Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Dr. Elly Marko Macha (1 total)

MHE. DKT. ELLY M. MACHA: Mheshimiwa Spika, swali moja dogo la nyongeza. Mheshimiwa Waziri Mkuu ahsante kwa majibu yako mazuri. Nafikiri huo mkataba una tija ndiyo maana Serikali yetu ulisharidhia. Naomba kuuliza, ni lini sasa hiyo ripoti itaandikwa na kupelekwa kwenye ile Committee?
Mbunge, kwa kuwa sasa tuna Waziri mwenye dhamana na anayeshugulikia jambo hili au watu wenye mahitaji maalum na ameshaanza kazi ya kupitia shughuli mbalimbali na mahitaji yao na kuingiza kwenye mipango; na kwa kuwa pia mmesharidhia hata kwenye bajeti yetu, basi wakati wowote na wewe ukiwa
mmoja kati ya Wabunge hapa na Mheshimiwa Waziri yupo hapa, tunaamini unaweza kuwa mshiriki wa kwanza kati ya washiriki ambao tunataka tuwaingize kwenye orodha ya watakaokuwa wanafanya mapitio haya ili tuweze kuona kama jambo hilo sasa litakamilika wakati gani.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ni wakati wowote kuanzia sasa. Kwa kuwa Mheshimiwa Dkt. Possi yupo, mtashirikiana naye katika hili na amelisikia, nimtake tu sasa aanze mchakato huo mara moja kuwakusanya wadau wote ili tuanze kupitia mahitaji yale ili yaweze kutekelezwa katika kusaini mikataba yetu kama ambavyo tumekubaliana.