Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Frank George Mwakajoka (30 total)

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Jambo la kwanza kabisa nipende kuchukua nafasi hii kukushukuru wewe kwa kunipa nafasi hii. Pia nichukue nafasi hii kuwashukuru sana wananchi wangu wa Mji wa Tunduma kwa kunipa nafasi hii ya kuhakikisha kwamba nakuwa Mbunge, nawawakilisha katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilichokuwa nataka kuzungumza ni utawala bora. Tunapozungumzia utawala bora katika nchi hii hakuna. Jmbo lingine tunasema kwamba tunakaa kwa amani hatukai kwa amani bali tunakaliana kwa amani katika nchi hii; ndicho ambacho kinaonekana katika Taifa hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninazungumza haya kwa sababu nina mifano mingi sana ambayo nataka kuitoa mbele yako. Mfano wa kwanza nilivyosema kwamba hakuna utawala bora, nimeona katika uchaguzi kwa ajili wa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, uchaguzi umefanyika tarehe 25/10 kupata Madiwani lakini Meya wa Jiji Dar es Salaam amekuja kupatika mwezi Machi, 2016. Jambo hili linaonesha ni jinsi gani Serikali ya Chama cha Mapinduzi haiko tayari kuheshimu utawala bora na pia kuheshimu demokrasia katika Taifa hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni aibu kubwa pia kwa Kiongozi wa Kitaifa kushindwa kuwaheshimu viongozi wa chini. Alivyokwenda kuzindua na kufungua miradi ya maendeleo katika Jiji la Dar es Salaam alishindwa kumtambulisha Meya wa Jiji la Dar es Salaam na kumpa nafasi ili aweze kuzungumza ili kuwakilisha Jiji la Dar es Salaam. Jambo hili linanikumbusha mbali sana, namkumbuka sana Mwalimu Nyerere aliwaheshimu mpaka Wenyeviti wa Mtaa na Madiwani katika maeneo waliyokuwa wakiishi. Nashangaa utawala wa Dkt. Magufuli umekuwa unadharau viongozi wadogo na wao wakitegemewa kuheshimiwa baadaye jambo hili litakuwa ni ndoto kwao kwa sababu hawaheshimu utawala bora na demokrasia hakuna.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni madai ya Walimu. Kila wakati tunasikia Chama cha Mapinduzi wanajinasibu kwamba kuna elimu ya bure, mimi nasikitika sana katika Taifa hili hakuna Mtanzania hata mmoja anayependa elimu ya bure wala kitu cha bure. Tunasema elimu inayotolewa sasa hivi itolewe kwa kodi za Watanzania na siyo elimu ya bure. Kwa hiyo, tafsiri kuanzia leo tunahitaji elimu inayotokana na kodi za Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia tusitegemee kupata elimu bora kama Walimu wanakuwa na madai makubwa, hawawezi kutimiziwa haja zao za kupata mishahara na wakati maisha yao na mishahara yao pia ni midogo. Ni vizuri Serikali hii ikajaribu kutazama kwanza huduma za Walimu ambao wanatoa elimu lakini pia ikaangalia ni namna gani inaweza ikaboresha maslahi ya Walimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni kuhusiana na mambo ya TAKUKURU. TAKUKURU ni taasisi muhimu sana katika Taifa hili na kama kweli tunahitaji uwazi na tunahitaji utendaji kazi mzuri ambao utaondoa mashaka ya rushwa katika nchi hii ni lazima TAKUKURU wapewe nafasi ya kuwa na uwezo wa kupeleka shtaka mahakamani bila kumpelekea mtu yeyote kufanya uchunguzi. Jambo hili katika rekodi mbalimbali linaonyesha kwamba kesi nyingi ambazo TAKUKURU wanajaribu kupeleka mahakamani wanashindwa kwa sababu kesi zile zinaandaliwa na watu ambao hawakuhusika.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ushauri huu Vyama vya Upinzani vinatoa kila wakati ndani ya Bunge ni vizuri mkasikiliza kwa sababu tunatoa kwa faida ya Taifa hili na si kwa faida yetu sisi. Inaonekana kwamba hakuna hata siku moja mmesimama mkakubali kusikiliza ushauri huu na mnaendelea kuanzisha taasisi ambazo hazina meno, wala hazina tija na haziwezi kutekeleza majukumu yake ipasavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niende katika suala la biashara. Nchi yoyote duniani haiwezi kuendelea kama wafanyabiashara wake wataendelea kuwa maskini na watakuwa hawatengenezewi mazingira mazuri ya kufanya biashara. Taifa hili wafanyabiashara wamekuwa kama wanyonge katika Taifa lao, wafanyabiashara sasa hivi wameshindwa kuangiza mizigo nje kwa sababu ya taratibu mbalimbali ambazo haziwapi nafasi ya kufanya biashara na kuwa na mitaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mataifa mengi duniani yanaandaa wafanyabiashara ili waweze kupata mitaji na baadaye wawe walipa kodi wakubwa katika Taifa lao. Nchi yetu ya Tanzania imeonekana kwamba sasa wafanyabiashara wote wanaoibuka katika Taifa hili wamekuwa wanabanwa na wanashindwa kutekeleza wajibu wao vizuri. Tunasema Serikali lazima ibadilike, iwatazame wafanyabiashara na iwaandae vizuri ili waweze kuwa wafanyabiashara wakubwa na waweze kulinufaisha Taifa hili na waweze kuwa walipa kodi katika Taifa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ninalotaka kulizungumzia ni kutoa mfano wa Bandari ya Dar es Salaam. Bandari ya Dar es Salaam sasa inakwenda kufa siyo muda mrefu kwa sababu tumeshindwa kuingia kwenye ushindani wa kibandari na mataifa yaliyoko jirani na sisi. Angalia leo katika takwimu za mizigo ambayo inashuka katika Bandari ya Dar es Salaam, Zambia peke yake ni asilimia 34 ya mizigo imeshapungua wanashusha katika Bandari ya Beira. Kwa maana hiyo tumeshindwa kuingia kwenye ushindani wa kibandari kwa sababu ya kuweka masharti ambayo hayana tija kwenye bandari zetu. Lazima tufike mahali tubadike na tutazame ni namna gani tunaweza tukajenga uchumi bora kama tutaendelea kuua vyanzo vya mapato ambavyo tunavyo sasa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, watu wa Kongo ni karibuni asilimia 46 wameacha kupita pale. Sababu ni kwamba Wizara ya Uchukuzi wameingia mkataba na Congo DRC Lubumbashi kuhakikisha kwamba mizigo yote wanayokuja kuchukua katika bandari ya Dar es Salaam wawe wanalipia kwanza. Wakongo wameona huu ni upuuzi, wameamua kuhamia kwenye Bandari ya Beira na sasa hivi wanapita kule wanaendelea na shughuli zao. Kwa hiyo, tunaomba sana Serikali inapoanzisha jambo ijaribu kupima na kutathmini jambo hili lina hasara gani katika Taifa letu.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine tumepata taarifa na tunasikia kwenye vyombo vya habari Mheshimiwa Rais anawaambia vijana waende vijijini wakalime. Vijana kwenda kulima vijijini kunahitaji pia maandalizi ya kutosha, je, wana mashamba, wamewezeshwa kiasi gani kwamba wanaweza wakafika kijijini na wakaanza kulima kilimo chenye tija na kujiletea maendeleo? Tunaomba sasa Serikali ya Chama cha Mapinduzi wanapotoa matamko wajaribu kutazama ni nini ambacho wanamaanisha, wasiwaswage wananchi na kueleza kwamba ni lazima waende kijijini, hata yule mwananchi ambaye yuko kijijini anayelima haoni tija ya kuendelea kulima kwa sababu hakuna masoko ambayo yako na pia haelewi ni namna gani ya kulima kwa sababu tija hakuna katika kilimo hiki. Tunaomba Serikali ijipange, iwawezeshe Watanzania ili kuhakikisha kwamba Watanzania hawa hata kama wanakwenda kulima watakwenda kulima kilimo chenye tija ambacho kitawasaidia zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia tunasikia matangazo mbalimali kuhusiana na vifo vya kina mama na watoto. Leo hii katika taarifa hii inaonesha kwamba mpaka 2018 watahakikisha kwamba kuna punguzo la vifo vya akina mama na watoto kwa asilimia 20, jambo hili ni aibu sana. Kwa kweli kifo kinafika mahala tunaweka takwimu za kupunguza asilimia 20, ni mambo ya ajabu kabisa. Lazima tufike mahali tujadili, hivi leo kama Wabunge wangekuwa wanatuwekea hapa wanasema jamani Wabunge tunakufa sana humu tupunguze asilimia 20 kwa bajeti ambayo tunaiweka, kila mmoja angekataa kwamba afadhali tuweke bajeti asilimia 100.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa tutazame jambo hili kwa umakini zaidi, tuangalie maisha ya watu, tuangalie maisha ya wananchi wetu kama kuna tatizo la kuweka fedha kidogo, fedha iongezwe kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wanasaidia akina mama na watoto ili waendelee kuwa wazima na watu wanaobeba ujauzito wawe na uhakika kuzaa watoto na watoto wao kuwa hai muda wote. Jambo hili tunaona lazima lifanyike haraka iwezekanavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni matangazo ya television kukatishwa…
Bado Mheshimiwa, kengele ilikuwa bado Mheshimiwa.
Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii nami niweze nitoe mchango wangu katika Wizara hii. Awali ya yote niwashukuru sana wananchi wangu wa Jimbo la Tunduma, pia niitumie fursa hii kumshukuru sana Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa hotuba nzuri na hotuba ambayo ikifuatwa na Mheshimiwa Nape akiitumia ninajua Tanzania hii itabadilika kwa ajili ya Wizara yake.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi kubwa ambayo nataka kuizungumzia siku ya leo ni kuhusiana na matangazo ya TBC kwa wananchi. Jambo hili linasikitisha sana, wananchi wanasikitika sana kwa kuzimiwa matangazo yao ya live ili waweze kuona Wabunge wao wanafanya nini. Tumepata taarifa hapa mara nyingi CCM wanasema wanataka kutukomesha ili umaarufu upungue, tunataka kutoa taarifa katika Bunge hili kwamba tulikotoka ni maarufu na ndiyo maana tuko Bungeni. Kwa hiyo, hatuoni sababu hata moja ambayo tunafikiri CCM watatupunguzia umaarufu, sisi ni maarufu na tutaendelea kuwa maarufu na wao wataendelea kushuka umaarufu kwa sababu wamekuwa waoga kupita kiasi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema, tumepata taarifa mbalimbali hapa wanasema gharama ni kubwa, lakini kuna vyombo ambavyo vilijitokeza kwamba wangeweza kutoa matangazo kwa wananchi, jambo la kushangaza ni kwamba pia wamewekewa mgomo na sasa hivi wanafika mahala wanachambua taarifa ambazo siyo sahihi na ambazo hazina umuhimu kwa wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa sana, Mheshimiwa Magufuli wakati anahutubia Bunge hili, alisema kwamba hii ni Serikali ya uwazi, sasa ni Serikali gani ya uwazi ambayo inaweza kufanya uwazi, bila kuweka masuala ya habari na kuweka taarifa hizi live wananchi waweze kusikia. Tunafikiri kama Upinzani tunajua kabisa kwamba Bunge ni chombo muhimu na kikao hiki ni kikao cha bajeti, ni jambo muhimu sana kwa wananchi wetu. Wananchi wanataka kujua wawakilishi wao waliokwenda Bungeni wanasema nini, ni fedha gani zinatengwa kwenda kwenye majimbo yetu na ni kazi gani ambayo Serikali itakwenda kufanya. Hatujaja hapa kuuza sura, kama wanavyosema Wabunge wa Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii ukiwauliza Watanzania, ni Waziri gani au ni mtu gani anayechukiwa sana katika nchi hii, watamtaja Mheshimiwa Nape Nnauye, kwa sababu tu ya kuzuia matangazo.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, watamtaja Nape Nnauye kwamba ni mtu ambaye anachukiwa sana katika nchi hii. Ninazungumza haya maneno kwa sababu tumejaribu kuangalia katika mitandao mbalimbali tumeona watu wanavyolalamika, wanavyolaani kitendo hiki na siamini kama Mheshimiwa Nape Nnauye atarudi Bungeni mwaka 2020.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, atang‟olewa tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie jambo lingine ambalo linahusiana na michezo, tusifikirie kama tunaweza tukabadilisha michezo katika nchi hii kama tutaendelea kuendekeza siasa kwenye masuala ya msingi. Masuala ya kitaalam yaende kwenye utaalam, na masuala ya kisiasa yaende kwenye siasa. Leo nchi hii imetekwa na wanasiasa kila jambo linalofanyika wanasiasa ndiyo wao wanalolifanya, hata jambo la kitaalam.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hauwezi kupata timu bora ya Taifa, hauwezi kupata timu bora ya mpira kama hutaanzisha shule za vipaji maalum kwa ajili ya michezo, haitawezekana hii itakuwa ni ndoto ya alinacha, hata mngetenga bilioni 100 hapa, hata mngetenga trilioni 10 jambo hili halitaweza kubadilika, tutaendelea kubaki kichwa cha wendawazimu. Brazil ni nchi ambayo inatoa wachezaji wengi sana ambao wanacheza professional, lakini leo bado wanaanzisha shule za vipaji maalumu. Ukienda Ivory Coast, ukienda Ghana, ukienda Nigeria na maeneo mengine, sisi tumekalia siasa tunakaa tunazungumza humu, badala ya kuweka mipango na mikakati mizuri kwa ajili ya kutengeneza ajira za vijana wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tukubaliane kwamba mpira na michezo yoyote ni ajira kwa vijana wetu, tunahangaika ajira wakati tukitengezeza ajira za kuwawezesha vijana wetu kuwajengea viwanja na kujenga shule ambazo zinaweza zikawasaidia wao kuinua vipaji vyao, tutakuwa tumeongeza ajira katika nchi hii, lakini tunakalia siasa, tunafanya siasa hata kwenye masuala ya msingi, nataka nimuulize Waziri, wakati anakuja hapa kujibu maswali haya, anataka kujibu hoja zangu afike ajibu hoja.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, wale vijana ambao walikwenda Brazil, wakaenda wakachukua kombe la Coca-Cola wako wapi wale vijana kama kweli Serikali hii ina dhamira ya kweli ya kuendeleza michezo na kuinua vipaji vya watoto na wananchi katika nchi hii. Wale watoto wako wapi, aje atuambie kama ni utaratibu, kama kweli vijana wanaotoka Tanzania wanakwenda kushiriki kombe la Coca-Cola nchini Brazil wanashinda wanakuja na kombe halafu vijana wale Mwaka mmoja wanapotea mpaka leo hawaonekani, leo tumekaa humu tunasema tunataka kutengeneza bajeti, ni bajeti ya aina gani tunayotengeneza ya kuinua michezo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya yote ni maigizo, ni maigizo ndani ya Bunge hili na lazima Serikali ya Chama cha Mapinduzi iendelee kupokea ushauri na isipoendelea kupokea ushauri tutaikuta ikisuasua mwaka 2020 kwa sababu haitaki kufuata ushauri tunaoutoa katika Bunge letu hili hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ninataka kulizungumza hapa ni kuhusiana na wasanii. Leo ukienda kwenye redio zetu na televisheni zetu asilimia 90 ya nyimbo zinazopigwa na kuoneshwa kwenye tv ni wageni ndiyo wanaooneshwa. Tunataka uzalendo wa namna gani, tunataka tuwafundisheje wananchi wetu wapende miziki yetu na kuwathamini wasanii wetu kama hatutaweza kuchukua hatua. Ni lazima Serikali ikae na iangalie ni namna gani itawajengea uzalendo wananchi, kuhakikisha kwamba wanawapenda wasanii wao na wanatumia nafasi ya kujinufaisha kwa kutumia nguvu za wasanii wao.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima tufike mahala tukubaliane, kwamba Serikali hii haijajipanga na la lazima ijipange, leo asubuhi nilikuwa najiuliza nasema, hivi kwa bajeti ilivyooneshwa humu katika bajeti hii ambayo imesomwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, nikawa nafikiria nikamuuliza Mheshimiwa Sugu nikasema, hivi kuna siku Nape amewahi kuwa mwanamichezo mpaka amepewa Wizara hii. Maana yake niliona ni maajabu yaliyomo humu, haya ambayo tunayazungumza hakuna hata moja lililoandikwa humu, sasa jambo hili ni la ajabu sana, Waziri unapimwa kutokana na mambo ya msingi ambayo yanaoneshwa humu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaamini kwamba bajeti hii, hata TFF hawajashirikishwa, na ndiyo maana mambo ya msingi ambayo yalikuwa yanatakiwa yahusu mambo ya soka kwenye nchi hii hayaonekani humu. Tunaona tu semina zinakuwa nyingi, semina elekezi zinakuwa nyingi, hatutaweza kwenda huko, ni lazima turudi tuangalie misingi ya kujenga nchi yetu. Haitajengwa nchi hii kwa sababu tu ya kuzungumza na kuja kucheka cheka humu ndani, kuna watu wengine wanasimama humu ndani, amesimama Mheshimiwa Malembeka, anazungumza hapa anasema eti akina mama wamepewa mimba, inawezekana na yeye imegoma mimba, tutajuaje.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwanamke yeyote ni wajibu wake kubeba mimba, na hiyo ni mipango ya Mwenyezi Mungu, siyo mipango ya binadamu. Leo anakuja Bungeni badala ya kuchangia hotuba hii, anaanza kuzungumza mambo ambayo hayastahili. Ni lazima Serikali ifike mahala ibadilike.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza haya maneno wengine wanasema ukiwa humu huonekani, ukiweka maji kwa wananchi watakukubali, kuweka maji siyo hisani, ni kodi za wananchi. Serikali lazima ifanye hivyo kwa sababu imepewa mamlaka ya kufanya hivyo, na inakusanya kodi za wananchi. Kwa hiyo masuala ya msingi ni lazima tufike mahala tuyajenge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ndugu zangu Watanzania, kwa nini tusijiulize miaka yote Filbert Bayi amestaafu kukimbia, mpaka leo hakuna mchezaji hata mmoja anayewakilisha vizuri nchi yetu huko nje, kwa nini hatujiulizi? Kwa nini tunaendelea kulala usingizi? Kwa sababu tu ya mambo ya kisiasa, tunatoa takwimu za uongo humu, wakati takwimu sahihi hatutaki kuzichukua na tuzifanyie kazi. Kutokana na hali halisi na kichefuchefu nilichonacho, ningeomba kwa kweli niishie hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru sana kwa kupata nafasi hii niweze kuchangia katika Wizara hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo langu liko mpakani kabisa mwa Zambia na Tanzania. Ni Jimbo ambalo ni lango kuu la nchi za Kusini na kati mwa Afrika. Jimbo la Tunduma linakuwa na wageni wengi sana ambao wanatoka nchi mbalimbali; South Africa, Botswana, Zimbabwe, Congo, Malawi na Zambia. Cha kushangaza katika Serikali yetu hii huwezi kuamini, Mji wa Tunduma hauna umeme wa kutosha kabisa. Wageni wengi katika Mji wa Tunduma sasa hivi wanakwenda kulala Zambia kwa sababu ya kuhofia usalama wao kutokana na giza kubwa linalokuwepo katika Mji wa Tunduma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimshauri tu Mheshimiwa Waziri wakati anakuja hapa atuambie, ni lini Tunduma tutapata umeme wa kutosha ambao utasaidia kuwavutia wawekezaji na watu wanaotumia Bandari ya Dar es Salaam ili waweze kutumia gesti zilizoko Tunduma na kuweza kukaa katika nyumba ambazo tumezijenga katika Mji wetu wa Tunduma kuliko kuwa na giza katika mpaka wetu?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni aibu kubwa sana kwa nchi kama Tanzania ambayo sasa mpaka wa Tunduma ni mkubwa unaoingiza fedha nyingi. Miezi sita tu ulikuwa umeingiza karibuni shilingi bilioni 22 kwenye mpaka wetu wa Tunduma. Huwezi kuamini, hata maji Tunduma pale, imefika mahali mashine zetu za kuvutia maji kila siku zinakufa kwa sababu ya umeme kuwa mdogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka Mheshimiwa Waziri atuambie leo, kwamba ni lini atahakikisha umeme wa pale utakuwa vizuri? Kama wameshindwa kuleta umeme Tunduma, tuna transforma pale upande wa Zambia, miaka ya nyuma tulikuwa tunatumia umeme wa Zambia. Tunaomba watuunganishe na umeme wa Zambia ili wananchi wetu wa Mji wa Tunduma waweze kuwa na umeme masaa 24. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna mitaa mingi sana kwenye Mji wangu wa Tunduma haina umeme. Mitaa hiyo ni Namole, Msambatuu, Chiwezi na Mtaa wa Niumba, hawana umeme kabisa. Tunavyozungumzia mitaa, ina maana ni maeneo ambayo yako mjini, lakini huwezi kuamini, hakuna umeme kabisa. Wananchi wanalima vizuri, wanazalisha, lakini wanashindwa kupata huduma muhimu za umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri, atuambie, ni lini atahakikisha kwamba wananchi hawa, maeneo ambayo nimeyataja wanahakikisha kwamba wanapata umeme kwa kipindi hiki ambacho tunacho.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia imekuwa ni tatizo kubwa sana katika nchi yetu, kwamba katika Wilaya zetu ambamo wamepelekwa Mameneja wa Wilaya, wamekuwa wanalalamikiwa sana na wananchi katika maeneo yale, kuna mambo ya msingi sana ambayo ilitakiwa Wizara ifanye, lakini imefika mahali wanashindwa kufanya kwa sababu fedha ambazo zinakuwa zimepangwa kwenye bajeti kwa ajili ya kuweka umeme, unakuta fedha zile hazifiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba sana, tunapotengeneza bajeti hapa Bungeni na tunapitisha, tunaomba hizi fedha ziende katika maeneo hayo ili zikawatumikie wananchi, waweze kupata huduma ya umeme. Kitendo cha kutengeneza bajeti hapa halafu baadaye bajeti zile zinashindwa kuwafikia wananchi kama tulivyokuwa tumepanga, ni kurudisha maendeleo nyuma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tukubaliane kabisa, hakuna nchi yoyote inaweza kupiga hatua kama nguvu ya umeme katika nchi hii itakuwa chini kiasi hiki. Wananchi wengi sana wamejiajiri, hasa vijana, wamejiajiri, wanachomelea, wana viwanda vidogo vidogo, lakini vile viwanda sasa hivi vimeanza kufa na wameshindwa kufanya kazi hizo kwa sababu ya kukosa umeme katika nchi hii. Tunaomba nchi hii iachane na mazoea ya kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki; wawe na muda mzuri wa kutekeleza na kufanya mambo ambayo yanaweza yakawasaidia wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Tunduma nimeshamwambia Waziri wa Uchukuzi, Waziri wa Maji na sasa namwambia Waziri Profesa Muhongo, wahakikishe kwamba wanaleta umeme na huduma zote za kijamii kwenye Mji wa Tunduma kwa Wizara zote, zinapatikana pale kwa sababu sisi ndio tunaolinda Bandari ya Dar es Salaam. Bandari ya Dar es Salaam asilimia 60 ya mzigo unapitia kwenye mpaka wa Tunduma. Kwa hiyo, tuna….
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima napenda kukushukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi nichangie mchango wangu katika Wizara hii. Nimepitia kitabu cha bajeti katika kusoma nimeona uendelezaji wa miji sijaona Mji wa Tunduma. Kila mmoja anajua kuwa Mji wa Tunduma unakua kwa kasi kubwa na ni lango kuu la kuingilia nchi za Kusini na kati mwa Afrika. Hivyo, kutokuweka Mji wa Tunduma katika miji itakayoendelezwa ni kutokuitendea haki Halmashauri ya Mji wa Tunduma. Kasi ya ujenzi katika Mji wa Tunduma ni kubwa sana na hatuna kiwanja hata kimoja kilichopimwa hivyo sasa ujenzi ni holela. Pamoja na kutokuona Mji wa Tunduma katika kitabu cha bajeti, naomba Waziri atuingize.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika miaka mawili iliyopita tulifanya mchakato wa kutafuta namna ya kukopa katika taasisi za fedha na baadaye turejeshe baada ya kuuza viwanja, lakini tulikataliwa na TAMISEMI. Hivyo, tunaomba Wizara itusaidie kupata fedha katika taasisi za fedha ili kupima haraka Mji wa Tunduma kabla haujaharibika sehemu zote. Wananchi wanahitaji viwanja, hata leo ukipima viwanja 5,000 ndani ya miezi miwili hutapata kiwanja watakuwa wamemaliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaomba sana Wizara itupatie pesa ili tupate master plan ya Mji wa Tunduma ili kurahisisha kazi za upangaji wa mji wetu wa Tunduma. Nashauri Halmashauri zote nchini zipate master plan katika kurahisisha kupima na kupanga miji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua mpango wa kurasimisha makazi (MKURABITA). Mwaka 2012-2013 walikuja Tunduma na kupima baadhi ya maeneo kama Kata ya Maporomoko na Kaloleni katika mitaa ya Kaloleni, Danida, Kastamu, Nelo, Migombani na wakawahamasisha wananchi kufungua akaunti wakaanza kukusanya pesa na kuziweka katika akaunti ile mpaka leo hakuna kinachoendelea pamoja na kuchimba mawe yaani kuweka alama ya kuwa eneo limepimwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini mpango huu uliowaacha njia panda wananchi wa kata hizo bila kujua nini kitaendelea utamalizika?
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mji wa Tunduma kuna migogoro ya ardhi kati ya wananchi wenye mashamba na Halmashauri baada ya Afisa wa Ardhi Mteule wakati bado tuko Mbozi kupima maeneo ya watu bila kuzungumza nao na bila kuwalipa fidia na kuwauzia wananchi wengine katika Kata za Mpemba, Katete, Chapwa na Chipaka huo ulikuwa mwaka 2011 na 2012. Hivyo tunaomba pia Waziri afike katika Halmashauri yetu awasaidie wananchi kwani wanamsubiri kwa hamu kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia mpaka wa Tanzania na Zambia ni tatizo. Nyumba zimeingiliana, Watanzania wameingia Zambia na Wazambia wameingia Tanzania hivyo kuzua sintofahamu kwa wananchi wetu pamoja na Zambia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kupata nafasi hii ya kuchangia Mapendekezo ya Mpango wa mwaka 2017/2018 pamoja na Mwongozo wake.
Ningependa nianze moja kwa moja na upungufu wa mizigo kwenye bandarii yetu ya Dar es Salaam. Nilikuwa nafikiri ni vizuri zaidi Serikali hii ikajikita kukubali kushauriwa na Waheshimiwa Wabunge wanavyotoa ushauri wao, na pia niwashauri sana Wabunge wetu katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tujikite kwenye majukumu yetu ya kuishauri Serikali na kuisimamia Serikali. Kazi ambayo inafanyika sasa hivi kwenye Bunge hili ninaifananisha sana na picha za zamani za kihindi ambazo wakati bosi anatembea, alikuwa anatembea na watu walikuwa wanaitwa masuzuki, yule suzuki alikuwa anakaa pembeni kwa bosi na bosi akigeuka tu hata akikohoa yeye anaondoa miwani kwenye macho akifikiri ameitwa au anaagizwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni vizuri sana tukapunguza uoga na tukasimama kwa miguu yetu kama Wabunge ili kulisaidia Taifa hili. Taifa hili lina watu wengi ambao wamepewa majukumu, ni wasomi wazuri, lakini pia ni wataalam ambao tumewaweka kwenye Wizara mbalimbali kuhakikisha kwamba wanaisaidia Taifa. Wataalam hawa tumefika mahala sisi wanasiasa tumeanza kuwaingilia, wameshindwa kutekeleza wajibu wao kufuatana na utaalam unaowaruhusu waweze kufanya kazi hizo. Jambo hili tukubaliane kwamba Taifa hili haliwezi kwenda kwa mtindo huu kama wanasiasa tutaingilia shughuli zote za kitaalam na sisi tukawa kwenye maagizo badala ya kuangalia ni namna gani tunaweza tukaishauri Serikali na kuhakikisha kwamba Serikali inatekeleza wajibu wake ipasavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi huwezi kuamini, nchi imebaki ni nchi ya matamko kila mmoja anatoa matamko pale anapoweza, hakuna mwongozo unaoonesha kwamba ni nani anatakiwa kufatwa hapa. Wataalam wetu sasa hivi wameshashuka thamani na utaalam wao haueleweki tena kwa sababu ya sisi wanasiasa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakumbuka sana wakati Mheshimiwa Rais ameapishwa na wakati anaanza kutembelea wadau mbalimbali kujaribu kupata mawazo alikutana na wafanyabiashara katika nchi hii. Wakati anakutana na wafanyabiashara kwenye nchi hii jambo la kwanza alilolizungumza aliwauliza ni nani mmoja wenu aliyenichangia hata shilingi moja wakati wa kampeni. Swali hili lilikuwa ni swali gumu sana kwa wafanyabiashara ambao waliitwa wakitegemea kabisa kwamba Mheshimiwa Rais angeweza kuwashukuru pia kwa kazi kubwa waliyoifanya kuhakikisha kwamba wanaendeleza viwanda vyao, wanaendeleza biashara zao na wanalipa kodi katika Taifa hili mpaka alipolikuta.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini aliwauliza swali tu kwamba nani ambaye amewahi kunichangia wakati niko kwenye kampeni aseme hapa, tafsiri yake ni nini? Alikuwa anaweka gape, anatengana na wafanyabiashara na sasa hivi ndio maana baada ya muda mchache alitangaza wafanyabiashara wengi ni watu ambao wanaihujumu Serikali, ni wezi na ikaonesha kabisa kwamba Taifa hili linaonesha kabisa kwamba wafanyabiashara wote katika nchi hii ni watu ambao hawaaminiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Taifa lolote duniani kama halitawathamini wafanyabiashara na kukaa na wafanyabiashara na kubadilishana na wafanyabiashara mawazo ni namna gani Taifa lao liende, Taifa hilo haliwezi kupiga hatua hata siku moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilichokuwa nataka kukizungumza hapa nilikuwa nataka kusema kwamba ni lazima sasa Mheshimiwa Rais, lakini pia Mheshimiwa Waziri wa Fedha aweze kurudi kukaa na wafanyabiashara, hakuna Taifa lolote linaweza likaendelea kwa sababu ya kutangaza kwamba yeye anapenda maskini, hakuna maskini anayependa kuwa na njaa, si siku nyingi maskini huyo akiwa na njaa akikosa dawa atamgeuka Mheshimiwa Rais kwa sababu hawezi kukubali kuendelea na mateso wakati anajua ana haki ya kupata maisha bora katika nchi yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, imekuwa ni mara nyingi sana wadau mbalimbali wanajaribu kutoa ushauri. Ninakumbuka sana Bandari ya Dar es Salaam tumezungumza mimi ni mjumbe wa Kamati ya PIC, tumezungumza sana tukiwa na Katibu wa Uchukuzi tukamweleza athari ambazo zimetokea kwenye Bandari ya Dar es Salaam, wateja ambao walikuwa wakitumia Bandari ya Dar es Salaam wakubwa ilikuwa ni Kongo pamoja na Wazambia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kama Mbunge wa Jimbo la Tunduma niko pale Tunduma, kwa takwimu za mwaka 2014/2015 kwenye nchi hii asilimia 71 ya mizigo inayoshuka kwenye Bandari ya Dar es Salaam inapita kwenye mpaka wa Tunduma, lakini leo hii ukienda kuangalia tulikuwa na foleni ya malori karibuni kilometa nane ili kuvuka mpaka lakini leo huwezi kukuta gari hata moja liko barabarani limepanga foleni wanasema hali ni nzuri wakati hali bado ni mbaya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wana Tunduma tumeathirika lakini pia Taifa tunaliona linaathirika kupita kiasi sasa wadau mbalimbali wanajaribu kutoa ushauri nakumbuka Mheshimiwa Sugu hapa alisema ndani ya Bunge hili akasema mtindo huu ambao Serikali imeanza kufanya kazi ya kuikusanyia Serikali ya Kongo kodi ni jambo ambalo linasababisha wateja wengi wa bandari yetu wakimbie waende Beira, waende Mombasa lakini pia wengine wameenda hadi Durban wanapitia kule japokuwa ni mbali lakini wameona afadhaili wapitie kule, hatukuweza kusikiliza tukaendelea kukomaza shingo zetu mpaka bandari inataka kukatika hapa sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ndugu zangu, ninakumbuka sana wafanyabiashara pamoja na wadau wa bandari tuchukulie watu wa TATOA. Watu wa TATOA wamejaribu kuishauri Serikali mara nyingi, wameishauri Kamati ya Viwanda na Biashara, wakawaeleza wakasema tatizo kubwa la upungufu wa mizigo hapa ni tatizo la Serikali kutokusikiliza ushauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo kubwa ambalo walizungumza walijaribu kutoa mfano wa kampuni moja tu ya Impala ambayo ilikuwa ikipitisha kwa mwezi mzima tani laki tano kwenye bandari ya Dar es Salaam. Wakasema magari ambayo yalikuwa yakipakia mzigo na kwenda kupakuwa mzigo Kongo yalikuwa ni zaidi ya 30,000 kwa mwezi na magari haya yalikuwa yakitumia lita 2,500 kutoka Dar es Salaam kwenda Lubumbashi kwenda kuchukua copper na kila lita moja ya mafuta Serikali ilikuwa inachukua shilingi 600 kwa ajili ya kodi, lakini pia wakasema kwamba copper tani moja walikuwa wanalipa dola 600 kwenye Bandari yetu ya Dar es Salaam lakini leo hii hakuna kinachoendelea na juzi kwenye takwimu za Durban imeonesha Kampuni ya Impala imesafirisha tani laki saba kutoka Kongo na Zambia wamekwenda kupita kule kwa sababu ya ukiritimba tuliokuwa nao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naomba sana mambo ya uchumi hayana utani, nchi za wenzetu zilizoendelea tunazoziona zina maendeleo mazuri si kwamba zinacheza na uchumi, uchumi sio jambo la kucheza nalo, leo watu wanasimama, Mheshimiwa Rais anasimama, Waheshimiwa Mawaziri wanasimama wanasema hata ikija meli moja, kauli hizi kwa kweli zinafika mahala zinawakatisha tamaa Watanzania na wanafikiria hawa ni viongozi kweli ambao tumewatanguliza kwa ajili ya kuleta ustawi wa Taifa hili. Ndugu zangu haitawezekana ukipata meli mbili au tano badala ya kupata meli 20 mpaka 30 huwezi kufananisha hata ungepandisha ushuru kiasi gani ni lazima tutakuwa na hasara katika Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndio maana leo tunazungumzia uchumi kushuka kwenye Taifa hili watu wanakomaa hapa wanasema uchumi haujashuka wakati huduma za jamii, fedha katika Halmashauri zetu hazijafika leo watu wanasema uchumi haujashuka katika Taifa hili. Tunataka tuseme ni lazima Serikali ifike ikubaliane na ushauri mbalimbali unaotolewa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine ni kuhusiana na wafanyabiashara katika nchi hii. Wafanyabiashara wengi sasa wamekuwa na wasiwasi wameanza kuhamisha biashara zao wanakwenda Kongo, Zambia, Malawi na maeneo mengine wanahamisha biashara kwa sababu hawana uhakika wa biashara zao katika nchi hii. Kuna wafanyabiashara ambao wamekamatiwa mizigo yao, kuna wafanyabiashara ambao tayari wamefungiwa akaunti zao bila sababu za msingi na bila taarifa za msingi na wanafunguliwa akaunti bila kuambiwa nini kilichoendelea, jambo hili wafanyabiashara wamekuwa na wasiwasi wameona kabisa Serikali hii inaonesha kabisa haiwezi kuwatendea tena haki na wanaamua kuhamisha biashara zao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na nikwambie tu takwimu zilizopo ukienda nchini Zambia kuna Watanzania zaidi ya milioni tatu wameamua kwenda kufanya biashara Zambia, lakini Malawi kuna Watanzania zaidi ya milioni moja na laki tano wanafanya biashara kule Malawi. Serikali imekaa kimya wanalipa kodi kule wananemesha nchi ya Malawi na Zambia kule Serikali imekaa kimya kwa sababu ya masharti magumu ambayo Serikali imeweka. Nataka nitoe mfano mmoja wa masharti ambayo Serikali inatakiwa iyatazame. Mimi niko mpakani mwa Zambia na Tanzania ukilipia mzigo wako eneo la custom pale ZRA - Zambia ukiondoka kwenda kufika Lusaka mzigo ule watu wa ZRA wanakuja kuchunguza risiti zako kama umelipia vizuri na mzigo ndio ule uliolipia, wakikuta mzigo ndio uliolipia wanachokifanya wao ni kukuruhusu ushushe mzigo na uendelee kufanya biashara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Tanzania mtu anatoa mzigo nje akishafikisha kwenye Bandari ya Dar es Salaam analipa ushuru, akishauchukua ule mzigo anafika Kariakoo watu wa TRA walewale wanakwenda kuchukua kodi, anatoka pale anakuja mtu wa Mbeya ananunua mzigo watu wa TRA walewale wanakwenda wanachukua mzigo ule kodi, anatoka pale anapeleka; mtu ananunua Mbeya pale anapeleka Sumbawanga watu wa TRA walewale wanakwenda kuchukua kodi, mzigo unatoka Sumbawanga mtu wa Nkasi anakwenda kununua mzigo mtu wa TRA yule yule anakwenda kufata mzigo Nkasi, ni sheria za wapi za kukusanya kodi katika dunia hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ndiyo vikwazo vikubwa vya wafanyabiashara katika nchi hii, ni lazima tufike mahali nchi yetu tunaipenda na hatuna nchi nyingine ya kukimbilia zaidi ya nchi hii; na sio nchi ya mtu mmoja ni nchi ya Watanzania wote tunahitaji kuipigania na lazima Wabunge tushikamane kwa jambo hili tuzungumze kwa nguvu zetu zote ili kuboresha uchumi wa nchi hii wananchi wetu waweze kupata madawa watoto wetu waweze kusoma na shughuli zingine ziweze kuendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nilikuwa najaribu kujiuliza elimu bure Serikali ya Chama cha Mapinduzi inaonesha ni jinsi gani ilivyofeli kwenye elimu bure. Wakati tunafanya mahesabu imeonesha kabisa kwamba karibuni shilingi bilioni 15.7 zinakwenda kila mwezi kwa ajili ya kulipia gharama za elimu bure kwa watoto 8,340,000; tafsiri yake ni kwamba kila mtoto anapewa shilingi 1,884.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Serikali inasema kwamba kila mtoto wa shule ya msingi anatakiwa kulipiwa shilingi 10,000 tunataka kujua shilingi 8,116 zinakwenda wapi na zitapatikana namna gani (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kama kweli bajeti ni shilingi bilioni 15.7 tafsiri yake ni kwamba ukifanya mahesabu ya haraka haraka kwa watoto 8,342,000 utakuta ilihitajika fedha bilioni 83 kwa mwezi lakini inapelekwa bilioni 15 leo mnatuambia kwamba huduma za watoto mashuleni zinakubalika, kazi hiyo haipo, Serikali imeshindwa na iwaambie wananchi kwamba imeshindwa na mzigo huu wananchi waendelee kuubeba mzigo huu. Ndio maana madarasa sasa hivi hayajengwi, ndio maana ukienda ukiona msongamano wa watoto unazidi kuongezeka kwa sababu Serikali imewadanganya wananchi na kazi haifanyiki hata kidogo katika maeneo yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tulikuwa Bungeni humu, tukaishauri Serikali tukasema kitendo cha kuwaambia watumishi wakusanye ushuru kwenye Halmashauri zetu manpower ya watumishi wetu ni wachache katika Halmashauri zetu, tukasema hili jambo litakuwa ni gumu, leo katika Mji wa Tunduma ambapo kwa kipindi hiki cha mavuno tulikuwa tunakuwa na asilimia 40 mpaka 45 ya makusanyo leo tuna asilimia 18 tu, leo hii tumekaa hapa vyanzo 42 havijakusanywa hata shilingi moja ukimuuliza Mkurugenzi anasema watumishi ni wachache siwezi kuwagawa watumishi katika Halmashauri yangu. Serikali ikafidia fedha hizi ili tuweze kufanya maendeleo katika maeneo yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kulizungumzia ni kuhusiana na kilimo, nilikuwa najaribu kuangalia kwenye Mpango huu naona kabisa kwamba kilimo kinaendelea kushuka…
MWENYEKITI: Ahsante.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Kwanza kabisa napenda kuwapa pole sana wananchi wangu wa Mji wa Tunduma kwa ajali ya moto ambayo imetokea katika soko kuu la Mji wa Tunduma na kuteketeza maduka mengi ambayo wamepoteza mali zao nyingi sana, nawapeni pole sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nianze na suala la utawala bora katika nchi hii. Nchi hii utawala bora kwa kipindi cha Awamu ya Tano inaonesha kabisa utawala bora katika nchi hii sasa umetoweka kabisa. Nasema kwamba utawala bora umetoweka, sasa hivi hali ya watumishi katika nchi hii imekuwa ni tete, kila mtumishi amekaa akisubiri matamko, ana wasiwasi na shughuli ambazo anakwenda kuzifanya, haamini kama kesho ataamka akiendelea kuwa mtumishi wa umma katika nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona hali ilivyo katika nchi hii sasa hivi. Jeshi la Polisi sasa wanakamata watu hovyo hovyo, Jeshi la Polisi wanaagizwa, Jeshi la Polisi wanasema wameshindwa kufanya kazi zao bila maagizo kutoka juu, hili jambo tumeliona hata kwenye uchaguzi uliopita. Katika uchaguzi uliopita wa Serikali za Mitaa, Madiwani na Wabunge tumeona hali ilivyokuwa tete katika uchaguzi huu. Imeonesha kabisa kwamba katika kituo cha uchaguzi hasa siku ya kupiga kura walikuja Polisi wengi ambao walikuwa wana mbwa na silaha nyingi kabisa, kiasi kwamba waliwatisha wapiga kura lakini pia walizuia hata Mawakala ambao walikuwa wanatakiwa kuhakiki uhesabuji wa kura wasiingie katika vituo vya kupigia kura. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema tu kwamba kutokana na jambo hili, hata leo Chama cha Mapinduzi wanajinafasi kwamba wamepata kura nyingi na wameshinda lakini tunataka kusema kwamba asilimia kubwa ya matokeo yaliyojitokeza yanaonesha kabisa yalihujumiwa. Tunasema yalihujumiwa na hili tunalizungumza hapa watu wengi watazomea na wataona ni jambo ambalo kama vile tunatania, lakini tunazungumza ukweli na hili lina mwisho. Itafika mahali Watanzania watachukia na watakataa dhuluma pamoja na uonevu unaojitokeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sana jambo la uchaguzi na jambo la haki za watu wanapokwenda kupiga kura ni lazima lilindwe. Sheria za nchi sasa hivi hazifuatwi na viongozi wengi wanakaa madarakani kwa sababu eti amesimamia vibaya uchaguzi na kuiba kura kuhakikisha kwamba CCM wanashinda uchaguzi. Jambo hili linasumbua sana na watu sasa hivi wameanza kukata tamaa ya kwenda kupiga kura.
Mheshimiwa Mweyekiti, nikupe mfano mmoja; Kata ya Kijichi wapiga kura walikuwa karibuni 16,800 mwaka 2015 kwenye Uchaguzi Mkuu lakini safari hii wapiga kura waliojitokeza ni 5,000 tu. Hii inaashiria kwamba Watanzania wameanza kukata tamaa na wanaona hawana haja ya kwenda kupiga kura kwa sababu hata wakipiga kura, kura zao na matokeo yao yanahujumiwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunataka kusema kwamba ni vizuri pia Serikali hii ikajua kwamba hizi ni haki za watu na watu wanavyokwenda kufanya uchaguzi, waacheni wafanye uchaguzi wamchague kiongozi wanayemtaka atakayeweza kuwaongoza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine imetokea sasa hivi, kila jambo linalozungumzwa na mtu hata kiongozi akisema kwake kuna njaa wanasema umekuwa mchochezi. Ni vizuri Serikali ikajaribu kutoa ufafanuzi, uchochezi maana yake nini? Jambo la kweli ambalo linazungumzwa nalo limeshakuwa uchochezi. Nchi hii watu watashindwa kuzungumza, watakaa kimya na wakikaa kimya tunakoelekea siyo kuzuri hata kidogo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa kwenye kampeni maeneo mbalimbali. Ukizungumzia hali halisi ya chakula katika nchi hii nashangaa baadhi ya viongozi ndani ya Serikali hii wamekwenda kutoa matangazo katika mikoa mbalimbali kwamba mtu yoyote atakayesema kwamba kuna njaa anatakiwa kukamatwa. Haya ni mambo ya ajabu kabisa. Njaa haifichiki hata siku moja, njaa iko wazi.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kukushukuru kwanza kwa kunipa nafasi hii, lakini pia naishukuru sana Kamati kwa maoni yake ambayo wamejaribu kutoa na ushauri mbalimbali walioutoa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba, siku zote nikisimama nikiwa nachangia hasa kuhusiana na mambo ya bajeti au na masuala ya fedha, najaribu kuzungumza sana kuhusiana na siasa kuondoka kwenye masuala ya kiutendaji. Masuala ya kiutendaji yakiingiliwa sana na siasa kama tunavyofanya sasa hivi katika nchi hii, lazima tukubaliane kabisa kwamba hatutaweza kufanya vizuri na tusitegemee kabisa kama Taifa hili litabadilika kama wataalam wetu ambao tumewasomesha kwa gharama kubwa na tumewapa majukumu wanashindwa kutekeleza wajibu wao, wanashindwa kuishauri Serikali kitaalam na sisi tunatoa maagizo kuhakikisha kwamba Serikali inatekeleza wajibu wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa najaribu kuangalia na nimejaribu kupima bajeti yetu ya mwaka 2016/2017 na ushauri mbalimbali ambao umetolewa na Kamati. Ukijaribu kuangalia utaona kabisa kwamba sisi wakati tuko Bungeni humu tunatengeneza bajeti hii, sisi kama Upinzani tulitoa Bajeti Elekezi, ili kidogo vitu ambavyo viko mle viweze kuchukuliwa kama msaada wa kusaidia bajeti hii. Kilichotokea, tulionekana watu wa hovyo, tulibezwa humu ndani na baadaye ilionekana kwamba hata bajeti yetu isingeweza kusomwa na watu hawakuipitia kuangalia nini ambacho kinaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa sana wenzetu ambao walikuwemo humu wanapitisha hii bajeti, leo wanalalamika na wao. Nami nashangaa, hata wewe Mheshimiwa Mapunda! Hata wewe fulani! Nashangaa sana, yaani wanalalamika wakati bajeti walipitisha wenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema tu kwamba uko upungufu mwingi sana ambao tuliukataa na tulishauri humu ndani. Tulianza na suala la VAT, tukajaribu kueleza hali halisi kwamba ndugu zangu mkiweka VAT kwenye masuala ya utalii mtapunguza pato la Taifa kwenye Idara ya Utalii. Tukawaambia ondoeni, angalieni wenzenu Kenya na Mataifa mengine yanafanya hivyo. Watu mkabeza mkasema haiwezekani, tunaweka sisi. Leo hii kila mmoja anashangaa humu ndani utafikiri hakuwemo Bungeni wakati wanapitisha bajeti hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme tu kwamba, sisi Wabunge tumepewa dhamana na wananchi kwa ajili ya kuishauri Serikali na kuisimamia Serikali. Kwa hiyo, wajibu wetu ni lazima tuutekeleze tukiwa ndani ya Bunge hili. Tukiendelea kuendekeza siasa ndani ya Bunge hili ni lazima tufike mahali ambapo tutaendelea kushindwa na kufeli na kila siku tutakuwa tunashtuka humu utafikiri hatukupitisha na kujadili sisi wenyewe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka kusema, tunachotaka kushauri hapa ni kwamba, ni lazima turudi kwenye misingi. Lazima Serikali ikubali kushauriwa na kama Serikali haitakubali kushauriwa, itaendelea kufunga masikio na kuendelea kuona Wabunge wanachozungumza ni hamna! Mheshimiwa Magufuli, kama Rais wetu, ni lazima akubaliane na sisi kwamba, sisi kama Wabunge tuliopewa majukumu haya, ni lazima akubali ushauri wa Wabunge. Sisi ndio tunaoishauri Serikali na kuisimamia Serikali, kwa hiyo, akubali ushauri wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tulizungumza sana kuhusiana na hali halisi ya watumishi kukusanya mapato kwenye Halmashauri zetu. Leo Halmashauri zetu kwenye nchi hii, zote ambazo zilipelekwa kwenye majaribio, ziko chini ya 24% kwenye nchi hii katika makusanyo yake. Ni kwa sababu, watumishi waliokwenda kukusanya yale mapato wameshindwa kufikia malengo kwa sababu, watumishi ni wachache katika Halmashauri yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Serikali tunazungumza hapa tunasema kwamba, makusanyo yanakwenda vizuri. Nataka kusema tu kwamba, fedha ambazo zimekusanywa kwenye Halmashauri zetu ziko chini kabisa. Sasa Serikali sijui kama nayo itachukua nafasi ya kuweza kufidia fedha ambazo tumeshindwa kukusanya kwenye Halmashauri zetu. Sielewi kama zitafidiwa fedha hizo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiangalia kwenye Taarifa ya Kamati hapa, ukisoma kwenye ukurasa wa 26 kwenye kipengele cha 2.52 - Matumizi ya Serikali. Ukiangalia, utaona kabisa katika quarter ya kwanza katika Halmashauri, fedha kwenye Halmashauri zetu haikupelekwa hata shilingi kwenye upande wa utawala. Kwa hiyo, fedha ambazo zinatumika sasa hivi kwa ajili ya kuendeshea shughuli za utawala kwenye Halmashauri zetu, zinatumika fedha za vyanzo vya ndani, kitu ambacho kinarudisha utendaji kazi wa Halmashauri zetu. Nasi kama Halmashauri, tunashindwa kutekeleza majukumu ya wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninachotaka kusema ni kwamba, ni lazima tukubaliane tukiwa tunatengeneza bajeti hii tujue kwamba ni bajeti ya Serikali, siyo bajeti ya vyama vya siasa. Kwa hiyo, lazima tunapoingia kwenye bajeti hizi, tukae tukubaliane, tusikilizane, tupokee ushauri wa kila mmoja wetu ili kujenga nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa najaribu kuangalia shughuli mbalimbali ambazo zimefanyika na mambo ambayo yameshindwa kufanyika katika bajeti hii. Ukijaribu kuangalia katika hali halisi, Serikali yoyote duniani ina wajibu wa kuwajengea wafanyabiashara wadogo wadogo na wafanyabisahara wakubwa mazingira ya kufanya biashara ili wafanyabiashara wakubwa waweze kupata mitaji mikubwa ili waweze kulipa kodi ya nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yoyote makini inaendesha Serikali yake kwa kutumia kodi. Leo hii Watanzania wengi katika nchi hii wameshindwa kufanya biashara kwa sababu ya masharti magumu ambayo Serikali imeyaweka. Pia, Serikali hii haichukui hata jukumu la kuwaelimisha walipakodi wa nchi hii, ni nini ambacho kinalipwa katika Serikali hii. Wananchi hawaelewi; Watanzania hawajui! Watanzania wanajiuliza, kinacholipwa ni mtaji? Ni faida au ni kitu gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Watanzania sasa hivi wanaviziwa, wanapangiwa fedha ambayo haiwezekani, wengine wanafunga maduka, wengine wanaacha biashara zao, wanahamisha biashara zao, Serikali haichukui jukumu la kuwafundisha na kuwaeleza wananchi nini ambacho kinatakiwa kilipwe kama kodi ya Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wajibu wa Serikali ni kuhakikisha kwamba inawaelimisha wananchi nini ambacho kinalipwa ili wananchi walipe kodi na Serikali iweze kupata fedha, lakini Serikali haina muda huo. Ni lazima tukubaliane, kama wananchi wataendelea kuwa maskini, biashara zao zitaendelea kufungwa na Serikali hii. Maduka sasa hivi tunahesabu. Ukienda Dar es Salaam wanakwambia maduka 300 yamefungwa; ukienda Mwanza wanasema maduka 200 yamefungwa; ukienda Mbeya wanasema maduka 300 yamefungwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inasema inatekeleza wajibu wake wakati watu wanaendelea kufunga maduka na uchumi unazidi kushuka katika nchi hii. Kwa hiyo, ninachotaka kusema, ni lazima Serikali ijikite kabisa kuwaelimisha wananchi na kuweka ustawi wa biashara zao ili wafanyabiashara wafanye biashara, mitaji ikue na waweze kuwa walipa kodi katika Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo lingine la mikopo. Wanafunzi wamepewa mikopo mwaka 2016, lakini kitu cha kushangaza, sasa hivi ukienda mashuleni, ukienda UDOM hapa sasa hivi kuna wanafunzi ambao wameambiwa hawana sifa tena za kukopeshwa. Tunataka Serikali itupe ufafanuzi; kama mtoto alipata mkopo awamu ya kwanza, leo hii wanasema kwamba hana sifa ya kupata mkopo, tafsiri yake ni nini? Serikali haina fedha? Au nini kilichotokea?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wananchi sasa hivi hawaelewi kinachoendelea. Watoto wao wanapata shida, hawaelewi nini kitakachotokea hapo mbele ya safari. Kwa hiyo, tunataka tupate majibu; kama Serikali haina fedha, iseme kwa wananchi kwamba Serikali haina fedha ili wazazi wa wototo hawa waangalie ni namna gani watahangaika na watoto wao kuliko kuanza kuwahangaisha watoto ambao wameshalipiwa mkopo kwa Awamu ya Kwanza na leo hii wanaambiwa kwamba hizo fedha hazipo na watoto hawana sifa za kuweza kupewa tena mikopo. Ni jambo la kushangaza sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni suala la kilimo. Wakati tunapitisha bajeti hapa, tulishangaa sana. Huko nyuma tulikuwa tunasema wakulima wanapata pembejeo kidogo, Serikali iongeze bajeti, lakini mwaka 2016 hapa wakati tunatengeneza bajeti, tulishangaa Serikali inaondoa shilingi bilioni 47 kwenye ruzuku ya Serikali kwa ajili ya wakulima, tukashangaa. Serikali hii inajinafasi kwamba inataka kuwa ni Serikali ya viwanda, huku inaondoa shilingi bilioni 47 kwenye bajeti. Leo hii mnashangaa kwa nini kuna 0.5 ambayo imeshuka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnashangaa kitu gani wakati mliondoa…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante sana.
Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii. Nichukue fursa hii kwanza kuwashukuru sana watumishi wa Wizara hii nikianza na Katibu Mkuu wa Wizara pia madaktari pamoja na wauguzi wote nchi nzima kwa kazi kubwa wanayoifanya katika mazingira magumu ambayo wanayo. Ninawapongeza sana kwa moyo wao na kwa kazi kubwa wanayoifanya na uzalendo wanaouchukua. (Makofi)


Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze moja kwa moja kuhusu suala la wazee; nimesikitika sana kuona kwamba suala la wazee katika nchi hii inaonyesha kabisa ni suala ambalo siyo kipaumbele cha Taifa hili, ukijaribu kuangalia hata kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri kuna mistari karibu mitano tu inayozungumzia suala la wazee na halieleweki ni namna gani Serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha kwamba inatatua tatizo la wazee kukosa huduma muhimu kama za afya na huduma zingine zinazohitajika kwa wazee hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la wazee ni suala muhimu sana. Humu ndani ya Bunge kuna wazee ambao sasa hivi siyo muda mrefu na wao watastaafu na watakwenda kuungana na wazee walioko mitaani. Pia na sisi vijana tunajua kabisa kwamba siyo muda mrefu tutakuwa wazee na baadae tutakwenda kuungana na wazee wengine walioko mitaani huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Taifa lolote ambalo halitawathamini wazee Taifa hilo ni lazima litakuwa na mapungufu makubwa na haliwezi kupata baraka za Mwenyezi Mungu. Ni lazima wazee hawa tuhakikishe kwamba tunawaheshimu na tunawatengenezea mazingira mazuri, ninaamini kabisa wazee hawa wamelitumikia Taifa hili kwa nguvu zao zote, kwa jasho na damu na mpaka sasa hivi wameishiwa nguvu zao wanahitaji msaada wa Serikali, lakini Serikali haijaweza kuonesha mpango thabiti kabisa wa namna gani wanaweza kuwahudumia wazee hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kuangalia kwenye takwimu za wazee, Serikali imetambua wazee karibuni 346,889, wazee hawa ni kati ya wazee asilimia 60 waliotambuliwa, lakini wazee waliopata vitambulisho, wanaopata matibabu na huduma zingine ni wazee 74,590 tu na wazee 272,299 bado hawajatambuliwa na hawapati huduma zozote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekaa inasema kwamba inataka kuwahudumia wazee, hatuhitaji huduma za kwenye makaratasi, tunahitaji huduma ambazo wazee watakwenda kuzipata na wazee hawa waweze kupata vibali haraka iwezekanavyo ili waweze kupata huduma na waweze kunufaika na Taifa ambalo wamelipigania kwa muda mrefu.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni kuhusiana na vifo vya mama na mtoto. Suala hili katika Taifa hili limeonekana ni jambo la kawaida tu. Tunakuja humu katika Bunge tunazungumza, bajeti zinatengwa na bajeti zinazotengwa ni kidogo sana, lakini fedha hizi haziendi kwa wakati na fedha hazipatikani kabisa. Akina mama wanaendelea kupoteza maisha, watoto wanaendelea kupoteza maisha, Taifa limetulia wanaona kama ni jambo la kawaida wanazungumza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii Taifa hili takwimu zinaonyesha kati ya vizazi 100,000 vifo ni 556 na hivi vifo ni kati ya akina mama wanaokwenda kwenye vituo vya afya na hospitali asilimia 64, asilimia 36 ambao hawajagusa kabisa katika vituo vya afya na hospitali hawa hawatambuliki kabisa ni wangapi wanaopoteza maisha. Kwa hiyo, tuna janga kubwa katika suala hili, tunaona Serikali haijaweka mkazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati Waziri anakuja kujaribu kutoa ufafanuzi wa mwisho atueleze Serikali ina mkakati gani, hatuoni vipaumbele muhimu ambavyo Seriakli inavichukua. Leo tunanunua ndege lakini watu wanapoteza maisha, Serikali haiangalii namna gani inaweza kuwahudumia wananchi hawa, Serikali inawakumbuka Watanzania hawa wakati wa uchaguzi, lakini baada ya kupata madaraka inawasahau na wananchi wanaendelea kufa, hakuna mkakati wowote ambao unaonekana kwamba ni wa kuwaokoa watoto pamoja na akina mama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nataka kujua, kwa nini Serikali hii haitaki kuona kwamba ni muhimu hospitali zetu zote za mikoa zikapata CT Scan, nataka hospitali zote za mikoa ziweze kupatiwa CT Scan.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna MRI, hospitali zetu zote za Mikoa zinatakiwa kupata MRI pamoja na CT Scan, kinachoonekana sasa hivi ni kwamba huduma hizi zinapatikana baadhi ya maeneo tu na zimekuwa na gharama kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, leo mgonjwa anakwenda kupima mgongo, anakwenda kupima kichwa kwenye MRI atatumia zaidi yashilingi 700,000 na kwenye CT Scan anatumia zaidi ya shilingi 200,000 mpaka 150,000 gharama ni kubwa, Serikali haijaonesha thabiti kuweka ruzuku katika matibabu haya, inaonyesha kabisa kwamba Serikali inafanya biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Serikali itueleze ni namna gani inaweza ikahakikisha kwamba inapunguza gharama ya vipimo hivi ili Watanzania waweze kupata vipimo vizuri na waweze kutibiwa sawa sawa. Kwa hiyo, jambo hili tunataka wahakikishe kwamba linafanyika haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiri, pia kuna suala la kuhakikisha kwamba hospitali zote za Wilaya na hospitali zote za kanda ambazo zingeweza kujengwa katika nchi hii, ukichukua gharama za ndege moja ya Bombadier inaweza ikajenga hospitali ambazo zina hadhi ya Ocean Road karibu kanda zote katika nchi hii, leo hiki siyo kipaumbele cha Serikali, wananchi wanakufa kwa cancer, wananchi wanakufa kwa magonjwa haya na tumesikia takwimu hapa inaonesha kwamba miaka inayokuja kati ya miaka 2020 kutakuwa na vifo vingi sana vya watu ambao wanaweza wakapoteza maisha kwa ajili ya cancer.

Serikali ijaribu kuangalia ni namna gani wanaweza wakapunguza matumizi kwenye maeneo ambayo hayastahili na wakapeleka kuokoa maisha na roho za Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunajaribu kuendelea kushauri kuhakikisha kwamba mambo haya yanafanyika haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuokoa vifo vya akina mama na watoto, tumeangalia ni namna gani Serikali ilivyojipanga. Hiki ambacho kimeoneshwa hapa kwamba kinaweza kikasababisha upungufu wa vifo vya akina mama na watoto, tumeona siyo sababu sahihi. Sababu sahihi zilizopo ziko takwimu mbalimbali ambazo zinaonesha, ukiangalia katika nchi hii, hospitali za Wilaya zilihitajika 139, leo kuna hospitali 119, kuna upungufu wa hospitali 20 katika Wilaya zetu nchi nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia vituo vya afya vilihitajika 4,420 leo kuna vituo 507, kuna upungufu wa vituo 3,913. Kwa hiyo, vituo karibuni 3,913 havipo mpaka sasa hivi katika nchi hii. Ukiangalia zahanati zilizokuwa zinahitajika ni 13,545 leo kuna zahanati 4,470, kuna upungufu wa zahanati 8,075.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kupunguza vifo vya mama na mtoto kama hatutasogeza huduma hizi kwa wananchi katika vijiji vyote nchi nzima na Wilaya zote tuweze kujenga hospitali za Wilaya ziweze kukamilika. Hivyo, tunafikiri ni vizuri Serikali ikajaribu kuangalia vipaumbele hivi muhimu kwa ajili ya kupunguza vifo vya akina mama na watoto katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo tunajiuliza sana kama Watanzania, sijui kama Tanzania imekuwa ni nchi ya majaribio ya dawa za malaria. Kila zikifika ndani ya mwaka mmoja tunapata matangazo kwamba dawa hii haifai kwa matumizi ya binadamu inatakiwa iachwe na inaletwa dawa nyingine. Sasa tunataka wakati Mheshimiwa Waziri anakuja kuzungumza hapa atueleze ni kwanini Tanzania imekuwa kama ni nchi ya majaribio ya dawa ya malaria, atueleze wakati wanatangaza kwamba dawa hii haihitajiki na haifai kwa matumizi ya binadamu ni Watanzania wangapi wanakuwa wameathirika na nini ambacho kinaendelea ili kuokoa athari ambazo zimewapata Watanzania hawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na dawa moja ambayo ilikuwa inatumika hapo nyuma, dawa ya chloroquine, dawa hii imefanya kazi kwa kipindi kirefu sana, ilikuwa inaokoa sana vifo vya akina mama kwa sababu pia walikuwa wanatoa kama chanjo kuhakikisha kwamba akina mama hawapati malaria kama kinga, leo dawa ile imefutika na hatuelewi ni utafiti gani ambao ulifanyika, Watanzania wanataka kujua utafiti uliosababisha dawa ya chloroquine ikaonekana kwamba haifai. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna jambo lingine la upungufu wa madaktari katika nchi hii. Imeonesha kwamba katika nchi hii kuna upungufu mkubwa sana wa madaktari, nataka kukuhakikishia kwamba nchi hii imesomesha madaktari wengi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda katika nchi za Kusini na Kati mwa Afrika, wanaofanya kazi karibuni asilimia 20 na 30 ni Watanzania wanafanya kazi katika hospitali zile. Ukienda katika nchi za Botswana, Congo, Mozambique na maeneo mengine, wanofanya kazi za kuwatibu wale watu ni Watanzania na hawa Watanzania wanaofanya kazi kule wametumia fedha kubwa kabisa ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuweza kumfundisha daktari mmoja haipungui karibu shilingi milioni 10. Madaktari hawa wametumia resources za nchi, lakini leo wanafanya kazi katika nchi zile, juzi tumesikia Mheshimiwa Rais pamoja na Wizara wameamua kuwachukua madaktari wetu kuwapeleka Kenya, jambo ambalo limekuwa ni jambo la kusikitisha na kushangaza wakati tuna upungufu mkubwa wa madaktari nchini. Ahsante.
Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi kwa kupata fursa hii ya kuweza kuchangia hotuba hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa niseme tu ninaunga mkono maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni. Pia nitumie fursa hii kuwashukuru sana viongozi wangu Mheshimiwa Mbowe pamoja na viongozi wote wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa jinsi ambavyo wameendelea kutuongoza vizuri kuhakikisha kwamba tunaishauri Serikali na tunaisimamia Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie fursa hii kuanza kusikitika sana kwa sababu ya tukio la Mkuu wa Wilaya ya Hai kuongoza Mgambo katika Wilaya ya Hai na kwenda kuharibu Mashamba makubwa ambayo yana zaidi ya bilioni kwenye green house ya Mheshimiwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Tuna uhakika kabisa kwamba haya ni masuala ya kisiasa ambayo yamefanyika; na kwa sababu Mheshimiwa Mbowe alikuwa ameamua kuwekeza kwenye kilimo kama mwekezaji mwingine katika nchi hii lakini tumeona hakuna taarifa yeyote wala kemeo lolote la Serikali kwa Mkuu wa Wilaya ambaye amekwenda kuharibu mashamba haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili linasikitisha sana, na leo katika Bunge hili tunazungumza kwamba tunataka utengamano wa kisiasa. Utengamano wa kisiasa hauwezi kuja kwa sababu kuna uonevu, kuna husda ambazo zinaendelea ndani ya nchi hii. Tumesikia baadhi ya viongozi wetu wanaendelea kuwekwa ndani. Jambo hili linaendelea kututengenisha na hatutaweza kuwa pamoja kwa sababu viongozi walioko madarakani wameshindwa kutuweka pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nijaribu kuzungumzia jambo lingine. Ninataka kuzungumza kwamba bajeti hii ya Mheshimiwa Mpango na niseme kwamba Mheshimiwa Mpango ndiye tatizo katika Taifa hili. Mheshimiwa Mpango kama Waziri wa Fedha ndiye anayelirudisha Taifa hili nyuma. Mimi nimeshangaa sana wakati anasoma bajeti yake hapa watu wamempigia makofi na anasoma kwa mbwembwe kali, lakini ukiangalia utekelezaji wa bajeti yake ya mwaka 2016/2017 unaona ametekeleza kwa asilimia 38. Kama nchi hii kungekuwa kuna uwajibikaji, Mheshimiwa Mpango angeshakuwa a meshaachia madaraka kwa muda mrefu asingeonekana katika Bunge hili la bajeti ambalo linaendelea. Hata Mawaziri wengine walioweza kuwasilisha bajeti zao wasingeweza kuonekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukijaribu kuangalia Serikali hii inasema kwamba inataka kupunguza umaskini wa Watanzania. Umaskini wa Watanzania hauwezi kupungua kwa sababu ya kununua Bombadier, umaskini wa Watanzania utapungua kwa sababu ya kuwahudumia Watanzania wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka kutoa mfano; asilimia 75 ya Watanzania ni wakulima katika nchi hii na asilimia 80 ni masikini; na kati ya asilimia 80 maskini hawa wanapatikana katika asilimia 75 ya Watanzania ambao ni wakulima, wavuvi na wafugaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo katika bajeti ya mwaka 2016/2017 katika Serikali ya Chama cha Mapinduzi tuliwaambia bajeti hii hamtaiweza kuitekeleza mkasema mtaitekeleza, hebu angalia, kwenye kilimo tulikuwa tumetenga shilingi bilioni 101 lakini utekelezaji na fedha zilizokwenda kuinua kilimo ili kuhakikisha kwamba viwanda vinakua katika nchi hii na umasikini unaondoka kwa Watanzania asilimia 75 imepelekwa shilingi bilioni tatu tu kati ya shilingi bilioni 101. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tuliamua kwamba tuendeleze pia kilimo cha umwagiliaji. Huwezi kuamini katika kilimo cha umwagiliaji tulikuwa tumetenga shilingi bilioni 35 kati ya shilingi bilioni 35 fedha iliyokwenda kwenye shughuli za maendeleo ni shilingi bilioni 1.2 ambayo ni sawa ya asilimia nane ya fedha ambazo zilikuwa zimetengwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili linaendelea kuonesha ni jinsi gani ambavyo Serikali ya Chama cha Mapinduzi haijajiandaa katika kuondoa umaskini wa Watanzania. Na ninataka kusema Watanzania hawataweza kuondolewa umasikini wao kwa sababu ya Bombadier wala hawataweza kuondolewa umaskini wao kwa sabau ya standard gauge. Ni lazima tuwekeze kwa wafugaji, kwa wakulima na kwa wavuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa Wabunge wa Chama cha Mapinduzi ndani ya Bunge hili wanafika mahali wanashangilia wanasema bajeti ya mwaka, bajeti ya msimu, bajeti haijawahi kutokea, wananchi wenu maskini, wakulima wako vijijini hawajapelekewa fedha kule mnasema bajeti ya mwaka ambayo haijawahi kutokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwakumbushe ndugu zangu Wabunge wa Chama cha Mapinduzi, mwaka 2015/2016 wakati wa uongozi wa Mheshimiwa Kikwete alitenga shilingi bilioni 88 kwa ajili ya wakulima, hizo ni pembejeo peke yake leo mnatenga shilingi bilioni 10 mnasema hii ni bajeti ya mwaka haijawahi kutokea, haya ni mambo ya ajabu sana, mnaongoza watu gani? Sisi tunakaa mjini kwa wafanya biashara, pale Tunduma ni mjini lakini tunaendelea kuwatetea wakulima ili kuhakikisha kwamba maisha ya wakulima yanainuka na yanapanda juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mnasema kwamba mnataka kuanzisha viwanda. Kwenye viwanda peke yake ilikuwa imetengwa shilingi bilioni 42 lakini kati ya shilingi bilioni 42 fedha ambayo imekwenda kwenye viwanda ambayo Mwijage ameipokea ni shilingi bilioni 7.6 peke yake. Leo mnasema Serikali imejipanga kuhakikisha kwamba nchi inakuwa ni ya viwanda, huu ni ubabaishaji na ni utani kwa Watanzania. Nchi hii hamjajipanga kuanzisha viwanda na hamko tayari kuanzisha viwanda. Msifikiri viwanda vinakuja kwa maneno, msifikiri viwanda vinakuja kwa maigizo yanayofanyika ndani ya Bunge hili. Viwanda vitakuja kwa vitendo, kwa kutenga fedha na kuhakikisha kwamba fedha zinakwenda kwenye matumizi na zinakwenda kufanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka kusema kwamba ni lazima tubadilishe mtazamio wetu. Tumefika humu ndani kila wakati ndiyoo, ndiyoo, ndiyoo! Hamjasema ni namna gani mtabadilisha maisha ya Watanzania. Tunataka maisha ya Watanzania yaweze kubadilika kwa vitendo, mnafanya usanii ndani ya nchi wakati mmepewa madaraka makubwa ya kuongoza nchi hii. Kwa nini mfanye usanii na maisha ya Watanzania? Haiwezekani! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti iliyotekelezwa mwaka 2016/2017 mmetekeleza asilimia 38, leo hii mmetenga bajeti shilingi trilioni 31 wakati shilingi trilioni 29 mmeshindwa kutekeleza, haya ni maajabu makubwa ambayo yanaonekana katika nchi hii. Tunataka mabadiliko katika Taifa hili, na mabadiliko haya kama mtaendelea kucheka namna hii Watanzania mliowaona miaka iliyopita ya 2000 si Watanzania wa sasa hivi na ndiyo maana mnaona kura zenu zinazidi kushuka kwa sababu ya kutowatekelezea yale wanayohitaji Watanzania, na lazima mtang’oka tu. Endeeni kupiga ngonjera humu, endeleeni kushangiliana, endeleeni kusema kwamba ndiyo mzee, tutawakuta humu mnaendelea kusua sua, tutawang’oa katika viti vyenu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine nililoshangaa, Mheshimiwa Mpango eti kuanzisha vyanzo vipya amekwenda kuwaorodhesha Wamachinga, wauza ndizi, wauza mbogamboga eti wajiorodheshe wakishajiorodhesha, wakitambulika waanze kulipa kodi, hii nchi iko namna gani? Haijaweka mipango thabiti ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara wadogo ili wawe na mitaji mikubwa na baadae waje wawe wafanyabiashara wakubwa, lini Mmachinga kalipa kodi? Hii itakuwa ni nchi ya kwanza katika dunia hii Mmachinga kumlipisha kodi, itakuwa ni nchi ya kwanza mtu ambaye anauza mbogamboga na matunda kulipishwa kodi katika nchi hii. Ni lazima tufike mahali tufikirie mbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mpango hata Buhigwe kule wananchi wameshatoa imani kwako kwa sababu inaonesha wale wanaotumia vibatari umewawekea pia ushuru, wanalipa kodi katika Taifa hili leo unataka wananchi wa Buhigwe wakuamini kwanza unaweza kuwa Mbunge wa Buhigwe, haitawezekana kabisa. Wewe ndiwe unayeshindwa kumshauri Mheshimiwa Rais, unalirudisha Taifa nyuma na ni lazima tufike mahali tukwambie, tuiambie Serikali kwamba imeshindwa kutekeleza wajibu wako sawa sawa ili kuhakikisha kwamba…

T A A R I F A....

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, siipokei taarifa yake kwa sababu najua anajikosha, sasa hivi ana adhabu ya mwaka mmoja ndani ya Chama cha Mapinduzi, kwa hiyo, anaendelea kuipunguzia punguzia makali, kwa hiyo, siipokei kabisa taarifa yake huyu. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumza tu kwamba liko suala lingine, kuna suala linalozungumzwa sasa katika Bunge hili. Wakati watu wanaendelea kujadili bajeti limekuja jambo la mchanga wa madini kwenye nchi hii. Ni vizuri Serikali ya Chama cha Mapinduzi pia ikakumbuka jinsi Wabunge wetu walivyopiga kelele ndani ya Bunge hili, wakakumbuka ni jinsi gani Wabunge wetu walivyoshauri Bunge hili kwamba ndugu zangu tunaibiwa, lazima tufike mahali tubadilishe mikataba hii, mikataba ni mibovu, ni mikataba ya kifisadi, wakasema hapana ni lazima mikataba hii ipite.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mlishangilia kama mlivyokuwa mnashangilia hapa, leo nashangaa mnatuona sisi ni wachawi katika Bunge hili. Sisi si wachawi, wachawi ni ninyi ambao tayari milipitisha mikataba na Watanzania.

Wachawi ni ninyi kwasababu mlipitisha mikataba hii, tena mikataba ya kifisadi ambayo Watanzania wamepoteza fedha nyingi sana, wameingia hasara…

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo nataka niseme…

T A A R I F A .....

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naona ana matatizo yake binafsi, hiyo lugha, na yeye ndiye Mbumbumbu pale. Mimi niko vizuri na ninajitambua na ndiyo maana niko Bungeni humu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, anasema mikataba haipitishwi humu, tuliishauri Serikali ilete mikataba Wabunge wetu waipitie, wajaribu kuishauri Serikali mikataba iko vizuri au haiko vizuri mkasema hapana, leo nyie wenyewe mnasema mikataba italetwa humu, inaletwa kuja kufanya nini? Inakuja kufanya nini? Mnaleta wakati watu wameshakula imebaki mifupa ndiyo mnatuletea mikataba hapa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachotaka kusema ni kwamba ni lazima tufike mahali tukubaliane, Wabunge wetu walifanya kazi ya ziada kuishauri Serikali, kwamba mikataba hii ni mibovu mkasema mikataba ni mizuri, mkagonga meza, wakasema sheria hizi ni mbovu, mkasema hapana. Zikaletwa hati za dharura hapa mkapitisha sheria tatu hapa kwa haraka haraka, kwa mkupuo siku moja, lakini mnataka kuniambia kwamba eti Chenge ana matatizo, sijui Ngeleja ana matatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukimshitaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali tafsiri yake umeshitaki Serikali ya kipindi kilichopita, ndiyo tafsiri yake. Mwanasheria Mkuu wa Serikali hafanyi kazi kwa jina lake kama Mwanasheria Mkuu wa Serikali, anafanya kazi kwa mujibu wa maagizo ya Mheshimiwa Rais pamoja na viongozi wake walioko juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo kama mtatuambia kwamba hawa watu ambao wanatajwa, Mawaziri, sijui Mwanasheria Mkuu wa Serikali anakwenda kujibu kwa nini alisaini, mimi nina uhakika kabisa hata Mzee Masaju hapa hawezi kusaini mkataba kama Mheshimiwa Rais hajamwambia asaini mkataba, lakini je, akisaini huo mkataba kesho tuje tumwambie Masaju mkataba huu ulikwenda vibaya kwa hiyo tunakufungulia mashitaka? Hapana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Mwanasheria Mkuu atakuwa amefanya makosa haya ni makosa ya Serikali nzima ya Chama cha Mapinduzi kwa kipindi hicho kwahiyo kama ni kuwajibika Serikali nzima ya Chama cha Mapinduzi ndiyo inatakiwa kuwajibika kwa jambo hili ambalo limejitokeza. Kwa maana hiyo waombeni msamaha, msijibaraguze kwamba mnawa… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kupata nafasi hii. Kwanza nitumie fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbilinyi (Mheshimiwa Sugu) kwa kutoka siku ya leo. Namshukuru sana Mungu aliyemwezesha kukaa gerezani kwa muda wote bila kutetereka na sasa ametoka anakuja kutekeleza majukumu yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuchangia hotuba hii na nataka kumaanisha ili ushauri wetu ambao tumekuwa tukiutoa kila wakati katika Bunge Serikali iweze kuufanyia kazi Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namkumbuka sana Mheshimiwa Mbilinyi alijaribu kuzungumzia sana kuhusiana na jambo ambalo lilikuwa linafanywa na Serikali ya kuikusanyia nchi ya Kongo mapato. Baada ya ushauri ule nafikiri Serikali ilikubali na sasa ilishaondoa na sasa hivi naona Wakongo wanatumia Bandari ya Dar es Salaam vizuri na mambo yanakwenda sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema tu kwamba siasa safi ni uchumi. Tusije tukajidanganya hata siku moja tukafikiri siasa za kibabe, siasa za kutenganatengana zinaweza zikasababisha nchi ikawa na uchumi bora. Siasa ni uchumi lakini pia uchumi ni sayansi. Kwa hiyo, sisi ni lazima tujue kabisa kwamba umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu, bila kujua hili tukaendeleza ubabe tunakoelekea siko kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kulizungumza ni kuhusiana na wafanyabiashara wengi Tanzania wanaohama nchi. Liko kundi kubwa sana la wafanyabiashara ambao wanahama katika nchi yetu na wanakwenda kufanya biashara kwenye nchi zingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili jambo liko wazi na Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara wajibu wake mkubwa ni kuhakikisha kwamba ustawi wa wafanyabiashara na biashara zao katika nchi hii ya Tanzania ni kipaumbele kikubwa kabisa. Huwezi kuamini wafanyabiashara wengi sasa hivi, ukienda Malawi wengi wamehamia kule. Ukienda Zambia maeneo yote kuna wafanyabiashara wametoka Tanzania wamehamia Zambia. Pia ukienda Kongo ambako hali kwa kweli ya usalama si nzuri lakini wafanyabiashara wako tayari kuondoka Tanzania waende wakafanye biashara Kongo, kwa sababu ya mazingira mabaya ambayo yapo kwa wafanyabiashara wetu ambao wanajitahidi kuwekeza kwenye nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema tu jambo moja kwamba leo Mtanzania akitoka na mzigo wake Dubai, akifika kwenye Bandari ya Dar es Salaam amekuja na invoice yake ya kiwandani kabisa alikonunua mzigo kinachotokea watu wa TRA wanamwambia kwamba hii wamekukadiria vibaya umetengeneza invoice, anaanza kukadiriwa upya akiwa bandarini Dar es Salaam. Amenunua mzigo wa Dola milioni 10 anaambiwa huu mzigo bwana ni milioni 20, mfanyabiashara anakimbia, anaacha mzigo, mizigo inakaa pale kwa muda mrefu na biashara baadaye zinakufa na huyo mfanyabiashara anapoteza fedha zake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi nakumbuka wakati tunajadili hapa, juzi nilikuwa nasikiliza Radio Clouds wanasema tumeshangaa sana Wabunge wetu, wanasema wakati Mbunge anaomba mwongozo watu walishangilia sana, wakati Mwijage anajibu watu wakashangilia sana lakini wakati Mheshimiwa Spika anatoa ufafanuzi na kutoa maelekezo kwa Serikali watu wakashangilia tena. Sasa wanasema Wabunge wetu hawa tatizo ni nini hapa yaani kipi ambacho walikuwa wakikishangilia, ni ule mwongozo uliotolewa na yale majibu ya Waziri au kilichokuwa kinashangiliwa ni yale maamuzi ambayo Mheshimiwa Spika aliiagiza Serikali? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana tumesikia hapa wakati Mheshimiwa Waziri Mkuu akitoa maelekezo kuhusiana na tatizo la mafuta ambayo yako bandarini. Ametoa maelezo hapa na akasema kwamba anatoa siku tatu. Tunaomba sana uchumi hauhitaji nguvu, unahitaji kukaa na kuzungumza. Hawa wafanyabiashara ambao wamekaa kule na mizigo yao nia yao kubwa ni kuja kuuza na kuhakikisha kwamba wanalipa kodi kwenye Taifa hili lakini kitendo cha kuendelea kutumia nguvu kwa kuwalazimisha haitaweza kutusaidia sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana Serikali ikubali kukaa na wafanyabiashara. Hata mwanzo tuliwaambia kukaa na wafanyabiashara na kuzungumza nao ni jambo kubwa katika nchi hii. Hawa ndiyo watu wanaoweza kulipa kodi na ndiyo ambao wanaweza wakaendesha Taifa hili, lakini bila wafanyabiashara kukubali kufanya biashara katika nchi hii na kuwekewa mazingira mazuri nchi hii haitakusanya kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana Mheshimiwa Waziri wa Fedha amekiri hapa ndani, amesema tatizo kubwa kwa nini mnasema fedha hazijaenda huku, kwa sababu makusanyo yamekuwa madogo, fedha hakuna. Tafsiri yake ni kwamba wafanyabiashara hawalipi kodi kwa sababu biashara zao zimeshadhoofi lakini wengine wamefunga biashara, wengine wamehama na biashara zao, sasa anataka kodi kutoka kwa nani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni jukumu la Serikali kuangalia ni namna gani wanaweza wakatengeneza mazingira mazuri kwa ajili ya wafanyabiashara wetu ili waweze kufanya biashara vizuri. Ukienda Tunduma pale mpakani tumepakana na eneo la Nakonde Zambia. Sasa hivi nyumba ambazo walikuwa wanaishi Wazambia zimeshafumuliwa Watanzania wameingia mikataba wameamua kuhamisha biashara zao na sasa wamefungua maduka makubwa upande wa Zambia kule. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumezungumza sana, nimesema ndani ya Bunge lakini pia nimewashauri Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya hawawezi kusikiliza wanaendelea kukomaa wanasema hapana tunataka tufunge barabara. Wamefunga njia ambazo watu walikuwa wanapita, wafanyabiashara wa Zambia na Kongo wakitoka wamenunua mizigo wanapita katika njia ambazo walikuwa wanazipita siku zote. Wamefunga wameweka mataruma wafanyabiashara wa Kongo na wa Zambia wamesema hatuji tena Tanzania tunakwenda kununua maeneo mengine. Kwa hiyo, walichokifanya wafanyabiashara wameamua kutumia akili zao za haraka haraka na kwenda kuhamia upande wa Zambia na leo Zambia maduka ni mengi. Wafanyabiashara walioko pale sasa hivi ni karibuni wafanyabiashara 3,000 waliohama kutoka Tunduma wanafanya biashara Zambia lakini wanalala Tanzania. Kwa hiyo, tunachokizungumza hapa tunakuwa tunamaanisha katika Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri wa Fedha ni lazima pia afike mahali aangalie kodi kwenye Taifa hili limekuwa ni tatizo. Kila mwaka wanaleta taarifa hapa kwamba wanakwenda kuzifanyia kazi hizi kero za kodi ili wafanyabiashara wetu waweze kwenda vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kuamini, wafanyabiashara wengi sasa hivi wanakadiriwa kodi, mtu anakadiriwa shilingi milioni 300, shilingi milioni 400, mwingine anakadiriwa shilingi bilioni 1, shilingi bilioni 2 bila sababu za msingi na kuelezwa kwa nini anatakiwa kulipa kodi hiyo. Wafanyabiashara sasa hivi wamekuwa kama wakimbizi, Serikali haiwaamini wafanyabiashara wa Tanzania. Serikali inawaona ni wezi wafanyabiashara wa Tanzania na Serikali inawaona wafanyabiashara wa Tanzania ni watu ambao wanakwepa kodi wakati si kweli. Kazi ya Serikali ni kuweka mazingira bora na safi ya kufanyia biashara na siyo kuwayumbisha wafanyabiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema ni lazima tukubaliane ukienda TRA sasa hivi wanakukadiria fedha wanayotaka na ukiwaambia sina fedha wanakwambia nenda halafu baadaye wanakwambia bwana ili tukufanyie vizuri tunaomba utupe labda shilingi milioni 10 au shilingi milioni 5 au shilingi milioni 6 na kwa sababu Serikali imewatia woga wafanyabiashara wanakwenda kutoa rushwa badala ya kuingizia mapato Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi wanatumia msemo mmoja wanasema wewe hujui kama ni Serikali ya Awamu ya Tano ya Magufuli hii, ni hapa kazi tu, hakuna namna yoyote utatoa na usipotoa tunakufilisi. Ndicho wanachowaambia wafanyabiashara, imefika mahala wafanyabiashara wameamua kusema sasa ngoja na sisi tuache. Wengine wanafunga biashara wanaona afadhali waende maeneo mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nirudi kwenye vitabu vya bajeti vya Waziri. Nakumbuka kwenye bajeti ya mwaka 2016/ 2017 fedha iliyokuwa imetengwa kwenye viwanda ilikuwa shilingi bilioni 45 lakini fedha iliyokwenda kwenye viwanda kutekeleza majukumu ya maendeleo ni shilingi bilioni 6.7 ambayo ni sawa na asilimia 8 ya bajeti yote. Hii inaonyesha ni jinsi gani Serikali ya Chama cha Mapinduzi inazungumza ndani ya Bunge lakini haijajiandaa kutengeneza viwanda na kuleta viwanda katika Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona ni jinsi gani ambavyo utekelezaji wa bajeti umeendelea kuwa chini mwaka hadi mwaka na hatujui tatizo ni nini. Leo mnasema viwanda, viwanda haviji kwa maneno, viwanda haviji kama alivyokuja Mwijage na Kitabu kikubwa hapa. Viwanda vinakuja kwa kutenga fedha na fedha hizo kuzipeleka katika maeneo husika ili zikafanye kazi. Kwa hiyo, yote haya ni lazima yaeleweke vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye bajeti ya 2017/2018 walikuwa wamepangilia kukusanya shilingi bilioni 28 kwenye Wizara lakini wamekusanya shilingi bilioni 6.6 peke yake. Hii inaonyesha hata uwezo wa kukusanya mapato kwenye Wizara yenyewe imekuwa ni chini kabisa. Yote haya yanafanyika kwa sababu ya kutokuwa na maandalizi ambayo yako sawasawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana nami kupata nafasi hii ya kuchangia kwenye bajeti hii.

Mheshimiwa Spika, Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kazi yetu kubwa ni kuishauri sana Serikali na kuhakikisha kuwa Serikali inatekeleza yale yote ambayo tunajaribu kuyaona kwa faida ya wananchi wetu. Kumekuwa na tatizo kubwa sana la utekelezaji wa yale tunayoyaamua ndani ya Bunge, mwaka 2016/2017 na mwaka 2017/2018 nilitoa ushauri kwenye Bunge hili na nikawaambia ni vizuri sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha akajaribu kujikita sana kutoa ushauri pia kuhakikisha kwamba utekelezaji wa bajeti zetu zote ambazo tunazipitisha ndani ya Bunge zinatekelezwa kama inavyotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, huwezi kuamini, utekelezaji wa bajeti kwenye nchi hii sasa hivi imekuwa ni kitendawili. Hoja kubwa hapa ya kutengeneza bajeti hizi ni kwa ajili ya kuinua maisha ya Watanzania, lakini pia Serikali hii inasema kwamba inataka kwenda kwenye uchumi wa kati. Kwenda kwenye uchumi wa kati kunahitaji hatua, huwezi kutoka kwenye ufukara ukaenda kwenye uchumi wa kati, ni lazima uchumi wa kati uwe na hatua zake.

Mheshimiwa Spika, leo huwezi kuamini, Watanzania wanazidi kuwa fukara, wanazidi kurudi nyuma, leo tunakazana tu kwamba tunataka kwenda kwenye uchumi wa kati, kwa sababu tunachokifanya sasa hivi kwenye bajeti hizi tunafanya bajeti ya vitu na siyo kwa ajili ya wananchi wetu na hili ni tatizo kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hili unaweza ukaliangalia katika bajeti zetu zote. Ukiangalia maeneo ambayo wananchi wengi maskini tunatakiwa tuwainue maeneo haya hayapelekewi fedha kabisa. Ukiangalia kwenye kilimo, mifugo pamoja na uvuvi, fedha haziendi kabisa. Ukiangalia kwenye kilimo mwaka 2016/2017, fedha iliyokuwa imetengwa ilitengwa bilioni 101 lakini kati ya bilioni 101 fedha iliyokwenda kuinua kilimo ni shilingi bilioni 3.3 peke yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka 2017/2018, ilitengwa bilioni 150 lakini fedha iliyokwenda kuinua kilimo imekwenda kupelekwa shilingi bilioni 27.2 peke yake. Sasa tunavyosema kwamba tunataka kuinua uchumi wa Tanzania ni lazima tuzungumzie kwa wananchi hawa ambao ni wavuvi, wafugaji pamoja na wakulima. Tusipoweza kuinua kilimo, tusipoweza kuwainua wavuvi pamoja na wafugaji, tunakoelekea tunatatwanga maji kwenye kinu, tutabaki hapa na tutaendelea kuishangaa Kenya na nchi zingine zinapiga hatua.

Mheshimiwa Spika, nataka kusema jambo moja, ukiangalia kilimo pamoja na uwekezaji wa bilioni tatu kwa mwaka 2016/2017, lakini mchango wa kilimo kwenye Pato la Taifa ulichangia asilimia 29.2, pamoja na uwekezaji mdogo ambao ulifanyika. Kwa hiyo, kama kweli tutawekeza vizuri kwenye kilimo, hata tungewekeza labda hii fedha bilioni 150 ingetumika yote, inawezekana kilimo kingeweza kuchangia Pato la Taifa hata kwa asilimia 50 au 45. Kwa hiyo tungekuwa tayari tunasonga mbele.

Mheshimiwa Spika, umeona wavuvi, leo wavuvi katika Taifa hili imekuwa ni janga, wanachomewa nyavu, wanaharibikiwa mambo yao, wanakamatwa, ziko sheria kandamizi ambazo zimetungwa na sasa hivi huwezi kuamini, wavuvi sasa katika Taifa hili hawaonekani kama ni watu muhimu katika kuchangia Pato la Taifa.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2016/2017 kwenye uvuvi peke yake, shughuli za maendeleo, tulitenga shilingi bilioni mbili ili fedha ziende kule lakini miaka miwili yote hakuna hata shilingi iliyopelekwa kule. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukienda kwenye mifugo, tulitenga bilioni nne kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunaimarisha mifugo yetu, pia na kuwawezesha wafugaji wetu lakini hakuna hata shilingi iliyopelekwa kwenye maeneo hayo. Leo tunakaa ndani ya Bunge tunasema tunatengeneza bajeti kwa sababu ya wananchi maskini, hao wananchi maskini tunaowasema ni watu gani?

Mheshimiwa Spika, kitendo cha kununua ndege tano kwa wakati mmoja tafsiri yake ni kwamba tunakwenda kuinua uchumi wa watu asilimia tano tu, kwa sababu katika nchi hii watu wenye uwezo wa kupanda ndege ni asilimia tano peke yake. Tunatumia mamilioni ya fedha kupeleka kule tunawaacha Watanzania maskini ambao tulipaswa kuwainua ili waweze kujenga nchi na kuhakikisha kwamba uchumi unaimarika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikitaka kukuonesha hali halisi ilyopo, ukiangalia kwenye nchi yetu kila mwaka wanafunzi wanaohitimu elimu ya juu ni karibuni 800,000 kati ya watu 800,000 wanaopata ajira ambazo ni rasmi wanapata watu 40,000 peke yake. Kwa hiyo, kuna wananchi ambao ni wasomi 760,000 hawapati ajira kabisa na wanategemea ajira hii ambayo siyo ramsi, kilimo, ufugaji pamoja na uvuvi, lakini hakuna fedha inayokwenda kule.

Mheshimiwa Spika, hii tafsiri yake ni kwamba hatujajiandaa kuondoa umaskini wa Watanzania badala yake tunaendekeza maneno ndani ya Bunge hili. Hakuna mtu yeyote, wanayemdanganya, wamepewa madaraka makubwa na wananchi wa Tanzania, nia na madhumuni wakiwa na matumaini kwamba wangeweza kuwafikisha wanapohitaji. Leo Watanzania kila maeneo wanalia, tunataka tuseme, ni lazima wabadilike! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mtu pekee unayeweza kujenga nchi sasa hivi ni wewe kwa sababu Muhimili wako ndiyo unaosimamia Serikali, Mhimili wako ndiyo unaoweza kutoa maagizo na kuhakikisha kwamba Serikali inafanya kazi vizuri, lakini kama na wewe utashindwa kuhakikisha kwamba unasimama kama kiongozi wa Mhimili na kuhakikisha kwamba unakemea bajeti hizi, kama kweli bajeti zinakuja tunatekeleza kwa asilimia 18, tunatekeleza kwa asilimia 20, tunatekeleza kwa asilimia sifuri, tutakuwa hatuwatendei haki Watanzania hawa.

Mheshimiwa Spika, tunaomba tutekeleze wajibu wetu wa kuisimamia Serikali kuhakikisha kwamba Serikali hii inatekeleza wajibu wake kama ambavyo tunapitisha bajeti humu ndani ya Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunazungumzia sana barabara. Ukiangalia mtandao wa barabara katika nchi hii ni karibuni kilometa 86,472, kati ya kilometa hizi mtandao wa barabara ambao sasa hivi uko kwa lami karibuni ni asilimia 9.7 peke yake. Kwa hiyo, hata kwenye barabara pia bado tuko nyuma sana, tafsiri yake ni kwamba tuna safari ndefu ya kujenga uchumi wa nchi kwa sababu hatutakwenda kwenye viwanda kama hata barabara hatuna. Kwa hiyo, ni lazima tuhakikishe kwamba tunaonesha ni namna gani tunaweza tukajenga uchumi huu kwa vitendo na siyo kwa maigizo kama ambavyo yanatokea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hii tunazungumzia pia madini. Tunasema, ooh! Sasa hivi tunataka tujikite kwenye madini, yatachangia Pato la Taifa, madini yanawezaje yakachangia Pato la Taifa kama uwekezaji unakuwa kidogo kiasi hiki! Ukienda kuangalia kwenye madini mwaka jana STAMICO tuliwatengea shilingi bilioni 20.9, fedha ambayo tuliwapelekea STAMICO tuliwapelekea bilioni 2.8 peke yake ambayo ilikuwa ni sawa na asilimia 10 tu ya bajeti.

Mheshimiwa Spika, tunawezaje tukahakikisha kwamba tunapata mapato mengi kwenye madini wakati hatuwekezi. Kwa hiyo, yako mambo mengi ambayo ni lazima pia tusimame tuangalie, kama Taifa ni namna gani tunaweza tukajenga Taifa hili kama inavyotakiwa.

Mheshimiwa Spika, naomba nimalizie la mwisho kabisa ni kampuni ya jotoardhi. Kampuni ya jotoardhi ukisoma kwenye ukurasa wa 24, ukiangalia Mheshimiwa Dkt. Mpango anasema, kati ya shilingi bilioni 409 zilipelekwa kwa ajili ya kuhakikisha kwamba umeme vijijini pamoja na jotoardhi. Hata hivyo, ukiangalia hapa mwaka jana fedha iliyokuwa imetengwa kwa ajili ya joto ardhi ilikuwa bilioni 21, lakini fedha iliyopelekwa ilikuwa ni Sh.53,715,000/= ambayo ilikuwa ni sawasawa na asilimia 0.24 ndiyo iliyokwenda kwenye jotoardhi. Katika taarifa ya Mheshimiwa Waziri anaonesha kwamba fedha nyingi ilipelekewa kitu ambacho hakikufanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tusisubiri miujiza, ni lazima tutekeleze bajeti zetu tunazozipanga ndani ya Bunge zikatekelezwe huko na watu wote wanamlaumu Mheshimiwa Waziri wa Fedha. Tunaomba abadilike na kama ameshindwa, atuachie nafasi ili tuweze kusogeza Taifa hili mbele.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, naikataa hoja.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuchangia taarifa hizi za Kamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita sana kwenye Kamati ya Nishati na Madini lakini nataka nizungumzie sana kuhusiana na sekta ya madini. Kila mmoja wetu anajua kabisa kwamba sekta ya madini ni eneo muhimu sana na rasilimali kubwa sana katika Taifa hili. Tulitegemea kabisa katika Serikali hii Awamu ya Tano tulitegemea labda ingeweza kuchangia fedha nyingi sana katika pato la Taifa. Ukweli tu ni kwamba mchango wa sekta ya madini kwenye pato la Taifa bado uko chini sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo ukijaribu kuangalia katika kipindi cha mwaka 2017/2018 tumeona sekta ya madini imechangia asilimia 4.8 lakini mwaka 2015 sekta ya madini ilichangia karibuni asilimia 5.8. Kwa hiyo, inaonyesha ni jinsi gani ambavyo sekta ya madini sasa hivi inazidi kushuka na haiwezi kusonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna sababu nyingi za msingi zinazosababisha sekta ya madini iendelee kushuka. Tusitegemee miujiza kama sekta ya madini inaweza ikafikisha asilimia 10 kama ambavyo Serikali ya Chama cha Mapinduzi ya Awamu ya Tano inavyosema. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2017/2018, Serikali iliweza kutenga fedha za maendeleo na tukazipitisha ndani ya Bunge hili shilingi bilioni 20 lakini zilizokwenda kufanya kazi kwenye miradi walipeleka Sh.1,183,000,000, tusitegemee miujiza hapo. Mwaka 2018/2019 fedha za maendeleo zilitengwa Sh.19,621,000,000 na fedha ambazo zimekwenda sasa hivi kutekeleza miradi ya maendeleo kwa muda wa miezi sita ni Sh.100,000,000 peke yake, hapa tunategemea nini? Kama tuna dhamira ya kweli ya kuinua sekta ya madini katika Taifa hili miezi sita sekta ya madini imeweza kupata Sh.100,000,000 kati ya Sh.19,621,000,000, hapa tunategemea kitu gani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tusitegemee miujiza katika kuinua sekta ya madini na tusitegemee kabisa kama sekta hii ina uwezo wa kuchangia asilimia 10 ambayo mnazidi kuzungumza ndani ya Bunge hili. Hili jambo haliwezekani kwa sababu mnatenga fedha, tunafanya maigizo ndani ya Bunge halafu hampeleki fedha kwenda kutekeleza miradi hii. Kwa hiyo, tunategemea kwamba tutaendelea kushuka mwaka hadi mwaka kwa sababu hatuoni ni namna gani Serikali imejipanga kuhakikisha kwamba sekta ya madini inakwenda sawasawa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, liko jambo lingine, kuna taasisi inaitwa TEITI ambayo inasimamia uwazi na uwajibikaji katika sekta ya madini. Mwaka 2017/2018 taasisi hii iliweza kufanya ukaguzi wa taasisi mbalimbali kwenye sekta ya madini na baadaye ikatoa majibu. Kati ya taasisi 1,230 walikwenda kukagua taasisi 55 ambazo walikuta kuna upotevu wa fedha karibuni shilingi bilioni 30. Taasisi hii ilishindwa kukagua taasisi zote kwa sababu ilikosa fedha za kutendea kazi katika kipindi chote hicho. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunasema hivi, kama hawawezi kutoa fedha kwenye maeneo muhimu kama eneo hili la TEITI tafsiri yake ni kwamba kuna ufisadi na kitu kinafichwa ndani yake ili tusiweze kutambua. Tunahitaji mashirika haya yote yaweze kukaguliwa katika kipindi kinachohitajika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna jambo lingine, uko mradi wa Tanzanite One pale Mererani. Ule mradi tulipata taarifa kwamba tayari Serikali inataka kubadilisha mkataba, iko kwenye mazungumzo na kampuni ambayo ni wabia na Serikali. Kilichotokea huwezi kuamini sasa ni mwaka wa tatu bado mazungumzo yanaendelea na pia Wizara ya Madini haina taarifa mazungumzo yale yamefikia wapi. Tunasikia tu kwamba Mheshimiwa Kabudi bado anafanya mazungumzo wakati miaka mitatu tunapoteza fedha na kodi. Ni mazungumzo gani ya miaka mitatu hayo? (Makofi)

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Frank Mwakajoka, kuna taarifa, Mheshimiwa Musukuma.

T A A R I F A

MHE. FRANK MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana nimesema siwezi kumjibu muhuni huyo namuacha tu.

WABUNGE FULANI: Aaaaa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka, usimuite Mbunge mwenzio muhuni, futa hilo neno halafu uendelee kuchangia.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nalifuta neno hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nilikuwa nafikiria kwamba Serikali itafanya majadiliano kwa haraka ili kuhakikisha kwamba Mradi huu wa Tanzanite unainufaisha nchi lakini pia wafanyakazi waliokuwa wanafanya kazi katika mradi huu waweze kupata haki zao. Cha kushangaza ni kwamba mradi huu mpaka sasa umesimama sasa ni miaka mitatu, tunasikia tu Kabudi, Kabudi, Kabudi yuko kwenye mikataba, hivi Kabudi ndiyo Serikali? Tunataka kujua mikataba hii itatoa majibu lini na wananchi waweze …

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka, ni Mheshimiwa Profesa Kabudi.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Profesa Kabudi. (Makofi)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, Watanzania wanavyosikiliza tunavyozungumza Profesa Kabudi wanashangaa sana kwa sababu walikuwa na matarajio makubwa kwamba akipewa nafasi hii angeweza kuisaidia nchi sasa tunaona hali ni mbaya zaidi.

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Frank, kuna taarifa nyingine, Mheshimiwa Kakunda.

T A A R I F A

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, akumbuke kwamba kwanza sisi huku tulikataa. Huku si tulisema hapanaaa, ndicho tulichokisema, huko wakasema ndiyo. Pamoja na hayo, Waziri wa Madini hajui majadiliano yanaendaje anayejua ni Kabudi, hivi kweli kuna usalama namna hii? Sisi kwenye Kamati yetu tunakutana na Mheshimiwa Waziri na tukisoma taarifa yake hapa inaeleza kabisa tumemuuliza kwenye kikao anasema hajui wanaendelea na mazungumzo, sasa sisi tunakuwa na wasiwasi. Kama kweli Serikali hii na viongozi ambao mmepewa madaraka mtakuwa hamna uchungu na maisha ya Watanzania na uchumi wa Taifa hili miaka mitatu mazungumzo yanafanyika ya kampuni moja tu na huyo mtu ni mbia, Profesa Kabudi inakuwaje? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tunachotaka kusema ni kwamba lazima mjadala huu uishe mapema na Serikali ianze kupata fedha. Pia tunataka tujue wafanyakazi wa Tanzanite One ambao ni zaidi ya 400 hali zao zikoje na Serikali imejipanga namna gani namna ya kuwalipa wananchi wale kwa sababu wanadai madai yao kwenye mgodi ule. Sasa hivi hawana kazi, familia zinakufa, watoto wanakufa, wameshindwa kupeleka watoto shuleni mnasema mko kwenye majadiliano. Yaani mnajadili fedha kwa taratibu namna hiyo, uchumi mnaweza mkajadili kwa utaratibu namna hiyo? Kama ni hivyo Mheshimiwa Profesa Kabudi atakuwa ameshindwa na amefeli kwenye mjadala huu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna jambo lingine la mapunjo ya wafanyakazi kwenye Mgodi wa Makaa ya Mawe Kiwira ambao jumla yao ni 800 ni miaka mingi imepita hawajalipwa. Mwaka 2015, Serikali imefanya majadiliano na kuhakiki madeni imekuta wanadai karibuni Sh.1,800,000,000, wafanyakazi wale wamefanya kazi miaka mingi lakini Serikali mpaka leo haijawalipa na hakuna mpango wowote wa kuwalipa kwa sababu hata bajeti ya mwaka jana hakukuwa na fedha zozote zilizotengwa kwa ajili ya kuwalipa wafanyakazi hawa. Tunaomba Waziri anavyokuja hapa aeleze ni lini wafanyakazi wa Mgodi wa Kiwira watalipwa fedha zao ili waweze kufuta jasho kwa kazi kubwa waliyoifanya kwa miaka mingi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna jambo lingine la makinikia. Watanzania bado wanajiuliza sana makontena 277 ambayo yalikuwa yamekamatwa kwenye Bandari ya Dar es Salaam na wakasema yale makinikia yatakwenda kuuzwa na wakiyauza inawezekana kila mmoja Tanzania akapata Noah. Watanzania wamesubiri Noah hawajaziona. Mpaka sasa hivi Watanzania wamesubiri Noah hazionekani. Juzi watu wameanza kupunguza wanasema kama Serikali imeshindwa kuwapa Noah basi hata Balimi tatu tatu wataridhika. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, haya majadiliano yote ni Mheshimiwa Profesa Kabudi anaendesha majadiliano ya namna hii. Kwa hiyo, tunaona ni jinsi gani ambavyo Mheshimiwa Profesa Kabudi alivyoshindwa kabisa kuweka vizuri mambo haya na zile kontena sijui kama bado ziko bandarini au zimeshatambaa na maji, hatujui. Tunaomba kujua pia Waziri akifika hapa atueleze haya makontena yako wapi na ni lini tutapata Noah moja moja au Balimi tatu, ijulikane hiyo. Kwa hiyo, hakuna namna ni lazima tujue ni mali ya umma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna fedha walisema wale Mabeberu wanaleta mpaka leo hizo fedha kishika uchumba hakionekani. Jamani hii nchi kweli kila siku tutakuwa tunadanganywa? Ndugu yangu Mheshimiwa Musukuma siku moja alichachamaa kwenye kikao baada ya kuona haoni Noah wala Balimi hazionekani lakini akawa hana namna yoyote. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii. Awali ya yote nitumie fursa hii kwanza kumpongeza sana Mwenyekiti wetu wa Chama cha Demokirasia na Maendeleo (CHADEMA), Mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, lakini pia nimpongeze pia Waziri Kivuli aliyewasilisha taarifa hii vizuri na naomba tu kwamba taarifa hii kwa jinsi ambavyo imeandaliwa vizuri, Mawaziri waichukue itasaidia kujenga Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumzia sana kuhusiana na utawala bora, mambo yote yanayozungumzwa, maendeleo hakuna na mambo mengine, kama Taifa litakuwa halina utengamano, kutakuwa hakuna maendeleo na maendeleo hayatapatikana. Kwa sababu tunachokizungumza hapa sasa hivi, kila mmoja analia, leo tukiangalia bajeti za Mawaziri wote, karibu zote hakuna bajeti ambayo imefikia asilimia 70, karibu bajeti zote ziko asilimia 30, 40, na 47 mwisho. Kwa hiyo, tutazungumza sana hapa, kinachohitajika ni fedha, zikipatikana fedha miradi itakwenda kutekelezwa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo kwa nini miradi hii haiwezi kutekelezwa vizuri na kwa nini fedha haziwezi kupatikana? Sababu ni kwamba tumesahau jambo moja. Katika Taifa hili utawala bora limekuwa ni jambo ambalo ni tatizo kubwa sana na lazima tuliangalie kwa umakini mkubwa sana. Tumefika humu ndani ya Bunge tunafanya siasa, tumefika ndani ya Bunge badala ya kujenga hoja za msingi za kutatua tatizo, ni kwa nini hatupati fedha ni kwa nini hatusongi mbele, tunaendelea kufanya siasa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wananchi waliotutuma, hawajatutuma kuja kufanya siasa za namna hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema, unapozungumzia utawala bora, una mapana yake, ukizungumzia utawala bora tafsri yake ni kwamba unazungumzia mambo mengi sana ambayo yanahusiana na maisha ya kawaida ya wananchi. Hata hivyo, unategemeaje maendeleo, kama wananchi wanabaguana, unategemeaje maendeleo kama kuna baadhi ya kikundi kinaonekana ni bora kuliko watu wengine, hayo maendeleo yatatoka wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashangaa sana, Mheshimiwa Rais sasa hivi anakozunguka kote huko, ameanza kuwanyooshea vidole Waheshimiwa Mawaziri, anasema hamfanyi kazi vizuri, ameongea na Wizara ya Fedha amesema wamekosea, kwa nini wanaendelea kupandisha kodi, anawaambia TRA kwa nini wanafanya hivi, haya yote tumeshayashauri sana, lakini wakatupuuza wakasema sisi hatufai, tunafanya mambo ya hovyo na sisi ni watu ambao hatuwezi kulijenga Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ukweli tu, hata angezunguka huko, anachokizunguimza Mheshimiwa Rais ni kitu kidogo sana, lakini kitu kikubwa ambacho lazima tukiangalie, ni kuhakikisha kwamba Taifa linakuwa pamoja. Kama Taifa halijakuwa pamoja, tusitegemee maendeleo katika Taifa hili, tusitegemee wawekezaji katika Taifa hili, kama hatutakuwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siasa ni jambo kubwa sana, demokrasia ni jambo kubwa katika maisha ya binadamu, demokrasia ni maendeleo, lakini leo demokrasia katika Taifa hili, kila wanachofanya CCM huku na Serikali yao wanafanya kwa ajili ya uchaguzi ujao, ndicho wanachokifanya, hawafanyi kwa sababu ya maendeleo na ahadi walizotoa kwenye Ilani yao ya Uchaguzi. Wanafanya mambo yote kwa sababu ya siasa ya kesho ili waweze kufanya vizuri katika uchaguzi unaokuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wananchi wanazidi kulia na sasa hivi utawashangaa sana Watanzania, kwa nini Watanzania hawasemi, Walimu wamekaa kimya, hawajapandishiwa mishahara muda mrefu, lakini wamekaa kimya wanawatazama tu. Ukienda kwa wakulima, wamekaa kimya, mazao yao hayanunuliki, soko limeshuka wamekaa kimya wanawaangalia tu. Kwa sababu wakizungumza wanawakamata wanawaweka ndani, wameamua kuwanyamazisha na wao wamekaa kimya, wanataka waone wanaelekea wapi. Wafanyabiashara wamekaa kimya, wananyanyaswa wafanyabiashara katika nchi hii, wamekaa kimya, hawazunguzi kabisa. Leo wanasiasa wameamua kutunyamazisha pia tukae kimya, waendeshe nchi hii kwa hivi wanavyotaka wao, lakini nataka niwaambie, tunakutana kwenye bajeti kila mwaka, tunaangalia utekelezaji wao kwenye bajeti, kila siku, kila Wizara tunakuta wametekeleza chini ya asilimia 50, chini ya asilimia 40, wanatekeleza bajeti hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba leo Mawaziri waweke commitment hapa, ndani ya Bunge, mbele ya Rais, wamwambie Mheshimiwa Rais, tunataka tutekeleze bajeti inayokuja kwa asilimia 80. Mbona Halmashauri zetu wamezipa masharti, kwamba kila Halmashauri ihakikishe kwamba inatekeleza kwa asilimia 80, lakini kwa nini Mawaziri hawataki kujiwekea malengo hayo ya kutekeleza kwa asilimia 80. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo tunaendelea kuwashangaa, wameendelea kujichanganya, wameanza kuchekana wenyewe. Leo mnasema Serikali ya Awamu ya Tano, ina maana Serikali ya Awamu ya Nne, ilikuwa ni Serikali ya CHADEMA? Haikuwa Serikali ya CCM? Kwa nini wasizungumze mipango yao ya miaka inayokuja, lakini wanaanza kuzomeana wenyewe, wanasema Awamu ya Tano imekuwa nzuri kuliko Awamu ya Nne. Awamu ya Nne imefanya kazi kubwa, hivi nyie Awamu ya Tano wangejenga chuo cha Dodoma hiki hapa, tungelala na kunywa maji kweli! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini hawawezi kuangalia, kwa nini hawawezi kuweka mipango ya muda mrefu. Serikali ni ya kwao, chama ni cha kwao, muda wote wamepewa madaraka ya kuongoza Taifa hili, leo wameanza kuzoemeana, Awamu ya Nne imefanya vibaya, lakini nataka nikwambie…

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwakajoka subiri kuna taarifa.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: We dogo vipi wewe!

T A A R I F A

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpa taarifa rafiki yangu, muda mrefu wa speech yake aliyokuwa anazungumza hapa au maelezo yake, mengi yanazungumzia kukosoa. Nilitegemea angalau katika muda ambao anazungumza angeweka maombi mawili matatu au ushauri katika maombi ya jimboni kwake, angalau maji, barabara, lakini yote anayozungumza ni siasa ambayo haina
faida kwenye jimbo lake na yeye ni mwakilishi ambaye anatoka kwenye jimbo ambalo… (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante. Mheshimiwa Mwakajoka taarifa hiyo. (Kicheko)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu bwana mdogo siwezi kupokea taarifa yake naona ana matatizo huyu bwana mdogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kukwambia, ndiyo maana nimetangulia kusema, leo kila mmoja anazungumza hapa, Waziri wa Fedha alikuja hapa akasema, hakuna fedha. Sasa unaposema kwamba hakuna fedha halafu unataka mimi nianze kusema eti nasifia, nasifia kitu gani wakati hakuna kazi iliyofanyika, hakuna kazi iliyofanyika nasifia kitu gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, jambo kubwa nililolizungumza tunahitaji utawala bora katika Taifa hili. Utawala bora ukiwepo, wawekezaji tunaowataka, wanaweza kuja kuwekeza katika Taifa hili na wakalipa kodi na nchi ikapata fedha.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa Frank subiri.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, linda muda watu wanana…

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumpa taarifa mzungumzaji, anaposema Waziri wa Fedha akisimama anasema hakuna fedha, lakini amesikia, vituo vya afya zaidi ya 352 vimejengwa ndani ya mwaka mmoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari tumeshatoa zaidi ya shilingi trilioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa reli ya kisasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari tumeshatoa bilioni 1.5 kwa hospitali za halmashauri 67. Anatakiwa aseme mambo ambayo yana ukweli ambayo wananchi wanayaona kwa macho yao, kwamba fedha ipo na Serikali inaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo katika majimbo yote likiwemo na jimbo lake yeye mwenyewe. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Frank, taarifa hiyo.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilifikiri kama Waziri wa Fedha, kwa sababu ndiye anayewaambia Mawaziri wengine kwamba hamtatekeleza kwa asilimia mnazozihitaji kwa sababu fedha hakuna amekusanya chini ya kiwango na anayekusanya fedha ni yeye. Cha kushangaza, namshangaa, lakini pia kama mama, tukiangalia takwimu za mwaka jana za vifo vya wanawake na watoto, kati ya vizazi laki moja katika nchi hii, watu wanaopoteza maisha ni vizazi elfu sitini na tano, kwa hiyo, elfu 44 wanakuwa wazima. Sasa huwezi kuniambia kwamba, eti umejenga vituo, unajenga vituo madawa hakuna, unajenga vituo vifaa hakuna, ee, una maana gani! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii ukijaribu kuangalia kwenye shule zetu za msingi, watoto wanakaa zaidi ya 250 kwenye shule za msingi. Hizo ndizo takwimu ambazo tunazo, lakini leo anatuambia kwamba, eti anasema kwamba fedha zinatoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kuzungumza ni kwamba, lazima tutengeneze utawala bora na nawaambia ndugu zangu, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, Mawaziri pamoja na Mheshimiwa Rais, asikie, wananchi wamekaa kimya, hawajakaa kimya eti kwa sababu wameridhika na utawala huu, wamekaa kimya na wanapata taarifa kwamba mnategemea kwenye uchaguzi ujao mtapeleka polisi wengi, mtapeleka majeshi mengi, lakini wamesema hawatagombana na jeshi la polisi, watakwenda sasa kujuana na ndugu zao ambao watasababisha wapigwe. Sawa jamani! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka niwaambie, lazima tuelewane, wanataka kuleta machafuko katika Taifa hili kwa sababu ya uroho wa madaraka. Haiwezekani wamekubali demokrasia, leo wanataka wabaki peke yao, wakati wananchi hawakubaliani na ninyi, wanahitaji upinzani ndani ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nilikuwa namsikia Mheshimiwa Jenista Mhagama, anasema watu ambao wamechangia kuhusiana na Katiba Mpya, anasema ni watu wawili, watatu……

MHE. MAULID S.A. MTULIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Frank taarifa.

T A A R I F A

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namheshimu sana mzungumzaji kaka yangu Mwakajoka, lakini nataka nimpe taarifa, si kweli kwamba wananchi hawaipendi au hawakipendi Chama cha Mapinduzi, ni kwamba wananchi wetu huko tunakotoka wameridhika, wanakipenda Chama cha Mapinduzi na mwaka 2020, hali itakuwa mbaya sana kipande cha kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo ndiyo taarifa yangu.

MWENYEKITI: Taarifa, Mheshimiwa Frank.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza huyo bwana Akwirina anamlilia sana. Kwa sababu ndiye aliyesababisha Mkurugenzi wake akazuia viapo vya…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Frank elekeza hoja yako kwenye kuchangia.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea….

MWENYEKITI: Taarifa nyingine, Mheshimiwa Frank kaa, taarifa ya mwisho hiyo.

T A A R I F A

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimpe Mheshimiwa Frank taarifa kwamba, anayoyasema ni ya kweli, kwamba bila jeshi la polisi CCM haitafika madarakani na uthibitisho upo, Mheshimiwa Frank kwa mfano Kata ya Turwa Tarime, tuliwashinda CCM kwa kura zaidi ya 76 lakini walitupiga mabomu wakachukua wakajitangaza. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa Frank.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napokea na mimi kwenye kata ya Ndarambo kule kwetu Momba, Mkurugenzi alikuja na polisi zaidi ya 100 ndani ya chumba na akanyang’anya matokeo na akaondoka nayo, kwa hiyo, hili lipo. Kama kweli Mtulia anasema kwamba eti CCM inapendwa na wananchi, wekeni mpira chini…

MWENYEKITI: Ahsante, nilikuongeza dakika moja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuchangia. Nataka kuchangia sana kwenye uhuru wa vyombo vya habari; najua kabisa kwamba katika Taifa hili sasa hivi kutoa habari imekuwa ni jambo hatari sana kuliko hata ugaidi.

Mheshimiwa Spika, nizungumze tu ukweli kwamba wako vijana wetu wengi sana ambao wamepata shida kubwa wamepigwa, wamewekwa mahabusu, wameteswa, wamekaa rumande zaidi ya miezi mine na bila kupelekwa Mahakamani na baada ya kupelekwa Mahakamani wameshinda kesi zao zote, lakini bado wana maumivu na vilema wamebaki navyo. Natoa mfano, kwa mfano, kijana mmoja anaitwa Mdude Nyagali ambaye yeye alikuwa anakosa kwenye mitandao, anakosoa utendaji wa Mheshimiwa Rais na kutoa maoni yake, huyu mtu alikamatwa usiku, alipigwa, alisafirishwa kutoka Mbozi mpaka kwenda Dar es Salaam na alikaa Dar es Salaam zaidi ya miezi miwili huku akiwa amepigwa, amevunjwa miguu yake na akiwa hoi kabisa.

Mheshimiwa Spika, pia wako vijana wengi sana ambao wamekamatwa na vijana hawa mpaka sasa hivi wengine hawajapelekwa Mahakamani, lakini mpaka sasa hivi bado wanaendelea kukamatwa. Tunaomba sana wakati Waziri anakuja kuzungumza hapa, aje atuambie ni vijana wangapi ambao wamekamatwa katika Taifa hili kwa sababu ya makosa ya kimtandao wakati wanatoa maoni yao kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wanaijenga nchi hii.

Mheshimiwa Spika, vilevile atueleze kwamba ni vijana wangapi ambao wamefunguliwa mashtaka na wamefungwa gerezani kwa sababu wamepatikana na hatia. Yote hii tunataka kujua ni namna gani nchi yetu ilivyoweza kuzuia uhuru wa vyombo vya habari.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine, ninataka kuzungumzia, yuko Mwandishi wa habari ambaye anaitwa Ansbert Ngurumo ambaye alikuwa anajaribu kuandika habari, kuwapasha habari Watanzania huyu mtu alianza kutishiwa kwamba anatoa habari ambazo zinaweza zikasababisha utulivu na amani ukatoweka katika nchi hii, huyu mtu aka…

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka vitu vingine una uhakikanavyo lakini?

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, nina uhakika. Hii ya Ansbert Ngurumo nina uhakika nayo, hayupo yupo Finland na alitoa…

SPIKA: Huko Finland na sisi, si kaenda mwenyewe!!

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: No, analalamika…

SPIKA: Haya andelea kuchangia

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, anazungumza kwenye vyombo vya habari. Haya tunayotoa ni mawazo, tunatoa ushauri humu ndani ya Bunge, nia na madhumuni ni kuona Serikali inafanya mabadiliko, nia na madhumuni ni kuona Serikali inaacha uhuru wa vyombo vya habari, inaacha Watanzania wanatoa habari na wanatoa maoni yao kwenye Taifa letu. Nchi haijaanza leo, nchi imeanza muda mrefu, hii ni Awamu ya Tano ya Serikali katika Nchi hii ya Tanzania. Serikali zote zilizopita sheria zilikuwepo lakini Serikali ya Awamu ya Tano imetunga Sheria nyingi za makatazo, sheria nyingi ambazo zimesababisha…

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka subiri kidogo. Naamini Waheshimiwa Wabunge mnapotaka kuchangia mnajiandaa. Ukitaka tu kuchangia unasimama tu, Serikali haitungi sheria anayetunga sheria ni ninyi wenyewe. Tunaotunga sheria ni Bunge, ukisema Serikali hii imetunga sheria nyingi, imefanya hivi unakuwa unawasingizia lakini cha muhimu hapa cha kuelewa; uhuru wa kutoa maoni siyo uhuru wa kwamba sisi tukishakuwa Wanasiasa ni kutukanwa na kila mtu, kusingiziwa na kila mtu, yaani ukishakuwa Mwanasiasa basi kosa. Mtu akutukane, akudhalilishe, afanye anachofanya, ukimuuliza nini anasema uhuru wa habari, hapana, hakuna uhuru huo.

Hivi wewe ukitoa maoni yako, ukayatoa tu maoni yako ukapinga jambo, ukafafanua jambo utagombana na nani? Tatizo when they go to the person na ili tuwafundishe vijana wetu wote tuna wafuasi hapa, tuwafundishe namna ya kutoa maoni yao badala ya kutumia kichochoro hicho cha uhuru kutukana watu, kudhalilisha, watu wana familia zao, tuna utamaduni wetu katika nchi, tunaheshimiana. Kitoto kidogo kinatukana mtu kama babu yake au baba yake itakuwa Taifa la aina gani hilo? (Makofi)

Kwa hiyo tunapoilaumu Serikali, mimi sikatai, lakini vilevile tuna jukumu sisi la kuwalea vijana wetu wajue hata kukosoa kwenyewe kuna utaratibu wake, kuna nidhamu yake. Unapotaka kuiambia Serikali iambie katika utaratibu fulani lakini unapomtukana mtu anafunga masikio, hasikilizi. Yaani kuwa kiongozi ndiyo basi utukanwe tu kukicha? Haiendi hivyo.

Ndiyo maana naishia kwa kuwashukuru sana wale wanaoliombea Taifa hili, tumemaliza Pasaka vizuri, nawashukuru sana Watanzania walioliombea Bunge na waendelee kuwaombea viongozi. Ndiyo viongozi tunakosea lakini pia huombewa si lazima uwe unatukana tu kila siku, upige na magoti kidogo tuweze kuiona njia vizuri zaidi kama nchi tusonge mbele. (Makofi)

Waheshimiwa Wabunge, nawaonea huruma sana kwani mnatukanwa sana, mnadhalilishwa sana bila hatia. Mtu hata hajui chochote, hana information yeye mwenyewe lakini uhuru wa habari, huu ni utamaduni wa wapi wa kutukana watu hovyo?

Mheshimiwa Mwakajoka, mimi sipingi hoja yako na dakika nazitunza, nachosema ni kwamba tuna wajibu na sisi wa kuwafundisha hawa vijana waache habari ya kutukana watu. Endelea Mheshimiwa Mwakajoka. (Makofi)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru tu kwa kutoa ufafanuzi, lakini niseme ukweli tu kwamba nachoshangaa ni kwamba mnajitahidi sana kusimamia hali halisi hasa tukizungumza sisi, hebu tuchukulie mfano Gazeti la Jamvi kila siku linatukana Watanzania, Mheshimiwa Waziri yuko hapa, kila siku linatukana viongozi wa Vyama vya Upinzani, kila siku wanazungumzia akina Mheshimiwa Membe na kadhalika yaani kila siku linatukana, hata siku moja hatujaona hatua yoyote inachukuliwa. Sasa yote haya tunavyosema kwamba tunataka tuone nchi yetu inakuwa na utulivu na inafuata misingi hasa ni misingi gani watu wengine wanatukanwa tuko kimya na kila siku tunazungumza humu ndani ya Bunge. (Makofi)

SPIKA: Yaani hilo tunakemea kwa pamoja, mimi na wewe tuko pamoja.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, tunazungumza ndani ya Bunge, Mheshimiwa Waziri yuko pale lakini hakuna hata siku moja kwamba hili Gazeti limefungiwa au limechukuliwa hatua yoyote kwa sababu tu hili gazeti inasemekana kwamba watu wanaolihudumia ni Serikali yenyewe, sasa hatuwezi kufika huko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jana Mheshimiwa Profesa Shivji amezungumza kwenye mtandao, akasema wakati wa Serikali ya Awamu ya Kwanza tulipewa uhuru wa kutoa mawazo na uhuru wa kusema na wakati tunasema Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Kwanza alivyosikia aliwatuma watu wake waje watusikilize, walitusikiliza, tukawaeleza na wakatuelewa vizuri. Leo Tanzania mtu akitoa mawazo na maoni yake amekuwa ni adui, hilo jambo halitawezekana. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka Profesa Shivji amezuiliwa na nani kuongea?

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, no, amesema hivyo lakini hata ukisikiliza jana na hotuba…

SPIKA: Kama anasema hivyo anazeeka vibaya Profesa. Endelea Mheshimiwa Mwakajoka. (Kicheko)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ukisikiliza Maaskofu wote waliohubiri siku ya Pasaka wamezungumzia jambo hili kwamba Tanzania uhuru wa habari kwa kweli imekuwa ni tatizo, ni lazima Serikali ikubali kupokea mawazo na maoni, iache uhuru wa vyombo vya habari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo tuko ndani ya Bunge pamoja na kwamba mlipiga kura nyingi humu mkasema Bunge lisiwe live lakini ukweli tu ni kwamba Watanzania wanahitaji sana kuona Wabunge wao wanasema nini lakini jambo hili limefungwa. Mambo mengi ambayo tunayazungumza ndani ya Bunge ambayo ni maslahi ya wananchi yamefungwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, juzi tumepata taarifa kwenye mitandao na vyombo vya habari, IMF wamesema kwamba wanatakiwa waruhusiwe tu na Tanzania watoe habari ya jinsi gani uchumi wa nchi yetu unakwenda lakini mpaka sasa hivi kimya. Tunaomba pia Mheshimiwa Waziri aseme hii ni kwa sababu ya kutokuwa na uhuru wa vyombo vya habari. Vyombo vya habari vinaogopa kuandika kwa sababu wanasoma kwenye mitandao lakini wanasema wakiandika na kama hawajaruhusiwa inakuwaje. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka, una uhakika IMF imeomba itoe habari?

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ndiyo.

SPIKA: IMF ndio imeomba?

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, wameomba Serikali ya Tanzania iwaruhusu ili wachapishe ile hali ya uchumi wa nchi yetu kwa jinsi ambavyo wameiangalia. Wamezuiliwa, wameambiwa wasitoe. Sasa kama mmezuia na taarifa hiyo na walipa kodi wanataka kujua kuhusu kinachoendelea.

SPIKA: Yaani Tanzania ina uwezo wa kuwazuia IMF wasichapishe chapisho lao?

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ni sheria lazima nchi husika iruhusu, sasa Tanzania haijaruhusu…

KUHUSU UTARATIBU

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika, Kuhusu utaratibu.

SPIKA: Kuhusu utaratibu Mheshimiwa Mwakajoka.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, anatuchelewesha.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika,
kuhusu utaratibu, natumia Kanuni ya 64(1)(a) ambayo inasema kwamba Mbunge hatatoa ndani ya Bunge taarifa ambazo hazina ukweli.

Mheshimiwa Spika, ndani ya Serikali tunachojua sisi bado tunaendelea kufanya mazungumzo na IMF kuhusu ripoti hiyo na si kweli Tanzania imezuia ripoti hiyo isitolewe. Sasa naomba kwa kuwa mimi nafahamu na Waziri wa Fedha yuko hapa anafahamu na ana maelezo ya kutosha tu kuhusu jambo hilo ambalo linapotoshwa na Mheshimiwa Mwakajoka, naomba ama Mheshimiwa Mwakajoka afute hizo statement zake za kuituhumu Serikali kwamba imeficha hiyo ripoti na haitaki ripoti hiyo itolewe au alithibitishie Bunge kwamba taarifa anazozisema ni sahihi na ripoti aliyonayo ni sahihi na hakuna jambo lolote ambalo linaendelea kwa sasa ndani ya Serikali. (Makofi)

SPIKA: Alichokisema Mheshimiwa Mwakajoka kidogo tu, unless unisahihishe Mheshimiwa Mwakajoka, alichokisema Mheshimiwa Mwakajoka ni kwamba Tanzania imewazuia IMF wasitoe hiyo taarifa yaani IMF inaomba kibali halafu IMF imezuiliwa Tanzania isichapishe hiyo ripoti, ndio jambo alilolisema. Mheshimiwa Waziri wa Fedha.

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Katika majadiliano ambayo yanaitwa Article Four Consultations, Timu ya IMF ilikuwa hapa nchini kuanzia tarehe 26 Novemba mpaka tarehe 7 Desemba, 2018. Baada ya pale walitoa taarifa na kwa utaratibu ni kwamba wakitoa ile rasimu ya taarifa inarudi Serikalini ili tuweze kuitolea maoni na wao waweze kuyazingatia kabla ya kuichapisha ripoti hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ripoti hiyo nilikuja kuiona tarehe 18 Machi. Hata hivyo, baada ya kuwa sisi tumepeleka maoni yetu lakini tuliona hayajazingatiwa kwenye taarifa hiyo. Nilipokuwa Washington juzi zilizungumza na Bwana Abebe Selassie, Mkurugenzi wa African Department na mpaka leo saa tisa bado tutaendeleza majadiliano kuhusu jambo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa utaratibu ni kwamba baada ya Executive Board ya IMF kuijadili taarifa hiyo, Serikali inakuwa na siku 14 za kuipitia na kusema itolewe au isitolewe. Kwa hiyo, wasiwahishe mjadala Serikali bado inazungumza na IMF na hakuna sehemu ambayo tumezuia ni utaratibu wa IMF yenyewe. (Makofi)

SPIKA: Tuendelee Mheshimiwa Mwakajoka, nafikiri imekusaidia.

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, kuhusu utaratibu.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, mimi nashukuru tu kwamba Mheshimiwa Waziri wa Fedha amekubali kwamba ni kweli maoni yao hayakuzingatiwa na ndiyo maana hawajaruhusu. Kwa hiyo, sikuwa muongo kama alivyokuwa anazungumza Chief Whip pale Mheshimiwa Mhagama, niko sahihi kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, liko jambo lingine ambalo nataka kulizungumza hapa, tumezungumzia uadilifu katika nchi. Kuna gazeti lingine linaitwa Tanzanite. Gazeti hili limekuwa linaandika matusi kila siku ya Mungu, kuwatukana viongozi, kuwagombanisha watu, kuwaita watu magaidi na mambo mengine, mabaladhuri sijui namna gani, wanataka kupindua nchi, hawa watu wanatakiwa kuuwawa lakini Serikali iko kimya inatazama tu. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka, Tanzania Daima nayo mbona hulitaji?

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, aah, aah, unaona sasa?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, kuhusu utaratibu.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, unataka kuniambia kwamba tusizungumze kwa sababu Tanzania Daima hatujalizungumza?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, kuhusu utaratibu.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, lakini haya tunayokuambia unapaswa kuyachukulia hatua.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, kuhusu utaratibu.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, kama kuna vijana wanapigwa na wananyanyaswa kwa sababu tu ya kuandika kwenye mitandao lakini leo gazeti …

SPIKA: Mheshimiwa Msigwa unamsumbua Mheshimiwa Mwakajoka dakika zake zinapotea.

MHE. MCH. PETER SIMON MSIGWA: Mheshimiwa Spika, utaratibu ni kanuni.

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka endelea.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, kuhusu utaratibu.

SPIKA: Wewe ulikuwa unataja magazeti nikakuongezea na lingine, endelea Mheshimiwa Mwakajoka.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, gazeti linaandika, wewe unatuambia leo hapa kama Kiongozi wa Mhimili ambapo tulitegemea ungekuwa unatoa maamuzi mazuri kwa sababu umepewa uongozi...

SPIKA: Mimi nimekuongezea kwenye idadi yako tena unanilaumu kwa sababu nimetaja? (Kicheko)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, umetoa mwongozo mzuri hapa ukasema Mheshimiwa Mwakajoka ulipaswa kuzungumzia kuhusiana na hali halisi kwamba watu wasitukanwe lakini tunaona magazeti haya yanatukana watu, wanasema watu wanyongwe. Wameongeza watu, wanamtaja Mheshimiwa Heche, sijui nani kwamba hawa watu ni hatari wanyongwe, wanataja watu wanyongwe. Hivi kweli nchi hii mnakubali kwamba ni kweli kwa sababu ya mtu kutoa maoni yake, kuzungumza ndani ya Bunge au kwa kuonyesha msimamo wake huyu mtu anastahili kunyongwa? (Makofi)

SPIKA: Bado dakika moja.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, lazima tukubaliane kwamba haya lazima tuyachukulie hatua na tusifananishe na kitu kingine. Ndiyo maana umesema kwamba tusiendelee kufananisha vitu ni lazima tuchukue hatua. Naomba pia hatua zichukuliwe, kama Mheshimiwa Waziri atashindwa kuzungumza kuhusiana na jambo hili tutaona kabisa kwamba hili gazeti ni la Serikali na wanatumwa kufanya hivi. Serikali inayoweza kuwatuma waandishi wa habari wakaandika vitu vya hovyo namna hii, hii Serikali itakuwa dhaifu sana na tunakoelekea kutakuwa siyo kuzuri hata kidogo. (Makofi)

SPIKA: Unakoelekea sasa, Mheshimiwa Mwakajoka. (Kicheko)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahaa, nimeisema Serikali siyo wewe, siyo mhimili wetu Mheshimiwa, huu nauheshimu. (Makofi/Kicheko)

SPIKA: Endelea, malizia. (Kicheko)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo nataka kulizungumza ni kuhusiana na mambo ya michezo. Kwenye nchi hii tunapenda sana michezo na Serikali imekuwa inashangilia sana tunaposhinda.

Mheshimiwa Spika, cha kushangaza hivi juzi Taifa Stars imeingia AFCON tumemsikia Mheshimiwa Polepole anasema kwamba hii ni Ilani ya CCM. Sasa juzi tumepigwa mechi tatu zote mfululizo sijui Ilani ya CCM imeshindwa, maana sasa tunaingiza siasa kwenye michezo. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, sasa mimi nataka nijue Ilani ya CCM imeshashindwa tayari maana tumepigwa mechi zote tatu. Tukishinda Ilani ya CCM, tukipigwa hamsemi, yuko kimya Polepole. Naomba pia mumwambie ajitokeze aseme Ilani ya CCM imeshindwa ili Watanzania wajue kwamba Ilani ya CCM imeshindwa kwenye mechi hizi. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lingine …

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka, mimi Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM. (Makofi)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ndiyo, ila unajua siasa zikiingia kwenye michezo haiwezi kuwa bora hata siku moja. Tunachohitaji ni kukaa pamoja, ushindi wa Timu ya Taifa ni wa pamoja, ni wa Watanzania wote wanashangilia, wanafurahi kwa pamoja lakini inavyotokea…

SPIKA: Kengele ya pili Mheshimiwa Mwakajoka. (Kicheko)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Katibu, Katibu, Katibu.

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Mwakajoka Frank. Mheshimiwa Frank bwana kila akisimama anatupiga kweli kweli bwana. (Makofi/Kicheko)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa kuwasilisha hotuba nzuri ambayo imetoa ushauri wa kutosha na tumemshauri sana Mheshimiwa Mwijage kwamba ajitahidi sana kutumia hotuba hii ili aweze kutekeleza malengo ya Serikali ya Viwanda katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ambacho nataka kukizungumza hapa, kwanza nianze kabisa na mazingira mabaya kabisa ambayo yako katika nchi yetu kwa ajili ya kuendeleza biashara katika nchi hii. Wote tunafahamu na wote tunajua kwamba katika nchi yetu kumetokea na wimbi kubwa sana la wafanyabiashara kufunga biashara zao yakiwemo maduka, mahoteli, lakini pia na wanaoendelea kuuza biashara zao hizo, wanafunga na hawafanyi tena biashara kutokana na mazingira magumu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa tunauliza sana ndani ya Bunge kwamba Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba inanusuru tatizo hili ambalo linajitokeza la wafanyabiashara kufunga biashara zao? Sababu kubwa ni nini? Wafanyabiashara wengi wamekuwa wanalalamika kwamba mazingira ni mabaya, Serikali inawabana tofauti na jinsi inavyotakiwa. Wajibu wa Serikali siku zote ni kuhakikisha kwamba inatengeneza mazingira mazuri ya wafanyabiashara kuendelea kufanya biashara zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imekuwa inatoa majibu ndani ya Bunge inasema kwamba kuna watu wanafunga, lakini kuna watu wengine wanafungua. Hayo majibu hayawaridhishi kabisa Watanzania. Hivi ni kweli Serikali inataka kwenda kwenye Serikali ya Viwanda, inaona biashara zinafungwa na inasema kwamba wacha zifungwe, nyingine zitafunguliwa. Kwa hiyo, tafsiri ni kwamba biashara nyingine zifungwe na nyingine zifunguliwe! Naona tunafanya biashara ya sifuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni vizuri sana Serikali hii ikagundua na ikashughulikia matatizo ya wafanyabishara. Lazima tuzungumze hapa ndani ya Bunge hili, kwamba mazingira ya kuanzisha viwanda katika nchi hii, kama wafanyabiashara wa ndani wanashindwa kufanya biashara na biashara zao zinafungwa, ni mwendawazimu gani mfanyabishara kutoka nje anaweza kuja kuwekeza na kufanya biashara katika nchi hii? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni lazima kwanza tuangalie mazingira mazuri ya kuhakikisha kwamba wafanyabiashara wetu ndani ya nchi hii wanafanya biashara vizuri na biashara zao zinaendelea, ndipo watu kutoka nje watakuja kufanya biashara ndani ya nchi hii. Kama hatuwezi kuangalia matatizo ya wafanyabiashara wetu ndani ya nchi, halafu tukafikiria kwamba kuna wawekezaji watatoka nje waje kuweka biashara zao hapa, hili jambo tulisahau, halitaweza kutekelezeka hata kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukubaliane kabisa kwamba nchi hii kumekuwa na matamko mengi sana ya vitisho. Juzi nilikuwa nasikiliza Taarifa ya Habari, wanasema kwamba hata wakulima sasa hivi wanaopata mazao mengi ni lazima waanze kulipa kodi. Nashangaa sana, yaani wanataka kutuambia kwamba wakulima hawa hawalipi kodi. Hakuna Mtanzania yeyote katika nchi hii ambaye halipi kodi. Tunalipa kodi katika njia tofauti tofauti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakulima hawa wanalima mazao haya kwa kutumia fedha zao na Serikali haiwasaidii hata kidogo. Tumeendelea kuzungumza kuhusiana na pembejeo za kilimo hapa, zinafika kidogo; lakini leo Serikali inafikiria kwamba ni lazima iwakamue wakulima hawa, eti hawalipi kodi. Hilo siyo jambo la kawaida. Ni kwamba kodi zinakusanywa katika maeneo mbalimbali, siyo lazima ukachukue kodi kwenye yale mazao, lakini kodi zinakusanywa. Yule mkulima akishalima anakwenda kuuza, analipa kodi. Bado pia yule mkulima anakwenda mbele zaidi, anakwenda kununua mizigo ambayo tayari imeshalipiwa kodi, anakuwa ameshachangia Taifa lake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunaomba sana, ni lazima Serikali iwe inafika mahali, inapotaka kuanzisha jambo fulani lazima ifikirie. Tunajiuliza sana kwamba mahusiano kati ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Wizara ya Fedha, kuna mahusiano gani hapa? Maana tunaona sana kwamba Waziri wa Viwanda na Biashara pamoja na watendaji wake wa Serikali wamejipanga sana kuhakikisha kwamba nchi inakuwa ya viwanda; lakini Wizara ya Fedha inakwamisha kutokana na sera na mipango mbalimbali ambayo inafika mahali inakuwa inapingana na dhana nzima ya kuanzisha viwanda katika nchi hii. (Makofi)

Kwa hiyo, ni lazima Wizara ya Viwanda na Wizara nyingine zinazofuatia na Wizara ya Fedha lazima wakae pamoja kupanga na kukaa, kuangalia ni namna gani wanaweza wakapunguza kero ambazo zinasababisha viwanda visianzishwe katika nchi hii.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii ili na mimi niweze kuchangia katika Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii pia kuungana na Waheshimiwa Wabunge wote ambao wanasema kwamba fedha hii iongezwe ili kuweza kutoa huduma bora kwa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo la kushangaza sana, sisi Wabunge tumekuja hapa nia na madhumuni ni kuishauri Serikali na kuhakikisha kwamba tunaisimamia pia. Huwezi kuamini kabisa kwamba bajeti ya mwaka wa jana mpaka mwezi huu wa Aprili kulikuwa na utekelezaji wa asilimia 19.8. Hata hivyo sisi hatuoni kama hili ni janga na hatuoni kama hili ni tatizo kubwa sana, kwamba tunaweka bajeti kwa ajili ya kuhakikisha kwamba maji yanapatikana katika nchi na Watanzania wanapata maji halafu utekelezaji unakua asilimia 19.8, haya ni maajabu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli hata kama leo tunasema tunataka kuongeza hizi fedha zifikie labda za mwaka jana, lakini kama tutakuwa tunatekeleza asilimia 19 mpaka 20 haitaweza kutusaidia hata kidogo. Tatizo kubwa ni kwamba Serikali haitaki kupeleka fedha. Ninampongeza sana ndugu yangu Kitila Mkumbo ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara hii, lakini pia na watendaji wote, lakini nawaonea huruma sana kwamba wameingia katika wakati mgumu sana kwa sababu wanakwenda kufanya kazi maeneo ambayo hawapelekwi fedha, kinachoendelea ni lawama na kuonekana kwamba sio watendaji wazuri wa kazi wakati wana uwezo wa kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba sana Serikali ihakikishe kwamba inawatimizia Watanzania mahitaji yao. Kwa sababu haiwezekani kabisa tukawa tunakaa Waheshimiwa Wabunge humu tunapanga bajeti halafu utekelezaji unakuwa asilimia 19, hii ni aibu kubwa na hii inaonyesha ni jinsi gani ambavyo Serikali ya Chama cha Mapinduzi inazidi kuwahadaa na kuwadanganya Watanzania kwa jinsi ambavyo inataka kusema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, najaribu kuangalia pia katika Mji wangu wa Tunduma. Mji wa Tunduma ni Mji ambao upo mpakani mwa Zambia na Tanzania, lakini mji huu unahudumia nchi karibuni kumi. Unahudumia nchi zote za Kusini mwa Tanzania kwa mfano nchi ya Zambia, South Africa, Namibia, Angola, Congo na Botswana zote zinapita pale na mpaka wa Tunduma ni nguzo kubwa sana ya Bandari ya Dar es Salaam, asilimia 71 ya mizigo inayoshuka kwenye Bandari ya Dar es Salaam inapita kwenye mpaka wa Tunduma, lakini kuamini mpaka wa Tunduma wananchi hawana maji, wageni wanaokuja pale hawapati maji na wageni wale sasa wanakwenda kulala Zambia upande wa Nakonde, hii ni aibu kubwa sana kwa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kukuhakikishia kwamba mpaka wa Tunduma unaingiza kwa mwaka zaidi ya shilingi bilioni 80 lakini leo hakuna maji safi na salama kwenye mpaka wetu wa Tunduma. Kwa hiyo, ninaomba sana wakati Mheshimiwa Waziri anakuja hapa kuzungumza ajaribu kutueleza kwenye mpaka wa Tunduma tatizo ni nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hata bajeti ya mwaka wa jana tulikuwa na bajeti ya shilingi milioni 753 lakini hakuna hata shilingi iliyokwenda kwenye Mji wa Tunduma kwa ajili ya utekelezaji wa maji. Waziri anatakiwa atueleze kwanini fedha hizi hazijakwenda?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mwaka jana pia kwenye bajeti kulikuwa na mradi ambao ulitaka kujengwa kwenye Mji wa Tunduma, mradi ulitaka kujengwa na kampuni ya ACCPAC International kutoka Ubelgiji; ulikuwa na thamani ya Euro milioni 100. Mradi ule mpaka leo ni hadithi na hakuna kinachoendelea, tunataka kujua na wananchi wa Mji wa Tunduma wanataka kujua ni lini mradi mkubwa huu ambao unatakiwa kutekelezwa utakwenda kutekelezwa haraka haraka iwezekanavyo kwenye Mji wa Tunduma? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka huu tunaona tena fedha zimepunguzwa. Mwaka wa jana tulikuwa tumetengewa shilingi milioni 753, mwaka huu wamepunguza mpaka kufika shilingi milioni 600; tunataka kujua pia ni kwa nini fedha zimepunguzwa ikiwa mwaka wa jana hatukupata hata shilingi moja iliyokwenda kwenye miradi ya maji kwenye Mji wa Tunduma, tatizo ni nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti lakini nilichoshangaa tena kwenye Mkoa wa Songwe ambako kuna Wilaya ya Ileje, Momba, Mbozi na Wilaya ya Songwe tumetengewa fedha shilingi bilioni nne katika Mkoa mzima wakati kuna Mikoa mingine wametengewa shilingi bilioni 20, ama kumi na tisa, wametengewa fedha nyingi, tatizo nini? Kwa nini Songwe tumetengewa fedha kidogo kiasi hicho?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati anakuja kusema aje tu...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii ya kuweza kuchangia taarifa za kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nipende kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa Msajili wa Hazina aliyetumbuliwa Ndugu Lawrence Mafuru kwa kazi kubwa aliyokuwa akitushauri mpaka sasa hivi tumeona kuna mabadiliko makubwa sana. Toka kupata faida ya shilingi milioni 443 mpaka tulipata milioni 885.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siwezi pia kupuuza mchango wa mzee wetu ambaye ni msajili wa sasa hivi, tunamshukuru pia. Nitumie fursa hii pia kuwashukuru sana Wanasheria wetu wanafanya kazi kubwa sana kuhakikisha kwamba wanatushauri na tunafanya vizuri kuishauri taasisi pamoja na taasisi zinazokuja kwenye vikao vyetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nianze na madeni ya Serikali. Ukijaribu kuangalia kwenye taasisi mbalimbali ambazo tumeweza kuziita na kuzikagua tumekuta Serikali inadaiwa fedha nyingi sana. Baadhi ya mashirika mbalimbali yameweza kutoa huduma, lakini Serikali imeshindwa kulipa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiyataja mashirika mbalimbali ambayo yanaidai Serikali ukianza na Mamlaka ya Kuchimba Visima inaidai Serikali karibu bilioni 2.7; ukija Mamlaka ya Maji DUWASA Dodoma hapa inadai Serikali bilioni mbili; ukija SUMA JKT wanaidai Serikali bilioni 5.8; ukija MSD wanaidai Serikali bilioni 144.9; Haya yote ni madeni ambayo Serikali inadaiwa, lakini wananchi wa kawaida wanapokuwa wanadaiwa hata Sh.10,000 wanapigwa penalty na wanakatiwa huduma katika maeneo yao, lakini Serikali imekuwa ikidaiwa na haijali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni madeni ya muda mrefu, si madeni ya siku moja wala ya mwaka mmoja. Haya ni madeni ambayo mengine yana miaka mitano, mengine miaka mitatu, Serikali haitaki kabisa kuhakikisha kwamba, inalipa haya madeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, dhumuni la kuanzisha mashirika haya tulitaka yatoe tija kwenye nchi hii, lakini pia, yaajiri watu wengi, lakini mashirika mbalimbali sasahivi yako katika hali mbaya na yanataka kufa sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nizungumzie kuhusu na Shirika la Ndege (ATCL). Shirika hili la Ndege ATCL ndani ya miaka mitatu limeendeshwa kwa hasara kubwa kabisa. Shirika hili mwaka 2014/2015, liliendeshwa kwa hasara, lakini matumizi yake kila mwaka yanazidi kuongezeka. Mwaka 2014/2015, walitumia karibu 94,359,000,000/=; lakini mwaka 2015/2016, walitumia bilioni 109.2; na mwaka 2016/2017 wakatumia bilioni 13.7. Fedha hizi ambazo zinatumika tofauti na mapato ambayo yanapatikana ni hatari kabisa kwa mashirika mbalimbali na shirika hili linataka kufa sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napata maswali mengi sana kwamba, sasa hivi tunaona Serikali inajumua ndege nyingine, maana si kununua ni kujumua; inajumua ndege nyingine kwa ajili ya kuhakikisha kwamba shirika hili linakuwa na ndege nyingi. Sasa nafikiria wamefanya utafiti gani wakati shirika linaendeshwa kwa hasara, halafu Serikali inakwenda kuwekeza fedha nyingi za Watanzania kwenda kununua ndege. Ni namna gani wamefanya utafiti ili shirika hili liweze kuleta tija kwenye nchi hii. Kwa hiyo, hali si nzuri. Shirika linaendeshwa kwa hasara na linaendelea kutumia fedha nyingi kupita kiasi ambacho kinapatikana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile kuna shirika lingine, kuna TANTRADE, shirika hili pia limeendeshwa kwa hasara miaka mitatu mfululizo. Shirika hili mwaka 2013/2014, lilitumia fedha milioni 397. 9; lakini mwaka 2014/2015, lilitumia milioni 614.6; na mwaka 2015/2016, likatumia milioni 838.2.

Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi haya ambayo yanatofautiana na mapato linayopata shirika hili yamesababisha hasara kubwa kwenye shirika na mtaji wa uwekezaji kwenye shirika hili umeshuka kwa asilimia toka 32.7 hadi 16.5, ni hatari sana. Ni kwamba, mpaka sasa hivi usimamizi wa mashirika haya umeonekana kwamba Wakurugenzi pamoja na bodi ambazo zinachaguliwa zimeshindwa kusimamia mashirika haya na Serikali isipochukua hatua mashirika haya yanakwenda kufa na kupotea kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, liko jambo lingine, nataka kuzungumzia pia, kuhusiana na sheria mbalimbali ambazo zinaendesha mashirika yetu. Kwa mfano, Sheria ya Manunuzi; ukiangalia MSD sasa hivi Sheria ya Manunuzi inaathiri sana shirika hili. Sheria ya Manunuzi inafika mahali MSD ili waweze kupata dawa wanatumia miezi mitatu kutangaza zabuni, lakini pia inasababisha dawa zichelewe kufika nchini, zaidi ya miezi tisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili ni jambo la kuangalia sana kwamba. Hivyo, ni muhimu Serikali ikajaribu kuangalia Sheria hizi za Manunuzi zimekuwa ni tatizo katika mashirika haya na yanashindwa kuendelea na kufanya vizuri kwa sababu ya sheria kandamizi ambazo zipo katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni kuhusu shughuli mbalimbali ambazo zinafanyika kwenye mashirika haya. Ukijaribu kuangalia mashirika mbalimbali katika nchi hii hayana bodi. Ukiangalia Shirika la MSD Bodi yake sasa hivi imekwisha muda wake karibu mwaka mzima umepita, lakini mpaka sasa hivi hakuna jambo lolote ambalo linaendelea kwa ajili ya kuhakikisha kwamba, bodi hizi zinateuliwa upya na kuhakikisha kwamba, zinafanya kazi kwa kusaidia mashirika haya ili yaweze kufanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie fursa hii kwanza kukushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia siku ya leo. Nafikiri leo tunajadili Mapendekezo ya Mpango wa Taifa. Nina mambo matatu ambayo nataka kujadili siku ya leo. Jambo la kwanza kabisa, nataka kuanza na Utawala Bora. Tunavyojadili Mpango, tunajadili mambo muhimu sana kwa ajili ya Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukweli tu ni kwamba utawala bora ndiyo itakuwa dira na itakuwa mwongozo mzuri sana kuhakikisha kwamba tunatekeleza Mapendekezo ya Mpango huu ambao tunaujadili siku ya leo. Kama hatutaweza kulinda utawala bora katika Taifa hili, tutakuwa tunafanya mchezo ambao hautaweza kutusaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nazungumza haya kwa sababu, ili wawekezaji waweze kufika katika nchi, hii ni lazima kuhakikisha kwamba utawala bora unakuwa ni kipaumbele, pia utulivu na amani katika nchi yetu lazima viwe kipaumbele zaidi. Ninazungumzia utawala bora kwa sababu ni lazima tuhakikishe kwamba sheria zinasimamiwa vizuri na zinafuatwa katika Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nataka kuzungumzia tu kuhusiana na suala la mchakato wa uchaguzi ambao ulikuwa unaendelea kwenye nchi yetu na ambao unaendelea mpaka sasa hivi. Nimemsikia Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI akizungumzia hali halisi ya kwamba wale wote waliojaza fomu na kurudisha na wale ambao hawakuteuliwa lakini walijaza fomu na kurudisha, waendelee na uchaguzi. Yako matatizo mengi sana yaliyojitokeza kwenye mchakato huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza kabisa, kwa mfano ukifika kwenye Mji wangu wa Tunduma na Wilaya ya Mbozi, kuna baadhi ya Kata kama sita Watendaji hawakuonekana kabisa na hakuna aliyechukua fomu katika maeneo hayo. Kwa hiyo, fomu hazikuchukuliwa kwa sababu milango ilikuwa imefungwa na hakuna mtu yeyote aliyepata fomu. Watu walishinda pale kuanzia asubuhi mpaka jioni na maeneo mengine ambamo Watendaji walikutwa, waliwaita Polisi wakawakamata na wananchi sasa hivi wanasota wako rumande.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kuna matatizo makubwa sana. Tulikuwa tunataka tupate ufafanuzi, kwa mfano yale maeneo ambayo watu hawakupewa ruhusa kabisa ya kwenda kuchukua fomu, namna gani watakwenda kushiriki uchaguzi huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia maeneo mengine, ni wale watu ambao walikataliwa kabisa wasirudishe fomu hizo, ni namna gani wangeweza kushiriki uchaguzi huo. Kwa hiyo, wakati unazungumza maneno haya, tumekwenda kwa Mheshimiwa Jafo zaidi ya mara tatu, tumemkuta Mheshimiwa Waziri, lakini pia tumemkuta Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, tumemweleza matatizo haya tukiongozana na baadhi ya Waheshimiwa Wabunge, lakini hakuna kilichoendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulistaajabu sana, wasimamizi wa uchaguzi ambao wamepewa fursa ya kusimamia uchaguzi huo wa Serikali za Mitaa wamepewa kazi na Ofisi ya TAMISEMI, lakini cha kushazangaza maelekezo ambayo Mheshimiwa Waziri alikuwa anasema anawalekeza, hawakuweza kutekeleza hata moja. Sasa tunakwendaje kwenye uchaguzi wa namna hiyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli utaratibu uliokuwa ukiendelea ni utaratibu wa kihuni ambao kwa kweli haustahili kabisa. Ninashangaa kwamba mpaka sasa hivi Serikali haijachukua hatua kwa hao watu ambao wamekwenda kuvuruga mchakato wa uchaguzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo naomba sana, kwenye suala la utawala bora ni muhimu tukaeshimu sheria tunazo zitunga wenyewe, lakini pia na kanuni na taratibu mbalimbali ambazo tunakuwa nazo ili kujenga imani pamoja na kujenga umoja na mshikamano ulio katika Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka pia kuzungumzia kuhusiana na suala la uchumi. Nimesikia mara nyingi sana Mheshimiwa Rais anazungumzia kuhusiana na vita ya uchumi. Vita ya uchumi tunayoizungumzia ni kuhakikisha kwamba fursa yoyote inayopatikana kwenye nchi ni lazima tuitumie kwa muda mwafaka; tumekuwa tunachelewa sana kufanya maamuzi katika taifa hili. Mara nyingi mipango mingi; na nimepata taarifa mbalimbali ambazo si rasmi; wanasema mipango tunayoipanga katika taifa hili inakwenda kutumika kwenye nchi nyingine na wanafanya vizuri, lakini sisi tumekuwa ni wazito na wagumu wa kuamua ni namna gani tunaweza tukatekeleza fursa na mipango mbalimbali ambayo inapatikana na ambayo tunaipanga katika taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe mfano kidogo, na wewe mwenyewe umekuwa unasisitiza sana; kwa mfano kama Bandari ya Bagamoyo, tumekuwa na hofu na tunapiga kampeni ya hofu badala ya kuingia. Tuna wataalamu wengi na tuna wasomi wengi. Hivi kweli wameshindwa kupata ukweli? Wameshindwa kupata uhakika wa namna gani tunaweza tukahakikisha kwamba fursa ya Bandari ya Bagamoyo tukatekeleza, na tusifikiri kwamba tuko peke yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda Beira kule Mozambique wana nafasi wanaweza wakafanya hayo tukienda Mombasa wanaweza wakafanya hayo hasa ni lazima twende na wakati tunashindwaje kujadili na watu tunawasomi wengi wa kutosha tumeshindwaje kujadili na watu ili miradi hii ambayo inaweza ikainua uchumi wa taifa iweze kutekelezwa katika taifa letu tunaona haya mambo hayatekelezeki na kila wakati tunaona kimya.

Mheshimwa Mwenyekiti, lakini yapo mambo mengine ambayo tunaona kabisa kwamba yanasababisha uchumi wetu usisonge mbele. Kwa mfano sasa kuna tume/ kamati uliiunda kwa ajili ya kuchunguza masuala ya madini, wakaenda Mererani wakaangalia mambo mabaya yaliyokuwepo kule na wakasema wanaweza wakafika mahala wakasitisha ule mgodi ili kujadili kwa manufaa ya taifa hii. Hata hivyo ni miaka mitatu leo au mwaka wa nne leo hakuna kinachoendelea; mgodi umesimama, wafanyakazi zaidi ya 400 wamefukuzwa kazi na hawajapewa hata mafao yao mpaka sasa hivi lakini kazi aiendelei na migodi ile imesimama na hakuna kinachozalishwa pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa lazima tufike mahala kama taifa tujuwe kwamba tunapokuwa tunahitaji uchumi upande ni lazima tuhakikishe kwamba tuna fanya haraka kwenye fursa ambazo tunazo. Leo tuna mgodi lakini hamna kinachoendelea; tanzanite imekaa pale inaoza watu wanaochimba pale hawaeleweki wanasema tunajadili, miaka mitatu mnajadili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, na huo mgodi si kwamba labda anamiliki mbia peke yake, ni sisi nay eye; sisi tuna asilimia 50 na yeye anaasilimia 50, lakini tunashindwa kujadili kitu kama hicho kitu kidogo tunakaa miaka 3. Wananchi wetu ambao ni Watanzania waliokuwa wanafanya kazi pale zaidi ya 400 wameshindwa kulea familia zao na kupeleka watoto wao shuleni kwa sababu ya majadiliano, ni siri ambayo mpaka leo hatuelewi. Kwahiyo tunaomba sana Wizara ya fedha pamoja na Serikali watuambie ni kwanini mpaka leo hawajafikia makubaliano kwenye majadiliano ya Mgodi wa Tanzanite ili uweze kuzalisha na kuhakikisha kwamba unachangia Pato la Taifa kwa kipindi ambacho tumekuwa nao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine; tumeshangaa sana, tunasema kwamba tuna madini na tunataka madini yachangie Pato la Taifa; na kila mwaka tunapanga bajeti humu ndani lakini fedha hazijawahi kwenda. Waziri wa fedha pia atuambie ni kwanini hapeleki fedha ili kuhakikisha kwamba tunakwenda kuinua uchumi kwa kutumia madini? miaka yote mwaka wa kwanza mpaka wa tatu mpaka miaka minne hakuna kilichoendelea. Mwaka jana tulitenga takriban bilioni sita ili waweze kufanya shughuli za maendeleo katika migodi yetu lakini haikwenda hata shilingi; na hata mwaka juzi pia. Sasa maaana yake ni nini? Kama kweli tukaanzisha shirika la kusimamia madini katika nchi kuhakikisha migodi yetu inafanya kazi na tunapata pato kubwa la taifa kutokana na madini lakini hatupeleki fedha. Kwahiyo mambo haya ni lazima tuyatazame sana, na kama Watanzania tuchangamkie fursa; tunapokuwa na mradi wowote ni lazima kuhakikisha kwamba twende na muda. Tunavyozidi kuchelewa ndivyo ambavyo tunachelewa kufanya maendeleo katika taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine ni kuhusiana na kilimo. Asilimia 65 ya Watanzania ni wakulima, wafugaji na wavuvi; fedha zimekuwa zinatengwa kila mwaka; nitoe mfano wa miaka mitatu tu. Mwaka wa 2016/ 2017 tulitenga ndani ya Bunge hapa bilioni 101 lakini fedha iliyokwenda kwenye shughuli za maendeleo bilioni tatu peke yake. Mwaka 2017/2018 tulitenga shilingi bilioni 150, fedha iliyokwenda kwenye kilimo ilikwenda bilioni 16 peke yake. Pia mwaka 2018/2019 tulitenga fedha hapa bilioni 95 lakini fedha iliyokwenda ni takriban bilioni 45.

Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia 65 ya Watanzania ambao ni kundi kubwa kuliko kundi lolote katika nchi hii hawapelekewi fedha; sasa leo tunasema tunakwenda kwenye uchumi wa kati; tunawezaje kwenda kwenye uchumi wa kati kama wananchi hawa ambao ni kundi kubwa wangeweza kuzalisha lakini pia wangeweza kuchangia Pato la Taifa hawapelekewi fedha. Kwahiyo tunaomba sana; tunapozungumzia uchumi ni lazima tuhakikishe kwamba tunalenga maeneo muhimu ambayo yanaweza yakainua uchumi wa taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ni lazima tukubaliane, leo katika takwimu za Serikali vijana wetu wanaomaliza kwenye vyuo mbalimbali hapa nchini ni takriban 800,000, lakini watu wanaoingia kwenye ajira rasmi ni takriban watu 40,000 watu takriban 760,000 hawana kazi; hawa watu wanakwenda kwenye kilimo na uvuvi lakini fedha haziendi kule tunasema tunataka kujenga taifa linaweza likatusaidia kuinua wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwahiyo mapendekezo ya mpango tunayoyaangalia leo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa ni kengele ya pili.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa, hauoneshi ni namna gani tunakwenda kwenye uchumi wa kati, inaonekana tunazungumza ndani ya Bunge lakini utekelezaji kwakweli hauko sawa sawa. Tunaomba uwe mkali lakini uendelee kutoa maagizo tukishirikiana na sisi Waheshimiwa Wabunge ili tuhakikishe kwamba Serikali hii inafanya yale tunayoyapitisha ndani ya Bunge hili. Ahsante.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na mimi niweze kuchangia bajeti hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kwanza kuunga mkono hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani, lakini pia nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Kivuli kwa jinsi ambavyo ameandaa bajeti vizuri, lakini pia nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mwenyekiti wetu wa Chama Taifa, Kamanda wa anga ambaye kwa kweli ni kiongozi imara anayesababisha tufanyekazi vizuri na Watanzania waweze kutuamini na chama hiki kinaaminika kweli kweli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mimi nimekaa hapa nasikiliza michango mbalimbali ya wenzetu watu wa CCM na nilikuwa namsikia pia Mheshimiwa Amina Mollel hapa anazungumza kuhusiana na ukusanyaji wa mapato, anasema kwamba tungepeleka jeshi yaani mpaka leo Serikali ya Chama cha Mapinduzi na Wabunge wake hawaelewi kwamba masuala ya fedha ni taaluma yaani wanaona jeshi pake yake tu kutumia nguvu, ndiyo kitu pekee ambacho kinaweza kikakusanya mapato katika Taifa hili yaani hapo ndipo milipofikia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nilikuwa nataka kuzungumzia jambo lingine; watu wengi wanasema sisi tunakataa Stiegler’s Gorge, tunakataa standard gauge huu ni mtazamo wa hovyo kabisa. Sisi hata siku moja hatujakataa standard gauge, sisi hata siku moja hatujakataa Stiegler’s Gorge, tulichokuwa tunasema sisi hapa tulikuwa tunatoa ushauri kutokana na matumizi makubwa ambayo yanakwenda kwenye miradi mikubwa miwili badala ya kuwahudumia Watanzania walio wengi, hicho ndicho ambacho tulikuwa tunajaribu kukizungumzia na siku zote tunaposema kwamba Serikali hii inakwenda kufanya shughuli za vitu, inaweka bajeti ya vitu badala ya bajeti inayowahusu wananchi tulikuwa tunamaanisha. Tunajaribu kuangalia ni namna gani bajeti zingine ambazo zimepewa fedha kidogo na hata hizo fedha kidogo ambazo zinakwenda kule hazipelekwi kabisa au zinapelekwa kidogo sana na ndiyo maana tunasema kwamba ni lazima mfike mahali mkubali. Tatizo kubwa CCM mnachokifikiri ni kwamba vyote tunavyoviongea kama uoinzani ndani ya Bunge hili mnaona kama sisi tunapinga kila kitu na kwa sababu ya kiburi mlichonacho ndani ya mioyo yenu hamuwezi kutekeleza ule ushauri ambao tunawapa, mnaendelea kubeza, lakini kesho mnarudi mnaanza kufanya hayo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Rais juzi amewaita wafanyabiashara Dar es Salaam, tuliyoyazungumza mwaka 2016/2017 amekwenda kuyazungumza Mheshimiwa Rais hayo hayo na amefanya mabadiliko. Leo Mheshimiwa Mpango tulichozungumza kwamba mnaleta sheria ambazo ni kero kwa wafanyabiashara zitakazosababisha wafanyabiashara wasifanye biashara mkasema hapana hizi ndiyo sheria nzuri, leo Mheshimiwa Mpango karibu kodi 54 anakwenda kuziondoa. Sasa yote tuliyazungumza yaani mpaka muue biashara mpaka mhakikishe kwamba biashara zinakwenda vibaya ndiyo mrudi nyuma muanze kufikiri kwamba sasa tumekosea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tunaona sisi ni macho ambayo yanaona kila siku tunafanyakazi ya kuchanbua ni namna gani mambo yanavyokwenda…

MHE. AMINA S. MOLLEL: Taarifa.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: …tofauti na ninyi mnakoelekea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo sisi…

MBUNGE FULANI: Tulieni.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Frank Mwakajoka kuna taarifa. Mhehsimiwa Amina Mollel

T A A R I F A

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana.

Naomba nimpe taarifa mchangiaji anayezungumza kwamba anaposema waliishauri Serikali na hatimae leo hii ndiyo yanachukuliwa, naomba tu nimkumbushe kwamba katika Bunge lililopita waliishauri sana Serikali kuhusiana na masuala ya madini na hatimae Serikali ikaonesha usikivu na ikaleta sheria hizo, lakini wale wale waliokuwa wanashauri hatimae ndiyo hao hao waliokuja kupinga sheria hiyo. Ahsante. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Frank Mwakajoka unaipokea taarifa hiyo?

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, haya ambayo anayafanya Mheshimiwa Mbunge aliyekuwa anatoa taarifa yaani hii inaonesha ni jinsi gani ambavyo mnandelea kuwa dhaifu sisi kazi yetu ni kushauri na kama hamsikii mtaendelea kufanya hivyo na hamtaweza kupiga hatua na hamtaweza kufanya chochote kwa sababu hamuwezi mkasikia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Bunge la mwaka 2017/2018 tulizungumzia hapa, ilikuja taarifa hapa kwamba tunataka sasa fedha zote za Taasisi za Serikali ziondoke kwenye benki za kibiashara ziweze kwenda BOT. Jambo hili tulilishauri sana na tukasema yaani sababu ni nini? Sababu waliyoitoa wakasema kwamba mabenki yanapata sana faida, lakini tukashangaa sana kwamba kazi ya benki za biashara katika nchi hii kazi yake zinaisaidia Serikali kuwakopesha wajasiriamali wadogo wadogo na wafanyabiashara wakubwa kuhakikishawkamba wanafanya biashara na wanapata mitaji. Sasa mkapeleka hizo fedha BOT na sasa hivi hizo fedha zimekaa kule na BOT haikopeshi wajasriamali na benki imeshindwa kukopesha wafanya biashara wadogo wadogo na wajasiriamali kwa hiyo mambo hayaendi. Yote haya najua baada ya mwaka huu mtakuja kesho kutwa mtaiondoa na kwasababu ndiyo kawaida yenu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mimi nia yangu kubwa nilikuwa nataka kuzungumzia sana kwenye kilimo; lengo kubwa la Serikali wanasema ni Serikali ya wanyonge na imekuja kuondoa umaskini kwa wanyonge, lakini nataka kuuliza wanyonge ni watu wa namna gani? Unapozungumzia wakulima, wafugaji na wavuvi unazungumzia asilimia 65 mpaka 75 ya Watanzania wote. Kundi hili la Watanzania ambalo ni kubwa kabisa leo limesahaulika kabisa katika bajeti ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi hasa Serikali ya Awamu ya Tano.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda nikukumbushe; mwaka 2016/2017 tulitenga fedha, tulipitisha fedha hapa shilingi bilioni 101; kati ya shilingi bilioni 101 fedha iliyokwenda kufanyakazi ya maendeleo kwenye kilimo ilipelekwa shilingi bilioni mbili peke yake, lakini mwaka 2017/2018 tulitenga fedha hapa shilingi bilioni 150 fedha iliyokwenda kufanyakazi ya kilimo ilipelekwa shilingi bilioni 16 peke yake, lakini mwaka jana tumetenga pia fedha imekwenda kupelekwa karibuni shilingi bilioni 46 peke yake.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo kubwa ambalo nashangaa na nasema kwamba jambo hili halihitaji hata kuwa profesa wala halihitaji kuwa daktari. Nazungumza hivi kwa sababu Watanzania asilimia 65 mpaka 75 tafsiri yake ni kwamba ndiyo wanunuzi wakubwa katika Taifa hili na ndiyo walipa kodi wakubwa. Ukitaka kujua kwa nini biashara zime- stuck katika mwaka 2018/2019 ni kwa sababu wakulima na wafanyabiashara wa mazao walishindwa kuuza mazao yao baada ya kukosa soko na ndiyo maana biashara zote zilisimama. Kwa hiyo, unapozungumzia biashara lazima uzungumzie kundi la watu asilimia 75 la wakulima, wafugaji na wavuvi. Usipozungumzia kundi hili ujue kabisa wanunuzi hawatakuwepo katika nchi hii kwa sababu wakikosa kipato hata wafanyabiashara wa maduka wanaofanya biashara za viwandani hawataweza kuuza kwa sababu watu wanaotegemewa sana ni wakulima, wafugaji na wavuvi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikwambie mchango wa sekta ya kilimo katika nchi hii ni mkubwa sana. Ukienda kuangalia kwenye suala la ajira karibuni asilimia 65 ya Watanzania wote wanajiajiri katika kilimo, ufugaji na uvuvi, lakini ukienda kwenye chakula karibuni asilimia 100 tunapata chakula kutokana na hao wakulima ambao ni wananchi waliojiajiri kwenye kilimo. Lakini ukienda pia kwenye pato la Taifa inachangia karibu asilimia 28 mpaka 30 lakini bado uwekezaji kwenye kilimo kwenye Serikali ya Awamu ya Tano iko chini ya asilimia mbili, sasa tusitegemee viwanda kwa sababu asilimia 65 ya malighafi ya viwandani yanategemea kilimo na kama yanategemea mazao ya kilimo tafsiri yake ni kwamba kama hatutawekeza kwenye kilimo tusitegemee kupata viwanda katika nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa leo mnasema kwamba hii ni Serikali ya viwanda halafu hamuwekezi kwenye viwanda mnapeleka kwenda kununua ndege, mnakwenda kujenga Stiegler’s Gorge, mnakwenda kujenga standard gauge na manatumbia kwamba hii ni Serikali ya viwanda, hivyo viwanda vitakuja kwa namna gani? Kwa hiyo ni lazima tuhakikishe kwamba tunainua kilimo na ninataka kutoa mfano, kwamba Serikali hii kwa kweli imeshindwa kabisa kuhakikisha wkamba inawasaidia Watanzania wanyonge ambao ni wakulima, wafugaji na wavuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2004/2005 katika bajeti ya kipindi hicho yaani uwekezaji ulikuwa ni asilimia 4.7 ya bajeti yote; mwaka 2005/2006 ilikuwa aislimia 5.8 ya bajeti yote; mwaka 2006/2007 ilikuwa aislimia 5.8 na pia mwaka 2009/2010 ilikuwa asilimia 8.6 na walitenga fedha karibu shilingi bilioni 666.9; leo mnatenga shilingi bilioni 208 miaka mingapi imepita mnatenga shilingi bilioni 208 mnasema mnakwenda kuinua kilimo na mtapata viwanda katika Taifa hili, mnajidanganya. Ni lazima tufanye mageuzi ya kilimo kwanza ndiyo tutakwenda kwenye viwanda na kama mnaota viwanda wakati hamjafanya mageuzi ya kilimo mnajidanganya na Serikali yenu itakuwa ni Serikali ambayo inazungumza uongo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, na ukisoma Ilani ya Chama cha Mapinduzi utaona kabisa walikuwa wamekubalina kwamba ni lazima wawekeze kwenye kilimo, watainua kilimo kwa asilimia nane ndani ya miaka mitano, lakini leo kilimo hakijainuka na kilimo hapa kimekua kwa asilimia 5.3 peke yake. Sasa kwa hiyo mmewadanganya wananchi ambao mlikwenda kuuza Ilani yenu iili mchaguliwe na mwongoze Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia kwenye Ilani yenu katika kifungu cha 27(n) mlisema kwamba mtanunua meli tano za uvuvi ili kuhakikisha kwamba mnawainua wavuvi lakini pia mnahakikisha kwamba kinachangia pato la Taifa kwenye upande wa uvuvi. Lakini nakwambia mpaka sasa hakuna meli hata moja wala boti iliyonunuliwa kwenye bahari ya Hindi kwa ajili ya uvuvi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ilikuwa ni kwamba mnatengeneza na kwenda kuuza sera zenu kwa wananchi lakini hazitekelezeki. Kwa hiyo, sisi tunasema kwamba tunawakumbusha Watanzania waelewe kwamba yanayozungumzwa kwenye majukwaa, yaliyowekwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi hayatekelezeki.

Mheshimiwa Naibu Spika, niwaambie tu ukweli Watanzania sio watu wajinga, leo wakulima wako kijijini wanalima kule, wanakosa masoko na hata wakipata masoko wanatafuta masoko yao tunakwenda kuzuia mipaka mnasema wasiondoke. Juzi Salum Sumri kule Sumbawanga aliamua kuacha mabasi akasema ngoja ajikite kwenye kilimo akagharamia vitu vingi sana kwa ajili ya kilimo, lakini cha kushangaza baada ya kugharamia haya amekwenda kulima amepata karibuni tani 47,000 lakini ameshindwa kuuza hayo mahindi yake yako ndani mpaka sasa hivi alipata soko Congo mkazuia mkasema asiende kuuza mkasema mtakula mahindi yote haya mnakulaje mahindi tani 40 na ngapi wakati fedha hamna za kununulia mahindi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naona...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kupata fursa hii ya kuweza kuchangia kwenye Hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Mheshimiwa Spika, nianze kwanza kuwapongeza viongozi wangu wa chama hasa Mwenyekiti wetu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa jinsi ambavyo anafanya kazi yake vizuri ya kukiongoza chama hiki lakini pia kuhakikisha chama kinasonga mbele na kinafanya vizuri zaidi na kuwa tishio kwa kweli kwenye Chama Cha Mapinduzi.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia nitumie fursa hii kuwapongeza na kuwashukuru sana wananchi wangu wa mji wa Tunduma kwa jinsi ambavyo wanazidi kuniunga mkono, toka walivyoniamini mwaka 2015 mpaka sasa hivi wanaendelea kunihitaji niendelee kuwa Mbunge wao na mimi nasema kwamba nimejiandaa kuendelea kuwaongoza na kuwahakikishia kwamba nawawakilisha vizuri. Kwa hiyo, mambo yanakwenda vizuri Mheshimiwa Spika hakuna matatizo yoyote.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kikubwa tu…

SPIKA: Hutarajii kuita waandishi wa habari hivi karibuni?

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, narudi tu wala usiwe na wasiwasi.Kikubwa tu nilichotaka kuzungumza hapa nilikuwa nimefurahi sana kumsikia Mheshimiwa Rais anasema kwamba uchaguzi utakuwa kama ulivyopangwa na sisi kama Upinzani tulikuwa na masikitiko makubwa sana tulivyosikia kwamba kuna fununu Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi wanasema uchaguzi uhairishwe tulikuwa tunajisikia vibaya kwa sababu tumejiandaa vizuri na tumejipanga vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunafikiri uchaguzi huu ni uchaguzi ambao tunaamini kabisa utakuwa huru na haki lakini pia nimepata moyo zaidi baada ya kuona Mheshimiwa Rais amekutana na wabalozi wa nje na kuwaambia kwamba uchaguzi utakuwa huru na haki lakini Waziri wa Mambo ya Nje amekutana na mabalozi wa nje pia amewaambia utakuwa huru na haki. Nimemwona Simbachawene pia juzi amesema uchaguzi utakuwa hiuru na haki ninaamini uchaguzi huu utakuwa huru na haki watanzania wanahitaji kuchagua kiongozi wanayemtaka na siyo kuchaguliwa kiongozi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niseme tu zipo tafsiri ambazo zimekuwa ni potofu sana sisi tunasema tunahitaji Tume huru ya uchaguzi wako watu wengine wanafikiri tunavyohitaji tume huru ya uchaguzi tunahitaji kushinda uchaguzi. Sisi hata tungekuwa na tume ambayo si huru tutashinda uchaguzi tu lakini ukweli tunahitaji tume huru ya uchaguzi kwa sababu ya amani ya nchi yetu kwa sababu tunajua kabisa kwamba kama kutakuwa na tume huru ya uchaguzi kutakuwa na uwazi na kila mmoja.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, taarifa

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, atajua kabisa kwamba kura yake aliyopiga

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, na atakayeshinda ameshinda sawasawa…

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Kuchauka.

T A A R I F A

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, nilindie muda wanachosha tu hawa

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, nataka nimpe taarifa mzungumzaji Wabunge wote humu ndani tumeapa kwa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Tume huru imetajwa kwenye katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba patakuwepo na katiba na patakuwepo na Tume ya Uchaguzi ambayo itakuwa huru haitaingiliwa na chombo chochote sasa hiyo tume ambayo yeye anaisema kwamba anaidai anataka itajwe vipi kwenye katiba ambayo yeye ataiona kwamba hii tume ni huru.

SPIKA: Taarifa hiyo unapewa Mheshimiwa Mwakajoka.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, unajua hawa ambao sio CCM halisi hawa wana matatizo makubwa sana wanahitaji uhalali wakati CCM halisi wamekaa wanajua nini nachokizungumza tulia kwanza.

Mheshimiwa Spika, tunahitaji tume huru nia na madhumuni ni kuhakikisha kwamba tunafanya uchaguzi ulio huru na haki na tunahitaji watanzania waweze kuona kwamba ndani ya chumba cha uchaguzi yale matokeo yanayotangazwa ni matokeo ambayo yako sahihi na wanaamini kwamba yametangazwa na aliyeshinda ameshinda uchaguzi, tunahitaji tume ya namna hiyo.

Mheshimiwa Spika, sisi hatuna wasiwasi na uchaguzi unaokuja tumejiandaa kushinda kwa asilimia 100 kabisa na safari hii tumesema hatutawaacha ni lazima kwa kweli mng’oke na muhakikishe kwamba mnang’oka kwa sababu zilizo sahihi kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nina sababu nyingi sana za kuzungumza kwa nini mtang’oka nataka sasa nianze kuchangia mchango wangu kwenye utakelezaji wa bajeti ya mwaka 2019/2020 na uone ni sababu tunasema mtang’oka kwenye uchaguzi unaokuja kwa sababu hamjafanya vizuri.

Mheshimiwa Spika, nakumbuka vipaumbele ambavyo mmeviweka kwenye mpango wa bajeti wa mwaka 2020/2021 mmeweka reli standard gauge, mmeweka Stiegler’s Gorge, mmeweka ununuzi wa ndege na mmeweka bomba la mafuta.

Mheshimiwa Spika, asilimia 75 mpaka asilimia 80 ya watanzania ni wakulima na wafugaji cha kushangaza ni kwamba Serikali ya Chama Cha Mapinduzi ambayo iliapa kwamba itakuwa ni Serikali ya wanyonge huwezi kuamini kilimo hawaoni kama ni kipaumbele kabisa. Hawaoni ni kipaumbele kwa sababu wanazungumza kwa maneno lakini vitendo hawawezi kutekeleza.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukisoma Ilani ya Chama cha Mapinduzi, walisema kwamba ndani ya miaka mitano watahakikisha kwamba kilimo kinakua kwa asilimia nane, lakini huwezi kuamini kilimo kimekua kwa chini ya asilimia tatu kila mwaka. Yale ambayo waliyazungumza kwa wananchi wakati wanaomba kura hawajatekeleza hata jambo moja.

Mheshimiwa Spika, nataka nitoe sababu za msingi; angalia Bajeti ya mwaka 2016/2017, tulitenga bilioni 101 wakatoa bilioni tatu peke yake kwenda kwenye kilimo, lakini mwaka 2017/2018 tulitenga bilioni 150 wakatoa bilioni 16 peke yake wakapeleka kwenye kilimo. Mwaka 2018/2019 tulitenga bilioni 95 mkatoa bilioni 42 peke yake.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia miaka yote ambayo tumekwenda kutenga bajeti hizi utaona kabisa kwamba utekelezaji wake miaka yote minne mmetekeleza kwa asilimia 17.55, miaka yote minne. Huu ni utani mkubwa sana kwa Watanzania. Nataka niseme, kama kweli wanataka kuondoa umaskini wa Watanzania ni lazima kuwekeza kwenye kilimo.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ukiangalia ukurasa wa 43 anasema Serikali imejikita kuhakikisha kwamba inainua kilimo na kuhakikisha kwamba umaskini unaondoka kwa Watanzania. Sasa kwa uwekezaji wa asilimia hizi ambazo zinawekezwa kwenye kilimo tusitegemee kabisa kwamba tunaweza tukawakomboa Watanzania na tukaondoa umaskini huu. Tunawatania Watanzania.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninachotaka kusema tu; kwa mwaka huu peke yake…

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Frank, pokea taarifa; Mheshimiwa Waziri wa Nchi.

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Atulie kwanza.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika,
naomba tu nimpe taarifa Mheshimiwa Frank; anapofanya uchambuzi wa bajeti na kuangalia bajeti ya kilimo, asijikite kwenye Wizara ya Kilimo peke yake. Bajeti ya kilimo ni bajeti mtambuka. Ukija kwenye Vote ya Waziri Mkuu tunao Mradi wa MIVARF na wenyewe unaji-address kwenye Sekta ya Kilimo, uongezaji thamani ya mazao, miundombinu ya masoko, lakini kutengeneza mfumo mzuri wa kilimo kwa wakulima mbalimbali. Kwa mfano mradi huo umefanyika kwa pande zote mbili; Bara na Visiwani. Ukienda TAMISEMI wanayo vote pia ambayo ina-deal na masuala ya kilimo kwa hiyo bajeti ya kilimo ni ya kisekta. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa namwomba anapofanya uchambuzi wa bajeti ya kilimo asi-concentrate tu na Wizara ya Kilimo, aende na kwenye sekta nyingine za kiwizara ambazo zina-support pia Sekta hiyo ya Kilimo na ndiyo atapata majibu sahihi ya Wizara ya Kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia naomba nimthibitishie kabisa kwamba Serikali ya Dkt. John Pombe Magufuli ni Serikali ya wanyonge, hayo ya kilimo ni machache tu lakini yapo mengine mengi ambayo yamekwisha kufanyika na mifano halisi imeelezwa kwenye hotuba ya Waziri Mkuu. Tumeshajenga zahanati, vituo vya afya, hospitali, kwa hiyo kwa vyote hivyo unaona kabisa ni Serikali ambayo inawajali wanyonge.

SPIKA: Nakufafanulia Mheshimiwa Mwakajoka, muda wako unatunzwa usiwe na wasiwasi; alichokuwa anasema

Mheshimiwa Waziri ni kwamba ukitaka kuichambua bajeti ya kilimo lazima uiangalie kwa mapana, sio narrowly, kwamba ukiwekeza katika Mradi wa Stiegler’s Gorge ule wa Mwalimu Nyerere wa kuzalisha umeme, umeme ule utaenda kwenye viwanda ambavyo navyo ni katika mnyororo wa kuboresha products za kilimo. Ukijenga reli itasafirisha na mazao ya kilimo; ukichonga barabara ukaweka lami kuelekea kila mahali ndiyo unafungua kilimo huko; maana yake ni hiyo. Kitazame kilimo katika upana wake huo. Ndiyo ujumbe tu anakupa huo. Unapokea utaratibu huo?

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, nafikiri Mheshimiwa Mhagama angekuwa anatuambia kwanza hicho anachokizungumza ni asilimia ngapi. Sisi tunapitia randama za Kamati, tunaangalia utekelezaji na ndiyo maana tunachangia hapa, sasa Mheshimiwa akianza kutuambia kuna hela nyingine zimejificha, alipaswa kuziweka wazi. Vile vile akumbuke kabisa kwamba hizo fedha anazozizungumza ukienda kuangalia barabara vijijini ambako sasa tunafikiria wakulima wetu waweze kutoa mazao, barabara ni mbovu, hata mazao hayawezi kusafirishwa sasa hivi. Kwa hiyo anakokuzungumza huko fedha kwa kweli hazijaenda ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, tukumbuke Mkataba wa Maputo kwenye Nchi za Afrika, walishauri kwamba hizi nchi ili ziweze kuondoa umaskini katika nchi zao ni lazima wawekeze asilimia kumi ya bajeti zao kila mwaka ili kuhakikisha kwamba wananchi wao sasa wanalima vizuri, lakini pia wanapata masoko mazuri na baadaye wanaondokana na umasikini, lakini Serikali yetu haijawahi kufikia bajeti hiyo hata siku moja, mpaka tunavyozungumza leo.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Taarifa Mheshimiwa Mwakajoka; Mheshimiwa Waziri wa Kilimo.

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Hasunga mbona unaharibu sasa?

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwanza namshukuru mdogo wangu kwa mchango wake anaoendelea kuutoa, lakini nataka nimwelimishe kidogo, labda pengine anaweza akawa hajaelewa vizuri; tunapozungumzia asilimia kumi ya kilimo hatuna maana hizo fedha zote lazima ziwe kwenye bajeti ya kilimo.

Kwa hiyo kwa mradi mkubwa kama huu kwa mfano wa ujenzi wa reli ya Standard Gauge maana yake tutasafirisha mazao. Kwa hiyo hela zote zilizoko kwenye uchukuzi zinakwenda kusaidia kilimo. Ukiangalia fedha zilizopo kwenye nishati zote zinasaidia kilimo.

Mheshimiwa Spika, lakini zaidi ya hapo, nataka nimpe taarifa kwamba sisi kama Wizara hatulimi, kazi yetu ni kutengeneza miundombinu na kutengeneza sera za kilimo. Utekelezaji wa bajeti ya kilimo unafanywa kwa kiwango kikubwa na Sekta Binafsi. Kwa hiyo ukitaka kujua kwamba ni kiasi gani kimewekezwa kwenye kilimo maana yake tujue Sekta Binafsi imewekeza kwa kiasi gani.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka kumjulisha tu mdogo wangu kwamba uchambuzi wa bajeti kama ulivyokuwa umempa anatakiwa achambue kwa undani; ni zaidi ya asilimia 7.5 sasa hivi tumefikia na Tanzania ni nchi ya tatu katika Nchi za Afrika katika kutenga kiasi kikubwa cha fedha kwenda kwenye Sekta ya Kilimo, ukiangalia katika upana wake kwa kuziangalia sekta zote ambazo zimetenga bajeti.

Mheshimiwa Spika, nilitaka kumpa taarifa hiyo.

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, mimi nasema hivi; Serikali ilitenga bajeti ikaja Bungeni tukaipitisha Bungeni hapa. Hizi bajeti ninazozitaja mimi ni bajeti ambazo zimepitishwa ndani ya Bunge zikatekeleze shughuli za maendeleo kwenye Wizara ya Kilimo. Bajeti hizi hazijafanya kazi yoyote, ziko chini ya kiwango. Kuna moja imetekelezwa 2016/2017 kwa asilimia tatu; 2017/2018 kwa asilimia 11; 2018/ 2019 kwa asilimia 16 na 2019/2020 asilimia 15.

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Taarifa iko wapi?

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, tunazunguka nini badala ya kuzungumza uhalisia…

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka kuna taarifa, ipokee.

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Spika, namheshimu sana mzungumzaji, Mheshimiwa Mbunge Mwakajoka, lakini nataka nimpe taarifa. Anaonekana anapambana sana kwa kile anachodai kwamba Chama cha Mapinduzi kinakwenda kuondoka 2020.

Mheshimiwa Spika, nimwambie Chama cha Mapinduzi hakiwezi kuondoka kwa takwimu hizo, lakini Chama cha Mapinduzi wamehama mbele hapa, akina Mwakajoka wamekwenda kukaa nyuma kabisa kule, mbele wamewaacha akinamama hawa akinamama mnaowaachia chama hapa mbele peke yao hawawezi kukiondoa Chama cha Mapinduzi madarakani hawa akinamama. Akina Mwakajoka sogeeni mbele hapa maana yake chama kimeachiwa akina mama peke yao…

MHE. ESTHER N. MATIKO: Kuhusu Utaratibu.

MHE. MAULID S. A. MTULIA: …mchanganyike, peke yenu chama hakiwezi kwenda.

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, unamwachia anaropokaropoka huyo.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, kuhusu utaratibu.

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka, Kaimu Kiongozi wa Upinzani amesimama, subiri kidogo; Mheshimiwa Halima nimekuona. (Kicheko)

KUHUSU UTARATIBU

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, kuhusu utaratibu; najua Kanuni zetu za Bunge zinakataza kutumia lugha za kuudhi, lugha za dharau, lugha za kibaguzi, lugha za kudhalilisha. Sasa nakuomba, kwa sababu tunakuheshimu kama Kiongozi wa Mhimili, kuna maeneo unaweza ukatania, halafu kuna maeneo mengine yanakera na yanachefua.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba umtake Mbunge wa Kinondoni aliyetangazwa kwa utaratibu anaoujua yeye, afute kauli yake.

SPIKA: Aliyefanyaje? (Kicheko)

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa, tulieni basi… Mheshimiwa Spika, naomba mtulie…

Mheshimiwa Spika, naomba umtake Mbunge wa Kinondoni afute kauli yake aliyoisema kwamba CHADEMA kwa kuwa hapa viti vya mbele kuna wanawake kwa hiyo hakina uwezo wa kushinda uchaguzi. Kwa hiyo anatuambia Mama Samia Suluhu, Makamu wa Rais wa Nchi hii, anatuambia Mheshimiwa Jenista Mhagama, Mnadhimu wa Kambi ambaye yuko kiti cha mbele hana uwezo wa kukisaidia chama chake kushinda uchaguzi. Naomba umtake afute kauli yake. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana Kaimu Kiongozi wa Upinzani.

Kama nimemsikia vizuri, tusubiriane kidogo, kama nimemsikia vizuri Mheshimiwa, amesema akina Mwakajoka mmerudi nyuma, mmeacha front bench yote akinamama watupu na kweli nikitazama naona akinamama watano wako mbele wao peke yao, akina Mwakajoka wamerudi nyuma, sasa ndiyo alikuwa anazungumzia hicho tu.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

SPIKA: Mheshimiwa Mbunge wa Kinondoni, weka sawa bwana ili tuweze kuendelea. (Kicheko)

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

SPIKA: Eeh, weka sawa tu bwana tuendelee.

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Naamini umenielewa vizuri kwelikweli kwa sababu mimi ninachojua chama cha watu wote na sio wakati wa mapambano wanaume wanarudi nyuma. Nilichotaka wanaume wasiwe wakati wa mapambano wanakimbia wanarudi nyuma, wanawaacha akinamama peke yao, sikusema kwa nia mbaya, nimesema kuwataka rafiki zangu akina Mheshimiwa Mwakajoka waje mbele washikane mkono kwa mkono, bega kwa bega pamoja washirikiane, isiwe wakati wa mapambano wanaanza kurudi nyuma taratibu mwisho watatoka kabisa. Ndiyo hicho tu nilichokisema, sikuwa na lengo la kubagua akinamama wala nini, nilikuwa nahimiza akinababa nao washirikiane na akinamama kuwa-support, sikusema kwa nia mbaya.

SPIKA: Ahsante. Amerekebisha jamani, amesema anataka bega kwa bega.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka, endelea, dakika zako karibu zinaisha, weka sawa.

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba unajua wanasema kwamba unapokuwa kiongozi ni vizuri sana ukawa na hekima. Sasa nina wasiwasi sana na Mbunge wa Kinondoni na inawezekana huyu Mbunge ndiyo maana alikimbia majukumu akatangazwa kwa njia anazojua yeye. Kwa sababu maneno haya sio ya mara moja, ni mara ya tatu sasa.

SPIKA: Sasa hapo na wewe unaharibu. Katoa wito tu kwamba uje mbele na wewe. Basi, hakusema zaidi ya hilo; endelea na hotuba yako ili umalize muda umeisha.

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ngoja niendelee tu kusema kwamba, hiki ambacho nilikuwa nakizungumza humu ndani ya Bunge ni utekelezaji hafifu kabisa wa bajeti uliofanyika na Serikali ya Awamu ya Tano kwenye kilimo; hilo lieleweke hivyo.

MHE. MWIGULU L. N. MADELU: Taarifa.

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, lakini lingine, wakati huo kila mmoja…

SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka, kuna taarifa; Mheshimiwa Mwigulu.

MHE. MWIGULU L. N. MADELU: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mwakajoka ameendelea kusemea kwamba utekelezaji ni hafifu na anafanya reference ya Azimio la Maputo. Nataka nimwekee kumbukumbu sawa kwamba Wakuu wa Nchi walipokutana Maputo, asilimia kumi walizokuwa wanazisemea, aende akalisome lile Azimio, zinaongelea kilimo kwa maana ya agriculture, forestryand fisheries. Ukichukua hizo components za agriculture in the broad sense ya kilimo, misitu na mifugo, sisi hapa Tanzania tulishavuka hiyo asilimia kumi na hiki anachokifanya Mheshimiwa Rais na kama alivyosema Mheshimiwa Jenista, ukienda mpaka ngazi ya halmashauri tumeshavuka muda mrefu mno na tunaelekea kwingine kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wenzetu hawa wasiwe na hii temperate ya uchaguzi, kwa haya mambo ambayo Serikali ya Awamu ya Tano imeshafanya hata ile kusoma namba, sasa hivi hata number plate hamtaiona kwa sababu gari ya Dkt. Magufuli itakuwa mbali mno. Kwa maana hiyo hebu twendeni kwenye facts zilizopo kwenye data na tusiweke blah blah zingine hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilitaka nimpe tu taarifa hiyo ili asiendelee kutumia vibaya muda wake.

SPIKA: Kabla sijairudisha mic kwa Mheshimiwa Mwakajoka ninayo mapendekezo kutoka kwa baadhi ya Wabunge. Wanasema kwa kuwa inaelekea uchaguzi ujao huenda hata Mbunge mmoja wa Upinzani asipatikane, patengwe viti maalum, tutengeneze utaratibu fulani maalum tuuandike kwenye Katiba pale ili tuweke hata viti kumi hivi kwamba hivi sasa tuwape bure, maana sasa kuna hatari kwamba itakuwa hakuna hata mmoja. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Mwakajoka, malizia bwana. (Kicheko)

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, kwanza sipokei taarifa ya Mheshimiwa Mwigulu kwa sababu naye ana stress sana, Kitila Mkumbo yuko anampumulia mgongoni. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa tu kingine ambacho nataka nimwambie ni kwamba Mheshimiwa amezungumza kuhusiana na ujumla wake kwenye bajeti ya kilimo, akiangalia kwenye mambo ya uvuvi ni miaka yote minne fedha hazijakwenda kabisa kwenye uvuvi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Ilani ya Chama cha Mapinduzi pia mliahidi meli tano ndani ya miaka mitano lakini mpaka leo meli ya uvuvi kwenye Bahari ya Hindi haijanunuliwa hata moja. Kwa hiyo yote anayozungumza tunajua nini tunachokizungumza ndani ya Bunge hili. Kwa hiyo kwa kweli utekelezaji ni hafifu sana.

Mheshimiwa Spika, niende kwenye afya; Mheshimiwa Waziri Mkuu kwenye ukurasa wa 26 ameonesha bilioni 256 zimetengwa badala ya bilioni 300 ambazo zilikuwa zinatengwa kipindi cha awamu ya nne lakini anasema utekelezai ni mzuri. Ukweli tu ni kwamba fedha iliyotengwa kwa mwaka huu ni bilioni 544, ndiyo iliyotengwa kwenye bajeti, lakini fedha iliyopelekwa sasa hivi ni bilioni 83 peke yake ambayo ni sawa na aslimia karibu 13. Sasa ukiangalia unaona kabisa fedha zinatengwa lakini haziendi na Serikali hii inasema inakusanya. Juzi Waziri wa Fedha wamesema TRA kwamba wamekusanya 1.7 lakini hatuoni, utekelezaji wa bajeti umekuwa chini ya kiwango kabisa. Sasa nashangaa kama kweli wana uhakika wa kurudi mwaka 2020 kwenye uchaguzi unaokuja.

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika,taarifa.

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: …mliowaona mwaka 2015 sio… niwaambie tu ni kwamba…

SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Mwakajoka, nakushukuru sana kwa mchango wako; muda umeisha Mheshimiwa Goodluck Mlinga..
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwakawa Fedha 2018/2018 – Wizara ya Kilimo
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na mimi kwa kupata nafasi hii niweze kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli kilichotokea kwenye nchi hii na kinachoendelea yako mambo ya ajabu sana, wakati Serikali hii ya Awamu ya Tano imeingia madarakani ilisema kwamba ni Serikali ya wanyonge, lakini huwezi kuamini kinachotokea, bajeti zinatengwa kila mwaka lakini utekelezaji wake haujawahi kuzidi asilimia 20. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka uliopita 2016/2017 ilitengwa bilioni mia moja na moja lakini fedha iliyokwenda kufanya shughuli za maendeleo ilipelekwa bilioni tatu. Mwaka 2017/2018 imetengwa bilioni 150 lakini fedha iliyokwenda kutekeleza majukumu ya maendeleo kwenye kilimo ni shilingi bilioni ishirini na saba ambayo ni sawa na asilimia 18.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaposema kwamba hii ni Serikali ya wanyonge huu ni uhuni kwa Watanzania, Watanzania wanasikitika kupita kiasi, wanaona kama wamepata mkosi kwa sababu ya Serikali hii. Haiwezekani kabisa hii Serikali siyo Serikali ya wanyonge imekuwa ni Serikali ya watu asilimia tano wenye kipato cha chini na kipatao cha juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii asilimia tano ya Watanzania ambao wanauwezo wa kupanda ndege ndiyo ambao wamepewa kipaumbele katika nchi hii, leo hawa watu ambao wa wana uwezo wa kupanda ndege katika Taifa hili wanaendelea kununuliwa ndege.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zimenunuliwa ndege tano kwa mkupuo na juzi wanasema wameongeza ndege ya sita kwa ajili ya kuhakikisha kwamba watu asilimia tano ambao wako katika Taifa hili wenye uwezo wa kununua magari, wenye uwezo wa kufanya kazi, wenye uwezo wa kujenga nyumba nzuri, lakini wale watu maskini wote wamesahauliwa kabisa. Jambo hili linasikitisha sana. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. FRANK J. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nimjibu kwamba taarifa yake siipokei kwa sababu hata fedha za afya ambazo zinakuja kwenye bajeti yetu ni fedha ambazo zinatoka nje. Fedha za ndani hakuna fedha yoyote inayokwenda kwenye Wizara ya Afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaomba Mawaziri wakae watulie, kazi yetu sisi kama Wabunge ni kuishauri Serikali. Sisi hapa hatugombani na Serikali bali tunaishauri iweze kufanya kazi vizuri lakini watu wanaomba taarifa ambazo hazitaweza kuisaidia nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema ni kwamba Serikali hii haijajipanga kuhakikisha kwamba maisha ya Watanzania yanakuwa bora. Watanzania asilimia 80 ambao ni maskini ambao ni wakulima na wafugaji wamesahaulika kabisa katika Serikali hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado naendelea kusisitiza Serikali hii ni Serikali ambayo imekuwa tofauti kabisa na Serikali zilizopita, ni Serikali ambayo haiwajali wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka kipindi cha Mheshimiwa Mkapa wakulima waliweza kuenziwa sana, walipelekewa pembejeo na walilima. Kipindi cha Mheshimiwa Jakaya Kikwete tumeona hali halisi ilivyokuwa kwenye bajeti ambazo zinaonekana kwenye taarifa za fedha mbalimbali kwa miaka ya nyuma lakini Serikali hii imekuwa Serikali ya vitu na siyo Serikali ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawa tunakoelekea watakwenda kuwauliza mwaka 2020 na kama mnafikiri wananchi wa miaka ya nyuma ndiyo wananchi wa sasa hivi, hawa wananchi wanaona na wanasikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna mawakala wetu walioweza kusambaza mbolea miaka iliyopita leo mnasema mnafanya uhakiki wa mawakala wetu kwamba wamedanganya, hivi mawakala wote nchi nzima ni wezi? Kwa nini tunaendelea kuishauri Serikali kwamba iendelee kuwaamini Watanzania, iendelee kuwaamini wananchi wake hamtaki kuelewa jambo hilo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda bado kwa sababu nimeibiwa muda. Nataka kusema mawakala wetu wapatiwe fedha zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine tumepata taarifa kwamba wanataka kutuletea mbolea ya Minjingu. Mbolea ya Minjingu kwenye Nyanda za Juu Kusini ni mbolea ambayo haikubaliki kabisa, imeshindikana. Tuliwahi kutumia mbolea hii lakini tulipata hasara kubwa. Tunaomba mbolea hii…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali Wizara ya Maji na Umwagiliaji 2018/2019
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii ili na mimi niweze kuchangia kwenye bajeti ya Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba hali iliyopo sasa hivi kwenye nchi hii ni lazima tufike mahali Wabunge tukubaliane, kila mmoja anasema hapa kwamba hali ni mbaya sana katika jimbo lake, lakini wako watu wanapongeza baadae wanaanza kulalamika kwamba hali ni mbaya. Hiki kitu ndiyo kinachotuchelewesha sana kuleta maendeleo kwa sababu tunazungumza jambo ambalo hatuna uhakika nalo huku tukijua kwamba hali ni mbaya sana katika majimbo yetu.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2016/2017 kwenye bajeti iliyopita kulikuwa na mradi mkubwa ambao ulitaka kutekelezwa kwenye Mji wa Tunduma na kampuni kutoka Ubelgiji. Mradi huu ulikuwa na thamani ya Euro milioni 100. Mradi huu umeyeyuka na sasa hivi hata kwenye vitabu hivi vya Waziri huwezi kuuona mradi huo. Ukiangalia kwenye Mji wa Tunduma ambao uko mpakani mwa nchi nyingi ambazo zinapitia pale karibu nchi nane hakuna maji kabisa. Wananchi wangu ambao wamewekeza kwenye Mji wa Tunduma leo hii wanakosa maji, wageni wanaokuja kutembelea kwenye Mji wa Tunduma na kuingia kwenye nchi sasa wanalala Zambia. Kwa hiyo, tunakosa mapato na Serikali inakosa mapato kwa sababu hoteli nyingi pia zimeanza kufungwa kwenye Mji wetu wa Tunduma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nikuambie tu kwamba mimi wananchi wangu wameathirika sana, sasa hivi pale kwenye Mji wetu wa Tunduma na Wilaya nzima ya Mbozi pamoja na Momba tuna tatizo kubwa la typhoid kwa sababu ya kukosa maji. Watu wengi wanapoteza maisha kwa sababu ya kupata maji ambayo si safi na salama. Mimi jambo hili kwa kweli sitakubaliana nalo kabisa na nataka niseme Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi wafike mahali waelewe kwamba kipaumbele kikubwa ni kuhakikisha kwamba afya za Watanzania zinakuwa bora ili waweze kuzalisha na waishi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nchi hii ukizunguka maeneo yote kwenye Taifa hili, tumejaribu kuzunguka kila maeneo tukiwa na ziara ya Kamati ya Nishati na Madini wanafikiri sisi ni Kamati ya Maji, kila mtu anasema jamani maji huku hatuna. Nchi nzima hakuna maji, hali ni mbaya sana katika Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi Tunduma pale nahitaji miradi mikubwa ya maji. Juzi kulikuwa na miradi imekuja midogo sana ambayo haiwezi kutosheleza wakazi wa Mji wa Tunduma, tunahitaji maji ya kutosha kwenye Mji wa Tunduma ili wananchi wangu waweze kupona magonjwa ambayo wanaendelea kupambana nayo ya typhoid kwenye mji wetu. Tumepoteza watu wengi mno kwa sababu ya uzembe wa Serikali kuendelea kutokutoa fedha kwenye Wizara ya Maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, watu wengi sana wanawaangalia vibaya Waheshimiwa Mawaziri lakini ukweli ni kwamba Mawaziri hawa wafanye nini? Ukiangalia miaka mitatu kuanzia mwaka 2015/2016, 2016/2017, 2017/2018 huwezi kuamini utekelezaji wa bajeti ya maji ni asilimia 26 tu kwa miaka yote mitatu ukichukua uwiano. Kweli tunaweza tukasema kwamba Serikali ya Chama cha Mapinduzi ina lengo la kupunguza tatizo la maji kwa wananchi wa Tanzania kama kweli inatekeleza kwa asilimia 26 ndani ya miaka mitatu uwiano tumejaribu kuangalia. Wananchi wa Tanzania wameiamini Serikali hii na mkapigiwa kura halafu baadae mmeanza kuwababaisha wananchi wa Tanzania. Tunataka maji kwenye Taifa hili, tunataka kuondoa matizo kwenye Taifa hili yanayotokana na maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo hii wameweka bajeti ya maji kidogo na utekelezaji wake kama tulivyozungumza lakini huwezi kuamini leo tunakwenda kununua ndege, tena juzi tumenunua ndege sita na juzi Mheshimiwa Rais anasema anaongeza ndege ya saba eti wanakwenda kuchukua tena cash hakuna kukopa. Hivi wananchi wa Tanzania asilimia tano wanaopanda ndege ndiyo waliomchagua Mheshimiwa Rais? Hivi asilimia tano wanaopanda ndege ndiyo waliowachagua Wabunge wa Chama cha Mapinduzi ambao ni wengi ndani ya Bunge hili wanashindwa kuona

huruma kwa wananchi wa Tanzania ili kuhakikisha kwamba wananchi wa Tanzania wanapata maji, afya nzuri na wanapunguza vifo ambavyo vinatokana na magonjwa ya maji? Mimi sikubaliani hata kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia kuna mambo ya msingi, tulisema tunahitaji tuwe na kilimo cha umwagiliaji ili tuwe na kilimo bora ambacho kitakuwa kinazalisha chakula kwa muda wote. Huwezi kuamini mwaka 2016/2017 tulitenga bajeti ya shilingi bilioni 25 fedha iliyokwenda ni shilingi bilioni
1.2 peke yake. Mwaka 2017/2018 tumetenga shilingi bilioni 24 lakini fedha iliyokwenda ni shilingi bilioni mbili peke yake, tunafanya nini katika Taifa hili.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Jambo la kwanza kabisa, napenda niseme tu kwamba naunga mkono hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili Taifa haliwezi kujengwa na kundi moja, Taifa hili litajengwa na Watanzania wote. Hotuba ambayo leo tumeisoma hapo, naomba sana Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango ajaribu kuitumia, italisaidia Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila mwaka tumekuwa tuna- table hotuba zetu lakini kila mwaka tunashauri ni namna gani Serikali yetu ihakikishe kwamba inachukua ushauri na baadaye inatekeleza ushauri huo lakini kila wakati ushauri huu hamuufanyii kazi. Nasi hatuchoki kwa sababu tuko kwenye nchi hii na hatuna nyingine ya kuishi, mngekuwa peke yenu kwenye nchi hii tungewaachia mwendelee na matatizo yenu lakini kwa sababu Taifa hili ni letu wote, tutaendelea kushauri mpaka kipindi ambacho mtakuja kuelewa na mkaamini kwamba tunahitaji kujenga Taifa hili tukiwa wamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuzungumzia sana kuhusiana na mpango ambao umeletwa siku ya leo. Ukweli tu ni kwamba shughuli ambazo zinafanyika katika nchi hii, tumeona kabisa badala ya kuhakikisha kwamba tunapeleka maendeleo kwa wananchi lakini tunaona maendeleo haya yanakuwa kwenye vitu badala ya wananchi. Hili ni tatizo kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumzia kuhusiana na hali halisi ya uchumi wa nchi hii. Hebu tuangalie, katika Taifa hili tunasema Serikali inataka kuondoa umasikini. Unaondoaje umaskini wa Watanzania kama hakuna namna yoyote ya kupeleka fedha katika maeneo ambayo wananchi wengi wanapatikana? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, nichukulie kwenye suala la kilimo, uvuvi na mifugo karibu 65% ya Watanzania wako kule lakini huwezi kuamini fedha za maendeleo hazipelekwi kule. Mpango unaletwa hapa lakini inaonesha siyo kipaumbele cha nchi. Sasa tunataka kujua ni namna gani Serikali hii ambayo mnasema ni ya Awamu ya Tano, maana mimi najua ni Serikali ya CCM ile ile, lakini nyie mnajipambanua kwamba Serikali ya Awamu ya Tano, huu ni uwongo mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016/2017 tulitenga bajeti kwenye kilimo shilingi bilioni 101 lakini fedha ambayo ilikwenda kutekeleza shughuli za kilimo kule ilipelekwa shilingi bilioni 3 peke yake. Hapa tunasema kwamba tunakwenda kupunguza umaskini wa Watanzania, unapunguzaje umasikini wa Watanzania wakati kinachoonekana ni kwamba mnatekeleza uchumi wa vitu na siyo uchumi wa watu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo hili limekuwa ni sugu. Ukienda kwenye upande wa mifugo, tulitenga shilingi bilioni 4 lakini mpaka sasa hivi fedha ambayo ilipelekwa kwenye mifugo ilikuwa karibu shilingi bilioni 3 peke yake. Tunaona kabisa ni jinsi gani ambavyo Serikali haijajipanga kumaliza umasikini wa Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine katika nchi hii tatizo kubwa lililopo ni mazingira mabaya ya biashara. Kwa kweli katika nchi yetu kumekuwa na tatizo kubwa sana la mazingira magumu ya kufanyia biashara. Tusipoliangalia jambo hili, tutaendelea kutwanga maji kwenye kinu. Sasa hivi tunasema kwamba wawekezaji waje katika nchi hii itakuwa ni jambo gumu, kwa sababu hata wawekezaji waliopo Tanzania ambao ni wazawa wameshindwa kufanya biashara zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unaona biashara inafungwa...

K U H U S U U T A R A T I B U . . .

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hajui kanuni, ngoja niendelee tu, nitamsamehe hivyo hivyo, kwa sababu ameamua kusimama tu na yeye auze sura kidogo. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukweli tu ni kwamba mazingira ya kufanya biashara ambayo yapo katika nchi hii ni tata sana. Lazima tukubaliane, tusipoweza kuondoa kero ambazo zinawahusu wafanyabiashara katika Taifa hili, tujue kabisa tunakoelekea Taifa hili linakwenda kuzama na tutaendelea kusema tu kwamba Taifa linaenda vizuri lakini ukweli ni kwamba mazingira ni magumu, hata wafanyabiashara wa ndani wanashindwa kufanya biashara, biashara zinafungwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka uliopita tulimwambia Mheshimiwa Dkt. Mpango atupe sababu ni kwa nini biashara katika nchi hii zinafungwa? Alichokisema Mheshimiwa Dkt. Mpango ni kwamba wafanyabiashara wengi wanakwepa kodi. Hiyo siyo kweli. Wafanyabiashara wanalipa kodi lakini mazingira yamekuwa magumu, hata taarifa za Kimataifa zinaonesha kabisa kwamba tuko kwenye nafasi mbaya sana. Nchi hii katika mazingira bora ya biashara tunashika nafasi ya 167 kwamba mazingira ni magumu. Kwa hiyo, tunaomba tunaposhauri jambo hili tuwe tunaeleweka tunashauri kwa sababu ya maslahi ya nchi hii. Hatushauri kwa sababu tu tunataka kuzungumza ndani ya Bunge hili. Naomba hilo jambo lieleweke vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na sekta binafsi hazishirikishwi ipasavyo katika Taifa hili. Kumekuwa na tatizo kubwa sana. Serikali hii inaonekana inafanya kazi kama vile ni Serikali ya ujamaa na ukisoma mpango hapa unasema sekta binafsi inashirikishwa lakini ukweli ni kwamba sekta binafsi haishirikishwi kabisa katika kupanga maendeleo ya nchi hii na kuhakikisha kwamba Taifa hili linasonga mbele. Kwa hiyo, naomba sana haya mambo yote yajaribu kutazamwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, leo tumepata taarifa kwamba wale wadau wa korosho ambao walikuwa wananunua korosho wameamua kuachana na korosho zetu na sasa hivi hawatanunua tena korosho. Kwa sababu Mheshimiwa Rais alisema kwamba Serikali itanunua, tunaomba kesho ikiwezekana tupate taarifa kwamba Serikali sasa inapeleka fedha na kuanza kupima hizo korosho za wakulima ili wakulima hawa waendelee kuuza korosho zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasikia tena yule mtu ambaye alinunua tani 500, anasema alikosea tu sifuri ile, lakini ukweli tu alikuwa ameamua kununua tani 50 ambazo alikuwa ameshalipia kipindi kile. Kwa hiyo, tunaomba Serikali pia ijiandae kununua hizi korosho kama ambavyo imewaahidi wananchi wa Mtwara na Lindi kuhakikisha kwamba korosho zao zinanunuliwa na wanapata hizo fedha kwa ajili ya kujiandaa na kilimo katika msimu unaokuja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kulizungumza ni kuhusiana na sekta binafsi ambavyo inashirikishwa katika Taifa hili. Ukiangalia kwenye mikopo ya Serikali, mkopo wa ndani mpaka sasa hivi umefikia karibu shilingi trilioni 5. Hizi fedha ambazo zinaoneshwa kwenye mkopo wa soko la ndani ni kwamba kama Serikali inaendelea kukopa kwenye sekta za fedha za ndani, tafsiri yake ni kwamba inaendelea kuhakikisha kwamba mabenki yanashindwa kukopesha wafanyabiashara wadogo wadogo ambao ni wajasiriamali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikopo hii ambayo Serikali inakopa kwenye soko la ndani badala yake tena imeshindwa kuziwezesha sekta binafsi ili ziweze kuhakikisha kwamba inatekeleza miradi yote ambayo Serikali inakuwa inakopea hizi fedha. Kinachoendelea ni kwamba tumeona makampuni makubwa ambayo yanatekeleza miradi mbalimbali katika nchi hii ni ya nje siyo makampuni ya ndani. Tunaomba Serikali hii ihakikishe kwamba inayawezesha makampuni ya ndani ili fedha ambazo zinazokopwa katika masoko ya ndani zihakikishe kwamba pia makampuni ya ndani yanatekeleza miradi mbalimbali ambayo inafanyika katika nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haiwezekani, tunaomba pia Serikali iweke sheria ikiwezekana makampuni ya ndani yashirikiane na makampuni ya nje ili percent kidogo ambayo inaweza ikapatikana kwa ajili ya kutekeleza miradi hii kwa wakandarasi wa nje, basi na wakandarasi wa ndani waweze kupata fedha hizo. Kwa hiyo, tunaomba jambo hilo lifanyike kama ambavyo tunashauri.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia. Napenda nizungumzie sana kuhusiana na suala la kilimo hasa kilimo cha mazao ya chakula. Najua kabisa kwamba Watanzania wote wanajua kwamba mchango wa kilimo kwenye pato la Taifa ni mkubwa na mazao haya yanategemewa sana na Watanzania wote na hata leo tuko humu ndani ya Bunge tunaonekana tuko vizuri na tunachangia ni kwa sababu tumepata chakula.

Mheshimiwa Spika, imeonekana kabisa kwamba Serikali haijatilia mkazo kabisa kuhakikisha kwamba inawasaidia wakulima hasa wakulima wa mazao ya chakula. Najua kabisa asilimia 65 ya Watanzania wanategemea kilimo, lakini huwezi kuamini pamoja na kilimo kuchangia asilimia 30 ya pato la Taifa, lakini uwekezaji kwenye kilimo umekuwa chini ya asilimia mbili. Kwa hiyo, ninachotaka kuzungumza ningeomba sana kwamba Serikali ijaribu kuangalia ni namna gani inaweza ikawekeza kwenye kilimo hasa kilimo cha nafaka.

Mheshimiwa Spika, imetokea sasa hivi kauli mbalimbali zimekuwa zikitolewa. Nakumbuka mwaka jana Mheshimiwa Rais amejaribu kuzungumzia akasema kwamba mazao ya chakula siyo biashara, lakini ukweli tu ni kwamba watu wamewekeza fedha nyingi sana, kuna watu wanavuna mpaka tani 80, wanavuna tani 200, wanavuna tani 300, kwa ajili ya mazao ya chakula lakini leo kuna kauli zinasema kwamba mazao ya chakula siyo biashara.

Mheshimiwa Spika, ukijaribu kuangalia kwenye upande wa pembejeo za kilimo mwaka jana wamesema kwamba wataagiza pembejeo kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wakulima waweze kupata pembejeo kwa bei ndogo, lakini ukweli tu ni kwamba katika mwaka ambao tumewahi kununua pembejeo kwa bei kubwa ni mwaka huu ambapo pembejeo zimepanda kwa asilimia zaidi ya 20 kwa kipindi hiki. Kwa kweli tunaomba Serikali ijaribu kuangalia ni namna gani inaweza ikaboresha pembejeo hizi ikaweka ruzuku kama zamani ilivyokuwa inafanya. Serikali ya Chama cha Mapinduzi katika miaka iliyokuwa imepita Mheshimiwa Kikwete na Mheshimiwa Mkapa walikuwa wameweka ruzuku kwenye pembejeo za kilimo, lakini sasa ruzuku imeondolewa na biashara inafanyika holela, Serikali inachokisema ni kwamba imeamua kusimamia pembejeo hizi kwa kuweka bei elekezi.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, bei elekezi imekuwa ni kiini macho, kwa sababu bei elekezi Serikali inasema lakini haijachukua tathmini ya kutosha kuangalia ni namna gani soko la pembejeo likipanda kwenye soko la dunia, haijaangalia mafuta yakipanda ni namna gani inaweza kuwasaidia wakulima hawa ili waweze kupata pembejeo kwa bei rahisi, kwa hiyo kumekuwa na tatizo kubwa sana. Kwa mfano mwaka jana walisema pembejeo za kilimo watu watanunua kwa mfano kama DAP walisema watanunua kwa Sh.58,000 lakini kutokana na bei za Soko la Dunia ilipanda mpaka kufika Sh.65,000 mpaka Sh.67,000, Urea pia ni hivyo hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunachoomba ni kwamba, Serikali iweze kurudisha mfumo wa ruzuku kwenye pembejeo za kilimo hasa kilimo cha nafaka ili kuhakikisha kwamba wananchi wote ambao wanalima mazao haya, waweze kupata ruzuku ili kuhakikisha kwamba mazao haya wanalima kwa urahisi lakini pia wanauza mazao yao kwa urahisi. Kama haitoshi imeonekana kwamba bei ya soko la mazao ya chakula sasa hivi imekuwa ni tatizo kubwa sana na hili tatizo siyo kwamba wakulima wamesababisha, Serikali ya Chama cha Mapinduzi ndiyo imesababisha tatizo hili la bei ya chakula kuwa chini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka 2017/2018, tulikuwa tumepata soko zuri kabisa Kenya, lakini Serikali ikazuia mipaka kwamba hakuna kuuza mazao nje na badala yake mazao hayakuuzwa nje, badala yake masoko haya yakahamia katika nchi zingine sasa hivi Wakenya wanakwenda kununua mahindi Zambia na Malawi, sisi tumekosa soko kwa sababu Serikali ilizuia mazao yasitoke. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini mwaka huu bado mwaka huu imetokea tatizo lingine...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

SPIKA: Muda hauko upande wako

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, dakika mbili na nusu hii.

SPIKA: Tayari dakika tano, muda unaenda haraka kweli, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahsantekwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia. Maji ni uhai na nitaanzia kwanza na bajeti ambayo tuliidhinisha kwaajili ya kuwapatia wananchi maji mwaka 2018/2019.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019, tulipitisha bajeti ya shilingi bilioni 672 kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wananchi wa Tanzania wanapata maji, lakini mpaka sasa fedha ambayo imekwenda kufanyakazi kuhakikisha kwamba wananchi wanapata maji, imetolewa shilingi bilioni 343.4.

Mheshimiwa Spika, tunajiuliza sana kama Wabunge kwa kazi ambayo tunaifanya ndani ya Bunge ya kupanga/ kutengeneza bajeti lakini pia kuhakikisha kwamba tunaidhinisha bajeti hii ili wananchi wetu waweze kupata maji, lakini cha kushangaza fedha haziendi kabisa kwenda kutekeleza shughuli za maji. Nataka nitoe mfano tu katika bajeti hii ya bilioni 672, kuna fedha karibuni shilingi bilioni 185, hizi fedha zilikuwa zinatokana na fedha za mchango wa wananchi kwenye mafuta ya petroli na dizeli, lakini pia kulikuwa na fedha karibuni shilingi bilioni 229.9, hii ni fedha ambayo ilikuwa inatoka kwa Washirika wa Maendeleo ambayo tulikuwa tunategemea zitaingia ili kuhakikisha kwamba zinatusaidia. Pia kulikuwa na ruzuku ya Serikali karibu shilingi bilioni 285 ambayo ilitakiwa pia kuchangia ili kutimiza hiyo fedha bilioni 672 kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Watanzania wanapata maji.

Mheshimiwa Spika, mpaka sasa hivi fedha iliyotoka ni kama nilivyosema ni bilioni 343 tu ndiyo iliyotoka. Sasa ni nusu ya bajeti yote ambayo tulikuwa tumeipitisha kwenye mwaka 2018/2019. Fedha hii ambayo tunaitenga kila wakati na tunaipitisha inakuwa ni ndogo na kila siku Wabunge tukiwepo humu tunalalamika kwamba fedha ni ndogo sana, iongezwe lakini cha kushangaza hata hii fedha ndogo ambayo inakuwa imeshapitishwa ndani ya Bunge, inashindwa kutolewa na Serikali ili kwenda kutekeleza miradi ya wananchi katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi chote hicho fedha ya mchango wa wananchi kwenye mafuta ya dizeli na petroli ambayo ilikuwa imetengwa shilingi bilioni 185, imetoka shilingi bilioni 155 imekwenda kutekeleza miradi ya maji. Pia fedha ya wafadhili, kati ya bilioni 229.9, fedha iliyotoka ni shilingi bilioni 188, ukizijumlisha fedha hizi inakupa hesabu ya shilingi bilioni 343.4. Tafsiri yake ni kwamba Serikali upande wa Hazina kama ruzuku ya Serikali bilioni 285 haijaonekana katika hesabu inayoonekana sasa hivi hapa.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nilikuwa napitia kitabu cha Mheshimiwa Waziri hapa kwenye ukurasa wa 104 na 105, Mheshimiwa Waziri amejaribu kuongea kuhusiana na changamoto mbalimbali ambazo zimejitokeza na ni kwanini wameshindwa kutekeleza miradi mbalimbali ambayo ilikuwa imepangwa. Tatizo kubwa wanalolizungumzia kama Wizara wanalalamika kwamba fedha hazitoki kwa muda na fedha haziendi ili kutekeleza miradi na hii imesababisha kukwamisha miradi mingi isiweze kutekeleza. Sasa kama Wizara Serikali imeanza kulalamika kiasi hiki, ni wajibu Wabunge sasa kuchukua hatua kujaribu kuiambia Serikali itoe fedha ili Wizara ikaweze kutekeleza miradi hii.

Mheshimiwa Spika, kwahiyo lazima tusimame tuangalie Waziri wa Fedha pamoja na Hazina waangalie ni namna gani wanaweza kuwa wanatoa fedha ambazo tunakuwa tunazipitisha ndani ya Bunge hili ili ziende kufanya kazi na Watanzania waweze kupata maji. Hatuwezi kuwa kila siku tunatengafedha halafu baadaye hizo fedha haziendi kufanyakazi. Hili ni jambo ambalo linatushangaza sana na ni wajibu wetu kama Wabunge, ni wajibu wako kama kiongozi wa Bunge kuhakikisha kwamba unalisimamia hili jambo na fedha zinatoka, maana yake nakumbuka mwaka uliopita ulijaribu kumweleza Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwamba kwanini hupeleki fedha katika miradi ya maendeleo kama ambavyo tumepitisha.

Mheshimiwa Spika, sasa hivi ningeomba Bunge lako hili lihakikishe kwamba Serikali wakati wote tunapokuwa tumetenga bajeti yetu,ni lazima bajeti hii ikatekeleze miradi kama tulivyokuwa tumepanga. Sasa miradi iliyotekelezwa mwaka 2018/2019 ni nusu ya fedha ambazo tulikuwa tumeshazitenga. Tafsiri yake ni kwamba mwaka 2019/2020 tunakwenda kutekeleza viporo ambavyo tulitakiwa kutekeleza katika mwaka uliopita. Kwahiyo, naomba sana jambo hili lazima tulifanyie kazi.

Mheshimiwa Spika,nilimsikiliza Mheshimiwa Musukuma pale amesema kwamba hataki Sh.50 iweze kuongezwa. Watu wengi wanaweza kuona hii ni hoja dhaifu, lakini si hoja dhaifu, ni hoja nzuri na inaendeleza kutukumbusha kwamba tunavyozidi kuongeza tozo kwenye mafuta kwa ajili ya maji tafsiri yake ni kwamba tunawaongezea wananchi mizigo, tunaendelea kuongezea gharama wananchi badala ya kuwapunguzia gharama wananchi. Hawa Watanzania ambao tunawazungumza leo kuwaongezea kila siku mafuta hawa wananchi wanalipa kodi, hawa wananchi kila siku tunaosema kwamba tuwaongezee ni wananchi ambao tayari wanalipa kodi katika Taifa hili.

Mheshimiwa Spika,kwahiyo lazima tuangalie tunachokizungumza tunamaanisha namna gani, je, kodi wanazozitoa wananchi na ambazo tunatenga kwenye bajeti hii kwanini Serikali inashindwa kutoa fedha hizi na kwenda kufanyakazi. Nimeshasema kuna fedha bilioni 285 zilitengwa mwaka jana ambazo Hazina walitakiwa wazitoe mpaka sasa hivi tukisema kwenye mahesabu ambayo tumeyapiga hapa kufikia bilioni 343 hutaiona fedha iliyotoka Hazina. Sasa tunataka fedha za wananchi ziweze kutumika kama ambavyo tunapitisha bajeti katika Bunge hili.

Mheshimiwa Spika,madhara ya kutokuwa na maji safi na salama kwa wananchi ni makubwa sana katika Taifa kwasababu wananchi wengi sasa wanaumwa matumbo na matumbo haya yanasababishwa sana na kupata maji ambayo ni machafu. Sasa Serikali inaingia gharama kubwa sana ya kununua madawa na tumekuwa tunajinasibu ndani ya Bunge hili kwamba Serikali inatenga fedha nyingi kwaajili ya kununua madawa. Kununua madawa kwa fedha nyingi sio sifa ni kwamba Watanzania wengi ni wagonjwa, Watanzania wengi wanaumwa na ndio maana tunatenga fedha hizi, lakini fedha hizi tunasababisha kuzitumia vibaya kwenye madawa kwasababu hatutaki kutengeneza mazingira mazuri ya kupata maji safi na salama. Ni lazima tujikite kuhakikisha kwamba tunawapatia wananchi wetu maji safi na salama na bajeti zingine hizi zitakwenda kufanya kazi zingine ambazo zinahitajika zaidi, lakini hiki tunakihitaji wenyewe.

Mheshimiwa Spika, pia kuna kiasi cha maji kwa mtu kwa mwaka, ukiangalia katika takwimu mwaka 1961 kiasi cha matumizi ya maji kwa mtu mmoja mmoja kwa mwaka ilikuwa ni ujazo wa mita za ujazo 7,862, lakini mpaka mwaka 2018, sasa hivi zimeshuka mpaka 2,300. Hii inatoa picha gani? Ni kwamba Serikali haijaweka uwekezaji mzuri ili kuweka uwiano mkubwa kulingana na ongezeko la Watanzania katika Taifa hili. Ni lazima tuone na ndiyo maana mjumbe mmoja jana amesema tunakoelekea Tanzania sasa hivi tuko kwenye mstari ambao uko kwenye hatari ya kukosa maji kabisa kwasababu wananchi wanazidi kuongezeka, lakini uwekezaji unazidi kushuka. Angalia katika bajeti ya mwaka huu, bajeti ya mwaka huu Mheshimiwa Waziri anahitaji bilioni 610 ili kutekeleza miradi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante Mheshimiwa.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA:…lakini kila mwaka bajeti inazidi kushuka. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia katika hotuba hii. Tunapozungumzia biashara tunazungumzia uwekezaji wa ndani na wa nje, hivyo, kama ambavyo Serikali inasema kuwa inahitaji nchi hii iwe nchi ya viwanda, lazima ifahamu kuwa viwanda ni biashara na kama mazingira ya kufanyia biashara siyo rafiki, basi hata viwanda havitaweza kuwepo. Ni vizuri Serikali ikaelewa kuwa kama wafanyabiashara wa kawaida wanashindwa kufanya biashara basi tusitegemee wafanyabiashara kutoka nje kuja kuwekeza katika nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ifahamike kuwa biashara ni mawasiliano, kila kinachofanyika hapa kwetu kinajulikana karibu dunia nzima, hivyo, kama tumeshindwa kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji wa ndani tusitegemee kupata wawekezaji toka nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaposema kuwa biashara zinafungwa lazima Serikali itafute namna ya kuondoa tatizo na siyo kuendelea kukomaa bila kuondoa changamoto zilizosababisha biashara kufungwa kila mahali hapa nchini na kama tukiendelea hivyo basi tutegemee kukosa kukusanya kodi kama tunavyokuwa tunategemea siku zijazo. Hata hivyo, kibaya zaidi wafanyabiashara wengi wametimkia katika nchi jirani na kusajili biashara zao huko.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni Taifa gani ambalo linaweza kuendelea na kufikia uchumi wa kati kama wananchi wake hawana uwezo wa kulipa kodi na kodi zinalipwa kutoka kwenye faida? Pia kodi zinalipwa kulingana na ukubwa wa biashara, sasa kila wakati tunaishauri Serikali kuwa irekebishe baadhi ya sheria za kodi na tozo mbalimbali ili kufanya urahisi wa kufanya biashara ili mitaji ya watu ikue na kutoa nafasi kwa wafanyabiashara kuchangia pato la Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hii haioneshi dhamira ya kuwa nchi ya viwanda, kama tunaweza kuidhinisha pesa ya maendeleo, shilingi bilioni 100 lakini pesa iliyotoka mpaka sasa ni bilioni 12 halafu unasema tuko tayari kuwa nchi ya viwanda, huo utakuwa uongo mchana kweupe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Taarifa ya Benki ya Dunia kuhusu urahisi wa kufanya biashara duniani, Tanzania sasa ni ya 137 kati ya nchi 190 duniani na changamoto zilizotajwa ni pamoja na kodi ambazo siyo rafiki kufanya biashara na ugumu wa kuanzisha biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali hii tangu imeingia madarakani imekuwa haiwaamini tena wafanyabiashara, imewapa majina mengi sana kama wizi, mara wapiga dili, yote hayo yanaonesha kuwa Serikali haitambui kuwa wafanyabiashara ni wadau muhimu kabisa katika Taifa hili na kama mpaka leo Watanzania wamewapa madaraka haya haitambui hilo, basi Taifa hili ni haki linavyoangamia kwa wafanyabiashara kuitwa majina haya.

Mheshimiwa Naibu Spika, yapo matukio ambayo yametokea hivi karibuni kwa wafanyabiashara wa maduka ya kubadilishia pesa za kigeni kufungwa na pia kuondoka na pesa pamoja na vitendeakazi, Watanzania wanataka kujua je, ni kwa nini Serikali ilifunga maduka hayo na kuchukua pesa zilizokuwa katika maduka hayo na je hiyo ndiyo elimu kwa walipakodi hao?

Mheshimiwa Naibu Spika, tulitegemea taarifa kutoka Serikalini sababu ya kufunga maduka hayo ambayo yameanzishwa kwa mujibu wa sheria ya nchi na kama kulikuwa na tatizo Serikali inawasaidiaje hawa wafanyabiashara? Pia taarifa ilitoka kuwa Serikali kwa sasa imeelekeza wapi huduma ya kubadilishia pesa itatolewa? Je, katika nchi hii hakuna tena mtu kufungua duka la kubadilishana pesa za kigeni? Kama ndivyo katazo hilo liko kwa mujibu wa sheria ipi?

Mheshimiwa Naibu Spika, hayo yote ni mambo yanayoiweka nchi yetu katika mtazamo mbaya wa kuonesha jinsi Tanzania isivyokuwa nchi salama katika kufanya biashara. Pia kama kuna pesa zilizochukuliwa kutoka katika maduka hayo ya kubadilishana pesa ni shilingi ngapi? Je, ni wafanyabiashara wangapi wanafikishwa mahakamani na kwa kosa gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, tunashuhudia pia wafanyabiashara mbalimbali wakisota mahabusu kwa muda sasa, je, Serikali inajua kuwaweka ndani wafanyabiashara bila taarifa yoyote kwa umma ni kuendelea kuongeza hofu kwa wafanyabiashara mfano Yusuph Manji, Lugemalira na wengine wengi bila taarifa rasmi za wazi kwa umma ili umma ujifunze na kujua kinachoendelea juu ya wafanyabiashara hao? Je, Serikali inaweza kutufahamisha ni wafanyabiashara wangapi wako rumande kwa kosa la kutakatisha fedha? Je, Serikali imepata faida gani katika kuwakweka rumande wafanyabiashara hao?

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hali isiyo ya kawaida bado Serikali haikubali kuwa sasa Tanzania siyo sehemu salama kwa kufanya biashara, ukienda Kariakoo sasa utaona vyumba vimefungwa na vimebandikwa matangazo chumba kinapangishwa. Jambo hilo hapo awali halikuwepo kabisa na ni kwa sababu wafanyabiashara wameshindwa kufanya biashara. Kuna kikosi kimeanzishwa kinaitwa task force, hiki kinakaa nje ya maduka na kukamata mtu anayetoka kununua mzigo katika maduka na kuuliza risiti, baadaye huwanyang’anya mizigo na kuutaifisha na kumtoza mwenye duka faini ya milioni tatu au zaidi na muda mwingine hupokea rushwa ya kati ya milioni moja au milioni moja na nusu na kumalizana na mfanyabiashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo faini ya milioni tatu imeongeza rushwa kwa hiyo task force, lakini pia imepelekea wageni kunyang’anywa mizigo na sasa stoo za TRA Dar es Salaam zimejaa mizigo ya wafanyabiashara hao wageni na baada ya muda TRA huipiga mnada mizigo hiyo. Kitendo hiki kimesababisha wafanyabiashara kutoka Congo, Zambia na kadhalika kuacha kuja Dar es Salaam kununua.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi nami niweze kutoa mchango wangu siku ya leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuko Bungeni kama Wabunge, nia na madhumuni ni kuishauri sana Serikali. Tunavyozungumza sisi upande wa Upinzani tuchukuliwe kama ni Wabunge ambao tuna haki na tunaishauri Serikali kama ambavyo Wabunge wa Chama cha Mapinduzi wanavyoweza kuishauri Serikali na kazi yetu kubwa ni kuangalia gaps ambazo mnashindwa kuziba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ziko kero nyingi sana za wafanyabiashara ambazo mwaka 2018/2019 Serikali ya Chama cha Mapinduzi ndani ya Bunge hili waliahidi kupunguza kero mbalimbali kwa wafanyabiashara. Huwezi kuamini, mpaka sasa hivi kwenye nchi hii bado kero za wafanyabiashara hazijatatuliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana 2019 wakati wa bajeti hapa ilionyesha kwamba kuna kodi karibu 54 ambazo zilitolewa. Sielewi kodi hizi ambazo zilitolewa kama kweli Serikali ilifanya utafiti na ikakutana na wafanyabiashara, kama kweli ndiyo zilikuwa kero za wafanyabiashara. Hata hivyo, bado kuna kero kubwa sana kwa wafanyabiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunakaa mpakani pale, tunaona jinsi ambavyo wafanyabiashara wengi wanahamia kwenye nchi za jirani na Tanzania. Ukiangalia wafanyabiashara wengi wa Tanzania wanakimbilia Malawi, wengine wanakimbilia Zambia, lakini pia wako wafanyabiashara wakubwa sana ambao sasa hivi wanahama nchi, wanakwenda kuwekeza viwanda katika nchi nyingine na Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi bado inaona wafanyabiashara kama ni watu ambao hawaaminiki. Hakuna nchi yoyote duniani ambayo inaweza ikapiga hatua kama itaona wafanyabiashara ni watu ambao hawaaminiki na siyo wadau wakubwa katika Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wajibu wa Serikali ni kuhakikisha kwamba wafanyabiashara mitaji yao inakua ili waweze kulipa kodi na Serikali iweze kupata fedha na kuhakikisha kwamba inatekeleza miradi mbalimbali ambayo inapendekeza katika Taifa hili. Leo Serikali hii inajinasibu kwamba inakusanya mapato mengi sana, lakini ukweli tu ni kwamba wafanyabiashara mitaji yao imeshuka na fedha ambazo zinakusanywa sasa hivi karibuni wafanyabiashara wanalalamika, wananyang‟anywa tu hizo fedha, siyo kwamba wanapenda. Ndiyo maana wafanyabiashara wengi ukienda Segerea na kwenye Magereza mbalimbali wamekamatwa wamewekwa kwa kesi za money laundering ambazo hazina ukweli wowote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaishauri Serikali iwajibike kuhakikisha kwamba biashara zinaboreka katika nchi hii ili kuhakikisha kwamba Watanzania wengi wanafanya biashara na mitaji inakua ili biashara Serikali iweze kukusanya mapato. Tunaamini kabisa katika mwaka unaokuja wa 2020/2021 tuna uhakika kabisa kwamba Serikali hii itashindwa kukusanya mapato ya kutosha kwa sababu wafanyabiashara wengi watakuwa wameshafilisika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka huu tulikuwa Uganda, tumeshangaa sana. Wafanyabiashara wote wa Dar es Salaam sasa hivi wanafunga bidhaa zao Kampala; wafanyabiashara wa Moshi, Arusha na Mbeya wameanza kufunga biashara zao Kampala pale badala ya Dar es Salaam. Sasa unashangaa, Jiji ambalo tulikuwa tunaamini kabisa kwamba ni soko la Afrika Mashariki, sasa hivi limeshakufa. Sasa hivi watu wanakwenda Kampala wanafanya biashara, wanafunga biashara kule, wanakwenda kufanya biashara Tanzania. Kwa hiyo, wanafunga mizigo ya madukani kwenye Mji wa Kampala. Sasa hivi Mji wetu wa Dar es Salaam umeshakufa kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunavyozungumzia biashara, tunazungumzia uchumi wa nchi. Tusipojua kwamba uchumi wa nchi ni biashara, tutakuwa tunapoteza muda. Nafikiri Waziri wa Viwanda na Biashara akae na Waziri wa Fedha wajaribu kuangalia matatizo ambayo yako Tanzania, ambayo tunaona yanaendelea kuua biashara na yatafilisi kabisa biashara za watu na biashara zitakufa katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza humu na ukijaribu kusoma unaona kabisa kwamba kuna mipango mizuri sana, lakini hakuna utekelezaji mzuri ambao unatoa mwanga kwa wafanyabiashara kufanya biashara katika Taifa hili. Ndiyo maana tunawaambia kila wakati kwamba bajeti ambazo tunatengeneza, Serikali hii inatekeleza bajeti hizi kwa kuangalia uchumi wa vitu na siyo uchumi wa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza kila wakati hamtuelewi. Ukiangalia bajeti ambazo zipo, kwa mfano bajeti ya miundombinu; ina-cost karibuni trilioni 4.6 lakini ukienda kuangalia kati ya hizo fedha, kwenye kilimo utaona kabisa wamewekeza shilingi bilioni 100, lakini inakwenda shilingi bilioni tatu. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Mwakajoka.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mifugo na Uvuvi
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia. Wabunge wote ambao wamezungumza ndani ya Bunge asilimia kubwa wamejaribu kuzungumzia hali halisi ambayo inajitokeza kwa wananchi wetu hasa ambao wanajishughulisha na suala la uvuvi na ufugaji.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na malalamiko makubwa sana; kwa mfano, Tunduma pale leo, tangu juzi, jana, leo, pamoja na mimi kukutana na Mheshimiwa Waziri na kujaribu kumweleza, lakini hali kwa kweli Tunduma ni mbaya sana. Sasa hivi Wananchi takribani 20 walikuwa wamekamatwa na wamewekwa ndani, ambao wanajihusisha na biashara ya samaki na dagaa. Vilevile wananchi hawa wanadaiwa dola 1.5, lakini pia waepigwa faini zaidi ya milioni mbili, milioni moja na nusu, sababu kwa nini wanafanya biashara na wageni ambao wanatoka Congo na wageni ambao wanatika Zambia. Jambo hili kwa kweli limetusikitisha sana.

Mheshimiwa Spika, na mwaka uliopita tulijaribu kumweleza hata Mheshimiwa Waziri; kwamba sheria hizi ambazo zimeonekana zinaleta unyanyasaji sana kwa wananchi na zinarudisha nyuma juhudi za wananchi ambao wameamua kufanya biashara ya samaki na dagaa tulimwomba azilete Bungeni ziweze kufanyiwa mabadiliko. Kwa kweli sheria hii imekuwa ni kikwazo kikubwa sana kwa wafanyabiashara.

Mheshimiwa Spika, na ukijaribu kusoma hata Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, ukisoma Kifungu cha 27 Kifungu Kidogo cha (n), Ilani inasema itawawezesha wavuvi wadogowadogo pamoja na wafanyabiashara kuhakikisha kwamba wanafnya shughuli zao vizuri bila kubughudhiwa na ikapunguza pia tozo mbalimbali ambazo zimekuwa ni kikwazo kikubwa kwa wavuvi hawa pamoja na wafanyabiashara wadogo.

Mheshimiwa Spika, lakini huwezi kuamini, sasahivi imekuwa ni kero Kanda ya Ziwa huko watu wanalia, lakini bado maeneo ambayo wanakwenda kufanya biashara. Kwa mfano Bahari Kuu, ukienda eneo la Pwani pamoja na Zanzibar wanapokuja kufanya biashara hizi imekuwa ni tatizo kubwa, lakini mpaka wawekezaji. Kwa mfano kwenye Mji wa Tunduma kulikuwa na eneo zuri kabisa la uwekezaji watu wanatoka Zambia, Congo, Angola na maeneo mengine walikuwa wananunua samaki pale, lakini leo huwezi kukuta watu wanakuja kununua pale. Sasahivi atu wanakimbiakimbia wanakamatwa, wavuvi wetu pamoja na wanaoleta dagaa pale na samaki, lakini pia wafanyabiashara wa pale wanakamatwa hovyo hovyo. Sasa tunataka kumuinua Mtanzania wa namna gani? Tunataka kumwinua masikini wa Kitanzania wa namna gani?

Mheshimiwa Spika, kama mtu anajiwezesha mwenyewe anakwenda anatafuta mtaji anaamua kufanya biashara ya samaki, anaamua kufanya biashara ya dagaa, lakini anakuwa ananyanyasika katika nchi yake anashindwa kufanya biashara hii; hivi Serikali ya Chama Cha Mapinduzi ndivyo ilivyojiandaa namna hii?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi naomba sana, kwa kweli jambo lililotokea Tunduma ninaomba Mheshimiwa Waziri alishughulikie haraka iwezekanavyo kwa sababu limeleta tatizo kubwa, limeleta tafrani kubwa. Wananchi wameshindwa kukaa, wananchi wameshindwa kufanya biashara na wageni ambao waliokuja kufanya biashara pale sasa wameamua kuondoka; sasa tunajenga nchi au tunabomoa nchi?

Mheshimiwa Spika, na leo tunakuwa humu ndani ya Bunge tunasema kila wakati kuwa tunahitaji wawekezaji waje katika nchi hii kuja kuwekeza; kama wafanyabiashara wa ndani wananyanyaswa wanashindwa kufanya biashara, hivi wawekezaji kutoka nje wanatoka wapi? Hiki ambacho tunakizungumza hakina uhalisia kabisa. Kwa hiyo, mimi nomba sana wafanyabiashara wangu kwenye Mji wa Tunduma, Mheshimiwa Waziri aweze kutoa maelezo ni namna gani wafanyabiashara hawa wataachiwa kutoka ndani, lakini pia hizi faini ambazo zinapigwa, milioni mbili, milioni tatu, wanapigwa wajasiriamali wadogo kabisa, maana yake nini katika Taifa hili? Kwa kweli, kumekuwa na tatizo kubwa sana kwenye Mji wetu wa Tunduma, lakini pia sheria hizi za uvuvi imekuwa ni unyanyasaji mkubwa sana kwenye Taifa hili.

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lingine, ukisoma kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi, waliahidi kwamba mpaka miaka mitano inakwisha watahakikisha kwamba wananunua meli tano za uvuvi, lakini mpaka leo hakuna meli hata moja iliyonunuliwa na bado mwaka mmoja. Sijui tafsiri yake ni nini; kwamba Ilani ya Chama Cha Mapinduzi haitekelezeki au Ilani imeachwa kama ambavyo ilikuwa inadanganya wananchi wapige kura halafu baadaye waachwe? Kwa sababu tulikuwa tumeambiwa katika ilani, ukisoma kulikuwa na meli tano zilitakiwa zinunuliwe, lakini hata meli moja haijanunuliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini pia huwezi kuamini katika taifa hili tuna utajiri mkubwa sana wa samaki, lakini kitu kinachoendelea samaki wanaoagizwa nje kila mwezi wana thamani ya bilioni 56, kila mwezi ambayo ni sawa na dola milioni 25. Pia kwa mwaka mzima tunatumia fedha bilioni 672 kuagiza samaki nje ilhali tuna maziwa na bahari yetu tunakoweza tukapata samaki kwa wingi. Sasa Serikali lazima ijaribu kuangalia, tunapoteza fedha nyingi kwenda kununua samaki nje, tunanunua China, tunanunua Vietnam, lakini samaki tunao; tuna maziwa, tuna bahari, lakini tunakwenda kununua samaki nje. Jambo hili Serikali iliangalie kwa umakini sana; kwa sababu kama tutaendelea kufanya haya tafsiri yake ni kwamba, tutakuwa hatulitendei taifa hili haki.

Mheshimiwa Spika, lakini pia tumesikia taarifa kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri, tumeona kabisa wanasema kwamba maduhuli yamepanda sana, lakini ukweli maduhuli haya ni mateso makubwa kwa Watanzania ambao walitegemea neema na nuru kutoka kwenye Serikali hii. Hali ni mbaya sana, Kanda ya Ziwa huko kuna watu wamefilisika kabisa, Kanda ya Ziwa huko kuna watu wamekimbia nchi hii kwa sababu tu ya sheria ambazo tumezipitisha ndani ya Bunge hili. Ninaomba sana sheria hizi zibadilishwe kwa sababu sisi ni Wabunge tunatunga sheria, sheria hizi zikibadilishwa ziwe rafiki kwa Watanzania ambao wamejiingiza kwenye sekta ya uvuvi pamoja na ufugaji. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi, wa Mwaka 2016
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii ili nichangie Muswada huu. Muswada huu umekuja kipindi muhimu sana lakini tunachotaka kukizungumza sisi kama Watanzania ni lazima tubadilike sana katika kuhakikisha kwamba tunatekeleza wajibu wetu vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tafiti mbalimbali zimekuwa zikifanywa katika nchi hii lakini tatizo kubwa ni kwamba zikishafanyika zinawekwa katika makabati haziwafikii wananchi na hata siku moja hawajaona ni namna gani tafiti hizi zimewasaidia. Ndiyo maana ukiangalia sasa hivi utaona wakulima wetu hawajui walime nini katika maeneo yao kwa kuongozwa na hawa watu ambao wamefanya utafiti. Kwa hiyo, tunaomba sana Serikali tunapokuwa tumepitisha Miswada hii na kuwa sheria ni lazima zianze kufanya kazi tena kwa vitendo kabisa.
Mheshimiwa mwenyekiti, nilikuwa najaribu kupitia Muswada huu na niliangalia baadhi ya maeneo ambayo nataka kuchangia sasa hivi lakini sijaona sehemu ambayo Msajili wa Hazina ametajwa. Jambo hili limenisikitisha kwa sababu ukisoma Sheria za Msajili wa Hazina zinaonesha kwamba Msajili wa Hazina ndiye mtu pekee ambaye anasimamia mashirika pamoja na taasisi mbalimbali ambazo zinaanzishwa katika nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kushangaza katika sheria hii sijaona inataja Msajili wa Hazina anahusika kuyasimamia mashirika pamoja na taasisi ambazo zinaanzishwa. Naomba sheria zote zinazotungwa sasa hivi zimtaje Msajili wa Hazina kama ndiye msimamizi mkuu wa mashirika na taasisi mbalimbali zinazoanzishwa katika nchi hii. Nia na madhumuni ni kumpa nafasi kubwa Msajili wa Hazina kuhakikisha kwamba anasimamia mashirika au taasisi hizi ambazo zinakwenda kuanzishwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nimeliona liko tofauti ni uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi, inaonesha kwamba Mheshimiwa Rais ndiye atachukua jukumu la kumteua Mwenyekiti wa Bodi lakini tumeona mashirika na taasisi mbalimbali ambazo Mheshimiwa Rais ameteua Wenyeviti hawa 90% ni wazee ambao walikuwa wameshastaafu na leo wamerudishwa kazini. Kwa hiyo, wanapata nafasi hizi kama vile fadhila kutoka kwa Mheshimiwa Rais.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunaomba sasa uteuzi huu wa Mwenyekiti wa Bodi ni lazima Mheshimiwa Rais ashauriane na Msajili wa Hazina ili Msajili wa Hazina aweze kumsaidia Mheshimiwa Rais ni namna gani anaweza akapata Mwenyekiti wa Bodi ambaye anaweza kuisaidia Bodi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana sasa hivi unaona mashirika na taasisi nyingi zinakufa na hazifanyi kazi ipasavyo kwa sababu watu wanaoteuliwa kwa kweli ni wazee na ambao hawawezi kutoa mawazo mazuri na wakafanya kazi nzuri. Kwa hiyo, tunashauri sheria hii ifanye mabadiliko na kuhakikisha kwamba wakati Mheshimiwa Rais anamteua Mwenyekiti wa Bodi lazima ashirikiane na Msajili wa Hazina ili kuboresha uteuzi huo tupate Mwenyekiti wa Bodi bora na anayeweza kusaidia taasisi au shirika kutekeleza wajibu wake ipasavyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumeona mashirika mbalimbali ambayo Mheshimiwa Rais amekuwa akiteua Wenyeviti wa Bodi ufanisi wake umekuwa ni mdogo sana. Kwa hiyo, tunaomba sana TR aweze kushiriki kwa 90% katika uteuzi wa viongozi mbalimbali au viongozi wa Bodi ambao wanateuliwa katika nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia sheria hii haijatuonesha tafiti mbalimbali ambazo zitafanyika kama zitakuwa zimekosewa na kusababisha hasara kwa wakulima au wafugaji wetu, ni namna gani wananchi hawa wanaweza wakafidiwa na Serikali kwa sababu ya utafiti ambao unakuwa umefanyika vibaya. Tunachokiona pale ni kwamba kama watakuwa wamefanya utafiti na baadaye utafiti ule ukasababisha hasara kwa wakulima na wafugaji ni kwamba wale watu hawawezi kushtakiwa wala hakuna hatua zozote ambazo zinaweza zikachukuliwa dhidi yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili linaleta mkanganyiko na tunaomba sana tujue juu ya suala hili. Hata Wabunge wengine wamesema wamenunua mbegu za mahindi wakipanda hazioti na kuingia hasara kwa sababu msimu unakuwa umeshapita. Kwa hiyo, lazima pia sheria ioneshe kwamba kama utafiti utafanyika vibaya na ukasababisha hasara kwa wananchi wetu ni lazima wananchi hawa ambao wamepata hasara waweze kufidiwa ili maisha yao yaweze kuendelea kama ambavyo walitarajia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, nilikuwa naangalia orodha ya vituo vya utafiti katika Jedwali sijakiona Kituo cha Utafiti cha Mbimba kilichopo Wilayani Mbozi katika Mkoa wa Songwe. Kituo kile kinaendelea kufanya utafiti kwa muda mrefu lakini hakipo hapa. Kwa hiyo, wakati Mheshimiwa Waziri anakuja kuhitimisha atueleze ni kwa nini Kituo hiki cha Mbimba kilichopo Wilayani Mbozi katika Mkoa wa Songwe hakionekani kabisa kama ni kituo ambacho kipo wakati ni cha muda mrefu. Kwa hiyo, tutaomba pia tupate maelezo kutoka kwa Mheshimiwa Waziri kuhusu kituo hiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni katika kifungu 27(1), kinasema kwamba Taasisi ya Utafiti inaweza ikakopa na ili iweze kukopa ni lazima Mheshimiwa Waziri wa Fedha pamoja na Waziri wa Kilimo watoe idhini. Naomba tuendelee kupitia Sheria za TR (Msajili wa Hazina) kwani ndiye mtu pekee ambaye amepewa majukumu na mamlaka ya kuamua kwamba shirika au taasisi hii inaweza ikakopa kutokana na mpango kazi ambao inao kama inaweza ikarejesha zile fedha au zinaweza zikaleta tija katika Taifa hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba wakati tunamzungumzia Waziri wa Fedha pamoja na Waziri wa Kilimo ni lazima pia TR ashiriki kujua endapo mkopo huo ambao taasisi inaenda kuchukua utaleta tija katika Taifa hili na siyo Waziri mwenye dhamana pamoja na Waziri wa Fedha kushiriki peke yao. Kwa hiyo, naomba sana…

MWENYEKITI: Ahsante.
Muswada wa Sheria ya Reli wa Mwaka 2017
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii kwanza kushukuru sana hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani, imeandaliwa vizuri na kama ushauri huu uliotolewa kwenye hotuba hii utazingatiwa unaweza ukaboresha zaidi sheria hizi na tukafanya vizuri zaidi kwenye Shirika letu la Reli. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa ambacho ninataka kukizungumza ni kwamba Shirika hili la Reli lilikuwepo huko nyuma baadae likafutwa na sasa limerejeshwa upya na hiki ni kilio cha Wabunge wengi ambao walikuwa wakidai kwamba tunatakiwa kuliunda upya shirika hili, lakini kikubwa tu ni kwamba ni vizuri sana Serikali iwe inafanya utafiti wakati inataka kuanzisha mashirika mbalimbali au kubadilisha sheria mbalimbali kwa ajili ya kuanzisha mashirika ili kuleta tija katika nchi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, imeonekana kabisa katika nchi hii, kitengo cha utafiti kimeonekana kabisa kwamba hakihudumiwi ipasavyo na hakifanyi kazi zinazotakiwa na ndiyo maana tunaona kila kinachoanzishwa kinaanzishwa halafu baadae kinakufa na tunarudi kuja kuanzisha kingine. Hii inaonyesha ni jinsi gani ambavyo tumekuwa na Hati za Dharura nyingi sana katika Bunge hili ambazo zinaletwa na Serikali. Tunafikiri kitengo cha utafiti kiimarishwe zaidi ili waweze kufanya utafiti ukiwa ni wa kiwango cha juu na ambao tukianzisha uwekezaji wowote uwekezaji ule unapata tija zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa nataka nizungumzie kuhusiana na bomoabomoa ambayo inaendelea katika maeneo mbalimbali hasa kwenye maeneo ambayo reli inakwenda kujengwa na reli inakopita. Wananchi wanalalamika sana na takwimu zilizopo sasa hivi ni kwamba karibuni nyumba 3,244 (makazi ya wananchi) yatakwenda kubomolewa wakati wa ujenzi wa reli na hao wananchi wote asilimia kubwa ni wananchi ambao wanaonesha kabisa kwamba wako kwenye mipango miji. Wengi wamepimiwa nyumba/viwanja vyao na wakapewa na Serikali lakini leo hakuna ufafanuzi wowote unaotolewa kwa wananchi hawa ni jinsi gani ambavyo wanaweza wakalipwa fidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, na jambo hili linaleta chuki kubwa sana kwa wananchi na linaathiri sana ustawi wa maisha ya wananchi wenyewe. Tunafikiri kazi ya Serikali ni kuhakikisha kwamba ustawi wa wananchi unakuwa vizuri na siyo kuharibu ustawi wa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni vizuri Serikali ingekuwa inatoa mwelekeo kwamba hawa wananchi wote ambao tayari wako kihalali na wamepewa ardhi hizo na Serikali na wamejenga, wamewekeza katika maeneo hayo Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba inawafidia wananchi hawa ili waendelee kuishi katika maisha yao ya kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine wananchi hawa wamekuwa wakienda Mahakamani mara kwa mara na Mahakama imekuwa ikitoa stop order ya utekelezaji wa uvunjaji wa nyumba cha kushangaza ni kwamba, unakuta Serikali inaendelea na uvunjaji wa nyumba pamoja na stop order. Tunafikiria sana kwamba Serikali inaleta miswada mbalimbali ya sheria hapa na sheria hizi zinakuwa zinatumika katika nchi hii lakini wananchi wakifuata sheria bado Serikali haitaki kufuata sheria na kuona Mhimili wa Mahakama una wajibu wa kuhakikisha kwamba unawasaidia wananchi hawa na badala yake inaonekana kwamba Serikali ina dharau Mhimili wa Mahakama, inaendelea kuvunja, wananchi wanaendelea kulalamika na hawajui waende wapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo lazima Serikali pia ijue kwamba Mhimili wa Mahakama ni muhimu sana na Serikali ndiyo inatakiwa kuwa ni ya kwanza kabisa kutekeleza Sheria za Nchi lakini inaonekana kwamba Serikali imeshindwa kutekeleza sheria za nchi, wananchi wamekwenda Mahakamani Serikali inaendelea kuvunja wakati Mahakama imeshazuia, sasa jambo hili kwa kweli linasumbua sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona pia kumekuwa na tatizo kubwa sana, sheria ambayo imeletwa leo hasa kwenye kifungu cha 28 ambacho huko nyuma kilikuwepo, kilikuwa ni kifungu cha 32 kwenye Sheria ya mwaka 2002, bado kimerejeshwa kama kilivyo. Kinaendelea kutoa haki kwa mwananchi kama reli ikipita kwenye nyumba yangu hakuna majadiliano, wanachokifanya wao ni kuangalia hili eneo linaweza likapitishwa reli basi, mimi ni mtu wa kuondoka hakuna ufafanuzi wowote uliotolewa kwenye sheria hii, kwamba nini ambacho kitaendelea baada ya kuona ya kwamba lile eneo reli itapita, mwananchi atafaidika namna gani.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata ile Sheria ya Fidia inaonekana kwamba kwenye Sheria ya Reli haitumiki kabisa, kwa maana hiyo wakiamua kupitisha kwenye eneo lako, kwenye shamba lako au wakiamua kupitisha kwenye nyumba yako ina maana kwamba hiyo reli itapita pale na hakuna fidia yoyote itakayotolewa kwako. Jambo hili linaonesha kabisa kwamba Serikali ni namna gani inajipanga kutokutekeleza ile sheria ambayo imeileta yenyewe na imeitunga yenyewe kuonesha kwamba mwananchi yeyote ana haki ya kumiliki ardhi na kwa sababu ni mtu anayeiendeleza ile ardhi kama kuna jambo lolote linakwenda kufanyika pale au kutekelezwa katika eneo lile basi atalipwa fidia, jambo hili halionekani kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ni pamoja na hawa wananchi ambao tumesema 3,233, hawa wananchi ni wengi sana na katika nchi hii imekuwa ni tatizo kubwa, bomoa bomoa kila maeneo. Ukienda kwenye barabara bomoa bomoa inaonesha kabisa Wizara ya Ujenzi haiko makini ni kwa nini imeshindwa kuweka alama katika maeneo yake yote, ukianzia barabara lakini pia ukienda kwenye reli na maeneo mengine, imeshindwa kuweka alama ambazo zinaonyesha kwamba wananchi wanapokuwa wapo kwenye maeneo yao au wanapotaka kujenga wawe wanajua kwamba haya maeneo ni maeneo ya reli au ni maeneo ya barabara, Wizara imeshindwa kutekeleza wajibu wake. Tunataka tujue Serikali sasa hivi ina mpango gani kuhakikisha kwamba inaweka alama hizo ili wananchi hawa wasiendelee kupata matatizo ya namna hiyo siku hadi siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali lazima ikubaliane nasi kwamba kitendo cha kumvunjia mwananchi wake nyumba ni kumrudisha nyuma na kurudisha maendeleo nyuma ya wananchi. Kwa hiyo, ni lazima Serikali ijipange kama inataka kufanya maendelezo sehemu yoyote ni lazima ikubali kwamba kama kuna wananchi wako pale basi wananchi wale wafidiwe na baada ya kufidiwa basi wakajenge makazi mengine katika maeneo ambayo wanaweza wakaishi na familia zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Watanzania wanapata shida ukienda kwenye barabara Watanzania wanalala nje, leo kwenye reli hawa wananchi nani atawahifadhi wananchi wote hawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haijaweka hata utaratibu ni namna gani wananchi hawa itakwenda kuwahifadhi, wanawaona kama ni watu ambao hawakustahili kabisa kuwepo pale wakati Serikali pia ilikuwepo kwa nini haikuweza kusimamia haya ambayo yalikuwa yanafanyika kipindi hicho? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, wananchi wapewe nafasi kubwa ya kusikilizwa na pia wahakikishe kwamba wanapewa maeneo ya kujihifadhi kwa kipindi hiki ambacho tayari Serikali inataka kuwaondoa katika maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine ni pamoja na sheria hii ukiangalia Kifungu cha 16 mpaka 23 Mamlaka ya Reli yule mtu anayesimamia yale maeneo anaweza akaenda kwenye kijiji au kwenye makazi ta mtu na akaanza kufanya tathmini ni namna gani wanaweza wakapitisha reli hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa yale maeneo wako viongozi wa Serikali za Mitaa, wako viongozi wa vijiji, wako Viongozi wa vitongoji na Waheshimiwa Madiwa wakashirikishwa katika yale maeneo nini ambacho kinaendelea pale na watoe ushauri wao na ikiwezekana wawe na nafasi kwenye sheria hii ni namna gani ushauri wao pia unaweza ukachukuliwa na kwenda kufanyiwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.