Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma (90 total)

MHE. DKT. CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri. Licha ya hivyo, nina maswali mawili madogo.
Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kuona umeanzishwa Mfuko wa Dhamana wa kuwasaidia akina mama hawa kupata mikopo. Kwa upande mwingine kuna mabenki mengine pamoja na taasisi ambazo bado wanatoa mikopo, lakini yenye riba kubwa.
Je, kwa upande wa Serikali kuna mikakati gani ya kushauri hizi taasisi na mabenki kutoa riba ndogo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa upande wa masoko ya uhakika, kwa upande wa Morogoro, kulikuwepo kiwanda cha matunda kinachotengeneza juice, lakini mpaka sasa hivi hakifanyi kazi. Je, kuna mkakati gani wa Serikali kushauri hiki kiwanda kiweze kufanya kazi au kuwezesha wawezeshaji waweze kujenga kiwanda Mkoani Morogoro kuwasaidia wanawake wanaolima matunda na wananchi wa Mkoa wa Morogoro kupata soko la uhakika pamoja na wajasiriamali? Ahsante sana. (Makofi)
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Dkt. Christina Ishengoma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kuhusu riba za mabenki na taasisi za fedha, kimsingi siyo rafiki kwa mtu yeyote kuweza kukopa na ukafanya biashara kwa tija. Serikali inapitia upya suala la riba na Mheshimiwa Waziri wa Fedha ikifika wakati, atakuja kutupa mwongozo.
Mheshimiwa Spika, suala la pili; Morogoro kuna mjasiriamali mmoja au mwekezaji alijasiria na kuanzisha kiwanda cha kutengeneza concentrate. Anakusanya matunda, anayakamua, anatengeneza concentrate na anaweza kuuza nchini na nje kwa wale watengeneza juice. Kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu, huyo mjasiriamali au mwekezaji, aliaga dunia.
Mheshimiwa Spika, juzi nilipokwenda Morogoro nimemwagiza Mkuu wa Mkoa akae na wanafamilia kusudi wajadiliane namna gani tunaweza kupata mtu wa kuwasaidia watu wao waweze kuendeleza hicho kiwanda cha concentrate.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge, juice nyingi tunazokunywa hapa zenye picha za matunda ya nchi hii hazizalishwi hapa! Kwa hiyo, tunawatia shime wanafamilia wakubaliane na mapendekezo ya Serikali. Hiyo iko kwenye score card yangu; nitakwenda kushirikiana nao kusudi kile kiwanda kifanye kazi.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, licha ya kuongeza ujazo wa mita za maji katika Manispaa ya Morogoro bado kuna sehemu za Lukobe, Kihonda, Kilakala, Folkland, SUA, Mbuyuni na sehemu zingine ambazo hawapati maji. Je, kwa nini hawapati maji wakati wote?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Manispaa ya Morogoro inakua na watu wanaongezeka. Licha ya mradi wa Milenia wa Halmashauri ambao umepita, je, kuna mkakati gani wa kubuni mradi mwingine wa maji kusudi maji yaweze kutosheleza Manispaa ya Morogoro?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Maji ya mwaka 2002 imeainisha kuhakikisha kwamba nchi yetu ifikapo mwaka 2025 watu wote watakuwa wamepata maji safi na salama. Hiyo itakuwa ni pamoja na wananchi wote wa maeneo ya Morogoro. Maeneo aliyoyataja kwa sasa hivi tunaanza programu ya pili ambayo imeanza Januari, 2016 ya kuendeleza miradi ya maji katika nchi yetu. Katika programu hiyo, tutaendeleza utafutaji wa maji katika Mkoa na Mji wa Morogoro kwa maeneo ambayo yamebaki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni kweli kabisa kwamba Mkoa wa Morogoro unapanuka na nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mikakati tuliyonayo, tutahakikisha kwamba maeneo yote na wakazi wote wa Mkoa wa Morogoro na Mji wa Morogoro hasa wanapata maji safi na salama. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, mara kwa mara umekuwepo usumbufu wa walimu wa awali kupata mishahara yao kwa wakati.
Je, kuna mkakati gani wa kuwapatia mishahara yao kwa wakati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri Mheshimiwa Waziri hapa amelizungumza punde kwamba walimu wa awali ni walewale ambao wapo katika utaratibu wa walimu walioajiriwa. Kwa hiyo, ina maana kwamba, hatutarajii mshahara wa mwalimu wa awali uchelewe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, walimu wote wanapata mishahara yao katika utaratibu ule wa kawaida sambamba na walimu wengine katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Isipokuwa inawezekana kama nilivyosema awali katika majibu yangu ya msingi ya mwanzo kwamba inawezekana katika maeneo mengine watu walikuwa wanawachukua walimu kutoka mtaani, kutoka katika mfumo usiokuwa rasmi, ambao wazazi walikuwa wanachangia. Kwa sababu jukumu letu kubwa sasa tumepeleka walimu wengi wa grade „A‟, ili sasa waweze kufundisha yale madarasa ya awali kama ilivyokusudiwa kwa sababu wamepewa ile package ya kufundisha watoto wa awali ili mradi matatizo hayo yote Mheshimiwa Ishengoma yatakuwa hayapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimeona, swali lako lilikuwa makini lakini huo ndiyo utaratibu, ambao tunaenda nao. Lengo letu ni kwamba, watoto wetu wapate elimu bora katika shule zetu.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Licha ya kupata majibu mazuri kutoka kwa Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa Mkoa wa Morogoro hauna hata hicho kituo cha kutolea mikopo na mafunzo ya ujasiriamali, je, kuna mikakati gani ya kuanzisha kituo hicho kwenye Mkoa wa Morogoro?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, kituo hicho kitaanzishwa lini? Ahsante
WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya 2016/2017, benki imetengewa shilingi bilioni 950. Kwa hiyo, nimuahidi kwamba katika mkoa ambao tutaupa kipaumbele ni Mkoa wa Morogoro ili tuweze kufungua dirisha la kuwawezesha wanaweke kupata mikopo. Hata hivyo, siyo katika Mkoa wa Morogoro tu tumepanga kwamba katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 tufungue dirisha maalum ambalo litawawezesha wanawake kupata mikopo yenye riba nafuu angalau kati ya asilimia 10 mpaka 12. Kwa hiyo, hili jambo tutaweza kulianza mara tu utekelezaji wa bajeti ya 2016/2017 utakapoanza.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Barabara ya Bigwa – Kisaki, Wilaya ya Morogoro Vijijini ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne na Awamu ya Tano kujengwa kwa lami. Mpaka sasa hivi hata kwenye bajeti iliyopita sikuona kitu chochote kinachoelezea kuwa itajengwa. Je, barabara hii kwa niaba ya wananchi wa Morogoro Vijijini itajegwa lini kwa kiwango cha lami? Ahsante
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumeongea na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo, ni kwamba hii barabara tutaijenga. Mheshimiwa Ishengoma anafahamu na tulishaongea kwamba hii barabara ambayo ni ahadi ya kiongozi wetu wa Kitaifa, tutaitekeleza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba kiwango kilichowekwa katika bajeti ya mwaka huu ni ya matengenezo peke yake, ujenzi tumeshindwa kuuweka safari hii kwa sababu tumetoa vipaumbele kwa zile barabara ambazo makandarasi wako site na tunataka tuwamalizie hawa makandarasi wasiendelee kulipwa fedha bila kufanya kazi. Kwanza, tuwalipe fedha ili wakamilishe barabara ambazo zilishaanza muda mrefu. Tukishamaliza hiyo, sisi baaada ya hapo, sina uhakika kama ni lugha nzuri, lakini sisi ni mwendo mdundo kutekeleza ahadi zote za viongozi wetu na ahadi zote zilizomo katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuanzia mwaka wa pili wa Awamu hii ya Tano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa naomba tupeni fursa ili tumalize kwanza hizi barabara ambazo zilikuwa zimeanza vipindi vya nyuma na wakandarasi wengi wako site wanapokea hela, interest na vitu vingine wakati hawafanyi kazi kwa sababu tulikuwa hatuna uwezo wa kuwalipa. Sasa tunafanya hilo, tukimaliza mwaka huu unaokuja hawa wote tutakuwa tumewamaliza na sasa tutaanza kutekeleza kwa kasi maeneo mengine yote ambayo viongozi wetu wakuu wameahidi na Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi imeongea
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mradi wa maji ni tatizo kweli, katika Wilaya ya Morogoro Vijijini, katika vijiji vya Furwe, Mikese, Gwata waliahidiwa mradi wa maji kwa muda wa miaka mingi, na wananchi wanateseka kwa maji kwa muda mrefu. Je, naomba kuuliza wananchi hawa ambao wameteseka kwa muda na wameahidiwa mradi wa maji watapata lini maji na mradi huu utatekelezwa lini?
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshatoa maelekezo katika kila Halmashauri namna ya kupanga vipaumbele katika vijiji ambavyo havina maji; sasa awamu hii ya kwanza siwezi kusema ni vijiji vipi vimepangwa, lakini Halmashauri yake inafahamu na wameleta vipaumbele na tumeweka kwenye bajeti na fedha zimetengwa. Kwa hiyo, sasa hivi ni ufuatilia tu utekelezaji, naomba nimuahidi Mheshimiwa Mbunge nitakaa naye ili kusudi niweze kuona hivyo vijiji anavyovisema vipo kwenye mpango wa mwaka huu au vipi, ili tuweze kuona namna ya kufanya.
MHE. DKT. CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii. Naomba kuuliza swali la nyongeza. Nashukuru sana kwa majibu ya Naibu Waziri kwa swali la msingi, lakini ningependa kuuliza kuwa kwa sababu Morogoro Vijijini hatuna mpaka sasa hivi Hospitali ya Wilaya na majibu yametolewa, naomba kuulizia je, inawezekana pia kuboresha Kituo cha Afya cha Dutumi ambacho mpaka sasa hivi na chenyewe kinatumika kwa kutupatia vitendea kazi? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Ishengoma ni Mbunge wa Viti Maalum kule na nimesema kwamba katika ziara yangu nina mpango wa kuja Mkoa wetu wa Morogoro. Lengo ni kutembelea Mkoa mzima wa Morogoro na kubaini changamoto zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Ishengoma najua ni mpiganaji wa siku nyingi sana katika eneo hili. Naomba nimhakikishie kwamba katika ziara yangu eneo hili tutakwenda kulitembelea na licha ya kulitembelea na kuangalia mipango ya pamoja jinsi tutakavyofanya, lakini nina maslahi mapana ya Mkoa wa Morogoro kwa sababu najua mkoa ule wananchi wanapata shida, wanatembea mbali, siyo jambo la kufichaficha.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna kila sababu, kipindi cha ziara yangu tufike eneo hilo, tushauriane kwa pamoja na linalotakiwa kufanywa kwa sasa tutalifanya, lakini linalotakiwa kuwekewa mipango mbadala kwa siku za usoni, tutalijadili kwa pamoja. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Ishengoma kwamba, katika hilo tutashirikiana kwa pamoja Mheshimiwa wangu.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Wananchi wa Tarafa ya Mikese, Wilayani Morogoro Vijijini, wameahidiwa muda mrefu mradi wa maji, lakini mpaka sasa wanapata taabu sana kwa kupata maji.
Je, ni lini wananchi wa Mikese watapata maji kusudi waondokane na tatizo hilo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niweke kumbukumbu sawa. Mheshimiwa Mama Ishengoma alikuwa
miongoni mwa Wajumbe wa Kamati ya Maji katika Bunge la Kumi na mimi tulikuwa katika Kamati moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri wakati ule Profesa Mark Mwandosya akiwa Waziri wetu wa Maji wa kwanza alikuwa akizungumzia sana suala zima la Mikese. Nadhani hapa tutakapo-table katika Bajeti ya Wizara ya Maji itakapofika, watazungumza jinsi gani Mfuko wa Maji ambao
mwaka huu tunatenga fedha kidogo za kutosha utagusa katika vijiji mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tusubiri Wizara ya Maji itakapokuja kuweka bajeti yake pale, tutajadili kwa upana zaidi jinsi gani tutawasaidia wananchi wa Mikese ambao najua kwamba kweli wana shida kubwa ya maji, lazima wapate mradi wa maji na ahadi ya siku nyingi.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri na Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya ngongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia 75 ya wakulima hapa Tanzania wakiwemo wakulima wa Mkoa wa Morogoro wanategemea kilimo kwenye uchumi wao. Serikali ina mkakati mzuri wa kupunguza bei kwenye mbolea kusudi iweze kuwa nafuu kwa wakulima. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanzisha viwanda vya mbolea hapa nchini sambamba na Kiwanda cha Minjingu na Kiwanda cha Mtwara kinachotegea kujengwa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mbolea hasa ya DAP pamoja na UREA ni mbolea ambayo zinatumika sana kwenye kilimo chetu, DAP ikiwa ni mbolea ya kupandia na UREA ikiwa ni mbolea ya kukuzia. Hapa nchini tuna mbolea ya Minjingu ambayo inazalishwa Manyara.
Je, mbona haijawekwa kwenye mkakati huu kusudi wananchi waweze kupata hamasa ya kutumia mbolea ya Minjingu? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala la Serikali kuanzisha viwanda, ni kweli kabisa kwamba Serikali ya Awamu ya Tano moja kati ya mikakati yake ya kuendeleza uchumi ni kuhakikisha kwamba kunakuwa na viwanda nchini. Kwa hiyo, Serikali imekuwa ikihimiza na kuweka mazingira wezeshi ili sekta binafsi na wadau wengine waweze kuanzisha viwanda nchini. Kwa sasa Serikali iko katika mikakati ya kushirikiana na sekta binafsi kuanzisha kiwanda cha mbolea Mkoani Lindi kwa kutumia gesi; na utaratibu huo ukikamilika, tunaamini kwamba mahitaji mengi ya mbolea yatakuwa yamepata suluhu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuna kiwanda cha mbolea kinajengwa Kibaha, kwa hiyo, tunaamini kwamba kadiri miaka inavyokwenda, tutakuwa tunazalisha mbolea zetu humu nchini, kuliko kuagiza ambayo inatusababishia kuwa na gharama kubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba katika utaratibu wa bulk procument (uagizaji wa mkupuo) tunaanza na mbolea za DAP na UREA, lakini baadaye tutaingia kwenye mbolea nyingine kama NPK na mbolea nyingine ambazo zinatumika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kwa nini hatujaweka mbolea ya Minjingu katika utaratibu huu? Ukweli wa mambo ni kwamba tunapozungumzia kuhusu uagizwaji wa mkupuo, tunazungumzia kuhusu mbolea kutoka nje.
Hata hivyo, bado kuna fursa ya kuendelea kuhimiza kiwanda cha Minjingu kiongeze uzalishaji, kwa sababu kwa sasa uwezo wao kwa mwaka ni tani 50,000 wakati mahitaji yetu ya mbolea ya aina hiyo kwa mwaka ni zaidi ya tani nusu milioni. Kwa hiyo, vilevile kuna suala la uwezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Serikali iko tayari kushirikiana na Minjingu waongeze uzalishaji ili mbolea yao iweze kutumika kwa wingi zaidi.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa ni mpango wa Serikali kuanzisha Vyuo vya VETA katika kila Wilaya: Je, kuna mkakati gani wa kuanzisha mkondo wa kilimo na uvuvi katika kila Chuo cha VETA kinachoanzishwa kwenye Wilaya zetu ili kuongeza Maafisa Ugani hawa wa kilimo na uvuvi ambao wanaweza kufanya kazi kwenye vijiji vyetu na kuinua kilimo chetu na uvuvi?
WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo la Mheshimiwa Ishengoma ni zuri sana. Nitaiagiza mamlaka yetu ya FETA iwasiliane na VETA kuona ni namna gani wanaweza kushirikiana katika kutekeleza wazo lake. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Manispaa ya Morogoro kumekuwa na tatizo kubwa la maji hasa kwenye mitaa kama mitaa ya Mlima Kola, Lukobe, Foko land, Manyuki na mitaa mingine na kwa kuwa Serikali inafanya vizuri; naishukuru Serikali ya Ufaransa na ya Tanzania kwa kupata fedha hizo Euro milioni 70; lakini napenda kujua mradi huo ni lini utakamilika ili wananchi ambao wamepata matatizo ya maji kwa muda mrefu wapate subira ya kupata maji?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pli, miradi ya maji katika Mji Mdogo wa Mikumi imechukua muda mrefu kiasi wananchi wa Mji wa Mikumi wana matatizo makubwa ya maji. Je, ni lini miradi hii itakamilika kusudi na wananchi waweze kupata maji safi na salama ya kutosha? Ahsante.(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa amesema Morogoro ina matatizo makubwa ya maji. Serikali imetambua hilo na imeweka miradi ya dharura, tunachimba visima vitano na visima viwili tayari vimeshachimbwa eneo la Kola. Visima viwili vinaendelea kuchimbwa eneo la SUA ili kuweza kupunguza tatizo la maji lililopo wakati tunasubiri utekelezaji wa mradi huu mkubwa. Hata Mbunge wa Jimbo Mheshimiwa Aboud, jana alikuwa ofisini nikawa nimepata taarifa hizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi tunaendelea vizuri na mhandisi tuliyemweka na tunatarajia ifikapo mwezi wa 12 atakuwa amemaliza, tutangaze tender. Baada sasa ya kumweka mkandarasi na kusaini mikataba, Mheshimiwa Mbunge tutajua sasa mradi utakamilika lini. Nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Morogoro kwamba tayari Serikali imeshaanza huo mradi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Mikumi sasa hivi tumekamilisha mradi mkubwa wa maji pale na nimeenda kutembelea na mradi umeanza kutoa maji tayari. Kwa hiyo, wananchi wa Mikumi tayari wanapata maji. Kama kutakuwa na upungufu, basi tutaendelea kuongeza kwa sababu watu wanazidi kuongezeka katika Mji wa Mikumi, lakini tayari mradi ule mkubwa umeshakamilika.
MHE. DKT. CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nashukuru kwanza kwa majibu mazuri ya Serikali, hata hivyo lakini nina maswali mawili mafupi. Swali la kwanza, kuwa wakulima wengi sasa hivi wamechangamkia kilimo cha miembe na kwa kuwa Serikali imetoa mwongozo wa mafunzo kwa Maafisa Kilimo 117 tu; na kwa kuwa ni vikundi 19 tu vimepewa mafunzo; je, Serikali haioni haja kuweka mpango wa kutoa mafunzo zaidi ya maafisa kilimo ili kuweza kueneza kilimo hiki cha miembe ambacho kimechangamkiwa sana na wananchi sasa hivi?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Serikali imekiri kuwa imeanza utafiti, naipa pongezi na kwa kuwa mpaka sasa hivi Serikali imetoa starter kit kwa kikundi cha wakulima ambacho kinalima maembe tu. Hiki kikundi cha wakulima sana kimejikita Mkoa wa Pwani ambapo Mikoa ya Morogoro, Tanga mpaka Zanzibar, Tabora wanalima maembe na kwa kuwa ni lita 560 tu za kivutia wadudu zimetolewa tu. Je Serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kutoa starter kit angalau moja kwa mikoa hii inayolima miembe na kuongeza hii dawa ya kivutia wadudu kwa mikoa hii ili wakulima waweze kuendelea na kilimo hiki cha miembe?
Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia nawapa hongera sana vijana wangu wa SUA na wajasiriamali na Chuo cha SUA ambao wanaeneza miche ya miembe, hongereni sana.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, kwanza nakubaliana nae kwamba mafunzo zaidi kwa Maafisa Kilimo yanahitajika na kwa fursa hii namwelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Engineer Mtigumwe aandae mafunzo zaidi na hasa kwa maeneo yaliyotajwa ambayo yanazalisha maembe zaidi.
Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu kugawa starter kit na dawa hii ya eugenol ya kivutia wadudu nayo nakubaliana nayo tutaangalia uwezekano wa kupata fedha zaidi ya kuweza kueneza hizi starter kit kwa vikundi vya wakulima zaidi ya hicho kikundi kimoja kilichopata.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pia nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Sasa naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa ni sera na mpango wa Serikali kila wilaya kuwa na hospitali, je, ni lini ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini utaanza licha ya jitihada nyingi za Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni lini ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mvomero utakamilika?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) : Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba ni sera ya Serikali kujenga hospitali moja kila wilaya na napenda nimhakikishie Mheshimiwa Dokta Ishengoma na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba Serikali itaendelea kuwezesha ujenzi wa hospitali moja kila wilaya kwa awamu. Katika Mkoa wa Morogoro tumeanza na Manispaa ya Morogoro na tutaendelea na wilaya nyingine kwa awamu zinazofuata. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wangu, katika sehemu ya pili ya swali lake Mheshimiwa Dokta Ishengoma kuhusu Hospitali ya Mvomero na bahati nzuri tulikuwa pale Mvomero tukabaini baadhi ya upungufu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeshatenga fedha ya kumalizia jengo lile baada ya kuona upungufu ule na imani yangu ni kwamba kabla ya mwezi Januari hospitali ile itakuwa imekamilika ili wananchi wa Mvomero waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Hospitali ya Tumbi ni hospitali ambayo ilikuwepo tangu enzi za Nordic countries, wakati huo ikiwa chini ya Nordic countries kama chini ya shirika. Ilikuwa inatoa huduma nzuri sana, lakini mpaka sasa hivi huduma yao imefifia, je, Serikali ina mpango gani wa kufuatilia huduma za Hospitali ya Tumbi ambayo inatolewa kwa wananchi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tukumbuke kwamba, Mheshimiwa Mbunge alikuwa Mkuu wa Mkoa ule wa Pwani kipindi hicho na naamini kwamba anaijua vizuri hospitali hiyo ndiyo maana swali lake limekuwa la msingi sana juu ya kuiboresha hospitali hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mwanzo ilikuwa inatoa huduma nzuri zaidi, lakini tukikumbuka zamani population ya watu waliokuwa wakitibiwa katika hospitali hiyo ni tofauti na hivi sasa. Hivi sasa takriban wagonjwa kati ya 300 mpaka 500 wanafika pale kila siku na wengine wanaolazwa. Kwa hiyo, idadi ya watu wanaotibiwa kwa sasa hivi ni kubwa zaidi kuliko hapo mwanzo na ndio maana sasa hivi Serikali imehakikisha inashirikiana na wadau mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kumshukuru Mbunge wa Kibaha Mjini na Serikali kwa ujumla, katika harakati zilizofanyika angalau sasa hivi kuna mashirika mbalimbali kama wenzetu kutoka Korea na taasisi zingine wametusaidia vifaa mbalimbali kwa lengo la kuboresha hospitali ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la awali ni kwamba, mwaka huu tumetenga shilingi bilioni 1.4, lakini tutaendelea kuhakikisha tunafanya kila liwezekanalo hadhi ya Hospitali ya Tumbi iweze kuwa nzuri zaidi kwa sababu sio Wanapwani wanaotibiwa pale peke yake isipokuwa wananchi wote ambao wanapita katika ukanda wa barabara hiyo, wakipata matatizo hospitali ya Rufaa ya Tumbi ni Hospitali ya karibu ambayo ni kimbilio la wananchi wengi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, naomba nikuahidi kwamba Serikali inalitazama kwa macho ya karibu zaidi jambo hilo na ndiyo maana Waziri wetu wa Afya, Naibu Waziri, walikwenda pale na Waziri wangu wa nchi alifika pale katika kutembelea Shirika la Elimu Kibaha kuangalia changamoto za pale. Katika mwaka huu wa fedha tutapambana kwa kadri iwezekanavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka uliopita ilitengwa milioni 700 haikuweza kupatikana, tutapambana mwaka huu ili bajeti iweze kupatikana ili hadhi ya Hospitali ya Tumbi iwe kama vile ilivyokuwa pale awali.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri bado nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, licha ya elimu kutolewa lakini bado kuna matatizo kuhusu haki ya ardhi. Sasa Serikali inaonaje kutoa kipindi maalum, narudia, kipindi maalum kwa muda muafaka kwenye luninga au kwenye redio kusudi elimu hii iwafikie hasa wanawake kwa wakati muafaka na kwa muda muafaka?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa sehemu kubwa ya ardhi inatumiwa sana na wanawake; kama asilimia 70 wanawake wanatumia hii ardhi hasa kwa uzalishaji mali hasa kwa kilimo. Hata hivyo wanawake hawa hawana maamuzi kuhusu ardhi hii. Je, Serikali inatoa kauli gani hasa ya kueneza elimu hii na kutokana na kwamba kwenye makabila mengine bado kuna mfumo dume ambao hauwapi ridhaa wanawake kumiliki ardhi? ahsante.
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Dkt. Christine Gabriel Ishengoma kwa sababu alifanya utafiti mmoja ambao ulikuwa ni utafiti mzuri sana kuhusu mfumo wa kumiliki ardhi kwa watu wanaotoka katika makabila ambayo ni matrilineal au matriarchal. Yaani wale ursine local matriarchal wa makabila ya Pwani kama Wazaramo, Wakwere, Wakutu, Waluguru, Wanguu, Wakaguru lakini pia wale matrilineal ambao ni Wamwera, Wayao, Wamakua, Wamakonde na kuonesha ni jinsi gani katika maeneo hayo mfumo ule ambao sasa sijui ni mfumo jike, lakini umiliki wa ardhi unatoa maeneo ambayo yangesaidia watu wa mfumo dume kujifunza; na labda ndiyo maana katika historia ya Bunge letu wanawake wengi mwanzoni walioshinda Ubunge wa Majimbo walitoka maeneo hayo ya Wamwera, Wayao, Wamakua na Wamakonde. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nakubaliana naye kwamba kuna umuhimu wa kuwa na kipindi maalum cha mambo ya ardhi katika luninga na redio kwa wakati muafaka ili wanawake wengi wakisikie. Kwa hiyo, nachukua fursa hii kumuahidi kwamba nitaongea na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ili kuandaa vipindi hivi kwa wakati muafaka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili, niseme tu kwamba tuendelee kuelimishana kuhusu umuhimu wa wanawake kumiliki ardhi hasa katika maeneo ya mfumo dume. Vilevile pia niwaombe Mahakimu na Majaji wengi waelewe umuhimu na utofauti wa umiliki wa ardhi katika maeneo ya Tanzania ya Pwani na Kusini yenye mfumo jike katika kumiliki ardhi kwa sababu hukumu zao zimekuwa hazielewi kwanini katika maeneo hayo wanawake wana sauti ya maamuzi. Na kwa maana hiyo basi tuendelee kuimarisha jambo hili ili mwisho wa siku jinsia zote mbili ziwe na haki sawa katika umiliki wa ardhi. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naomba kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, mradi wa maji wa visima Gairo umekamilika lakini kwa bahati mbaya maji haya ni ya chumvi kiasi wananchi wanapata shida kuyatumia. Je, mradi wa maji ambayo hayana chumvi kutoka milima ya Nongwe utakamilika lini? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tulichimba visima saba pale Gairo vina maji mengi lakini yale maji hayafai kwa matumizi ya binadamu. Ndani ya ule mkataba tulikuwa tumepanga kununua mashine kwa ajili ya kitu wanaita desalination tumeiondoa hiyo badala yake tumeenda kutafuta sasa visima kwenye milima iliyoko na Gairo na ripoti yake inakamilika leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuwasiliane na Mheshimiwa Mbunge wiki ijayo tutapata majibu tunataka sasa tuchukue maji kutoka kule milimani ambayo hayana chemicals tuyalete pale Gairo ili wananchi wapate maji yaliyo safi na salama, tutatumia miundombinu ile ambayo imeshajengwa iko pale Gairo.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali fupi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Manispaa ya Morogoro licha ya mipango mizuri ya Serikali imekuwa na matatizo kweli ya maji. Je, kuna mkakati gani wa kuanzisha vyanzo vingine vya maji katika Manispaa ya Morogoro ikiwa ni mkakati wa muda mfupi? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, mahitaji halisi kwa sasa ya Mji wa Morogoro ni lita 45,000 mita za ujazo kwa siku, lakini Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira (MORUWASA) yanatoa maji 34,000 lita za ujazo kwa siku; kwa hiyo kuna uhaba katika suala zima la maji. Serikali kwa kuona haja ya kuongeza kiwango cha maji ndiyo maana tupo katika utaratibu wa kusaini Euro milioni 70 katika kuhakikisha tunaondoa kabisa tatizo la maji katika Mji wa Morogoro.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Ni lini Serikali itakamilisha kutengeneza Barabara ya Bigwa – Kisaki kwa kiwango cha lami ikiwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKA): Mheshimiwa Naibu Spika, nimelitembelea eneo hili la barabara kutoka Bigwa – Kisaki kwenda mpaka Dutumi, nimeona upo umuhimu wa kufanya maboresho mbalimbali pamoja na kupanua madaraja. Ukienda upande wa Dutumi lipo daraja jembamba sana. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia eneo hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la barabara hii ni muhimu kwa sababu tunategemea pia barabara hii kupitisha mitambo na vifaa vingine wakati wa ujenzi wa umeme kule Stiegler’s Gorge kilometa 189 kutoka Ngerengere.
Kwa hiyo, tutaitazama barabara hii na ni muhimu. Kwa sasa kuna fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya kuboresha ili huduma ziendelee kufanyika wakati tunaendelea kujipanga kutengeneza hii barabara kwa kiwango cha lami.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Licha ya majibu mazuri, nina maswali mawili mafupi ya kumuuliza.
Kwa kuwa mpaka sasa hivi tafiti zinaendelea hapa duniani kuhusu ugonjwa wa kisukari, lakini mpaka sasa hivi azijazaa matunda, napenda kujua; je, tafiti hizi zimehusishaje tiba mbadala au tiba asilia kuhusu kutibu ugonjwa huu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa ugonwja huu umeenea sana na unaleta vifo na inaonekana kuwa inawashambulia pia watoto wadogo na wajawazito na njia mojawapo inahusisha mambo ya lishe; je, kuna mkakati gani wa kutoa elimu kwa watu wote na hasa tukianza na Waheshimiwa Wabunge humu ndani kuhusu ugonjwa huu wa kisukari na hasa na mambo ya lishe? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli sisi kama Serikali, tunatambua kwamba sasa hivi hatuna tiba dhidi ya ugonjwa wa kisukari, lakini Serikali vilevile inatambua umuhimu wa tiba asili na tiba mbadala, ndiyo maana ndani ya Wizara ya Afya tuna Kitengo Maalum ambacho kinasimamia tiba asili na tiba mbadala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kupitia taasisi zetu za Utafiti za Magonjwa ya Binadamu (National Institute of Medical Research) na Taasisi ya Tiba Asili ambayo iko Muhimbili, tumekuwa tunaendelea kufanya utafiti wa tiba mbalimbali ambazo zinapunguza kiwango cha sukari mwilini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, hatujapata tiba mbadala, lakini mtu yeyote ambaye amekuja na dawa ambayo anadhani inaweza kusaidia kupunguza makali ya ugonjwa wa kisukari, tumekuwa tunazifanyia utafiti na kuziangalia ili ziweze kutumika kwa binadamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ameuliza kuhusiana na masuala ya lishe. Serikali mwezi Julai, 2017 imezindua mkakati wa Kitaifa wa masuala ya lishe na uzinduliwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu na lengo ni kuhakikisha sasa tunaongeza nguvu na kuongeza juhudi kuhusiana na magonjwa ya kuambukiza. Magonjwa ya kuambukiza yanazidi kuongezeka. Tunakadiria kwamba wastani wa asilimia 13 za Watanzania wana ugonjwa wa kisukari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nasi tunaendelea kuhamasisha wananchi pamoja na Waheshimiwa Wabunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi tunavyoongea hapa Bungeni, wenzetu wa Bima ya Afya tumeleta Madaktari Bingwa wa magonjwa yote pamoja na kisukari na mimi nitoe rai kwa Waheshimiwa Wabunge, twende pale kliniki tupime afya zetu; siyo suala tu la Kisukari lakini magonwja yote pamoja na Saratani huduma hizi zinapatikana Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niishie kwa kutoa rai kwa wananchi wa Tanzania, magonjwa yasiyoambukizwa ikiwa ni pamoja na kisukari na shinikizo la damu, yanatokana kwa kutozingatia masuala ya lishe, kutofanya mazoezi na matumizi yaliyopindukia ya vilevi na sigara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kuwasisitiza Watanzania kuzingatia msingi ya afya bora. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini nina maswali mawili mafupi.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa wavuvi wana-complain kuwa hawapati elimu ya uvuvi ambao unatakiwa na wanaopaswa kusimamia ni Afisa Ugani lakini mara kwa mara hawafanyi hivyo. Je, Serikali inafanyaje kusudi kuwapatia elimu ili hawa wavuvi waweze kuelewa ni nyavu zipi zinazotakiwa? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa ufugaji wa samaki kwa kutumia mabwawa au fish ponds wananchi wameitikia kwa nguvu lakini bado hawajapatiwa elimu sawasawa. Je, Serikali ina mkakati gani wa kutoa elimu hii ya ufugaji wa samaki wa mabwawa ili kupunguza utapiamlo pamoja na kuinua kipato na kuhamasisha wananchi wa mikoa yote waweze kufuga ukiwepo na Mkoa wangu wa Morogoro maana hata wanawake wanaweza wakafuga kwa mabwawa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma na nichukue fursa hii kumpongeza sana kwa ufutiliaji na umakini wake katika kuona sekta hii ya uvuvi na kilimo zinasonga mbele.
Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza anataka kujua namna ambavyo sisi Serikali tumejipanga katika kuwasaidia wananchi wetu katika kupata elimu ya kujua ipi ni nyavu halali na ipi isiyokuwa nyavu halali, hasa ikizingatiwa kwamba Maafisa Ugani wetu hawafanyi kazi yao ipasavyo. Nataka nimhakikishe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imejipanga vyema na ndiyo maana katika mabadiliko na maboresho ya sheria ambayo tunakwenda nayo katika mwaka huu, katika jambo moja kubwa tutakalolifanya ni pamoja na kuhakikisha tunaziboresha BMUs zetu, kwa sababu BMUs ni mali ya wananchi wenyewe na zinachaguliwa na wananchi wenyewe. Tuna hakika kwamba kwa kufanya hivyo tutakuwa tumewafikia wananchi, wapeane elimu waweze kujua.
Mheshimiwa Spika, lazima niseme ukweli kwamba bahati nzuri nyavu zinazotumika ni chache. Kwa mfano, nyavu ya dagaa kwa upande wa ziwani inafahamika wazi kwamba ni nyavu inayotakiwa kuwa na jicho lisilozidi au lisilopungua milimita nane. Kwa hivyo, mtu anapokwenda akanunua nyavu inayoshuka chini ya ukubwa wa milimita nane hilo jambo tayari amevunja sheria. Kwa upande wa baharini, inafahamika wazi kwamba ni nyavu isiyopungua ukubwa wa milimita 10. Kwa hivyo, kwa wavuvi ambao hiyo ndiyo shughuli mara nyingi wamekuwa wakifahamu.
Mheshimiwa Spika, swali la pili anataka juu ya mkakati wetu kama Serikali. Naomba nimhakikishie habari njema kabisa kwamba sisi kama Serikali katika moja ya jambo kubwa tunalokwenda kulifanya sasa ni kuhakikisha vituo vyetu vyote vya uzalishaji wa vifaranga vya samaki nchi nzima, Kituo kama kile cha Morogoro pale Kingolwira na vingine vya Luhira kule Songea na Mwaipula kule Tabora vyote tunakwenda kuviboresha ili tuweze kuzalisha vifaranga vya kutosha na hatimaye wafugaji wetu waweze kuvipata.
Mheshimiwa Spika, lakini lingine ni kuhakikisha tunakwenda sambamba na wenzetu wa Wizara ya Fedha kwa sababu tumeshapeleka mapendekezo yetu ya kupunguza tozo na kodi mbalimbali ambazo ndizo zimekuwa kikwazo katika uwekezaji kwenye eneo hili la ufugaji wa samaki. Naomba tu Mheshimiwa Mbunge na wadau wengine wote waendelee kujipanga kuhakikisha kwamba huko iko fursa ya kuendeleza sekta hii ya uvuvi.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipatia swali la nyongeza.
Je,ni lini Serikali itaendeleza ujenzi wa barabara ya Ludewa - Kilosa - Mikumi kwa kiwango cha lami? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabra aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge tayari ilikwishafanyiwa upembuzi yakinifu na ikafanyiwa usanifu wa kina na hivi karibuni tumekwishapata fedha ambayo itaanza kutekeleza mradi huo awamu kwa awamu. Kwa hiyo, tunamuomba Mheshimiwa Mbunge na ninamshukuru sana kwa kufuatilia sana barabara za Mkoa wa Morogoro ambazo zinaunganisha avute subira ataona wakandarasi wakiwa eneo la kazi kwa ajili kutekeleza barabara hiyo muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, namshukuru Naibu Waziri amejibu vizuri lakini waendesha bodaboda hawa wengi hawana ujuzi wa Sheria na Kanuni za Barabarani. Je, kuna mkakati gani wa kuwapatia elimu hii ili kusudi waweze kuepukana na usumbufu na faini wanazozipata?
Swali la pili, kwa kuwa usafiri wa bodaboda unatoa usafiri kwa watu wengi lakini waendesha bodaboda hawa hawana leseni na hawana ujuzi wa kuendesha pikipiki hizi, kiasi kwamba wanasababaisha ajali nyingi na vifo.
Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti tatizo hili? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la elimu kuna jitihada mbalimbali ambazo zinafanyika katika kutoa elimu kwa waendesha bodaboda. Miongoni mwa jitihada hizo ni kwanza Jeshi la Polisi limekuwa likitumia utaratibu wa kuwafuata kwenye vijiwe vyao hawa ambao wanaendesha bodaboda na kuwapa elimu, pia kupitia vipindi mbalimbali ambavyo vinaandaliwa kwenye television, kwenye radio na kupitia kwenye wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani ambavyo vinatumika kwa ajili ya kutoa elimu, kwa hiyo jitihada za kutoa elimu zinafanyika kwa kiwango kikubwa sana.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali lake la pili kwamba vijana ambao wanaendesha bodaboda bila leseni. Kwanza nichukua fursa hii kuendelea kusisitiza kwamba kuendesha bodaboda ama chombo chochote cha usafiri bila leseni ni kuvunja sheria na hivyo basi Jeshi la Polisi litaendelea kuwachukulia hatua wale wote ambao wanakiuka sheria za nchi katika eneo la usalama barabarani ikiwemo kuendesha bodaboda bila leseni. Kwa hiyo, nitoe wito kwa vijana wetu ambao hawana leseni kufuata taratibu za Kisheria ili waweze kujipatia leseni.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, hata hivyo nina maswali mawili mafupi.
Swali la kwanza; katika baadhi ya Wilaya, Vijiji pamoja na Kata mpango huu wa kupima ardhi mpaka kupata hatimiliki unachukua muda mrefu kiasi wananchi wanasumbuka, wanahangaika wakifuatilia hati zao. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi hawa kusudi waweze kutumia muda mfupi wasitumie muda mrefu na Hatimiliki zao ziweze kupatikana kwa muda mfupi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; napongeza Serikali kwa kuanza kupima ardhi kwenye Mkoa wa Morogoro katika Wilaya za Ulanga, Kilombero pamoja na Mvomero; na huu mpango wa kupima ardhi unapunguza migogoro ya ardhi kwa upande wa wafugaji pamoja na wakulima.
Je, nauliza Serikali, mpango huu utakamilika lini kwa kupima ardhi kwenye Mkoa wote wa Morogoro kwenye Wilaya zake saba ambazo itasaidia kutatua migogoro ya ardhi ambayo imekithiri kwa muda mrefu katika Mkoa huu wa Morogoro? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA YA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza amesema kwamba mpango wa matumizi bora ya ardhi unachukua muda mrefu na hatimaye watu wanachelewa kupata hati zao. Napenda tu nilifahamishe Bunge lako, mpango wa matumizi bora ya ardhi hauwezi kwenda kwa kasi kama tunavyotarajia kwa sababu inategemea pia maridhiano kati ya wanakijiji na matumizi yao katika maeneo yale ambapo unapoandaa mpango huo lazima uhusishe makundi yote ya wafugaji, wavuvi na kila watu walioko pale na lazima pia waangalie ukubwa wa ardhi yao waliyonayo na mpango wanaotaka kuweka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, lazima uende taratibu kuhakikisha kila mmoja ameshirikishwa na amekubaliana na mpango, sasa hatuwezi kwenda kwa kasi kwa sababu unashirikisha. Pengine labda elimu iendelee kutolewa hata kabla hatujafika sisi basi elimu iendelee kutolewa ili watu waone umuhimu wa kupanga mpango wa matumizi bora ya ardhi katika maeneo yao ili kuepusha migogoro ambayo mara nyingi inajitokeza.
Swali la pili, Mheshimiwa Mbunge anaulizia ni lini tutakamilisha kupima ardhi yote katika Mkoa wa Morogoro na kuondoa migogoro iliyopo. Napenda nimhakikishie tu kwamba mpango wa Wizara tulionao siyo wa Morogoro tu, Morogoro ilikuwa ni eneo la mfano katika zile Wilaya tatu ambazo zilikuwa na migogoro pia ili kuweza kujua gharama za upimaji tukitaka kupanua mpango huu utatugharimu kiasi gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naona kwamba zoezi lile pale limekwenda taratibu sana kwa sababu linahusisha Wananchi na pia kuweza kujua tunawezaje kukamilisha kupima katika nchi nzima. Ni mpango wa Wizara kuhakikisha kila kipande kinapimwa sasa uzoefu wa Morogoro utatusaidia ku-scale up upimaji na kuweza kujua gharama halisi zinazoweza kutumika na mpango huu tunaendelea nao na kwenye bajeti pia tumeonesha hivyo naomba tu Waheshimiwa Wabunge wawe na subira wakati Wizara inajipanga vizuri.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, hata hivyo nina maswali mawili madogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa kilimo cha bustani kinamtoa mkulima na hasa akinamama na vijana kwenye umaskini kwa uharaka na kupata ajira, lakini licha ya kuwaunganisha na pamoja na TAHA na SAGCOT kuwasaidia wakulima hawa, tatizo kubwa wanalolipata ni mitaji. Je, kuna mkakati gani wa kuwasaidia kupata mikopo nafuu ili akinamama hawa na vijana wanaoshughulika na kilimo cha bustani waweze kupata mikopo hiyo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, licha ya kuwaunganisha na kuanzisha viwanda kwenye mikoa mbalimbali, Mkoa wa Morogoro ni Mkoa unaolima sana mbogamboga na matunda. Je, kuna mkakati gani wa kuweka wawekezaji katika Mkoa wa Morogoro kuanzisha kiwanda cha matunda na mbogamboga? (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tatizo la mitaji limekuwa ni moja ya changamoto zinazowafanya wakulima hao hasa ambao wanajihusisha na shughuli za mbogamboga na bustani washindwe kufanya vizuri zaidi. Hata hivyo, kwa kuwa halmashauri zetu zinayo asilimia 10 ambayo inawasaidia akinamama, vijana na watu wenye ulemavu katika kupata mitaji, ni vema Halmashauri basi zielekeze nguvu katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwa kupitia Mfuko wetu wa NEDF ambao uko katika Shirika la SIDO, tutahakikisha kwamba hawa wananchi wanafikiriwa zaidi katika kuhakikisha kwamba wanapata mikopo ya aina hiyo pamoja na taasisi nyingine za kifedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili kuhusu kuhamasisha viwanda, Wizara imekuwa ikiendelea kuhamasisha viwanda mbalimbali viweze kuwekeza katika nchi yetu na Mkoa wa Morogoro ambao umeonesha kuwa na fursa kubwa za mbogamboga na matunda. Vilevile, sasa hivi nchi ipo katika majadiliano ya mkataba ambao utawezesha kuwa na soko huru la Afrika litakayowezesha mitaji ya aina mbalimbali kuweza kuingia katika nchi ikiwepo na Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msingi huo tunaamini kwamba, wawekezaji wengi watakuwa na ari ya kuja hasa baada ya kuona kwamba sasa fursa hizo zinafunguliwa na baadhi ya kodi zisizo za lazima au vikwazo vinapunguzwa ili waweze kuwekeza zaidi. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Mzumbe – Mgeta ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne kujengwa kwa kiwango cha lami. Je, ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, uko utaratibu wa kuratibu ahadi zote za viongozi wetu wakuu kuhusu ujenzi wa miundombinu hii ya barabara. Kwa hiyo, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia barabara hii ya Mgeta, tutaitazama kadiri itakavyowezekana tuweze kuijenga kwa kiwango cha lami. Nilikuwa nimepata kabrasha kwa maana ya kuziangalia ahadi zote za viongozi kuanzia Awamu zilizopita mpaka sasa hivi, labda hata baadaye tunaweza tukazungumza ili tuone tumejipanga vipi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini fursa zimekuwa nzuri kwa kuwa zile harakati za kuunganisha mikoa hatua iliyofikiwa ni nzuri sasa tutakwenda kuunganisha wilaya na mikoa. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge avute subira lakini tutazungumza ili tuione sasa kwenye strategic plan yetu kwamba barabara hii tumeipangia nini. Muhimu zaidi ni kuhakikisha kwamba ahadi zote ambazo viongozi wakuu wamezitoa na sisi kama Wizara tunazitekeleza ili kutekeleza ahadi za viongozi.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali dogo. Barabara ya Msangani –Kwa Mathias ni sawasawa na barabara ya Ifakara – Mlimba kwa umuhimu wake kwa uzalishaji wa mpunga. Je, ni lini barabara hii ya Ifakara – Mlimba itajengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Serikali inatambua umuhimu wa kuboresha maeneo haya, kwa sababu maeneo haya ambayo Mheshimiwa Mbunge anayazungumza ni korido ambalo lina uzalishaji mkubwa wa mazao ya mahindi na mazao ya mpunga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kuanzia Kidatu sasa ujenzi wa kilomita 66 unaendelea kwenda Ifakara na ili tuweze kuwa na muunganiko mzuri, hii barabara ya kutoka Ifakara kwenda Mlimba na kutoka Mlimba kwenda Madeke itaenda kuungana na wenzetu kule upande wa Njombe. Barabara hii tayari iko kwenye utaratibu, mchakato wa kuitengeneza barabara hii na kuiboresha kwa kiwango cha lami unaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, huduma zitakuwa nzuri pia kwa wananchi ambao wako maeneo haya ya Mlimba tutaweza kuwaunganisha na wenzao wa upande wa Malinyi, kwa maana tutakuwa na kivuko ambacho tutakiweka ili kuboresha huduma ya mawasiliano ya huko.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Licha ya majibu mazuri ya Naibu Waziri nina maswali mawili mafupi ya kuuliza. Swali la kwanza; kwa kuwa tafiti bado zinaendelea kwenye Taasisi zetu hapa nchini na mara kwa mara tafiti hizi huchukua muda mrefu ili mbegu ziweze kutolewa na kuthibitishwa na kuanza kutumika kwa wakulima. Je, kwa msimu huu kuna mkakati gani wa Serikali wa kuwawezesha wakulima kupata mbegu hizi ambazo hazipatikani mara kwa mara?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; kwa kuwa viwanda vyetu vinakabiliwa sana na tatizo hili la malighafi ya alizeti ili viweze kuzalisha mafuta ya kutosha ya alizeti ambayo ni mazuri sana kwa upande wa lishe. Je, kuna mkakati gani wa kuhamasisha wakulima katika mikoa mbalimbali hapa nchini ili waweze kulima zao hili la alizeti ili tuweze kupata mafuta ya kutosha hapa nchini?
Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA):
Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kama nilivyotangulia kujibu kwenye swali la msingi, kuna mbegu zaidi ya aina tano mpya zimeshasajiliwa na vituo vyetu ambavyo nimevitaja. Kwa hiyo lile tatizo la zamani, kwamba mbegu ya record ilikuwa haizalishwi vizuri na haitoi mafuta vizuri lilishamalizika kwa sababu vituo vyetu hivi vya utafiti vimefanya utafiti na vimeshaiboresha. Kwa hiyo sasa hivi inazalisha zaidi ya asilimia 48 mpaka 50.
Mheshimiwa Spika, kuanzia sasa ni kwamba mbegu hizi zinapatikana, tuna mawakala tumewaongeza kwa hiyo sasa upungufu huo hautakuwepo. Pia tumeweza kuendeleza shamba letu la Msimba. Tumeshapata wafadhili, wadau wa maendeleo na Serikali, tumeongeza bajeti kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji kwenye shamba la Msimba kule Kilosa ili kuongeza uzalishaji wa mbegu na kumaliza tatizo hili.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuhusu mikakati ya kuhamasisha wananchi. Mikakati hiyo kama Serikali tumeshaianza.
Mheshimiwa Spika, mkakati wa kwanza ni kuingiza mazao yote yanayotakana na mbegu za mafuta kwenye zao la kimkakati, mbegu za mafuta kwa maana ya alizeti, michikichi, nazi, karanga, ufuta, soya na mengineyo, yote sasa tutayaundia bodi kwa ajili ya usimamizi wa kuzalisha mbegu hizi na kumaliza tatizo la upatikanaji wa mazao ya mbegu ya mafuta nchini na kuongeza uzalishaji wa mafuta wa hapa hapa nchini badala ya kuagiza nje ya nchi .
Mheshimiwa Spika, lakini pia katika hamasa hiyo tumeanza kama miezi miwili iliyopita Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Majaliwa Kassim Majaliwa pamoja na Wizara ya Kilimo tulikwenda Mkoani Kigoma kwa ajili ya kufua na kuhamasisha uzalishaji wa mazao ya mbegu mafuta nchi nzima kwa kuanzia na zao la michikichi. Kwa hiyo mikakati hiyo ndani ya Serikali tumeshaianza na hivyo nimwondoe hofu tu Mheshimiwa Mbunge; Serikali tunalitambua hilo. Lengo letu kubwa ni kuanza kujitosheleza kuzalisha mafuta ndani ya nchi ili tuweze kuokoa fedha za kigeni .
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru sana kwa majibu ya Naibu Waziri, ni kweli muda mfupi umeanza ambao ni mzuri sana, ambao wanaweza wakatoa maji kwenye kata mbalimbali, lakini kuna Kata ya Magadu ambao waliahidiwa maji, ambao hakuna maji kabisa na ilikuwa wachimbiwe kisima cha muda mfupi angalau waweze kupata maji, lakini mpaka sasa hivi Kata ya Magadu wana shida sana ya maji. Je, ni lini wataweza kupatiwa hicho kisima au kuchimbiwa maji wakaweza wakapata maji?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, mradi huu ambao unafadhiliwa kwa Euro milioni 70 umechukua muda mrefu na tukiwa tunasubiri kwa muda mrefu wa miaka zaidi ya mitatu sasa tunaambiwa kuwa imebaki kusainiwa; je, kwa sababu wananchi wa Morogoro Manispaa wanategemea maji yao kutoka bwawa la Mindu, kuna mkakati gani wa muda mfupi ambao Serikali inaweza ikafanya kukarabati bwawa la Mindu?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge, mama yangu, Mheshimiwa Christine Ishengoma, kwa kazi kubwa ambayo anaifanya katika kuhakikisha anawasemea wananchi wake wa Mkoa wa Morogoro. Kubwa ni kuhusu suala zima la maji katika Kata ya Magadu. Nimuagize tu Mhandisi wa Maji wa Mkoa, sisi ni Wizara ya Maji, siyo Wizara ya ukame, ahakikishe anasimamia suala hili la uchimbaji wa kisima wananchi wa Magadu waweze kupata maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala zima la mradi huu mkubwa wa Euro milioni 70. Tunapozungumzia maji, ni rasilimali muhimu sana, lakini sasa hivi Morogoro kumekuwa na uhitaji mkubwa sana, uzalishaji wetu sisi ni lita milioni 30 lakini kutokana na ongezeko la watu pamoja na taasisi na viwanda, kumekuwa na uhitaji wa zaidi ya lita milioni 59 na ndiyo maana sisi kama Serikali tukaona haja sasa ya kuwekeza kwa maana ya kuongeza bwawa la Mindu, katika kuhakikisha kwamba linakuwa na uzalishaji mkubwa ili wananchi wa Morogoro waweze kupata maji safi, salama na kuweza kukuza uchumi wao.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kilio hiki cha muda mrefu, lakini kubwa nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, utekelezaji wa miradi ya maji unategemeana na fedha, kwa hiyo, pamoja na utoaji huu wa fedha lazima tufuate utaratibu. Nataka nimtie moyo kwamba wawe na subira, subira yavuta heri na heri itapatikana katika upatikanaji wa maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimwia Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Katika Gereza la Morogoro Mjini kuna msongamano mkubwa sana wa mahabusu na wafungwa hasa kwa upande wa wanawake. Je, kuna mkakati gani wa kupunguza msongamano huu wa wafungwa na mahabusu hasa wanawake kwenye Gereza la Morogoro?
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mkuu wa Mkoa Mstaafu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kuna msongamano kwa wafungwa na mahabusu katika magereza mbalimbali katika nchi yetu. Gereza alilolisema Morogoro ni mojawapo ya magereza yenye msongamano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali kupitia sheria mbalimbali tumekuwa tukijaribu kuzitumia ili kuwaondoa wafungwa ambao wana vifungo vifupi. Pia tumekuwa tukitumia Sheria yetu ya Parole kupunguza msongamano. Vilevile Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa akitoa msamaha kwa wafungwa ili kupunguza msongamano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue fursa hii kuwataka Watanzania popote pale walipo wasijihusishe katika uhalifu utakaowasababishia wawe wafungwa ama mahabusu. Waelewe kwamba watakapofanya uhalifu wataenda kwenye magereza ambazo zina msongamo. Kwa hiyo, nichukue fursa hii kuwasihi wasijihusishe katika uhalifu. Ahsante sana.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi. Naipongeza Serikali kwa upande wa Morogoro kwa kuanza upimaji wa ardhi hasa kwa upande wa Wilaya za Malinyi, Kilombero na Ulanga, lakini upimaji unakuta migogoro bado inaendelea kwenye Wilaya nyingine, lakini ni matatizo kweli kwa vifaa vya upimaji kwa sababu vinanunuliwa kwa bei ghali na halmashauri zingine hazina uwezo wa kununua hivyo vifaa. Je, Serikali inasemaje kwa kusaidia hizo Halmashauri ambazo haziwezi kununua hivyo vifaa?
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ishengoma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nipokee shukrani zake kwa Serikali kwa kazi inayofanya katika Wilaya ya Malinyi, Ulanga na Kilombelo, kwa kupima ardhi yote katika maeneo yale na niwashukuru wananchi wa maeneo hayo kwa sababu wamekuwa wakitoa ushirikiano mzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kumaliza migogoro hiyo kama ambavyo tumeanza ile ni kama pilot area, lakini tayari tutakuwa na resource persons wengi kutokana na wananchi wenyewe kwa sababu pia watakuwa wamepata ujuzi mzuri wa kuweza kufanya scale up kwenye maeneo mengine na lengo la Wizara ni kuhakikisha maeneo yote yanapimwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu vifaa vya upimaji, napenda nitoe rai kwa halmashauri zetu zote, Wizara ilikwishatoa vifaa katika maeneo yote ya kanda zetu nane, lakini halmashauri haziendi kuomba vifaa vile. Bahati nzuri kwa kuwa ameuliza hili swali, basi nitatayarisha takwimu niletehapa baada ya kuwa tumeshapata vifaa, ni halmashauri ngapi zimeomba. Halmashauri nyingi hawaendi kuchukua vifaa, lakini wana-opt kutafuta vifaa vya kukodi wakati kuna vifaa vya bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa halmashauri zetu, watumie vifaa hivyo ambavyo Wizara ilishafundisha watumishi wawili, wawili kutoka kila halmashauri kwa nchi nzima ambao wana Wapima kwa ajili ya kuweza kutumia vile vifaa. Matokeo yake wamefundishwa, hawaleti maombi na vifaa vimekaa idle,halafu Wabunge wanalalamikia suala la upimaji. Naomba usimamizi katika halmashauri, watumie vifaa ambavyo tayari Wizara imegharamia.Ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Lumuma inayotoka Wilaya ya Kilosa ni mashuhuri sana kwa kilimo cha vitunguu, lakini kata hii haina umeme na inategemea umeme kutoka Wilaya ya Mpwapwa ambayo ipo kwenye mkoa mwingine wa Dodoma. Je, kata hii ni lini itapatiwa huduma ya umeme ili iweze kupata huduma ya umeme?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa mama yangu Dkt. Christine Ishengoma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naye pia naomba nimpongeze kwa kufanya kazi nzuri kama Wabunge wengine wa Viti Maalum kufuatilia sekta mbalimbali. Katika swali lake hili la nyongeza ameuliza hii Kata ya Lumuma ambayo ipo jirani kabisa na Wilaya ya Mpwapwa nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge hata Diwani wa Kata ile mwanamama amekuwa akifuatilia na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kilosa naye nataka nimtaarifu Mheshimiwa na wananchi wote wa Kata ya Lumuma kwamba, tunatambua changamoto hii na kwa kuwa wapo karibu na Wilaya ya Mpwapwa tumeiagiza TANESCO, yapo maeneo tumeamua kuwapa TANESCO ili wasambaze umeme vijijini na mpaka sasa zaidi ya maeneo 200 yametwaliwa na TANESCO ili isaidie REA katika kusambaza umeme vijiji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuahidi mama Mheshimiwa Dkt. Ishengoma tutaambatana katika ziara kwenye kata hii ya Lumuma kuelezea ujumbe huu pamoja na TANESCO na REA na kwamba watapatiwa umeme katika nyakati za kuanzia mwezi Julai, 2019 na kuendelea. Ahsante sana.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana licha ya barabara ya Meimosi kuwa haina matatizo yoyote, lakini Manispaa ya Morogoro barabara za pembezoni ni mbovu kiasi hazipitiki kwa muda wa mvua. Kwa hiyo, kuna mkakati gani wa kutengeneza hizi barabara ? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, swali hili jana limeuliza naomba nirudie majibu ya Serikali kama ambavyo amesema Mheshimiwa Naibu Waziri yule wa Ujenzi, tumeshafanya tathimini kuangalia maeneo mbalimbali ambayo kwa kweli yameathirika na mvua na baadhi ya maeneo hayapitiki, tumeagiza watu wetu Meneja wa TARURA SO, tumeagiza Meneja wa Mikoa yote na Meneja Wilaya walete tathimini yao taarifa tumeshaipata tunaifanyia kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuwahakikishie hivyo Waheshimiwa Wabunge na Waheshimiwa watanzania kwamba ndani ya muda mfupi sana maeneo yote ambayo hayapitiki kwa dharura, lakini tutaendelea kuwa tunaboresha ili kuimarisha barabara zetu katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaelekeze TANROAD Meneja wa TANROAD Mkoa wa Morogoro apitie maeneo ambapo Mheshimiwa Mbunge amezungumza na yako mambo ambayo unaweza kufanya ndani ya uwezo wao kwa bajeti ndogo iliyopo katika halmashauri na mikoa yetu, lakini yale maeneo makubwa ambayo ni changamoto kwao tumewaambia tuwapokee TAMISEMI ngazi ya taifa tuweze kuyafanyia kazi lengo ni kwamba barabara hizi zipitike wakati wote na huduma kwa jamii yetu iendelee kutolewa kama kawaida. Ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii:-

Mheshimiwa Naibu Spika naishukuru sana Serikali nilishawahi kuongea na Mheshimiwa Waziri kuhusu tatizo la maji katika Kata ya Magadu, wananchi wanapata matatizo kwa muda mrefu. Na chanzo cha maji kutokana na utafiti ni kuwa tayari kilishapatikana kutoa mbete. Je, kuna tatizo gani la kuendeleza hicho chanzo cha maji kuhusu Wananchi wa Magadu na mitaa mingine waweze kupata maji ya kutosha?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, kiukweli nimpongeze Mheshimiwa Mbunge amekuwa mfuatiliaji sana na ameshafanya kikao na Mheshimiwa Waziri. Nataka nimuombe basi baada ya Bunge tukutane na wataalam wetu tuangalie namna gani ya kuweza kuwasaidia Wananchi wa Magadu.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza. Mradi huu ingawaji Serikali wanajitahidi kuwatafutia maji wananchi wa manispaa ya Morogoro, mradi huu naona unachukua muda mrefu.

Je, una mpango gani wa kuwapatia maji wananchi wa manispaa ya Morogoro wa muda mfupi wakiwa wanasubiria mradi wa muda mrefu? Hasa kwenye kata ambazo hazipati maji kabisa ikiwepo Kora A na Kora B, Mkundi, Amagadu, Rukobe, Kilimanjaro pamoja na mitaa mingine ya Manispaa ya Morogoro.

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, mradi wa Furwe, Mikese unahusisha pamoja na vijiji vya Newland pamoja na mtego wa Simba. Mradi huu wa maji tayari unawapatia maji wananchi wa Furwe. Lakini mpaka sasa hivi ninavyoongea wananchi wa Newland pamoja na mtego wa simba hawajapatiwa maji.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia maji wananchi hawa wa Newland pamoja na Mtegowasimba?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze kwa kazi kubwa sana anayofanya kwanza kuwatetea wananchi wa Morogoro. Sio mara yake ya kwanza kuuliza maswali yanayohusiana na maji katika Mkoa wa Morogoro. Lakini nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge sisi katika mamalaka yetu ya maji safi na usafi wa mazingira MORUWASA imekuwa ikitenga 20% katika kuhakikisha inawapatia wananchi maji kabla ya mradi huu mkubwa nataka nimuhakikishie zipo kazi zinazoendelea sasa hivi tupo katika upanuzi wa miundombinu ya maji katika maeneo ya Kihonda Kaskazini maeneo ya Kilimanjaro na maeneo ya viwandani.

Mheshimiwa Spika, lakini pia, tuna utekelezaji wa buster pump station katika maeneo ya Mkundi lakini pia tuna ujenzi wa mradi mkubwa pale zaidi ya milioni 496 katika maeneo ya Mundu na Kilala hii yote ni katika jitihada katika kuhakikisha tunapunguza tatizo la maji katika Mkoa wa Morogoro. Lakini kwa kuwa mama yangu, Mheshimiwa Dkt. Ishengoma amekuwa muulizaji mkubwa sana katika suala zima la maji, nimuombe leo tukutane na Katibu Mkuu tuangalie namna gani tunaweza tukasaidia katika maeneo ambayo aliyoorodhesha ili wananchi wake waweze kupata huduma hii ya maji, ahsante sana. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Hospitali yetu ya Ulanga ina tatizo na tatizo ni kuwa haina gari la wagonjwa: Je, Serikali ni lini itatupatia gari la wagonjwa kwenye Hospitali yetu ya Ulanga?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ni kweli kwamba kuna maeneo mengi ambayo bado tuna upungufu wa vitendea kazi. Tunaomba tulipokee swali hili. Kadri tutakavyopata uwezo tutapeleka gari katika eneo hili pamoja na maeneo mengine ya nchi ambayo kwa kweli kuna changamoto ya mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa tumeelekeza kwamba katika maeneo ya jirani au kwenye Hospitali ya Wilaya ya jirani inapotokea shida au hata magari ya Halmashauri yatumike kutoa huduma hiyo. Tutajitahidi kadri itakavyowezekana magari yapatikane katika Hospitali ya Wilaya, ikitokea shida ya mgonjwa basi apate huduma haraka kupelekwa kwa hatua nyingine ya mbele.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, pia naipongeza Serikali kwa kutenga shilingi milioni 100 kwa kuanza matengenezo haya ya barabara ya Iyogwe – Chakwale – Ngilori. Barabara hii ni muhimu sana na hasa kwa upande wangu naona ni muhimu sana kwa upande wa jamii pamoja na uchumi. Nikisema jamii ni kwa sababu wakati wa kipindi cha mvua inakuwa matatizo kupitika hii barabara. Mto huu wa Chakwale, Nguyani na Matale mpaka sasa hivi zina drift culverts, lakini inakuwa muhimu sana na inakuwa matatizo kwa sababu maporomoko ya maji yanakuwa mengi sana wakati wa mvua kiasi wanafunzi wanashindwa kupita na magari.

Je, nauliza Serikali kwa sababu mpaka sasa hivi kuna drift culverts ambazo bado matatizo, kwa nini haikufikiria kuwa iweke box culverts kwa mito hii mikubwa yote mitatu ya Chakwele, Nguyani pamoja na Matale? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, barabara ya Gairo – Enongwe pamoja na barabara ya Mzumbe – Mgeta ni barabara muhimu sana kwa mazao ya mboga mboga. Barabara hizi zina ahadi za Mheshimiwa Rais kwa kutengeneza kwa kiwango cha lami; Je, ni lini barabara hizi zitaweza kutengenezwa kwa kiwango cha lami? ahsate. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwenye barabara hii ni barabara ambayo ina changamoto. Mimi nimeitembelea barabara hii, nimeona maeneo haya anayataja Mheshimiwa Mbunge, lakini pia Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano hivi karibuni alitembelea eneo hili akajionea changamoto ambazo zipo. Kuna maeneo korofi kwa mfano eneo la Nguyani ambalo tunasema tutaweka drift daraja ili iweze kutusaidia wakati ule mpango mkubwa wa kufanya box culvert kubwa inatengenezwa pale.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tatizo la eneo hili tunalitambua, wapo watu ambao wamepoteza maisha katika eneo hili, ukienda eneo hili la Nguyani wanapaita ni mto kaburi kwa sababu ya historia kwa muda mrefu kumekuwa na changamoto. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tunalitambua hili na niseme katika bajeti yetu ya mwaka huo unaokuja ziko fedha ambazo tumezitenga kwa ajili ya kushughulikia maeneo korofi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo sambamba na kuweka hii culvert, lakini pia tunaitazama kwa mapana kwa sababu Mheshimiwa Mbunge wa eneo la Gairo tumekubaliana tutafuatana naye pamoja na Katibu Mkuu kwa sababu ya kuona namna ya kwenda kwa haraka kuwarekebishia wananchi hawa.

Kwa hiyo, nikutoe hofu kwamba eneo hili tunalifahamu na tunachukua hatua, na kupitia fedha ambazo Bunge hili limetupitishia yapo maeneo pia ambayo tuna allocation ya fedha kwa maana ya kushughulikia maeneo korofi. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na kiasi cha fedha tulizotenga, lakini jicho la pili linatazama eneo hili tuweze kuliboresha ili wananchi tuwaokoe kwenye hatari waliokuwa wanaipata, lakini waweze kupita kwenda kwenye shughuli za kwao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ahadi za Mheshimiwa Rais barabara unayoitaja ya Mzumbe – Mgeta kama nilivyozungumza, ahadi zote za viongozi wakuu ikiwemo Mheshimiwa Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu tutaendelea kuzitekeleza. Katika Mkoa wa Morogoro yako maeneo ambayo utekelezaji wake wa ahadi hizi uko karibu asilimia 100. Kwa hiyo, uone kwamba tunakwenda hatua kwa hatua, kwamba baada ya kufanya utekelezaji wa ahadi za Mheshimiwa Rais kwenye baadhi ya meneo kwenye Mkoa wa Morogoro, itafika zamu ya eneo hili tutakwenda kufanya matengenezo kulingana na ahadi ya kiongozi mkuu Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Namshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Naishukuru Serikali kwa kuwa na mpango wa kujenga Hospitali ya kisasa kwenye Mkoa wetu wa Morogoro. Hata hivyo, bado kuna tatizo la umilikishaji na nimeambiwa kuwa karibu watakamilisha umilikishaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la kwanza, Hospitali hiyo ya Rufaa ya Morogoro ambayo tunaipanua mpaka sasa hivi haina kifaa cha CT-Scan na hili swali nilishauliza humu ndani, nikaahidiwa lakini mpaka sasa hivi hatujapata kifaa hicho. Je, kifaa hicho tutapatiwa lini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kutokana na Mkoa wa Morogoro kuwa katikati na kupokea majeruhi wengi lakini tuna tatizo la mtambo wa oxygen. Je, Serikali ina mkakati gani wa kutupatia mtambo wa oxygen ili kupunguza matatizo tuliyonayo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali imedhamiria kuhakikisha inaboresha huduma za afya za kibingwa katika Hospitali za Rufaa za Mikoa ikiwepo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro. Katika mipango yake, Serikali imeweka mipango ya kuhakikisha vifaa tiba kama CT-Scan zinapatikana katika hospitali kubwa za mikoa ikiwemo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali iliahidi na ahadi yake bado ipo pale pale. Kazi inayoendelea sasa ni kutafuta fedha ili tuweze kupata mashine hiyo ya CT- Scan na kuifunga katika Hospitali ile ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro ili kuweza kuboresha huduma. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hilo bado linafanyiwa kazi na Serikali na litakamilika ili tuweze kuboresha huduma za afya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na umuhimu wa kuwa na mtambo wa oxygen katika hospitali ile, ni kweli, Mkoa wa Morogoro upo kwenye highway ambapo mara nyingi kunakuwa na matukio ya ajali. Kwa hiyo, tuna kila sababu ya kuwa na mitambo ya oxygen ili kuwezesha mkoa kuwa na uhakika wa kupata oxygen pale inapohitajika. Jambo hili pia limechukuliwa na Serikali, linafanyiwa kazi, fedha inatafutwa ili mtambo uweze kuwekwa pale na kuboresha huduma kwa wananchi.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Polisi Kisaki ambacho kiko Morogoro Vijijini kwa umuhimu wake kina matatizo ya usafiri. Je, ni lini kitapewa usafiri angalau pikipiki?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nikiri kwamba, bado tuna changamoto ya usafiri hasa katika maeneo ya vituo vya polisi, ikiwemo pikipiki na gari na aina nyingine za usafiri. Sasa nimwambie tu Mheshimiwa kwamba, aendelee kuvuta subira, Serikali kama Serikali tumo mbioni kuhakikisha kwamba, vituo vya polisi na maeneo mengine ambayo yanatoa huduma za ulinzi na usalama kwa wananchi tunahakikisha tunapeleka hivyo vyombo vya usafiri, ili sasa wananchi waweze kupata hizo huduma kama inavyotakiwa. Nakushukuru.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Barabara za Ulanga ni sawa sawa na barabara za Mlimba:-

Je, ni lini barabara ya kutoka Mlimba Mjini mpaka Tanganyika Masagati ambayo inatengenezwa na TARURA itaweza kukarabatiwa na kutengenezwa kwa sababu kutokana na mvua ni mbaya sana kiasi cha kuleta taabu ya kupitika? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mheshimiwa Mbunge anauliza ni lini barabara ya kutoka Mlimba kwenda Tanganyika Msagati itajengwa kwa sababu ipo katika hali mbaya?

Mheshimiwa Naibu spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tumelipokea ombi lake na Ofisi ya TARURA watafanya tathmini na watatafuta fedha kwa ajili ya matengenezo ya eneo hilo. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi hawa wanaelewa lakini suala hili limechukua muda mrefu, walikuwa wanatumia maeneo haya kulima na wanajua faida ya Bwawa la Mwalimu Nyerere lakini wanachohitaji ni kupata uelewa na kufahamishwa. Kwa kuwa Mawaziri wameshapitisha na suluhisho limeishafikiwa, je, ni lini Mheshimiwa Waziri atakwenda kuongea na wananchi hawa kusudi waweze kupata suluhisho? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, tatizo hili lipo pia katika Kitongoji cha Dutumi, Kata ya Bwakila Chini, Wilaya ya Morogoro Vijijini ambapo kuna tatizo la Hifadhi ya Selous pamoja na wananchi wa Dutumi hasa wakiwemo wakulima na wafugaji kiasi kwamba kuna kijana mmoja alitobolewa macho, mwingine amejeruhiwa mkono, ni lini Mheshimiwa Waziri atakwenda kuwasikiliza kwa sababu vikao vimekaa lakini hakuna suluhisho? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kabla ya bajeti hii kuisha Juni tutaongozana naye kwenda Kilombero lakini pia Morogoro Vijijini ili kutatua mgogoro huu wa wakulima na wafugaji.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nashukuru kwa ujenzi unaofanyika. Licha hivyo nina maswali mawili mafupi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, tukiwa tunasubiri upatikanaji wa fedha na kwa kuwa upembuzi yakinifu umefanyika kwa muda mrefu, je, kuna mkakati gani wa Serikali wa muda mfupi wa ukarabati na kutambua sehemu korofi za barabara hii ya Mikumi – Kilosa ambao unaweza ukafanyika kwa upande wa lami nyepesi kwenye sehemu korofi?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa barabara hii inaendelea mpaka Magore, Tuliani, Mziha, Handeni kule Tanga; na sehemu ya Tuliani mpaka Mziha bado haijajengwa kwa kiwango lami. Ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami ili barabara hii ikamilike? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Dkt. Ishengoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara kipande cha kuanzia Kilosa mpaka Mikumi fedha ya matengenezo ipo.

Kwa kuwa mvua ilikuwa inanyesha baada ya mvua tu kukatika wakandarasi watakwenda kazini kuhakikisha kwamba maeneo yote yale ambayo yalikuwa yana tatizo yanarekebishwa.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu kuweka lami nyepesi itakuwa ni gharama kwa sababu barabara hiyo iko kwenye mpango wa matangenezo na fedha inapopatikana tunaendelea kuijenga. Tutakachofanya tu ni kuikarabati kwa kiwango cha changarawe ili iendelee kupitika lakini tutakapopata fedha tutajenga barabara zote kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili kuhusu barabara ya kuanzia Mziha – Turiani, katika bajeti ya mwaka huu fedha imetengwa kwa ajili ya kuendelea kuanzia Turiani na kuendelea upande wa kwenda Tanga. Kwa hiyo, kama ataangalia bajeti iliyopitishwa fedha imetengwa kwa barabara zote hizo mbili kwa ajili ya kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa
Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya mchepuo ya Morogoro Manispaa ambayo Mheshimiwa Naibu Spika unaifahamu na unaitumia kila mara unapokwenda Dar es Salaam ili kupunguza msongamano wa magari pale Msamvu? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ishengoma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayosema ambayo itakuwa barabara ya by-pass ni barabara ambayo muhimu, binafsi nimepita na Mheshimiwa Ishengoma tumeongea naye. Ni kweli kwamba barabara hii ni muhimu na tutaingiza kwenye mpango ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami kupunguza msongamano wa kupita magari yote katikati ya Mji wa Morogoro. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Ishengoma kwamba mpango huo upo na katika siku zinazokuja kadri ya fedha zitakapopatikana barabara hii itajengwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini barabara ya Mzumbe – Mgeta itajengwa kwa kiwango cha lami ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Awamu ya Nne? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba, alichozungumza hapa ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne ya utekelezaji wa Barabara ya Mzumbe mpaka Mgeta, niseme tu kama nilivyojibu katika jibu la msingi na la nyongeza la Mheshimiwa Charles Kimei kwamba, na yenyewe tunaiingiza katika mpango, tutaizingatia. Barabara nyingi tutaziongeza katika mpango baada ya kupata ongezeko la fedha hii ambayo jana Bunge lako Tukufu lilipitisha. Ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Licha ya majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwanza niishukuru Serikali, nina furaha sana kuona kuwa Mradi wa Chagongwe, ambao ni wa muda mrefu, unaanza. Je, mradi huu wa kutoka Milima ya Chagongwe na Nongwe utaanza kutekelezwa lini?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Manispaa ya Morogoro, nashukuru Serikali inaendesha miradi ya maji kwenye manispaa yetu, lakini hata hivyo bado tunapata maji ya mgao. Je, miradi hii, hasa mradi wa Bwawa letu lile la Mindu, ni lini hasa litakamilika na miradi mingine, ili wananchi wa manispaa waweze kupata maji kila siku na waondokane na maji ya mgao? Ahsante sana.
WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge mama yangu Dkt. Christine Ishengoma ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati yetu ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa kazi kubwa na nzuri na anatusimamia vizuri sana ili sisi Wizara kuhakikisha watu wanapata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge, ambacho ninataka kukuhakikishia Mheshimiwa Mwenyekiti wetu ni kwamba eneo la Mradi huu wa Chagongwe, katika mwaka huu wa fedha tunaokwenda nao tumepata fedha ambazo ni za ziada za Mheshimiwa Rais, zaidi ya bilioni 207. Hili ni eneo ambalo tutalipa umuhimu mkubwa kuhakikisha katika mwaka huu unaoanza wa fedha, kwenda kuanza mradi huu na wananchi wa Gairo waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili la Mheshimiwa Mbunge ni kuhusu suala zima la maji katika eneo la Morogoro. Mji wa Morogoro uzalishaji wake ni lita milioni 35, lakini mahitaji yake kwa sasa ni lita milioni 67, kwa hiyo, kuna uhitaji mkubwa sana wa maji, kwa hiyo mkakati wa haraka katika siku 100 za Mheshimiwa Rais, mama Samia Suluhu Hassan, ametupatia fedha zaidi ya bilioni nne kwa ajili ya kujenga mradi wa haraka.

Mheshimiwa Naibu Spika, na tumejenga tenki la lita milioni mbili eneo la Mgulu wa Ndege ambapo tutakwenda kutumia chanzo cha maji cha Mambogo ambao tumeweka maji katika tenki lile la Mgulu wa Ndege ambapo maji yale yatakwenda Kihonda, maji yale ambayo yatakwenda eneo la SGR, Lukobe na Mkundi katika ili kuhakikisha wananchi wa Morogoro wanapata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mkakati wa kumaliza kabisa tatizo la maji katika Mji wa Morogoro, tumepata fedha zaidi ya Euro milioni 70, ambapo tumekwishasaini mkataba na wahandisi washauri, mradi ule tunakwenda kuhakikisha unaanza kwa haraka ili wananchi wa Morogoro waweze kupata huduma ya maji safi na salama.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, naamini kuwa Wizara ya Maji inafanya kazi sana kwa jitihada zao, licha ya jitihada hizo, lakini bado watu wanataka maji. Kata ya Ruaha ambayo iko kwenye Jimbo hilohilo la Mikumi, Wilaya ya Kilosa waliahidiwa na Mheshimiwa Rais Awamu ya Tano kupatiwa maji. Kwa hiyo, nauliza ni lini watapatiwa maji? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Kata ya Lukobe ambayo iko Manispaa ya Morogoro tulitembelea kamati yangu na wananchi wakaahidiwa kuwa watapariwa maji kuanzia mwezi wa nane hilo tanki la mguru wa ndege, lakini mpaka sasa hivi ninavyoongea tanki hilo halijawahi kupata maji na sasa ni mwezi wa 11 na ahadi ilikuwa mwezi wa nane, wananchi wanakunywa maji ya visima ambayo ni maji yasiyo Safi na salama. Na wamenituma wanauliza ni lini watapatiwa hayo maji kupitia kwenye tanki hilo la Mguu wa Ndege? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kipekee nipende kumshukuru Mheshimiwa Mama yangu Dkt.Christine Ishengoma kwa namna ambavyo anaendelea kufuatilia suala hili la maji katika maeneo ya Mkoa wa Morogoro na nikushukuru sana Mheshimiwa Christine Ishengoma kwa ushirikiano ambao umeendelea kutupa sisi Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Spika, kwa swali la kwanza Kata ya Ruaha; tayari RUWASA wameshafanya taratibu zote na sasa hivi wametangaza ili tuweze kumpata mkandarasi. Na tunaamini kwa kasi ambayo tunaenda nayo watu wa Ruaha nao watakwenda kunufaika muda si mrefu.

Mheshimiwa Spika, kwa eneo hili la mguru wa ndege wakati wa ziara na mimi nilikuwepo. Mheshimiwa Dkt. Christine kama ambavyo tumekuwa tukiwasiliana kwenye suala hili, lile tanki hata ukipita pale barabarani unaliona kubwa, zuri, lenye ubora kabisa limeshakamilika na sasa hivi tunaingia kwenye awamu sasa ya usambazaji na tayari Wizara tunapeleka fedha kwenye mgawo huu unaokuja kwa lengo la kuona sasa maji yanakwenda kuwafikia wananchi wote wa eneo la Lukobe. Ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kituo cha Afya cha Mwaya – Mahenge – Ulanga majengo yake yamejengwa kwa muda mrefu na ni mabovu. Je, ni lini kitafanyiwa ukaratibu Kituo cha Afya hiki cha Mwaya? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa DKt. Christine Ishengoma Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vituo vyetu na hospitali zote za halmashauri chakavu ambazo zimejengwa muda mrefu zinaandaliwa utaratibu wa kwenda kuzifanyia ukarabati. Kwa hivyo tumeshaanza na utaratibu wa hospitali za halmashauri, tumeshazitambua hospitali 23 kongwe, lakini tutakwenda kutambua vituo afya chakavu vya siku nyingi ili tutafute fedha kwa awamu kwa ajili ya kuvifanyia ukarabati, lakini pia kuvifanyia upanuzi wa vituo vile. Kwa hiyo, naomba nimuhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba wakati zoezi hilo linafanyika tutahakikisha pia Kituo cha Afya cha Maya kinapitiwa na kufanyiwa tathimini hiyo. Ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Napenda kuuliza na kujua tatizo lililopo hasa TANESCO kwa upande wa Morogoro Mjini; baadhi ya wananchi wamelipia umeme kuwekewa kwenye nyumba zao lakini imechukua muda mrefu hawajawekewa mpaka sasa hivi. Kwa mfano, Kata ya Kasanga kuna wananchi wamelipia lakini mpaka hivi sasa hawajawekewa: -

Je, kuna tatizo gani?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba wapo wateja ambao wamelipia huduma ya TANESCO lakini walikuwa hawajaipata na hii ni kutokana na kwamba kulikuwa kuna mwamko mkubwa sana kwa wananchi wanaohitaji umeme na uwezo wetu TANESCO kidogo ulikuwa umepungua kwa sababu ya kutokuwepo na vifaa vya kutosha kukamilisha kazi hizi.

Mheshimiwa Spika, tayari Mheshimiwa Rais ameshaelekeza, Wizara yetu inasimamia TANESCO kuhakikisha kwamba vile viporo ambavyo ni vya nyuma angalau visiwepo zaidi ya miezi mitatu iliyopita. Yaani mtu akilipa Februari hii, angalau mwezi Machi au Aprili awe ameunganishiwa umeme. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Ishengoma pamoja na Wabunge wengine wote kwamba Serikali inajitahidi kuhakikisha kwamba vile viporo vya kuunganisha umeme vinaunganishwa na kukamilika ndani ya muda mfupi ili kila mtu aweze kunufaika na umeme ambao unazalishwa.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo. Nauliza kuwa, je, ni lini Serikali itatimiza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne ya kujenga barabara ya kuanzia Gairo hadi Kata za Chagongwe na Nongwe kwa kiwango cha lami? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ameainisha hapa ahadi ambayo imeahidiwa katika Awamu ya Nne ya Serikali na anataka Awamu ya Sita tuikamilishe kwa wakati. Jibu moja kubwa la msingi ambalo Wabunge wote wanapaswa kufahamu ni kwamba Ahadi zote za Viongozi, sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tumeziainisha na zote zinathamani halisi ya fedha ambayo tumeziwekea kila ahadi, kama ni barabara, maji, Kituo cha Afya zote zipo katika vitabu vyetu na utekelezaji wake ni kwamba tumekuwa tukitenga fedha katika kila mwaka wa fedha. Kwa hiyo, hata hili la Awamu ya Nne na lenyewe lipo katika utekelezaji huo. Kwa hiyo, ninachoweza kukisema ni kwamba, litatekelezwa kulingana na fedha tunavyokuwa tunazipata kila wakati ili kuhakikisha tunamaliza ahadi zote za viongozi zilizopo. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, licha ya majibu mazuri niliyoyapata kutoka Serikalini, naomba kuuliza maswali mengine madogo mawili.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; je, kuna mkakati gani wa kutatua tatizo la upungufu wa dawa unaojitokeza kwenye Mkoa wa Morogoro?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, kuna mkakati gani wa Serikali kukabiliana na changamoto zinazojitokeza kwenye upande wa chanjo, hasa chanjo za akina mama wajawazito na watoto wachanga ambao unajitokeza Mkoani Morogoro, hususan Manispaa ya Morogoro? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mkakati wa kutatua changamoto za upatikanaji wa baadhi ya dawa katika vituo vyetu, kwanza Serikali imeongoza bajeti ya dawa inayopelekwa Bohari ya Dawa (MSD) kwa zaidi ya mara saba na hivi sasa Serikali ilishapeleka MSD takribani shilingi bilioni 300 kwa ajili ya dawa, lakini pia mpango umewekwa kupeleka angalau kila mwezi shilingi bilioni 15 ili kuhakikisha kwamba dawa zinapatikana.

Mheshimiwa Spika, mpango wa pili ni kuhakikisha kwamba dawa zinazonunuliwa na kupelekwa kwenye vituo vyetu zinatumika ipasavyo na kuepuka matumizi mabaya ya dawa kwa maana ya upotevu wa dawa, lakini pia na fedha zitokanazo na uchangiaji wa huduma za dawa.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na mkakati wa kukabiliana na changamoto za chanjo katika Mkoa wa Morogoro. Kwanza naomba nipokee hoja ya Mheshimiwa Mbunge na baada ya hapa nitajifunza changamoto ni zipi ili tuweze kuona namna ya kwenda kuzitatua. Lakini jambo la muhimu ni kwamba ni haki ya msingi ya watoto na akina mama kupata chanjo na Serikali imeendelea kuhakikisha chanjo zinapatikana ili kuboresha huduma za wananchi. Ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Je, ni lini treni ya mwendokasi itaanza kufanya kazi kati ya Dar es Salaam na Morogoro? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, matarajio yetu yalikuwa reli ya SGR kutoka Dar es Salaam kuja Morogoro yenye urefu wa kilometa 300 tulitegemea ingeanza mwezi huu wa Septemba kama ambavyo tulijibu hapo awali wakati wa Bunge la Bajeti. Lakini kutokana na changamoto mbalimbali hususan katika kusafirisha vipuri na mabehewa ambayo kulikuwa kuna changamoto ya kupata meli ya usafirishaji kutoka nchini Ujerumani kuja Tanzania, lakini habari njema kwa Watanzania wote watambue ya kwamba tayari vichwa vya treni, mabehewa ya abiria na mizigo, hivi ninavyosema vimekwishapakiwa kwenye meli kuja nchini Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tunataraji kwamba ifikapo mwezi Novemba, mwaka huu vitakuwa vimeshaingia na tutafanya majaribio mpaka mwezi Januari. Kwa hiyo, mwezi Februari mwakani standard gauge kutoka Dar es Salaam kuja Morogoro itaanza rasmi, ahsante. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itaanzisha huduma za upasuaji katika Kituo cha Afya cha Mafiga, Mkoani Morogoro Manispaa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dokta Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Spika, vituo vya afya vikijengwa vinajengwa na majengo ya upasuaji na dhamira ya Serikali ni mara tu majengo ya upasuaji yakikamilika huduma za upasuaji zianze. Kwa hiyo, kama Kituo hiki cha Afya, Mafiga, jengo la upasuaji limekwishakamilika, naelekeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro waanze huduma za upasuaji haraka iwezekanavyo, lakini kama kituo hakijakamilika wakamilishe na baada ya hapo wasajili ili huduma za upasuaji ziweze kuanza. Ahsante. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza naishukuru Serikali kwa barabara hii ya kuanzia Magole hadi Tuliani.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu jibu hili limekuwa la muda mrefu tangu 2010 mpaka sasa hivi mnaendelea hivyo hivyo, ndiyo jibu hilo hilo na kipande ni kilomita102 tu.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutenga bajeti kwenye kipande hiki cha Km 102 kwenye bajeti ijayo?

Swali langu la pili; je, barabara ya Lupilo mpaka Mahenge ni lini nayo itajengwa? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeshaanza kuijenga hii barabara hizo kilomita na hata katika bajeti ya mwaka kuna fedha imetengwa kwa ajili ya barabara hiyo, lakini Serikali inaendelea kutafuta fedha kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa iko kwenye mpango tunaweka katika miaka inayokuja ya bajeti tutaendelea kutenga fedha ili kuikamilisha barabara yote hii.

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili kwa barabara ya Lupilo – Mahenge, barabara hii ni kati barabara kuu kwa maana ya trunk road na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wako Wakandarasi ambao tayari wameshapita Lupilo – Mahenge kwa ajili ya kuangalia kama itajengwa kwa mpango wa EPC. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii pia Serikali inategemea kuijenga kwa kiwango cha lami.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa
Naibu Spika, ahsante sana. Mji Mdogo wa Gairo ni mji ambao una matatizo ya maji, sasa naomba kujua Mradi wa Maji wa kutoka kwenye Milima ya Nongwe ni lini utakamilika ili wananchi wa Gairo waweze kupata maji ya kutosha?
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Morogoro, Mwenyekiti wetu wa Kamati ya Maji, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi hii anayoiongolea uendelevu wake unatokana na mapato ya fedha, kwa hiyo kadri tutakavyoendelea kupata fedha, namna ambavyo tumekuwa tukipeleka fedha nyingi sana kwenye maeneo yote, tutapeleka fedha kwani na Gairo pia tunatamani waondokane na tatizo la maji.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili mafupi ya kuongeza: -

Mheshimiwa Spika, kupanda miti na kutunza miti ni mambo mawili tofauti. Hata hivyo, na mimi nilishiriki kupanda hiyo miti Wami-Ruvu. Je, kuna mpango gani ambao umewekwa madhubuti wa kutunza hiyo miti 96,500 iweze kustawi angalau asilimia 70?

Swali la pili; Chuo cha Kilimo SUA mnakishirikishaje katika utunzaji wa vyanzo vya maji na pia katika utunzaji wa uoto wa asili, hasa kwenye milima ya Uluguru ambako ndio kuna vyanzo vya maji ambavyo vimeharibiwa kwa wingi?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Charistine Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma ambaye pia ni Mwenyekiti wetu wa Kamati ambayo inafanya vizuri sana. Mheshimiwa Dkt. Ishengoma kama alivyosema naye alishiriki kupanda miti, hii miti sote tumepeana majukumu kuona kwamba haifi na itapona zaidi ya asilimia hizo 70 ambazo amezitolea mfano.

Mheshimiwa Spika, suala la ushirikishaji wa Chuo cha SUA Wizara tumekuwa tukishirikiana na wataalam mbalimbali katika makongamano na namna ya kuona tunabadilishana uzoefu. Hata hapa juzi tulikuwa na kongamano zuri pale Dar- es-Salaam, yote ni kuona kwamba, tunashirikisha wataalam mbalimbali ili tuweze kuona tunapata elimu nzuri kwa watendaji, vilevile kutoa elimu kwa wananchi kuona vyanzo vya maji inakuwa ni jukumu la wote, tunavitunza na vyanzo hivi vinabaki kuwa ni endelevu kwa sababu tuna miradi mikubwa ambayo inaendelea kutekelezwa kwa kupitia fedha za Wizara. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Napenda kuuliza, je, ni lini barabara ya mzunguko kwenye Manispaa ya Mororogoro kuanzia Juniour Seminary mpaka Kihonda itajengwa ili kupisha msongamano wa magari sehemu za Msamvu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum Morogoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Ishengoma kwa jinsia anavyofatilia ujenzi wa hii barabara ya mzunguko Morogoro. Taratibu bado zinaendelea za kufanya usanifu wa hiyo barabara ili kupunguza msongamano katika barabara kuu inayopita Msamvu kwenda Dar es Salaam. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mara usanifu utakapokamilika barabara hii itaanza kujengwa. Ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa
Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi kwa kuuliza swali. Ningelipenda kujua Chuo Kikuu cha Kilimo cha Mwalimu Nyerere kinachojengwa Butiama ni lini kitaanza kufanya kazi? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tuna Kampasi ya Mwalimu Nyerere kule Butiama na ilianzishwa toka mwaka 2014 lakini bado ilikuwa haijanza kufanya kazi, lakini naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge tulifanya ziara na Kamati yako ya Bunge hili mwezi uliopita na tulikwenda pale kwa ajili ya kufanya tathmini na naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, chuo kile kitaanza kufanya udahili katika mwaka huu ili kuweza kuanza kutoa mafunzo katika eneo lile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa
Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Kwa kuwa kwa kupunguza bei na matumizi ya mkaa mpango mmojawapo ni kutumia gesi asilia: Je, mna mkakati gani wa kuwaingizia majumbani gesi asilia wananchi wa Mkoa wa Morogoro? Ahsante sana.
WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, gesi asilia inatoka Mtwara mpaka Dar es Salaam kwa bomba na uwekezaji ule ni wa gharama kubwa kutona na gharama kubwa za ujenzi wa miundombinu ya bomba. Tunaamini kwamba kwa wakati huu mfupi wa sasa, miundombinu ya kujenga bomba la gesi asilia kutoka Dar es Salaam - Morogoro mpaka Dodoma ni mpango wa muda mrefu. Imani yetu ni kwamba tutashirikiana na sekta binafsi kujenga vituo vidogo, vinaitwa ‘vituo dada’ ambavyo vitachukua gesi iliyogandamizwa kutoka Dar es Salaam na kuisambaza katika vituo mbali mbali nchini na baada ya hapo itasambazwa kutokea katika vituo hivyo.

Mheshimiwa Spika, tumeshapokea mpango wa uwekezaji wa jambo hilo na tutautangaza pale tutakapokuwa tumefikia makubaliano na sekta binafsi ya kupeleka gesi hii katika maeneo ambayo ni mbali na Dar es Salaam ambapo bomba halijafika.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili madogo. Swali la kwanza; licha ya mpango mzuri na unaoendelea wa upanuzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro lakini kuna mpango wa kujenga Hospitali ya kisasa ya Rufaa ya Mkoa wa Hospitali ya Morogoro.

Je, ni lini ujenzi huu utaanza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; katika Kituo cha Mafiga Manispaa ya Morogoro wanawake wengi wajawazito wanapenda sana kujifungulia kwenye kituo hicho lakini tatizo mojawapo linalojitokeza kituo hiko hakina jengo la upasuaji.

Je, kuna mpango gani wa kuweka jengo la upasuaji katika Kituo hicho cha Mafiga? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mbunge nikupongeze. Unakumbuka ulikuja na ukaniambia na tulikwenda hospitali ya mkoa na uliona miundombinu na uwekezaji mkubwa ambao umefanyika kwenye hospitali yenu ya mkoa. Najua lengo lenu, pamoja na upanuzi unaozungumziwa kwenye eneo hili la hospitali mnahitaji kujenga hospitali nyingine eneo lingine. Mimi nikuombe, kama nilivyosema hapa, majadiliano yanayoendelea kati ya Wizara na Ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro tukiyamaliza basi tutakaa pamoja ili tuweze kwenda forward tukiwa pamoja. Kwa sababu sasa hivi nikikupa majibu inawezekana huo mchakato wa kimkoa wakawa na mawazo mengine tofauti na hayo ambayo wewe unayo. Kwa hiyo tutashirikiana kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili unazungumzia kwamba pale kwa akina mama hakuna jengo la upasuaji. Mheshimiwa Mbunge naomba nikimaliza hili swali tukae mimi na wewe tukae na TAMISEMI tuweke mkakati wa pamoja tuhakikishe hicho unachokisema kinaenda kutokea.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika,
lini kipande cha barabara kutoka Kilosa hadi Mikumi kitaanza ujenzi kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara hiyo aliyoitaja Mheshimiwa ipo inaendelea kuanzia barabara ya Morogoro - Dar es Salaam na tumeshafika Kilosa ikiwa ni mwendelezo wa kwenda Mikumi, ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kuanzia Ifakara -Kihansi- Madeke mpaka Njombe? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum Morogoro, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja Serikali itaanza kujenga kadiri fedha itakapopatikana. Ahsante.
DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi kuuliza swali dogo. Barabara ya kuanzia Kilosa, Lumuma Mpwapwa Ulering’ombe mpaka Ruaha ni mbovu sana.

Je, ni lini angalau itafanyiwa ukarabati kwa kiwango cha changarawe? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ishengoma Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara zote za TANROADS zinatengenezwa kwa kiwango cha changarawe. Kwa hiyo nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo katika mwaka huu wa fedha tutahakikisha kwamba tunaitengeneza kama kuna sehemu ina udongo tutahakikisha kwamba tunapeleka fedha ili tuweze kutengeneza barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe ili iweze kupitika muda wowote ili kutoa huduma bora kwa wananchi wahusika, ahsante. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINA G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ni lini Shule ya Msingi SUA ambayo ina matatizo ya upungufu wa vyuo itafanyiwa ukarabati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sababu tathmini yetu itaisha mwezi Julai 2022 na tutakuwa na shule zote nchini, ikwemo ya Shule ya Msingi SUA ambayo ameiainisha hapa. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge, kwamba mara baada ya hiyo tathmini kila mmoja atajua shule yake inahudumiwa lini. Ahsante sana.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je, ni lini barabara ya kuanzia Mzumbe kibaoni kwenda mpaka Lubungo mpaka Kibambila ambayo ni Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero, mpaka Kimamba, Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa itajengwa na kupitika kwa mwaka mzima kwa kuunganisha wilaya zote mbili? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tutalifuatilia suala hili kwa kuona barabara hii kama imetengewa bajeti katika mwaka huu wa fedha tunaokwenda. Nafahamu Waziri wa Nchi, Mheshimiwa Angellah Kairuki amekaa na Waheshimiwa Wabunge wa Mikoa yote na kuangalia vipaumbele katika barabara, afya na elimu. Hivyo, tutaangalia kama barabara hii na yenyewe imo ili tuone ni namna gani ambavyo tunaweza tukawafikia wananchi hawa wa kwa Mheshimiwa Ishengoma.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika,
ahsante kwa kunipatia nafasi kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kabisa nashukuru sana kwa majibu ya Serikali kusikia kuwa barabara ya Mikumi – Kilosa imeanza kufikiriwa na itaanzwa kujengwa, lakini naomba ipewe kipaumbele kwa sababu ni barabara muhimu.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza: Kutokana na msongomano wa pale Msamvu, Morogoro Manispaa, naomba kujua barabara ya bypass ni lini itajengwa?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili: Ni lini itajengwa Barabara ya Ubena – Ngerengere mpaka Mvuha kwa kiwango cha lami? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya bypass katika Mji wa Morogoro ni sehemu ya Mpango wa Express Way ambayo itajengwa kutoka Chalinze hadi Morogoro na iko tayari kwenye usanifu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba itatokea Kingorowira – Makunganya hadi Sanganga eneo la Mzumbe. Kwa hiyo, hilo litaondoa changamoto ambayo ipo katika Mji wa Morogoro kwa maana ya msongamano. Kwa hiyo, tayari Serikali imelifanyia kazi na limeingizwa kwenye huo mpango.

Mheshimiwa Spika, swali la pili la barabara ya Ubena – Zomozi kwenda Ngerengere, barabara hii ilitangazwa kwanza kwa awamu kilometa 11.6 lakini haikupata Mkandarasi, imetangazwa tena kuijenga kwa kiwango cha lami, na hivi tunavyoongea sasa hivi, tathmini ya zabuni inaendelea kwa barabara hiyo kwa kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaanza kukarabati barabara ya kuanzia Bwakila Chini mpaka Bwakila Juu katika Halmashauri ya Morogoro Vijijini ili iweze kupitika bila ya matatizo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Dkt. Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutenga fedha kadri ya upatikanaji wa fedha kwenye bajeti kwa ajili ya ukarabati wa barabara. Ninaomba nichukue nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumwelekeza Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro na Meneja wa TARURA Wilaya ya Morogoro Vijijini kuhakikisha kwamba wanaenda kuiangalia hii barabara na kuona kama imetengewa fedha kwenye bajeti hii ambayo tumetoka kuiombea na Bunge lako Tukufu imepitisha ili kama ilitengewa fedha basi ukarabati wake uanze mara moja.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika,
ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Napenda kuuliza, ni lini Kituo cha Afya Mwaya, kilichopo Tarafa ya Mwaya, Wilayani Ulanga, kitafanyiwa ukarabati? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ni kipaumbele cha Serikali kufanya ukarabati kwenye vituo vya afya ambavyo ni vya muda mrefu na tutaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuweza kufanyiwa ukarabati kituo cha afya ambacho amekitaja Mheshimiwa Dkt. Ishengoma.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika,
ahsante sana kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; ni lini barabara ya Gairo hadi Milima ya Nongwe ambayo ni agizo la viongozi wa kitaifa, itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; barabara ya Ifakara – Mbingu – Chika – Mlimba ni mbovu sana; je, ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Gairo kwenda Nongwe ni barabara ya mkoa ambayo haijafanyiwa upembuzi yakinifu wala usanifu wa kina. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii TANROADS kupitia Mkoa wa Morogoro wameomba iwekwe kwenye upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa maana ya kufanya maandalizi ya kujenga kwa kiwango cha lami kwa mwaka huu wa fedha tunaouendea.

Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara aliyoitaja ya Ifakara - Mlimba - Kibena. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ya Awamu ya Sita tayari ilishatangaza barabara hii kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami, ambapo imegawanya katika lot mbili kuanzia Ifakara hadi Mbingu na Mbingu hadi Chita. Kwa hiyo, tayari iko kwenye hatua za manunuzi na tunategemea kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha barabara hii itakuwa pengine imeshaanza kujengwa, ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na foleni inayotokana kati ya Mkoa wa Morogoro na Pwani. Ni lini ujenzi wa barabara nne kuanzia Chalinze mpaka Morogoro Mjini utajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii ya Chalinze kwenda Morogoro ni barabara ambayo tumeifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kupitia makampuni ya Korea Kusini na mwezi wa nne walileta ripoti maalum inayoonesha ni kwa kiwango gani tujenge. Je, iwe ni kwa mfumo wa PPP ama iwe ktika mfumo wa EPC + Financing? Sasa Serikali imeona umuhimu wa barabara hii iwe katika mfumo wa PPP. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge niwahakikishie na wananchi wote wa eneo hilo kwa sababu ni barabara kuu, kwamba barabara hii itajengwa kwa mfumo wa PPP na tayari tumeshaanza ku– engage na wakandarasi, ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naishukuru Serikali kwa majibu mazuri, hasa kwa mradi wa Chagongwe kusikia kuwa utaanza. Licha ya hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata 29 za Manispaa ya Morogoro zinapata maji ya mgao. Je, kuna mkakati gani wa kupata maji safi na salama kila siku kwenye Kata hizo 29 za Manispaa ya Morogoro? (Makofi)

Swali la pili, mradi wa Magadu ambao upo kwenye Manispaa ya Morogoro umechukua muda mrefu na haujakamilika; je, ni lini utakamilika na kuanza kutoa maji kwa wananchi kwenye Kata hizo zinazozunguka? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, kwenye maeneo yote ya Mji wa Morogoro tuna mradi mkubwa wa AFD ambao tunatarajia ukaongeze uzalishaji wa maji na tatizo hili la mgao mkali wa maji pale Morogoro tunatarajia litapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile mradi wa Magadu tayari tumeutekeleza kwa asilimia 90, Mheshimiwa Mbunge anafahamu tulishaongea pamoja hili na tumefuatilia kwa pamoja Wakandarasi wanaendelea na kazi na tayari Wizara tumeshapeleka fedha, tunatarajia kufika mwezi Juni huu mradi wa Magadu nao uanze kutoa huduma kwa wananchi. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Je, ni lini skimu ya umwagiliaji ya Kwamtonga iliyopo kwenye Kata ya Sungaji Wilayani Mvomero itafanyiwa uboreshaji kusudi wananchi wengi waweze kulima kwa mwaka mzima kwani maji ya kutosha yapo? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kiambatanisho Na. 8 katika bajeti ya Wizara ya Kilimo aliyosoma Mheshimiwa Waziri, tumeorodhesha skimu zote ambazo tutazifanyia ukarabati na ikiwemo skimu ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja. Nimwondoe hofu, hii kazi itafanyika.
MHE. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema kuwa wawekezaji kuingiza hizi nyavu zilizo bora wanahamasisha; je, kuna mkakati gani wa Serikali wa kuhamasisha hawa wawekezaji wanaoleta hizi nyavu badala ya kuleta wakaanzisha viwanda hapa Tanzania vya kutengeneza hizi nyavu zinazotakiwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mto Kilombero kuna wavuvi wanaovua sana sana kutoka Wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi; je, kuna mpango gani wa kuhamasisha na kuwapatia nyavu bora za uvuvi? Ahsante sana.
WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Morogoro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, je tumejipangaje kwenye kuhamasisha juu ya ujenzi wa viwanda vya nyavu hapa nchini? Jambo hili tayari linafanywa na tumekwisha kuanza kupata viwanda ambavyo vinatengeneza nyavu. Pale Mwanza tunacho kiwanda kipya kinaitwa Ziwa Net ambacho kinatengeneza nyavu na kuwauzia wavuvi na tunayo maombi pia vilevile ambayo tunashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa ajili ya uwekezaji kwenye eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili ni suala la zana kwa ajili ya wavuvi kwenye mto Kilombero. Jambo hili nimelichukua kama ombi la Mheshimiwa Mbunge, Dkt. Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum na nitakwenda kuzungumza naye ili kuweza kuandaa wavuvi wa Mto Kilombero katika vikundi na baadae na wao ikiwezekana waweze kupata hizi zana kama ambavyo wanapata wavuvi wengine nchini.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Wananchi wa Kiegea, Mkundi pamoja na Kilimanjaro bado hawapati maji ya kutosha; je, ni lini watapata maji ya kutosha kutoka kwenye mradi wa Mguu wa Ndege? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Christine. Huu mradi mimi na yeye akiwa Mwenyekiti wa Kamati tulifika na kuufuatilia kwa karibu sana na anaendelea kuufuatilia. Mpaka sasa tumeshaweza kutekeleza mradi kwa asilimia 86. Maeneo ya Kihonda Kaskazini na Kilimanjaro, hivi navyoongea tayari wameshaanza kupata huduma.

Mheshimiwa Spika, maeneo haya aliyoyataja Mheshimiwa Dkt. Christine na yenyewe pia tunaendelea kufanya jitihada kuona kwamba kufikia Desemba, mwaka huu 2023 na yenyewe pia yaweze kupata huduma ya uhakika.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga Barabara ya kuanzia pale SUA mpaka Mzinga Jeshini - Magadu, katika Manispaa ya Morogoro Mjini? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaangalia katika bajeti hii iliyopitishwa na Bunge lako tukufu ya 2023/2024 kwa TARURA, kuona kama barabara ya SUA kwenda Mzinga imetengewa fedha. Kama haikutengewa fedha katika mwaka huu wa fedha basi tutaiangalia ni namna gani inaweza ikatengewa fedha katika mwaka wa fedha 2024/2025.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Je, ni lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji katika maeneo ya Mavimba, Lupilo, Minepa, Kivukoni, Namilela katika Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tumeainisha maeneo mengi ambayo tunakwenda kuyafanyia kazi katika mwaka wa fedha ujao. Nitakaa na Mheshimiwa Mbunge kuangalia maeneo ambayo ameyataja kama hayajajumuishwa basi tuweze kuyaweka katika mpango wetu ili kuhakikisha wananchi hao pia wanafanya kilimo cha umwagiliaji.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kufuatana na swali la msingi, nilikuwa natanguliza tu, maombi yatakuja, tayari tumeshaongelea, kwa hiyo, yatakuja. Yakija naomba mtufikire.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza. Manispaa yetu ya Morogoro ina kata 29 lakini ina tarafa moja. Kata zake ni kubwa sana: Je, Serikali haioni kuwa inaweza angalau ikatupatia tarafa ya pili kusudi kuwe na tarafa mbili kwa sababu kata ni nyingi sana? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili. Kwa sababu mkazo wa Serikali sasa hivi ni kuimarisha miundombinu pamoja na huduma za jamii; miundombinu ya Manispaa ya Morogoro bado siyo mizuri hasa kwa upande wa Barabara: Je, ni lini Serikali itaweza kuwapa fedha na kuwaongezea kusudi barabara zetu za Manispaa ya Morogoro ziweze kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la kuongezwa tarafa ya pili. Naomba kumshauri Mheshimiwa Mbunge na pia kuishauri Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kufanya vikao kwa ajili ya maombi hayo kama ambavyo amesema juu ya maombi ya kuwa Halmashauri ya Jiji. Utaratibu uko wazi. Kikao cha kwanza ni cha Bodi ya Ushauri ya Wilaya (DCC), baada ya hapo maamuzi yenu yanapelekwa katika kikao cha Mkoa, yaani Bodi ya Ushauri ya Mkoa (RCC) na baada ya hapo tunakwenda kumwasilishia Mheshimiwa Waziri ili sasa maamuzi ya kugawa Halmashauri yenu au Manispaa yenu ili mweze kupata tarafa ya pili na taratibu nyingine kwa ajili ya kuwa jiji ziweze kufanyika.

Mheshimiwa Spika, hilo ni jibu kwa swali la kwanza. Swali la pili, nataka kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, Serikali kupitia TARURA imeendelea kutenga bajeti kwa ajili ya kuhakikisha kwamba inaimarisha miundombinu katika majiji yetu, Manispaa zetu na Halmashauri zetu zote zilizopo ndani ya nchi yetu. Hivyo nataka nimhakikishie tena Mheshimiwa Mbunge kupitia Halmashauri yake, watengeneze bajeti yao, watengeneze vipaumbele vyao, watuletee Ofisi ya Rais, TAMISEMI na tutakwenda kufanyia kazi.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyonyeza. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kuanzia Gairo – Chanjale - Kibakwe hadi Mpwapwa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ishengoma kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hii barabara ilifanyiwa usanifu wa awali na bado haijafanyiwa usanifu wa kina. Kwa hiyo, barabara hii ikishafanyiwa usanifu wa kina, Serikali itakuwa imefahamu gharama ya hiyo barabara na ndiyo tutaanza sasa kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, je lini Serikali itajenga Barabara ya Mikumi, Kisanga, Maroro kwa kiwango wa changarawe? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itajenga Barabara hii ya Mikumi, Kisanga kama ambavyo ameuliza Dkt. Ishengoma kadiri ya upatikanaji wa fedha na tutaangalia katika mwaka wa fedha huu unaoanza, ambapo TARURA vile Bunge hili lilipitishia bajeti kubwa ya kuweza kutekeleza barabara hizi kuona kama imetengewa fedha na kama haijatengewa fedha tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata ili barabara hii iweze kutengewa fedha.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Kituo cha Afya cha Mafiga ni kituo kikubwa ambacho hasa kinatoa huduma kwa akinamama wajawazito. Je, ni lini Serikali itatoa hela ya kumalizia jengo la upasuaji?
NAIBU WAZIRI OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itatoa fedha kwa ajili ya umaliziaji wa Kituo hiki cha Afya Mafiga kadri ya upatikanaji wake, lakini tutaangalia katika mwaka wa fedha 2023/2024 kama kuna fedha imetengwa ili iweze kupelekwa mara moja kwa ajili ya kumalizia kituo hicho.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je ni lini Serikali itapeleka fedha kwenye ukarabati wa shule ya Sekondari ya SUA?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la Dkt. Ishengoma la Serikali kupeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa shule ya Sekondari ya SUA. Tutatuma timu pale ya Afisa Elimu wetu wa Sekondari katika Halmashauri ile kuweza kufanya tathmini ya nini kinachohitajika kufanyika katika ukarabai ule na watawasilisha taarifa ile Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya ukarabati wa Shule ya Sekondari SUA.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro iko katikati ya Majiji ya Dodoma, Arusha na Dar es Salaam. Je, ni lini Manispaa ya Morogoro itakuwa Jiji?

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Dkt. Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, endapo Manispaa ya Morogoro itakuwa imekidhi vigezo na itakuwa imefuata taratibu zote, jukumu letu kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI, ni kufanya tathmini na kupeleka mapendekezo hayo kwa mamlaka ili iweze kufanya maamuzi. Ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kufuatia swali la msingi, Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Kilosa – Lumuma ambayo ni barabara muhimu kwa kuchukua vitunguu, iweze kupitika mwaka mzima bila ya matatizo?

Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali Mheshimwia Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya barabara muhimu zote katika halmashauri zetu zote kote nchini na tumewaelekeza mameneja wa TARURA katika wilaya hizo kuweka kipaumbele kwenye barabara zote muhimu kama ambayo hii ameitaja Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma. Kwa hiyo, nitoe maelekezo kwa meneja wa TARURA wa Wilaya hii ya Kilosa lakini pia wa Mkoa wa Morogoro kuhakikisha wanaipa kipaumbele barabara hii katika bajeti ili iweze kutimiza malengo ya kusafirisha bidhaa muhimu ambazo Mheshimiwa Mbunge amesema, ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kufuatia swali la msingi, Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Kilosa – Lumuma ambayo ni barabara muhimu kwa kuchukua vitunguu, iweze kupitika mwaka mzima bila ya matatizo?

Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali Mheshimwia Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imefanya tathmini ya barabara muhimu zote katika halmashauri zetu zote kote nchini na tumewaelekeza mameneja wa TARURA katika wilaya hizo kuweka kipaumbele kwenye barabara zote muhimu kama ambayo hii ameitaja Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma. Kwa hiyo, nitoe maelekezo kwa meneja wa TARURA wa Wilaya hii ya Kilosa lakini pia wa Mkoa wa Morogoro kuhakikisha wanaipa kipaumbele barabara hii katika bajeti ili iweze kutimiza malengo ya kusafirisha bidhaa muhimu ambazo Mheshimiwa Mbunge amesema, ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini hata hivyo nina swali la nyongeza.

Kwa kuwa nchi yetu imefaidika sana kutokana na balozi mbalimbali ambazo tumefungua nchi mbalimbali na hasa kwenye uwekezaji, biashara, pamoja na utalii na hasa kwenye biashara ya mazao ya kilimo.

Je, nchi hii ya Pakistan kwa sababu wana ubalozi wao hapa nchini tunashirikianaje pamoja na nchi hii?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana; naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ingawa Tanzania haina ubalozi nchini Pakistan lakini tunawakilishwa na ubalozi wetu ambao upo Abu Dhabi UAE. Kwa hiyo, mahusiano ya nchi zetu mbili hizi ni makubwa na tumekuwa tukishirikiana katika masuala mbalimbali hasa ya kibiashara ambapo nchi yetu imekuwa ikisafirisha kwenda Pakistan bidhaa kama pamba, chai na madini ya vito kama vile Tanzanite pamoja na nafaka kama vile maharage. Lakini pia kutoka Pakistan tumekuwa pia tukishirikiana nao na tumekuwa tuki-import bidhaa za dawa za binadamu pamoja na dawa za viwanda vya nguo na nafaka. Nashukuru sana.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, asante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaboresha na kupanua Kituo cha Afya cha Mvomero? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwenye mpango mkakati wa kupanua na kuboresha vituo vya afya tutahakikisha pia tunakifanyia tathmini kituo hicho na kutenga fedha ili tuende kukarabati na kupanua kituoo hicho kwa awamu, ahsante.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Serikali, nina maswali madogo mawili.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Kata ya Mgambazi ipo kwenye Manispaa ya Morogoro, lakini mpaka sasa hivi Mtaa mzima wa Mgambazi pamoja na Chambilazi na Vilengwe hawajapatiwa umeme, licha ya kuwa kwenye Manispaa ya Morogoro: Je, ni lini watapata umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kijiji cha Zongo ambacho kiko kwenye Kata ya Kisemo pamoja na Kijiji cha Bwakila Juu katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini, hawajapata umeme. Ni lini vijiji hivi vitapatiwa umeme? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Dkt. Christine Ishengoma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na umeme katika Mitaa ya Mungazi, Chambilazi na Vilengwe tayari tumeshaiweka kwenye Mpango wa fedha wa 2025 na mitaa hii itapatiwa umeme.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Vijiji vya Zongo na Bwakila Juu, tayari wakandarasi wamepatiwa site na muda wowote kazi itaanza, ahsante. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa naishukuru Serikali kwa ujenzi wa Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali kwenye Mkoa wetu wa Morogoro. Hii Zahanati ya Uwanja wa Ndege ina upungufu wa wafanyakazi hasa manesi na madaktari. Je, ni lini mtapeleka hao Manesi na Madaktari ili kutimiza ikama? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Kituo cha Afya Mafiga kimekuwa na tatizo sana la theatre na wanawake wengi wajawazito wanapenda sana kujifungulia pale, na mara wanapopata matatizo, wanapelekwa Hospitali Kubwa ambapo kuna mwendo. Je, ni lini Kituo hiki cha theatre kitajengwa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu kwamba Zahanati hii ya Uwanja wa Ndege ina watumishi watano; Afisa Tabibu mmoja, Wauguzi wawili, Mtaalamu wa Maabara mmoja na Mhudumu wa Afya mmoja. Kwa idadi ya wananchi ambao wanatibiwa pale, tunahitaji kuongeza wataalamu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tayari Serikali imeshaitambua Zahanati hiyo, mara ajira zitakapojitokeza, tutahakikisha tunawapa kipaumbele kwa ajili ya kuongeza idadi ya watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la pili, Kituo cha Afya cha Mafiga ni kweli kipo mjini na kinahudumia wananchi wengi na kina upungufu wa baadhi ya miundombinu ikiwepo majengo ya upasuaji na majengo mengine. Tushamwelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kuandaa mchoro wa upanuzi wa Kituo cha Afya cha Mafiga. Nitumie fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafuatilia ili tuweze kuona umefikia hatua gani na tuone uwezekano wa kuongeza majengo katika Kituo cha Afya cha Mafiga, ahsante. (Makofi)
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itajenga skimu za umwagiliaji kwenye Kata za Minepa, Mazimba na Lupiro Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kama nilivyojibu swali la msingi, lakini vilevile swali la nyongeza la Mheshimiwa Rashid Shangazi, nimjibu tu Mheshimiwa Christine Ishengoma kwamba maeneo yote haya ambayo yanafaa kwa ajili ya umwagiliaji tumeiagiza Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kuyapitia yote nchini kuyaweka katika mpango makakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mpaka sasa hivi tumeshafikia takriban asilimia 70 ya maeneo yote ambayo yanafaa kwa kilimo. Kwa hiyo, hata haya nayo mengine yamefikiwa mengine tunaendelea na utekelezaji wake. Kwa hiyo nimuondoe shaka kazi hiyo inafanyika. Ahsante sana.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, licha ya kupeleka umeme katika Kata za Chenzema, Langala na hizo nyingine zote, naishukuru Serikali kwa sababu inachukua huduma sana kwenye umeme: Je, ni lini vijiji vya Kidunda pamoja na Ngolehanga vitaweza kupatiwa umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini vijiji na vitongoji vya Morogoro vijijini vitaweza kupata umeme? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Morogoro kwa ujumla wake una vijiji vilivyohitaji kupatiwa umeme takribani 668. Vijiji ambavyo vilikuwa vipo katika mpango wa kupelekewa umeme ni vijiji 239. Mpaka sasa tumeshapeleka umeme kwenye vijiji takribani asilimia 90. Makusudio yetu ni kwamba vijiji vyote vya Mkoa wa Morogoro ikifika mwezi Juni mwaka huu viwe vimepatiwa umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile mkakati wetu ni kuhakikisha kwamba tupo katika hatua ya mwisho ya kupeleka umeme kwenye vitongoji 15 vya kila jimbo la nchi yetu na matarajio yetu ni kwamba kazi hii itakamilika, uratibu wa kazi hii utakamilika hivi karibuni na tutaweza kuanza kufanya kazi hiyo.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye vijiji sita vilivyobakia kwenye Tarafa ya Mikumi?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mkandarasi katika vijiji hivi yuko site anaendelea na kazi. Nimhakikishie tu, ifikapo Juni, 2024 vijiji hivi vyote vitakuwa vimepatiwa umeme, ahsante.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa naishukuru Serikali kwa ujenzi wa Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali kwenye Mkoa wetu wa Morogoro. Hii Zahanati ya Uwanja wa Ndege ina upungufu wa wafanyakazi hasa manesi na madaktari. Je, ni lini mtapeleka hao Manesi na Madaktari ili kutimiza ikama? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Kituo cha Afya Mafiga kimekuwa na tatizo sana la theatre na wanawake wengi wajawazito wanapenda sana kujifungulia pale, na mara wanapopata matatizo, wanapelekwa Hospitali Kubwa ambapo kuna mwendo. Je, ni lini Kituo hiki cha theatre kitajengwa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu kwamba Zahanati hii ya Uwanja wa Ndege ina watumishi watano; Afisa Tabibu mmoja, Wauguzi wawili, Mtaalamu wa Maabara mmoja na Mhudumu wa Afya mmoja. Kwa idadi ya wananchi ambao wanatibiwa pale, tunahitaji kuongeza wataalamu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tayari Serikali imeshaitambua Zahanati hiyo, mara ajira zitakapojitokeza, tutahakikisha tunawapa kipaumbele kwa ajili ya kuongeza idadi ya watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la pili, Kituo cha Afya cha Mafiga ni kweli kipo mjini na kinahudumia wananchi wengi na kina upungufu wa baadhi ya miundombinu ikiwepo majengo ya upasuaji na majengo mengine. Tushamwelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kuandaa mchoro wa upanuzi wa Kituo cha Afya cha Mafiga. Nitumie fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafuatilia ili tuweze kuona umefikia hatua gani na tuone uwezekano wa kuongeza majengo katika Kituo cha Afya cha Mafiga, ahsante. (Makofi)