Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Anna Richard Lupembe (35 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, wale watu ambao walikuwa hawalipi kodi, lakini Mheshimiwa Rais wetu amethubutu kufanya kazi hiyo na matokeo yameonekana na kodi sasa zimeonekana mpaka hatimaye sasa watoto wetu wameweza kwenda kusoma bure
kwa sababu ya mambo mazuri ambayo Rais wetu alituahidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa ni kazi, mimi nitaendelea. Kuna kazi ambayo tunatakiwa tuifanye na Serikali inatakiwa iangalie kwa makini kuhusu Halmashauri zetu upande wa Wakurugenzi pamoja na Watendaji. Kuna sehemu nyingine watendaji
wanakaimu na kama Mkurugenzi mara nyingi anakaimu siyo Mkurugenzi kamili inakuwa kazi kufanya kazi ya maendeleo katika maeneo husika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, unakuta sehemu nyingi kuna miradi mbalimbali ambayo Serikali iliainisha ili iweze kufanyika. Katika maeneo mengi miradi hiyo haikuweza kukamilika kutokana na utendaji. Ukienda pale anasema mimi Kaimu, Mkurugenzi kasafiri siwezi kufanya
jambo lolote. Hilo limekwamisha sana miradi yetu tuliyokuwa nayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kazi inaendelea, kuna Wakurugenzi wengi wamesimamishwa kutokana na majipu, lakini bado kuna maeneo mengi ambayo uaminifu ni mdogo. Naomba kazi hiyo iendelee, tuweze kusafisha ili fedha za maendeleo tukipanga bajeti
ziweze kufikia malengo yale tunayoyatarajia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende upande wa wakulima na wafugaji. Kifike kipindi sasa Serikali, iainishe maeneo ya wakulima na wahainishe maeneo ya wafugaji.
Limekuwa tatizo kubwa sana kiasi ambacho sasa hivi kuna vitu ambavyo vinaashiria siyo vizuri, wanapigana, wanauana na sisi nchi yetu ni nchi ya amani na utulivu. Naomba Serikali yetu ijipange vizuri kwa ajili ya eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Waziri wa Ardhi, ametuandikia barua Wabunge wengi tuainishe migogoro ya ardhi. Naomba nikupongeze sana Waziri wa Ardhi kwa kuliona hilo, tuweze kukusaidia na tuainishe maeneo yote yenye migogoro.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakwenda kwenye reli, watu wengi wamezungumza kuhusu masuala ya reli. Kwangu Mpanda ni kitu muhimu sana kutokana na na hali halisi ya sasa hivi barabara zote hazifai, wananchi wa Mpanda wako hewani, mambo yao hayaendi vizuri.
Namwomba Mheshimiwa Waziri reli hii ya Mpanda hata kesho treni ianze kwenda kwa sababu wananchi wa Mpanda wanapata shida, taabu kwa ajili ya mahitaji yao binafsi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja kwenye masuala ya uchumi, uchumi hauwezi kukua bila miundombinu. Maeneo ya Tabora, Kigoma, Mpanda ni maeneo ambayo yana uchumi mkubwa, wanalima sana, wana mazao mengi, ambayo yanatakiwa yatoke kwa ajili ya
Watanzania wote, lakini kutokana na miundombinu mibaya, barabara hazifai. Mtu anatoka Tabora kwenda Mpanda anatumia siku tatu, analala njiani, kusema kweli tunasikitika sisi Wabunge tunaotoka maeneo hayo kuwa tumesahaulika muda mrefu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali, mtuangalie kwa jicho la huruma wale wananchi ni Watanzania kama Watanzania wengine, wanahitaji mahitaji muhimu. Shughuli zao za kilimo, basi waweze kutoa mazao yao ili waweze kupata mahitaji yao binafsi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja upande wa polisi, nawapongeza sana polisi wetu, wamefanya kazi nzuri, lakini kuna maeneo mengi nyeti hakuna vituo vya polisi, wananchi usalama wao unakuwa mdogo, maeneo mengi utakuta wana mazao mengi, lakini usalama
wao haupo kutokana na kukosekana kwa kituo cha polisi katika maeneo hayo. Tunaomba Serikali ijipange basi kupeleka vituo vya polisi katika maeneo hayo ili wananchi waweze kupata usalama wao.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende kwenye mapato tena. Zamani kulikuwa kuna Shirika lilikuwa linaitwa NASACO, Shirika la NASACO lilikuwa linakusanya mapato bandarini, ile mizigo yote inayotoka kwenye meli, lile shirika sasa hivi halipo. Sasa naomba kama kuna
uwezekano Serikalini, lile lilikuwa linasaidia sana mapato yalikuwa hayawezi kupotea ndani ya bandari zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba basi Serikali ijipangwe vizuri, kuona ni jinsi gani ya kuweza kupitisha makontena ndani ya bandari zetu, maana kuna maeneo mengine hakuna usalama mzuri, watu wanaingiza mizigo bila kulipa ushuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshuhudia Tanga, bandari bubu nyingi, lakini na Mpanda, Kalema kuna bandari, mpaka leo hatuwezi kujua hatima yake itaisha vipi. Kuna sehemu nyingi muhimu, nyeti ambazo zinaweza kuliletea Taifa hili mapato, lakini tumeliacha wazi. Tunaomba
basi na sisi bandari ile ya Kalema ifanyiwe kazi, ina miaka sijui sita sasa hivi, majengo yalianza, Mkandarasi sijui ka-disappear wapi hatufahamu. Tunaomba basi ili uchumi uweze kukua, bandari, reli na barabara ziweze kutengenezwa vizuri kwa kiwango cha lami. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi Serikali ijipange, mnapoteza hela nyingi…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa muda wako umekwisha, tafadhali naomba ukae
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa ninaombanimshukuru Mungu aliyetupa uzima na uhai tumeweza kufika kwenye Bunge hili ambalo ametupa kibali yeye. Hatukuja kwa uwezo wetu tumekuja kwa uwezo wa Mungu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa ambayo anaifanya kuwatumikia Watanzania, tunaona jitihada zake ni nzuri mno kupita kiasi maana yake bajeti hii ni ya kupongeza tu kwa sababu kazi kubwa inafanyika na tunaona jinsi Serikali inavyowatumikia Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba nimpongeze sana Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoifanya katika nchi yetu. Vile vile naomba nimpongeze Mheshimiwa Jenista Mhagama kwa kazi kubwa anayoifanya. Tunaiona kazi yake, juzi alikuwa Geita kwenye Mwenge, tumekuona dada yetu mpendwa umefanya kazi nzuri sana. Pia niwapongeze Naibu Mawaziri kwa kazi kubwa wanayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa najua ajira ni shida sana, lakini naiomba Serikali yangu sikivu najua mpaka sasa hivi kweli kuna watendaji ambao walikuwa darasa la saba lakini watendaji hawa wametufanyia kazi kubwa sana Watendaji wa Vijiji, Watendaji wa Kata wamefanya kazi kubwa wemetujengea shule, wametujengea dispensary na vituo vya afya. Tunaomba watendaji hawa warudishwe kazini wasubiriwe muda ambao wataweza kustaafu ili waweze kupata haki zao. Najua Serikali yangu sikivu mmesikia mnaweza kutenda kitendo hicho ili hawa watu waweze kurudi makazini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipongeze tena kwa ndege ambayo imefika tumeona uzinduzi wake. Nasi Mkoa wetu wa Katavi tuna uwanja mkubwa sana wala hatuombi uwanja leo. Sisi tayari tuna uwanja, lakini hauna ndege. Hivyo, tunaomba sasa kwa sababu kuna ndege
nyingine imefika mpya na sisi sasa Serikali mtupangie ratiba ili na sisi wananchi wa Katavi sasa tuweze kufaidi matunda ya Serikali ya Awamu ya Tano, kwa sababu jitihada ni kubwa tunaziona kwa macho na wananchi wa Katavi wana maeneo ambayo watajivunia kwa sababu wana eneo kubwa sana la utalii, tuna Mbuga ya Katavi, sasa watalii wataweza kufika Katavi kwa urahisi kwa sababu uwanja wa ndege tunao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Serikali yangu kwa route zitakazopangwa sasa hivi ya ndege hii mpya, basi na Katavi mtuangalie kwa jicho la huruma ili na sasa na sisi tuweze kupata watalii na Serikali yetu iweze kuingiza mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua ndani ya nchi yetu kuna mikoa ambayo tuliongeza Katavi, Njombe, Geita pamoja na Simiyu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakuu wa Mikoa mpaka leo hawajapata makazi, hawajengewa nyumba za kuishi pamoja na Ofisi zao. Kwa mfano, ndani ya Mkoa wetu wa Katavi Mkuu wa Mkoa mpaka leo anatumia jengo la Halmashauri ya Manispaa. Naomba basi sasa hivi tupange mikakati mizuri tuweze kuwajengea ofisi kwa sababu Mkuu wa Mkoa anahitajika apate ofisi yake ili aweze kufanya kazi vizuri. Vilevile akipata makazi atakaa vizuri sana na akafanya kazi vizuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana tuangalie Mkoa wa Katavi kwa sababu hana nyumba wala hana ofisi na siyo vizuri hawa watu kuhangaika hangaika, wanatakiwa wapate sehemu ya kukaa mahali pazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mawasiliano, naomba niipongeze sana Serikali kwa jitihada ya kuweka mawasiliano katika maeneo mengi. Mkoa wa Katavi bado kuna maeneo mawasiliano hayajafika kabisa na mazingira yetu Mkoa wa Katavi ni magumu. Ukiangalia kama Kata ya Ilunde. Ilunde jiografia yake ni ngumu sana, vilevile Ilunde kuna biashara nyingi ambazo zinafanyika maeneo yale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali yangu iangalie basi Kata ya Ilunde iipeleke mawasiliano, wakipata Kata ya Ilunde na kuna Kata jirani inaitwa Kata ya Ilela, Kata ya Ilela nayo watapata mawasiliano kwa urahisi. Naomba sana maeneo haya ni maeneo ya biashara wanalima karanga, wanavuna asali, kuna vitu vingi vinavyofanyika maeneo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna maeneo mengine ya Utende, kuna maeneo mengine Wilaya ya Tanganyika, maeneo ya Sibwesa, kuna biashara, wanalima mpunga na wanafanya shughuli nyingi za kijamii ambazo zinaingiza mapato ndani ya Serikali yetu. Naomba katika maeneo haya mtandao uweze kufika, kwa sababu mtandao sasa hivi ni maisha, kwa sababu mtandao ukipiga simu biashara kila kitu kinakuja kwa wepesi zaidi.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika maeneo ya Ilela pamoja na Ilunde wanatamani sana na wenyewe wapate TBC Radio, hakuna usikivu wa radio yetu ya Serikali. Wanatamani sana waweze kusikia matangazo ya TBC. Naomba sana upande wa radio basi tupate mawasiliano hayo ili nasi tusikie matangazo ya Kitaifa, Kimataifa pamoja na Watanzania wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba niipongeze Mifuko ya jamii PPF, LAPF pamoja na NSSF. Wamekuwa miongoni mwa jamii kwa asilimia kubwa sana. Wanasaidia sana maendeleo ndani ya jamii zetu, vilevile kusaidia jinsi gani wananchi wanavyofanya kazi zao na wenyewe wanawasaidia kupitia maombi ambayo yanafika katika maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona kabisa ni jinsi gani kupitia elimu bure wananchi wengi wamehamasika kupeleka watoto mashuleni. Sasa hivi ndani ya maeneo yetu ndani ya vijiji vyetu na vitongoji vyetu wananchi wengi wamehamasika kujenga majengo, wamehamasika kujenga vitu vingi ambavyo Serikali inaenda kuwahamasisha, unakuta maboma yale yanaishia kwenye lenta.

Mheshimiwa Mwenyekiti,aiomba sana Serikali yetu kupitia Halmashauri zetu yale maboma wananchi walikoyafikisha basi waweze kumaliza kwa sababu watoto wetu wengi sana wanasoma kwenye miti wengine, hatuna vyoo vya kutosha, najua kwa sababu wanafunzi wamekuwa wengi ndani ya madarasa na maeneo yetu, vyoo tulivyovijenga kupitia wananchi vimekuwa havitoshi, basi naomba Serikali yangu sikivu, tuweke mikakati maalum, kwa sababu tumeona jinsi gani sasa hivi Serikali yetu ilivyokumbuka zile shule za Sekondari za zamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wetu wa Elimu. Waziri wa Elimu amesimamia vizuri sana, shule zile kongwe zote zimeboreshwa zimekuwa nzuri sana kusema kweli, lazima tupongeze kwa hili, kwa sababu tumekwenda kwenye shule kongwe tumeona jinsi gani matengenezo yalivyotengezwa, basi tunaomba Serikali kupitia shule za misingi sasa, kwa sababu shule nyingi za misingi zimeharibika mazingira yake siyo rafiki kwa watoto wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri mtoto akikaa kwenye mazingira rafiki atasoma vizuri. Hivyo, naiomba Serikali yangu sasa ichukue jukumu hili, kupitia TAMISEMI tuanze kuboresha shule zetu za msingi pamoja na mazingira yao ya kwenda maeneo nyeti ili watoto wale waweze kusoma vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu umeme, ndani ya Mkoa wetu wa Katavi REA III haijafanyika kabisa kwa sababu Mkandarasi sijui alipelekwa Mahakamani, hakuna kitu chochote kinaweza kufanyika. Sasa wananchi wa Mkoa wa Katavi wanahitaji umeme, maeneo mengi tukipita kwenye Kata zetu hakuna umeme na kuna sehemu zingine ni za biashara, watu wanajishughulisha na mambo mengi, sasa unakuta umeme hakuna.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali yangu sikivu, sasa hivi katika bajeti hii najua bajeti hiyo imeshapita ya wakati ule REA III, lakini bado tuna nafasi ya kuweka tena mikakati mipya ili Mkoa wa Katavi katika yale maeneo yote REA III haijapita, tunaomba iweze kufanyika kwa sababu wananchi wa Mkoa wa Katavi kupitia maeneo mengi wanahitaji nao waweze kupata umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Jeshi la Polisi. Najua Jeshi la Polisi tunalipenda sana wanatulinda usiku na mchana, basi nao tuwawekee vizuri mazingira yao. Unakuta kwenye kituo cha Kata ukienda kuona nyumba ya Askari wetu ni nyumba ya udongo inasikitisha. Naomba basi tujitahidi kuwawekea mazingira mazuri, wanafanya kazi vizuri tuwawekee mazingira mazuri ili waweze kufanya kazi vizuri na kuendeleza amani ndani ya nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga Mkono hoja. Nashukuru kwa barabara inayoanzia Tabora – Mpanda, nashukuru sana na Wakandarasi wako site, hongera sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. ANNA L. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi na naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu aliyetulinda, ametuleta tena mara nyingine hapa Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende moja kwa moja kwenye hoja, naomba nimpongeze Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanazozifanya. Wizara yao ni kubwa sana lakini wanajitahidi sana, wana majukumu mazito, naomba mpambane Mungu atawasaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Katavi sasa hivi una miaka kama minne inaelekea mitano, hatuna Hospitali ya Mkoa. Tumeambiwa tumetengewa pesa tujengewe Hospitali ya Mkoa wa Katavi lakini mpaka leo hatuoni jitihada ya aina yoyote. Sasa hivi Mkoa wa Katavi una watu wengi, ukishasema mkoa ina maana umepanua wigo mkubwa kwa hiyo, shughuli mbalimbali zinafanywa ndani ya Mkoa wa Katavi lakini hatuna Hospitali ya Mkoa, tumebaki na Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ambayo ndiyo imebeba majukumu yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya Wilaya ya Mpanda ni ndogo na wafanyakazi ni wachache, nashukuru na wao wenyewe wamejionea. Wameainisha hapa kwenye hotuba ndani ya Mkoa wetu wa Katavi ukiangalia Wilaya ya Mpanda Vijijini, Mpanda Mjini na Wilaya mpya ya Mlele kuna sehemu wamesema asilimia 100 hakuna wahudumu. Sasa sijui wananchi wa Mkoa wetu wa Katavi wanaoumwa wanafanyaje. Naomba Mheshimiwa Waziri uliangalie kwa makini sana suala hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wengi wamekukaribisha uende kwenye Mikoa yao, naomba Mheshimiwa Waziri uje Katavi ujionee mwenyewe hali halisi ya Mkoa wetu na jinsi wananchi wanavyopata shida ya matibabu. Hospitali ile ya Wilaya, manesi pamoja na madaktari saa nyingine wanachoka, wakichoka sasa lugha zinakuwa tofauti. Wagonjwa wakienda pale kauli zinakuwa tofauti, zinakuwa mbaya kwa sababu si wao, wamechoka. Naomba Mheshimiwa Waziri muangalie kutupatia Hospitali ya Mkoa wa Katavi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mlele ina hospitali ambayo imejengwa na Serikali. Naomba niipongeze Serikali imejenga hospitali nzuri sana Inyonga lakini mpaka leo ni kituo cha afya. Mmeweka vifaa vingi na vizuri lakini kasoro yake ni ndogo sana, ni choo tu hakuna ndiyo imefanya hamtaki kuipandisha iwe Hospitali ya Wilaya ina maana Wilaya ya Mlele hakuna Hospitali ya Wilaya. Mheshimiwa Waziri tunaomba tupandishie hii hospitali na tuletee wafanyakazi. Vile vifaa mlivyoleta vimekaa sasa vimeanza kuharibika kwa sababu hakuna wataalam wa kuvitumia. Sasa inakuwa tunachezea hela za Serikali kututangulizia vitu wakati wahudumu na wataalam hakuna. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii hospitali ambayo iko Inyonga imejengwa vizuri sana lakini tatizo lake ni choo tu. Mmejenga majengo makubwa, mazuri, lakini sijui ilikuwaje huyo mkandarasi aliyewekwa hakuweka choo mpaka leo hii tunashangaa ilikuwaje. Kila mtu anashangaa kwa sababu tunaomba muipandishe hadhi inashindikana, ukiuliza tatizo unaambiwa hamna choo. Sasa sijui katika utaalam ilikuwaje, mmejenga majengo mazuri, mmeleta vifaa vikubwa na vizuri halafu choo hakipo halafu hamtaki kutoa kibali ili iwe Hospitali ya Wilaya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa unyenyekevu mkubwa naomba mtusaidie kwani wananchi kule wanapata shida, jiografia yetu ya Mkoa wa Katavi jamani ni ngumu, naomba chonde chonde mtusaidie. Ukienda kule Mheshimwa Waziri utasikitika wananchi wanavyohangaika huduma hamna. Naomba Mheshimiwa Waziri ile hospitali hata kama haina vyoo tupandishieni iwe na hadhi ya Hospitali ya Wilaya ili wananchi wa Wilaya ya Mlele wapate huduma safi na salama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja upande wa Chuo chetu cha Msaginya. Tuna chuo pale kinaitwa Msaginya, Chuo cha Maendeleo lakini hakifanyi kazi yoyote. Chuo kile ni kizuri, mnakitolea pesa kila mwaka, lakini kwa nini hamna mipango mizuri mkapeleka watu wakajifunza pale? Kuna vijana wengi ambao wamekaa bure hawana kitu chochote cha kufanya wangeenda huko. Vyuo mmevijenga vizuri, wataalam mmewaweka kwa nini vijana wasiende pale wakajifunza useremala na akina mama wakaenda pale wakajifunza ujasiriamali? Vile vyuo majengo yanaharibika na mnapoteza hela nyingi.
Naomba hivi Vyuo vya Maendelo ya Jamii viwekewe mikakati mikali ili vijana wengi wajifunze ujasiriamali kupitia Vyuo hivi vya Maendeleo ya Jamii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja upande wa Benki ya Wanawake. Kwanza, naomba nimpongeze Mkurugenzi wa Benki ya Wanawake, Mama Chacha, amefanya kazi nzuri lakini bado hajatufikia sisi akina mama kwenye Mikoa, Wilaya na Vijiji vyetu, ameishia Dar es Salaam na asilimia kubwa ya akina mama wako vijijini. Najua watu wengi wamesema hii benki haiwezekani lakini wanawake wote wana haki ya kupata benki hii kila mkoa kwa sababu hela iliyochukuliwa kuianzisha ni Serikali. Kwa hiyo, kila mkoa tunahitaji Benki ya Wanawake ili wanawake wa Tanzania hii wajivunie benki yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda sasa kuzungumzia Bima ya Afya, hii mimi naisemea kila siku. Bima ya Afya dawa hakuna! Tunaomba sasa Bohari Kuu waende moja kwa moja viwandani kuchukua dawa. Kama dawa ziko huko Ujerumani, India waende moja kwa moja wakachukue dawa huko ili waje kuwahudumia Watanzania. Hizi dawa wanazochukua kwa wafanyabiashara hazikidhi mahitaji.
Tunaomba sasa Serikali iwape fungu kubwa Bohari Kuu ya Dawa ili sasa wananchi wote waweze kupata huduma safi na salama wajivunie Serikali yao kupitia Bima ya Afya. Sisi tuko tayari kufanya hamasa, wananchi wote waingie kwenye Mfuko wa Bima ya Afya lakini tunaomba mtuwekee dawa ili wananchi wapate huduma safi na salama. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niunge mkono hoja kwa asilimia mia moja, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ninaomba nimshukuru Mwenyezi Mungu ambaye aliyetuumba, ametupa uzima na uhai, siku hii ya leo ametutunza na tuko Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ninaomba niunge mkono asilimia mia kwa mia bajeti hii iliyopo mbele yetu.
Ninaomba nimpongeze Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya kwa kuwapa imani Watanzania, kwa elimu bure, Watanzania wameona matunda yake, vilevile Watanzania wote wanampongeza jinsi anavyofanya kazi nzuri ya kutumbua majipu, Watanzania wanaona, wanafurahi na jinsi ya kubana matumizi. Zile pesa zinawaendea wenyewe kwa ajili ya matatizo yao na kuwapa shilingi milioni 50 kwa kila kijiji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uchaguzi wa Zanzibar ulikuwa wa haki na uhuru. Jana nilikuwa Zanzibar, kuna amani tosha. Nimepata marashi ya karafuu murua kwa ajili ya Watanzania jinsi tunavyoishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nimpongeze Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Mawaziri wote wanavyofanya kazi vizuri na yaliyokuwa mbele yetu kwa ajili ya Taifa letu, kwa ajili ya kutimiza Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Endeleeni, kazeni buti, mnafanya kazi nzuri ambayo sasa hivi kila mtu anaona jitihada zenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niende upande wa Halmashauri kupitia elimu. Shule zetu zimezeeka sana ambazo ziko upande wa kijijini, zina nyufa, chini sakafu hakuna, ninaomba basi miundombinu hiyo itengenezwe na Halmashauri zetu sasa zifanye mikakati mikubwa na mipango mizuri ya kuboresha shule zetu kila mwaka waweze kujenga madarasa manne au mawili kwa ajili ya uboreshaji wa shule zetu za primary, pamoja na kuanza kujenga kwa kasi kubwa…
TAARIFA...
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, siikubali taarifa yake kwa sababu mimi nilikuwa Zanzibar, nimekaa siku nne, kuna amani na utulivu, na uchaguzi umefanyika kwa haki. Kama kuna mabomu yeye anafanya nini humu ndani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Zanzibar ni tulivu kabisa, hakuna mabomu na Serikali ya Chama cha Mapinduzi ndiyo maana yeye yuko humu ndani, anakula upepo, ina maana kama uchaguzi usingefanyika wa haki yeye asingekuwepo hapa. Demokrasia imechukua mkondo wake, Wazanzibari wamefanya kazi yao nzuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Precision Air inaanza kwenda Pemba, safari ya Dar es Salaam, Unguja - Pemba, naomba nimpe taarifa hiyo, kwa sababu ya amani na utulivu wa nchi hii.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna vijiji vingine havina shule kabisa ya primary, ninaomba Serikali iangalie kupitia Halmashauri zake, vile vijiji ambavyo havina shule za msingi ziweze kujengwa. Pia shule za sekondari, zipo shule za sekondari ambazo hazikujengwa kwa kiwango leo hii ukienda zina ufa, ninaomba zichukuliwe hatua ambazo zitaboresha shule zile pamoja na nyumba za walimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la afya. Tuna Bima ya Afya ambayo tumewahamasisha wananchi wetu ambao Wabunge wengi wamezungumzia. Ninaomba Bima ya Afya ni matatizo makubwa sana kwa wananchi wetu. Wakienda hospitali kwenda kuchukua dawa wanaambiwa dawa hakuna waende kununua dawa. Tunaomba mikakati mizuri ya Bima ya Afya iwekwe vizuri ili wananchi wetu waweze kupata huduma nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vituo vya afya hasa Wilaya ya Mpanda vimekaa vibaya. Ukienda Kituo cha Afya Kalema, Mwese na Mishamo ni distance ndefu mno, hatuna gari hata moja. Ndiyo maana tumepata matatizo makubwa sana, asilimia ya vifo vya wanawake wajawazato mwezi wa nane na mwezi wa tisa, kila mwezi tulikuwa tunapoteza akina mama 40 wanaokufa kutokana na vifo. Tunaomba sana mtuangalie kwa jicho la huruma, mtupe ambulance za kuweza kusaidia akina mama Wilaya ya Mpanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye zahanati unakuta muuguzi mmoja tu, hakuna msaidizi, matokeo yake muuguzi yule akiondoka, maana muuguzi huyo ndiye daktari, ndiye nesi, ndiye mhudumu. Ina maana akitoka akina mama wakienda pale au mgonjwa akiwa serious hatapata huduma kutokana na muuguzi kuchoka, hayupo, amekwenda kunywa chai, matokeo yake tunapata matatizo mengi makubwa ya vifo ambavyo hatukuweza kuvitegemea. Ninaomba tuweke mikakati mizuri, tutengeneze kila Mkoa, tuwe na vyuo ambavyo ni vya kuwa na wahudumu wetu pamoja na manesi, tuibue manesi kila Mkoa ili waweze kusaidia vituo vyetu vya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda zahanati nyingi, watu wengi wamesema, zahanati nyingi, shule nyingi hazina maji safi na salama ni shida. Tunaomba Serikali ijiwekee mikakati mizuri kwa ajili ya maeneo ya zahanati na shule zetu za msingi na shule zetu za sekondari kuwe na maji safi na salama kwa ajili ya watoto wetu. Unakwenda unakuta vyoo hakuna, vyoo vingi vimechakaa, vyoo vingi vimeshaanza kutitia. Tunaomba uboreshaji kwenye shule zetu za primary na sekondari vyoo vijengwe upya ili watoto wetu waweze kuishi kwenye mazingira mazuri na salama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la mazingira. Upande wetu wa Mpanda eneo kubwa ni misitu. Misitu ile imevamiwa na watu, wameingia wanakata miti kama mchwa, mazingira yanaharibika. Tunaomba mikakati mizuri ya Serikali kutunza mazingira kwa ajili ya afya zetu za mvua ili tuweze kupata mahitaji muhimu ndani ya jamii yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakuja upande wa bibi maendeleo. Hatuna mabibi maendeleo ndani ya Wilaya zetu na Kata zetu. Akina mama wanapata shida sana jinsi ya kuweza kufundishwa ujasiriamali na jinsi ya maendeleo kutokana na kutokuwa na mabibi maendeleo, hatuna mabwana shamba kila kata. Tunao mabwana shamba wachache sana. Sasa unakuta akina mama wanaohitaji kufundishwa jinsi gani ya kulima kilimo bora hakuna watalaam ambao wanaweza kuwafundisha. Tunaomba jitihada za Serikali tuongeze mabibi afya, tuongeze mabibi maendeleo, tuongeze mabwanashamba kwa ajili ya huduma nzuri ya wananchi wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la maji. Ndani ya vitongoji vyetu na vijiji vyetu akina mama wanapata shida sana ya maji. Maji wanafuata maeneo ya mbali ambapo wakati mwingine maeneo mengine akina mama wanaamka usiku sana, saa nane za usiku, saa tisa za usiku kwenda kutafuta maji. Ninaomba mikakati ya maji iwe mikubwa na mipana zaidi kwa ajili ya akina mama ambao wanapata shida ya kutafuta maji. Maji yenyewe wanapoenda kuyatafuta ni maji machafu, siyo maji salama. Ninaomba Serikali yangu sikivu iweze kupanga mikakati mizuri ili iweze kupata maji salama kwa ajili ya wananchi wetu waweze kupata manufaa ya sera yetu ya Chama cha Mapinduzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi, ninaomba niunge mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuongea machache kuhusu bajeti iliyokuwa mbele yetu. Naomba niingie moja kwa moja kwenye hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wengi wanategemea reli hususani mkoa wangu wa Katavi na Wilaya ya Mpanda. Alikuwepo Mbunge mwenzangu Mheshimiwa Arfi, alikuwa anatetea sana reli ya kutoka Tabora - Mpanda. Mimi kila siku najiuliza Wabunge humu ndani wanazungumza kuhusu reli, lakini utekelezaji wake haupo. Mheshimiwa Arfi alivyokuwepo humu ndani alikuwa anazungumza kila siku, reli ya Mpanda - Tabora siyo salama. Mpaka leo reli ya Mpanda - Tabora ina pounds 40 na reli hiyo inabeba mizigo mingi, inailetea pesa nyingi Serikali na wananchi wa Mpanda wanategemea reli lakini mpaka leo reli ile wala haijashughulikiwa kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini unasikia kuna sehemu reli zinang‟olewa zinapachikwa pound nyingine. Sasa najiuliza zile pound zinatoka zinakwenda wapi? Hivi karibuni walizing‟oa pound 60 Tura, sasa zile zilipelekwa wapi? Badala ya kutolewa pale na kupelekwa sehemu ambapo kuna pound ndogo ili reli yake iweze kuimarishawa lakini ndugu zangu hakuna kitu kama hicho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kila siku wananchi wa Mpanda tunalalamika kuwa hatuna barabara, tunategemea reli na ndiyo maana Wabunge wengi wanasema RAHCO na TRL waunganishwe hili shirika lingine life kwa sababu hawana faida. Kuna pound zingine wameziacha pale makao makuu, pound 80 zimekaa hawajui kama wananchi wengine wanahitaji hizo pound, sasa wana maana gani? Hii RAHCO tunaomba Serikali sheria ilikuja Bungeni na ikaunganisha RAHCO na TRL, sasa sheria hiyo ije tena tutenganisha Shirika la RAHCO pamoja na TRL, sheria hiyo ije tena tupangue tuunganishe hili shirika liwe moja. Kwanza ukiangalia wanapewa hela nyingi halafu vitu vyake havieleweki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kila mwaka mnasikia Godegode kuna matatizo, treni inaanzia Dodoma, ina maana Serikali mpaka leo haina ufumbuzi wa tatizo la pale Godegode? Kila siku Godegode treni imeishia Dodoma, Godegode treni imeishia Dar es Salaam, Godegode kuna mafuriko. Mnajua kabisa Godegode tatizo, kwa nini msichukue hatua za kurekebisha kwa sababu treni inayotoka Dar es Salaam – Mwanza – Kigoma - Mpanda inabeba abiria wengi sana na wananchi wengi maskini wanategemea reli, kwa nini hapo Godegode hapashughulikiwi, kila siku Godegode shida. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze kwanza Kaimu Mkurugenzi mpya, nashangaa kwa nini hawampi ukurugenzi, amethubutu safari hii, wananchi wamekwama njiani na treni amechukua chakula yeye kama yeye kuwapelekea wananchi. Tunaomba hawa Wakurugenzi ambao wanao uthubutu wapewe ukurugenzi. Kitu cha kushangaza, mimi naomba niseme, leo hii mashirika yote makubwa, bandari Mkurugenzi Kaimu, uwanja wa ndege Mkurugenzi Kaimu, TRL Mkurugenzi Kaimu, wapeni ukurugenzi kamili ili waweze kufanya kazi nzuri, wameweza kuthubutu hawa wapeni basi ukurugenzi waweze kufanya kazi vizuri. Mnavyowaacha na ukaimu wanafanya kazi kwa wasiwasi, wapeni mamlaka ili waweze kutekeleza yale mliyowakabidhi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Waziri akija hapa aniambie kabla ya standard gauge haijaanza maana haya ni majaliwa, Mbunge ametoka hapa kusema hayo ni majaliwa, tunaomba kujua reli ya kutoka Tabora - Mpanda mtatubadilishia lini zile pound 40 iwe angalau tu 60 ili ile reli iweze kuwa stable. Kwa sababu wananchi wa Mpanda wapo rehani huku barabara ikiziba huku treni wasiwasi. Kabla standard gauge haijaanza tunaomba uimarishaji wa reli ya kutoka Tabora - Mpanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tunaenda kwenye standard gauge na tumesema inafika mpaka Karema, Karema tunategemea bandari, lakini hatujaona mwamko wowote wa bandari Karema. Naomba hii mikakati ianze ili wale wananchi wa Karema waone kama na wenyewe wapo Tanzania kwa hii bandari inayopelekwa huko kwa ajili ya standard gauge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja darala la Kavuu; kuhusiana na barabara ya kutoka Inyonga – Majimoto, hii ni Wilaya mpya. Wananchi kutoka Mpimbwe huko Majimoto, Kibaoni, Usevya, Kasansa mpaka wafike makao makuu yao ya Wilaya Inyonga wanatembea siku mbili. Mtu anatoka Kasansa aje Mpanda alale kesho yake aondoke aende Inyonga, hiyo ni Wilaya au kitu gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Wabunge wengine hapa wamesema kuhusu masuala ya barabara, hili daraja la Kavuu limechukua miaka saba. Hebu jamani mtuangalie watu wa mkoa wa Katavi, kila siku tunazungumza, tunaomba hili daraja liishe ili wananchi wa upande wa Kibaoni, Usevya, Kasansa waweze kufika kwenye makao makuu yao ya Wilaya siku moja. Tunaomba chonde Waziri akija hapo atuambie daraja la Kavuu litaisha lini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilizungumza ile barabara ya kutoka Stalike - Mpanda na nikasema pale Mpanda kuna shimo, lile shimo linaisha lini? Ni kero kwa wananchi wa Mpanda, kila siku ajali zinatokea. Nilizungumza Januari lakini mpaka leo hakuna mkandarasi, hakuna kitu chochote, kila kitu kipo vilevile. Tunazungumza mpaka lini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba niunge mkono hoja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia bajeti. Kwanza kabisa, naomba niipongeze bajeti yetu, bajeti nzuri, naomba niiunge mkono kabla sijaendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niipongeze Serikali yangu sikivu kwa kututengenezea barabara ambayo ilikuwa inasumbua sana wananchi wa Mpanda; Mpanda – Tabora kwenye Daraja la Ipole. Lile daraja sasa hivi limekwisha. Nomba tu Serikali yangu basi itoe kauli hilo daraja liweze kufunguliwa ili wananchi wa Mpanda sasa waweze kupata maisha mazuri, waweze kufanya biashara zao na kufanya shughuli zao kwa amani kwa sababu daraja lile la Ipole lilikuwa ni kikwazo, walikuwa hawawezi kusafiri, walikuwa wanazunguka mwendo mrefu. Naomba Kauli ya Serikali kwa ajili ya daraja hilo, kwa kuwa limekwisha ili tuweze kupata manufaa ndani ya maisha ya wananchi wa Mpanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naomba kuchangia bajeti hii kwa upande wa akinamama. Kwa kuwa mimi ni Mbunge wa akinamama, nianze na akinamama. Asilimia tano ya akinamama mara nyingi tunaitenga lakini akinamama hawaipati kutokana na Halmashauri zetu kwamba hazina uwezo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi ukiangalia, makusanyo mengi yameingia Serikali Kuu, ina maana TRA ndiyo watakusanya. Ina maana Halmashauri watakuwa hawana kipato cha kuwapa akinamama pamoja na vijana zile asilimia tano. Sasa sijui Serikali itafanyaje kwa sababu akinamama wengi sasa hivi wameshapata mwamko, ni wajasiriamali. Nanyi wenyewe mnaona sasa hivi hata mkienda vijijini mnakuta akinamama wengi ni wajasiriamali kutokana na juhudi nzuri za Serikali ya Chama cha Mapinduzi. Sasa tunaomba hii asilimia tano iliyowekwa na hivi vigezo ambavyo viliwekwa, hela nyingi zimechukuliwa Halmashauri, akinamama hawa wajasiriamali watapataje mikopo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata sasa hivi kupata hiyo asilimia tano kwenye Halmashauri zetu ni shida. Sasa naomba Serikali yangu sikivu kwa bajeti hii ione ni jinsi gani ya kuweza kutenga au kutafuta ili hawa akinamama waweze kupata asilimia tano ili waweze kufaidika na Serikali yao.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja kwenye upande wa maji. Hakuna kitu kigumu na shida katika maeneo yetu kama maji. Nikiangalia, Wilaya yangu ya Mpanda kuna vyanzo ambavyo Serikali ilifanya jitihada kubwa, lakini unakuta miradi ile haiishi na ile bajeti inayopangwa haiendi kwa wakati ile miradi ikaisha.
Sasa sijui bajeti hii ambayo imekuja mbele yetu, itaweza kukamilisha miradi ile ya maji na wananchi waweze kupata kwa urahisi na wepesi zaidi. Hususan Wilaya ya Mpanda, kuna mradi wa Ikorongo One; bajeti ya mwaka 2015 mkatupangia kuwa mtatupatia shilingi bilioni nne, lakini zile pesa hazikuweza kupatikana. Matokeo Wilaya ya Mpanda Mjini, Manispaa, maeneo mengi maji ni shida. Yaani maji yale yakipatikana leo, kesho hawapati; au wanaweza wakakaa siku tatu ndiyo wanapata maji. Maeneo mengine kama Makanyagio, Ilembo, hakuna maji kabisa, ni shida. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba basi, hii bajeti ya safari hii, miradi ambayo inaelekezwa, iweze kukamilika ili wananchi waweze kupata maji safi na salama. Nafikiri na Waziri alivyotusomea bajeti yake, alisema sasa ni kipindi cha akinamama kufurahi; anawatua ndoo. Sasa naomba basi akinamama hususan wa Mpanda Vijijini, kuna vijiji havina maji kabisa wala havina miradi kabisa. Akinamama wanapata shida sana. Naomba bajeti hii iweze kutimiza yale malengo waliyoyataja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, migogoro ya ardhi ni mikubwa mno. Ukiangalia kama Wilaya yangu ya Mpanda, Kata ya Ilembo ni shida. Naiomba Serikali sasa kupitia bajeti hii, migogoro hii ya ardhi iweze kwisha. Tunaomba bajeti hii ambayo leo tunaisema hapa ifanye kazi kama mlivyoileta mbele yetu, kwa sababu, migogoro ya ardhi haiishi. Kwa nini haiishi? Mimi nashangaa kila siku, kwa nini haiishi? Lazima sasa bajeti hii ambayo tunaichangia hapa, tunaomba migogoro ya ardhi kupitia bajeti hii, iishe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vijijini mwetu wanavijiji wanavaa mitumba na ndiyo nguo rahisi walizozizoea, ndiyo maana ukienda sasa hivi vijijini unawakuta akinamama wengi ni wasafi kutokana na mitumba. Leo sisi bado viwanda vya kutengeneza malighafi ya nguo havijafika, lakini leo tumeipandishia mitumba ushuru mkubwa, ina maana wale wananchi wa vijijini washindwe kuvaa kabisa?
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali kuhusu mitumba iangalie upya, watoe ushuru wa mitumba kwa sababu wananchi wetu ndiyo mavazi yao wanayayategemea kuliko kitu kingine chochote.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nishukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia bajeti hii. Katika nchi yetu kuna miradi mingi ambayo tuliiandaa na sera yetu inasema kuhusu Zahanati na Vituo vya Afya, lakini tukiangalia sehemu nyingi Vituo vya Afya, havijakamilika, unakuta sehemu nyingine kuna jengo zuri sana Serikali imejenga, lakini vifaa vya mle ndani havijakamilika. Naomba kupitia bajeti hii Serikali ijitahidi sana, miradi yote ya vituo vya afya pamoja na zahanati walizojenga wananchi ziweze kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna vifaa kama dawa, vifaa tiba; katika sehemu nyingi, zahanati nyingi hazina vifaa tiba, wananchi wanapata taabu. Kwa mfano, sisi pale Mkoa wetu wa Katavi, Wilaya ya Mpanda, ile hospitali ni ya Wilaya lakini tunasema ni kama Hospitali ya Mkoa. Hakuna kabisa vifaa, wananchi wa Wilaya ya Mpanda wanapata shida, ina maana kama ni ya Mkoa, maana yake ndiyo Makao Makuu ya Mkoa, lakini hawana vifaa kabisa. Naomba kupitia bajeti hii, Serikali ijitahidi kufikisha vifaa ili wananchi wetu waweze kupata matibabu mazuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa akina mama, kuna tatizo la maji vijijini. Tunasema maji vijijini kwa sababu sisi akina mama tunahitaji maji na utakuta maeneo mengi vijijini akina mama wanapata shida, wanaenda kutafuta maji sehemu za mbali, anaamka saa 8.00 za usiku, saa 9.00 za usiku anaacha familia yake. Naomba kupitia bajeti hii tunaomba sana Serikali itufikishie maji vijijini. Kwa sababu tutakuwa tumewakomboa sana wananchi kupitia maji hususan akina mama.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kupitia bajeti hii ambayo tumesema kuhusu shilingi milioni 50 za kila kijiji, napendekeza kupitia bajeti hii, fedha hizo ziende kila kijiji. Vile vijiji ndiyo vinawajua wananchi katika maeneo yao husika, maana kuna vijiji halafu kuna Mitaa. Mijini wanatumia mitaa; kwenye maeneo ya vijijini, kuna vijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunaomba zile fedha, kwa sababu kama mtaa ndiyo unawafahamu watu, Mwenyekiti wa Mtaa na ile Kamati yake ndio anawajua watu wa mtaani kwake. Sasa fedha zile shilingi milioni 50 zikifika pale wale watajuana ni jinsi gani watagawana zile fedha na kukopeshana ili waweze kupata faida ya Serikali yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mambo mengi mazuri ambayo yanayofanywa Serikali, tunaomba Serikali kupitia vile vile michezo, mara nyingi bajeti hii imekumbuka michezo, sanaa lakini bado mfumo wetu wa michezo haujakaa vizuri, hususan vijana wetu wa vijijini wako vijana wachezaji mpira wazuri ambao wanaweza kulikomboa Taifa hili, lakini bado hatujawafikia na bajeti zetu haziwafikii kule wakatambulika.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile wako wasanii wazuri ambao wanajua mambo ya usanii huko vijijini, lakini kutokana na uwezo, hawawezi kufika mijini au hawawezi kufika sehemu ambayo anaweza akajulikana au akafahamika. Basi tunaomba kupitia bajeti hii sasa, Serikali ikatambue wale watoto walioko vijijini, ambao wanaweza kuja kulipatia faida Taifa hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mambo mengi yanayotakiwa yafanyike ndani ya nchi yetu, kupitia bajeti hii. Pia kuna haya mashirika makubwa hususan bandari na viwanja vya ndege. Wao wanapata mapato ndani ya shirika kama vile bandari, lakini unakuta kuna mfuko wa Serikali na tumesema safari hii fedha yote iingie Serikalini, lakini vilevile kuna mambo wao kama shirika, wanatakiwa waboreshe ili waweze kupata faida zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa tunaomba kupitia bajeti hii, kama bandari kuna fedha ambazo wanaingiza katika Mfuko wa Hazina, tunaomba yale mahitaji wanayoyataka wenyewe kuboresha bandari ili iweze kufanya kazi kwa ufanisi mzuri zaidi, wapewe zile fedha haraka ili waweze kuinua uchumi ndani ya nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika viwanja vya ndege, tunajua kuna miinuko ambayo inaruka ndege, kuna faida kubwa ndani ya viwanja vyetu, lakini wana mahitaji ambayo wanataka kuweka labda taa, na kadhalika, naomba basi Serikali iwape zile fedha haraka kwa ajili ya mahitaji yanayoweza kuleta faida katika viwanja vyetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mambo mengi yanayofanyika katika mashirika ambapo sasa hivi pesa nyingi zitakuja kwenye Mfuko wa Hazina. Maana yake sasa hivi fedha zinazotoka katika mashirika mengi tumesema kupitia bajeti hii zitaingia kwenye mfuko maalum. Naomba Serikali, pindi watakapohitaji fedha zile wafanye jambo fulani, naomba wapewe ili waweze kuongeza ufanisi ndani ya kazi zao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niipongeze Serikali yetu kwa mpango mzuri kwamba kwa kupitia bajeti hii tumepanga kununua ndege tatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa naomba nchi yetu hapo katikati usafiri ulikuwa ni shida. Sisi tumefarijika sana kupitia bajeti hii kuona sasa Serikali yetu imekumbuka kununua ndege tatu, kusema kweli tumefarijika sana. Tunaomba sasa mikakati na utaratibu kuhusu Shirika la Ndege la ATCL, mikakati yake ipangwe vizuri tusije tukaharibu kama tulivyoharibu mwanzo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninajua shirika letu hili lina madeni mengi, lakini najua Serikali imeamua kufanya kitu ambacho safari hii hatuwezi kuharibika tena, kwa sababu madeni yale najua kuna bajeti ambayo mtaipanga, tulipe yale madeni, halafu shirika sasa lisimame kama shirika na sisi Tanzania sasa tuwe na Shirika la Ndege. Tutafurahi kwa sababu kama mimi Mkoa wangu wa Katavi, nashukuru Serikali naomba niipongeze, mlitujengea uwanja mzuri sana, lakini hakuna ndege hata moja inayotua.
Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia hili sasa, hizi ndege tatu, nami najua sasa Mkoa wa Katavi, ndege itatua. Naomba niwapongeze kwa hilo, basi tununue hizo ndege ili sehemu nyingi ambazo ndege zilikuwa hazifiki, sasa ziweze kufika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukurru sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuongea kengele ya pili isinigongee. Naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante sana.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ili kuweza kuzungumzia mpango wa nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu aliyetulinda ametuleta tena kwa mara nyingine mahali hapa, tunaendelea kuomba neema yake na rehema yake atulinde mpaka tumalize Bunge hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kazi nzuri ambazo wanazifanya kwa ajili ya kupigania nchi yetu na maslahi ya Taifa zima. Naomba nipongeze sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri ambazo kwa muda mfupi kwa muda wa mwaka mmoja wameweza kuzifanya.
Leo hii naomba nimpongeze Rais wangu kwa kazi nzuri na maamuzi magumu ambayo ameyafanya kuhamia Dodoma, leo hii Serikali inahamia Dodoma ni mafanikio makubwa kwa sababu ilikuwa inazungumzwa kwa muda mrefu na miaka mingi leo Awamu ya Tano imeweza kufanya leo hii Serikali imehamia Dodoma.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ninaomba niipongeze Serikali, ingawa bado pesa hizi hazijatoka za kwenda kila kijiji shilingi bilioni 59.5, tuna mategemeo Serikali hii ya Awamu hii ya Tano hizo hela zitafika kwa wananchi wetu kwa ajili ya uchumi wa Tanzania hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niipongeze Serikali ya Awamu ya Tano kwa kununua ndege mbili mpya. Leo hii tunajivunia Serikali ina ndege, alama yetu ya twiga ipo ilikuwa haipo lakini leo sasa ipo kutokana na malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano yameendelea kuwa mazuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite sana kwenye masuala ya dawa. Ninaomba sasa Waziri wetu aweke mpango mkakati wa ujumla ili wananchi wetu waweze kupata dawa. Dawa ni kitu muhimu sana kwa wananchi wetu wa Tanzania. Ninaomba mikakati mikubwa ichukuliwe sasa hivi, ufanywe mkakati maalum kwa ajili ya dawa ili hospitali zote zipate dawa. Ninajua Serikali ya Awamu ya Tano ni sikivu, mipango inayopanga sasa iweke mikakati ili tuweze kupata dawa kwa ajili ya wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili; lazima sasa tufanye mikakati ya kujenga vituo vya afya kila Kata ili wananchi wetu waweze kupata huduma za ukaribu. Tukiweka mipango mizuri na mikakati mizuri kila Kata iwe na kituo cha afya akina mama wengi wataende kufanyiwa operation ndani ya kata zetu na maeneo yetu husika, hiyo mipango iweze kupangwa. Mimi najua Serikali ya Chama cha Mapinduzi ni sikivu, mipango yote tunayomweleza Waziri wetu ataifanya na ataitenda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la maji; bado maji hatujawafikia wananchi vizuri husasan maji mijini bado kuna maeneo ambayo maji hayajawafikia wananchi vilevile maeneo ya vijijini, lazima sasa hivi tuamue kuweka mipango mikakati.
Kuna Mbunge hapa amezungumza kama sisi tunapakana na maziwa, mfano Ziwa Tanganyika li-supply Mkoa wa Katavi inawezekana, kwa sababu kuna mipango iliyopangwa nyuma. Leo hii Mwanza, Shinyanga wanapata maji kutoka Ziwa Victoria, tunaomba na sisi tunaokaa Katavi, Mkoa wa Rukwa na maeneo mengine kama Kigoma yale maziwa yetu yaweze kunufaisha maeneo husika, vijijini pamoja na mijini, mpango ukikaa vizuri nafikiri tutaweza kufanikiwa vizuri sana upande wa maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu elimu; ninaomba mipango mizuri ifanyike kwenye elimu. Tunajua Serikali ya Awamu ya Tano imefanya kazi nzuri ya kutafuta madawati, leo hii tuna madawati mengi. Vilevile kutokana na Serikali ya Awamu ya Tano imefanya elimu imekuwa bure, kutokana na elimu bure sasa hivi wanafunzi tumekuwa nao wengi ndani ya shule zetu. Sasa tunaomba Serikali ipange mpango makakati wa kujenga madarasa ili watoto wote waweze kuenea ndani ya madarasa. Kwa sababu madawati, mpango umekwenda vizuri hakuna sehemu sasa hivi watu wanalalamika kuwa mtoto anakaa chini, tunaomba bajeti hii inayokuja tuweke mikakati ya kujenga madarasa nchi nzima ili watoto wetu wote waweze kukaa madarasani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa ardhi; leo hii tunawaleta wawekezaji, lakini kuna matatizo kidogo ndani ya maeneo yetu husika. Leo hii migogoro ya ardhi kati ya wawekezaji na wananchi imekuwa mikubwa mno. Ninaomba Serikali sasa kwa sababu tuna lengo zuri la kuweka mikakati mizuri ya wawekezaji nchini na vilevile tunaendelea kuwaleta wawekezaji ndani ya nchi yetu, kwenye upande wa ardhi tujipange vizuri na Watanzania tumeongezeka, lazima sasa hivi Serikali ipange mikakati ya kuongeza ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna sehemu nyingine tumeweka mipaka, mipaka ile tuipanue ili wananchi sasa pamoja na wawekezaji wakae sehemu nzuri. Wawekezaji wengine wanatukimbia kutokana na migongano kati yao na wananchi. Ninaomba Serikali iweke mipango mizuri, mikakati mizuri ili wananchi na wawekezaji waweze kukaa vizuri na waweze kujenga viwanda vyao ndani ya nchi yetu ili vijana wetu wapate ajira, mama lishe zetu wale wanaohangaika waweze kupata ajira kwa ajili ya mipango mizuri ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la mikopo ya akina mama. Akina mama wengi bado hatujawafikia kwa elimu. Tunapenda akina mama wapate mikopo, tunapenda akina mama waweze kuinuka, lakini bado hatujawafikia ili waweze kupata elimu nzuri waweze kutumia hayo mabenki tunayoyasemea leo hii mambo yamekuwa siyo mazuri, akina mama tukiwafikia tukiwapa elimu nzuri wakiweza kujikomboa wao kama wao, tukiwawekea mikakati mizuri ninafikiri Taifa hili ukimwezesha mwanamke, tumewezesha jamii nzima. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kilimo; bado Watanzania tunalima asilimia 80 ni wakulima, asilimia 20 ni wafanyakazi. Mpaka leo hapa tulipo wananchi kule hawajapata mbolea na hili lazima tuliwekee mikakati mikubwa na mipana ili kipindi cha mvua kabla hakijafika wananchi hawa waweze kupata mbolea kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa katikati tulikuwa tuna mawakala, leo hii hiyo mipango ya mawakala tumeitoa na wale mawakala ambao tuliowatoa bado hatujawalipa wanatudai na mpaka sasa hivi hatuna mawakala wala hatuna nini, wananchi wameilewa. Hatujui hiyo mbolea itauzwaje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba Serikali ichukue jukumu ambalo sasa kupanga mikakati mizuri na mipango mizuri ili wananchi waweze kupata manufaa kupitia Serikali yao kwa ajili ya kilimo kwa sababu upande wa kilimo ndiyo uwekezaji upo mkubwa sana kuliko upande mwingine, ninaomba Serikali hii sikivu mipango hiyo iweze kupangwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepanga mipango mingi, tunaongea mipango mingi, lakini kuna watu ambao ni muhimu sana ambao tukiwajengea uwezo na tukiwafanyia mipango mizuri, mikakati mizuri wanaweza wakakaa vizuri zaidi. Hapa mara nyingi tunawasahau sana askari wetu na sehemu nyingi ukienda unakuta askari hawana sehemu ya kuishi, lazima sasa Serikali ichukue jukumu la kuweka mpango mkakati wa kuwajengea askari nchi nzima ili hawa askari wanaotulinda wananchi wawe na sehemu nzuri za kukaa ili nchi yetu iweze kuwa na amani na utulivu kama tulivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima sasa tuwawekee mikakati mizuri na mipana ili kila sehemu nchi nzima, nyumba za askari, nyumba za manesi, nyumba za walimu ziweze kuwekewa mikakati mikubwa na mipana zaidi ili sasa nchi yetu iweze kutulia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la utalii, kwetu Mpanda nilishasema kipindi kilichopita tumejengewa uwanja mzuri. Naomba nirudie kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri ambayo ilifanyika kununua ndege mbili. Ninajua sasa uchumi wa Tanzania na uchumi wa Mkoa wangu wa Katavi utazidi kuongezeka, ninajua sasa ndege itatua Mpanda, Katavi kwa ajili ya kuleta watalii ili uchumi wa Katavi uweze kukua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana, ninaomba niunge mkono asilimia mia kwa ajili ya mpango huu mzuri.
Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa ninaomba niunge mkono hoja za ripoti za Kamati zote tatu ambazo zimewasilishwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za Kamati. Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijielekeze kwenye nyumba za askari wetu. Askari wetu wanaishi kwenye mazingira magumu sana katika nchi yetu ya Tanzania, unaweza ukasema labda Mkoa wa Katavi wanaishi labda vibaya, hawana nyumba, hawana nini, lakini ukitoka ukienda sehemu nyingine unasema loh, afadhali kwangu kuliko sehemu nyingine. Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaiomba Serikali hizi bajeti tunazipanga ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunaomba zifike kwa wakati ili askari wetu waweze kujengewa nyumba au hata kuboreshewa nyumba wanazoishi, kwa sababu askari wetu ndiyo wanaotuweka sisi kwenye mazingira ya amani na upendo katika maeneo yetu husika. Tunaomba Serikali ijipange kuangalia hao askari. Tunawapa majukumu mengi makubwa ambayo wanatakiwa watekeleze lakini mazingira yao ambayo wanaishi sio mazingira rafiki. Tunaiomba Serikali hizi bajeti tunazopitisha safari hii Serikali ijipange kujenga nyumba angalau nyumba za askari. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tumeona at least Jeshi la Kujenga Taifa wamejengewa maghorofa sehemu mbalimbali, hapo tunaweza tukawapongeza kwa sababu wamejitahidi kwa upande mwingine, lakini kwa upande wa askari polisi bado hatujawatendea haki, wanaishi kwenye mazingira magumu sana. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende upande wa bodaboda. Bodaboda ni vijana wetu ambao wanajitafutia tuseme maisha yao na maisha haya wanajitafutia kutoka vyombo hivi ambavyo vimekuja kuwarahisishia maisha yao, lakini unakuta sasa ndani ya maeneo yetu kuna baadhi ya maaskari wanawanyanyasa sana bodaboda. Ninaomba basi Serikali, tunajua wale ni watoto wetu tumewapa ajira, wamejitafutia ajira kupitia bodaboda, tupange mikakati ya kuwafundisha usalama barabarani kwa sababu tunaona labda wanafanya vitendo vibaya, wanakwenda vibaya, wanaumia, wanapata ajali usiku na mchana, tufanye mikakati ya kuweza kuwapa semina ili waweze kujua jinsi gani watakavyotumia zile bodaboda. Ninaomba sana Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi itekeleze hayo.(Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaenda upande wa magereza. Magereza zetu zimejaa sana; sasa mimi najiuliza, kuna wengine wamekaa kule magerezani miaka kumi, kesi zao haziishi, uchunguzi bado unachunguzwa. Tunaomba Serikali sasa hivi ifanye mikakati ya kuwatoa wale watu wenye kesi zao za muda mrefu waweze kutoka mule ndani kwa sabaabu wanakula bure, wamekaa kama vile mahabusu wengine mpaka leo wamekaa miaka sita, saba, nane hawajahukumiwa sasa wanajaza magereza na chakula kila siku tunasema kinapotea, tunaendelea kuwaweka watu ambao wanatakiwa waweze kuondoka ili magereza ile iweze kupungua. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, mahakama ndani ya nchi yetu. Mahakama bado, kama sisi kwetu Katavi mahakama hatuna ya Mkoa, hatuna hata Mahakama ya Wilaya huwezi ukasema kama tuna mMahakama. Tunaomba basi Serikali ijitahidi kujenga mahakama ndani ya nchi yetu ili tuweze kupata urahisi katika huduma mbalimbali za kimahakama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaenda kwenye Balozi zetu. Balozi zetu Wabunge wengi wamesema pesa haziendi kwa wakati. Wako nchi za nje huko wanaishi kwenye mazingira magumu sana. Tazameni Balozi zetu kuzipelekea pesa, unakuta sehemu nyingine balozi nyingine mazingira wanayoishi na lile jumba walilonalo utafikiri ni gofu. Hampeleki pesa za kutengeneza majengo ambayo yako maeneo hayo. Tunaomba Serikali, jitahidini jamani bajeti tunazopitisha, tafuteni pesa za kupeleka maeneo hayo ili mazingira yawe rafiki kwa wale watu tunaowapeleka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nipongeze kazi nzuri sana ya Serikali ya Awamu ya Tano na Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa sana ambazo anafanya kwa Watanzania. Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Mawaziri, hongereni sana kwa kazi nzuri ya kujenga nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna changamoto chache za shule za msingi hususan madarasa pamoja na matundu ya vyoo. Naomba sana Serikali ielekeze mpango mkakati kwa ajili ya mambo muhimu sana hayo kwa ajili ya watoto wetu ili waweze kusoma vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Walimu wetu ni wachache sana hususan vijijini pamoja na wahudumu wa zahanati zetu, Manesi, Madaktari, Watendaji wa Vijiji, Kata vilevile kada ya kilimo na Maendeleo ya Jamii. Tunaomba sana Serikali iweke nguvu katika maeneo hayo kwa sababu ndio wanaosimamia maendeleo yetu katika vijiji vyetu pamoja na kata zetu kwa ajili ya wananchi kwa ajili ya huduma mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maji vijijini bado wananchi wa Mkoa wa Katavi kupitia vijiji vyake maji bado shida sana. Huo ndio ushauri wangu. Ahsante.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2017/2018.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Spika, naomba nikushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia Ofisi ya Waziri Mkuu. Kwanza kabisa, naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu aliyetupa uzima na uhai leo tuko katika Bunge hili tukichangia bajeti ya Serikali.
Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze sana Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoifanya katika nchi yetu ya Tanzania. Waziri Mkuu unajituma sana, hongera sana na kote ulikopita kuna mafanikio makubwa sana. Naomba tukupongeze sana.
(Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba nimpongeze Waziri Mheshimiwa Jenista pamoja na Naibu wake kwa kazi kubwa waliyoifanya. Kama safari hii sisi mmetupa nafasi ya kuwasha mwenge katika Mkoa wetu wa Katavi, tumepata manufaa na mafanikio makubwa, naomba niwapongeze sana.
(Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba niwapongeze Mawaziri, mnyonge, mnyongeni lakini haki yake mpeni. Mawaziri wetu mnafanya kazi kubwa sana, mnatembea usiku na mchana kwa ajili ya nchi yenu ya Tanzania.
Mheshimiwa Spika, naomba nijielekeze kwenye elimu ya msingi. Serikali imefanya jitihada kubwa, imeondoa kero ya Watanzania na watoto wetu wanasoma bure. Vilevile kulikuwa kuna changamoto ndani ya shule zetu za misingi tulikuwa hatuna madawati lakini Serikali ilifanya jitihada kubwa kutafuta madawati pamoja na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na wananchi, wote kwa ujumla wakachangia, sasa shule zetu zina madawati. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, lakini bado tuna tatizo moja kubwa sana ndani ya shule zetu za misingi la vyumba vya madarasa. Sasa hivi kutokana na elimu bure, wazazi wengi wanaenda kuandikisha watoto ili waweze kusoma na kupata elimu ya msingi. Unakuta takibani watoto 1,000 darasa la kwanza hawana sehemu ya kusomea, sehemu nyingine watoto wamepangiwa madawati nje wanasoma. Maeneo yetu kama Mkoa wa Katavi ni ya mvua, mvua ikinyesha wale watoto hawapati elimu, inabidi watawanywe warudi nyumbani.
Mheshimiwa Spika, kwa vile hii ni changamoto, tunaomba Serikali ipange mpango mkakati kuhakikisha tatizo hili linashughulikiwa. Wananchi wanajitoa kwa hali na mali kuchangia elimu. Unaenda unakuta wananchi wamejenga madarasa, wengine wamemaliza wengine uwezo wao wanafika kwenye lenta. Tunaomba Serikali ipange mkakati mpana kwa ajili ya kuongeza madarasa katika shule zetu. Tunapongeza kwa jitihada kubwa wanazofanya lakini inabidi mpango mkakati uwe mpana zaidi ili watoto waweze kupata sehemu ya kusomea. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, niende kwenye elimu ya sekondari. Katika hotuba ya Waziri Mkuu ameelekeza wananchi wahamasishwe ili watoto waweze kusoma sayansi. Ni kweli, shule zetu nyingi za sekondari walimu wa sayansi hatuna, wako wachache sana. Unakuta shule ya sekondari ina mwalimu mmoja wa sayansi au hakuna kabisa, watoto wengi wanajielekeza kwenye masomo ya biashara. Tunaomba Serikali iwaajiri walimu wa sayansi ili waweze kwenda kwenye shule zetu za kata kwa sababu ndizo wananchi wengi watoto wao wameenda kusoma huko ili
tuweze kuibua walimu wa sayansi na vipaji vipya. Kuna shule baadhi kama kwetu Shule ya Usevya ina walimu wachache sana wa sayansi lakini wamesaidia kuibua wale watoto wa Form V au Form VI wanatoka wanaenda kusaidia kufundisha wanafunzi sehemu nyingine.
Mheshimiwa Spika, naomba niongelee maji vijijini. Hakuna Mbunge atakayesimama hapa asizungumzie maji kwa sababu tunavyoenda huko vijijini tunaona hali halisi. Serikali ilifanya jitihada kubwa ya kuchimba visima virefu na vifupi. Hata hivyo, kuna sehemu nyingine watalaam walienda kuangalia wakaona kabisa hapa pana maji lakini walipochimba yale maji yakapotea kutokana na hali halisi sasa hivi Watanzania wengi wanakata miti, wanaharibu sehemu nyingi ambazo maji yanatokea, unakuta kunakuwa kuna ukame mwingi. Naomba Serikali ijipange vizuri upande wa maji. Vijijini wananchi hawana maji kabisa. Unakuta kijiji hakuna hata kisima kimoja. Mwananchi anatoka maeneo husika anaelekea maili 20 au 30 kwa ajili ya kutafuta maji. Tunaomba Serikali ipange mkakati mpana kwa ajili ya maji vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, vilevile tunaipongeza Serikali kwa ajili ya maji mijini. Mamlaka za Maji Mijini zinajitahidi, miradi mbalimbali inaelekezwa huko. Tunaomba Serikali, kuna miradi ambayo ipo lakini bado wale wakandarasi hawajaweza kulipwa pesa zile wanazodai. Tunaomba wawalipe
wakandarasi ili waweze kutimiza miradi ile ambayo iko kwenye Mamlaka ya Maji Mijini.
Mheshimiwa Spika, Hospitali yetu ya Wilaya ya Mpanda ilikuwa haina duka la dawa lakini Mheshimiwa Waziri Mkuu alivyofika alielekeza na leo hii tunajivunia Mkoa wa Katavi, Wilaya ya Mpanda tuna duka la dawa, tunapongeza sana. Hata hivyo, kuna tatizo kidogo, dawa zinakuja chache. Tunaomba dawa na vifaa tiba viongezeke ili wananchi waweze kupata huduma safi na salama kwa ukaribu zaidi.
(Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba nipongeze kwa Kituo cha Afya Kalema kupata gari na sasa hivi tumepata chumba cha upasuaji, akinamama pale wanazaa kwa uzazi salama zaidi. Pia Tarafa ya Mishamo tuna Kituo cha Afya ambacho upasuaji unafanyika na vilevile tumepewa gari. Bado tarafa nyingine tunahitaji mtufikirie tuweze kupata vyumba vya upasuaji na vilevile tuweze kupata magari ya afya kwa sababu kutoka kwenye tarafa mpaka mjini ni mbali.
Mheshimiwa Spika, naomba niipongeze Serikali, najua Wabunge wa Katavi wengi wanasema hili, sisi Mkoa wetu wa Katavi tuna uwanja mzuri sana Serikali mlitujengea. Naomba tuipongeze Serikali kwa kutujengea ule ule uwanja. Tuna ndege ambazo tumenunua ndani ya Serikali yetu ya Awamu ya Tano. Tunaomba basi na sisi Mkoa wa Katavi tuweze kupata huduma hiyo ya ndege hata moja, katika route yoyote ile inayoenda Tabora au Kigoma ili wananchi wa Katavi nao waweze kufurahia matunda ya Serikali yao ya Awamu ya Tano. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tuna Ziwa Tanganyika ambalo linapita Ikola na Kalema. Kuna hii meli ya MV Liemba ina miaka 110… (Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
SPIKA: Ahsante sana.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Spika,
tunaomba Serikali ijenge meli hii kwa sababu sisi wa Mkoa wa Katavi inatuhusu kupitia Ikola na Kalema. Tunaona meli
nyingi zinajengwa…
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuzungumza bajeti hii muhimu sana ya maji, kwa sababu maji ni uhai, bila maji hatuwezi kuishi, kila binadamu lazima atumie maji ili aweze kuishi. Bajeti hii tunaiomba Serikali kwa ajili ni jambo muhimu sana kwa binadamu tunaomba iongezwe kama ilivyokuwa 2016/2017 kwa sababu maji ni uhai. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri pamoja na Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya, tunaona jinsi gani wanavyoipigania Wizara yao kwa ajili ya kufungua miradi mbalimbali. Hata hivyo, bado kaka zangu wana kazi kubwa sana kwa sababu Wizara waliyokuwa nayo ni ngumu sana inawagusa wananchi moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeomba bajeti iongezwe kwa sababu kama nilivyosema maji ni muhimu sana kwa binadamu. Vilevile ukiangalia kuna mifuko mbalimbali ambayo tunaiona imefanya kazi vizuri. Tukizingatia REA imefanya kazi vizuri sana kwa upande wa umeme. Tulikuwa tunaiomba Serikali kwenye tozo ya Mfuko wa Barabara tutoe at least shilingi hamsini, Mfuko wa Umeme tutoe shilingi hamsini ili iwe shilingi mia iende kwenye Mfuko wa Maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaona ni jinsi gani REA ilivyofanya kazi vizuri ndani ya vijiji vyetu; leo hii wananchi wanafurahi wanapata huduma safi ya mwanga. Sasa maji ni uhai, kila mtu anahitaji maji na tukiangalia maeneo yetu ya vijijini hakuna maji kabisa, akina mama wanahangaika. Tukienda kwenye ziara zetu, ndiyo maana unakuta Waheshimiwa Wabunge wengi wanapiga kelele kwa sababu ya maji kwa kuwa tunapokwenda kwenye ziara zetu huko tunaona hali halisia ya jinsi gani maji hakuna.

Mheshimiwa Naibu Spika, akinamama wanatoka saa tisa za usiku, vijiji vingine saa nane za usiku wanakwenda kutafuta maji na akienda kutafuta maji hapati yale maji safi na salama anapata maji machafu. Matokeo yake sasa unakuta asilimia kubwa ya maji yale ya vijijini ambayo ni ya vijito kuna maradhi mengi yanapatikanika huko, watu wanaumwa vichocho na kuharisha. Halafu sasa hivi mpaka mijini kwa sababu hatutumii maji safi na salama, mjini sehemu nyingi maji hayatibiwi matokeo yake watu asilimia 90 tunapata magonjwa ya UTI.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunaomba Serikali kwa hili sasa hivi lazima tujipange vizuri, bajeti ongezeke ili nchi yetu ya Tanzania tuweze kujivunia kwa hilo. Tunaomba asilimia 70 iende vijijini na asilimia 30 ibaki mjini kwa sababu mijini kuna miradi mbalimbali mikubwa ambayo inatekelezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende sasa kwangu Mpanda. Naomba niishukuru Serikali kwa sababu Mpanda tuna miradi mikubwa kama vile mradi wa Ikolongo ambao umefanyika na sasa asilimia 60 ya wananchi wa Mpanda wanapata maji, lakini asilimia 40 pale Manispaa hawapati maji. Hapa ndani ya ukurasa wa 66 Mpanda kuna huu mradi wa mwaka 2016/2017 tulipangiwa bilioni mbili. Huwezi ukaamini kuna watu wanatafuta maslahi yao wenyewe badala ya kutafuta maslahi ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pesa hizi zilivyofika Mpanda Tender Board imerudiwa mara tatu, mpaka leo ninavyokwambia mradi huu unakutana na pesa za bajeti hii ya 2017/2018. Mradi haujatekelezeka kwa sababu ya ubinafsi; watu wanataka maslahi yao wenyewe binafsi badala ya maslahi ya wananchi. Wananchi wa Mpanda wanahangaika maji wenyewe wanataka waweze kupata mradi wajinufaishe wao. Inasikitisha sana kwa Mpanda! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali Mheshimiwa Waziri, najua sasa hivi Tender Board ime-tender mara tatu kiasi ambacho wamekwenda kushtakiana kwa ajili ya ubinafsi. Naomba Mheshimiwa Waziri alifuatilie hili jambo ili wananchi wa Mpanda Mjini waweze kupata maji, mradi huu uweze kufanyika na hizi bilioni mbili ziweze kufanya kazi kutoka Kanoge mpaka Mpanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii Hospitali ya Mpanda Mjini ambayo wananchi tunaitegemea haina maji, na huu mradi wa bilioni mbili ulitegemewa ukifika pale maji yafike kwenye Hospitali yetu ya Mpanda Mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba hizi bilioni mbili ambazo zilikuwa za bajeti iliyopita ziweze kufanya kazi na kama safari hii wametupangia bajeti vilevile iweze kufanya kazi kwa sababu wananchi wa Mpanda Mjini wanapata tabu kwa sababu ya watu wachache ambao wanataka maslahi yao binafsi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii sisi Mkoa wa Katavi tuna Ziwa Tanganyika; sisi tunafurahi wenzetu hapa wana Ziwa Victoria leo ziwa lile limewapa manufaa. Hata hivyo, sisi Wanakatavi tuna Ziwa Tanganyika ambalo lina kina kirefu, kina chake kirefu kushinda Ziwa Victoria. Kwa nini sasa Serikali na Ziwa Tanganyika… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 – Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuzungumza jioni hii. Kwanza kabisa naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu ambaye aliyetupa uzima na uhai, ametupa muda mwingine tena wa kuweza kumtumikia. Pili, naomba nimpongeze Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri ambayo aliyoifanya jana kwa ajili ya kulitumikia Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa kazi kubwa nzuri ambayo anaifanya katika Wizara hii pamoja na Naibu Waziri. Wanafanya kazi kubwa ambayo inaonekana kihalisia, tunaomba tuwapongeze sana na Mungu aendelee kuwasimamia ili waweze kufanya kazi vizuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze na Mkoa wangu wa Katavi nikiongelea kuhusu masuala ya Wilaya mpya ya Tanganyika. Wilaya ya Tanganyika ina vijiji vingi sana ambavyo mpaka leo havijafikiwa kupata hati miliki ya kimila. Wananchi wengi wanaoishi maeneo haya hawana faida na rasilimali zao walizonazo. Kwa sababu tumeona Wizara hii ni sikivu, tunaomba basi wanavijiji wale wa Wilaya ya Tanganyika, Mkoa wa Katavi wafikiwe ili waweze kupata hati miliki za kimila.

Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia 70 ya Mkoa wa Katavi ni pori, asilimia 30 ndiyo maeneo wanayoishi wananchi; na siku hadi siku ndani ya Mkoa wetu wa Katavi wananchi wanaongezeka na maeneo yetu ya kufanyia shughuli za kibinadamu ni machache. Naomba Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Wizara ya Maliasili na Utalii; kwa kuwa Wizara ya Maliasili wana sehemu kubwa sana ya hifadhi; na ukizingatia sasa hivi siku hadi siku tunazaana. Sasa binadamu tumeongezeka, mapori yamekuwa makubwa mno, tunaomba Wizara hizi zitutazame kwa hali ya ukaribu zaidi Mkoa wa Katavi kuweza kutupunguzia maeneo ili tuweze kupata sehemu ya kuishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unakuta kata nyingine hawana kabisa sehemu za kulima, wakiingia tu wanaingia kwenye hifadhi, wakienda huku mapori ambayo yanahifadhiwa na Serikali, sasa wanashindwa jinsi gani ya kufanya shughuli za kibinadamu. Tunaomba Wizara hii ya Ardhi pamoja na Maliasili waweze kutuona kwa ukaribu zaidi kwa ajili ya kutuongezea maeneo ili wananchi wa Mkoa wa Katavi waweze kupata maeneo ya kufanyia shughuli zao kibinadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya yangu ya Mpanda Manispaa ninaomba nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri, alifika katika Wilaya ya Mpanda, alijionea mwenyewe hali halisi. Katika Wilaya ya Mpanda Kata yetu ya Kashaurili ambayo ndiyo Makao Makuu ya Wilaya ya Mpanda katika zile nyumba za wenyeji hakuna mtu mwenye hatimiliki mpaka leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kama Wizara itusaidie kutokana na hali halisi. Kwa upande wa ardhi Manispaa hatuna kabisa wafanyakazi. Wafanyakazi ni wachache sana; wafanyakazi ambao wameajiriwa ni watatu tu, wengine wote ni vibarua. Sasa wale vibarua wanakuwa hawafanyi kazi yao kimakini kwa sababu, wanajua wenyewe ni vibarua. Sasa naomba kama Wizara itusaidie sasa kutuletea watumishi ambao wameajiriwa ili waweze kufanya kazi vizuri pale Manispaa, Mpanda Mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya ardhi katika Wilaya ya Mpanda. Katika Kata ya Ilembo kuna migogoro ya ardhi kati ya wananchi na Jeshi. Najua Mheshimiwa Naibu Waziri alielezwa, basi tunaomba suala hili liweze kufanyiwa kazi haraka iwezekanavyo kwa sababu, wananchi wa Mpanda pale Kata ya Ilembo pamoja na Kata ya Misunkumilo kila wakiingia kidogo tu Jeshi linasema eneo lao. Sasa tunaomba huu mgogoro uweze kwisha, ili wananchi waweze kupata fursa ya kuweza kufanya kazi zao za kijamii wakiwa katika hali ya usalama zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nilipongeze Shirika la National Housing, limefanya kazi nzuri sana kiasi kwamba hatimaye na sisi wananchi ambao tunaoishi katika wilaya mbalimbali tumeona jitihada za National Housing. Tunaomba tumpongeze sana Mkurugenzi wa National Housing, Mchechu kwa kazi kubwa ambayo anaifanya katika nchi yetu ya Tanzania. Ameweka alama kubwa sana katika nchi yetu, ameweka alama kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Mpanda Mjini tumejengewa nyumba za National Housing. Nyumba zikijengwa zinatakiwa zitumike na binadamu, zisipotumika na binadamu zile nyumba zikishafungiwa miaka miwili, ama mitatu lazima zinakuwa na ufa. Ina maana kuwa binadamu akiishi ndani ya nyumba zile nyumba zinaendelea kuishi, lakini kama ndani ya nyumba haishi mtu nyumba nayo inapata uharibifu, inaweka ufa matokeo yake inaonekana kama nyumba nzee (iliyozeeka). Sasa pale Mpanda mmetujengea nyumba nzuri sana, tunaomba tuwashukuru, lakini zile nyumba bado hazijapata wanunuzi, zile nyumba zinakaa bure, zimefungwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba, sasa hivi Wilaya ya Mpanda ni Mkoa wa Katavi, kuna wafanyakazi mbalimbali wa kisekta, wa Wizara, wa maeneo mbalimbali wamekuja maeneo yale, hawana sehemu ya kuishi. Tunaomba hizi nyumba ambazo zimejengwa Wilaya ya Mpanda, Ilembo, zipangishwe. Zikishapangishwa hapo badaye wale wafanyakazi wanaweza kuzinunua kuliko kuzifungia, zile nyumba hazina mtu wa kuishi, matokeo yake zinakuwa kama vile maboma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Wizara pamoja na Shirika letu la National Housing waangalie upya hizi nyumba ambazo hazijaweza kununuliwa basi wazipangishe ili ziweze kupata wanunuzi mbele ya safari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niingie tena kwenye masuala ya migogoro ya ardhi. Naiomba Serikali, tunajua Awamu hii ya Tano kusema kweli imejitahidi sana, migogoro ya ardhi imepungua, lakini bado kuna kazi kubwa. Tunaomba Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri, migogoro ya ardhi ni mikubwa sana ndani ya maeneo yetu husika. Waheshimiwa Wabunge wengi wamesema, ifike kipindi sasa tutafute maeneo ya wafugaji na maeneo ya wakulima, maana wengi unakuta wakati mwingine wanatetea wafugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile kuna wakulima ambao nao wanapaswa wapate stahiki yao. Tunaomba Serikali kwa ujumla wake, sasa hivi kifike kipindi cha kuwapangia wafugaji maeneo yao na wakulima maeneo yao, ili nchi yetu ya Tanzania iendelee kuwa na amani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru sana na naomba niunge mkono hoja kwa asilimia mia moja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia bajeti yetu muhimu sana kwa ajili ya Watanzania. Naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu aliyetuumba ametupa uhai na uzima leo tumekuwa hai na tunaendelea na wale wote wanaofunga nawatakia funga njema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nimpongeze Rais wa Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya kwa ajili ya Watanzania. Leo Watanzania wameona jitihada za Mheshimiwa Rais za kutetea maslahi ya Watanzania. Naomba Watanzania wote tumuunge mkono Rais kwa kazi kubwa anayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanayoifanya. Vilevile naomba nimpongeze Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa kuwa makini sana na kuchukua yale mahitaji yanayotakiwa na Wabunge na mnachukua mawazo, mmechukua mambo mengi kwa Wabunge ambayo mmeyafanyia kazi na mmeweka kwenye bajeti, naomba niwapongeze sana. Wananchi wote wanaunga mkono bajeti hii kwa asilimia mia moja. Ina maana leo kama kungekuwa kuna uchaguzi CCM ingepata asilimia mia moja. (Vigelegele/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono bajeti ya Serikali kwa asilimia mia moja kwa sababu bajeti hii imeeondoa kero za wananchi kwa asilimia mia moja. Leo hii mimi mtu wa Mpanda ukiniambia bajeti haijawasaidia wananchi siwezi kukuelewa kwa sababu nilikuwa najua kero za wanachi wa Mpanda hususani Mkoa wa Katavi. Mkoa wa Katavi ni wa kilimo, leo hii tani moja yule mfanyabiashara mdogo mdogo anasafirisha mazao yake bure ina maana kuwa bajeti hii imemkomboa mfanyabiashara mdogo na mkulima nayetoa mahindi yake Mlele, Mpimwe magunia kumi anayaleta mjini anakuja kuyauza, mmemkomboa kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niipongeze sana Serikali kwa hilo ndiyo maana na wenyewe wameiunga mkono asilimia 100 bajeti hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naomba niipongeze Serikali kwa kuanza kujenga standard gauge kwa sababu inafika Mkoa wangu wa Katavi. Reli hii itaturahisishia sana sisi wa kanda hii kwa sababu usafiri wetu mkubwa ni reli ya kati. Sasa kwenye reli ya kati mnatupitishia sasa reli ya kisasa ambayo ni standard gauge, naomba niipongeze sana Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba niipongeze Serikali kwa kununua ndege mbili ambazo zipo tayari na vilevile mmenunua tena ndege zingine tatu ambazo zitasaidia na uchumi wa nchi yetu utaongezeka mara mbili, tatu. Naomba sana niipongeze Serikali, leo ni kuipongeza kwa sababu haijawahi kutokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba niipongeze Serikali kwa kufuta leseni za magari. Leo wananchi wengi walikuwa wame-park magari yao, walikuwa hawana pesa za kulipia lakini mmewaondolea mzigo magari yote sasa yatatembea barabarani. Naomba niipongeze sana Serikali kwa kazi kubwa mliyoifanya kwa kuwaondolea adha wananchi kwani sasa watatembea na magari yao na watafanya biashara. Wengi walipaki magari, walikosa hela za kulipia lakini leo watatembeza magari, wataenda kufanya shughuli zao mbalimbali ili uchumi wao uweze kukua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na vilevile naunga mkono mapendekezo ya Kamati ya kupeleka fedha za tozo ya shilingi 40 kwenye maji itakayotoka kwenye dizeli, petroli na mafuta ya taa. Najua kabisa hii pesa ikienda Hazina siyo lazima ifanye jambo lingine inaweza kupendekeza hizi pesa shilingi 40,000 zikaenda kwenye maji kwa sababu akina mama wengi sana wanateseka na ukosefu wa maji. Naomba hii tozo ya shilingi 40,000…

MWENYEKITI: Mheshimiwa ni shilingi 40.

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni shilingi 40, si unajua tena, raha imezidi kutokana na bajeti nzuri sana, nzuri mno. Sasa hii shilingi 40 itaenda kwenye maji ili wananchi waweze kutatuliwa matatizo mazito tuliyonayo. Naomba Serikali, najua Waziri upo makini sana tunaomba hii tozo ya shilingi 40 iende kwenye maji ili wananchi sasa waweze kupata unafuu kwa sababu vijijini akina mama wanapata taabu sana kwa ajili ya maji. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile mambo mengi yanayofanyika katika Serikali hii ni makubwa na mazuri sana. Naomba tuendelee kuiunga mkono kwa sababu mnaiona jinsi gani inavyofanya kazi kwa ajili ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja upande wa kilimo. Mkoa wa Katavi sisi ni wakulima, naomba sasa tuweke mikakati mizuri, wale wananchi wa Katavi waweze kupelekewa mbolea kwa ukaribu zaidi na mapema ili kilimo chao kiwe na tija. Naomba Serikali yangu sikivu sasa hivi twende kwenye mbolea tuweke mikakati ya mbolea kwa mikoa yote inayolima ya Katavi, Rukwa, Mbeya na Ruvuma. Naomba Serikali yangu mbolea iwe kipaumbele, wapelekewe mbolea mapema na ukizingatia Mkoa wa Kigoma wenyewe wanalima mapema basi iwekwe mikakati mizuri ya kupelekea mbolea wakulima mapema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Mkoa wangu wa Katavi tuna shida sana ya maji. Tuna Ziwa Tanganyika ambalo lina kina kirefu, tukilitumia ziwa hili nafikiri Mkoa wa Katavi matatizo ya maji yataisha kabisa. Naomba Serikali yangu sikivu tutumie Ziwa Tanganyika. Tumepata mafanikio makubwa sana kwenye Ziwa Victoria, tumeilisha Mwanza, Shinyanga na sasa tunaelekea kuilisha Tabora na bado hapo hapo hata watu wa Mkoa wa Singida wanatamani maji ya Ziwa Victoria yafike. Tukiilisha maji Mkoa wa Katavi kupitia Ziwa Tanganyika tutakuwa tumeondoa kero kubwa sana ya maji kwa sababu yale maji yatapita kwenye maeneo mengi na kwenye vijiji vingi na hatma yake maji yatakuwa mengi katika Mkoa wetu wa Katavi na shida ya maji itakwisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niunge mkono hoja asilimia mia moja bajeti hii ya historia ya Chama cha Mapinduzi. Chama cha Mapinduzi tuna raha sana. Unajua ukifanya kitu kizuri lazima ujisifie, naunga mkono hoja asilimia mia moja, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nikushukuru kwa kunipa muda huu wa kuweza kuzungumzia Wizara hii muhimu sana kwa sisi akinamama. Naomba nimshukuru kwanza Mungu ambaye ametulinda siku hii ya leo, ametupa kibali tuko mahali hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa kazi kubwa ambayo anaendelea kuifanya, tunaona kwa ajili ya afya na pesa nyingi ambazo amezitenga tunaona na kushuhudia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze sana Waziri Mheshimiwa Ummy Mwalimu pamoja na Naibu wake kwa kazi kubwa nzuri. Kusema kweli Mheshimiwa dada Ummy Wizara ameiweza, lazima tumpongeze, Wizara ameiweza na ameimudu, hongera sana, Mungu ataendelea kukutetea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikipongeze Kitengo cha Jakaya, Profesa Janabi pamoja na Mkurugenzi wa Ocean Road, Kitengo cha Sukari, Meno, MSD kwa kazi nzuri ambayo walikuja Mkoa wa Katavi kupima afya za wananchi wa Mkoa wa Katavi. Naomba sana kazi hii Mungu ataendelea kuwalipa na waendelee kuwatumikia Watanzania kwa sababu Katavi ni mbali, lakini walikuja kuangalia afya za Watanzania wa Mkoa wa Katavi na wasichoke nitawaomba waje tena kuangalia kwa sababu walipunguza matatizo mengi ingawa hawakumaliza lakini matatizo waliweza kuyaona na kuweza kuyamudu kiasi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Katavi ni mkoa mpya. Tunajua Serikali katika ile mikoa mipya imepanga kujenga hospitali za mikoa. Mkoa wa Katavi 2017/2018 tulipangiwa bilioni moja, lakini pesa hii hatuwezi kuijua ilienda wapi, kwa sababu mpaka leo uwanja ule uko wazi

wala hakuna kitu chochote ambacho kilifanyika, wala kuonesha dalili ya kujengwa hospitali ya Mkoa wa Katavi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka huu vilevile sijaona kama tumepangiwa pesa au kuna dalili kwamba tumeambiwa kuwa tutajengewa hospitali ya mkoa sijaona dalili ya aina yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Mkoa wetu wa Katavi, jiografia ni mbaya sana. Nashukuru sana Mheshimiwa Ummy alifika alijionea uhalisia, maana angekuwa hajajionea uhalisia angesema sifahamu, lakini uhalisia wa Mkoa wetu wa Katavi anaufahamu vizuri sana. Nashukuru sana Mheshimiwa Ummy alikuja Mkoa wa Katavi na vilevile aliniahidi Wadi moja katika hospitali ya Manispaa ya Mpanda. Naisubiri sana hiyo Wadi ambayo aliwaahidi wananchi wa Wilaya ya Mpanda Manispaa, alisema atawajengea Wadi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishauri kwa sababu hii hospitali ya Mkoa inapangiwa pesa na mpaka sasa hivi hakuna kitu kinachoendelea, naomba kwa vile hospitali ya Manispaa ya Mpanda ina eneo kubwa sana na ndani ya hospitali ya Manispaa ya Mpanda tuna matatizo mengi makubwa kwa sababu majengo ya Wadi ni machache, Madaktari hatuna, Manesi ni wachache mno, Wahudumu ni wachache mno kusema ukweli!

Mheshimiwa Mwenyekiti, ile hospitali ya Manispaa ya Mpanda ndiyo imekuwa kama hospitali ya Mkoa, sasa wananchi wote wa Mkoa wa Katavi wanakwenda kwenye ile hospitali, wodi chache, vitanda hakuna! Sasa namwomba sana dada yangu Mheshimiwa Ummy, mpenzi wangu, atusaidie basi aongeze hata Wadi tatu ndani ya hospitali ya Manispaa ili tuweze kukidhi mahitaji ya wananchi wa Wilaya ya Mpanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba sana Mheshimiwa Waziri atusaidie kwa sababu wananchi wa Mpanda wanapata shida sana kimatibabu, ukiangalia vifaa tiba hatuna, vifaa tiba vyote, x-rays na kila kitu ni vibovu. Namwomba sana dada Ummy, Mheshimiwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto atusaidie vifaa tiba hatuna, wananchi wa Mpanda wanapata shida sana, wanakwenda Mbeya, wanakwenda Ikonda, lakini tukiiboresha hospitali ya Mpanda sidhani kama wananchi wa Mpanda watahangaika. Namwomba sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Ummy alikuja katika Mkoa wa Katavi akaenda katika Wilaya ya Mlele katika Tarafa ya Inyonga. Namshukuru alipandisha ile hospitali ikawa hospitali ya Wilaya, kile kituo cha afya cha Inyonga. Hata hivyo, mpaka leo hatujapata hati na kama hujapata hati ya kuwa hospitali ya Wilaya ina maana vitu vyote vinasimama, ina maana Madaktari wale bado wanaendelea kuwa Madaktari wa kituo cha afya na dawa zinaendelea kuwa zile za kituo cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ummy, akitusaidia kutupa hati kamili sasa kwa sababu jengo la mortuary limekwisha, kila kitu ambacho vile vigezo vyote walivyoviweka, vimekwisha, tunaomba hospitali ya Mlele ipatiwe hati iwe hospitali kamili ya Wilaya ya Mlele ili iweze kupunguza kasi ndani ya Manispaa ya Mpanda. Namwomba sana Mheshimiwa Ummy ili tuweze kupunguza matatizo kwa wagonjwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Wilaya yetu ya Manispaa ya Mpanda tuna vituo viwili vya afya. Vituo hivyo ni kituo cha Ilembo pamoja na Mwangaza. Vituo hivi havijapangiwa pesa, Mheshimiwa Ummy naomba atuoneshe katika hivi vituo vya afya ambavyo vinapunguza kasi ya uzazi salama, kwa ajili ya msongamano pale Makao Makuu Manispaa na hajavipangia pesa. Naomba Mheshimiwa Waziri kesho wakati anafunga basi atanionesha vituo hivi viwili vya afya, Kituo cha Afya Ilembo pamoja na Mwangaza pesa yake iko wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tunahitaji Kituo cha Afya kati ya Mwamkulu na Kakese kwa sababu ni distance ndefu kuja Mjini vilevile kuna watu wengi zaidi. Tulikuwa tunahitaji kituo cha afya katika maeneo hayo ya Mwamkulu na Kakese. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru masuala ya Bima ya Afya hususan Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya. Nashukuru Mfuko huu unafanya kazi vizuri sana na Mkurugenzi anafanya kazi vizuri sana, ndani ya mikoa yote vituo vipo na wafanyakazi wapo. Hata hivyo, kila Mtanzania anahitaji kutibiwa vizuri na vilevile katika mfumo wao waliouweka ndani ya makundi kuwapa kikundi cha SACCOS na kadhalika ndiyo uwalipie Bima ya Afya Sh.79,000 ni sawa, lakini kila Mtanzania anahitaji matibabu, naomba huu mfuko…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia Wizara hii muhimu sana kwa ajili ya wananchi pamoja na akina mama. Naomba nimshukuru Mungu ambaye ametupa uzima na sasa hivi tupo muda huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Maji pamoja na Naibu wake, Kaka yangu Mheshimiwa Kamwelwe kwa kazi kubwa nzuri anaoyoifanya, anafanya kazi nzuri sana lakini Wizara yenyewe ndiyo ngumu, wananchi wanatakiwa watuliwe ndoo ya maji kichwani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nizungumzie Mkoa wangu wa Katavi hususan Wilaya ya Mpanda, Makao Makuu ya Mkoa wa Katavi. Naomba niipongeze Serikali ilileta miradi; Mradi wa Ikorongo I na Ikorongo II, lakini siku hadi siku watu wanaongezeka. Tulivyotegemea kuwa labda Ikorongo I katika vyanzo vile vya maji, yale maji yanaweza kututosheleza wananchi wa Wilaya ya Mpanda, imekuwa tofauti. Naishukuru Serikali haikuchoka, ikaongeza mradi mwingine tena wa Ikorongo II, lakini bado. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna tatizo kubwa sana ndani ya Wilaya ya Mpanda hususani pale mjini. Serikali ilijitahidi kutuletea maji, mabomba yale makubwa, lakini bado ndani ya maeneo yetu, miundombinu ya maeneo husika ambayo yanatakiwa yapelekwe maji hatukuweza kubadilisha ile miundombinu, ipo vilevile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, miundombinu ya zamani, ilikuwa ni yale mabomba ya zamani ya chuma. Mabomba ya chuma yanaota kutu. Sasa kama yanaota kutu, sidhani kama yanaweza kuchukua au kubeba mzigo mzito ambao unakuja kutoka katika matenki yetu. Maana yake maji kwenye matenki yanajaa, lakini sasa kwenye kupita njiani kule, lazima kuna mfumuko yale maji yanaweza kuvuja na mabomba yanapasuka. Sasa imekuwa shida sana pale Wilaya ya Mpanda maji ni shida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninajua Serikali bado ina jitihada kubwa na sasa hivi kwenye bajeti ya Wilaya ya Mpanda nimeona shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya marekebisho mbalimbali kwa ajili ya matengenezo pale mjini. Bado kunatakiwa kazi kubwa sana kwa sababu wananchi wa Mpanda hawana maji kabisa sasa hivi, hususani Makanyagio, Majengo na Kashaulili ambapo ndiyo katikati ya Makao Makuu ya Mkoa wa Katavi pale Wilaya ya Mpanda. Hawana maji kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia huu mradi wa Ikorongo, tulijenga magati Ilembo na Airtel. Magati haya katika Kata ya Ilembo, sasa hivi hayatoi maji kabisa. Airtel nako kwenye yale magati hayatoi maji. Katika huu Mradi wa Ikorongo nao vilevile haujaweza kutimiliza kwa sababu wataalam wamesema yanaweza kufika asilimia 50 tu wananchi wa Mpanda wakapata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi Mwenyezi Mungu ametupa bahati kubwa sana. Ninashukuru Serikali kwa Mkoa wa Mwanza na Shinyanga wametoa maji kutoka Ziwa Victoria, Mungu ametupa neema yake, tumepata maziwa na mito. Sasa naomba nasi ndani ya Mkoa wetu wa Katavi, Mungu ametupa neema, tuna Ziwa Tanganyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakitupa maji ya Ziwa Tanganyika, shida ya maji itakwisha kabisa katika Mkoa wa Katavi kwa sababu maji ya Ziwa Tanganyika yatatumika ndani ya Wilaya yetu mpya ya Tanganyika; Wilaya nzima itapata maji ya Ziwa Tanganyika, tutakuja sisi Wilaya ya Mpanda na Halmashauri ya Nsimbo wote watapata maji ya Ziwa Tanganyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali yangu sikivu na kaka yangu Mheshimiwa Kamwelwe, sasa hivi afanye mipango ya kuleta maji kutoka Ziwa Tanganyika ili wananchi wa Mkoa wa Katavi waweze kupumua kwa sababu maji vijijini hakuna na ukiangalia Makao Makuu ya Mkoa hatuna maji. Naomba sana hilo liweze kushughulikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Mkoa wetu wa Katavi, katika Mkoa lazima sasa tuanze system ya majitaka. Ndani ya Mkoa wetu wa Katavi hatuna system ya majitaka kabisa wala gari na matokeo yake mvua zikinyesha ni adha kubwa sana ndani ya Mji wa Mpanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali yangu sikivu, iweke mipango mikakati, nimemsikia Mheshimiwa Waziri kuna sehemu ambayo tayari miundombinu ya majitaka kwa mikoa kadhaa basi sasa na sisi Mkoa wetu wa Katavi ni mkoa, Wilaya ya Mpanda ni Makao Makuu ya Mkoa, tuanze sasa hivi mpango wa kujenga majitaka au basi tutafutiwe gari la kuweza kunyonya majitaka kwa sababu hatuna gari, hatuna kitu chochote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye umwagiliaji; ninaishukuru Serikali, mipango ni mizuri sana ya umwagiliaji, lakini sisi tulijengewa miradi ya umwagiliaji Urwila, Ugala, Halmashauri ya Nsimbo, Kamsisi na Kata ya Mbede, lakini ile miradi sijaona kama imefanya kitu chochote. Naomba niulize swali moja, Mheshimiwa Waziri, hii miradi ya umwagiliaji hivi kwa nini tunatumia gharama kubwa sana lakini wananchi hawanufaiki kabisa. Leo hii ukiniambia Urwila wamenufaikaje kwa umwagiliaji, hakuna wananchi wa Urwila waliofaidika kwa ajili ya umwagiliaji na pesa nyingi sana zimetumika pale. Vilevile Kamsisi na Ugala pesa nyingi sana zimetumika, halafu tukija Mbede pesa nyingi zimetumika lakini miradi ya umwagiliaji bado hatujafanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa ninaomba Serikali ijipange upya, miradi ya umwagiliaji bado hatujafanikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kazi kubwa na nzuri ambayo inaendelea kufanyika, lakini ninaomba kuunga mkono hoja Mamlaka ya Maji Vijijini. Mamlaka hii itatusaidia sana kwa sababu wananchi wa Vijijini wengi wao ndani ya vijiji vyetu hatuna maji, lakini mamlaka hii ikiundwa itatusaidia sana kwa sababu itafanya kazi vizuri. Tulianzisha TARURA, tumeona jitihada za TARURA, nafikiri tukianzisha Mamlaka ya Maji Vijijini nayo inaweza kutusaidia sana akina mama, tutawatua ndoo kichwani. Naomba niunge mkono hoja hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba katika ile shilingi 50 tuongeze iwe shilingi 100 ili sasa mamlaka hii iweze kuwa na nguvu... (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Ahsante sana naomba nipongeze.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nimshukuru Mungu ambaye ametupa uzima na uhai mpaka leo tuko mahali hapa. Naomba nikushukuru sana kwa kunipa nafasi, naomba nimpongeze sana Waziri kwa kazi kubwa ambayo anaifanya pamoja na Naibu wake, wanafanya kazi kubwa sana kusema kweli. Lazima tuwape pongezi kwa sababu wamejitahidi kadiri ya uwezo wao, lakini Mungu ataendelea kuwasimamia kwa sababu kazi mnayofanya ni ngumu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Katibu Mkuu wa Wizara hii naye anajitahidi sana. Ni mama, naomba nikupongeze mama yetu, endelea kufanya kazi, Mungu ataendelea kukusimamia na kukupigania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Rais kwa kuona sasa jukumu la ardhi ni kubwa ameona kwenye manispaa, halmashauri, vile vitengo vyote vitoke viwe vinaripoti kwa Katibu Mkuu moja kwa moja ili kurahisisha kazi iweze kuwa nzuri zaidi. Naomba nimpongeze sana Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ametufanyia kazi kubwa, sasa tunajua Wizara imekuwa Wizara kamili kwa ajili ya kazi ambayo inatakiwa kufanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Mkoa wetu wa Katavi; Katavi ni mkoa na pale Mpanda Mjini ni Manispaa. Tuna Maafisa wachache sana wa Ardhi na Mkoa wa Katavi unakua kwa kasi kubwa sana. Mkoa wetu wa Katavi maeneo mengi hayajapimwa, hususan Mji Mkongwe pale Mpanda Mjini, Kata ya Kashaulili; ule mji umepimwa lakini wananchi wale hawajapata hati mpaka leo. Tunajua hati ni muhimu sana ndani ya maisha yetu ya kifamilia maana hati ndio msingi wa maisha ya kila jamii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Wizara ya Ardhi ndani ya Mkoa wetu wa Katavi kwa sababu sasa hivi imekuwa ni Wizara ya Ardhi, tunaomba watuongezee watumishi, hatuna watumishi kabisa. Ndiyo maana sasa hivi ukiangalia Mpanda migongano ya ardhi imekuwa ni mikubwa sana kutokana na kwamba watumishi hatuna na wananchi wanajenga kiholela. Sasa ukija upimaji inakuwa ni shughuli kwa sababu viwanja vile vinagongana na maeneo mengi yanakuwa kuna migongano ya ardhi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Kata yetu ya Semulwa, Mtaa wa Kichangani, haujapimwa kabisa na ni ndani ya Manispaa ya Mpanda Mjini, haijapimwa kabisa. Naomba Wizara ya Ardhi sasa hivi kwa sababu, imeshakuwa Wizara kamili ndani ya maeneo yetu husika, tunaomba tuletewe Wilaya ya Mpanda wafanyakazi wa kutosha, ili migogoro ya ardhi Mpanda iweze kupungua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna Kata ya Mpanda Hoteli na Kata ya Ilembo. Wananchi wa Mpanda Hoteli na Kata ya Ilembo walikuwa wana mashamba walikuwa wanalima kwa muda mrefu, lakini sasa imekuja kuwa migongano na jeshi; jeshi wanasema ile ardhi ni ya kwao, wananchi wanasema ardhi ile ni ya kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Wizara ya Ardhi, Mheshimiwa Waziri au Naibu Waziri pamoja na Wizara ya Ulinzi, tuje tutatue hili tatizo Mpanda. Ni tatizo kubwa mno kiasi ambacho ni mfarakano kusema kweli, naomba sana msaada wao, waje mtatue tatizo hili. Wananchi wanasema ardhi ni ya kwao na Jeshi wanasema ardhi ni ya kwao. Sasa migongano hii; na ukizingatia ndani ya Wilaya ya Mpanda imekuwa ni Mkoa, tunahitaji nafasi kubwa zaidi. Nashauri Jeshi waweze kutafutiwa sehemu nyingine, yale maeneo wapewe wananchi kwa sababu migongano yao haifurahishi kusema kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Wilaya yetu ya Mpanda tulijengewa nyumba za National Housing. Tunaishukuru sana Serikali pamoja na shirika lenyewe, limejenga nyumba nzuri sana lakini hapa kuna tatizo. Hizi nyumba zimejengwa kwa sasa hivi ni takriban miaka kama mitano iliyopita. Hizi nyumba hazina watu na zimekwisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hapa kuna tatizo; wamepanga sijui, wamenunua watu takriban kama sita tu katika nyumba mia mbili na kitu. Sasa sielewi: Je, hizi nyumba bei yake ni kubwa au National Housing hawana mpango mkakati wa kuweka hizi nyumba ziweze kupangishika kwa bei nafuu, wakawapangisha wananchi? Sasa hapo sielewi, kwa sababu zile nyumba sasa hivi zinaishi nyoka, manyasi yamelundikana pale, hazifanyiwi ukarabati wa aina yoyote. Kwa kawaida ukijenga nyumba, kama haiishi binadamu nyumba ile inakuwa boma. Sasa nyumba hizi zimetumia pesa nyingi sana za Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana hizi nyumba, National Housing watafute jinsi ya kufanya; aidha, wapunguze bei wapangishe wafanyakazi ambao wako ndani ya Mkoa wa Katavi, kwa sababu Katavi sasa ni Mkoa. Wawapangishe wafanyakazi wa Mkoa wa Katavi au waende wawakopeshe wafanyakazi wa Serikali ndani ya Manispaa, Halmashauri ili zile nyumba ziweze ku-survive kwa sababu pesa nyingi zimetumika kujenga zile nyumba na ni nyumba nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Serikali itumie hekima kwa hizi nyumba za National Housing zilizojengwa kwenye Wilaya. Walijenga kwa manufaa ya Watanzania ili kupitia Serikali yao waweze kupata nyumba hizo kwa bei nafuu. Sasa kutokana labda na kuuziwa viwanja vile kwa bei kubwa na wenyewe wanataka kuweka bei kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba niunge mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Vilevile nimshukuru sana Mungu kwa kibali alichotupa katika Bunge hili la Bajeti, tunamwomba aendelee kutulinda na kututunza katika Bunge mpaka tumalize.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze sanaMheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kazi kubwa anayoifanya katika kusimamia na kuhimiza maendeleo ndani ya nchi yetu. Vilevile naomba nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa ambayo anaifanya katika ziara ya nchi yetu kwa ajili ya kuangalia juhudi na maarifa ya Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze sana Waziri, Mheshimiwa Jenista Mhagama pamoja na wasaidizi wake, Mheshimiwa Mavunde pamoja na Mheshimiwa Ikupa kwa kazi kubwa wanayoifanya. Tumeona jinsi gani Mheshimiwa Ikupa anavyokwenda kufanya kazi katika mikoa, kuangalia jitihada za walemavu. Nataka nimkumbushe tu Mheshimiwa Ikupa, ametembea katika mikoa mingi, naomba basi Katavi nako wanamsubiri aje kuongea na walemavu wa Mkoa wetu wa Katavi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naipongeza Serikali kwa kutuletea Mkoa wa Katavi bilioni moja kwa ajili ya uanzishwaji wa Hospitali ya Mkoa, tunashukuru sana na vilevile mmetuletea fedha kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya Mkoa pamoja na nyumba ya Mkuu wa Mkoa. Nilizungumzia bajeti ya mwaka jana, lakini utekelezaji umeshafanyika, naomba niipongeze sana Serikali kwa sababu inafanya kazi kwa vitendo. Naomba tuwashukuru sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, mkoa wetu sisi una uhaba mkubwa sana wa watumishi, hususan kwenye Halmashauri zetu pamoja na ndani ya ofisi za mkoa. Ndani ya mkoa wetu kuna takriban ya wafanyakazi elfu sita mia saba na kitu. Ina maana kuwa tunatakiwa tuwe na wafanyakazi elfu sita na kitu, lakini ndani ya mkoa wetu kupitia Halmashauri zote tuna wafanyakazi takriban elfu nne na upungufu wetu kama elfu mbili hivi, kwenye sekta ya afya, kilimo pamoja na elimu. Nategemea Serikali yangu sikivu, hivyo itatuongezea staffskwa sababu mkoa wetu una uhaba sana wa wafanyakazi, tunaomba wasitusahau kwa ajili ya utendaji kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya mkoa wetu sisi na sasa hivi ni sera ya viwanda, hatuna umeme wa uhakika sana, tunaomba Serikali itusaidie kutuletea umeme wa grid ya Taifa ili wananchi wa Katavi waweze kujenga viwanda kwa sababu sera yetu ni ya viwanda. Tunaombasana kwa sababu umeme wetu si wa uhakika kabisa, tunaomba grid ya Taifa iweze kutufikia katika Mkoa wetu wa Katavi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wetu wa Katavi, ma- DC wetu toka wateuliwe, hawajawahi kupata magari mapya na ukizingatia jiografia ya Mkoa wa Katavi ni ngumu sana, wanabahatisha tu magari, wanachukua magari ya watendaji ndio wanafanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashukuru kwa kuwakumbuka kuwajengea nyumba na wameshawaletea fedha kwa ajili ya nyumba za Wakuu wetu wa Wilaya, lakini vitendea kazi, ukianzia mkoani mpaka hata Mkuu wa Mkoa mwenyewe, gari hana, kwa sababu gari lake lilipata ajali, mpaka leo anatumia tu magari ya kubahatishabahatisha.

Sasa niaomba Serikali yangu iangalie sanaMkoa wa Katavi, upande wa ma DC wetu, wanafanya kazi kubwa sana ya kuhamasisha maendeleo ndani ya mkoa wetu na kusimamia maendeleo ndani ya mkoa wetu, lakini vitendeakazi hawana na Halmashauri zetu hazina magari kabisa mpaka mkoa. Naomba Serikali yangu sikivu iangalie Mkoa waKatavi kwa ajili ya vitendea kazi ili waweze kuendelea kufanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja sasa kwenye mambo yetu ya uchumi, naomba niishauri Serikali yangu, najua Wabunge wengi wamesema, wamezungumzia kuhusu masuala ya uvuvi, najua zamani ndani ya Wizara yetu ya Uvuvi, tulikuwa tuna Shirika lilikuwa linaitwa TAFIRI, lilikuwalinavua samaki na samaki wale walikuwa wanawasaidia sana Watanzania kwa kuwapata kwa bei nafuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile naomba niipongeze Wizara ya Mifugo, pamoja na Uvuvi kwa kuweka Dawati la Sekta Binafsi kupitia Uvuvi, wamefanya vizuri sana. Naomba nimpongeze sana Waziri, Mheshimiwa Mpina pamoja na Naibu wake ninajua dawati hili linafanya kazi vizuri sana na usimamizi unaendelea kuwa mzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika,naomba niikumbushe Serikali yangu, naomba sana, tununue meli yetu. Kazi aliyofanya Mheshimiwa Mpina na Naibu Waziri wamefanya kazi kubwa, sasa hivi samaki kwenye maziwa ni wakubwa kwelikweli. Tulienda Mwanza, wenyewe tulishuhudia jinsi gani kazi imefanyika, mpaka samaki wakubwa wapo katika maziwa yetu.

Sasa tukinunua meli kupitia bahari, meli ikafanya kazi hiyo ya kuvua kwenye maziwa, nafikiri Tanzania yetu itapata uchumi mkubwa, Taifa litafaidika na vilevile wananchi wetu watafaidika kupitia uvuvi. Ukizingatia sasa hivi wenzetu Uganda na Kenyawamefungua viwanda vingi sana kwa ajili ya kuchakata samaki, sisi ndani ya Tanzania kupitia Mkoa wetu wa Mwanza tuna viwanda vichache sana kwa ajili ya uchakataji wa samaki.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niipongeze Serikali kwa kazi kubwa kwa upande wa mifugo, tumejenga sana viwanda na tumeshuhudia, Longido tumeona kiwanda kikubwa cha machinjio kwa ajili ya kusindika mifugo yetu.Hata hivyo,ng’ombe wengi wanasafirishwa kupelekwa Kenya.

Naomba, kwa sababu na sisi Tanzania tunataka kusindika mifugo yetu, tupunguze tozo. Tumekuta pale tozo ni kubwa sana kwa upande wetu wa Tanzania, naiomba sana Serikali yetu sikivu ili tuweze kufaidika na usindikaji wa mifugo yetu, basi ninaomba tupunguze tozo ili wale Watanzania wa Longido waweze kuuza mazao yao ndani ya nchi yetu sisi wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, sasa hivi naipongeza Wizara hii, inafanya kazi vizuri, sasa hivi ngozi. Sisi tumesema sera ya viwanda, ngozi nyingi zinasafirishwa nje ya nchi na sisi tunazitaka hizo ngozi zibaki Tanzania. Naomba sana ngozi hizi zibaki katika nchi yetu kwa sababu ni sera yetu ya viwanda, viatu vitengenezwe hapahapa ili uchumi wa Tanzania uweze kukua.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile ninakuja kwenye sekta ya maziwa, naomba kuipongeza Serikali, sekta ya maziwa inakuana inatuletea kipato kikubwa ndani ya nchi yetu, tumeona, sisi wenyewe tumefanya ziara, kuna viwanda vya maziwa ambavyo vinafanyakazi vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kupita huko, tumekuta matatizo machache, kwa sababu ndani ya maeneo yetu…

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari!

MBUNGE FULANI: Tayari, unga mkono.

MHE. ANNA R. LUPEMBE:Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sanana naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi siku ya leo kuweza kuchangia Wizara hii muhimu sana katika maisha ya wanadamu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshukuru Mungu ambaye ametuumba na kutupa uzima na uhai na ametupa kibali siku ya leo, tu wazima tukiendelea kutenda kazi ya Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa ambayo anaifanya kwenye sekta hii ya afya. Mkoa wa Katavi tunajivunia sana jinsi pesa za Wilaya pamoja na Mkoa zilivyokuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwapongeze Waziri pamoja na Naibu Waziri, Mheshimiwa Ummy hongera sana kwa kazi. Mwanamke mwenzetu unafanya kazi lazima tukusifie na tunaendelea kukuombea Mungu aendelee kukupa nguvu kwa sababu Wizara hii ni ngumu, inahusu wanadamu, tunaendelea kumsihi Mungu aendelee kukutetea katika kazi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wa Mkoa wa Katavi tushukuru katika bajeti ya mwaka 2017/2018 tuliletewa shilingi bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Mkoa. Vilevile katika Wilaya za Tanganyika na Mlele pamoja na Jimbo la Kavuu tumeletewa pesa kwa ajili ya kujengewa Hospitali ya Wilaya. Tunaishukuru sana Serikali kwa kazi kubwa wanayoendelea kuifanya kwa ajili ya kuwatibu Watanzania hususan wa Mkoa wa Katavi. Sisi tunajivunia sasa vifo vya akina mama wajawazito na vifo vya utotoni vitapungua kwa asilimia kubwa sana kwa sababu tulikuwa tuna asilimia kubwa sana. Kupitia jitihada kubwa za Serikali mambo yataendelea kuwa mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Mkoa wetu wa Katavi, Manispaa ya Mpanda tuna Hospitali Teule ambayo imeteuliwa kama ndiyo sasa Hospitali ya Mkoa. Hii hospitali ina mabweni manne tu. Katika wodi ya wazazi kuna sehemu wameweka kwa ajili ya kulea watoto njiti. Naomba sana Wizara itusaidie kwa sababu hospitali zote za Mkoa na hii tayari teule Mheshimiwa Ummy na wewe uliniahidi kuwa utatujengea bweni moja katika Hospitali ile Teule ya Mkoa wa Katavi, Manispaa ya Mpanda. Wale watoto njiti wanakaa pamoja na mama zao humohumo watu wakienda kuwatizama, nafikiri unajua watoto njiti wanatakiwa wakae katika hali ya usalama zaidi ili waweze ku-survive.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na matatizo ya mabweni haya kuwa machache, wodi ile ya magonjwa mchanganyiko ipo moja tu. Wodi ile wanalazwa watu wazima, watoto kuanzia miaka 5 mpaka 13, ina maana hawa watoto ni wadogo. Pia wagonjwa wanaoingia katika wodi ile ni mahtuti watoto wale wanashuhudia vifo vya wagonjwa mle ndani, ina maana tunawapa woga wakiwa wadogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Mkoa wa Katavi hususan Wilaya ya Mpanda Manispaa tunaomba Mheshimiwa Ummy utujengee mabweni mawili mengine…

MBUNGE FULANI: Ni wodi.

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Wodi ndiyo mabweni Waheshimiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba tujengewe wodi mbili ili hawa watoto umri wa kuanzia miaka mitano wawe wana wodi yao kwa sababu kisaikolojia tunawapa uwoga kwa sababu wakati mwingine wako kitanda kimoja na mkubwa yule mkubwa anafariki pale yeye anaendelea kuweweseka. Katika maisha yake anakuwa na uwoga, tunamjenga hofu katika maisha yake yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ummy alishakuja Mkoa wa Katavi Manispaa na aliona hospitali ile jinsi ilivyo tunaomba tujengewe wodi mbili. Tunashukuru mmetuletea shilingi bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Mkoa na jumla ya fedha zote mpaka hospitali iishe ni shilingi bilioni tisa. Mmetupa shilingi bilioni 1 nafikiri na sasa hivi mtatupa shilingi bilioni 1 ina maana mpaka ujenzi uishe ni miaka tisa ijayo tutakuwa bado tuna matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Waziri utuongezee fedha ili Hospitali ya Mkoa iweze kuisha haraka. Tukipiga hesabu ya shilingi bilioni moja moja ile hospitali itaisha baada ya miaka tisa mbele ya safari. Ina maana kuwa lazima tupate msaada wowote ili ile Hospitali Teule iweze kurekebishwa mambo mbalimbali ili iweze kukidhi haja ya wananchi wa Mkoa wa Katavi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya hospitali hii watumishi ni wachache sana na ndiyo teule na tunaitegemea kama Hospitali ya Mkoa. Hatuna madaktari bingwa wanaokidhi haja ya kutibu magonjwa mbalimbali. Ndiyo maana unakuta wananchi wengi wa Mkoa wa Katavi wanahangaika sana. Wengine wanafia nyumbani kwa sababu akienda hospitali kumefurika, hapati matibabu halisia, vifaatiba hatuna na manesi ni wachache. Tunaomba mtusaidie ili hospitali hii iweze kukidhi vigezo vinavyohitajika kimkoa. Wakati mnaoendelea kutuletea pesa na hii hospitali iendelee kufanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakuja upande wa bima ya afya. Bima ya afya ni kiwango kikubwa sana na Watanzania uwezo wao bado ni mdogo, Sh.1,500,000 mtu aweze kukata bima ya afya ni pesa nyingi sana. Wengi wanakufa wakiwa nyumbani kwao na mimi mwenyewe nashuhudia. Sasa hivi tuna maradhi makubwa makubwa ya moyo, kansa, figo aje Benjamin huku na hana bima matokeo yake huyu mtu anakufa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ile bima ya afya tuliweka ya vikundi ya Sh.79,000 tuichanganue akate mtu mmoja mmoja mwenye uwezo, tumpe fursa akate hiyo bima. Naomba niipongeze Serikali mmeleta bima ya mkoa ya Sh.30,000 wananchi wameitikia lakini sasa unakwenda kwenye Hospitali ya Mkoa hakuna vile vifaa mfano moyo umepanuka wanakwambia nenda Muhimbili, ukienda Muhimbili ile bima haifiki kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba hii bima tui- separate tufanye hata Sh.100,000 yule mwenye uwezo aweze kukaa Bima hii ya Taifa ili aweze kutibiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona kwenye kitabu chake ukurasa wa 85, Mheshimiwa Ummy anataka kuleta sheria kwa ajili ya bima ya afya. Naomba nikupongeze sana, tuletee hii sheria tuweze kurekebisha yale mapungufu ili Watanzania waweze kupona. Watanzania wengi wanakufa majumbani, kuna wagonjwa majumbani mpaka unashangaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye magari ya wagonjwa ndani ya Mkoa wetu wa Katavi. Jiografia ya Mkoa wa Katavi ni ngumu mno. Tunaomba mama yetu atupe hata ambulance tatu tu ziweze kutusaidia kwani tuna shida. Mheshimiwa Ummy ni msikivu naamini atatusaidia haya magari ya wagonjwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wale mabinti zako wa Kalema Girls Mheshimiwa Waziri wanakukumbusha ile bajaji uliowaahidi kwa ajili ya matibabu ya asubuhi. Usisahau, naomba nalo unijibu utawaletea lini hiyo bajaji. Nafikiri ulisahau, naomba nikukumbushe bajaji Kalema Girls.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende maendeleo ya jamii. Ndani ya Mkoa wetu tuna Chuo cha Msaginya na safari hii kimepata bahati mbaya kimeshaungua mara mbili. Katika hotuba ya Waziri kuna vyuo ambavyo vimepatiwa pesa ya marekebisho na amesema vimefanya kazi nzuri kwa ajili ya hamasa mbalimbali. Nakuomba Mheshimiwa Waziri utusaidie hiki Chuo cha Msaginya kiweze kufanya kazi kama Vyuo vingine vya Maendeleo ya Jamii. Chuo hiki kwa Wanakatavi ndiyo kitakuwa msaada mkubwa sana kwa sababu tumeona vyuo vya wenzetu vimefanya kazi nzuri. Ukitupatia fedha na kikafanyiwa marekebisho mazuri, nafikiri Wanakatavi wanaoishia darasa la saba wataenda kujifunza kozi mbalimbali na kupata manufaa ya Chuo hiki cha Msaginya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia 100.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia muda huu. Naomba nimshukuru Mungu kwa kutulinda mchana kutwa na ametupa fursa tena kwa mara nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Waziri pamoja na Naibu Mawaziri wote wawili kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya. Kusema kweli Mheshimiwa Hasunga hongera sana, tunamwona jinsi anavyokimbizana. Nafikiri mafanikio kupitia kilimo kwa Watanzania yatawezekana, hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Mkoa wetu wa Katavi tunalima zao la tumbaku. Zao hili sasa hivi limeweza kuyumba kwa sababu, makampuni ambayo yanakuja kuchukua zao hili katika Mkoa wetu wa Katavi wameleta makisio kwa wakulima, kila mwaka wanaweka makisio, sasa kila siku wananchi wa Katavi wanavyopewa yale makisio sio ya kupanda ila makisio yale ya kushuka. Sasa kutokana na hiyo uchumi kidogo wa Mkoa wetu wa Katavi umepungua kwa sababu zao hili kupitia halmashauri zetu zilikuwa tunapata manufaa makubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba kwa sababu, zao hili ni zao la kibiashara. Najua Waziri ana mikakati mingi mikubwa, mipana, naomba hili zao lifufuliwe upya, tutafute wadau ambao watakuja kununua zao letu la tumbaku kwa sababu, sasa hivi Mkoa wetu wa Katavi kupitia halmashauri zetu mapato yamepungua sana. Sasa sio kwenye halmashauri zetu tu hata Taifa mapato yameshuka, naomba tukazie mkazo kupitia tumbaku zao hili liweze kutafutiwa wadau ili waweze kununua katika msimu ujao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niipongeze Serikali, katika Mkoa wetu wa Katavi msimu huu na msimu uliopita tulilima pamba. Pamba imeitikiwa sana hususan katika Wilaya yetu ya Tanganyika wamelima takribani kilo milioni 16 wananchi wameweza kufanikiwa kupata. Naomba sasa Bodi ya Pamba iweze kuja kuchukua kwa sababu, wananchi wetu wa Katavi pamba hiyo wameivuna wameweka majumbani. Sasa ili tuweze kupata manufaa makubwa na wale tuweze kuwapa hamasa kubwa wananchi wa Mkoa wa Katavi tunaomba basi hii Bodi iweze kuja kununua ili sasa wananchi hawa waweze kutafuta mbegu nyingine kwa ajili ya msimu ujao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja katika mbolea. Pembejeo ni kitu muhimu sana, naomba, ndani ya nchi yetu tuna mazingira tofauti ya hali ya hewa. Ukiangalia Mkoa wa Katavi, Rukwa, Kigoma mvua zinaanza kunyesha mwezi wa Kumi, Kigoma mwezi wa Tisa katikati mvua zinaanza kunyesha. Sasa pembejeo zinakuja Mkoa wa Katavi Januari, je, Januari huyu mkulima atapata manufaa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkulima hawezi kupata manufaa hata kidogo. Vilevile sasa hivi kuna matapeli wengi wanawaletea wakulima wetu pembejeo feki ambazo hazina tija kwa sababu, wanajua kabisa huku mjini watu wanaelewa; wanajua kuwa wakipeleka vijijini kule watu hawaelewi wanawapelekea pembejeo, wanawapelekea viatilifu ambavyo ni vya bandia, fake, sasa tija inakosekana. Mkulima analima akiweka ile mbolea, vile viatilifu havina manufaa katika ule mmea, sasa wananchi wetu wanapata hasara. Naomba kwa sababu tuna Shirika la ASA, shirika hili ni zuri sana, sasa hivi shirika hili linafanya kazi nzuri na ukizingatia sasa hivi wanajiendesha wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wao wanalima mbegu na mbegu yao ni bora halafu wanauza bei rahisi. Kwa kilo ya alizeti wanauza Sh.3,500 lakini tukienda madukani mbegu ileile inaizwa Sh.35,000 mpaka Sh.70,000, sasa tuimarishe Shirika hili la ASA ili sasa Watanzania waweze kupata tija kwa sababu, shirika hili litafanya kazi nzuri zaidi. Vilevile shirika hili halipati pesa miaka mitano sasahivi hawajapeleka pesa kwenye Shirika la ASA. Naomba tuliimarishe Shirika hili la ASA litakuja kuwaletea tija Watanzania kwa sababu ni shirika la wazalendo, sasa sidhani kama wanaweza wakafanya vitu tofauti, vilevile hizi mbegu fake, viatilifu fake, vitapotea shirika hili tukiliimarisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naenda kwenye umwagiliaji. Kwetu Mpanda, Wilaya ya Tanganyika, Kata ya Kalema tulipeleka pesa kwa ajili ya umwagiliaji, ile skimu haijamalizika mpaka leo. Wanajua kama hizi skimu zinatumia pesa, wakandarasi, siku hadi siku value for money inabadilika, ina maana hii skimu sasa hivi haiwezi kufaa tena na wananchi wa Kalema hawawezi kupata tija. Sio Kalema tu katika Mkoa wetu wa Katavi kuna Kata ya Ugala, skimu yake mpaka leo ilimalizika, lakini haifanyi kazi, ina maana kuwa inaharibika haitaendelea kufanya kazi vizuri. Tuna Kata ya Urwila skimu yake haijakaa vizuri, tuna Kata ya Mbede skimu yake nayo haijakaa vizuri, naomba katika kata hizi ambazo tumeweka umwagiliaji, umwagiliaji ndio mkombozi wa Watanzania. Tukiweka skimu hizi vizuri, hawa wananchi wakilima mara mbili mara tatu tutapata faida kubwa na mazao mengi yataweza kuonekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya nchi yetu ya Tanzania kuna Kanda ambayo Iringa, Njombe, Ruvuma, Songwe, Rukwa, Katavi, katika zone hii ni wakulima sana wa mahindi. Sasa hivi ukiangalia katika nchi ya Zaire kuna uhaba sana wa chakula wananchi wengi wanapeleka mazao yao Zaire na sisi ndani ya Mkoa wetu wa Katavi kupitia Kata yetu ya Kalema inajengwa bandari pamoja na Rukwa inaweza kujengwa bandari, ili kanda hizi zote wakapeleka mazao yao katika Bandari ya Kalema pamoja na Kasanga, mazao haya yakapelekwa Zaire Watanzania hawa wakapata kipato kupitia bandari hizo mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana kwa sababu, nchi ya Zaire hakuna chakula, Burundi wanategemea sana Tanzania, tukiweka mazingira mazuri nafikiri tutapata mafanikio makubwa sana. Naomba sana kupitia Waziri Mheshimiwa Hasunga, najua alikuwa anafanya ziara sana wakati ule alivyokuwa maliasili...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba niunge mkono hoja. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuzungumzia Bajeti yetu ya Taifa kwa siku hii ya leo. Kwanza kabisa ninaomba nimshukuru Mungu aliyetuumba ametupa uzima na uhai leo tunazungumzia bajeti yetu ya Nne kwa ajili ya Awamu ya Tano. Namshukuru sana Mungu.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba niipongeze sana Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi kubwa sana ambayo imeifanya mpaka leo kupitia miradi mbalimbali ambayo Watanzania wanaona miradi inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ile ya manufaa ya wananchi wa Tanzania kwa sababu inaonekana na pesa ambazo zinapelekwa kwenye miradi ile na ile miradi inaonekana siyo kusema labda haionekani, inaonekana sasa ndiyo maana watu wanahangaika sana kwa ajili ya hiyo miradi, kwa sababu italeta mafanikio makubwa sana katika nchi yetu na Watanzania watanufaika sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna Mtanzania yeyote ambaye anafunga mkanda Watanzania wote wameridhika wanafanya kazi zao kwa sababu wamejua wanatakiwa wafanye kazi ili Tanzania iweze kwenda juu na tumeona kabisa jinsi gani Serikali imefanya kazi kubwa na leo hii uchumi wetu umepanda asilimia 7.1. Hongereni sana Serikali msirudishwe nyuma songeni mbele.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango pamoja na Naibu wako, mnafanya kazi nzuri sana na kazi mnayoifanya tunaiona na jitihada mnazozifanya tunaziona na mmekuwa wasikivu tunavyowaelekeza ndiyo mnavyofanya, hongereni sana endeleeni kuwa wasikivu nchi yetu itasonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Awamu zote Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi ilisema itaunganisha Mikoa kwa ajili ya uchumi, Mkoa kwa Mkoa lazima barabara za lami ziweze kufunguka kwa ajili ya uchumi wa Watanzania, ni jambo zuri na imefanyika tumeona kila sehemu barabara za lami zimejengwa na watu wanafanya shughuli zao za maendeleo, ombi langu katika Mkoa wa Katavi, ndani ya Mkoa wetu wa Katavi, Mkoa wa Rukwa na Katavi haujaungana kwa lami, kuna kipande kama kilomita 90 hivi bado hakijawekewa lami, nayo ilitakiwa iwekewe lami lakini sasa kuna tatizo kwa sababu ni Mbuga ya Wanyama ya Katavi, sasa katika ile Mbuga yetu, ina barabara mbili kuna barabara iko juu na barabara nyingine iko chini, kuna barabara ambayo inatoka Kizi kwenda Stalike na nyingine ya chini Kibaoni kwenda Stalike.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo hapa wanyama wanazaliana sana, lakini tukiangalia upande wa chini huku Kibaoni Stalike ndiko mazalia ya wanyama wanakozaliana na kuna mabwawa mengi na kuna uchumi mkubwa sana kwa ajili ya hiyo barabara, barabara ya kutoka Kizi kwenda Stalike Wanyama ni wachache sana, tunaiomba Serikali kupitia uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Katavi Mkoa wa Katavi, tunaomba katika barabara hiyo moja au ya Kizi - Stalike iwekwe lami ili Mkoa ule uweze kufunguka kwa ajili ya mchumi na kwa sababu sasa hivi Mheshimiwa Waziri nimeona katika vitabu vyako unaelekeza kujenga bandari katika eneo letu la Kalema ili uchumi Mkoa wa Katavi uweze kukua zaidi, naomba ili basi Mkoa wa Katavi uweze kufunguka tuwekewe barabara ya lami kutoka Kizi mpaka Stalike.

Mhesimiwa Naibu Spika, vilevile tuwekewe barabara ya lami kwa sababu hata Standard Gauge inakwenda Kalema na bandari inajengwa Kalema na tunashukuru tunaipongeza Serikali gati lile limekwisha na kwenye vitabu vyako Mheshimiwa Waziri umeandika gati limekwisha, sasa hivi ni mwendelezo wa kujenda bandari, kwa sababu ya mazao yote ambayo yanaenda katika nchi yetu ya jirani ya DRC. Naomba tujenge barabara ya lami kutoka Mpanda mpaka Kalema ili Standard Gauge itakapofika inakuta barabara ya lami tayari imeshajengwa basi yale mazao ambayo yanatarajiwa kwenda kwenye bandari au vifaa mbalimbali vinavyoenda kwenye bandari yetu ya Kalema viweze kwenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile hii barabara kwa nini tunaomba ili uchumi ufunguke kwa sababu bandari ya Kalema ikijengwa mazao yote ambayo yanahitajika kwenda Congo yatapita na barabara ya lami ambayo tayari tutakuwa tumeshaunganisha kile kipande cha Kizi, ambako barabara sasa ya lami itakuwa imeungana ile ya Rukwa Kizi Kibaoni, Kizi Stalike itakuwa imeshakamilika kwa kiwango cha lami, uchumi utakuwa mkubwa sana ndani ya Mkoa wetu wa Katavi ninaomba sana Waziri.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tulikuwa tunajua barabara ya lami imeishia Vikonge, tunaomba ili tuweze kufika Kigoma kile kipande cha Vikonge kwenda Uvinza nacho tuwekewe barabara ya lami ili sasa tuunganishe Mkoa wa Katavi pamoja na Mkoa wa Kigoma ili uchumi ndani ya Mkoa wa Katavi uendelee kukua zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mazao ya kibiashara kama tumbaku, pamba, korosho, kahawa ndani ya Mkoa wetu wa Katavi tunalima sana Tumbaku, ninaomba zao hili ndani ya Mkoa wetu wa Katavi limeshuka sana katika na wengine watu wa Tabora wamesema tunaomba Serikali sasa kwa sababu zao hili lilikuwa zao la kibiashara wananchi wa Katavi walikuwa wanalitegemea sana kwa ajili ya uchumi, naomba tuweze kulipangia mkakati mzuri ambao wananchi wote wanaolima zao hili la Tumbaku waweze kufaidika na kunufaika ili uchumi wa wananchi wa Tanzania wale wanaolima tumbaku waweze kurudisha uchumi wao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya Mkoa wetu wa Katavi, hili kila mwaka ninalisemea, tuna Ziwa Tanganyika, kwa wananchi Katavi matatizo ya maji mkitusaidia kama wenzetu wa Ziwa Victoria ambao walipata maji katika Mkoa wa Mwanza, Shinyanga, sasa maji yale yanaenda mpaka Tabora, naomba sana Ziwa hili la Tanganyika nasi watu wa Mkoa wa Katavi litatusaidia sana matatizo ya maji yakaisha kabisa tunaomba tutolewe maji kwenye Ziwa Tanganyika kuletewa ndani ya maeneo yetu ya Mkoa wetu wa Katavi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la scheme, tunalima sana na sasa hivi mvua zetu hazitabiriki lakini tuna mabonde mengi makubwa na Awamu zote zilijaribu kutengeneza scheme mbalimbali, kuna scheme ambazo zilitengenezwa zikatoa manufaa makubwa sana, naomba Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi ijikite kwenye scheme ili kilimo cha umwagiliaji kiweze kufuatiliwa kwa undani zaidi, kitaleta manufaa makubwa na tija ndani ya nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba sana Serikali yangu sikivu, umwagiliaji sasa ndiyo utatutoa, utaleta tija kwa sababu katika mabonde yetu tayari kuna unyevunyevu na mvuke mvuke, ule mvuke utatusaidia na kuweka utaalam mkubwa kwenye ulimaji wa mazao mbalimbali kupitia mabonde yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mabonde yetu Mkoa wa Katavi tuna mabonde mengi tunaona jinsi gani wananchi wanajitahidi kupitia hayo maji ya kuchotelea kwenye vikopo wakamwagilia lakini wanatoa mazao. Serikali ikiingiza nguvu yake katika scheme mbalimbali katika nchi yetu nafikiri tutapata manufaa makubwa sana na ukombozi wa Kilimo katika nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bado tuna tatizo TRA, leo hii kuna ndugu yangu mmoja ameenda TRA amehangahishwa kupata TIN amefungua kampuni mpya ili apate TIN, leo siku ya saba kupata TIN, huko TRA kuna tatizo gani, TIN inatolewa siku moja na ana kila kitu kafungua Kampuni ana vigezo vyote lakini leo anakwenda siku ya saba anaambiwa bado sijui hujaleta sijui hiki, hujaleta hiki, sasa kwa nini siku ya kwanza wasimwambie, wasimwandikie vitu vyote TRA? Imeshakuwa usumbufu TRA mpaka yule Dada akaanza kuwafokea watu wa TRA anasema ninyi Vijana ndiyo mnaowafanya hawa watu wakubwa wanatumbuliwa kila siku kwa ajili yenu ninyi. Ninaomba bado huyu Kamishna mpya bado ana kazi kwa sababu bado Vijana wako hawajaelewa somo. (Makofi)
Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa ninaomba nimshukuru Mungu ambaye ametuumba, ametupa uhai, hatimaye tu wazima kabisa. Vilevile naomba niwashukuru sana wananchi wa Jimbo la Nsimbo kwa kuniamini niwe Mbunge wao wa jimbo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikushukuru kwa kunipa muda huu niweze kuchangia hotuba ya Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwanza kabisa ninaomba nimshukuru sana Rais na kumpongeza kwa kazi kubwa sana ambayo ameifanya kuanzia mwaka 2015 mpaka 2020. Tumeona jitihada zake kubwa ambazo zimewafanya Watanzania wawe na imani kubwa sana na Rais wetu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona katika hotuba yake alivyoendelea kusema ataendelea kuwatumikia Watanzania kwa kila hali na nguvu zote. Ninaomba niipongeze sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi kubwa, miradi mikubwa imefanyika, tumeiona kwa macho miradi ambayo ilikuwa inaenda sambamba, miradi ya maji, miradi ya barabara, miradi ya standard gauge, bandari, kila kitu kimekwenda sambamba. Tunaomba tuipongeze sana Serikali kwa kazi kubwa na nzuri ambayo wameifanya kwa muda mfupi na malengo ni mazuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzangu wengi wameongea na nijikite kwenye ajira. Rais amesema ataendelea kuboresha ajira na tumeona ajira nyingi sana, yupo ndani ya kampeni lakini akamuagiza Waziri Jafo aongeze staff kupitia walimu ajira 13,000 ndani ya kampeni. Ni jitihada kubwa sana. Tuliona jinsi gani anaongeza madaktari ili kuendelea kutibu wagonjwa, madaktari bingwa. Tumeona jitihada ambazo zinaendelea kupitia ajira, lakini bado tunahitaji ajira kwa sababu kila sehemu tukienda mapungufu ni mengi sana kupitia ajira.

Tunahitaji sana tuongeze ajira kwa sababu tunaendelea kujenga zahanati,tunaendelea kujenga vituo vya afya na Rais wetu ametujengea hospitali katika mikoa mingi, hospitali za mikoa zingine za kanda, hiyo ni jitihada kubwa nzuri lakini bado watenda kazi ni wachache. Tunaomba Serikali iendelee kupambanua kuhusu ajira kwani inahitajika sana kwa kipindi hiki kwa sababu tumeongeza vitu vingi, shule zetu za secondary tunaongeza siku hadi siku, shule zetu za kata tunajenga, tunafungua shule, tunahitaji watenda kazi kwa ajili ya kutufundishia watoto wetu

Mheshimiwa Naibu Spika, Rais amejitahidi sana kwenye upande wa kilimo, tulikuwa tunapata shida pembejeo viatilifu matrekta, mbegu lakini sasa hivi mkulima anakuta mbolea madukani, anakuta pembejeo madukani, mbegu madukani, kusema kweli hali ya kilimo imeendelea kuwa nzuri siku hadi siku kutokana na uwezo ambao imeonesha Serikali ya Awamu ya Tano tunaomba tuwapongeze sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, bado kidogo kwa sababu kilimo ni uti wa mgongo na tunategemea sana, kilimo kije kutusaidia kupitia viwanda, Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli anatamani sana nchi yetu ya Tanzania tuwe na viwanda ili vijana wetu waweze kupata ajira na vile vile malighafi yetu iweze kufanya kazi ndani ya nchi yetu. Kilimo ndiyo kinaweza kufanya hivyo ili tuweze kupata viwanda vingi, lakini bado kuna maeneo ambayo hatujaweza kuwafikia wakulima vizuri, tukawapa semina mbalimbali na tukawawezesha wapate matrekta ili waweze kulima kilimo bora ambacho kitaweza kuleta tija. Naomba sana Serikali kwenye kilimo tuendelee kupaweka vizuri kwa ajili ya vifaa ambavyo vitawafanya wakulima waweze kulima vizuri ili tuweze kupata viwanda ambavyo tutapata ajira na vitu vingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nakwenda kwenye ufugaji; kwenye mambo ya ufugaji leo hii tumeshuhudia kuna viwanda vya kuchakata nyama viko viwanda vya samaki, tumetoa ajira na vile vile sasa hivi tunaweza tukasafirisha wanyama wetu nje ya nchi. Naomba nipongeze kufikia hatua nzuri ambayo tumeona ndege ya Ethiopia ilishakuja hapa kubeba cargo zetu za mizigo mbalimbali ambazo zinasafirishwa nje ya nchi ili kuendelea kukuza uchumi wa Watanzania, ndiyo maana unakuta sasa hivi watu wengi wametamani kufuga ili kuweza kupata uchumi mzuri. Naomba niipongeze sana Serikali ya Awamu ya Tano, kazi ni nzuri inaonekana wazi wazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, upande wa barabara, Serikali imejipambanua sana kuhusu barabara za lami, tumeunganisha mikoa, sasa hivi hata sisi watu wa Mkoa wa Katavi tukitoka Dodoma mpaka tufike Katavi ni masaa saba, nane, tunaomba tuipongeze sana Serikali, tunakwenda kwa lami sehemu zote. Rais wetu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuliamefanya kazi kubwa sana, lakini bado sisi Wabunge wa Majimbo tunaomba Serikali sasa ijikite kuongeza bajeti ya TARURA ili sasa zile malighafi ambazo zinatoka ndani ya vijiji vyetu, vijiji vyetu barabara hazipitiki kabisa, wakulima wanalima, lakini sasa kutoa mazao ndani ya vijiji vyetu ili tuweze kufisha sokoni na kipindi hiki cha mvua, inakuwa ngumu.

Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti ya mwaka jana ya TARURA sidhani kama ilitumika kabisa, kulikuwa kuna mitaro barabara zimekatika lakini hazikuweza kurekebishwa kabisa mpaka imekutana na mvua nyingine. Tunauliza shida ninini? Wanasema shida ni bajeti, kwa sababu barabara za vijiji zikitengenezwa vizuri, zikawa zinapitika ina maana malighafi zote zinazopatikana ndani ya vijiji vyetu zitatoka kwa urahisi.

Sasa hivi sisi tunasafiri vizuri, tukitaka kwenda sehemu tunakwenda, ndege zipo tunamshukuru sana Rais wetu amenunua ndege,usafiri ni mrahisi na mwepesi. Tatizo linakuja sasa ndani ya TARURA, hatujajipangia bajeti nzuri, naomba sana Serikali kwenye upande wa TARURA waongeze bajeti ili tuweze kutengeneza barabara na madaraja ndani ya maeneo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, muda umeisha?

NAIBU SPIKA: Ndiyo.

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naomba niunge mkono hoja. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia Mpango ulio mbele yetu kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitajikita upande wa TARURA kwa sababu nimeona Wabunge wengi wanaongelea kuhusu masuala ya kilimo. Asilimia kubwa katika nchi yetu ya Tanzania ni wakulima na Wabunge wengi wamesema kuwa kilimo kitatufikisha mbali zaidi kwa ajili ya kuongeza uchumi wa Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna mifuko mbalimbali ambayo tumeshaiweka katika Bunge hili, mfano Mfuko wa Maji na tumeona jinsi gani mifuko hiyo inavyosaidia maendeleo katika nchi yetu. Naomba kupitia Mpango wetu tuanze kutafuta Mfuko wa TARURA kupitia mitandao yetu ya simu. Tukipata shilingi 10 katika kila call nafikiri tutapata hela nyingi sana ambapo tutafungua mfuko mkubwa kwa sababu kwenye mitandao yetu ya simu hatujawahi kuchukua kitu chochote kwa ajili ya maendeleo ya jambo lolote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua Mfuko wa Maji tunachukua kwenye petroli na dizeli, sasa hivi tuchukue kwenye mitandao ya simu kwa ajili ya TARURA. Wananchi wetu wakilima vizuri na barabara zetu zikawa nzuri ina maana uchumi wa nchi yetu utakuwa mkubwa zaidi kupitia wakulima na vilevile Taifa letu litaongeza kipato kupitia kilimo chetu. Naomba sana TARURA itafutiwe mfuko maalum kwa ajili ya kuchangia mfuko huo ili tuweze kupata manufaa kupitia barabara zetu za vijijini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niende upande wa elimu. Najua toka Awamu ya Tano ni bure. Ilivyoingia elimu bure tulianza kupata wanafunzi wengi ambapo darasa la kwanza au darasa la awali tulikuwa tunaingiza watoto 1,000 shule zingine mpaka 1,200. Tutambue kuwa lazima tuweke mpango maalum kuanzia sasa hivi tujipange vizuri ili baada ya miaka saba inayokuja mbele yetu tuwe na madarasa mengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tu unakuta darasa moja lina watoto 80, tunakuja kuanza kuhangaika na pressure lakini tutambue kuanzia Awamu ya Tano imeanza kuwa na watoto 1,000 darasa la kwanza ina maana mpaka sasa hivi watoto 1,000 wako darasa la sita kwa darasa moja. Sasa ni lazima tuanze kuweka mikakati ya kuelekea sekondari tuwe na madarasa mengi ili tuweze kupata manufaa zaidi na elimu ikaendelea kuwa bora zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tutambue kuwa lazima sasa tuwekeze katika kutoa ajira. Tutoe ajira kwa walimu elimu ya shule za msingi na sekondari kwa sababu walimu wetu ni wachache sana na kila siku tunajenga shule za sekondari, tunajenga shule za msingi, wanafunzi wanaongezeka lakini kasi ya kuongeza walimu haipo. Naomba sana Serikali sasa hivi ijiwekeze kuanza kuweka mkakati wa ajira kwa ajili ya walimu wa kufundisha watoto wetu kwa sababu ni wachache sana na tunaendelea kufungua shule siku hadi siku, shule za kata zinafunguliwa siku hadi siku…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa, kengele imegonga.

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nashukuru. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali wa Mwaka 2016
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Ninaomba nimpongeze Waziri pamoja na Naibu Waziri kwa ajili ya kuleta muswada huu mzuri ambao unaweza ukabadilisha kitu fulani katika nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naingia katika Muswada wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali. Naomba niende moja kwa moja kwenye kifungu cha 7(2), nilikuwa nashauri kile kifungu cha Kiswahili kiandikwe vizuri na ninapendekeza kisomeke; “Bodi itakuwa na Mwenyekiti, atakayeteuliwa na Rais miongoni mwa watu wenye uzoefu usiopungua miaka kumi katika masuala ya utawala katika utumishi wa umma.”
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri tuna uzoefu, kiongozi yeyote ambaye anachaguliwa kwa kipindi kirefu kama miaka kumi anakuwa na uzoefu mzuri anaweza kufanya kazi vizuri zaidi. Nilikuwa naomba nipendekeze hivyo. Ndiyo maana unakuta hata Katiba yetu, Rais wetu anakaa madarakani miaka kumi, anapanga kitu kizuri na anafanya vizuri katika uongozi wake katika nchi, nilikuwa napendekeza hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nilikuwa naomba wahanga wa DNA na matumizi ya maabara hii ni wanawake. Nakumbuka tukiwa Katavi na Rukwa kesi nyingi za maalbino, wanawake wengi ndio wanaosingiziwa kama wanazaa nje. Wanawake wanakuwa wanapata matatizo kwa sababu wanatelekezwa na watoto maana mwanamke mwaume anaweza kamuacha kasema huyu mtoto si wangu. Ingawa mtoto ni wa yule baba lakini unakuta anamwambia huyo mtoto si wa kwangu, sasa unakutwa mwanamke anakuwa, Mhanga anakuwa mwanamke.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile wanawake na watoto wengi wananyimwa urithi kutokana na kusema kuwa huyu mtoto si wa kwangu kutokana na vipimo vya DNA.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeona kipindi hiki kifikie sasa na katika taasisi nyingi wanawake wengi wanawekwa nyuma katika shughuli mbalimbali ambazo zinatakiwa zifanyike. Napenda niweke idadi maalum, kiongezwe kifungu kingine cha 3, kisomeke; “Bodi itakuwa na Wajumbe wanawake.”
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ile Bodi haijasema wanawake ni wangapi, haijasema kitu chcochote. Sasa ina maana kuwa tukiacha hivi hivi ina maana wanawake watasahaulika kabisa. Nilikuwa napendekeza Wajumbe wanawake wasiopungua wawili. Tunataka neno wanawake lionekane bayana, ina maana wanawake waonekane, katika ile Bodi haijasema wanawake wangapi. Tulikuwa tunaomba katika kifungu kinachofuata wanawake waonekane katika Bodi.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kupitia ufafanuzi wa kifungu 16(4), kwa nini Serikali isiwajibike na mabadiliko ya sampuli? Serikali yenyewe ibadilike. Nafikiri ni haya niliyokuwa nayo ya kwangu.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi kwa siku hii ya leo kuweza kuchangia bajeti yetu ya TAMISEMI. Naomba nimshukuru sana Mungu ambaye ametupa uzima na uhai hatimaye tuko leo hapa tukiendelea kutetea wananchi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri Ummy kwa kazi kubwa, tunamjua, tunamfahamu alifanya kazi kubwa akiwa Wizara ya Afya, ni mwanamke ambaye ni shujaa, ni Hodari; tunajua kabisa kutokana na jitihada zake, hii wizara ataiweza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wengi wamezungumzia kuhusu suala la TARURA. Kwangu kuna maeneo, kata nyingine sasa hivi wako kisiwani kabisa. Madaraja yote yamechukuliwa na maji, barabara zote zimehama, maana sijui niseme nini? Sina hata la kusema, maana tunaonekana kama vile hatufanyi kazi kabisa. Hii ni kutokana na uwezo wa TARURA. Maana yake hata TARURA wa wilaya na wa mkoa wanashindwa hata kujitokeza kwa sababu hawana fedha ya kwenda kurekebisha mambo mbalimbali ambayo yanatokea katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa sababu Wabunge wengi wamezungumzia TARURA tunaomba kwa unyenyekevu mkubwa sana, Serikali iongeze fedha kwa TARURA kwa sababu maendeleo yote yanatokea ndani ya vijiji vyetu. Vijiji vyetu sasa hivi wamelima, lakini maeneo ya kupitishia mazao yao hakuna, siyo barabara wala madaraja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi nikikwambia, madaraja sijui mangapi huko yamekatika, wananchi Kata hii na hii hawaonani, kijiji hiki na hiki hawawasiliani, ni shida. Naomba kwa unyenyekevu mkubwa sana, TARURA iongezewe fedha ili waweze kutekeleza hii miradi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hizi barabara miaka miwili sasa hazijatengenezwa. Sasa mvua ya mwaka juzi, 2019, mvua ya mwaka jana, 2020 na inayoendelea, basi mambo yamezidi kuharibika zaidi. Serikali tunajua ni sikivu, lakini kwa TARURA safari hii tunaomba muipe kipaumbele cha kwanza. Kipaumbele cha kwanza ni TARURA ili njia zetu ziweze kupitika. Kata yangu ya Itenka ambayo ni kata ya uchumi sasa hivi wako kisiwani. Ninaomba sana tusaidiwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niingie kwenye upande wa Watendaji. Tuna vijiji na kuna maendeleo mbalimbali ambayo tunapeleka ndani ya vijiji vyetu, lakini hatuna watendaji. Utamkuta Mtendaji Kata ndani ya vijiji sita au saba ana Watendaji wa Vijiji wawili au watatu. Unakuta vijiji vine au vitano hakuna watendaji, wanachukuliwa walimu ndio wanakuwa mbadala wa watendaji. Wabunge wengi wamesema kuhusu watendaji, tunaomba mtuongezee Watendaji wa Vijiji, hatuna kabisa katika maeneo yetu ambapo ndiko kunapelekwa miradi mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, unakuta wakati mwingine Mwenyekiti wa Kijiji hana msaidizi, inabidi aombe msaada kwa mwalimu akaenaye kwa ajili ya miradi mbalimbali ambayo inayofanyika katika eneo la kijiji husika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile utamkuta huyo Mwenyekiti wa Kijiji hana posho, hana mshahara, wanapewa fedha nyingi za miradi, lakini yeye mwenyewe; Mwenyekiti wa Kijiji au Kitongoji hana mshahara. Nilikuwa naiomba sana Serikali, kwa sababu miradi mingi inakwenda vijijini na hao Wenyeviti wa Vijiji ndio utakuta wakati mwingine yeye mwenyewe ndio Mwenyekiti wa Kijiji, yeye ndio mtendaji, hana posho wala kitu chochote.

Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba sana Serikali, tuwaangalie Wenyeviti wa Vijiji ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi wapatiwe posho. Wengi wamezungumza kwamba wengine wanachukua rushwa kwa sababu hawana posho. Tukiwatazama kwa umakini zaidi na tukawapelekea posho, wanaweza kufanya kazi kwa umakini Zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile naomba niungane na Wabunge wenzangu kuhusu Madiwani. Madiwani wanafanya kazi nzuri sana na utamkuta Diwani ana vijiji 16 au vijiji 10, lakini umbali wa kutoka kijiji kwenda kijiji posho yake ni ndogo. Tunaomba Madiwani waongezewe posho ili ufanisi uweze kuwa mzuri, waweze kufanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya Halmashauri zetu magari hakuna. Miradi mingi inaenda katika Halmashauri zetu, lakini kutokana na uhaba wa magari kwa ajili ya kuzungukia kukagua miradi, Mkurugenzi pamoja na watendaji hawana usafiri. Tunaiomba Wizara iangalie upya kuwapa Halmashauri zetu vitendea kazi kwa ajili ya kukagua miradi mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri mnaona sasa hivi fedha nyingi tunapeleka kwa kutumia force account. Sasa force account, tunapeleka fedha huko, lakini kama mtendaji mkuu hana usafiri kwenda kuangalia kwa umakini ujenzi wa shule na madarasa itakuwa ni shida. Fedha nyingi zinapotea na miradi mingi inajengwa chini ya kiwango. Naomba sana magari kwenye Halmashauri zetu yapelekwe ili ufanisi wa kazi uweze kuwa mzuri na miradi mbalimbali ifanyike kwa ufanisi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzangu wameongea kuhusu uboreshaji wa bima. Mfuko wa Afya wa Jamii ni shida. Kwenye zahanati zetu, vituo vya afya hakuna vifaa tiba, hakuna dawa, mgonjwa akienda pale anaambiwa kipimo hakuna, hakuna dawa, sasa ni shida. Jamani tunaomba tujitahidi kwa hili. Kwa sababu tunaenda kuwaambia watoe shilingi 30,000; tulianzia shilingi 10,000 tukawaambia mtoe shilingi 30,000 kwa sababu bima hii imeboreshwa; utatoka ndani ya zahanati, utaenda kwenye kituo cha afya, utaenda wilayani, utaenda mkoani, lakini matokeo yake anakwenda kote kule, hapewi huduma ambayo inastahiki. Naiomba Serikali iangalie upya uboreshaji wa hii Bima upya kwa sababu nayo inaleta shida kwa ajili ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya Jimbo langu la Nsimbo, naomba niishukuru Serikali imenijengea Hospitali ya Wilaya ingawa haijakamilika. Ila kuna kata ziko mbali kama Kata ya Ugala. Kutoka Kata ya Ugala mpaka ufike kwenye Makao Makuu ya Wilaya au kwenye Makao Makuu ya Kituo cha Afya, wanatembea kilometa 80. Mtu anatoka kwenye zahanati kwenda kwenye kituo cha afya, anatembea porini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Kata ya Ugala nijengewe kituo cha afya kwa sababu watu wanatembea umbali mrefu, watu wanakufa. Acha Kata ya Ugala, kuna Kata nyingine ya Stalike. Kutoka Stalike mpaka uikute Hospitali ya Makao Makuu ya Wilaya ni kilometa 50. Naiomba Serikali iangalie haya maeneo yenye mazingira magumu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Itenka kama sasa hivi wako kisiwani, wana zahanati ndogo ambayo haina huduma nzuri. Naomba Kata ya Itenka nayo ijengewe kituo cha afya ili sasa kuweza kupunguza yale matatizo. Hata kama watu wako kisiwani, basi wawe na huduma bora, safi na salama katika maeneo yao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maji
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuweza kuchangia. Kwanza kabisa, naomba nimshukuru Mungu ambaye ametuumba na ametupa kibali muda huu tuko katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku hii ya leo. Naomba nimpongeze sana Waziri wa Wizara hii ya Maji, Naibu Waziri, Katibu Mkuu kwa kazi kubwa wanayoifanya, tunajua mnahangaika sana kutuletea pesa na kuhakikisha kila mtu anapata manufaa ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya Jimbo langu mimi kusema ukweli kuna miradi Serikali imeleta pesa mbalimbali, lakini miradi yote haiendi, wananchi hawana maji. Miradi ipo lakini imechukua muda mrefu takriban miaka miwili, mitatu mpaka miaka minne mitano miradi ile haiendi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mradi mmoja wa Mtakuja - Songambele ambao mpaka sasa hivi uko asilimia 70 lakini mkandarasi anadai shilingi milioni 112 mpaka leo hajapata pesa zake mradi umesimama. Naomba nishukuru Serikali tanki na vile vituo 11 vimekwisha lakini hakuna mabomba wala pump ya kusukuma maji katika maeneo yale ili maji yaweze kufika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mradi wa Stalike – Igongwa, mkandarasi anadai shilingi milioni 68 mradi umefika 80% leo miezi mitatu mkandarasi hajalipwa pesa zake. Kuna mradi Katisunga, huu mpaka leo ulikuwa una takriban shilingi milioni 138, mkandarasi mpaka leo hajalipwa pesa zake miezi sita mradi umesimama.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna miradi ambayo Serikali imeleta pesa lakini tumeshindwa kumalizia takriban miaka minne, mitano, wananchi bado wanaiangalia miradi ile tunasema matanki yamekwisha lakini wananchi bado hawajanufaika na miradi ile. Najua kuna kazi kubwa inayofanyika lakini tunaomba mliangalie suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze Mkurugenzi wa DAWASA wa Dar es Salaam, Mkurugenzi huyu tunamuona site, anatoka ofisini anaenda kusimamia miradi. Sasa Wakurugenzi na ma-engineer wengine wanashindwa nini kwenda site? Kwa usimamizi huu wa Mkurugenzi wa Dar es Salaam matokeo yake Dar es Salaam sasa hivi shida ya maji kila siku inapungua. Wahandisi wengine wanafanya nini maofisini? Kazi yao ni kwenda kuhakikisha wananchi wanapata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Nsimbo kuna Kata ya Ugala wana Mto Ugala uko pale pale kijijini wananchi wale wanaliwa kila siku na mamba, tunashindwa kuchukua maji pale kutoka pale kwenye mto kuwawekea hapa gati ili waweze kupata maji? Tunajua mnafanya kazi nzuri lakini kuna upungufu mkubwa sana ndani ya maeneo yetu, ma-engineer hawatoki tunaomba watoke wakafanye kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, najua kuna mradi ambao sasa hivi nimepewa hela wa Kijiji cha Matandarani lakini unachukua Kitongoji cha Magula ambako kuna wananchi wengi sana pale. Mradi wa Magula unaenda mpaka kwenye Kata ya Ibindi lakini pesa zimeletwa toka mwaka jana mpaka sasa hivi mradi huu uko asilimia 10. Mpaka sasa hivi mmetuletea takriban shilingi milioni 100 na kitu lakini umesimama. Kabla sijaingia hapa nimemuuliza Mhandisi wangu kule mradi unaendaje anasema bado ndiyo kwanza tunaanza kujenga tanki, tutafika kweli? Ukiona tuna mradi huu na ule lakini haiendi wananchi wanapata shida. Mfano, Kata yangu ya Litapunga ina vijiji 10, Kijiji cha Litapunga hawajui maji hata bomba hawajawahi kuona. Najua Waziri anafanya kazi nzuri sana lakini tunaomba miradi hii iende. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ya Katumba yenye vijiji 16 wametuletea kama shilingi milioni 200 lakini mradi umesimama, uko vilevile. Mheshimiwa Waziri anatembea sana katika miradi na shughuli mbalimbali tunamuona anahangaika lakini watendaji wake wamelala. Waziri anahangaika lakini watendaji wake wamelala usingizi. Kama wangekuwa wameamka kufuatilia miradi wala haya mambo yasingetokea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndani ya Mkoa wetu wa Katavi tuna Ziwa Tanganyika. Suluhisho la maji ndani ya Mkoa wetu wa Katavi ni maji kutolewa Ziwa Tanganyika na kusambazwa kwa sababu hatuna vyanzo vingi vya kuweza kutosheleza maji ya wana Katavi zaidi ya maji kutoka katika ziwa hili. Naomba sana, najua kuna mikakati mingi na mambo mengi najua Mpanda kuna programu ile lakini naomba katika ile programu ambayo mmetuweka maji yatoke Ziwa Tanganyika ili yaweze kusaidia Mkoa mzima wa Katavi. Maji yakitoka kule haya matatizo ndani ya Mkoa wetu wa Katavi tutakuwa hatuna shida tena.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana na naomba niunge mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi. Naomba nikupongeze kwa kuteuliwa kuwa Mwenyekiti, kiti kimekufaa, hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshukuru Mungu ambaye ametupa uhai na uzima na ametupa kibali sasa hivi tuko ndani ya Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tukiendelea kufanya shughuli mbalimbali za Kiserikali. Naomba nimshukuru na kumpongeza sana Rais wetu, Mheshimiwa Mama Samia Suluhu kwa kazi kubwa ambayo anaendelea kuifanya katika nchi yetu ya Tanzania. Tunaona jitihada zake, na kazi zake, nasi tunaendelea kumuunga mkono kwa asilimia mia moja ili aweze kufanikiwa kuijenga nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Waziri pamoja na Naibu Waziri. Waziri ni mtani wangu pamoja na mdogo wangu, hongereni kwa kazi kubwa, tunaona jitihada zenu mnazozifanya. Naomba nimpongeze Katibu Mkuu wa Wizara hii, Ndugu Kijazi kwa kazi kubwa. Tunajua anahangaika, ametokea mbali pamoja na kupitia Wizara hii katika sekta mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba nimpongeze Mkurugenzi wa TFS, ni msikivu chief ni msikivu, lakini sasa vijana wake ndio tatizo. Naomba nianze kwa TFS ambayo ni tatizo kupitia wananchi wetu. Tunajua Serikali ni moja, lakini ukienda katika maeneo yetu ya vijijini TFS wamejitenga wao kama wao. Wanafanya kazi wao kama wao, hawathamini kabisa viongozi ndani ya vijiji vyetu. Wakiingia pale vijijini, wenyewe wakishasema hii ni hifadhi, basi wamesema, wanaanza kutandika wananchi; na wakati mwingine inakera zaidi wanapochukua mali zao. Inasikitisha sana maana wakikuta hata ng’ombe wanabeba. Sasa tunajiuliza, hii TFS ni chombo kiko tofauti kabisa, kinajitegemea chenyewe kama chenyewe? Ina maana hakina suluhu na wananchi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimshukuru sana Mkurugenzi wa TFS, tumeendelea kumlalamikia kwa ajili ya Meneja wa Kanda, tunamshukuru sana kwani amechukua hatua ya kumhamisha. Tunamshukuru sana kwa sababu ilikuwa ni kero kubwa sana kwa wananchi, alikuwa hataki suluhu na viongozi wa Serikali ndani ya wilaya na ndani ya mkoa, na alikuwa hataki kuonana na sisi Wabunge, anasema sisi ni wanasiasa. Sasa kama ni wanasiasa, ni lazima tuwatetee wananchi wetu kwa sababu mali mazao wanayolima wakulima wale ndiyo inayoleta maendeleo ndani ya nchi yetu pamoja na kukuza uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe ushauri, ifike mahali sasa TSF ipite katika maeneo yote nchi nzima, waonyeshe mipaka yao na wananchi. Unakuta sasa hivi kama Kata yangu ya Ugala, wanasema yote ile ni hifadhi. Sasa unajiuliza, hii ni kata, ina vijiji, ina vitongoji; wanasema wananchi wote wahame kwenye Kata ya Ugala, waende wapi sasa? Wameshakaa zaidi ya miaka 50 mpaka 60, leo mnasema ni hifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna Kijiji cha Usense Kata ya Urwila, wameweka beacon katikati ya Kijiji, wanasema yote hiyo ni hifadhi. Sasa siku zote hizo mlikuwa hamuoni, leo ndiyo mnakuja kuona kama ni hifadhi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba sana TFS wapite katika maeneo sasa tukubaliane, twende kuanza kuonyeshana mipaka ili tujue mipaka ya TFS iko wapi; na mipaka ya wananchi? Tujue wananchi waende wapi kwa ajili ya maendeleo mbalimbali ya kilimo na ufugaji. Kwa sababu tukienda namna hii tutaendelea kuwavuruga wananchi kwa sababu wanapigwa, wananyang’anywa mali zao, hawana amani, wanaishi maisha magumu sana katika nchi yao na maeneo yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Waziri kipindi hiki atoke, asikae ofisini pamoja na watendaji wake wote, twendeni tukaonyeshane mipaka ili wananchi tujue mipaka yetu iko wapi ili tusiweze kuwaingilia kazi zenu. Kwa hiyo, tunajua mnafanya kazi kubwa ya kuendelea kuhifadhi…

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Engineer Stella Manyanya, karibu.

T A A R I F A

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Taarifa ninayotaka kumpa ni kwamba malalamiko hayo ya kuweka mipaka ya hifadhi yanafanana sana na kule jimboni kwangu Nyasa katika eneo la Lipalamba. Wananchi wanasema mpaka waliokuwa wanaujua, wanauona kabisa, lakini sehemu waliyoenda kuweka kama ndiyo mwisho wa eneo la kwao, wamepitiliza ndani huko kiasi kwamba hata wanavyoelezwa, wao hawaelewi. Wanasema kwa sababu kwanza kwa nini waende kuweka hiyo mipaka peke yao bila kuwashirikisha hao viongozi wa vijiji? Ndiyo taarifa yangu.

MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Lupembe, unaipokea hiyo taarifa?

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea. Ni tatizo kusema kweli. Hawataki maelewano kabisa TFS. Mkisema mkae pamoja mkaelezana jambo, hawakubali. Naomba nimuunge mkono kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya jimbo langu, nina Hifadhi ya Katavi. Hifadhi hii bado haijatangazwa vizuri. Hifadhi ya Katavi ni nzuri, ina wanyama wakubwa, ina mambo mazuri sana, ina twiga mweupe, tembo wakubwa sana, lakini bado hatujaitanga vizuri na hatujajenga mahotel na mazingira yake siyo mazuri sana ya kuvutia watalii kuja katika Hifadhi ya Katavi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba basi Serikali, najua Waziri ana jitihada kubwa sana ya kufanya kazi na uhamasishaji, tunaona leo hii kuna mtu yupo Serengeti. Basi siku nyingine mlete Mbunga ya Katavi ili iweze kutangazika kwa sababu najua ikitangazika, sasa hivi tuna uwanja wa ndege, anatua Mpanda bila matatizo na kutoka pale mpaka kwenye hifadhi yetu, siyo mbali sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hifadhi ya Katavi ambayo inasimamiwa na TANAPA, ule ujirani mwema bado haujawa mzuri sana. Ndani ya Kata ya Stalike nina mto pale. Ule mto una samaki pale…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Haya, ahsante Mheshimiwa.

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niunge mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naomba nimshukuru Mungu ambaye ametupa uzima na uhai hatimaye ametupa kibali tuko katika eneo hili la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwamba kabisa naomba nimshukuru Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mama yetu mpendwa Mheshimiwa Samia Suluhu kwa kazi kubwa ambayo anaifanya kwa Watanzania. Naomba nimpongeze sana. Vile vile naomba nimpongeze Waziri Mkuu kwa kazi kubwa ya kuendelea kuisimamia Serikali. Anafanya kazi nzuri, tunaona anahangaika katika Mikoa mbalimbali kuhakikisha nchi yetu inasonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niipongeze Serikali kwa ujumla kwa kazi kubwa kupitia mama yetu Mheshimiwa Samia; tulipewa fedha nyingi kupitia fedha za UVIKO ambazo zimekuja katika Majimbo yetu, zimetuwezesha kujenga Zahanati, Vituo vya Afya, Shule Shikizi na Shule za Sekondari. Naomba niipongeze sana Serikali kwa kazi kubwa ambayo wameifanya. Kusema kweli sisi Wabunge wa Majimbo tunajivunia sana kwa sababu kazi imeonekana na bajeti imeonekana. Naomba tuipe pongezi kubwa sana Serikali ya Awamu ya Sita kwa kazi kubwa ambayo wameifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kazi kubwa imefanyika, tumeona kwenye majengo ya Shule Shikizi na Shule za Sekondari tumeweka vifaa kama madawati na kadhalika, pia tumejenga Vituo vya Afya na Zahanati, lakini mpaka leo bado hatujapata vifaa. Tumeanza kujenga majengo mengine mwezi wa Tatu mwaka 2021, mengine tumepewa fedha mwezi wa Kumi mwaka 2021, tayari yamekamilika lakini mpaka leo vifaa tiba hatujapata. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo langu nimepewa fedha za Hospitali ya Wilaya, nimejenga Hospitali ya Wilaya lakini mpaka leo hatujaweza kuifungua kwa sababu hatuna vifaatiba. Tunaiomba Serikali sasa ijielekeze kwenye vifaatiba ili majengo yale yaweze kufanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa tuna kero kubwa sana ya watendaji wa kazi ambao ni walimu, manesi na madaktari. Leo naomba nimshukuru sana Waziri mwenye dhamana ambaye ni Waziri wa Utumishi, ametuambia kutakuwa na ajira kama 30,000 ambapo atakuja kwenye bajeti yake kuisema. Naomba tuipongeze sana Serikali kwa kazi kubwa ambayo wanaendelea kutuonyesha sisi Watanzania. Tulikuwa tunapata kero kubwa kwa ajili ya watumishi, lakini leo tunatarajia sasa watumishi watapatikana katika maeneo yetu kwa sababu tumejenga Shule na Zahanati lakini hakuna watumishi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini bado kidogo kuna changamoto kwa ajili ya walimu wenye madai yao, bado hatujaweza kuwafikia wote, wengine hawajapata madai yao, wanadai malimbikizo ya madeni yao. Tunaomba hilo tulifanyie kazi kwa sababu wanafanya kazi kubwa, wanakaa katika mazingira magumu. Naiomba sana Serikali yangu sikivu iwaangalie hawa walimu wanaodai madai yao limbikizi waweze kulipwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niipongeze sana mifuko ya kijamii pamoja na mashirika. Hii mifuko inajitegemea na vilevile kuna vikwazo kupitia mashirika yetu haya, yana uwezo wa kuajiri, sasa tumewawekea vikwazo wasiajiri mpaka kibali kitoke Utumishi. Nilikuwa naomba haya mashirika kwenye ngazi labda kuanzia vibarua, makarani na wengineo hapa tumewapa fursa waajiri wenyewe, lakini kupitia ngazi ya Mameneja na Wakurugenzi iende Utumishi ili waweze kuajiri. Kwa sababu kuna vikwazo, unakuta wanatamani kuajiri watu, lakini kuna vikwazo lazima wapate vibali ili kazi ziweze kusonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa naiomba Serikali yangu kupitia utumishi tuwape ruhusa waajiri kuanzia ngazi ya vibarua mpaka makarani, zile kazi ambazo ni za kawaida, waajiri wenyewe ili kazi zile nyepesi na rahisi zaidi waweze kuzifanya ili majukumu yao yaweze kwenda vizuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja TARURA. Naomba niipongeze Serikali yangu; na kupitia Rais wetu, Mheshimiwa Mama Samia, najua bajeti iliyopita kila Mbunge wa Jimbo alipata shilingi bilioni 1,500. Zile fedha zimetusaidia sana, zimefungua barabara, kazi kubwa imefanyika, inaonekana; barabara za vijiji na vitongoji sasa hivi zimeunganika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, ndani ya maeneo yetu ya vijijini kuna madaraja makubwa. Tumeona Mheshimiwa Waziri Mkuu hapa wakati akiwasilisha bajeti yake, ameonesha madaraja makubwa yaliyojengwa na mama yetu Mheshimiwa Samia kwa fedha nyingi. Naomba Serikali sasa iongeze bajeti kwenye TARURA ili sasa madaraja yote ya vijijini, kuunganisha vijiji na vitongoji yaweze kujengwa kwa ajili ya usalama wa wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia kipingi hiki cha mvua, leo hii mvua zikinyesha katika maeneo yetu, vitongoji na vijiji watoto wa shule katika mito yetu wanashindwa kuvuka kabisa. Ina maana mvua zikianza kunyesha watoto wengi hawaendi kwenye masomo inavyotakiwa katika muhula.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa naomba sana, sasa ifike kipindi TARURA tuiongezee bajeti. Madaraja yote makubwa ndani ya vijiji na vitongoji vyetu, yajengwe na TARURA yenyewe. TANROADS inashughulika na barabara kubwa na madaraja makubwa, sasa naomba TARURA tuiongezee fedha ili iweze kufanya kazi vizuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, najua kuna vitu vingi tunavyovifanya katika nchi yetu, tunajenga vituo vya polisi katika maeneo yetu na tunaendelea kuchangia na wananchi wanaendelea kuchangia, kuna maboma, lakini naomba ndani ya kata zetu unakuta polisi anakaa kwenye Ofisi ya Mtendaji anakuwa yeye polisi peke yake. Sasa kama kuna uhalifu ndani ya maeneo yetu au kuna kitu chochote kimefanyika katika maeneo yetu ya kata, ina maana wale wahalifu wanachukuliwa wanapelekwa katika Ofisi ya Mtendaji maana yake hana sehemu ya kuwatunza. Nilikuwa naomba kupitia Serikali yetu sikivu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ufike muafaka katika kila kata tujenge vituo vidogo vidogo vya polisi ili wajitegeme. Ukiangalia sasa hivi katika maeneo yetu kuna uhalifu mwingi. Watu wako mbali unakuta kilometa 20, kilometa 30, kilometa 60, kilometa 70 hawana kituo cha polisi. Naomba sana tujielekeze sasa kuhakikisha tunajenga vituo vidogo vidogo kwenye kata zetu kwa ajili ya ulinzi na usalama wa Watanzania tunaoendelea kuwatumikia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, najua kuna mengi ambayo yamefanyika katika nchi yetu na ni mazuri, sasa hivi hatuna hata la kusema, kazi kubwa imefanyika. Tumeomba pesa tumeletewa, kero nyingi kusema kweli zimepungua hata leo Wabunge sidhani kama tutaongea sana kwa sababu tunaona pesa tunaletewa miradi inafanyika, kero kubwa tu tuliyokuwa nayo sisi Wabunge, watendaji kazi hatuna, tunaomba sasa ajira ya watendaji kwa sababu tayari tumeshaambiwa watendaji wataajiriwa au kuna ajira zinakuja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naomba niseme ahsanteni sana. Naomba niunge mkono bajeti hii ya Waziri Mkuu kwa asilimia mia moja. Ahsante sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2022
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Spika, naomba nikushukuru kwa kunipa muda huu wa kuweza kuchangia maazimio ya Kamati zetu mbili zilizowasilishwa mahali hapa kwa ajili ya maendeleo na mustkabali wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, naomba nimshukuru Mungu ambaye ametulinda na ametupa muda huu tukiendelea kupumua na kuwa wazima wa afya njema.

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimshukuru Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuingiza ruzuku na kuwapunguzia wananchi makali kwenye mbolea. Tumeona jitihada za mwaka huu, wananchi wengi wamelima, mazao yatakuwa mengi sana mwaka huu kwa sababu kila mwananchi amelima na kutumia mbolea.

Mheshimiwa Spika, changamoto kwenye mambo mazuri lazima ziwepo. Mbolea zile zilitakiwa zifike katika maeneo yetu ya vijiji, lakini ilishindikana ikafika kwenye maeneo yetu ya wilaya, na wananchi wameendelea kulima na kununua mbolea kwa wingi kwa ajili ya faida na mafanikio ya Taifa kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeona ni kwa nini miradi mingi haiendi kwa haraka na kwa nini miradi mingi inachelewa? Kwa kipindi hiki cha miezi sita, Wizara ya Kilimo imepokea asilimia 17 tu. Wizara ya Kilimo ina miradi mingi ya umwagiliaji ambayo haikufikiwa vizuri kupitia Wakandarasi ambao wamewekwa katika maeneo ya miradi hiyo. Miradi mingi mpaka sasa hivi haijaenda vizuri kutokana na kwamba fedha hazijawafikia Wakandarasi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tatizo kubwa tumeliona Hazina. Hazina wanachelewesha fedha na kusababisha kutofikia yale malengo. Kwa sababu sasa hivi ni miezi sita, lakini ni asilimia 17 tu katika Wizara ya Kilimo, ina maana hayo maendeleo yatakuwepo? Tukiangalia ruzuku ya mbolea, ilipangiwa shilingi bilioni 150, mpaka sasa hivi Wizara imepokea shilingi bilioni 50. Ina Wakandarasi wale ambao wanaingiza mbolea nchini wamepokea robo ya zile fedha. Ndiyo maana umekuta mzunguko wa mbolea umekuwa shida katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Spika, kuna mbolea ambazo hazijafika, na kuna mazao ambayo yanahitaji mbolea, hususan wakulima wa tumbaku. Kama imechelewa kufika katika maeneo ya wakulima mpaka zao la mbolea likaanza kuharibika, ina maana hapo tunamwondoa mkulima katika hali ya kulima lile zao kwa haraka.

Mheshimiwa Spika, vile vile naomba niishauri Serikali, ndani ya nchi yetu kuna maeneo ambayo yanajulikana kabisa; kama Mkoa wa Katavi, Kigoma na Kagera, mvua zinaanza mwezi wa Kumi, lakini mbolea zinakuja Januari. Huyu mkulima ameshalima. Leo hii anaichukua ile mbolea anaweka tu basi afanyaje lakini msimu wake wa kuweka mbole umeshapita. Nilikuwa naomba Serikali ijipange vizuri kupitia mbolea. Inatambua kabisa mikoa ya huku Rukwa, Katavi, Kigoma pamoja na Kagera wanaanza msimu wao wa kulima mwezi wa Kumi. Ina maana mbolea inatakiwa Mwezi wa Nane iwe imeshafika site.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba sana Serikali iboreshe kwenye masuala ya mbolea ili kuendelea kuhamasisha wananchi kulima kupitia Rais ambaye amewapa ruzuku ya mbolea na wananchi wamefurahi. Sasa zile jitihada za Rais zisiweze kupotea bure. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nipongeze Wizara ya Maji, wanafanya kazi kubwa sana. Tumeona Mheshimiwa hapa amesema, tulienda kukagua miradi ya Dar es Salaam, DAWASA. Jitihada zilizofanyika kwa kipindi cha ukame, maji Dar es Salaam ilikuwa shida, lakini Wizara ya Maji kupitia Shirika la DAWASA likafanya kazi kubwa na kuondoa kabisa ule upotevu wa maji. Sasa hivi wananchi wanapata maji kama kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naenda kwenye miundombinu. Naomba niungane kabisa na Kamati kuhusu masuala ya Shirika la TAA. Viwanja vya ndege sasa hivi vinatengenezwa na TANROADS. TANROADS wameshakuwa na majukumu mengi. Wana madaraja makubwa, barabara na sasa hivi tumeona nchi yetu barabara nyingi zinatakiwa kufanyiwa marekebisho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nami naunga mkono Kamati ya Miundombinu waliposema kuwa hii miradi ya viwanja vya ndege warudishiwe TAA ili waweze kuendelea kufanya kazi kwa ubunifu mzuri ili yale mambo tunayotaka yafanyike yaweze kufanyika.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu sasa hivi tunaona hata kwenye Wizara yetu ya Kilimo kuna wananchi mbali mbali, vikundi mbali mbali wanalima mboga mboga na maua, ambapo mwisho wa siku yanatakiwa yatoke katika nchi yetu yaende katika nchi nyingine. Ina maana tukiwaachia TAA watafanya kazi vizuri, viwanja vitajengwa kwa haraka na kupitia mapato yao ya ndani wataendeleza pale palipopungua kwenye fedha ya bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sana niungane mkono na Kamati ya Miundombinu kuhusu miradi yote ya viwanja vya ndege virudishwe TAA.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono Kamati yetu ya Kilimo, ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa ninaomba nishukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuweza kuchangia Wizara yetu ya TAMISEMI. Naomba nimshukuru Mungu ambaye ameendelea kutupa uzima na uhai leo tuko hapa tukichangia kwa ajili ya maendeleo ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nichukue fursa hii kwanza kabisa kumshukuru Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa ambayo anaifanya kwa ajili ya Watanzania. Amefanya kazi kubwa, hivi leo kwa kipindi hiki kifupi katika Jimbo langu nimepokea Bilioni 6.2 kazi kubwa sana, sana, sana. Ninaomba nimpongeze Spika wetu Dkt. Tulia, amefanya kazi kubwa tumeiona kwa macho, maendeleo ndani ya Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni maendeleo makubwa kuna mabadiliko makubwa. Hongera sana Dkt. Tulia, kwa kazi kubwa ambayo unaifanya katika Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nimpongeze Waziri pamoja na Naibu Mawaziri kwa kazi kubwa wanayoendelea kuifanya kusimamia miradi mbalimbali na maendeleo ya jumla katika Wizara yetu ya TAMISEMI, pia ninaomba nimpongeze kwa kipekee Mkuu wangu wa Mkoa Mwamvua Mlindoko, kwa kazi kubwa anayoifanya ndani ya Mkoa wetu wa Katavi. Anasimamia miradi, anafuatilia, anahakikisha maendeleo yanasonga mbele katika Mkoa wetu wa Katavi, anastahili pongezi Mkuu wetu wa Mkoa wa Katavi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaenda TARURA, ninaomba nichukue fursa hii ya kumpongeza Chief anayesimamia TARURA. Anastahili tuzo, anastahili tuzo Mheshimiwa Waziri, tunaomba umpe tuzo. Chief wa TARURA kwa kazi kubwa nzuri anayoifanya. Leo hii katika maeneo yetu, Majimbo yetu, barabara zinapitika, madaraja yalikuwa hayapitiki watoto walikuwa wanapata shida hawawezi kuvuka kipindi hiki cha masika lakini leo lhii madaraja yamejengwa wananchi wanavuka, watoto wa shule wanavuka, anastahili pongezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoomba leo hii TARURA waongezewe pesa kwa sababu wanafanya kazi kubwa na vilevile TARURA wana mtandao mkubwa wa barabara kuhakikisha vijiji vyetu na vitongoji vyetu uchumi wa wananchi unakua, kwa sababu tumeona kwa kipindi hiki barabara zimefunguka, wananchi wetu wamepata uchumi mkubwa, mazao yote yamebaki shambani, wafanyabiashara wanawafuata wakulima katika maeneo yao sasa tunaomba TARURA waongezewe pesa na vilevile madaraja yaendelee kujengwa na wapangiwe bajeti kwa ajili ya matengenezo. TARURA hawana bajeti ya matengenezo, lazima wapangiwe bajeti ya matengenezo ili barabara ziweze kuboreshwa siku hadi siku. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano sasa hivi barabara mvua zinanyesha, barabra nyingi zinaharibika, hawana fungu, tunaomba TARURA wapewe fungu la matengenezo ili barabara zetu ziweze kupitika mwaka mzima bila tatizo la aina yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakuja upande wa elimu ya msingi. Nimepongeza, ninaomba niishukuru Serikali kwa kazi kubwa ambayo inaendelea kuhakikisha kuboresha na leo hii tumepata pesa kwa ajili ya kujenga shule mpya, ninaomba nishukuru kwa kupewa pesa hizo, nimepewa pesa kuhakikisha zile shule zote shikizi ambazo tulizijenga wakati uliopita, vyoo vyao vijengwe, tumepokea hizo pesa, ninaomba nishukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima sasa tujiwekeze, walimu walio katika maeneo ya mazingira magumu kama vijijini hawana nyumba, lazima sasa hivi tuweke mikakati kuhakikisha tunawajengea nyumba ili waweze kukaa katika maeneo husika. Tatizo walimu hawakai kwa sababu hawana sehemu ya kuishi katika maeneo yetu ya vijiji. Ninaomba sana, sasa tujiwekeze kuhakikisha tunajenga nyumba ili walimu waweze kukaa katika maeneo safi na salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninajua Serikali imefanya kazi kubwa kupitia vituo vya afya, zahanati zote hizo tumepokea pesa, lakini ninaomba kwenye Jimbo langu, Kituo cha Afya cha Ugala niliahidiwa milioni 800 lakini mpaka sasa hivi nina Milioni 500, Kituo cha Afya cha Itenka niliahidiwa Milioni 800, mpaka sasa hivi nina Milioni 500, ina maana kuwa bado ninadai kuna maeneo ambayo majengo hayajakamilika ninaomba Serikali kupitia Waziri wetu wa TAMISEMI, ni msikivu pamoja na Naibu Mawaziri, tunaomba basi mtumalizie hizo pesa tuweze kumaliza vituo vya afya viweze kukamilika ili wananchi wa Jimbo la Nsimbo waweze kupata huduma safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nipongeze tumeshaanza kupata vifaatiba vimeshaanza kuwasili na dawa katika Zahanati tulizozijenga na vile ile nilikuwa ninaomba, kuna Zahanati ambayo maboma wananchi wamejenga, zile Zahanati naomba pesa kwa ajili ya umaliziaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi kubwa imefanyika na Serikali ya Mama Samia, kazi kubwa lazima apongezwe Mama huyu amefanya kazi kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi kubwa inafanywa na Watendaji wa Vijiji lakini ninaomba nishukuru kwa ajira ambazo sasa hivi tumepata ajira 13,000 lakini Watendaji bado hatuna, ninaomba tufanye ajira ya Watendaji. Watendaji wa Mijini kule Vijijini hawapo, tunaomba sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ninaiomba Serikali tunaendelea kuomba kila siku Wenyeviti wa Vijiji tunawapelekea miradi mikubwa wanashika hela nyingi, hebu tuwatazame huko Wenyeviti wa Vijiji, tuwawekee posho at least wapate ari ya kufanya kazi. Tunapeleka miradi mikubwa lakini posho yao haijulikani. Ninaomba Wenyeviti wetu sasa hivi wanapokea miradi mikubwa, tunaomba watazamwe kwa jicho la huruma, wapewe chochote ili waweze kufanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maji
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nimshukuru Mungu ambae ametupa afya njema na uzima leo tuko hapa tukiendelea kujadili mambo ya maendeleo ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa ambayo anaendelea kuifanya kupitia Wizara ya Maji. Tumeona kazi kubwa, Miradi mikubwa ambayo tumeiona katika nchi yetu ikiendelea kujengwa na wananchi wakiendelea kufaidika na maji hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Waziri Aweso, kwa kazi kubwa ambayo anaifanya usiku na mchana anawahangaikia Watanzania. Naomba nimpongeze Naibu Waziri wa maji Mhandisi Maryprisca nae vilevile anafanya kazi kubwa sana kuzunguka na kuhakikisha matatizo ya maji yanapotea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze sana Katibu Mkuu, Kemikemba, kwa kazi kubwa anayoifanya kuhakikisha miradi yote na pesa zote zinakwenda kwa ajili ya miradi mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Naibu Katibu Mkuu, Cyprian Luwemeja, kwa Kazi kubwa, tunajua alifanya kazi kubwa sana DAWASA na Rais kamuona sasa aje kusaidia wizarani aweze kukimbia na yale aliyoyafanya makubwa DAWASA sasa aweze kuyafanya katika miradi yote ya nchi nzima. Naibu Katibu Mkuu, Cyprian, hongera sana kwa kazi kubwa, watanzania tunakutegemea utahangaika kuhakikisha watanzania tunapata maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Meneja wangu wa Mkoa wa Katavi pamoja na Meneja wa Wilaya, wanafanya kazi kubwa. Lakupendeza zaidi wanapenda kushirikisha, wanashirikisha Wabunge, hakuna kitu wanweza kufanya wao bila kuwashirikisha Wabunge. Ninaomba niwashukuru sana na niwape pongezi kubwa kwa sababu ushirikishwaji ndio unaofanya mambo yanakuwa mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze waziri pamoja na Katibu Mkuu, kupitia maelekezo ambayo wamewapa watendaji wao wote katika nchi nzima. Tuseme tu kutokana na maelekezo haya, Managers wote wa mikoa pamoja na wilaya tunafanya nao kazi Vizuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Jimbo langu la Nsimbo, miradi yote ambayo niliyopewa na kama kuna changamoto wananishirikisha kwa ukaribu tunafanya kazi kwa pamoja. Naomba niwapongeze sana Meneja wa Mkoa pamoja na Meneja wa Wilaya, kila jambo lazima wanishirikishe na miradi yote ya Mkoa wetu wa Katavi lazima watushirikishe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nishukuru hapa karibuni gari limekuja katika Jimbo langu la Nsimbo, visima vimechimbwa. Nilikuwa naomba nishauri, kazi kubwa inafanywa na watendaji na visima vinachimbwa na tumeona mara nyingi visima vingi vikichimbwa vinaachwa muda mrefu. Vinaweza vikakaa hata miezi sita pengine visima vinakaa mwaka mzima.

mhesh ninaomba nitoe ushauri wangu, basi sasa hivi tuchimbe visima kwa sababu wananchi wanaona visima vinachimbwa wanakuwa wana matumaini ya kuwa tunapata maji kesho, lakini hatimaye kile kisima kinakaa muda mrefu, ile hali tena inapungua. Ninaomba nishauri tuchimbe visima, muda huo huo tuvijenge ili wananchi waweze kupata maji safi na salama. Tusikawie kwa sababu tayari mmeshafanya utafiti, watu wa bonde wamepita wameona na mmekuja kuchimba mmeona maji. Basi tuchukue hatua sasa ya kujenga ili wananchi wale waweze kupata maji safi na salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, natokea Mkoa wa Katavi, suluhisho la maji ndani ya Mkoa wetu wa Katavi, tupate maji kutoka Ziwa Tanganyika. Kwa sababu yale maji ndiyo yatakayofanya maeneo yetu ya Mkoa wetu wa Katavi wakapata maji safi na salama. Lakini naomba nikupongeze Mheshimiwa Waziri, umesema kuwa tutatumia sasa hivi maziwa, tutatumia mito kuhakikisha watanzania wanapata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nikupongeze sana ili basi hatua hii tuichukue haraka. Tunajua hii miradi ni mikubwa ambayo itachukua muda mrefu ili wananchi waweze kupata maji. Tunakutakia kila la heri kuhakikisha maji haya ya maziwa yanafika sasa kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nichangie kuhusu miradi mbalimbali mikubwa inayopita katika maeneo yetu. Miradi hii mikubwa inaweza ikapita katika vitongoji na vijiji. Ninaomba sana miradi hii inayopita katika maeneo mbalimbali inasafiri, tunaomba yale maeneo ya vijiji na vitongoji husika ambako mradi ule unapita, wale wananchi waliopitiwa na ule mradi wapate maji. Kwa sababu tunapita wale wananchi wanakuwa hawana maji, matokeo yake uharibifu unatokea. Lakini tukiwapatia maji vitongoji vile vinavyopitiwa na mradi ule pamoja na sehemu nyingine kuna wafugaji, wafugaji wale wanaona bomba lile kubwa limepita na hawana maji, ile mifugo inahangaika matokeo yake wanapasua yale mabomba ili wanyama wale waweze kupata maji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ninaomba kuishauri wizara, tuhakikishe yale maeneo ambayo miradi ile mikubwa inayopita kama kuna wananchi wanaishi pale, kuna mifugo, tujenge mabwawa na wale wananchi waweze kupata maji safi na salama ili ule mradi tuulinde na yale mabomba tuweze kuyalinda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna changamoto ya mabomba makubwa na viwanda vyetu havitoshelezi. Leo hii ukiwauliza wakandarasi wanakwambia kuwa tuko kwenye foleni tunahitaji mabomba. Kuna miradi mingi mikubwa imechelewa kwa ajili ya malighafi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilikuwa naomba, kwa sababu tumekwishaona kuna malighafi mbili, kuna mabomba ya plastic na mabomba ya chuma na mabomba yale ya chuma makubwa kupitisha miradi mikubwa mikubwa viwanda vyetu havitoshelezi. Nilikuwa naomba aidha tushawishi wawekezaji waje kwenye nchi yetu wawekeze ili tuweze kupata mabomba kwa ajili ya malighafi au basi tuainishe nchi ambazo tunaweza tukapata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niunge mkono hoja naomba nipongeze kwa kazi kubwa ya Mheshimiwa Waziri, pamoja na safu yake yote. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia siku hii ya leo. Kwanza kabisa ninaomba nimshukuru Mungu ambaye ametupa uzima na uhai tuko hapa kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama yetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoendelea kuifanya kwa ajili ya Tanzania. Ninaomba nimpongeze Waziri pamoja na Naibu Mawaziri kwa kazi kubwa ambayo wanaendelea kuifanya katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Sisi Mkoa wa Katavi ametujengea bandari, alitupa bilioni 47. Bandari imekwisha kwa asilimia 100, tunategemea bandari ile tuweze kupata mizigo. Sasa tunaipataje hii mizigo bila kuboresha Bandari ya Dar es Salaam, lazima sasa hivi Watanzania tukubali wawekezaji waje kwenye Bandari yetu ya Dar es Salaam wawekeze ili uchumi wa Watanzania uweze kuongezeka. Kwa sababu maendeleo tunayapenda, tukienda kwa wenzetu, nchi za wenzetu tunafurahi, tunasifia, sasa tunakuja kwetu kuhakikisha sasa maendeleo yanakuja, Serikali inajitahidi kuleta maendeleo, mabadiliko sisi wenyewe tunaanza kupinga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiki ni kitu ambacho hakikubaliki, Mheshimiwa Waziri songa mbele, weka wawekezaji Bandari ya Dar es Salaam wametujengea bandari ili wawekezaji waje, uchumi wa Watanzania uweze kuongezeka. Nakuja kwenye jimbo langu, fidia; Wabunge wenzangu wameongea hapa, najua Waziri anahangaika, safari hii bado hajaweka bajeti yake kuhakikisha analipa fidia, lakini tunaomba Serikali tujipange vizuri, tuhakikishe bajeti inayokuja tuweke pesa ilituweze kuwalipa wananchi wanaotudai fidia. Wengine sasa hivi wameshakufa, huko tukienda katika majimbo yetu watu wanalalamika. Tunaomba sana Serikali ijipange kuhusu fidia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niingie kwa upande wa TRC. Naomba niishukuru Serikali kwa ajili ya standard gauge na kuhusu reli yetu ya kutoka Tabora - Kaliua mpaka Mpanda. Najua Serikali ina mkakati mzuri ina mpango mzuri kuhakikisha gauge zile zinabadilishwa ili treni yetu ya kutoka Tabora kuelekea Mpanda iweze kubadilika. Hata hivyo, nina masikitiko, tuna wafanyakazi ambao ni vibarua ambao wanakaa katika magenge. Wale vibarua wamekaa sasa takribani miaka 15, wengine miaka 20 mpaka leo bado vibarua, lakini wale ndio wanatulindia reli yetu, kwa sababu bila kutunzwa reli ile uharibifu unaweza ukatokea wakati wowote, halafu majanga yanaweza yakatokea wakati wowote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali iwatazame wale vibarua, kulipwa kwao ni shida. Hawalipwi kwa wakati, wanaweza kukaa miezi mitatu, wanakaa porini, wanakaa kwenye mazingira magumu. Naiomba Serikali iweze kuchukua jukumu hili kwenda kuonana nao hususan Mkurugenzi wa TRC, aende akaongee na hawa vibarua. Najua wana mipango mzuri, mikakati mizuri kwa ajili yao lakini waende wakaongee nao ili waweze kupata morale kwa ajili ya kuhakikisha wanakaa kwenye mazingira mazuri hususan wanaokaa Genge la Ugala, Kamini, Kabuziyoti, Katumba, lazima twende tukawaone tuwape moyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana mabehewa ni machache, wasafiri ni wengi. Tunaomba tuongezewe mabehewa, wananchi wanahangaika kutoka Mpanda behewa linakuwa moja au mabehewa mawili, wasafiri wako wengi. Tunaomba wasafiri wa kutoka Mpanda kuelekea Tabora tunaomba tuongezewe behewa. Tuongezewe behewa kwa sababu wananchi wanahangaika, usafiri umekuwa mzuri na usafiri ukiwa mzuri watu wanafurahia ndio maana wanatamani kupanda treni yao, basi tunaomba mabehewa yaongezeke. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilituahidi barabara ya kutoka Kawajese ya lami kupitia Ugala na kujenga Daraja la Ugala. Barabara ile inaenda mpaka Kaliua, Kaliua mpaka Kahama. Naomba Waziri aje kutueleza barabara hii kwa kiwango cha lami na kujenga Daraja la Ugala, vitajengwa lini na lini tutaweka pesa, kwa sababu barabara hii iko kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Tunaomba sana barabara hii iweze kujengwa kwa sababu itafungua fursa kubwa sana kwa ajili ya kutoka Mpanda mpaka Kaliua, Kaliua mpaka Kahama, Kahama mpaka Mwanza, kwa ajili ya maendeleo na fursa mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuna Ziwa Tanganyika, wenzangu wamesema, Ziwa Tanganyika hatuna meli. Tunaomba meli, tulikuwa tuna meli ilikuwa inapita, lakini toka ilivyosimamishwa meli ile mpaka leo hii hakuna meli ya aina yoyote inayofanya kazi katika Ziwa Tanganyika. Tunahitaji meli na sisi watu wa Ziwa Tanganyika tunataka tujengewe meli, kwa sababu maendeleo tunaona, wanatuletea maendeleo mengi na sasa hivi wanatujengea barabara ya lami kutoka Mpanda mpaka Kalema. Sasa ina maana mizigo itakuwa mingi, abiria wako wengi na ndio maana tunasema basi kama hivyo, tuwaweke wawekezaji ili waweze kufanya kazi hii ili maendeleo yaweze kukua katika Nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba niunge mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba nimshukuru Mungu ambaye ametupa uzima na uhai saa hizi tuko hapa tukiwatumikia Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti. Naomba nimpongeze Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa ambayo ameifanya kwa ajili ya utalii. Tumeona jitihada kubwa amefanya kupitia Royal Tour, tumeona kazi kubwa sana, tumeona watalii wakija katika nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Waziri pamoja na watendaji kazi wake wote, Katibu Mkuu na wote wanaowasimamia katika Wizara hii. Kwanza kabisa, naomba niseme ndani ya Jimbo langu la Nsimbo, Mbuga ya Katavi ndiyo ilipo. Hii mbuga haitangazwi kabisa. Sasa Rais katuonesha mfano, kaonesha ubunifu, lakini ninamuamini Waziri wetu Mheshimiwa Mchengerwa, atafanya ubunifu ili Mbuga yetu ya Katavi iweze kutangazwa kwa sababu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwanja wa ndege Katavi upo, ndege zinafika, barabara kutoka kwenye uwanja wa ndege mpaka kwenye eneo letu la mbuga ni ya lami. Sasa sidhani kama kuna kitu ambacho kinaweza kushinidikana kufanya jitihada za kuhamasisha ili mbuga yetu iweze kutangazwa ili watalii waweze kufika Katavi kwa sababu, mazingira tayari yameshakuwa mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji chetu cha Stalike kinapakana kabisa na Mbuga ya Katavi. Kuna mto ambao umetenganisha; naomba nimshukuru sana Kamishna Mwakilema, tumeongenaye amekubali kwenda kuongea na wananchi. Tatizo ni moja tu, wale wananchi toka mwaka 1974 katika ule mto, huko kijijini kabisa wanavua Samaki, lakini leo tumewazuia kabisa kuvua Samaki, nao ndiyo kipato chao cha uchumi. Sasa na Kata ya Stalike ndiyo inayoathirika kwa wanyama wakali. Wakulima wa Kata ya Stalike, wakilima mazao yao yote yanaliwa na tembo, wanaofanya vurugu katika maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani ni jambo la busara tu, sasa hivi twende tukakae tukaongee na wananchi wa Kata ya Stalike ili tuelewane. Kama ni kujengewa mabwawa, basi wajengewe mabwawa, kuliko kuacha na kuwazuia kabisa ili wasiweze kufanya shughuli zozote za kibiashara na kiuchumi katika Mto ule wa Stalike.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni TAWA. Kuna msitu wa Ugara Game Reserve na Msitu wa Msimu Game Reserve. Wananchi walikuwa wanaenda mle ndani katika hayo maeneo kuvuna asali na wameweka mizinga yao ya asali, lakini leo TAWA wamewazuia kuingia kuvuna asali na vilevile wanawa-charge pesa. Akiingia na baiskeli analipa shilingi 10,000, akiingia na pikipiki analipa shilingi 30,000, wakiingia na gari wanalipa shilingi 50,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hii misitu tumeikuta na hizi games tumezikuta, kama wananchi wa Ugalla wao katika Game Reserve ya Ugalla walikuwa wanaishi, ni maisha yao walikuwa wanaishi, ndiyo makazi yao. Wanafanya mila zao za jadi, leo tumewakuta tunawazuia wasifanye mambo yao ya jadi na mila zao. Vilevile kila akiingia atoe shilingi 10,000, akiingia na pikipiki shilingi 30,000. Najua Kamishna wa TAWA, Ndg. Nyanda ni msikivu. Ninavyoongea ananisikia, naomba twende tukakae na wananchi tuweze kukubaliananao ili waweze kupunguziwa ghasia hii ambayo wanaipata sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni TFS, wenzangu wengi wameongea. Nimi jimbo langu limezungukwa na misitu, lakini TFS ndiyo wanaolinda misitu na wananchi wanachotaka ni kitu kidogo tu, wanataka tuwape elimu, tuwashirikishe, tuwaoneshe mipaka kuliko kuwapiga na kuwa-fyekea mazao yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Deus amesema hapa, wananchi wanalima. Sasa hivi TFS wametulia kimya. Saa hizi wametulia. Mvua zikianza kunyesha, wananchi wanalima, wanawatizama, mazao yakishakamilika ndiyo kipindi sasa cha kwenda kufyeka mazao yao na kuwanyanyasa na kuwapiga. Ni dhambi kubwa sana. Kwa nini tusiwaelimishe? Kwa nini tusikaenao kitako tukawaambia hapa ni mipaka yetu, hapa msiingie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge tupo, watushirikishe, twenenao wakaongee na hao wananchi kuliko jinsi wanavyofanya. Wananchi wanateseka mpaka wanapata hasira na Serikali yao. Mheshimiwa Waziri tunajua wewe ni msikivu, tumekuona jitihada zako, kwa kipindi kifupi hiki tumeona kazi kubwa, miezi mitatu ulivyokabidhiwa Wizara tumeona jitihada zako. Tunakuomba Mheshimiwa Waziri, pita katika Mikoa yako yote yenye hifadhi ili uweze kuongea na wananchi. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Lupembe.

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie moja tu, kuna…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, tunakushukuru kwa mchango wako…

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kidogo tu…

MWENYEKITI: …muda wako umekwisha.

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kuunga mkono hoja.
Muswada wa Sheria ya Reli wa Mwaka 2017
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia muswada huu muhimu sana kwa ajili ya wananchi wa Tanzania. Naomba nimshukuru Mungu ambaye ametupa uzima na uhai, tuko mahali hapa kwa mara nyingine tena. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba niipongeze sana Serikali kwa kazi kubwa ambayo wameifanya kwa kuunganisha TRL pamoja na RAHCO kwa sababu tulikuwa tunaipigania sana kwa sababu tulijua shirika hili likiwa pamoja litakuwa shirika kubwa kwa ajili ya wananchi wa Tanzania na tukiangalia Shirika la Reli ambalo lilikuwa linaitwa TRC zamani lilifanya kazi kubwa na shughuli zao zilikuwa nzuri; sasa tulivyogawanyika pale kazi zilikuwa haziendi vizuri kwa sababu TRL walikuwa peke yao na RAHCO walikuwa peke yao, lakini leo tunazungumzia kuunda shirika lingine tena jipya ambalo litafaya kazi vizuri kutokana na sheria hii ambayo tumeileta leo hapa Bungeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kama wenzangu walivyosema; sisi watu wa Mpanda tunahusika sana na reli hii kwa sababu reli hii ndiyo tegemeo kubwa la wananchi wa Mpanda kwa ajili ya kupitia mizigo na abiria. Ndani ya Wilaya ya Mpanda kuna maeneo makubwa sana ambayo wananchi wa Mpanda watabomolewa nyumba zao. Hili jambo ni kilio kikubwa sana kwa wananchi wa Mpanda kwa sababu ukiangalia pale Mpanda Mjini kuna maeneo ya Tambuka Reli na Ugala wananchi wote watabomolewa nyumba.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba tu tusisitize kama sisi Waheshimiwa Wabunge. kwa sababu tunatetea wananchi wetu, Wabunge wengi wamesema kwa ajili ya bomoabomoa hii tunaomba kwa sababu hawa wananchi ni maskini, wengine hawana uwezo kabisa wa kujenga nyumba nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Serikali waliangalie upya wale ambao wapo mbali kidogo wawaache kwa sababu ni tatizo. Sisi Wabunge tunavyorudi huko majimboni, tulirudi kipindi hiki cha nyuma kidogo ilikuwa shida, kila mwananchi anakuja kukulilia tutakwenda wapi tunabomolewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi, ni sikivu, basi waliangalie upya zile mita ambazo wale ambao wako mita mbali kidogo wawaache kwa sababu hii itatuletea shida kidogo kwa sababu wananchi wengi ambao wako katika mguso huu wa kubomolewa nyumba ni maskini sana. Tunaomba Serikali ipitie upya ili tuweze kuwasamehe ambao wapo mbali kidogo wasibomolewe nyumba zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile shirika hili lilikuwa lina wafanyakazi; wafanyakazi wa RAHCO na TRL, kama wenzangu walivyosema, wengine bado wanadai haki zao.

Basi tunaomba Serikali, tunasisitiza walipwe ili hili shirika liweze kwenda vizuri. Vilevile tunampongeza sana Mkurugenzi aliyepewa dhamana ya shirika hili, kulishika TRL na sasa linaingia kwenye TRC, Ndugu Masanja, anafanya kazi vizuri tunaona. Sasa hivi treni yetu inatembea kwa wakati na muda kamili, lakini kuna tatizo kidogo sisi watu wa Mpanda mmetuletea mabehewa machache sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Mpanda wanategemea sana treni. Sasa hivi watu wanaotaka kuunganisha treni kutoka Mpanda mpaka Dar es Salaam wanachaguliwa wanawake 15 na wanaume 15. Hii imekuwa kero wananchi wa Mpanda wanaamka saa 10 za usiku, wanaenda kukaa foleni kusubiri tiketi, mlinzi akitoka pale anawapa wanawake 15 na wanaume 15, hii ni kero kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa sababu hili shirika sasa linaundwa upya, nafikiri mipango na mikakati yake itakuwa mizuri sana. Mpanda kuna abiria wengi sana, tunaomba muitazame Mpanda kwa jicho la huruma; badala ya kutuletea behewa moja, tuleteeni mabahewa hata matatu kwa sababu wananchi wa Mpanda wanapanda sana treni. Sasa hii wanavyopewa wanawake 15 na wanaume 15 inakuwa ni kero na ni shida.

Tunaomba sana mtusaidie kwa hilo kwa sababu shirika hili linaimarishwa upya. Tunaomba basi kuimarisha reli. Sasa kwa sababu shirika hili linakuwa shirika moja, kuna maeneo ambayo RAHCO walikuwa hawajayapitia sasa reli haikuwa nzuri, ilikuwa inadengadenga (inasuasua). Basi sasa kwa sababu shirika ni moja, tunaomba uimarishaji wa reli kutoka Mpanda mpaka Tabora uwe mzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwenzangu amezungumzia kuhusu magenge. Haya magenge yalikuwa yanasaidia sana kwa sababu kutoka genge moja mpaka genge lingine kama hakuna uangalizi, kuna watu majangili ambao wanakwenda kung’oa reli, wanang’oa reli treni ikifika pale inaweza kudondoka.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi hii nina mfano nayo kabisa, kuna siku moja nilikuwa nasafiri kutoka Katumba kuelekea Ugala, hapo katikati kulikuwa na magenge yamefungwa. Sasa kuna majangili walienda kung’oa zile reli, bahati nzuri kulikuwa kuna mwehu akaisimamisha treni na yule dereva alikuwa mtiifu akasema huyu mwehu anaisimamisha hii treni acha nisimamishe; alivyosimamisha yule mwehu akamwambia usipite huko wameng’oa mataluma, yule dereva alimsikiliza yule mwehu, kweli kushuka kwenda kuangalia akakuta mataluma 10 yametolewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa huyu dereva asingekuwa msikivu yale mabehewa ya ile treni yangeanguka na watu wangepata ajali na wengine wangepoteza maisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, haya magenge yalikuwa yanasaidia kwa sababu wale maafisa magenge kule vijijini walikuwa wanapita kuisafisha, ile reli, ilikuwa inakuwa imara treni ikija inapita kwa usalama na wananchi wanakuwa wako katika hali ya usalama zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, TRC ilikuwa ina majengo makubwa sana, shirika hili lilikuwa kubwa, lilikuwa na mtazamo mpana, walikuwa wana Mahoteli kama Railway Hotel, Iringa Hotel, walikuwa wana mabasi, shirika hili lilikuwa kubwa sana. Sasa kutokana na kuingia kwenye ubia yela majengo yote yakagawanyika, yakauzwa na mengine yakatelekezwa maana yake mengine yamekuwa kama vile magofu. Ninaomba kupitia hili Shirika jipya ambalo tunaliunda upya, yale ambayo yaliyokuwa yanafanywa wakati ule, walikuwa wana magari ya mafuta, walikuwa wana mabasi, viimarishwe zaidi kwa ajili ya wananchi ili waweze kupata usafiri wao kwa urahisi na wepesi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ahsante naunga mkono hoja asilimia mia moja.
The Water Resources Management (Amendment) Act, 2022
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia Muswada wetu huu wa leo, wenye manufaa katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa naomba nimshukuru Mungu ambaye ametupa nafasi hii ya uzima na uhai. Naomba nimshukuru sana Waziri ambaye ametuletea Muswada huu kwa ajili ya manufaa ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niipongeze Serikali kwa kuona sasa ni kipindi cha kulinda rasilimali zetu za maji, kwa sababu maji ni uhai na bila maji hakuna kitu chochote kinachofanyika katika maisha ya binadamu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangali kupitia maji katika maeneo mbalimbali ya mabonde na kupitia mabwawa, bila kuweka udhibiti hakuna kitu chochote kinaweza kufanyika. Sasa tunaona jitihada za Wizara kutuletea huu Muswada, ambao utatuwezesha kudhibiti maji, kwa sababu katika maeneo mengi kupitia vyanzo vya maji, kupitia hifadhi mbalimbali tumeona uharibifu ni mkubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niIpongeze Serikali kwa kuona sasa ni kipindi cha kulinda rasilimali zetu za maji kwa sababu maji ndio uhai na bila maji hakuna kitu chochote kinachofanyika katika maisha ya binadamu. Ukiangalia kupitia maji katika maeneo mbalimbali ya mabonde na kupitia mabwawa na nini, bila kuweka udhibiti hakuna kitu chochote kinaweza kufanyika. Sasa tunaona jitihada za Wizara kutuletea huu Muswada sasa tunaweza kudhibiti maji, rasilimali ile maji kwa ajili ya manufaa kwa sababu katika maeneo mengi kupitia vyanzo vya maji, kupitia hifadhi mbalimbali tumeona uharibifu ni mkubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unakuta kuna watu wengine wanathubutu kuingia katika maeneo ya vyanzo vya maji ambavyo vile vyanzo vya maji ambavyo tukivitunza na tukaviweka katika mazingira mazuri ambayo sisi wenyewe tunakuja kuvitumia na kupata manufaa na faida kwa ajili ya mahitaji ya binadamu. Tumeona kwenye mabwawa mbalimbali watu wanaingiza mifugo, watu wanafanya wanavyotaka wao, watu wanavuta maji kiholela, ina maana udhibiti haukuwepo, lakini leo tunaona Serikali imeleta Muswada huu ambao utasaidia sasa kuhakikisha mazingira yetu yatakaa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia sasa katika hali halisia, uoto wa asili katika nchi yetu unaanza kupotea na uoto wa asili ni kitu muhimu sana. Vile vyanzo ambavyo zamani sisi wakati tunakua kulikuwa kuna chemchem, maji tu yanatoka chini, lakini zile sehemu zote zimepotea kutokana na uharibifu mkubwa ambao uliofanyika. Hata hivyo, kupitia Muswada huu utaweza kudhibiti sasa vile vyanzo vyote vya maji na mazingira yatakuwa mazuri. Tunajionea katika nchi yetu hata mvua sasa imekuwa ni ya kusuasua, mazingira yamekuwa si rafiki sana, unakuta tunapata tabu kwa sababu tumeshaharibu mazingira yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zamani tulikuwa tunatunza miti, sasa ile miti yote tumeshaiharibu, matokeo yake sasa hata mvua zimekuwa za kusuasua. Ingawa tunasema tumwombe Mungu atuletee mvua lakini mazingira tumeshayaharibu, lakini kupitia Muswada huu uliokuwa mbele yetu sasa tutaweza kupata mvua nzuri na vile vyanzo vyote vinaweza kudhibitiwa, kulindwa na tukaweza kupata manufaa makubwa kupitia miradi mikubwa mikubwa. Hii ni kwa sababu tukitunza vyanzo vya maji vizuri, tukitunza rasilimali zetu za maji, mazingira yetu yatakuwa mazuri, uoto wetu utarudi kama kawaida, tunaweza sasa tukatengeneza miradi mikubwa mikubwa kwa manufaa ya wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niipongeze Serikali kwa kuona sasa kupitia rasilimali hizi za maji, kuhakikisha kwenye maeneo yetu sasa udhibiti na usimamizi na wanawake nao wamekumbukwa kwa ajili ya kuwa katika vile vikao, upande wa jinsia wanawake wawili wapo. Tunajua akinamama ndiyo wahusika wakubwa wa tatizo na wanawake ndiyo wahangaikaji wakubwa kupitia maeneo yetu katika vijiji na vitongoji. Naomba niipongeze sana Serikali kwa kukumbuka uwiano wa kijinsia katika uongozi mbalimbali kwa maslahi yetu katika maeneo yetu katika masuala ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua watu wengi wanapenda kuchangia kwa sababu Muswada huu uliokuwa mbele yetu ni mzuri na ni jambo muhimu sana. Naomba niishukuru Wizara kwa kuwa itaweka maabara maalum kwa ajili ya kuhakikisha sasa ubora wa maji unapatikana katika kila eneo. Maana yake zamani maabara ilikuwa iko moja tu na Wizara kama Wizara ilikuwa haina maabara kila wilaya au kila mkoa, lakini sasa hivi tunaona Serikali inaamua sasa kuanza kuweka maabara kwa ajili ya usafi wa maji yetu na kuhakikisha tunapata maji safi na salama kupitia maji taka na usafi wa mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naomba nimpongeze sana Waziri kwa kazi kubwa ambayo anaendelea kuifanya. Anafanya kazi tunaona jitihada zake na watu wa mabonde wapo katika maeneo yetu wakiendelea kutafuta mazingira ya maji ili wananchi waweze kupata maji, naomba nimpongeze sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kuunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. (Makofi)