Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula (6 total)

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA aliuliza: -

Je, lini mgogoro kati ya wananchi wa Kiwanja cha Ndege Mwanza na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege – Mwanza utatatuliwa?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali Kuu kwa kushirikiana na Serikali ya Mkoa ina nia ya dhati na imeendelea na jitihada mbalimbali katika kushughulikia mgogoro huu ili kuhakikisha unaisha. Aidha, taratibu za utwaaji ardhi zinaendelea kwa kufanya uthamini wa mali za wananchi, pindi uthamini utakapokamilika taratibu nyingine zitaendelea kulingana na Sheria ya Ardhi pamoja na Sheria ya Uthamini.
MHE. STANSLAUS S. MABULA K.n.y. MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA aliuliza:-

Je, lini mgogoro kati ya wananchi wa Kiwanja cha Ndege Mwanza na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege - Mwanza utatatuliwa?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Angeline Sylvester Mabula, Mbunge wa Ilemela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali Kuu kwa kushirikiana na Serikali ya Mkoa ina nia ya dhati na imeendelea na jitihada mbalimbali katika kushughulikia mgogoro huu ili kuhakikisha unaisha. Aidha, taratibu za utwaaji ardhi zinaendelea kwa kufanya uthamini wa mali za wananchi. Pindi uthamini utakapokamilika, taratibu nyingine zitaendelea kulingana na Sheria ya Ardhi pamoja na Sheria ya Uthamini.
MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA aliuliza:-

Je, lini ujenzi wa Kingo za Mto Msuka Ilemela utakamilika ili kuepusha vifo vya mara kwa mara pindi mvua zinaponyesha?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Ujenzi wa Kingo za Mto Msuka unaendelea ambapo hadi sasa ujenzi wa daraja na kingo zake zenye urefu wa takribani meta 500 umekamilika. Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Manispaa ya Ilemela kupitia Mradi wa Tanzania Cities Transforming Infrastructure and Competitiveness ambao unafadhiliwa na Benki ya Dunia imeomba kiasi cha shilingi bilioni 6.7 kwa ajili ya ujenzi wa barabara na kukamilisha ujenzi wa Kingo za Mto Msuka ambapo ujenzi wake utaendelea baada ya fedha hizo zilizoombwa kupatikana.
MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA aliuliza: -

Je, lini Wananchi wa Kiwanja cha Ndege Mwanza watalipwa fidia zao kwa kuwa tathmini imefanyika mara mbili sasa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI K.n.y. WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Uchukuzi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela na Nyamagana zinaendelelea kukamilisha taratibu za uteuzi wa eneo ambalo litapangwa na kupimwa ili wananchi watakaoondolewa wamilikishwe kwa gharama nafuu. Katika zoezi hilo jumla Kaya zipatazo 1,404 zinatakiwa kupisha eneo la Uwanja wa Ndege wa Mwanza, ahsante.
MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA aliuliza:-

Je, lini ATCL itaanzisha usafiri wa Ndege kutoka Dodoma – Mwanza - Mbeya na Arusha ili kupunguza gharama kwa wasafiri wanaokwenda mikoa hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ATCL inaendelea kupanua mtandao wa safari kwa kuzingatia mpango mkakati wake na mahitaji ya soko. Kwa sasa, ATCL inahudumia vituo 26 kutokea Dar es Salaam vikiwemo vituo 14 vya ndani ya nchi. Safari za Dodoma – Mwanza zinatarajiwa kuanza Desemba 2025, huku tathmini ikiendelea kwa safari za Dodoma – Mbeya na Dodoma – Arusha.
MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga uzio katika Shule za msingi ambazo hazina uzio maeneo ya mijini?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuboresha miundombinu ya elimu nchini ikiwa ni pamoja na kujenga uzio katika shule mbalimbali za msingi kwa kuzipa kipaumbele shule zenye watoto wenye mahitaji maalumu. Katika mwaka 2022/2023 na 2023/2024 Serikali imetoa shilingi bilioni 5.57 kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika shule 185 za watoto wenye mahitaji maalumu. Vilevile, Mamlaka za Serikali za Mitaa zimekuwa zikitenga fedha kupitia mapato ya ndani kujenga uzio ili kuimarisha ulinzi katika maeneo yenye changamoto za kiusalama. Serikali kupitia mapato ya ndani ya halmashauri itaendelea kutenga fedha za ujenzi wa uzio kwa ajili ya usalama wa wanafunzi na mali za shule kadiri ya upatikanaji wa fedha, ahsante.