Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. Dr. Elly Marko Macha (1 total)

MHE. TASKA R MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante naomba kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa matatizo ya Mkoa wa Geita yanafanana na matizo ya Mkoa wa Katavi. Mkoa wetu wa Katavi hauna Hospitali ya Mkoa na hauna pia Hospitali ya Rufaa.
Je, ni lini sasa Serikali itamaliza ujenzi wa Hospitali ya Mkoa wa Katavi na kuleta Madaktari Bingwa wa magonjwa mbalimbali kama upasuaji wa macho, meno kwa sababu siku nyingine watu wanavimba ufizi wanashindwa kupasua? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri Mkoa wa Katavi nimeutembelea ikiwa ni sehemu ya Mikoa 12 ambayo nimetembelea ndani ya miezi minne tangu nimeteuliwa kuwa Naibu Waziri. Nimeiona changamoto hiyo katika Mkoa wa Katavi, lakini kama nilivyojibu katika swala langu la msingi ni kwamba sasa hivi Serikali imechukua majukumu ya kuendesha Hospitali za Rufaa za Mikoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ninachokuomba Mheshimiwa Taska Mbogo na Wabunge wengine wa Mkoa wa Katavi ni kuendelea kuihimiza Serikali yetu ya Mkoa kuhakikisha kwamba wanatenga eneo na kuanza maandalizi ya awali na sisi kama Serikali tutaendelea kujipanga kuhakikisha kwamba tunajenga Hospitali ya Rufaa ya Katavi.