Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Mansoor Shanif Jamal (1 total)

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA K.n.y. MHE. SHANIF J. MANSOOR aliuliza: -

Je, ni lini Chuo cha VETA Ngudu Kwimba kitakamilika?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shanif Jamal Mansoor, Mbunge wa Jimbo la Kwimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kukamilisha ujenzi wa vyuo vya VETA Nchini. Kwa sasa inakamilisha hatua ya uwekaji wa samani pamoja na kuandaa rasilimaliwatu kwa lengo la kuviwezesha vyuo vya VETA ikiwemo Chuo cha Ngudu kuanza kutoa mafunzo kwa mwaka wa masomo 2023/2024.

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Chuo cha VETA Ngudu upo katika hatua ya ukamilishaji na umefikia asilimia 97. Aidha, Wizara kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeshapeleka kiasi cha shilingi 189,607,486.00 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa chuo hicho, nakushukuru.