Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Stella Ikupa Alex (37 total)

MHE. STELLA IKUPA ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza:
(a) Je, ni lini Serikali itaziagiza Halmashauri na Manispaa, kutenga fungu maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu kama ilivyo ile asilimia 10 kwa wanawake na vijana?
(c) Je, Serikali haioni sasa ni muda muafaka wa kufanya zoezi la utambuzi kwa watu wenye ulemavu, aina ya ulemavu walionao, pamoja na hali zao kiuchumi ili zinapotokea fursa iwe rahisi kuwafikia walengwa?
NAIBU WAZIRI WA SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU (MHE. DKT. ABDALLAH S. POSSI): Mheshimiwa Naibu Spika, moja, kuhusu kutenga asilimia ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya watu wenye ulemavu. Kwanza niseme kabisa natambua utaratibu wa sasa wa kutenga asilimia 10 kwa maendeleo ya wanawake na vijana ulifanywa kutokana na kutambua tatizo la kuachwa nyuma kwa makundi haya muhimu. Falsafa hiyo hiyo inajengeka kwa watu wenye ulemavu. Hivyo basi, Serikali kwa kupitia taratibu zake za kiutawala na kisheria itaanza utaratibu wa kuutekeleza mpango huu pale hali itakaporuhusu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya mpango huo haujaanza kutekelezwa, nitoe wito kwamba katika asilimia hii 10 ya vijana na wanawake, basi kipaumbele maalum kitolewe kwa watu wenye ulemavu kwa mujibu wa Sheria Namba T isa (9) ya Mwaka 2010 kama nilivyoelezea kwa mujibu wa Kifungu cha tatu (3), pia kwa mujibu wa Kifungu namba 34(2), lakini pia kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inasema maana ya kubagua haitoizuia Serikali kuchukua hatua za makusudi ili kutatua matatizo mahsusi katika jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni wajibu wa Taasisi za Serikali kupitia Katiba na kupitia vifungu hivyo nilivyovitaja kutoa kipaumbele maalum kwa watu wenye ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, namba mbili, kuhusu zoezi la utambuzi. Hapa kuna mawili; kwanza, tayari nilishazindua kazidata yenye taarifa za watu wenye ulemavu. Kazidata hiyo itatumika kufanya mambo mbalimbali ikiwemo utambuzi wa watu wenye ulemavu na mahitaji yao na inatarajiwa pale fedha itakapopatikana na hali ya teknolojia itakapoendelea, kazidata hii iunganishwe pia na kazidata nyingine zinazohusiana na taarifa ya hali ya watu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia niongeze kitu kimoja, kwamba tayari Serikali imeshatoa maagizo ya kuundwa kwa Kamati za Watu Wenye Ulemavu katika Halmashauri mbalimbali. Kamati hizi ndizo zitafanya kazi nzuri ya kuzishauri Halmashauri kuhusiana na mahitaji maalum ya watu wenye ulemavu. Hivyo, kupitia Bunge hili nisisitize kutekelezwa kwa agizo hilo la Serikali la kuundwa kwa Kamati Maalum za Watu Wenye Ulemavu katika ngazi mbalimbali za Serikali za Mitaa.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Naitwa Ikupa Alex, samahani. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, wachimbaji hawa wadogo nchini ni muda mrefu sasa wamekuwa wakikumbwa na migogoro ya mara kwa mara na wachimbaji wakubwa hasa kule Mererani. Je, Serikali ina mpango ama mkakati gani wa kuhakikisha kwamba inatatua migogoro hii na kuhakikisha kwamba haijirudii tena?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa wachimbaji wadogo wadogo na siyo Mererani peke yake ni kote nchini, wamekuwa wakikumbwa na migogoro hasa kati yao na wawekezaji wakubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Mererani, kwanza kabisa kuna migogoro ya aina mbili; iko migogoro ya wao kutoboza chini kwa chini kuingia kwenye mgodi wa Tanzanite One ambao ni mgodi mkubwa kwa ajili ya kuchukua kidogo Tanzanite. Huo mgogoro tunashughulika nao.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia wachimbaji wa Mererani wana maeneo madogo, lakini hatua tuliyofikia sasa ni kuwatafutia maeneo wananchi wa Mererani ili wachimbe karibu na eneo la mgodi ule kwa sababu na kwenye kuna Tanzanite ya kutosha. Hiyo ni hatua ya pili.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya tatu, mgogoro ambao sana sana ni wa kiufanyakazi, ni mgogoro kati yao na waajiri wao. Mgogoro huu tunawasiliana kwa ukaribu sana na Wizara ya Kazi. Mwezi uliopita tulikaa kama Kamati na kusuluhisha mgogoro huo. Kwa sasa tunaamini kwamba wananchi wa Mererani kwa sababu watapata maeneo yao na taratibu za ajira zitazingatiwa. Kwa hiyo, matatizo sasa ya mgogoro kati yao na wachimbaji wakubwa zinakoma mara moja.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ameelezea kwamba katika hivi viwanja vya ndege kuna wheel chairs na stretchers, lakini swali langu la msingi lilihoji kwa habari ya ambu-lift. Ukisema wheel chair inamsaidia tu yule mhitaji kumpeleka mpaka eneo la ndege, lakini anapofika pale inabidi abebwe juu juu na wale staff wa airport kitu ambacho kinakuwa ni very risk!
Mheshimiwa Naibu Waziri, kutokana na umuhimu wa ambu- lift, ni nini commitment ya Serikali kuhusiana na uwepo wa huduma hii katika viwanja vyote vya ndege nchini? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana naye kwamba ambu-lift ndiyo kifaa kinachohitajika zaidi na chenye usalama zaidi kuliko hivyo vingine. Kama nilivyojibu katika jibu langu la nyongeza, Wizara yangu itahakikisha wale wanaotoa huduma kwa maana ya uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere, tunawaongelea Swissport, na ninawataka Tanzania Airport Authority nao wahakikishe wanaongeza huduma hiyo ya ambu-lift katika kiwanja cha Mwalimu Julius Nyerere International Airport pamoja na Kilimanjaro, Songwe na viwanja vingine.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (WATU WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niseme natambua majibu mazuri ya Naibu Waziri wa Ujenzi. Niongezee tu mambo machache kuhusu huduma kwa watu wenye ulemavu katika viwanja vya ndege na maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Sheria Na. 9 ya mwaka 2010 ilifuta sheria za zamani zilizokuwa zinazungumzia masuala ya watu wenye ulemavu, na moja ya mambo ambayo yameelezwa wazi katika sheria mpya hii ni kutambua suala la kufikika kirahisi na kupata huduma mbalimbali kirahisi kwa watu wenye ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria hii ilianza kufanyakazi mwaka 2012 na ni wazi kwamba katika kipindi ambacho sheria hii imeanza kufanya kazi yapo, majengo na ipo miundombinu mingi sana ya Serikali ambayo kwa namna moja au kwa namna nyingine ilikuwa imejengwa kizamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, commitment ya Serikali kuyabadilisha ipo, lakini hili ni suala ambalo litachukuwa muda na Ofisi ya Waziri Mkuu itakuwa inawasiliana na Wizara nyingine kadri inavyowezekana kuhakikisha kwamba taasisi zote za Serikali katika nyanja mbalimbali, elimu, afya, miuondombinu na kadhalika, zinachukuwa hatua zinazofaa ili kuhakikisha kwamba watu wenye ulemavu wanapata huduma stahiki, kokote wanakokwenda.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ameelezea kwamba katika hivi viwanja vya ndege kuna wheel chairs na stretchers, lakini swali langu la msingi lilihoji kwa habari ya ambu-lift. Ukisema wheel chair inamsaidia tu yule mhitaji kumpeleka mpaka eneo la ndege, lakini anapofika pale inabidi abebwe juu juu na wale staff wa airport kitu ambacho kinakuwa ni very risk!
Mheshimiwa Naibu Waziri, kutokana na umuhimu wa ambu- lift, ni nini commitment ya Serikali kuhusiana na uwepo wa huduma hii katika viwanja vyote vya ndege nchini? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (WATU WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niseme natambua majibu mazuri ya Naibu Waziri wa Ujenzi. Niongezee tu mambo machache kuhusu huduma kwa watu wenye ulemavu katika viwanja vya ndege na maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Sheria Na. 9 ya mwaka 2010 ilifuta sheria za zamani zilizokuwa zinazungumzia masuala ya watu wenye ulemavu, na moja ya mambo ambayo yameelezwa wazi katika sheria mpya hii ni kutambua suala la kufikika kirahisi na kupata huduma mbalimbali kirahisi kwa watu wenye ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria hii ilianza kufanyakazi mwaka 2012 na ni wazi kwamba katika kipindi ambacho sheria hii imeanza kufanya kazi yapo, majengo na ipo miundombinu mingi sana ya Serikali ambayo kwa namna moja au kwa namna nyingine ilikuwa imejengwa kizamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, commitment ya Serikali kuyabadilisha ipo, lakini hili ni suala ambalo litachukuwa muda na Ofisi ya Waziri Mkuu itakuwa inawasiliana na Wizara nyingine kadri inavyowezekana kuhakikisha kwamba taasisi zote za Serikali katika nyanja mbalimbali, elimu, afya, miuondombinu na kadhalika, zinachukuwa hatua zinazofaa ili kuhakikisha kwamba watu wenye ulemavu wanapata huduma stahiki, kokote wanakokwenda.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa suala la ujenzi wa barabara linaenda sambamba na uwekwaji wa alama za barabarani na kwa kuwa tayari Serikali imeshaanza kuweka alama hizi za barabarani kwa ajili ya watu wenye ulemavu kwa baadhi ya mikoa, kwa mfano Tanga, je, nini mpango wa Serikali kwa mikoa mingine?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba alama zote tunazoweka barabarani zinazingatia mahitaji maalum ya walemavu. Naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge na najua ameshakutana na Waziri wangu pamoja na wawakilishi wa walemavu ambao walikuja hapa Dodoma na wamelizungumzia hili suala kwa undani.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru kwa juhudi anazozifanya za kufuatilia mahitaji ya walemavu. Nina hakika kwa namna ambavyo ameanza tutafika mahali kila barabara ambayo walemavu wanaihitaji, tutaiwekea hayo mahitaji maalum kadri uwezo wa fedha utakavyokuwa unapatikana.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, katika jibu lake la msingi amesema kwamba, pindi biashara hii itakapoendelea, Serikali itachukua hatua zinazostahili. Sasa biashara hii ipo inaendelea na hasa katika Majiji makubwa kama Dar es Salaam na ni hatarishi kwa sababu mtu anakuja anajifanya kama anakuuzia kisu, mimi mwenyewe ni muathirika, pindi akikuona umeshika kitu anajifanya kama anakuuzia kisu lakini anakuamuru utoe kile kitu ulichokishika. Sasa naomba tamko la Serikali kwa habari ya biashara hii. Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuliona hilo. Kama ilivyo kwa uhalifu mwingine, Serikali inapiga vita uhalifu wa aina yoyote na nitoe rai kwa mtu yeyote ambaye atakutana na mambo ya aina hiyo na yeyote aliye karibu na mtu anayepatwa na jambo hilo, tushirikiane kuhakikisha kwamba tunakomesha uhalifu wa aina hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Polisi litakuwa bega kwa bega na litakuwa mstari wa mbele kuhakikisha kwamba wale wote wanaotumia vibaya mazingira hayo watafikishwa katika mkono wa sheria ili kuweza kukomesha uhalifu wa aina hiyo.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mawaziri, kuna hivi vyuo viwili Chuo cha Yombo na Chuo cha Singida, pamoja na uwepo wa vyuo hivi viwili lakini bado kuna changamoto nyingi sana ambazo zinavikabili vyuo hivi. Naomba niongelee specific Chuo cha Yombo kwa sababu ni chuo ambacho nimekitembelea. Chuo hiki kina changamoto ya deni kubwa la umeme, miundombinu chakavu pamoja na vifaa vya kujifunzia na kufundishia. Naomba nisikie kauli ya Serikali ni hatua gani za haraka na za makusudi za kunusuru vyuo hivi ili visije vikafungwa kama ambavyo vimefungwa hivi vyuo vingine? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa upande wa chuo hicho nikiri pia hata mimi nimewahi kukitembelea kilikuwa na upungufu fulani lakini kama ilivyozungumzwa na Ofisi ya Waziri Mkuu ni kwamba kimewekwa kwenye bajeti. Hata hivyo, kwa mwaka huu wa fedha tayari Wizara ya Elimu tulikuwa tumeagiza vifaa kwa ajili ya watu wenye ulemavu vya gharama ya shilingi takribani bilioni tatu na tayari vimeshawasili. Kwa hiyo, tutaangalia katika ugawaji na wao waweze kufikiriwa. Ahsante.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, Baraza hili limekuwa likifanya kazi kwa kusuasua sana. Kisheria linatakiwa lifanye kazi, ama likutane, ama lifanye vikao vyako japo mara nne kwa mwaka, jambo ambalo halijawahi kutokea.
Je, ni nini commitment ya Serikali kuhakikisha kwamba Baraza hili linakutana, ama linafanya vikao vyake kama sheria inavyolitaka? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, agizo la kuundwa kwa hizi Kamati kuanzia ngazi ya Vijiji mpaka Mkoa, ni agizo ambalo limetolewa mara kadhaa lakini kamatii hizi haziundwi. Je, Serikali haioni sasa kwamba ni muda muafaka wa kutoa deadline ya uundwaji wa Kamati hizi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA NA AJIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa mujibu wa Sheria Na. 9 ya Watu wenye Ulemavu ya mwaka 2010, Mabaraza haya yanatakiwa kukaa mara nne kwa mwaka. Sheria Na. 9 ya Watu wenye Ulemavu ya mwaka 2010 imeanza kutekelezwa mwaka 2012.
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya sheria hii, Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 1982 ilizungumza pia kuhusu Mabaraza haya. Wakati wa Tume ya Marekebisho ya Sheria walipokuwa wakiangalia Sheria za Watu wenye Ulemavu waligundua kwamba mabaraza haya hayakukaa kwa muda mrefu sana, takribani miaka kumi na kitu.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya Serikali ya Awamu ya Tano kuingia, katika utekelezaji wa sheria hii, ndani ya mwaka mmoja, tayari Mabaraza haya yameshakaa na yameanza kutoa ushauri kwa Serikali. Baraza la kwanza lilikaa mwaka 2016 mwezi wa nne ambalo alifungua Mheshimiwa Dkt. Possi na Baraza la pili tayari limekaa tarehe 14 Januari, 2017. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba commitment ya Serikali ni kuhakikisha mabaraza haya yanakaa kwa mujibu wa taratibu kama ilivyoelezwa kwenye sheria na tutaendelea kuitengea fedha ili watu wenye ulemavu wapate fursa ya kuishauri Serikali ipasavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia mabaraza haya, Serikali imekuwa ikipata ushauri mbalimbali na sisi tumekuwa tukiyafanyia utekelezaji hasa kupata ushauri kutoka kwenye haya mabaraza.
Mheshimiwa Ikupa, jambo moja tu la ziada, ukisoma kwenye sheria yetu kifungu namba 46(1)(b) kimetoa mazingira ya kusaidia mafunzo ya ufundi stadi kwa watu wenye ulemavu ambayo imekuwa ni mapendekezo ya baraza hili. Na sisi katika utaratibu wetu, tumeshazungumza na watu wa VETA na wamesha-mainstream mfumo wa utoaji wa mafunzo kwa walimu wao ambapo kwa sasa hivi wanafundishwa elimu ya msingi kabisa ya kuwafundisha watu wenye ulemavu. Lengo letu ni kuweza kuwafikia wengi zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo hili tunao ushahidi wa mtu mwenye ulemavu, ndugu yetu mmoja anaitwa Boniface Kayenzi, ana umri wa miaka 63, amefundishwa VETA, sasa hivi anatengeneza na kuranda mbao na amekuwa akitumiwa katika sehemu mbalimbali za Maonesho ya Kimataifa na Biashara. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la Mheshimiwa Mbunge, amezungumzia kuhusu uundwaji wa Kamati hizi za watu wenye ulemavu kuanzia ngazi ya Kata mpaka huku juu.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa mujibu wa sheria yetu, kuna kitu kinaitwa sectorial plan ambapo inafanya kazi, Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara nyingine. Mheshimiwa Waziri wa Nchi alikwishaandika barua Ofisi ya Rais - TAMISEMI), ambapo kule chini ndiko wanakosimamia hizi Kamati, kwa maana ya Halmashauri na Mikoa ili sasa agizo hilo lishuke chini. Mheshimiwa Simbachawene alikwisha kuiandika barua hiyo kufika chini ili Kamati hizi ziundwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Mheshimiwa Mbunge, niwaombe tu na Wabunge wote mlioko hapa, sisi Wabunge tunapata fursa kuingia kwenye vikao vya Halmashauri, mtusaidie na ninyi katika vikao vyetu kuendelea kutoa msisitizo ili Kamati hizi ziweze kuundwa.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kutokana na majibu mazuri ya Serikali kuwa msamaha wa matibabu utatolewa kwa mtu mwenye ulemavu ambaye atabainika hana uwezo; ikumbukwe kuwa ugonjwa unampata mtu bila taarifa.
Je, Serikali ina utaratibu gani wa kuwabaini watu wenye ulemavu wasio na uwezo ili waweze kupata msamaha huu wa matibabu?
Swali la pili, je, Serikali ipo tayari kuziagiza mamlaka husika na kutoa waraka ili majibu yaliyotolewa hapa leo yaweze kutekelezwa?
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, maswali anayozungumzia Mheshimiwa Stella ni muhimu sana kama ulivyosema wewe mwenyewe na ni maswali yanayohusu uwiano na usawa kwenye jamii yetu, ambapo kama Taifa ni lazima tutoe uwiano sawa kwa watu wote bila ubaguzi wa aina yoyote ile kama ambavyo waasisi wa Taifa letu waliweka misingi kupitia sera yetu ya ujamaa na kujitegemea.
Mheshimiwa Spika, ni kwa msingi huo, Serikali kupitia
Sera yake ya Afya ya mwaka 2007 inatoa matamko ya kisera ya namna ambavyo makundi maalum kwenye jamii yanalazimika kuhudumiwa ikiwemo kundi hili la watu wenye ulemavu.
Mheshimiwa Spika, sasa utaratibu wa utekelezaji unawekwa na sheria na taratibu mbalimbali ndani ya Serikali. Katika awamu hii ya tano, tunakusudia kuleta hapa Bungeni mapendekezo ya Bima ya Afya ya lazima kwa watu wote ambapo ndani yake tutakuwa tumeweka utaratibu mahsusi wa kuhakikisha uwiano huu tunaouzungumza unatekelezeka kupitia Bima ya Afya ambapo tutaweka utaratibu sasa kwamba watu wanaopewa msamaha kwa mujibu wa sera, basi wawe na kadi ya Bima ya Afya kuliko ilivyo sasa. Kwa sababu inajitokeza katika nyakati mbalimbali ana msamaha anastahili kupata huduma bure, lakini anapofika kwenye kituo cha kutolea huduma, anakosa dawa ama anakosa vipimo fulani na analazima kwenda kwenye private. Kwa hiyo, hata ile bure inayokusudiwa na sera yetu inakuwa haipo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, sisi ndani ya Serikali tunaamini kama tutafanikiwa kupitisha sheria hii ya Bima ya Afya kwa wote, utaratibu utakuwa mzuri. Kwa hiyo, anachokizungumzia sasa hivi tumekianzisha kwa mfano tu kwa kujaribisha kwenye kundi la wazee wenye umri wa zaidi ya miaka 60 wasiojiweza ambapo Halmashauri zinalazimika kuwabaini wazee wote katika eneo lao na kuwawekea utaratibu wa kuwapa kadi za CHF ili kujaribisha utaratibu tunaozungumza.
Mheshimiwa Spika, kwenye kundi la walemavu, bado hatujaanza.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali na vigezo ambavyo vimetolewa vya upangaji na uhamishaji watumishi wa umma, je, Serikali haioni kuwa ulemavu nao uwe ni miongoni mwa vigezo ambavyo vimetolewa ili mtu mwenye ulemavu awe comfortable na hatimaye aweze kutimiza wajibu wake ipasavyo?
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru kwa swali zuri au kwa ushauri. Hili ni eneo ambalo tutakwenda kuliangalia, tumekuwa tukiangalia sababu za kiafya, wengine kuwafuata wenzi wao, niseme na lenyewe tutalifanyia kazi ili kuona ni namna gani na hii pia inaweza kuwa ni moja ya kigezo.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wiki iliyopita Mkoani Dar es Salaam lilitokea tukio la kusikitisha dhidi ya watu wenye ulemavu ambao ni waendesha bajaji ambapo walifanyiwa vitendo vya udhalilishaji pamoja na vitendo vya kinyama, walipigwa sana na baadae kuburuzwa chini. Pamoja na makosa ambayo walidaiwa kuwa nayo lakini approach ambayo ilitumika na askari wetu haikuwa nzuri kabisa. Je, nini kauli ya Serikali kwa hili? (Makofi)
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Ikupa kwa kuleta swali hilo na yeye ni Mbunge anayewakilisha kundi hilo, kwa sababu yupo ni-apologize kwa niaba yake awafikishie salamu hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyosema kwamba pamoja na utaratibu kuwepo ama ukiukwaji wa utaratibu, kwa kuzingatia hali yao ni nguvu kubwa imetumika. Serikali tumeshajadiliana na wenzetu wa TAMISEMI, watakutana na Wizara ya TAMISEMI pamoja na wenzao wa ngazi ya Mkoa ili kuweka utaratibu ambao utakuwa una taswira nzuri na kufanya jambo hilo ili lisiweze kujirudia kuweka utaratibu ulio wa kudumu ili liweze kufanya utaratibu huo wa kudumu. Kwa hiyo, tumepokea concern hiyo na linafanyiwa kazi ili jambo la aina hiyo lisijirudie.(Makofi)
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ninaomba niendelee kutambua juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali kupitia Wizara hii na hasa pale ilipotamka wazi kwenye hotuba yake kwamba imetoa kipaumbele cha elimu kwa watoto wenye ulemavu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunapoongelea elimu jumuishi tunamaanisha kwamba watoto wenye ulemavu wasome na wasio na ulemavu. Sasa Serikali inaonaje hii elimu maalum ikafundishwa kwenye vyuo vyote vya ualimu nchini tofauti na ilivyo sasa hivi kwamba ni walimu wachache wanaopata ujuzi huu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili katika hii mitaala mipya inayoandaliwa Serikali inaonaje ikaingiza lugha ya alama kuwa miongoni mwa masomo ambayo yatafundishwa ili kizazi kijacho kiweze kuwasiliana na viziwi kwa urahisi? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Ikupa kama ifuatavyo; ni kweli ili wanafunzi hawa waweze kupata haki yao ya msingi ya kuweza kujifunza vizuri popote walipo ni pale tutakapokuwa na walimu wa kutosha ambao wana uwezo wa kuwasiliana na kutoa elimu husika kwa watoto hao.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali hii ni muhimu sana, lakini kwa sasa tunachoangalia ni kuona kwamba ni namna gani tunafanya hivyo, kwa mfano katika suala la lugha ya alama, Wizara tayari inaliangalia jambo hili ili kuwezesha walimu wote angalau wawe na msingi wa lugha ya alama ili kuweza kuwasaidia wanafunzi hao. Kwa hiyo, jambo hilo mimi naona tulichukue tuone ni namna gani tutalifanyia kazi. Kwa msingi huo nimejibu maswali yote mawili kwa pamoja, ahsante.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kutokana na umuhimu wa taulo hizi za kike kwa wanawake na watoto wa kike Tanzania na kutokana na ughali wake ambao unapeleka wanawake wengi na watoto wa kike kushindwa kumudu kuzitumia na kwa kuwa Serikali imekiri kwamba maombi haya yameshawasilishwa na wadau wengi.
Mheshimiwa Spika, sasa Serikali inaweza ikatuambia nini wanawake wa Tanzania kwamba watoto wengi wanapata shida hasa watoto wa vijijini kwa sababu wanashindwa kuzipata hizi taulo kwa ughali wake. Sasa Serikali inaweza ikatuambia ni lini tutegemee kwamba lini huu mchakato utakamilika?
Mheshimiwa Spika, ingekuwa ni vizuri wakatuambia ni lini mchakato huu utakamilika kwa sababu kweli hili jambo ni suala nyeti sana kwa wanawake na watoto wa kike Tanzania? Ahsante. (Makofi)
WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, na mimi kwa kweli namshukuru sana Mheshimiwa Stella Ikupa kwa swali lake zuri la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, mimi ni mwanamke lakini pia nina watoto wa kike wawili, kwa hiyo, nakubaliana na yeye kabisa kwamba tuna changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa taulo za kike hasa kwa watoto walio vijijini na tunazo taarifa kuna watoto wanaweka mpaka majini ili kuweza kujisitiri pale wanapokwenda shule, lakini pia kuna watoto wanakosa hadi siku tano za masomo kwa sababu hawana zana za kujisitiri ili waweze kufanya masomo yao bila shida. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwahiyo, Wizara yangu nimeshamuandika Waziri wa Fedha kumuomba aharakishe mchakato huu, nilikuwa namtimizama hayupo lakini naamini wenzetu wa Wizara ya Fedha wanalifanyia kazi na tutakuja na majibu mazuri kadri itakavyokamilika, ahsante sana. (Makofi)
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba nitambue juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi katika kuhakikisha ustawi wa maisha ya watu wenye ulemavu. Pia naishukuru sana Serikali kwa majibu haya mazuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kuna watu wenye ulemavu ambao wamejitahidi kuondokana na utegemezi na hivyo kuanzisha biashara zao, je, Serikali iko tayari kuondoa kodi kwenye biashara za watu wenye ulemavu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa kuna ile 10% ya Halmashauri ambayo inatengwa kwa ajili ya wanawake na vijana; na kwa kuwa Serikali ilishakubaliana na pendekezo langu la kugawanya asilimia hii, kwamba 4% iwe kwa wanawake na 4% iwe kwa vijana halafu 2% iwe kwa ajili ya watu wenye ulemavu, je, ni lini sasa pendekezo langu hili litafanyiwa kazi? Ama ni nini tamko la Serikali kuhusiana na huu ugawaji wa hii 2%?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameuliza kama Serikali ipo tayari kuondoa kodi kwa watu wenye ulemavu wanaojishughulisha na shughuli za kibiashara na ujasiriamali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, napenda kuchukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwasemea watu wenye ulemavu na amekuwa mchango na msaada mkubwa sana ndani ya Wizara yetu. Pia Serikali inawathamini sana na tunaendelea kuwaendeleza watu wenye ulemavu katika kuhakikisha kwamba na wenyewe wanapata ujuzi mbalimbali ili waweze kujitegemea pamoja na biashara mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, tumeweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba watu wote wenye ulemavu ambao wanafanya shughuli mbalimbali, lakini ambao wangependa pia kujifunza masuala mbalimbali katika kila programu chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, tumetenga nafasi maalum ili watu hao wenye ulemavu waweze kupata nafasi ya kushiriki katika programu mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, programu mojawapo ya mfano kabisa ni programu ya Youth Economic Empowerment ambayo ilikuwa chini ya Plan International ambapo tulitenga nafasi zaidi ya 950 kwa watu wenye ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la kwanza, aliuliza kama Serikali ipo tayari kuwaondolea kodi. Mheshimiwa Mbunge ameleta wazo hili, nasi tunalipokea, lakini kwa sasa kwa sababu ya taratibu za nchi zilivyo, siwezi kusemea hapa moja kwa moja lakini kubwa ambalo tutalifanya ni kuhakikisha tu kwamba tunawajengea uwezo zaidi ili na wao waweze kujitegemea. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ridhaa yako, nakuomba swali la pili kuhusu 10% atalijibu Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ikupa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Mheshimiwa Ikupa, siku ya uwasilishaji wa bajeti yetu alileta hiyo concern ya watu wenye ulemavu na siku ile tuliweka commitment kwamba kwa sababu katika ule mgawanyo wa 10%, kuna kundi la vijana, akina mama na kundi specific la watu wenye ulemavu ambalo halijazungumzwa. Tulifanya commitment siku ile kwamba tutaangalia utaratibu tuone ni jinsi gani tutafanya, hata 2% kutokana na mapendekezo yake; na siku ile liliridhiwa katika bajeti.
Mhehimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, lipo katika mchakato, tutalifanyia kazi na tutatoa waraka maalum katika eneo hilo. (Makofi)
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Wakati Serikali inajibu swali mwezi Januari mwaka huu iliahidi kutenga fedha kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya ukarabati na kuvifufua vyuo vya watu wenye ulemevu; na kwa kuwa fedha hii haijatengwa, je, Serikali ina kauli gani kwa hili? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Wizara inazo fedha kwa ajili ya kufufua baadhi ya vyuo vya watu wenye ulemavu kupitia mradi wake wa P4R. Kwa hiyo naomba uwe na amani ni kwamba zoezi hilo litafanyika kama ambavyo tumeanza katika shule nyingine ikiwemo shule ya Luwila pale Songea, shule ya Kipera pale Iringa na nyinginezo.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wiki iliyopita Mkoani Dar es Salaam lilitokea tukio la kusikitisha dhidi ya watu wenye ulemavu ambao ni waendesha bajaji ambapo walifanyiwa vitendo vya udhalilishaji pamoja na vitendo vya kinyama, walipigwa sana na baadae kuburuzwa chini. Pamoja na makosa ambayo walidaiwa kuwa nayo lakini approach ambayo ilitumika na askari wetu haikuwa nzuri kabisa. Je, nini kauli ya Serikali kwa hili? (Makofi)
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Ikupa kwa kuleta swali hilo na yeye ni Mbunge anayewakilisha kundi hilo, kwa sababu yupo ni-apologize kwa niaba yake awafikishie salamu hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyosema kwamba pamoja na utaratibu kuwepo ama ukiukwaji wa utaratibu, kwa kuzingatia hali yao ni nguvu kubwa imetumika. Serikali tumeshajadiliana na wenzetu wa TAMISEMI, watakutana na Wizara ya TAMISEMI pamoja na wenzao wa ngazi ya Mkoa ili kuweka utaratibu ambao utakuwa una taswira nzuri na kufanya jambo hilo ili lisiweze kujirudia kuweka utaratibu ulio wa kudumu ili liweze kufanya utaratibu huo wa kudumu. Kwa hiyo, tumepokea concern hiyo na linafanyiwa kazi ili jambo la aina hiyo lisijirudie. (Makofi)
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kundi kubwa la watu wenye ulemavu wana vipato duni na hivyo inawapelekea kushindwa kumudu gharama za matibabu. Je, Serikali inaonaje ikiwatambua kama ilivyofanya kwa wazee na kuwapatia vitambulisho vya huduma za afya bila malipo? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, swali la Mheshimiwa Mbunge ni swali nzuri sana, lakini kwa sababu tunaenda kuleta Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote, naamini wakati wa mjadala haya maswali yote na kuwahudumia watu wa namna hiyo tutaweza kupata namna ya kufanya. Ahsante.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi. Tatizo ambalo lipo katika Mkoa wa Songwe linafanana kabisa na tatizo ambalo liko katika Mkoa wa Dar es Salaam kwenye baadhi ya maeneo, na hasa katika Jimbo la Ukonga kwenye baadhi ya Mitaa ya Kata za Msongola, Chanika, Zingiziwa na Buyuni:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inasema nini kwa habari ya kuhakikisha kwamba Mkoa wa Dar es Salaam unapata umeme?
WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Dar es Salaam una mahitaji makubwa sana ya umeme, ingawa Dar es Salaam tuna jumla ya Megawati 572 zinazotumika kwa Dar es Salaam, lakini mahitaji yanaongezeka kila leo. Tumejenga dedicated line ya kutoka Kinyerezi kupita Gongo la Mboto kwenda mpaka Ukonga – Pugu mpaka Dondwe kule Chanika Zingiziwa kwa ajili ya kupelekea umeme wananchi wa huko.

Mheshimiwa Spika, tumewapatia mkandarasi wa peri-urban atakayepeleka umeme katika maeneo ya Bomba Mbili, Majohe, Mvuti, Songambele pamoja na Zingiziwa mpaka Kisasa, mpaka Magerezani kule Dondwe ndani. Kwa hiyo, wananchi wa Dar es Salaam watapata umeme, na ni ndani ya miezi sita utaratibu utakamilika na wananchi kupata umeme wa uhakika.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa kuweka ulemavu kama kigezo kimojawapo cha upatikanaji wa mikopo kama ambavyo Bunge la Kumi na Moja liliweza kushauri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali hili si mara yangu ya kwanza naliuliza ndani ya Bunge hili, lakini pia mara kadhaa nilipopata kuchangia niliweza kuchangia na jibu limekuwa ni hili. Kama ambavyo jibu limesema kwamba Serikali italifanyia kazi, ni lini Serikali itaanza kulifanyia kazi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SANYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ikupa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwishajibu katika majibu yangu ya swali la msingi kwamba Serikali inaendelea kulifanyia kazi suala hili. Kama nilivyokwishaeleza hapa punde kwamba katika mjadala wetu wa bajeti tulisema kwamba tunakwenda kuwa na mjadala mpana kuhusiana na elimu yetu nchini kwa maana kwamba tunaenda kuangalia Sera yetu ya Elimu ya mwaka 2014, lakini tunaenda kuangalia Sheria yetu ya Elimu ya mwaka 1978. Hili nalo kwenye mjadala huo litakwenda kujadiliwa kwa kina na kuona ni namna gani tunaweza kuyafikia makundi haya badala ya kuwapa mikopo tukatoa ruzuku. Nadhani kabisa katika mjadala huo tunaweza tukayaingiza.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaishukuru Serikali kwa majibu mazuri; nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ugonjwa hautasubiri mpaka mpango huu mzuri wa bima ya afya kwa wote ukamilike, na kwa kuwa miongozo ambayo inatolewa na Serikali kiuhalisia haizingatii na watendaji; ni nini kauli ya Serikali kwa watendaji hawa?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia ikumbukwe kwamba wakati wa Bajeti ya Wizara hii ya Afya, Mheshimiwa Waziri wakati akihitimisha hotuba ya bajeti yake alisema kwamba Serikali imeandaa utaratibu mzuri wa matibabu kwa wazee, ambapo alisema kwamba zitaandaliwa tisheti nzuri ambazo zitahamasisha utoaji wa huduma bora kwa wazee.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Serikali inaonaje mpango huu mzuri ukawajumuisha na watu wenye ulemavu?

Kwa mfano kama tisheti hizi zitaandikwa mzee kwanza, basi iwe mzee kwanza na mtu mwenye ulemavu, lakini pia kama itaandikwa kwamba tuwajali wazee basi tuwajali wazee na watu wenye ulemavu.
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO (MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL). Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kwa kusema kwamba ni kweli kama Mheshimiwa Mbunge anavyosema, kwamba ugonjwa na matatizo hayasubiri mswada kutengenezwa. Lakini kama ambavyo unajua kwamba kwa sasa kwenye hospitali zetu; na kwenye eneo hilo anachotaka kujua Mheshimiwa Mbunge ni tamko gani linatolewa. Kwa sababu kwa kweli pamoja na kuwepo na sheria na vitu, vingine inawezekana kuna maeneo ambayo haizingatiwi maelekezo ya Serikali kwa mambo ambayo kwa sasa yapo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mimi niseme na nitoe ari kwamba, kwanza agizo, Waganga Wakuu wa Mikoa na Ma-DMO wanapokuwa wanazunguka; cha kwanza kwenye CCP zetu na kwenye supervision zao wahakikishe kwamba wamekagua na kuhakikisha kwamba hizi haki zimezingatiwa. Pia kuwaomba kupitia TAMISEMI Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala kusimamia suala hilo ipasavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ni kuhusu suala la kuunganisha huduma za watu wenye ulemavu pamoja na huduma za wazee. Kama ambavyo tayari Mheshimiwa Waziri ameshazindua hili suala la tisheti na kuzindua huo mkakati wa kuweza kuboresha huduma za wazee kama ambavyo mmeona kwenye vyomba vya Habari; tunachukuwa wazo lake kwamba hilo suala liende kuunganishwa pamoja na suala la watu wenye ulemavu.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie nafasi hii kuipongeza na kuishukuru sana Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo inazishughulikia changamoto mbalimbali za watu wenye ulemavu ikiwemo changamoto hii ya lugha ya alama; na ikikumbukwa kwamba changamoto hii niliweza kuizungumzia sana katika Bunge la Kumi na Moja, lakini hatimaye leo hii Serikali ya Awamu ya Sita imeanza kulifanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii itasaidia jamii yetu, yaani tunandaa kizazi ambacho kitaweza kuwasiliana na viziwi kwa maana ya Polisi, Walimu, Madaktari hata kwenye familia zetu. Kwa hiyo, naipongeza sana Serikali. Sina uwezo wa kupiga magoti, ningepiga magoti kuishukuru Serikali ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza la nyongeza ni kwamba, ni lini sasa mchakato huu utakamilika na hatimaye mitaala hii kuanza kutumika ndani ya nchi yetu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wakati tunasubiri ukamilishwaji wa mchakato huu, Serikali ina njia gani mbadala ya kuinua kiwango cha elimu kwa wenzetu viziwi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza naomba tupokee hizo pongezi za Mheshimiwa Rais kwa niaba yake, lakini tunaamini pongezi hizi zimemfikia na hiyo ndiyo Serikali ya Awamu ya Sita, Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan na huo ndiyo wajibu wetu kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba mchakato huu wa maboresho ya mitaala yetu ni agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alioutoa tarehe 22 Aprili, 2021. Mara tu baada ya maagizo yale, sisi kama Wizara tulikaa na kuanza kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchakato huu huwa unachukua muda mrefu, ni kati ya miaka mitatu mpaka mitano. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutajitahidi kuhakikisha kwamba katika kipindi kifupi kisichozidi miaka mitatu na miezi tisa mitaala yetu hii mipya iweze kuwa tayari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilihakikishie Bunge lako Tukufu, ifikapo mwaka 2025 Januari, mitaala yetu mipya itakuwa tayari kuanza kutumika katika maeneo yote kama tulivyokusudia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili amezungumzia juu ya namna gani watoto wetu tunawachukuwa kwa sasa hivi? Nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ipo mbioni na inaendelea kuwahudumia wanafunzi hawa au watoto wetu hawa. Kwanza tuna shule ya msingi ambazo tumejenga kule Mtwara inayoitwa Lukuledi kwa ajili ya kuwachukua wanafunzi hawa wenye matatizo ya uziwi kwa upande wa Shule za Msingi. Vilevile kule Patandi Arusha, tuna Shule ya Sekondari kwa ajili ya wanafunzi hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, katika kipindi hiki tumeweza kutoa mafunzo kwa Walimu kwenye shule ambazo zinachukua wanafunzi wenye uziwi katika shule zetu zote za Sekondari katika kipindi kilichopita; na pia mwezi Machi mwaka huu Walimu wetu wa Shule za Msingi kwa shule zinazochukua wanafunzi hawa, nao vilevile tutawapa mafunzo ya lugha ya alama na kuwapa mbinu za namna ya kuwafundisha wanafunzi hawa. Ahsante. (Makofi)
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa watu wenye ulemavu wanahitaji privacy zaidi na miundombinu rafiki wakati wa kujifungu. Je, Serikali inaonaje ikatenga vyumba maalum ambavyo vitatumika na wanawake hawa wenye ulemavu wakati wa kujifungua pale wanapojitokeza? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stella Ikupa, Mbunge wa Viti Maalum anayewakilisha watu wenye mahitaji maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naye nimpongeze kwa kuwa anafanya kazi nzuri ya kufuatilia watu wenye mahitaji maalum nchi nzima. Hili alilolileta hapa kama swali. Ameeleza vizuri, kwamba watu wenye mahitaji maalum wanahitaji privacy, na je, Serikali tunalionaje hili kama moja ya mahitaji yetu ya msingi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwamba tumepokea mawazo na mapendekezo yake, na tutalipeleka katika timu yetu ya wataalam ili kuhakikisha kwamba walau katika baadhi ya hospitali na maeneo yote ambayo huduma ya afya inahitaji tuweze kutenga hivi vyumba maalum ili kuwasaidia wenzetu wenye mahitaji maalum. Kwa hiyo, tumelipokea na tutalifanyia kazi. Ahsante sana.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, kwenye mpango huu wa kunusuru kaya maskini kulikuwa na mapendekezo ya kutoa kipaumbele kwa watu wenye ulemavu wanaokidhi vigezo. Je, ni kwa kiasi gani mapendekezo hayo yamezingatiwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI
WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kipaumbele kimewekwa hasa kwa watu wenye mahitaji maalum na kuangalia kwamba wanakidhi vigezo vile. Kwa sababu unakuta kuna watu wana hitaji maalum wenye ulemavu, lakini wanapopitiwa na dodoso lile wanagundulika kwamba vigezo vile vinavyotakiwa kuingia katika kaya ya walengwa hawajavifikia, lakini wengi ambao wamefikia huwa wanapewa kipaumbele na wanaingizwa katika mpango.

Mhshimiwa Spika, nimwongezee tu Mheshimiwa Mbunge, tunayo vile vile program ambayo inasaidia watu wenye ulemavu ili kuwa kwenye vikundi vya uzalishaji na wanapewa fedha kutoka Mfuko huu wa TASAF kuweza kuanzisha biashara zao, kwa hiyo tunatoa kipaumbele kwa watu wenye ulemavu.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru na kuipongeza Serikali kwa majibu yake mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa maeneo ambayo Kamati hizi zimekwishaundwa hazifanyi kazi kwa mujibu wa Sheria Na.9 ya Mwaka 2010. Je, ni sababu zipi zinazosababisha Kamati hizi kutokufanya kazi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; naipongeza pia Serikali kwa mikakati mizuri ambayo imewekwa kwa ajili ya ukamilishwaji wa kuundwa kwa Kamati hizi. Kutokana na umuhimu wa Kamati hizi na hasa ikizingatiwa kwamba zoezi hili limechukua muda mrefu kukamilika, je, ni lini Kamati hizi zitakamilika kuundwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Alex Ikupa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kuna baadhi ya maeneo ambapo Kamati hizi pamoja na kuundwa hazijawa na utekelezaji mzuri wa ufanyaji kazi. Changamoto hii siyo ya kisheria zaidi, sheria imeelekeza ziundwe na tayari zimekwishaundwa, changamoto iko katika eneo la kwanza ni elimu kwa wahusika wenyewe walio kwenye Kamati, lakini sehemu kubwa ni uwajibikaji wa wale ambao wamechaguliwa kuzihudumia Kamati hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la tatu ni usimamizi wa Kamati zenyewe. Jambo hili naomba nitumie Bunge lako Tukufu kwa niaba ya Waziri Mkuu kuwaomba na kuwaelekeza pia Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala, pamoja na Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya na Makatibu Tawala wa Wilaya waweze kusaidia na kusimamia utekelezaji wa sheria hii ili kuweza kuhakikisha inaleta ufanisi kama jinsi ilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la nyongeza ameuliza kuhusu utekelezaji, kwamba lini tutakuwa tumekamilisha zoezi hili. Nieleze tu kwamba Serikali tunaendelea kufanya ufuatiliaji wa karibu kuweza kuhakikisha Kamati hizi zinafanya kazi effectively na wale ambao hawajaunda kupitia Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya wahakikishe kwamba Kamati hizo zinaundwa na ufanisi upatikane.

Mheshimiwa Naibu Spika, itambulike kwamba suala la kutekeleza Sheria Na.9 ya Mwaka 2010 ya Watu Wenye Ulemavu sio suala la hiari, ni suala kisheria na ni la haki za binadamu.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, nini mkakati wa Serikali kuboresha na kuhimarisha umwagiliaji wa Agricultural Seed Agency (ASA) na hasa ikizingatiwa kwamba msimu wa kilimo uliopita wakulima walipata hasara kubwa kwani maji yalikuwa hayafiki kwenye mashamba yao?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella Ikupa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika ni kweli tunayo mashamba kumi na saba yaliyo chini ya Wakala wa Mbegu Tanzania na hivi sasa baada ya kuongezewa bajeti katika eneo hili kutoka shilingi bilioni 10.5 mpaka shilingi bilioni 43 hivi sasa tunaweka mifumo ya umwagiliaji katika mashamba yetu na tumeanza katika Shamba la Nsimba pale Kilosa ambako tunajenga centre na lateral pivot kwa ajili ya kuhakikisha kwamba ASA anakuwa na uwezo wa kumwagilia mbegu katika mashamba yake mwaka mzima pasipo kutegemea mvua.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa fursa; nini mkakati wa Serikali kutoa kipaumbele kwa vijana wenye ulemavu wenye sifa kwenye mradi huu wa uvuvi wa vizimba? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Stella Ikupa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango na katika mipango yetu tumewapa vipaumbele watu wote wenye ulemavu na katika elimu ambayo tunaitoa sasa hivi moja wapo ya kigezo ni kuwa na wavuvi ambao wanatokana na watu wenye mahitaji maalum, ahsante sana. (Makofi)
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hatua zote za uanzishwaji wa mfuko huu zilikwisha kamilika, ninaomba kufahamu tathmini iliyoelezwa kwenye jibu la msingi itakamilika lini.

Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu wa mfuko huu kwa watu wenye ulemavu, Serikali inaonaje ikauacha mfuko huu ujitegemee kuliko kuuunganisha na mifuko mingine? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tathmini inayofanyika kwa sasa lilikuwa ni suala tu la kibajeti na kwa mwaka huu wa fedha tunakwenda kulikamilisha hilo kwa sababu tayari mipango yote imekwisha kukamilika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la mfuko kutokuunganishwa na mifuko mingine. Ni kweli lakini pamoja na hilo tunatambua kundi hili ni muhimu sana na ni kundi ambalo ni maalum. Kwa umaalum wake tumekwisha kuona katika eneo la tathmini ni pamoja na kutambua kwanza vyanzo vya mapato na sera na sheria ambazo zitaongoza mfuko husika.

Mheshimiwa Spika, tatu, ni usimamizi wa fedha hizo, na nne, ni jinsi gani ambavyo fedha hizi zinazopatikana, zipo zitakazopatikana kutokana na ruzuku ya Serikali, lakini kwa sababu ya umaalum wake, zipo fedha ambazo zitatokana na wadau ndiko huko kunakopeleka umuhimu wa baadhi ya mifuko kusimama yenyewe kwa sababu msingi wa mfuko huu unaanzishwa na Sheria Na. 9 ya mwaka 2010 ambayo inataka uwepo wa mfuko huu. Kwa hiyo, kuna mifuko ambayo baada ya tathmini haitakuwa imeungwanishwa pamoja.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya tathmini tutakuwa tumepata picha kamili ya namna ya kuongoza mfuko huu ili uweze kuleta tija na faida zaidi kwa ndugu zetu watu wenye ulemavu, ahsante.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, ninaishukuru na kuipongeza Serikali kwa hatua hii kubwa na muhimu iliyofikiwa kama ambavyo imeelezwa kwenye jibu la msingi. Kwa sababu haya yalikuwa ni maombi na mapendezo ya muda mrefu na mara kwa mara kupitia Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Spika, ninaomba niishauri Serikali, mapendekezo yaliyoelezwa kwenye jibu la msingi yaweze kuzingatiwa ili kwa siku za usoni lugha ya alama iweze kuwa lugha ya kufundishia na mawasiliano katika nchi yetu ya Tanzania. Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ndiyo, ushauri huo Serikali imepokea.
MHE. STELLA A. IKUPA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, ili kuendelea kutokemeza malaria nchini, pamoja na majibu mazuri yaliyotolewa hapa, Serikali inaonaje ikajielekeza pia kutuhamasisha sisi wananchi kufanya fumigation kwenye makazi yetu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza swali lake hilo liko straight, kwanza nimuombe awe balozi wa kwanza na niwaombe Wabunge mliopo hapa mtusaidie kuhamasisha na tunalichukua kama alivyolisema, tunaenda kutekeleza. (Makofi)
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Hivi karibuni Serikali imetangaza uwepo wa Mvua za El nino. Ni upi mkakati wa haraka wa Serikali kupunguza athari zitakazotokana na mvua hizi ndani ya Jiji la Dar es Salaam na hasa mafuriko ambayo yanasababishwa na Mto Msimbazi?

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba kipindi cha mvua kubwa mara nyingi kunakuwa na mafuriko makubwa ambayo yanasababisha athari hasa kwenye makazi ya wananchi. Wakati mwingine inafika hatua mafuriko yanagharimu maisha ya wananchi. Namwambia Mheshimiwa kwamba huwa tunachukua hatua nyingi. Moja, ni kuelimisha wananchi; kwa mfano sasa hivi tumeanza kutoa elimu kuhusu Mvua za El nino ambazo zinategemea kuja. Tunawaambia wananchi wasijenge kwenye maeneo au karibu na maeneo ambayo yanajaa maji ili kama wana mpango huo waanze kuondoka mapema ili zitakapokuja mvua wasiweze kupata mafuriko hayo ama mafuriko hayo kuleta athari kwa wananchi. (Makofi)
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, Mheshimiwa Kisangi angependa kufahamu ni kwa kiasi gani wananchi kwenye maeneo tajwa wananufaika na uwepo wa madini haya kwa maana ya CSR?
NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Stella Ikupa kwa swali lake zuri, kwa sababu manufaa ya wanaokaa katika maeneo yanayochimbwa madini, yako ya aina mbalimbali. Kwa upande wa Serikali kodi zinazokusanywa kutokana na hiyo mirabaha pamoja na ada za ukaguzi zinaingia kwenye Mfuko Mkuu wa Taifa na kuingia kwenye bajeti ambayo kila mwaka Mama Samia anapitisha na miradi mbalimbali ya maendeleo kama barabara, zahanati na shule zinapata fedha hizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa upande wa wawekezaji wenyewe au wenye leseni huwa wanatoa michango kwenye miradi mbalimbali ya jamii katika maeneo hayo, sambamba na kutoa ajira katika maeneo ya migodi. Hivyo, manufaa yapo mengi katika mtizamo huo. Pia wale wanaojiongeza, wanafanya huduma za kuwahudumia wenye migodi kama akina mamalishe wanavyokwenda kupika pale na kutoa huduma mbalimbali.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, wakati tunasubiri mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, Serikali inatumia utaratibu gani kuwapatia matibabu watu wenye ulemavu wasiokuwa na uwezo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kuna utaratibu wa kutoa matibabu bure kwa watu wasio na uwezo wa kujilipia. Kwenye eneo lake la kata yake, akishapata barua ya Katibu Kata akienda hospitali na kuna watu wa Maendeleo ya Jamii kwenye kila hospitali yetu, ambao wanashughulikia mambo hayo na wanaweza kumsaidia na akapata huduma bure kama hana uwezo wa kujilipia.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Serikali imetoa wito kwamba Wabunge tutoe elimu. Mimi kama Mbunge wa kundi hili, nimetoa elimu sana na kundi hili limekuwa likiitikia, lakini Halmashauri na Manispaa huwa hazitekelezi mwongozo huu na kanuni ambayo imeelezwa kwenye jibu la msingi: Nini kauli ya Serikali kwa Halmashauri na Manispaa zetu nchini? Kwa sababu kama mwongozo upo na kanuni zipo, kwa nini halitekelezeki? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, natambua kwamba huenda kukawa kuna mabadiliko ya jinsi ya utolewaji wa mikopo hii. Niendelee kuiomba Serikali kwamba kwa kundi hili la watu wenye ulemavu, iendelee kufikiria kukopesheka mtu mmoja mmoja, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Ikupa kwa maana amekuwa champion hasa katika mabadiliko ya kanuni hizi za kuwezesha walemavu kuweza kupata mkopo kwa mtu mmoja mmoja.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake kuhusu kwa nini kanuni hizi hazitekelezeki, nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kuwaelekeza Wakurugenzi wote wa Halmashauri nchini, kutekeleza mabadiliko haya ya sheria na kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata mkopo kwa mtu mmoja mmoja. Pia kama Mheshimiwa Ikupa alivyosema kwenye ushauri wake, katika mapitio mapya ambayo yanafanyika kwa maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tutaweka kipaumbele kwenye kundi hili la walemavu vilevile kuweza kuendelea kupata mkopo mtu mmoja mmoja.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini kwa uhalisia hawa Maafisa Ustawi wanakua hawapo kwenye hivi vivuko wakati watu hawa wanatumia huduma hii. Nini kauli ya Serikali kwa vivuko vyote nchini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa suala hili halijatamkwa wazi kwenye Sheria ya Leseni za Usafirishaji Nchini. Nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba suala hili linatamkwa wazi kwenye Sheria hii ya Leseni za Usafirishaji Nchini? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, ni kweli kwamba hatuwaweki watu wa ustawi wa jamii kwenye vivuko lakini tunachotaka wafanye ni kwamba waende kwenye ofisi za Wakuu wa Wilaya pamoja na ofisi za ustawi wa jamii ambapo wanapewa barua ama vibali kwamba waweze kusaidiwa kwa sababu hawana uwezo hivyo waweze kuvuka kwenye vivuko ama kutumia kwenye vivuko kwa kupunguziwa ama bila kulipa, ndiyo maana tumesema Waheshimiwa Wabunge waendelee pamoja na Wakuu wa Wilaya na watu wa ustawi kuwafahamisha watu wenye ulemavu ama mahitaji maalum kwenda kabla hajaanza safari basi apate kile kibali ama barua ambayo atakapofika kwenye kivuko husika hatabughudhiwa na hilo limekuwa likifanyika.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la kutamka kisheria, kulipa ama kutolipa kwa watu wenye ulemavu linategemea na uwezo. Watu Wenye Ulemavu, kuna ulemavu wa aina mbalimbali, wako wenye ulemavu ambao kimsingi wana uwezo nadhani hapa tunachoongela kupunguza ama kutolipa ni wale kabisa ambao wamethibitika hawana uwezo na ndiyo maana pengine wanatakiwa waende kwenye ofisi husika ambao watasema kweli huyu hana uwezo kwa hiyo hastahili kulipa, lakini wale wenye uwezo nadhana ndiyo maana sheria haikutungwa ili waweze kulipa.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo kama kutakuwa na umuhimu nadhani tunazo sekta mbalimbali ambazo zinashughulikia hawa Watu Wenye Ulemavu labda sasa litachukuliwa na Serikali liangaliwe kama kuna haja ya kulitungia sheria. Ahsante. (Makofi)
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa fursa.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wanafunzi wenye ulemavu ambao wanafanikiwa kufika hatua hii ya elimu ya juu ni ndogo sana yaani idadi ya wanafunzi ambao wanafanikiwa kufika hatua hii ya eleimu ya juu ni ndogo sana, na kwa kuwa kundi hili linakabiliwa na changamoto nyingi za kimaisha.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa mikopo hii ya elimu ya juu kama ruzuku kwa kundi hili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stella Ikupa Alex, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba miongoni mwa vigezo au sifa za upataji wa mikopo, mojawapo ni kwa wenzetu wenye mahitaji maalum wakiwepo watu wenye ulemavu. Kwa hiyo, kwanza tumeanza na kipaumbele kwa hawa, lakini tunatoa kama mikopo.

Mheshimiwa Spika, swali la Mheshimiwa Mbunge yeye anataka tufanye kama ruzuku, naomba tulichukue pendekezo lake hili au ushauri wake huu twende tukaufanyie kazi, tufanye tathmini ya wangapi hawa watu wenye ulemavu, na tuweze kuangalia namna bora ya kufanya, kama tulivyofanya kwenye Samia Scholarship, Mheshimiwa Rais alitoa fedha hizi zaidi ya shilingi bilioni tatu kwa ajili ya watoto waliofanya vizuri. Nadhani na hili la watoto wenye ulemavu linawezekana, nakushukuru.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, Mheshimiwa Mariam Kisangi ana maswali mawili ya nyongeza.

Swali lake la kwanza linasema; ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam kumekuwa kuna ucheleweshwaji wa upatikanaji wa kadi za bima za afya yaani toka tarehe mtu analipia mpaka kuja kuipata ile kadi inaweza kuchukua hata miezi sita. Nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba kadi hizi zinapatikana kwa wakati? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili; linasema kumekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa wa figo wagonjwa ambao wanahitaji huduma ya kuzisafisha hizi. Nini kauli ya Serikali kuruhusu wagonjwa hawa kuwa na Bima za Afya hata kama ni zile za vifurushi vikubwa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, labda nijibu maswali yake mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja; ni ucheleweshaji wa bima ya afya ukilipia; ni ukweli kwamba umewekwa utaratibu kwamba toka unapolipia basi upate bima yako baada ya miezi mitatu na lengo lilikuwa ni moja tu kwamba watu wengi wakiwa na afya, wakiwa salama, wanakuwa hawana tabia ya kujiunga na bima watu wakadhani kwamba ni vizuri mtu akajiunga wakati hana ugonjwa wowote ili kulinda mfuko huo.

Lakini hili la miezi sita kwakweli nilakushughulikia kwamba tulishughulikie mapema ili watu wapate ndani ya muda uliopo. Lakini sasa wakati muswada unakuja hapa ambao sisi Wabunge ndiyo tutakaojadili basi tujadili tuone tunatakiwa upate kwa wakati gani na tutaweka utaratibu mzuri ambao hautaleta matatizo ambayo sasa mnayaona.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu wenzetu wenye matatizo ya figo; moja ni kwamba sisi wote tushirikiane kwa sababu suala moja ni kuhakikisha kwamba watu hawafiki mahali wanapata matatizo hayo ya figo, lakini ikitokea sasa wamepata basi kwa kweli Serikali inajitahidi.

Moja; ilikuwa kufanya dialysis kwa mara moja ni shilingi 380,000 lakini sasa hivi imeshuka mpaka shilingi 120,000 lakini bado ni gharama kubwa. Tutaendelea kuona namna ya kufanya ili hao watu wapungukiwe na mzigo kwa sababu kwanza wengi hawana uwezo wa kufanyakazi na wengine hawana kazi. (Makofi)
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012 tuna idadi ya watu wenye ualbino wapatao 16,000 lakini kutokana na jibu la Serikali inaonesha kwamba watu wenye ualbino ambao wamenufaika na mafuta haya ni 3,389 kwa kipindi cha mwaka 2020 hadi 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tukumbuke kwamba Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI alishatoa maelekezo kwa Halmashauri hizi kwamba zihakikishe zinanunua na kugawa mafuta haya ya watu wenye ualbino.

Nini kauli ya Serikali kwa Halmashauri ambazo hazitatekeleza takwa hili, na hasa ikizingatiwa kwamba maelekezo yameshatolewa mara nyingi, lakini pia miongozo ipo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili la nyongeza; kwa kuwa sasa hivi tunakwenda kuwa na zoezi hili la sensa, hivyo tunategemea kwamba tutapata idadi halisi ya watu wenye ulemavu, aina za ulemavu na mahali wanapopatikana ama mahali walipo.

Serikali inaonaje sasa ikianza kuyanunua mafuta haya ikawa inayashusha moja kwa moja kwenye vituo vya afya na zahanati, tofauti na utaratibu uliopo sasa ambapo mafuta haya kwa maeneo ambayo yalikuwa yakinunuliwa yalikuwa yakipatikana kwenye Hospitali za Mikoa na Wilaya? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Alex Ikupa, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Stella Ikupa amekuwa mstari wa mbele sana kuhakikisha anawasemea watu wenye ulemavu wakiwemo wenye ulemavu wa ngozi na Serikali ya Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, inawajali na kuwathamini sana watu wote wenye ulemavu na ndiyo maana katika mipango yetu tumekubaliana kwamba kwanza ni maelekezo ya Serikali kwamba Halmashauri zetu zote zinapotenga fedha kwa ajili ya dawa lazima zitenge fedha kwa ajili ya mafuta haya kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba kurudia tena kauli hiyo ya Serikali ambayo ilikwishatolewa kwamba Halmashauri zote zihakikishe zinatenga fedha, miongoni mwa bajeti ya dawa lazima mafuta haya ya watu wenye ualbino yaweze kuwepo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari kwenye bajeti ya mwaka 2022/2023 Halmashauri zote zimefanya utambuzi na kufanya maoteo ya mahitaji ya mafuta hayo na katika mwaka huu tutakuwa na mafuta hayo kwa kiasi kikubwa zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, kuhusiana na kusogeza huduma hizi karibu zaidi na watu wenye ulemavu, ni kweli tutakuwa na Sensa ya Watu na Makazi tarehe 23 Agosti, 2022. Niwaombe watu wote wenye ulemavu, pamoja na Watanzania wote, tujitokeze wote ili tuhesabiwe, na hii itasaidia sana Serikali kuwatambua watu wenye ulemavu na kujua mahali walipo na mafuta haya sasa yatasogezwa kwenye vituo vile kwa idadi kulingana na watu wenye ulemavu walipo katika maeneo hayo, ahsante.