka nje ya Tanzania ambazo nyingi ni mavumbi ya mbao, siyo mbao halisi kama zile furniture zinazotengenezwa hapa nchini kwetu Tanzania. Naiomba Serikali, i-discourage uingizaji wa furniture kwa kuweka kodi kubwa katika bidhaa hii na kupunguza gharama za kodi katika raw materials kama msasa na zile accessories ambazo zinatumika kunakshia furniture ili kuchochea uanzishwaji wa viwanda vingi vya furniture ndani ya Tanzania yetu na kuweza kukuza uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakuwa nimejipunja sana kama sitazungumzia malighafi ya zao la parachichi ambalo liko ndani ya Mkoa wangu wa Njombe. Halikadhalika Songwe, Iringa, Katavi na mikoa mingine ya Tanzania wanalima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali imefanya jitihada kubwa sana ya kuweza kuwasaidia wakulima wetu wa parachichi kuweza kusafirisha parachichi nje na kuuza ikiwa ghafi. Naona ni wakati sasa Serikali ijikite katika kuhakikisha kwamba inahamasisha viwanda vinavyotengeneza cosmetics inayotumia malighafi ya parachichi kama conditioner ya nywele au lotion, majani ya parachichi unaweza ukatengeneza asali au dawa. Serikali ihamasishe viwanda hivi vya kutengeneza cosmetics ambayo inatokana na malighafi ya parachichi, viwekezwe kwa wingi nchini wakati huo tukiendelea kuhamasisha wakulima kuendelea kulima parachichi kwa wingi. Kwa kufanya hivyo, itasaidia pia kuongeza ajira kwa viwanda hivi ambavyo vitaenda kufunguliwa ndani ya mikoa yetu hii ya kulima parachichi na kuweza kukuza uchumi wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kuzungumzia malighafi inayotokana na wanyama. Naipongeza Serikali kwa jitihada mbalimbali inazochukua kuhakikisha wameweza kuhamasisha na ku-convince viwanda mbalimbali vinavyotumia ngozi kutengeneza mikoba, viatu na mikanda. Naomba tusiishie level hiyo ya kutengeneza tu viatu, mikanda na mikoba, hebu tuige kwa wenzetu wa Ethiopia. Wao ndio wanao-supply ngozi katika Kampuni ya Mercedes Benz kwenda kutengeneza zile seat cover zake. Naomba Serikali ifikirie katika mlengo huo, hii yote ni katika kuweza kukuza pato la Taifa letu na uchumi wetu na kuufanya uweze kuwa endelevu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Wizara ya Kilimo. Juzi hapa Mheshimiwa Hussein Bashe alizungumza namna bora ya kuboresha mbegu ili tuweze kupata malighafi nyingi kwa kuwa na mbegu bora katika masuala mazima ya kilimo. Haitoshi, inabidi Wizara ya Kilimo ishirikiane na Wizara ya Viwanda, baada ya kuwa Wizara ya Kilimo inaweka mikakati mizuri ya kuboresha mbegu zetu ili kuweza kupata malighafi bora na kuongeza mavuno, inabidi Wizara ya Viwanda ikae makini katika kuhakikisha kwamba malighafi hizo zinazotokana na kilimo zinatumika hapa hapa Tanzania katika kuchochea viwanda, kwa kuhamasisha viwanda vingi kufunguliwa ndani ya nchi yetu na kukuza uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuweza kuchangia Hotuba hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa nianze kwa kutoa pole kwa watanzania wote kwa msiba mkubwa uliotupata lakini vilevile nitambue mchango mkubwa uliofanywa na Hayati Dkt. Magufuli kwa kushirikiana na mama yetu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Ni mchango mkubwa sana uliofanyika ndani ya muda mchache sana na mafanikio makubwa sana, tumeyaona na tutayaendelea kuyaona.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nijielekeze katika masuala ya kilimo na mazao ya mbogamboga. Ni zaidi ya asilimia 90 ya mazao ya mbogamboga yanayosafirishwa kupitia bandari ya Mombasa, kitu ambacho kinawapa gharama kubwa sana wafanyabiashara na wakulima wa mazao haya ya mbogamboga. Natambua Wizara ya Kilimo na Wizara ya Viwanda wamekaa kwa pamoja na kuweza kuanzisha mradi wa Kurasini Agricultural Logistic Hub itakayokuwa once stop center ambayo ndiyo itakuwa cold chain ya mazao haya ya mbogamboga yanapokuwa yanasubiri kwenda kusafirishwa nje ya nchi kwa kutumia bandari yetu ya Dar es Salaam. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na mradi huu ni mradi ambao umehusisha sekta binafsi. Niwapongeze sana Wizara ya Kilimo na Wizara ya Viwanda kwa kuwa wasikivu kwa sababu haya ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ambayo aliyatoa wakati akiwa Makamu wa Rais mwaka jana. Kwa kweli viongozi wa namna hiyo ndio ambao tunawahitaji katika Taifa letu la Tanzania; pale mkubwa anapotoa tu maelekezo na kuweza kuyafanyia kazi mara moja. Lakini kwa kuwa Kurasini Agricultural Logistic Hub ndio muarubaini wa mazao ya mbogamboga kusafirisha kupitia bandari kwenda nje, nilitaka kujua, ni lini mradi huu utakamilika na kwa sasa hivi mradi huu umefikiwa wapi? Ili tuweze kujua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Kilimo tunatambua kwamba imeanzisha mchakato wa Bodi ya Horticulture. Nataka kujua pia bodi hii ipo kwenye stage gani na lini itakamilika. Sababu katika mazao ya mbogamboga kuna zao ambalo linakuja kwa kasi sana, zao la parachichi. Na kama tunavyojua ni mikoa zaidi ya kumi Tanzania inalima zao hili la parachichi ikiwemo mkoa wa Njombe, Iringa, Songwe, Mbeya, Rukwa, Tanga na mikoa mingine. Kuna umuhimu sana wa bodi hii ya horticulture kukamilika ili zao hili la parachichi pamoja na mazao mengine ya mbongamboga yawe yanafanyiwa kazi kwa utaratibu mzuri na kuweza kuleta tija kwa wakulima wa mazao haya ya mbogamboga likiwemo na zao la parachichi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika zao hili la parachichi, Mheshimiwa Waziri Mkuu alikuja Njombe akatembelea baadhi ya mashamba ya parachichi, nilimuomba Mheshimiwa Waziri Mkuu kwamba zao hili sasa ikiwezekana liwekwe katika zao la kimkakati kutokana na umuhimu na unyeti wake. Zao hili kama tutalisimamia vizuri tutaweza kuongeza mapato ndani ya Taifa letu lakini vilevile tutawakwamua wananchi kupitia ajira kupitia ajira mbalimbali zitakazotokana na zao hili la parachichi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, fursa hii tunayoiona sisi ya kulima zao la parachichi na kusafirisha nje, imeonwa na nchi nyingine nyingi. Ombi langu kwa Serikali ni kuhakikisha kwamba wanawasaidia wananchi ambao wanalima zao hili la parachichi kwa kuweka mikataba mizuri na nchi walaji kwa maana kwamba watakapokwenda kuuza hili huko nje Serikali imeshaweka mikataba itakayokuwa inawasaidia wananchi wetu wasikandamizwe. Kama hii fursa imeonwa sasa hivi na nchi nyingi baadaye soko linaweza kuharibika. Kama sisi tutakuwa tumewahi kuweka mikataba mizuri ina maana tutakuwa tumewasaidia kuwalinda wananchi wetu wasiweze kutaabika siku zijazo kutokana na supply kuwa kubwa na demand kupungua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kuwa Serikali imefanya kazi nzuri, imeshaagizia ndege ya mizigo kwa ajili ya kuweza kusafirisha mazao haya ya mbogamboga ikiwemo na parachichi na vilevile natambua kwamba Serikali imeandaa mfumo mzuri wa cold-room katika Kiwanja cha Ndege cha Songwe, lakini bado siyo wote wanaweza kusafirisha kwa kutumia ndege wengine watatumia Bandari ya Dar es Salaam. Pamoja na kuanzisha mradi mzuri ule wa Kurasini, bado kuna umuhimu wa kuboresha mfumo wa cold room kwenye baadhi ya mabehewa katika Reli yetu ya TAZARA ili wale wananchi wa Nyanda za Juu Kusini ambao wanalima zao hili la parachichi waweze kusafirisha parachichi yao kuanzia ile process ya kutoa shambani, kusafirisha sasa kutoka kule Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, kupelekeka Dar es Salaam waweze kutumia reli hii ambapo gharama ni nafuu kuliko usafiri mwingine watakaotumia mfano kama vile maroli na kadhalika ambayo gharama ni kubwa sana. Kwa hiyo, kwa kutumia reli, wanaweza wakasafirisha kwa gharama nafuu na hapo ndiyo tutaona umuhimu wa kutumia ile Bandari ya Dar es Salaam baada ya kumaliza mradi ule. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwa kuzungumzia Bima ya Afya. Tunashukuru Bima ya Afya iko vizuri lakini kuna maboresho makubwa yanatakiwa yafanyike kwa wananchi, kwa sababu wanalalamika, wanapotumia Bima ya Afya ya Serikali kule hospitali hawapati dawa, kuna umuhimu wa kuboresha. Vilevile, ukija kwa Wabunge humu ndani, Wabunge wengi Bima hii ya Afya haiwafaidishi kwa sababu utakuta watu wengine ni wazee, kwa mfano, Mzee Mheshimiwa Athuman Maige, mama yangu Mheshimiwa Margaret Sitta, hawana watoto wenye chini ya miaka 18. Vilevile utakuta kuna Wabunge vijana humu, hawana watoto wadogo, hawajazaa kabisa. Kwa hiyo, bima hii ijielekeze kutumika kwa watu tegemezi, kwa maana kama mama yangu pale Mheshimiwa Margaret Sitta na baba yangu Mzee Mheshimiwa Athuman Maige, bima ile ikasadie wazee wao maana wazazi wao wapo. Vilevile kwa vijana hawa ambao hawana watoto ikasaidie wazazi wao.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa, kengele ya pili imeshagonga.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Bima hii ya Afya iangaliwe na ifanyiwe maboresho makubwa kwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakini vilevile kwa wananchi wetu ili iweze kuleta tija na maana halisi ya Bima ya Afya. Kwa sababu nia yetu ni kusaidia wananchi lakini vilevile kuwasaidia Wabunge ukiwemo na wewe na Mheshimiwa Naibu Spika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha, ahsanteni sana. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja na siyo kwamba nafagilia kugombea Ukamishna. (Kicheko)

NAIBU SPIKA: Aaah, kwa hiyo hugombei tena? Ndiyo unamaanisha hivyo?

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nagombea ila hoja muhimu. (Kicheko)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Viwanda Na Bishara
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi na mimi kuweza kuchangia katika Wizara hii ya Viwanda na Biashara. Nimpongeze Mheshimiwa Waziri na timu yake nzima ya Wizara hii ya Viwanda na Biashara kwa kazi nzuri wanazozifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nitazungumzia maeneo matatu, nitazungumzia katika Mamlaka ya Viwango (TBS), lakini vilevile, nitanzungumzia Liganga na Mchuchuma na nitamaliza kwa kuzungumzia malighafi ya parachichi katika kuchochea uwazishwaji wa viwanda vya kuchakata zao hili muhimu la parachichi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mamlaka ya Viwango (TBS) ninavyojua mimi kazi yake ni kuangalia afya za wananchi wa Tanzania kuwa salama kutokana na bidhaa zinazoingizwa ndani ya nchi. Hivi karibuni kumekuwa na mabadiliko ya bidhaa zinazoingia ndani ya nchi kama magari yale ambayo used yanayoingia ndani ya nchi yakabadilishiwa mfumo wa ukaguzi kutoka kwenye ile system ya zamani ya pre-arrival inspection kuja kwenye destination inspection.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zamani TBS waliingia mikataba na makampuni ya Japan pamoja na Dubai katika ukaguzi wa magari haya na kazi ilikuwa inafanyika vizuri sana, lakini vilevile TBS haikuingia gharama yoyote katika ukaguzi huu wa magari zaidi ya kupokea percent ambayo waliokuwa wanapewa na makampuni yale na katika ukaguzi wa magari haya magari yalikuwa yanakaguliwa katika dola 150 mpaka 300 kwa gari moja inategemea na ukubwa wa gari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile ndani ya miaka 10 TBS iliweza kupata USD milioni 10 kama percent waliokuwa wanapewa na yale makampuni. Mimi najiuliza kwa kuwa kazi ya TBS ni kuangalia na kulinda afya za Watanzania kutokana na hizi bidhaa zinaingia ndani ya nchi. Leo imeamua kubadilisha mfumo wa ukaguzi wa magari haya yawe yanakaguliwa hapa nchini, mashaka ambayo niliyonayo, kazi ile ni ngumu na ni nzito. Lakini vievile inatakiwa tujiandae vizuri kuhakikisha kwamba tunaweza kuthibiti uingizwaji wa magari mabovu ndani ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema hivyo? Nina wasiwasi na miundombinu ambayo inatumika kukagua magari haya, mfano kule Japan katika kampuni hizo tano walikuwa na uwezo wa kukagua magari 2,000 ndani ya mwezi mmoja, lakini nimefuatilia hapa Tanzania gari moja inakaguliwa ndani ya masaa mawili na kuna meli ambazo zinabeba magari zaidi ya 2,000, mashaka yangu hakutakuwa na mrundikano wa magari pale bandarini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile unapoileta gari hapa, mteja ameshanunua gari ameshaileta hapa Tanzania, inakaguliwa na TBS itakaposema hii gari ni mbovu hii gari itakwenda wapi? nina wasiwasi nchi yetu isijekwenda kuwa dumping country. Lakini vilevile huyu Mtanzania ambaye amejikwamua mwenyewe ameona gari mtandano kuna hawa watu wanaitwa Wapalestina wanauza magari mpaka dola 500 mpaka dola 1,000 bila kujali iko kwenye ubora gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mtantanzia wa watu amejikwamua amenunua gari ameileta imefika bandarini hapa anaambiwa aikarabati ili iweze kukidhi viwango zaidi ya ile pesa aliyoinunulia, hatuoni kwamba tunakwenda kuwanyanyasa wananchi wetu wanyonge ambao yeye amependa kujikwamua aweze kuwa na usafiri wake wa kumpeleka kazini na kwenye shughuli zake. Leo anaambiwa kwamba hii gari haina ubora unabidi ugharamie kuikarabati na ataingia gharama kubwa. Wakati zamani zile kampuni zinazouza magari kwa mfano kama hawa wanaojiita Beforward ukinunua gari kwa Beforward yeye kule anaponunua kwenye mnada anaiangalia kabla hajaileta Tanzania ataipeleka kwenye zile kampuni za kuangalia ubora wa gari; akiipelekea kwenye ile kampuni akiona kama kuna changamoto zozote za kurekebisha ile gari Beforward ilikuwa inafanya yenyewe kwa niaba ya mnunuzi aliyenunua.

Sasa leo kubadilisha mfumo ule ina maana sasa tunamuongezea gharama mnunuzi ambaye ni mwananchi mnyonge Mtanzania. Mimi nilikuwa naomba suala hili mliangalie kwa umakini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile Serikali imekwenda kuwekeza bilioni 20 kwa ajili ya kutengeneza miundombinu hii ya ukaguzi wa magari, wakati bilioni 20 hii si mngetuletea sisi Njombe, Mbeya kule, Rukwa maeneo tunayolima parachichi tukaweza kufungua viwanda vya kuchakata zao la parachichi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la Liganga na Mchuchuma; naiomba sana Serikali sana iongeze kasi ya majadiliano yanayoendelea ili mradi huu uanze mara moja. Sisi wananchi wa Mkoa wa Njombe na wananchi wa Nyanda za Juu Kusini na Kusini kwa ujumla pamoja na Watanzania wote mradi huu utakwenda kuwa ni kichocheo kikubwa sana kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja lakini vilevile Tanzania kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tumekuwa tukizungumza miaka mingi sana ndani ya Mbunge tangu mwaka 2010 tunazungumzia Liganga na Mchuchuma. Nilifikiri kipindi kile tumeanza kutengeneza standard gauge mradi huu ungekuwa tayari umeshaanza kufanya kazi ili raw materials za chuma ziweze kutumika katika vile vifaa ambavyo vinatengeneza reli, lakini vilevile tuna miradi mingi inayoendelea madaraja hii malighafi ya chuma ingeweza kutumika katika kutengeneza standard gauge pamoja na reli zingine ambazo zinaendelea na ambazo zinatakiwa kutengenezwa na madaraja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ukizungumizia makaa ya mawe juzi hapa nilimuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri wana mkakati gani kuhakikisha kwamba NDC kuachia baadhi ya vitalu ili wananchi waweze kuchimba makaa hayo kwa sababu kuna uhitaji mkubwa sana wa makaa haya ya mawe. Na Serikali ilikubali kwamba wananchi sasa waanze mchakato wa kuomba ili waweze kupewa vitalu hivyo. Sikupata nafasi ya kushukuru, nashukuru kwa majibu hayo na wananchi wa Ludewa pamoja na Njombe na wadau wengine wa maeneo mbalimbali ambao wanajishughulisha na biashara hizi za wachimbaji wadogo wadogo wapo tayari na wataanza kuleta maombi hayo ili muweze kuyafanyia utekelezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sitojisikia vizuri kama nitamaliza kuchangia bila kugusa malighafi ya zao la parachichi. Kama tunavyojua malighafi ya parachichi inalimwa mikoa mingi takribani mikoa 12, jirani yangu hapa anatoka Jimbo la Hai naye ameniambia Hai wanalima sana zao la parachichi. Hebu hii Wizara sasa iangalie ni namna gani inakwenda kuwakomboa vijana katika suala zima la ajira katika kuhakikisha kwamba wanaleta wawekezaji wengi ndani ya nchi ili waweze kuanzisha viwanda hivi vya kuchakata parachichi kama ni takribani mikoa 12 ina maana tuna uwezo wa kuanzisha viwanda vingi sana vya kuchakata zao hili la parachichi na hii itakwenda mkombozi kwa Taifa letu kwa sababu vijana wetu watakwenda kupata ajira, lakini vilevile tutawasaidia wakulima hawa wa zao la parachichi kuweza kuboresha malighafi hii iwe na thamani zaidi baada ya ku-export parachichi kama parachichi, sasa tuanza ku- export mchuzi wa parachichi, lakini vilevile majani, mbegu zile zote zifanye kazi na wananchi wetu waweze kupata mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Viwanda nakuomba sana ukae na Waziri wa Kilimo muone namna bora ya kuweza kulipeleka mbele zao hili la parachichi. Ulimwenguni wanajua zao hili la parachichi inaitwa green gold, kwa hiyo, ni wakati sasa kuhakikisha kwamba mnaweka kipaumbele na mnaweka mkakati mahususi na mnaweka jitihada kubwa katika kuhakikisha kwamba mnapeleka zao hili mbele hili kuweza kumkwamua mkulima mmoja mmoja na vilevile kuweza kuchochea uchumi na kuongeza mapato ndani ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi ndio njia za kuweza kuongeza mapato,…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Neema.

MHE. NEEMA W. MGAYA: …siyo kwenda kuongeza mapato kwa TBS. TBS haina kazi ya kuongeza mapato, kazi yake ni kuangalia afya ya Mtanzania, kuzuia bidhaa ambazo zitakwenda kuathiri afya ya Mtanzania sio kazi ya TBS kuongeza mapato. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia. Kwanza nikupongeze kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti katika Bunge hili Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niwapongeze; Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri; Katibu Mkuu, Dkt. Allan Kijazi; na watendaji wote wa Wizara hii ya Maliasili na Utalii kwa kazi nzuri wanayoifanya. Vile vile niwapongeze Mheshimiwa Waziri na timu yake kwa kuweza kusaini Mkataba wa REGROW. Pia tunawashukuru sisi Nyanda za Juu Kusini kwa kutupatia magari 12 kwa ajili ya operesheni za mbuga ambazo ziko Nyanda za Juu Kusini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Waziri pia kwa kusaini GN. Najua huu ni mwanzo mzuri wa kuanza ujenzi wa Ofisi ya Makao Makuu kwa ajili ya kutangaza utalii Nyanda za Juu Kusini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua REGROW Phase I imechukua Mikumi National Park, Nyerere National Park, Udzungwa pamoja na Ruaha. Ni matumaini yangu kwamba Phase II mtachukua Kitulo National Park pamoja na hifadhi nyingine za Taifa zilizopo Nyanda za Juu Kusini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Taifa ya Kitulo ni hifadhi nzuri sana; ina maua mazuri ya kila aina. Ni hifadhi ambayo hakuna ulimwenguni inayofanana na Kitulo National Park. Ina maua mazuri pamoja na ndege wa ajabu ambao wanakuja kila mwaka mara moja; wanatoka Australia moja kwa moja mpaka Kitulo, hawasimami sehemu yoyote. Kuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba Phase II ya REGROW, Kitulo National Park ambayo iko Wilaya ya Makete ndani ya Mkoa wa Njombe inaingizwa kuwa sehemu ya mradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwanzo nilishawahi kuwauliza watu wa Utalii, hivi kwa nini hawakuiingiza Kitulo National Park katika huu Mradi wa REGROW? Wakaniambia, unajua barabara kule haziko rafiki na nini; lakini nitumie nafasi hii kusema kwanza, nampongeza Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa kushirikiana na Mheshimiwa Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kutengeneza ile barabara ya Njombe – Makete. Hivi sasa nina habari njema; Mheshimiwa Rais Samia ameshatuingizia pesa za kilometa 25 kutoka Makete kupitia Hifadhi ya Kitulo kutokea Mbeya. Kwa hiyo, sitategemea tena kuwe na sababu ambazo zinahusiana na masuala ya miundombinu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, asubuhi hapa Mheshimiwa Mrisho Gambo amejinasibu sana akasema kwamba asilimia 80 ya pesa zinazotokana na utalii zinatoka Kaskazini. Niwakumbushe basi Wizara, sasa hivi mwangalie maeneo mengine. Mje Nyanda za Juu Kusini, kuna vivutio vingi vya utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Nyanda za Juu Kusini mfanye ile mnaita package tourism (utalii wa vifurushi). Mtalii anatua Iringa, anaenda Ruaha National Park, anaenda kuangalia historia ya Mkwawa, anakwenda Sao Hill kufanya utalii wa picha, akitoka hapo anakwenda Njombe, anakwenda Kitulo National Park, anapita pale Kipengele, anatoka anaenda Songwe kuangalia kimondo pamoja na maji moto; anaweza akatoka hapo akaenda Mbeya kuangalia zile waterfalls na mambo mengine ambayo yanavutia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile anaweza akaamua kwenda kwa Mheshimiwa Waziri kule Ruvuma kuangalia historia ya wamisionari kwenye Jimbo la Mheshimiwa Jenista. Kuna njia ambayo wamepita watumwa zamani; na huo ndiyo mwanzo wa umisionari kule Ruvuma. Yote hayo mnaweza mkayaweka kwa pamoja mkafanya hiyo package tourism. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia msisahau kule Njombe kuna mashamba mazuri ya chai, kuna mashamba mazuri ya miti, mnaweza mkafanya farm tourism. Hivyo vyote ni vivutio. Sisi hatujajaliwa wanyama wengi sana kule Southern Highland, lakini tuna utalii ambao wanaita wa ikolojia, mnaweza mkafanya vizuri na tukaweza kuiingizia nchi yetu mapato. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna baadhi ya vivutio ambavyo wananchi na Waheshimiwa Wabunge wa kutoka Nyanda za Juu Kusini waliweza kuviainisha. Ni kazi sasa ya Wizara kuvifanyia kazi ili vithibitishwe rasmi. Kwa mfano, kuna Gereza hili la Kihesa Mgagao Iringa; Wabunge wa Iringa hapa miaka mitano wamezungumza. Lile gereza lina wafungwa 17 tu, yaani wafanyakazi ni wengi kuliko idadi ya wafungwa. Lile gereza, Nelson Mandela alipita pale akalala. Kile chumba ni historia nzuri, nayo ikaingia katika package ya utalii kwa Iringa na Nyanda za Juu Kusini kwa ujumla. (Makofi)

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.


MWENYEKITI: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa mzungumzaji, Mheshimiwa Neema Mgaya, kuhusiana na hilo gereza. Ni kwamba aliwahi kuja Balozi wa South Africa hapa nchini, alipokuta kuwa ni gereza, akakataa kuingia pale kuona kile chumba ambacho mzee Mandela alilala pale. Kwa hiyo, unaweza kuona kwa namna gani tunapunguza watalii, maana yule angeweza pia kuwa balozi wetu wa utalii kule South Africa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Neema Mgaya, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea kwa mikono miwili. Hapo sasa ndiyo Wizara iangalie namna gani tunapoteza mvuto katika suala hili la utalii kwa vitu vidogo vidogo lakini vyenye msingi na ambavyo vinaweza vikatuongezea pia mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule Ogidivai, kule Wanging’ombe, kuna lile jiwe linaitwa Ogidivaa, lina ramani ya Afrika na jiwe lingine hapo hapo pembeni lina ramani ya South America. Vitu kama hivyo mvichukue. Pia kuna Msitu wa Nyumbanitu. Huo msitu uko Wanging’ombe, una kuku Weusi mbao hawajawahi kufugwa na mtu na wanazidi kuongezeka siku hadi siku. Ukienda pale unawakuta, hawafi, wapo tu. Kwa hiyo, vitu kama hivyo ni vya kuviongeza katika hiyo package tourism. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilishasema kule Iyangweni na Matuhu, unajua majina ya huku Songea ni magumu magumu; hiyo nayo mnaweza mkaiingiza pia ikawa kwenye sehemu ya package tourism. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa, nizungumzie suala la migogoro ya ardhi kati ya hifadhi za TANAPA pamoja na…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Mgaya.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba mwende mkatatue mgogoro wa Hifadhi ya Mpanga Kipengele inayozungukwa na Vijiji vya Malangali, Mlangali, Mpanga, Iyai, Igando na Ruduga. Migogoro ya ardhi kati ya hifadhi na wananchi imekuwa mingi. Mheshimiwa Waziri nendeni mkashughulikie mmalize migogoro hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naunga mkono hoja. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia bajeti hii. Kwanza kabisa nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuonyesha upendo mkubwa kwa Watanzania, ukisoma mapendekezo ya bajeti hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameonyesha upendo kwa makundi mbalimbali ya wananchi wa Tanzania kwa kupunguza tozo kandamizi mbalimbali katika makundi mbalimbali wakiwemo wakulima, wafanyabiashara, kama bodaboda, kwa kupunguza tozo ya faini kutoka shilingi 30,000 mpaka shilingi 10,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, kipee kabisa nampongeza Rais, Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa aliyoifanya jana kwa maelekezo mazuri na maamuzi mazuri aliyoyatoa kuhusiana na mradi mkubwa wa Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa Liganga na Mchuchuma kuna takribani tani milioni 128 za chuma pamoja na madini mengine. Mradi huu ukianza kutekelezwa utakwenda kutupatia malighafi ya chuma ambayo itatumika kutengezea nondo kwenye viwanda vyetu vya nondo, mabati, viwanda vya vifaa vya kutengeneza madaraja na viwanda vya vifaa vya kutengeneza reli. Kwa mradi huu, utatachochea uanzishwaji wa viwanda vingi vinavyotumia malighafi ya chuma. Sina shaka SGR aliyokwenda kuifungua kuanzia Mwanza huenda ikatumia malighafi ya chuma inayotokana na Liganga na Mchuchuma kama tutatekeleza vizuri kufuatana na Mheshimiwa Raisi alivyosema.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile nampongeza Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu kwa sababu ameona kwamba mradi huu wa Liganga na Mchuchuma tutakwenda kuokoa takribani shilingi bilioni 640 ndani ya mwaka mmoja kwa muda wa miaka 30 ya uhai wa mradi huu wa Liganga na Mchuchuma. Hivyo natoa pongezi nyingi sana kwa mama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile hiyo ni sambamba na kuzalisha ajira 35,000. Hii pesa tutakayoenda kuokoa ni shilingi bilioni 640 kila mwaka ndani ya miaka 30. Itasaidia miradi ya maendeleo ndani ya nchi yetu. Wale watakaokwenda kuajiriwa, hao watu 35,000 watatusaidia pia katika kulipa kodi na kuendelea kupata mapato na kuweza kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nampongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri pamoja na timu yao nzuri ya Wizara ya Fedha. Naunga mkono pendekezo waliloleta la kutatua changamoto ya fedha ambazo zilikuwa zikirudi Hazina kila mwisho wa mwezi wa Sita na kuzifanya fedha zile sasa ziwe zinaenda kwenye akaunti ya amana ili ziweze kuendelea kutekeleza miradi ambayo ilikuwa haijamalizika. Hii itasaidia kuchochea kumalizika kwa miradi mapema na vilevile kwa ufanisi mkubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimekuwa nikuzungumza mara kwa mara umuhimu wa zao la parachichi ndani ya Bunge hili la Tanzania. Kwa sababu Parachichi sasa hivi ni green gold, ni zao ambalo linakua kwa haraka. Takribani mikoa 12 ikiwemo na Mkoa wangu wa Njombe tunalima zao hili la parachichi. Tunawashukuru sisi wakulima wa hot culture, wa mbogamboga, kwa pamoja na maua.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya mbogamboga tunakuta hili zao la parachichi. Tunawashukuru kwa kutoa kodi ya vyumba vya ubaridi (cold room). Tunawashukuru sana, kwani hii itatusaidia sisi wakulima wa mazao ya mbogamboga pamoja na maua hususan wakulima wetu sisi ambao wanalima parachichi kuhifadhi mazao yale, kwa sababu mazao haya ya mbogamboga pamoja na maua, biashara yake kubwa ni kwa ajili ya kusafirisha nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa kutoa kodi ina maana sasa wakulima wataenda kutengeneza vyumba hivi vya ubaridi kwa wingi na kuweza kuhifadhi mazao hay ana kuweza kuyasafirisha nje ya nchi yakiwa na ubora na itasababisha kuongeza pato la Tanzania. Kwa sababu bidhaa zetu zitakuwa zinafika kwa mlaji zikiwa bora. Vilevile itawajengea imani kwa mazao ya mbogamboga na maua yanayotoka Tanzania na kuweza kuongeza wateja wengi ambao watakuwa wananunua mazao kutoka nchini kwetu Tanzania na kuweza kuongeza pato la Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimalizie kwa kusema, hakuna kitu kilichokuwa kinaniudhi na kilichokuwa kinanikosesha raha na kilikuwa kinaniuma sana kama kutoza kodi mara mbili (double taxation). Wale wafanyabiashara wa Zanzibar ambao walikuwa wanakuja kununua bidhaa huku Tanzania Bara kwa kweli tulikuwa hatuwatendei haki. Isitoshe sisi Watanzania Bara na Tanzania Zanzibar, tuna mahusiano, tumeoleana, kwa hiyo, tuna undugu. Unaweza ukaenda kwa mkwe wako; kwa mfano, kama mimi, naweza nikafika Tunguu kule Zanzibar kwa wakwe zangu wakaniambia tunakupa TV hii umpelekee mjukuu wetu. Nafika pale custom tena nalipishwa ushuru kweli! Hapana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono asilimia mia moja, tozo hii ya kulipa mara mbili mbili kwa kweli mmewatendea haki Wazanzibar. Wazanzibar ni ndugu zetu, ni jamaa zetu, ni marafiki zetu, ni wakwe zetu; Zanzibar na Tanzania Bara ni Tanzania moja. Kwa hiyo, kwa kuondoa tozo hizi mbili mbili itatusaidia kuendelea kuujenga Muungano wetu wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawashukuru. Naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia katika Wizara hii ya TAMISEMI. Nimpongeze Mheshimiwa Waziri pamoja na wasaidizi wake wote kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wizara hii ya TAMISEMI. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikianza na TARURA tumeona kuna ongezeko kubwa la bajeti ya TARURA, ukilinganisha kuanzia mwaka 2020/2021 bajeti ya TARURA ilikuwa bilioni 275, ikaja 2021/2022 ikapanda mpaka bilioni 722 na hivi sasa tunavyozungumza bajeti ya TARURA 2022/2023 ni bilioni 802. Hi ni hatua kubwa sana ambayo itasaidia kuboresha barabara zetu za vijijii. Napenda kuwaambia TARURA Mkoa wa Njombe, sisi wananchi wa Mkoa wa Njombe ni wazalishaji wazuri sana wa vyakula pamoja na zao la chai. Kwa kuwa tumekuwa na changamoto kubwa sana kwa wakulima wetu wa chai, chai kuharibika zinapotoka kule mashambani kwenda kwenye viwanda, zinafika zikiwa hazina ubora kutokana na changamoto za barabara.

Mheshimiwa Spika, sasa hivi naamini kwa bajeti hii na kwa mwendo huu mzuri wa Serikali ya Rais Samia kuhusiana na suala zima la kuboresha barabara zetu za vijijini, naamini sasa barabara hizi zitakwenda kuwa mkombozi wa chai zetu kutoharibika na kufika kwa ubora na wakulima wetu wa chai wataweza kupata pesa nzuri wanapokwenda kuuza kule viwandani. Ushauri wangu kwa TARURA Njombe ni wakati sasa wa kufanya survey za barabara zetu mapema ili barabara zetu za vijijini ziweze kujengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa nizungumzie suala la afya ya msingi. Katika suala la afya ya msingi nimeona kwenye bajeti ya TAMISEMI wanaendelea kukamilisha ujenzi wa zahanati, vituo vya afya, hospitali zetu, lakini sambamba na kupeleka vifaa tiba katika hospitali, zahanati na vituo vya afya ambavyo vimekamilika. Ni jambo zuri ni kazi nzuri wanayoifanya, lakini ushauri wangu nawaomba kuna changamoto kubwa sana ya wauguzi kwenye vituo vyetu vya afya, kwenye hospitali zetu, kwenye zahanati zetu na Mkoa wa Njombe kwa kweli tatizo hili limekuwa ni kubwa mno kwa Majimbo yetu yote sita ndani ya Mkoa wa Njombe na hata ukizungumza na baadhi ya Wabunge kwenye mikoa yao bado changamoto ya wauguzi ni kubwa sana. Kwa hiyo naiomba Serikali wajikite katika kuhakikisha kwamba wanamaliza tatizo la wauguzi, wakae pamoja na Wizara ya Utumishi ili waone namna gani wanaweza kuongeza wauguzi katika zahanati zetu, vituo vya afya na hospitali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niende kwenye elimu msingi; katika elimu msingi nataka nizungumzie masuala ya majengo, Walimu na wanafunzi na niseme jamani, kusema ukweli katika suala la majengo Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameupiga mwingi. Ndani ya mwaka mmoja amejenga madarasa 15,000, madarasa 3,000 kwa ajili ya elimu ya awali na hii imesaidia watoto wetu wale walikuwa wakitembea umbali mrefu kwenda kufuata elimu sasa changamoto hii imekwenda kwisha.

Mheshimiwa Spika, vile vile tulikuwa na changamoto watoto hapa walikuwa wanaenda second selection madarasa 12,000 yamejengwa ajili ya shule za sekondari. Kwa kweli Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anahitaji pongezi nyingi sana haijapata kutokea ndani ya mwaka mmoja Serikali kujenga madarasa 15,000. Ushauri wangu sasa pamoja na kuwa tumejenga madarasa mengi 15,000 ndani ya muda mfupi, naiomba Serikali sasa iangalie umuhimu wa kuongeza walimu wa sayansi. Walimu wa sayansi ni changamoto sana kwenye shule zetu. Nashukuru juzi nimeona Waziri wa Utumishi ametoa kibali kwa ajili ya kuajiri Walimu naomba sasa Wizara hii ya TAMISEMI ikae na Wizara ya Utumishi ione namna ya kutoa kipaumbele kwa Walimu wa sayansi. Ukizingatia sasa hivi ulimwengu wetu huu ni ulimwengu wa sayansi tujitahidi tuajiri Walimu wa sayansi ili kusudi watoto wetu tuwaandae vizuri katika kukabiliana na ulimwengu huu wa sayansi.

Mheshimiwa Spika, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri kuna salamu zake kutoka Kata ya Igwachanya kwa Mheshimiwa Diwani Mawata. Tarehe 22 mwezi wa kwanza mwaka 2022 alienda pale shuleni, kuna changamoto ya bwalo. Bwalo lile limeanza kujengwa tangu mwaka 2012 kwa nguvu za wananchi pamoja na Serikali wameshajenga foundation wameweka na nguzo. Vile vile Mheshimiwa Jafo alipita pale mwaka 2020, akaahidi kwamba watawapa milioni 100 mpaka leo hawajawapa na kukamilisha ujenzi ule wa bwalo lile inahitaji milioni 275 tu, kwa nyie watu wa Kagera ni hela ya mboga tu. Naomba wajitahidi wapeleke pesa ili kusudi bwalo lile likamilike na Mheshimiwa Diwani aamini kweli alinituma na salamu zimefika.

Mheshimiwa Spika, nimalizie kwa kuwaomba sana pamoja na bima za afya ambazo wametoa kwa Madiwani lakini bado kuna umuhimu wa kuwaongezea posho Madiwani hawa kutokana na kazi kubwa wanayoifanya. Niwaombe sana sana katika hili.

Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia, nilisahau kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa zile bilioni 1.5, kila Jimbo la mkoa wa Njombe za TARURA tulizipata, tunashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja. Ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema ya kuweza kusimama tena katika Bunge hili Tukufu. Napongeza Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara pamoja na wasaidizi wake wote kwa kazi nzuri wanayoifanya ndani ya Wizara hii ya Viwanda na Biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Viwanda pamoja na Kilimo inasisitiza katika suala zima la agro-processing kwa maana ya kuchakata mazao ili kuyaongezea thamani sambamba na kuongeza ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona kwenye tumbaku tumefanya vizuri tuna TCC, vile vile kwenye chai tuna viwanda mbalimbali vya kuchakata chai. Tukienda kwenye pamba, tuna asilimia 70 tunasafirisha pamba nje, hatujafanya vizuri. Nilikuwa naomba kilichotokea kwenye pamba tujitayarishe kisije kutokea kwenye zao la parachichi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wangu wa Njombe ni wazalishaji wazuri sana wa zao la parachichi pamoja na baadhi ya mikoa mingine ndani ya nchi yetu ya Tanzania. Kwa hiyo, tuna uhakikia kabisa wa malighafi nyingi ya zao la parachichi. Ushauri wangu kwa Serikali ni kuona namna ya kuhamasisha na kuwashawishi wawekezaji wafungue viwanda vingi sana ndani ya Tanzania ili malighafi hii ya parachichi itumike hapa kwetu, ichakatwe katika viwanda vyetu ili kuwaongezea thamani wakulima na kilimo chao kiwe na tija, sambamba na kuongeza ajira ambayo ni changamoto kwa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile napenda kuiomba Wizara iangalie namna ya kuongeza viwanda vya chuma vya msingi, kwa sababu Tanzania tuna viwanda vya msingi vya chuma viwili tu; tuna KMTC ambacho kipo Moshi na Mang’ula kile ambacho kipo Morogoro. Viwanda hivi vipo chini ya NDC, ni vya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiuhalisia tuna viwanda vya nondo 15 ndani ya nchi yetu ya Tanzania. Viwanda hivi vyote vina-suffer raw material ya chuma, na matokeo yake vinatumia vyuma chakavu katika uzalishaji. Vile vile tumeona tumekuwa na changamoto nyingi sana ya uharibifu wa miundombinu, watu kutafuta hivyo vyuma chakavu ili viweze kwenda ku-supply kwenye viwanda vile vya nondo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais aliwahi kuzungumza kule Arusha na kutoa maelekezo kwamba Serikali ifanye mchakato haraka wa kumaliza mazungumzo na yule mwekezaji wa Liganga na Mchuchuma.

Naiomba Serikali tuendeleze hili zoezi la kuzungumza na huyu mwekezaji; huu mradi wa Liganga na Mchuchuma uweze kufanya kazi ili tuweze kupata viwanda vingi vya msingi vya chuma, tuweze kuzalisha vyuma vingi na tuweze kupata raw material nyingi ya chuma ambayo itatumika kwenye viwanda mbalimbali kama hivyo vya nondo.

Pia vitaanzishwa viwanda vingine vya kutengeneza mabati na misumari ili tusiwe na adha ya malighafi hii kwa sababu tunayo, tuitumie ili wananchi wa Mkoa wa Njombe, kule Ludewa na Tanzania kwa ujumla ili tuweze kunufaika nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi huu wa Liganga na Mchuchuma tumeanza kuuzungumza tangu mwaka 2015. Hivi sasa ni takribani miaka saba. Kwa kweli naomba kama Mheshimiwa Rais alivyoelekeza, Serikali tufanye haya mazungumzo haraka ili tuweze…

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa, Mheshimiwa Neema Mgaya.

T A A R I F A

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpa taarifa Mheshimiwa Neema Mgaya kwamba mradi huu siyo tu kwamba tumeanza kuuzungumza toka mwaka 2015 bali pia ulikuwa ni sehemu ya miradi ya kimkakati katika Taifa letu. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Neema unapokea hiyo taarifa?

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naipokea taarifa kwa mikono miwili kwa sababu alichokisema ni uhalisia kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu mradi wa Liganga na Mchuchuma ukifanya kazi, nimeshazungumza mara nyingi sana ndani ya Bunge hili, tangu mwaka 2010, takribani miaka 12 nazungumza suala la Lianga na Mchuchuma. Kila Bajeti ina maana nimezungumza zaidi ya mara 20 ndani ya Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna reli ya kisasa ambayo tunatengeneza. Kama mradi huu ungekuwa tayari umeshaanza kazi, ina maana tungetumia chuma kwa bei nafuu kuliko vyuma ambavyo vinaagizwa kutoka nje. Lakini nipende tu kukwambia na niiambie Serikali kwamba, wanasayansi ulimwenguni wako busy kuumiza kichwa kuangalia namna gani watapata nishati mbadala ya makaa ya mawe. Kumbumbuka kwenye Liganga na Mchuchuma kuna makaa ya mawe. Na kama wako busy kutafuta nishati mbadala ya makaa ya mawe kwa sababu tu ya kulinda mazingira ili kumaliza mambo ya air pollution; na inasadikika kwamba baara ya miaka 10 haya makaa ya mawe nchi nyingi hayatokwenda kutumika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hofu yangu ni kwamba, yasije kutokea kama yale yaliyotokea kwenye mkonge.

Wakati tuko tayari kuzalisha hayo makaa ya mawe ndipo hapo nchi sasa hazihitaji tena. Soko tena halipo na yale makaa sasa yanakuwa hayana maana tena. Kwa hiyo, bado naendelea kuisisitiza, Serikali mmalize hayo mazungumzo ili tuwe ndani ya muda. Serikali itambue kwamba dunia haitusubiri, dunia haitusubiri, dunia inakwenda kasi hivyo lazima na sisi twende kasi ili tuweze kwenda sambamba na dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nichukue nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Rais, lakini vilevile kumpongeza. Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ni msikivu, lakini vilevile ni mlezi. Tulizungumza sana hapa masuala ya destination inspection na pre-arrival inspection; na juzi kwenye moja ya mikutano yake ametoa maelekezo kwa Serikali, kwamba waangalie system ya high breed atakayejisikia kufanya ukaguzi nje ya nchi sawa, atakayejisikia kufanya ukaguzi wa gari lake ndani ya nchi sawa. Hii inadhihirisha jinsi gani Mama alivyo mlezi na jinsi gani Mama anavyotaka kila mtu afanye mambo kutokana na vile anavyojisikia bila kuvunja sheria za nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Rais na ninaomba hayo maelekezo Mheshimiwa Rais aliyoyatoa Wizara hii ifanyie kazi haraka na wale watakaojisikia kufanya destination inspection wataendelea na wale ambao wanataka pre-arrival inspection wataendelea ili mradi tu kila mtu aweze kufanya mambo yake kwa uhuru na kuweza kuona namna gani inaleta tija kwa huduma atakayoipata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haya machache naomba kuunga mkono hoja. Ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa kibali cha kuweza kusimama katika Bunge hili la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Wasaidizi wake wote kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wizara yao hii ya TAMISEMI, kipekee kabisa nimpongeze Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania wa Awamu ya Sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri aliyoifanya katika suala zima la kuongeza bajeti ya TARURA. Ukiangalia Rais alipoingia madarakani bajeti ya TARURA ilikuwa bilioni 275 lakini mwaka wa kwanza wa bajeti ya Rais wa Awamu ya Sita bajeti ya TARURA iliongezeka kwa zaidi ya asilimia mia moja na hivi leo tunavyozungumza bajeti hii ya TARURA imeongezeka hadi kufika bilioni 778, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa sana ndani ya muda mfupi wa miaka miwili. (Makofi)

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Neema, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Mwita Getere.

T A A R I F A

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Hili neno mnyonge huwa linatumiwa vibaya, haijawahi kutokea duniani Rais akawa mnyonge. Ahsante. (Kicheko)

MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Neema taarifa unaipokea?

MHE. NEEMA W. MGAYA: Naomba niendelee. Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ya TARURA imeongezeka mpaka kufikia hiyo bilioni 7,78 lakini bado kuna changamoto katika utekelezaji kwa baadhi ya maeneo katika suala zima la Wakandarasi. Kuna baadhi ya Wakandarasi wanapewa kazi maeneo mengi lakini ili hali uwezo wao wakufanya kazi unakuwa mdogo, hivyo ufanisi wa kazi unakuwa hauonekani lakini vilevile kunakuwa hakuna tija kwa wananchi wa maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu kwa Serikali ni kwamba tuwape Wakandarasi kazi kutokana na uwezo waliokuwa nao, mwenye uwezo mdogo apewe kazi ndogo, mwenye uwezo mkubwa apewe kazi kubwa, isiwe mtu anafanya kazi kijanjajanja akisikia Songea wanalalamika anahamisha mitambo kutoka Lindi anapeleka Songea, hapo hatutafika kwakweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba nichukue nafasi hii sasa kuomba maombi katika Halmashauri zetu za Mkoa wa Njombe. Nikianzia na Halmashauri ya Wilaya ya Makete, naiomba Serikali ituongezee pesa katika barabara inayotoka Kipengele kwenda Lupila barabara ya zaidi ya kilomita 30. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwetu mvua inanyesha miezi nane theluthi mbili ya mwaka mvua zinanyesha tu, ukizingatia kule Lupila ndiyo wazalishaji wakubwa wa viazi pamoja na mbao. Kuboreshwa kwa barabara hii kutasaidia mlaji wa mwisho wa kule Dar es Salaam ninyi mnaopenda kula chips Dar es Salaam watapata kwa bei nafuu. Kwa hiyo, kuna umuhimu mkubwa wa kuhakikisha kwamba barabara hii inaboreshwa kwa maslahi ya Watanzania kwa ujumla pamoja na wananchi wa Makete. (Makofi)

Mheshimwa Mwenyekiti, nilikuwa naiomba pia Serikali ituongezee pesa katika kuboresha barabara ya Makete – Isaplano kilometa 12 kule Halmashauri ya Makete, vilevile katika Halmashauri ya Wanging’ombe naiomba Serikali ituongezee pesa kama milioni 870 hivi kwa ajili ya kuboresha barabara inayotoka Malangali kwenda Wangama kilometa 15 kwenye mradi mkubwa wa maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile TARURA wasisahau Waziri Mkuu alikaa na Watendaji wote wa TARURA Tanzania nakuwapa maelekezo kwamba namna ya kuboresha barabara za Vijijini Nyanda za Juu Kusini, ichukuliwe kwa namna ya kipekee kutokana na wingi wa mvua katika maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Napenda niwakumbushe hilo na wazingatie hayo maelekezo ya Waziri Mkuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye afya msingi. Nimpongeze Rais wa Awamu ya Sita Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa aliyoifanya ya kujenga Vituo vya Afya, Hospitali za Mikoa, Hospitali za Wilaya, Zahati zetu lakini naomba nitoe ushauri kutokana na changamoto hii Wauguzi na wafanyakazi wa Kada ya Afya ambao kila Mbunge anaesimama anaizungumzia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wakati sasa Wizari hii ya TAMISEMI ikae pamoja na Wizara ya Utumishi waone namna ya kuongeza wafanyakazi, watumishi wa Kada hii ya Afya katika vituo vyetu vya afya, zahanati zetu, hospitali zetu ili kuweza kuleta tija katika suala zima la majengo haya ambayo tayari tumeishayajenga katika maeneo mbalimbali ya Kata zetu, Wilaya zetu na Mikoa yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Wanging’ombe mahitaji ya watumishi wa Kada ya Afya ni 1,051, mpaka sasa hivi waliokuwepo ni watumishi 342 sawa na asilimia 32.6 kupungufu ya watumishi 709 ambayo ni sawa na asilimia 67.4. Tunaiomba Serikali ituangalie Halmashauri hii ya Wanging’ombe kwa jicho la huruma tuweze kupata watumishi hawa hili tuweze kutoa huduma nzuri kwa wananchi wetu, sambamba na katika Halmashauri ya Makete kuna upungufu, Halmashauri ya Njombe Mji, Njombe Vijijini, Halmashauri ya Ludewa pamoja na kule Makambako. Kwa ujumla Mkoa wetu wa Njombe tuna upungufu mkubwa wa watumishi wa Kada ya Afya, tungeiomba Serikali ituongezee watumishi hawa wa Afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye elimu msingi. Niseme tu kazi kubwa imefanyika katika Awamu hii ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, mtakumbuka ndani ya mwaka mmoja alijenga madarasa karibia 15,000, madarasa 12,000 kwa shule za sekondari, madarasa 3,000 kwa shule za msingi na hii ilitusaidia hata watoto wetu kutokwenda second selection kwa wale wa sekondari lakini vilevile kwa wale wa elimu ya msingi ule umbali wa kutembea kwenda kutafuta shule umbali mrefu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amejitahidi sana kupunguza umbali kwa watoto wetu kutembea kwa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado kuna changamoto, changamoto inarudi palepale kwenye wafanyakazi. Walimu hatuna wa kutosha ndani ya Mkoa wetu wa Njombe, Halmashauri zote Sita, hasa changamoto ya walimu wa sayansi imekuwa kubwa sana katika Mkoa wetu wa Njombe katika Halmashauri zetu zote Sita kwa maana Halmashauri ya Wanging’ombe, Makete, Ludewa, Njombe Mjini, Njombe Mji na Makambako. Kama unavyojua ulimwengu wa sasa hivi ni ulimwengu wa sayansi ni vyema tukawandaa watoto wetu waweze kukabiliana na ulimwengu huu wa sayansi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie katika suala la mikopo ya asilimia kumi. Nampongeza Mheshimiwa Rais…

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Neema, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Amar.

T A A R I F A

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpa taarifa mchangiaji kwamba upungufu wa walimu wa sayansi siyo wapi huko anakosema Njombe, ni kwa nchi nzima upungufu huu upo ikiwemo pia na Nyang’hwale.

MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Neema, muda umeisha basi malizia sekunde mbili.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Kwa kumalizia napokea taarifa yake na naunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuweza kuchangia katika Wizara hii ya Viwanda na Biashara. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya. Nianze kuchangia kwa kumpongeza Rais wa Awamu ya Sita, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoifanya ndani ya nchi yetu. Nimpongeze pia Mheshimiwa Waziri, Dada yangu, Mheshimiwa Dkt. Ashatu kwa kazi nzuri anayoifanya katika Wizara hii ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Naibu Waziri wake na watendaji wote wa Wizara hii ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kusema kwamba, sera kubwa ya viwanda ni agro processing. Sisi Tanzania tunataka tuchakate malighafi zetu ili tuweze kusafirisha bidhaa nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, kwa kufanya hivi tutasaidia kuongeza thamani ya tunachokizalisha, lakini vilevile sambamba na kuongeza ajira ndani ya nchi yetu. Lakini tukisema tusafirishe mazao ina maana tutakuwa tunapoteza ajira na tunapoteza mapato. Na hii ajenda tumekuwa tukiizungumza takribani miaka mitano sasa, lakini hivi sasa kama inaenda kuwa kimya. Labda ningependa Mheshimiwa Waziri aweze kuniambia akija kufanya majumuisho, ile ajenda tuliyokuwa tukiimba ya Tanzania viwanda bado ipo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulianza kutengeneza industrial park pale kurasini miaka miwili iliyopita, nafikiri kipindi kile Waziri wa Viwanda na Biashara alikuwa Mheshimiwa Prof. Kitila Mkumbo, kama sijakosea. Tulikubaliana tuanzishe kiwanda cha chai, kiwanda cha kahawa, kiwanda cha parachichi na viwanda vingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini vilevile tulikubaliana Tanzania tuwe na soko kubwa la chai kama lilivyokuwa kule Mombasa kwa majirani zetu. Hii ingeweza kusaidia wakulima wetu wa chai waache yale manung’uniko, ya kwamba tunakosa soko la chai, na hivi sasa mpaka wameamua hata kuacha uzalishaji wa chai na kung’oa baadhi ya mashamba ya chai kwa kukosa soko. Na ningependa kujua Mheshimiwa Waziri huu mchakato umefikia wapi? Ukija kuleta majumjuisho hapo utuambie kwamba, huu mchakato ambao tuliuanza pale Kurasini wa industrial park umeishia wapi?

Mheshimiwa Spika, sasa nipende kuzungumzia suala la zao la parachichi. Kama tunavyojua kwamba, Tanzania kwa East Africa ni moja ya nchi ambazo zinazalisha parachichi kwa wingi na Mkoa wa Njombe ndio unaoongoza. Paparachichi yetu tunazalisha kwa wingi na yenye ubora, lakini ni miaka mingi sana tumakuwa tukipigia kelele Wabunge wa Mkoa wa Njombe na wa Nyanda za Juu Kusini wa mikoa mingine kuhusiana na suala zima la uanzishwaji wa viwanda vya kuchakata zao la parachichi ndani ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ufike wakati sasa kama tutakuwa tunatoa ushauri haujapokelewa, basi Serikali ituambie kwamba, ushauri huu bwana, sisi hatujaupokea, ili tusiendelee kupiga makelele humu ndani ya Bunge. Maana sasa tunapiga makelele mpaka sasa tunataka kufanana na hayo maparachichi yenyewe.

Mheshimiwa Spika, katika biashara yoyote duniani kitu cha kwanza unachotakiwa kufanya katika uzalishaji wowote ni kuhakikisha kwamba una uhakika wa soko la ndani. Ili kuwa na uhakika wa soko la ndani lazima tutengeneze miundombinu ya kuwa na viwanda vya kuzalisha hili zao la parachichi. Hii fursa tuliyoiona ya kusafirisha parachichi nje ya nchi, nchi nyingi zimeona hii fursa. Hebu tukae chini tutafakari, tujiulize, je, nchi nyingine zote zilizoona fursa hii zikiamua kuzalisha kwa wingi, vipi soko huko mbele? Vipi mustakabali wa wakulima wetu wa zao la parachichi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana sisi Wabunge tunasisitiza kwamba, tuanzishe viwanda vya kuchakata zao hili, ili badaye supply ikiwa kubwa, demand ikishuka kule, huku sisi tuwe na uhakika wa soko letu ndani ya nchi. Na hii itasaidia kuwalinda wakulima wa zao la parachichi wawe na uhakika na wafurahie kile ambacho wanacho…

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Nilikuwa sijamuita, ili umalizie sentensi yako maana naona umeishia, “kwa kuwa…”. Sasa sijui ataanzia wapi kutoa Taarifa. Malizia sentensi uliyokuwa unasema, ili nimpe nafasi.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, nilitaka kusema hivi, ni kwamba, umuhimu wa zao hili la parachichi, ili liweze kuleta tija kwa wananchi ambao tunazalisha zao hili la parachichi ni kuhakikisha kwamba, tuna viwanda ambavyo vitakwenda kuchakata zao letu la parachichi, ili tuwe na uhakika wa soko la ndani endapo soko la nje likija kuharibika hapo badaye.

SPIKA: Haya, Mheshimiwa Neema Mgaya, kuna Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Halima Mdee.

TAARIFA

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, nilikuwa nampa Taarifa Mheshimiwa; hotuba ya Waziri inaonesha kwamba, tunaagiza mafuta kutoka nje tani 365,000. Hoja ya Mheshimiwa Neema ni kwamba, tukiwa na viwanda vyetu vya kuchakata maana yake vilevile na mafuta yanayotokana na zao la parachichi tutaweza kutengeneza ndani. Maana yake sasa tutafidia hicho anachokisema, lakini vilevile kuzuia fedha za kigeni kwenda nje. (Makofi)

SPIKA: Haya, Mheshimiwa Neema Mgaya, unapokea Taarifa hiyo?

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naipokea Taarifa ya Mheshimiwa Halima kwa mikono miwili kwa sababu, ina tija kwa mustakabali wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nizungumzie suala la Liganga na Mchuchuma. Katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri ametueleza taarifa njema za kulipa fidia wananchi wetu wa Mkoa wa Njombe ili kuweza kuendelea na zoezi hili la Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Spika, kulipa fidia tu haitoshi. Sisi wananchi wa Mkoa wa Njombe na Watanzania kwa ujumla kwa unyeti wa mradi huu wa Liganga na Mchuchuma tunataka kujua, ni lini chuma kitaanza kuchimbwa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi nilikuwa nafikiria kwa kuwa, tumeshasema faida nyingi sana za mradi huu, na tumesema hasara za kucheleweshwa kwa mradi huu, ikiwa na kupitwa kwa wakati kwa makaa ya mawe, tumezungumza sana ndani ya Bunge hili. Mimi nafikiri ni wakati sasa Bunge lako liunde Kamati Teule ya kuchunguza Mradi huu wa Liganga na Mchuchuma; na mimi nitaleta hoja binafsi ya kuunda kamati teule ya kuchunguza suala la Liganga na Mchuchuma ili kusudi suala hili liende kufanyiwa kazi kwa uharaka zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nikileta hoja hiyo Mezani kwako unikubalie na uniunge mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya na uhai wa kuweza kusimama mbele ya Bunge letu hili Tukufu na kwa kuanza mchango wangu. Nianze kwa kumpongeza Rais wetu, Mama yetu kipenzi Dkt. Samia Suluhu Hassan. Hii ni mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu kuwa na miradi mikubwa ya barabara yenye jumla ya kilometa 2,035, ambayo itagharimu zaidi ya trilioni 3.7 na ikatekelezwa kwa wakati mmoja. Hivyo basi nichukue fursa hii kumpongeza mama kwa kuona umuhimu wa kuweza kuifungua Tanzania yetu ili tuweze kukua kiuchumi. Kwa sababu panapokuwa na miundombinu mizuri ni moja kwa moja unachochea uchumi wa nchi yako. Rais Mheshimiwa Dkt. Samia anakwenda kufanikiwa katika hili nampongeza na namtia nguvu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Waziri wetu wa Ujenzi, Mheshimiwa Profesa Mbarawa pamoja na Naibu Mawaziri wake na Watendaji wote wa Wizara hii ya Ujenzi kwa kazi nzuri wanayoifanya. Sisi tuko nyuma yao kwa yale yote watakayoyafanya ambayo wanajua yatakuwa yanaleta tija katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendeele kumshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kilometa 107.4 ya barabara ya kutoka Njombe pale Ramadhani kwenda Makete. Barabara ilishakamilika ilishaanza kufanya kazi, lakini kuna changamoto ndogo ndogo, tunaomba sasa wale wananchi ambao hawakulipwa fidia waweze kumaliza kulipwa fidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo pia tunaendelea kuishukuru Serikali kwa Barabara ya Mawengi – Lusitu, kilometa 50 kule Ludewa, lakini vile vile Lusitu - Itoni kilometa 50 kwenye Jimbo lile la Njombe Mjini kilometa 50, kazi inaendelea pale mkandarasi yuko site, lakini bado tunasisitiza changamoto ya kulipwa wananchi wetu fidia. Wananchi wanafurahia barabara, lakini bado wanakuwa na machungu ya kutokulipwa fidia. Tunaomba hili Wizara ilimalize ili tusiwe na dosari katika utekelezaji wa kazi hii nzuri inayofanywa na Rais wetu mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Barabara ya kutoka Makambako kilometa 295 kwenda Songea. Hii barabara ni mbovu sana imejengwa tangu mwaka 1980. Barabara hii ina mashimo mengi, ni nyembamba inasababisha ajali nyingi, ni hatari hata kwa misafara ya Viongozi wa Kitaifa, ni hatari kwa wananchi, tumeona vifo vingi vinatokea katika barabara hii. Barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa kusini, barabara hii ikiboreshwa ikitengenezwa kwa kiwango cha lami upya itasaidia hata ule usafirishaji wa makaa ya mawe ambayo yanaendelea kusafirishwa hivi sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa katika bajeti ijayo angalau waangalie kile kipande cha Makambo kuishia pale Njombe Mjini kwenye makutano ya Mkoa wa Njombe na Songea panaitwa Lukumburu, waangalie sana kipande hicho ni muhimu sana na waweze kukitengeneza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niombe ombi rasmi la barabara hii ambayo tumekuwa tukiizungumza tangu mwaka 2010. Barabara ya Ramadhani – Ndandu - Iyayi kutokea Mbeya, hii barabara haina pesa kabisa na tunaomba iingie kwenye mpango mahususi ya kutafutiwa pesa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ina sifa inaunganisha mkoa na mkoa, kwa maana Mkoa wa Njombe na Mkoa wa Mbeya, lakini imekuwa inajengwa kilometa tano tano inakuwa haileti tija, haina maana. Hebu ifike wakati sasa tuweke umakini katika barabara hii, ipewe pesa ya kutosha na ijengwe kwa mwenendo mzuri ili iweze kukamilika mapema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Barabara ya Kibena - Stop Lupembe, tunamshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kibali cha kujengewa kilometa 51 na hivi sasa kilometa 25 kutoka Kibena - Nyombo imeshaanza kuandaliwa, iko mwishoni katika kuandaa tenda. Tunaomba lakini wafanye haraka haraka ili kusudi barabara hii iweze kukamilika. Barabara hii ni muhimu inaunganisha Mkoa wa Njombe na Mkoa wa Morogoro, itafunguka kiuchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Barabara ya Makete - Kitulo – Mbeya, kilometa 96, tulishapata mkandarasi lakini kinachosubiriwa ni advance payment ili mkandarasi huyu aweze kuanza kazi, kwa sababu ule mkataba ulishasainiwa tangu Desemba mwaka 2022. Tunaomba waanze haraka kule Makete mvua ni nyingi sana. Tuanze mapema kabla mvua za Novemba hazijaanza kunyesha, sasa hivi mvua zimetulia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Barabara ya Matamba – Kitulo, kilometa 51, barabara ya kimkakati ya kwenda kwenye Hifadhi ya Kitulo, barabara hii ni muhimu katika kufungua utalii wa Nyanda za Juu Kusini. Kuna Barabara ya Mlangali – Lupila – Ikonda, barabara hii tayari wameshajenga madaraja mazuri na barabara hii ni barabara ya kiusalama kutoka Mkoa wa Ruvuma, Njombe kwenda Mbeya. Tunaomba waiwekee umuhimu barabara hii ili iweze kujengwa katika kiwango cha lami na kuweza kuwasaidia sio lazima mtu anatoka Ruvuma anaenda Mbeya, aanze kuzunguka huku Njombe aende Makambako apite Igawa, ndio aende tena Mbeya, hapana barabara hii ni nzuri kwa shortcut ya kutoka Ruvuma kwenda…

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie katika suala la airport; Njombe tunahitaji airport ni muhimu sana, sisi ni wazalishaji wakubwa wa zao la parachichi. Kuna ndege ya mizigo inakuja na katika wazalishaji wakubwa wa horticulture ikiwepo parachichi, mbogamboga pamoja na maua ni Mkoa wa Njombe. Kuna umuhimu sana wa Kiwanja cha Ndege cha Njombe kukamilika ili kusudi tuweze kusafirisha bidhaa hizi na kumfikia mlaji zikiwa na ubora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Awali ya yote ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya na uhai kwa kuweza kusimama ndani ya Bunge hili Tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na Watendaji wote ndani ya Wizara hii ya Maliasili na Utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kipekee ninampongeza Mhifadhi namba moja Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi nzuri aliyoifanya kwenye programu ya Royal Tour na tumeona watalii wanaendelea kuongezeka ndani ya nchi yetu na naamini wataendelea kuongezeka kama vile walivyo ongezeka katika nchi ambazo zili – practice programu hii ya Royal Tour kama wenzetu wa Mexico, Poland, Ecuador na Rwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tunamshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuja Mkoa wa Njombe tarehe 26 Agosti, 2022 alisema kwamba itakuja phase two the hiding place of Tanzania na hii ita – cover maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Namshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuonyesha nia ya dhati ya kukuza utalii wa Nyanda za Juu Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Nyanda za Juu Kusini tuna vivutio vingi sana. Ukianza Iringa tuna Hifadhi ya Ruaha ambayo ina simba ambao wanatembea kwa makundi makubwa, ambayo huwezi ukaona simba hao kwenye Hifadhi zingine nchini. Vilevile ukienda Rukwa kuna maporomoko ya Karambo, maporomoko haya ni ya pili kwa ukubwa Afrika yakitanguliwa na yale ya Victoria Fall kule Zimbabwe. Ukienda Songwe tunakuta Kimondo, kivutio pekee ambapo huwezi kukiona sehemu nyingine. Ukienda Njombe unakuta Hifadhi ya Kituro ambayo ni ya kipekee ulimwenguni, lakini ukirudi huku Mbeya unakuta Kijungu, maji yanapanda mlima, utakuta Kisimba vilevile utalikuta Ziwa Ngosi ambalo lina ramani ya Afrika na lina maji mazuri yenye rangi ya bluu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna fukwe nzuri Matema Beach, ukienda Ruvuma utazikuta fukwe hizi Njombe pia kule Ludewa. Ushauri wangu kwa Serikali, iendelee kuvitambua na kuvifanyia kazi vivutio vya Nyanda za Juu Kusini ili kuweza kuongeza Pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri mwingine Serikali iharakishe kumaliza phase one ya regrow ili ianze phase two ambayo itatoa fursa kwa hifadhi ambazo hazikuingia kwenye phase one. Hifadhi kama ya Kituro na Katavi ziweze kufaidika na mradi huu. Kwa kufanya haya itarahisisha programu ya phase two ya The hidden place of Tanzania kuja kufanya kazi vizuri kwa sababu muda huo tutakuwa tumeishajiandaa vizuri kutambua na kuainisha vivutio vya Nyanda za Juu Kusini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ninaombi kwa TANAPA Serikali iangalie namna ya kuwaongezea bajeti TANAPA. Kwa sababu wakati wana hifadhi 16 TANAPA walikuwa wanapata bilioni 104. Sasa hivi hifadhi imeongezeka ziko 22 wanapata bilioni 111, lakini hitaji halisi la Bajeti ya TANAPA ni bilioni 222 unaweza ukaona hapo ni fifty percent tu ya wanayoipata kutokana na hitaji lao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia TAWA, TAWA mapori yameongezeka lakini bajeti ni ndogo. Serikali iangalie namna ya kuwaongezea pesa ili waweze kufungua njia au barabara kwenye mapori hayo lakini vilevile wawaongezee watumishi. Baada ya kumaliza hiyo Nyanda za Juu Kusini, sasa napenda nizungumzie utalii wa fukwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inabidi sasa ifanye mikakati mikubwa ya kuhakikisha ya kwamba tunaendeleza utalii wa fukwe. Tunazo fukwe nzuri lakini Serikali bado hawajazifanyia kazi. Ukienda Seychelles wamefanikiwa sana katika utalii wa fukwe na wanafanya vizuri, kwa sababu wao wana mamlaka maalum ya kusimamia fukwe na hiyo mamlaka iko chini ya Bodi ya Utalii. Kazi ya mamlaka hiyo kuandaa mipango ya matumizi ya hizo fukwe vilevile kusimamia utekelezaji wa mipango ya hizo fukwe, pia wanakazi ya kuratibu na kuzitangaza fukwe hizo kwa kushirikiana na sekta binafsi, kwa mikakati hii madhubuti ndiyo maana Seychelles imefanikiwa sana kuuza katika utalii wa fukwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu sasa kwa Serikali, jambo la kwanza Serikali inatakiwa irudishe fukwe ziwe chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Serikali ikirudisha hizi fukwe kuwa chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii inaweza ikapeleka kwenye Taasisi kama ya malikale. Vilevile irudishe na Visiwa vyote viwe chini ya Wizara ya Malisili na Utalii na hivi Visiwa vinaweza vikasimamiwa na Jeshi USU kule maliasili wana Jeshi USU kwa ajili ya sababu za kiusalama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hiyo Serikali inatakiwa itoe fursa kwa wawekezaji, wananchi waweze kujenga hotel ili kuiongeza idadi ya vyumba. Hivi sasa tuna vyumba 132,667 ukilinganisha na competitive wenzetu hawa hapa Kenya maana hao ndiyo washindani wetu wakubwa, wanavyumba zaidi ya milioni moja. Kwa hiyo, Serikali ione umuhimu wa kuangalia jambo hili na kulifanyia kazi ili tuweze kuongeza mapato katika sekta ya utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala lingine la pale Kilwa, yale majengo ya kale, Serikali ione umuhimu wa kuyakarabati ili kuanza kufungua utalii na watalii waendelee kwenda zaidi na zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kuzungumzia masuala la migogoro. Migogoro ya binadamu na wanyama, migogoro ya ardhi kati ya Hifadhi na Vijiji. Nilikuwa naiomba Serikali, Wizara hii ya Maliasili na Utalii ifanye kazi kwa ukaribu na Wizara ya TAMISEMI, Wizara ya Mifugo, Wizara Kilimo ili kuweza kutatua na kuweza muda mwingine kuepusha migogoro isiyokuwa na sababu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano mzuri ni ile Ofisi ya Mkuu wa Wilaya pale Mvomero, imejengwa ndani ya muda mfupi, lakini pale kuna mgogoro kwamba wanyama wanakwenda, wanapita mpaka kwenye baadhi ya vijiji pale, lakini inawezekanaje Ofisi ya Serikali wanapewa hati, wanapewa kibali cha kujenga, mipango inafanyika katika Wizara ya TAMISEMI, wanaelekeza ijengwe pale na baadae inakuja kuona kwamba imejengwa katika maeneo ambayo wanyama wanapita! Nafikiri kuna haja sasa Wizara hizi za Serikali zote kabla hamjafanya matumizi ya ardhi mkae kwa pamoja, mshauriane ili muweze kufikia muafaka muone je hili jambo linalofanywa ni sahihi ama litakuja kuleta madhara baadaye? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile sasa hivi kuna programu inaendelea ya BBT, Wizara ya Kilimo kule kwa Kaka yangu Hussein Bashe, ninataka kujua yale mapori, mashamba waliyoainisha ya kuweza kufanya hizo programu za BBT wamewasiliana na Wizara ya Maliasili? Isije ikawa baadaye tena waanza kulima mazao yamekua tembo wanaingia wanaanza tena kulalamika kwamba tembo wanapita, isije ikawa wameweka hizo programu zao katika maeneo ambayo yanaushoroba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiria ni wakati muhimu sasa wa kuangalia umuhimu wa kujua matumizi ya ardhi katika sehemu sahihi kwa wakati sahihi ili baadaye isije kuleta migongano na migogoro hii hifadhi, vijiji, Wanyama na binadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)
Azimio la Bunge la Kuridhia Kufutwa kwa Hifadhi ya Taifa ya Kigosi ili Kuruhusu Kuanzishwa kwa Hifadhi ya Msitu wa Kigosi na Azimio la Bunge la Kuridhia Kurekebisha Mpaka wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kuunga mkono mapendekezo ya maazimio haya yote mawili, Azimio la kwanza la Kurekebisha Mpaka wa Hifadhi ya Ruaha na Azimio la Kushusha Hadhi Hifadhi ya Kigosi kwenda kuwa Hifadhi ya Misitu ya Kigosi.

Mheshimiwa Spika, ninampongeza Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa nia njema na ya dhati ya kutaka kutatua migogoro mbalimbali kati ya hifadhi na wananchi. Tukianza na mgogoro wa Mbarali, mgogoro wa Mbarali ni mgogoro mrefu wa tangu mwaka 2008 ilipowekwa GN ya 28.

Mheshimiwa Spika, tukianza na mgogoro wa Mbarali, mgogoro wa Mbarali ni mgogoro mrefu wa tangu mwaka 2008 ilipowekwa GN ya 28. Mheshimiwa Rais alituma Mawaziri nane kwenda kutatua mgogoro huu, vilevile viongozi wakubwa wa Serikali, akiwemo Waziri Mkuu, walikwenda pia Mbarali katika kutatua tatizo hili la mgogoro wa Mbarali. vilevile Mheshimiwa Rais hajaishia hapo, aliamua kutoa hekta 74,432.12 na kuwapa wananchi ili waweze kuendelea na shughuli za uzalishaji.

Mheshimiwa Spika, mama yetu ana nia njema, ana nia ya dhati, tumuunge mkono. Ametoa pesa nyingi, vigingi vimewekwa, mipaka imewekwa ili kuzuia uvamizi na kuweza kudhibiti migogoro isiweze kuendelea tena.

Mheshimiwa Spika, kwa nia hii njema, ya dhati, ambayo Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameionesha, naiomba Serikali sasa tumuunge mkono Mheshimiwa Rais kwa kutekeleza haya yafuatayo; ombi la kwanza, Serikali itayarishe mipango na utaratibu wa uwekezaji ambao unaonesha tarehe na lini zoezi litakwenda kuisha sambamba na kukamilisha zoezi hili la wakati.

Mheshimiwa Spika, ombi langu la pili kwa Serikali; tathmini ifanyike haraka, walipwe fidia wale wote ambao wamekutwa kwenye mpaka huo wa Hifadhi ya Ruaha ili kuweza kupisha na waweze kuondoka. Fidia zao zilipwe kwa wakati. maana yake matatizo huwa yanakuja kuanza hapa kwenye kuchelewesha fidia, mmalize ili mambo yaweze kuendelea.

Mheshimiwa Spika, pia nimpongeze Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuridhia kushusha hadhi Hifadhi ya Kigosi na kuweza kuruhusu Hifadhi hii ya Kigosi kuwa Hifadhi ya Misitu ya Kigosi. Kwenye Kamati mara nyingi tumekuwa tukilalamika kwamba TANAPA ina mzigo mkubwa wa kuendesha hifadhi hizi.

Mheshimiwa Spika, TANAPA ina takribani hifadhi 22. Tangu ilivyokuwa na hifadhi 16, bado TANAPA walikuwa na bajeti ya bilioni 104, hifadhi zikaongezeka kuwa 22, TANAPA wakawa wanapewa bilioni 111. Hitaji halisi la pesa ili TANAPA waweze kuendesha hifadhi hizi ni takribani bilioni 222.

Mheshimiwa Spika, kwa uhaba wa pesa ambazo wanapewa TANAPA kuendesha hifadhi hizi, naona suala hili ni muhimu, linaendelea kushusha gharama za uendeshaji wa hifadhi za TANAPA. Ukizingatia kwamba Hifadhi hii ya Kigosi mwaka huu wamekwenda watalii 10 tu, kwa hiyo, mapato ni madogo na uendeshaji TANAPA inalemewa mzigo.

Mheshimiwa Spika, vilevile nimpongeze Rais kwa kuona umuhimu wa kushusha Hifadhi hii ya Kigosi kwa sababu hifadhi hii inakwenda kuwa Hifadhi ya Misitu ya Kigosi, itaruhusu wananchi kuweza kufanya shughuli za uzalishaji ikiwa ni pamoja na kurina asali, uvuvi na kufanya shughuli zao za matambiko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuruhusu uzalishaji wa asali kuendelea itatusaidia vile viwanda vyetu tulivyovianzisha vya asali kupata malighafi ya asali kwa wingi. Kwa hiyo, malighafi hii itakwenda kulisha viwanda vyetu vya asali na yale mazao ya asali tutaweza kuyauza nje ya nchi na Serikali itapata pesa za kigeni, na inasemekana kwamba tutakwenda kupata takribani dola milioni 50 kwa kuruhusu shughuli hizi za uzalishaji wa asali ndani ya Hifadhi hiyo ya Misitu ya Kigosi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hivyo, nimpongeze Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa kutatua migogoro, sambamba na kuona matumizi sahihi ya Hifadhi hii ya Misitu ya Kigosi ambayo itakwenda kuleta manufaa zaidi kuliko ikiendelea kuwa hifadhi, tunapata watalii wachache, na pesa tunapata kidogo na TANAPA inapata mzigo mkubwa wa kuhudumia hifadhi hii.

Mheshimiwa Spika, baada ya kuongea haya machache, naunga mkono hoja ya mapendekezo haya yote mawili. Ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Awali ya yote kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na uhai na kuweza kusimama ndani ya Bunge hili tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Waziri pamoja na watendaji wake kwa utendaji mzuri katika Wizara hii. Lakini kipekee nimpongeze sana Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan kwa programu nzuri ambayo aliizindua tarehe 22 Aprili, kule Marekani programu hii ya Royal Tour nina uhakika na ninaamini kwamba itakuja kuleta matunda makubwa zaidi. Nina kila sababu ya kusema hivyo kwa sababu ukitizama nchi mbalimbali ambazo zime-practice hii programu ya Royal Tour tukienda East Africa tu hapa Rwanda na mwigizaji alikuwa yuleyule Bwana Peter Greenberg walifanya vizuri baada ya programu hiyo na matunda yanaonekana watalii wengi Rwanda wameweza kwenda. Lakini si Rwanda tu zipo nchi mbalimbali ikiwepo Mexico, Poland, Ecuador, Israel wote hao wame-practice hii programu ya Royal Tour na matunda, matokeo chanya yameonekana kwa nchi zote hizi. (Makofi)

Kwa hiyo, sina shaka, sina hofu, nampongeza Rais wangu Mama Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi huu kwa sababu naamini Tanzania itakwenda kukuza utalii kupitia programu hii ya Royal Tour. Hongera sana Mama Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile hata kwenye interview ambayo Mama Samia Suluhu Hassan aliyofanyiwa pale New York City aliweza kujitanabaisha na kuainisha vivutio mbalimbali vya utalii ndani ya nchi ya Tanzania na watu wengi wakaweza kuvifahamu. Lakini tukienda mbali zaidi hata Gazeti la New York Times lilimuandika vizuri sana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan na kumpongeza na tukumbuke jamani gazeti hili siyo la udaku ni kati ya magazeti ambayo yanaheshimika Marekani. Kwa hiyo, naamini kabisa kwa kupitia programu hii matunda makubwa yanakuja kwa kupata watalii wengi sana ndani ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kazi kubwa hii iliyofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan, ni wajibu sasa Wizara ikaangalia namna bora ya kuendelea kumuunga mkono mama na kuendelea kuchakata suala hili la utalii kuelekea Nyanda za Juu Kusini. Nyanda za Juu Kusini kama tutaweza kuchakata vizuri suala hili la utalii tutakwenda kufanya vizuri zaidi. Nyanda za Juu Kusini ukianza tu pale Mkoa wa Njombe kuna Hifadhi ya Kitulo, hifadhi ile ni bustani ya Eden, hifadhi ile hakuna inayofanana na ile ulimwenguni ni hifadhi ya kipekee ina ndege wazuri, ina maua mazuri, kama tutaweza kuipigia chapuo tutakwenda kuongeza watalii Nyanda za Juu Kusini. Lakini ukienda pale Rukwa, kuna maporomoko yale ya Kalambo, maporomoko ya Kalambo Afrika ni maporomoko ya pili yakitanguliwa na Victoria Falls kule Zimbabwe, bado tuna kitu kikubwa cha kuweza kukiuza na watalii wakaja nchini kwetu kwa kupitia kule Nyanda za Juu Kusini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile tuna mbuga nzuri ya Ruaha, ni ya kipekee ina makundi makubwa ya simba ambayo East Africa hakuna makundi yale makubwa ya simba, tunaweza tukaweka kwenye package ya Nyanda za Juu Kusini na utalii ukaweza kukua na kuweza kuongeza mapato.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile tuna utalii wa picha kwenye mashamba mazuri ya chai, mashamba mazuri miti, Mufindi kule, Njombe, Mbeya pamoja na huko Rukwa pia. Lakini vilevile tuna Kimondo kiko Songwe, hivi vitu vyote vikiwekwa kwenye package moja ya Nyanda za Juu Kusini tutaweza kuendelea kukuza utalii wetu na kuendelea kuongeza mapato katika sekta hii ya utalii. Tuna beach nzuri, kuna mzungumzaji hapa wa kutoka Zanzibar alizungumza masuala ya fukwe, tuna beach nzuri kule ya Matema beach Nyanda za Juu Kusini. Lakini vilevile unazikuta beach hizi na kule Ruvuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni wakati sasa Wizara iangalie namna bora ya kuendeleza na kukuza utalii Nyanda za Juu Kusini ili kuweza kuendeleza watalii zaidi, lakini vilevile kuongeza kipato katika sekta hii ya utalii. Tusing’ang’anie tu Kaskazini, Kaskazini inajulikana sana, tuangalie tuna fursa nyingine za Nyanda za Juu Kusini na maeneo mengine. Bado hayajafanyiwa kazi inavyotakiwa, yakifanyiwa kazi inavyotakiwa tuna vivutio vya kipekee sana ambavyo vinaweza vikaongeza mapato ndani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukienda kule Ruvuma Jimbo la Mheshimiwa Jenista kuna mapitio yale ya Wakatoliki na Makanisa makubwa ambayo yamejengwa zamani, tukiweka vizuri wale wakoloni, Wajerumani ambao walijenga yale makanisa watavutiwa kuja kuona. Nafikiri kuna umuhimu sana wa Wizara kuangalia…

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, Taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, nataka kumuongezea taarifa Mheshimiwa Neema kwamba kule Nyanda za Juu Kusini, lakini kwenye Jimbo la Momba tunayo pia maporomoko ambayo yako kwenye Kijiji cha Mfuto na Yala, kwa hiyo pia na yenyewe tunaomba Wizara ya Maliasili yaweze kuyatambua ili yaendelee kuongeza watalii.

NAIBU SPIKA: Haya, Mheshimiwa Neema, taarifa.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naipokea taarifa kwa mikono yote kwa sababu nayo itaingia kwenye package ya utalii wa Nyanda za Juu Kusini na kuweza kuinua utalii Nyanda za Juu Kusini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda sasa kuzungumzia suala la migogoro katika hifadhi, game reserve na forest reserve ambazo zinazunguka ndani ya Mkoa wetu wa Njombe. Mpanga Kipengele upande wa Makete na upande wa Wanging’ombe kuna changamoto ya migogoro ya ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda upande wa Makete kuna Kijiji cha Ikovi, Kimani, Ibaga hivi vyote vina mgogoro katika game reserve hii ya Mpanga-Kipengere. Nilikuwa naiomba Wizara itafute namna ya kutatua mgogoro huu, umekuwa mgogoro wa miaka mingi sana, ifike namna sasa ijulikane game reserve mipaka yake iko wapi na vijiji viko wapi. Lakini vilevile, upande wa Wanging’ombe kule kuna vijiji kama vya Ruduga, Igando, Ihanja, Hanjawanu, Mpanga, Malangali, Wangamiko, Iyai na Mayele bado nako kuna shida ya migogoro ya mipaka kati ya vijiji na hiyo game reserve. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vil vile ukienda Mpanga-Kipengere Forest Reserve kuna vijiji vya Masage, Wangama, Ikanga na Kipengere yenyewe bado napo kuna changamoto ya migogoro hii ya mipaka ya ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawaomba Wizara hii Mheshimiwa Waziri unatoka Njombe ninamatumaini makubwa mgogoro huu utakwenda kuumaliza hivi punde. Vilevile Waziri wa Ardhi kipindi hicho akiwa Naibu Waziri nilishawahi kuzungumza hapa ndani ya Bunge, akaja kule Wanging’ombe, tatizo lililokuja alikuja mwenyewe, issue kama hizi Mheshimiwa Waziri wa Maliasili mnatakiwa mshirikiane na Waziri wa Ardhi, wote mkifika site kwa pamoja mkakubaliana mtaweza kumaliza matatizo haya, lakini mmoja akienda mwingine akienda siku nyingine hamuwezi kufikia muafaka. Kwa sababu, kila mtu atakuwa anaangalia upande wake ni vizuri mkafanya kazi kwa kushirikiana, ili kuweza kumaliza matatizo haya ya hifadhi na vijiji vinavyozunguka hifadhi na mapori ya akiba. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kule Hifadhi ya Kitulo pia bado kuna changamoto hiyo kuna changamoto kubwa sana maana yake Hifadhi ile ya Kitulo ilianzishwa mwaka 2005 lakini migogoro ikaanza mwaka 2019 mpaka mwaka 2020; sababu ya migogoro hiyo ni kwa sababu waliweka beacon mpya kwa mara ya pili. Kwa hiyo, kuna vijiji kama cha Misilo, Lugoda, Igenge… (Makofi)

NAIBU SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Neema kwa mchango mzuri.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)