Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. Halima James Mdee (1 total)

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nimefurahi kusikia kwamba Tanzania tuna ligi ya under 17 lakini ligi hii haionekani kuwa promoted.

Je, Serikali haioni haja sasa ya kuvitaka vilabu vya premier league kulazimishwa kuwa na timu za under 17 ambazo zinashiriki katika hiyo premier league?
WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze Mheshimiwa Tarimba Gulam Abbas kwa mchango wake kuendeleza michezo. Nilimwona akishangilia kombe lile la Yanga hivi juzi, lakini ningemwomba pia angeshangilia na lile la Simba la Muungano. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali lake la msingi, ligi ya under 17 inaendeshwa na vilabu vya championship, league under 20 inaendeshwa na vilabu vya premier league lakini nimepokea wazo lake kwamba vilabu vya premier league sasa navyo viwe na league ya under 17 na league ya under 14 katika mkakati wa kukuza na kuibua vipaji. (Makofi)