Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Grace Victor Tendega (62 total)

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali la kwanza, katika majibu ya Mheshimiwa Waziri amesema kuwa REA III imeanza Machi, 2017. Kwa kuwa wananchi katika vijiji hivyo vya Wangama, Ikuvilo, Tagamenda, Lupembelwasenga pamoja na Lyamgungwe ni wakulima na wanajihusisha na kilimo cha umwagiliaji na kuna wawekezaji ambao wameonesha nia ya kujenga viwanda na tunasema tunahitaji Tanzania ya viwanda lakini umeme haupo. Naomba commitment ya Serikali ni lini watapata umeme kwa sababu imekuwa ni muda mrefu kutopatiwa umeme katika maeneo hayo ili wanufaike na viwanda? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika kipengele
cha kwanza majibu ya Waziri ni tofauti kabisa na hali halisi ya eneo hilo la Malulumo kwa sababu mimi natokea eneo hilo na wanasema utekelezaji umefanyika kwa 90%. Je, Waziri yuko tayari kuongozana na mimi akaone huo utekelezaji wa 90% uliopo maeneo yale? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze na swali la pili, niko tayari kufuatana na Mheshimiwa Grace kwenda kwenye eneo lake ili kuangalia utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya Tatu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Grace tukimaliza Bunge tu mguu mmoja mimi na wewe Iringa tukamalize kazi hiyo, lakini kwa ruhusa yako Mwenyekiti. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini sasa vijiji vilivyobaki vitapatiwa umeme. Awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Grace na Wabunge wote wa Mkoa wa Iringa kwa jinsi ambavyo wanafuatilia utekelezaji wa miradi ya umeme. Niwahakikishie kwamba tarehe 21 Machi, 2017 tulizindua rasmi utekelezaji wa Mradi wa Umeme Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Iringa na eneo la Iliwa kwa Mheshimiwa Mwamoto ndipo tulipofanyia uzinduzi kwa niaba ya mkoa.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niwahakikishie kabisa Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Iringa pamoja na Mufindi, Kilolo, Njombe, tumeshawakabidhi wakandarasi wawili, NACROI na NAMIS na wameshaanza utekelezaji wa kazi hiyo. Kwa hiyo, kuanzia Machi tumeshaanza kutekeleza mradi huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji ambavyo amevitaja Mheshimiwa Grace vya Wangama, Lupembelwasenga, Tagamenda na Mseke pamoja na vijiji vingine ambavyo amevitaja na kwa Mheshimiwa Mwamoto vitapatiwa umeme katika awamu hii ya mradi. Nimeenda kwa Mheshimiwa Mwamoto na Waheshimiwa Wabunge wengine, nimeenda Nang’uruwe, Kihesa Mgagao na huko tumeshawapelekea umeme. Kwa hiyo, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba utekelezaji wa mradi huu umeanza na utakamilika mwaka 2020/2021.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza nitoe masikitiko makubwa sana kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri, ambapo tarehe 8 Juni, 2016 niliuliza swali kuhusu vijiji na kata hizo hizo na aliyekuwa Naibu Waziri na sasa ni Waziri mwenye dhamana TAMISEMI alinipa majibu ambayo yalikuwa yanaeleza kwamba vijiji hivyo vimetengewa bajeti ya shilingi milioni 49.5 ambayo itatekelezwa mwaka 2016/2017. Mpaka sasa hivi hakuna kinachoendelea, ni Bunge hili hili ambalo linatoa majibu hayo na leo tena nimepewa asilimia hiyohiyo 49.5 kwamba itatekelezwa 2018/2019. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali langu, ni lini Serikali itapeleka pesa kwa wananchi hawa, toka mwaka 1995 mpaka leo ni upembuzi yakinifu unafanyika, ni lini hawa wananchi watapata maji? (Makofi)
MheshimiwaMwenyekiti, swali la pili, ni kwa nini hawakufanya upembuzi wa kina wakati bajeti ilitengwa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, ni kweli kwamba usanifu wa kina haukufanyika ule wa zamani, lakini kwa sasa tunatarajia usanifu kina utafanyika mwaka 2018/2019 kwa ajili ya utekelezaji wa kumaliza kabisa matatizo ya maji kwenye maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ambalo lilikuwa ndiyo la kwanza, ni kwamba kazi ambazo zimefanyika kuanzia 2016 mpaka Desemba, 2017 nimesema hapa kwamba tumejenga visima sita katika Kata za Magulilwa, Luhota, Maboga na Mgama. Hii kazi imefanyika na taarifa hizi zimetoka kule kule kwenye Halmashauri yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, taarifa za kina zaidi namuomba sana tushirikiane naye baada ya kikao hiki ili tuweze kushauriana vizuri namna bora ya kuhakikisha kwamba tunamaliza matatizo ya wananchi kwenye maeneo hayo.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza:
Mheshimiwa Naibu Spika, majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kabisa yanaonyesha jinsi ambavyo walimu wetu wamekuwa wakikosa nyumba za kuishi, walimu wa sekondari 52,000 hawana mahala pa kuishi na walimu 130,300 wa shule za msingi hawana nyumba za kuishi. Tumesema tunataka kuwa na elimu bora katika nchi yetu na hatufahamu walimu wanaishi wapi.
Je, Serikali sasa haioni ni wakati muafaka sasa wa kuamuru Jeshi la Polisi liweze kujenga nyumba hizi za walimu kama walivyofanya kwa Mererani kuzuia ile migodi yetu, tatizo hili ili liweze kuisha kwa haraka?
Swali la pili, walimu wamekuwa wakikosa udhamini katika mabenki mbalimbali kwa kutokuwa na mali za kudhaminiwa na taasisi alizozitaja Mheshimiwa Naibu Waziri ni hizo ambazo huwezi kudhaminiwa kama huna dhamana ya vitu visivyohamishika kama viwanja, magari na vitu vingine na tunatambua hali za walimu wetu zilivyo.
Je, sasa Serikali haioni haja kwamba ni wakati muafaka Mifuko ya Hifadhi ya Jamii iweze kuwa dhamana kwa walimu wetu wakati bado wakiwa kazini na siyo baada ya kustaafu? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda nisisitize kwamba katika jibu langu la msingi ile takwimu niliyoitaja kwa faida ya Bunge lako tukufu haikumaanisha kwamba walimu hao hawana makazi kabisa. Nimesema kwamba walimu hao wanaishi katika aidha, nyumba za kupanga au nyumba zao binafsi, hilo ndilo jibu langu la msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya kwanza ya swali lake kwamba kwa nini Serikali isiamuru Jeshi la Polisi kujenga nyumba za walimu nchi nzima, hilo ninaomba sana majeshi yetu yana kazi zake maalum ambayo yamepewa kufanya na waliojenga ukuta wa Mererani siyo Jeshi la Polisi ni Kitengo cha Ujenzi cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Tumekuwa tukiwapa kazi nyingi sana, SUMA JKT kujenga nyumba za walimu kujenga nyumba za walimu katika mahali pengi. Hata kwake kule Iringa tumewapa sehemu nyingi tu SUMA JKT kujenga nyumba na tutaendelea kuwapa mikataba ya kujenga nyumba.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumesema kwamba ujenzi wa nyumba ambao unafanywa na Serikali utaendelea kuwa kidogo kidogo kwa sababu unategemea sana bajeti ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, napenda nimuondoe wasiwasi kuhusu dhamana. Karibu mabenki yote na taasisi zote zinazokopesha hakuna dhamana zaidi ya mshahara wa mtumishi. Kinachotakiwa tu ni kwamba mtumishi asiwe anadaiwa mikopo mingine hilo ndiyo jambo la msingi, kama mtumishi hadaiwi mikopo mingine anao uwezo wa kukopa na ataamua mwenyewe, je, akope kwa kurejesha miaka mitatu au akope kwa kurejesha miaka 10 au akope kwa kurejesha miaka 25 ni yeye mwenyewe katika makubaliano ya fomu yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, napenda kuwasisitiza watumishi wote nchi nzima na Wakurugenzi wa Halmashauri ambao wako chini yangu nataka niwaambie kwamba mikopo hiyo ya watumishi ipo, waingie makubaliano maalum na hizo taasisi na mabenki ili kusudi watumishi waweze kukopesha waweze kujenga nyumba zao binafsi. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mradi wa Ibofwe uko Mkoani Iringa ambao unahudumia vijiji 10. Nilikwishauliza swali la msingi nikajibiwa kwamba shilingi milioni 49 zitatolewa baada ya kutoka certificate. Certificate ilishatolewa pesa hazijapatikana toka mwaka jana, naomba kujua ni lini pesa hizo zitatolewa?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nitumie nafasi hii kumjibu Mheshimiwa Mbunge, kwa kuwa maji ni uhai na sisi kama Wizara ya Maji hatupo tayari kupoteza uhai wa wana Iringa, namuomba Mheshimiwa Mbunge baada ya Bunge tukae na wataalam wetu tuangalie namna ya kuzipeleka fedha hizo wananchi wapate maji.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa nasikitika Waziri anavyojibu, anaingiza suala la Mbunge wa Jimbo wakati mimi niliuliza swali langu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, majibu ya Waziri hayajaniridhisha kabisa. Kuna vijiji vya Kimala, Idete, Uluti, Nyamuhanga, Ibofwee na Itimb. na vingine ambavyo sijavitaja wanajihusisha sana na kilimo kwa ajili ya biashara pamoja na kuzalisha zao la mbao, ambayo yote haya yanahitaji mawasiliano kwa ajili ya kupata soko. Je, ni lini Serikali itahakikisha kuwa wananchi hawa wanapata mawasiliano ili waweze kuuza mazao yao na kupata masoko wanayoyahitaji? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Waziri amesema minara hiyo imejengwa na inatoa huduma kama kawaida, yuko tayari twende akaone hiyo minara anayosema inatoa huduma ili ahakikishe mwenyewe kwamba huduma hiyo haipatikani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASIALIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Tendega, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimuondoe masikitiko kwa sababu hizi shughuli tunazifanya kwa kuwa tunazijua na tumeshatembelea na kufanya survey ya kutosha nchi nzima kujua maeneo gani yana shida ya mawasiliano critical na eneo gani ambalo lina shida ya mawasiliano ya kawaida ambayo yanahitaji kuongezewa coverage na ni maeneo gani ambayo yana shida za mawasiliano kwa vipindi tu vifupi kutokana na kufungiwa solar badala ya umeme wa kawaida. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza kujibu maswali yake kuhusu eneo la Kimala, Kidete na vijiji vinavyohusiana, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba nitafanya ziara baada ya Bunge hili la bajeti kwenye maeneo yote pamoja na maeneo ya Kata nzima ya Kising’a najua kuna changamoto za mawasiliano, lakini nitafanya ziara kwenye Kata ya Mahenge, maeneo ya Magana na Ilindi ambako kuna shida kabisa ya mawasiliano, vilevile nitafanya ziara kwenye Kata ya Ibumu kwenye Kijiji cha Ilambo kuangalia kuhusu changamoto ya mawasiliano ya simu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, nitakuwa tayari kuongozana naye pamoja na Mbunge wa Jimbo kuangalia maeneo hayo. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa kutokana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri napenda Serikali isikwepe wajibu wake wa kuhudumia watu wasiojiweza. Natambua kabisa kuwa kuna walemavu wenye uwezo lakini watu wengi wenye ulemavu wana matatizo mengi; kuna wale ambao ni yatima, kuna wengine ambao wametelekezwa na kuna wengine ambao kaya zao ni maskini sana. Ni kwa nini Serikali isiwajibike kuwahudumia watu hawa wenye ulemavu hasa kwa kuwatambua na pili kuwapatia bima ya afya bure? Hilo ni swali la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika majibu ya Mheshimiwa Waziri amesema wagonjwa kuna wagonjwa wengi sana wa msamaha ambao wako katika hospitali zetu. Sawa wako wagonjwa wengi lakini ni lini Serikali sasa itatekeleza wajibu wake wa kutoa ruzuku katika hospitali zetu za mikoa au hospitali zetu za rufaa kwa sababu hawa wagonjwa ambapo wengine ni watu wenye ulemavu, watoto umri chini ya miaka mitano na wazee wanakwenda katika hospitali hizi kutibiwa na hizi hospitali zinakuwa na watu wengi ambao wanatakiwa kupata vifaatiba na vitendanishi? Ni lini Serikali itatoa ruzuku katika hospitali zetu ili ziweze kujikimu na kutoa huduma bora? Ahsante (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba Serikali inaendelea kutoa huduma za afya na haijawahi kusitisha kutoa huduma ya afya kutokana na sababu eti kwamba mtu anashindwa kugharamia matibabu. Hilo lipo vizuri ndani ya Sera yetu ya Afya na kuna makundi ambayo tumeyaainisha katika sera ambapo watu wanapata matibabu bure.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili suala la walemavu kama nilivyojibu katika swali langu la msingi, si kila mlemavu hana uwezo wa kupata matibabu, nataka niweke msisitizo. Ndiyo maana nimesema katika Sera hii Mpya tutaweka utaratibu mzuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mazingira ya sasa kati ya asilimia 60 - 70 ya wagonjwa ambao wanafika katika vituo vyetu vya kutolea huduma za afya wanapata matibabu bure. Sasa hivi tunataka tuweke mfumo mzuri na kuhuisha na mifumo mingine kama ile ya TASAF kuhakikisha kwamba tunawatambua tu wale ambao kweli hawana uwezo na wanahitaji kupata matibabu. Tutakapokuja na huu utaratibu wa bima ya afya kwa wananchi wote tutakuwa na kundi dogo sana ambalo limebaki ambalo litakuwa linagharamiwa na Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili ameuliza kwa nini Serikali haipeleki ruzuku. Nimthibitishie Mheshimiwa
Mbunge na bahati nzuri naye ni Mjumbe wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii na analijua na hivi karibuni tumetoa taarifa ya utekelezaji ya nusu mwaka, Serikali inapelekea mishahara hatujashindwa kupeleka mishahara, dawa na hela ya uendeshaji. Hakuna hospitali ya rufaa ya mkoa ambayo haijapata huduma zote hizo ambazo nimezitaja.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo tuna vyanzo vingi vya mapato ndani ya hospitali. Pamoja na ruzuku ya Serikali tuna fedha za papo kwa papo, fedha za bima na nyingine zinapata basket fund. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Ninapozungumza watoto njiti nina maana wanazaliwa kabla ya miezi tisa haijatimia:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; dawa ya kusaidia mtoto ili aheme vizuri inayoitwa surfactant inauzwa shilingi laki sita kwa dozi moja na inategemea hali ya mtoto ambayo amezaliwanayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama una mtoto mmoja shilingi laki sita, kama umejifungua watoto wawili ni shilingi 1,200,000/=. Na watoto walio wengi wanatoka katika familia zenye hali duni na kipato cha hali ya chini, kama wanashindwa tu kwenda nao kliniki itakuwa na hii shilingi laki sita. Je, sasa Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba, dawa hizi zinatolewa bure, ili kunusuru maisha ya watoto hawa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Katika majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba, likizo ni siku 84 kwa mtoto mmoja na siku 100 kwa watoto mapacha, lakini hawa ni watoto njiti. Kama amejifungua kabla ya miezi tisa tusema miezi saba ina maana kuna miezi miwili ambayo iko kabla ya miezi ile tisa. Sasa je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba, wazazi wote wawili, baba na mama, wanapata likizo yenye malipo kwa miezi hiyo iliyopo kabla ili waweze kutunza hawa watoto njiti? Asante.
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Grace tendega kwa swali lake zuri. Na nianze kwa kutoa tafsiri ya mtoto njiti, watoto njiti wako katika makundi mawili; kuna wale ambao wamezaliwa kabla ya wiki 37 na kuna wale ambao wanazaliwa na uzito mdogo kuliko ule ambao tunatarajia, kwa maana ya kilo 2.5 kwa hiyo, wote hawa tunawaweka katika group hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, watoto ambao wanazaliwa njiti mara nyingi wanazaliwa na changamoto mbalimbali, hususan wale ambao wamezaliwa kabla ya umri wa wiki 37. Na moja ya changamoto ambayo wanayo ni matatizo ya kupumua, mapafu yanakuwa hayajakomaa na wanahitaji dawa ambayo ni surfactant kukomaza yale mapafu. Na nikiri kweli, gharama za surfactant ni kubwa na sisi kama Seriakali tumeliona hilo, tunajaribu kuliangalia utaratibu mzuri wa kuhakikisha kwamba, tunatoa afua kwa akinamama ambao wamezaa watoto njiti. Hatutaweza kuitoa bure, lakini tutaweka utaratibu ambao unaweza ukapunguza gharama katika utaratibu ambao tunao sasa hivi wa kuagiza dawa moja kwa moja kutoka viwandani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili linahusiana na kuongeza muda wa likizo ya uzazi kwa wazazi ambao wana watoto njiti:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, watoto njiti wanazaliwa wakiwa na changamoto nyingi pamoja na matatizo ya kupumua, wengine wanazaliwa na viungo bado havijakomaa, ikiwa ni pamoja na ubongo na wengine wanaweza wakapata matatizo mengine endapo hawatapata matunzo ya karibu. Lakini jiwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba, sasa hivi kwa mujibu wa teknolojia watoto ambao wanazaliwa hata akiwa na wiki 22 kwa maana ya miezi mitano, wana uwezo mzuri sana wa kuweza kukua na kuishi vizuri. Na mtoto ambaye ameweza kuzaliwa na…

MWENYEKITI: Muda, muda.

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninalotaka kulisema kwa kifupi tu kwamba, Serikali inaweza ikaliangalia suala hili kwa maana ya kuwa, pale kama mtoto ana matatizo mzazi anaweza akawa anapewa ruhusa kwa mujibu wa kanuni na taratibu ambazo tunazo.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona, barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda Wilaya ya Kilolo kilometa 133 ambayo kuna kipande cha Jimbo la Kalenga napo kuna changamoto ya barabara mvua zimenyesha barabara nyingi zinakuwa hazipitiki vizuri wananchi wanapata adha na mazao yao yanashindwa na ni ahadi ya Rais ambayo alitoa kwamba kufikia 2020 itakuwa imetengenezwa.

Ni lini sasa Serikali itahakikisha barabara hii inatengenezwa na wananchi wanapita bila matatizo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge watakubaliana na mimi kwamba kipindi hiki tumepata mvua myingi sana na uharibifu wa miundombinu umekuwa ni mkubwa sana, sisi
kama Seriikali tumejipanga kuhakikisha kwamba tunakwenda kufanya urejeshaji wa miundombinu hii. Niseme tu kilometa 4217 hadi Desemba zimekuwa na hali mbaya hizi ndiyo barabara katika nchi tunaendelea na uratibu nimuombe Mheshimiwa Mbunge avute subira tumeshatambua maeneo yote yenye shida na tunahitaji fedha za ziada kwenda kufanya marejesho ya miundombinu ya barabara.

Kwa hiyo, wananchi wavute subira sisi kama Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi kwa kushirikiana na wenzetu upande wa Serikali za Mitaa kwa maana TARURA tunafanya uratibu wa pamoja ili tuhakikishe kwamba tunaenda kufanya uridhishaji maeneo mbalimbali ya nchi maeneo ambayo yameharibiwa na mvua, ahsante sana. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona pamoja na ukosefu wa nyumba za walimu katika Jimbo la Kalenga ni mwaka wa nne sasa walimu hawa hawajapandishwa madaraja na wamekuwa wakipata adha kubwa sana katika masuala hayo ya nyumba.

Ni lini sasa Serikali itawapandisha madaraja walimu hawa ili waweze kuongeza morale katika utendaji kazi wao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tuna malalamiko mbalimbali mengi ya walimu katika maeneo mbalimbali ya nchi wakionesha kukerwa na kutopandishwa madaraja.

Niwaombe pia katika jambo hili pia kwa sababu ya mchakato wa kupandisha madaraja unaanzia kule ngazi ya halmashauri zetu ambako kila Mbunge pale yupo, mchakato unaanzia pale ngazi ile inaenda kwa Afisa Utumishi inakuja kwa Mkurugenzi mpaka maeneo mengine. Tupeane taarifa tumeshatoa maelekezo tumekutana walimu wote na mawakilishi wao kwa maana Maafisa Elimu wa Wilaya na Mikoa na Wakurugenzi na Makatibu Tawala, juzi walikuwa hapa Dodoma, tukaagiza kwamba tupate taarifa.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu unakuta, mwalimu yupo kwenye halmashauri yako Mheshimiwa Mbunge, lakini mwenzake yeye kapanda mara ya kwanza, mara ya mwisho 2013 mpaka leo hajapanda, lakini kuna wengine wamekuwa wakipandishwa. Kwa hiyo, tukipata taarifa mahusui katika maeneo haya tutazifanyiakazi haraka sana. Walimu wanalalamika na wanakwazwa, tungependa tuwaondolee adha, yale mambo ambayo yapo ndani ya uwezo tuyaondoe ili tuondoe kero kwa walimu wetu waendelee kufundisha kwa moyo. Ahsante sana.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, nasikitika sana swali langu halijajibiwa kama nilivyokuwa nimeuliza. Katika majibu ya Naibu Waziri anasema kwamba wao wametenga zaidi ya ekari 217 ambazo ziko katika mikoa mbalimbali lakini hajaainisha ni mikoa ipi na wilaya zipi makambi hayo yapo ili tuweze kujua kwa sababu sisi ndiyo wawakilishi wa hao vijana na tunawaona jinsi ambavyo wanapata adha huko tuliko. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wamesema kwamba kuna programu mbalimbali na mazingira ambayo wamewawezesha, ni program zipi na mazingira yepi ambayo wameyaweka ili hawa vijana tukawaona wanafanya kazi. Amekiri kabisa hakuna hata sensa waliokwisha kuifanya ya kufahamu ni vijana wangapi ambao wanafanya kazi hizo mchana na usiku kwa maana ya kwamba hakuna wanachokijua kuhusu vijana wetu na tunawaona wakiwa wako na hali ngumu na hawana ajira na ajira hazijapatikana. Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Victor Tendega (Viti Maalum), kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika eneo lake la kwanza amehoji kwa nini hatujaainisha maeneo yote ya ekari 217,882 ambayo yametengwa. Katika utaratibu wa uwasilishaji wa majibu nimetoa majibu ya jumla kuonyesha ekeri zilizotengwa lakini bado hii haizuii Mheshimiwa Mbunge kupata taarifa ya maeneo ambayo yametengwa. Kupitia TAMISEMI tutawasilisha orodha ya maeneo yote haya ambayo yametengwa ili Waheshimiwa Wabunge pia wafahamu ardhi ambayo imetengwa kwa ajili ya shughuli za vijana kwa ajili ya kilimo, viwanda na ufugaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili anahoji kuhusu program ambazo tunaziendesha. Ofisi ya Waziri Mkuu kwa 2016/2021 tunaendesha Programu Maalum ya Ukuzaji Ujuzi Vijana yenye lengo la kuwafikia vijana milioni 4.4 kwa mwaka 2021 ili vijana hawa wapate ujuzi waweze kujiajiri na kuajiri vijana wengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu ameomba azisikie program, kwa ruhusa yako naomba nimtajie chache tu ili ibaki kwenye kumbukumbu sahihi za Bunge hili. Program ya kwanza ambayo tunaifanya inaitwa RPL (Recognition of Prior Learning), ni mfumo wa Urasimishaji wa Ujuzi kwa vijana wenye ujuzi ambao hawajapitia mfumo rasmi wa mafunzo ya ufundi. Ukienda leo mtaani kuna vijana wanajua kupaka rangi au kutengeneza magari lakini hawajawahi kusoma VETA wala Don Bosco. Serikali inachokifanya inarasimisha ujuzi wao na kuwapatia vyeti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna Program ya Greenhouse ambapo kila wilaya tunawafikia vijana 100 katika awamu ya kwanza. Mpaka sasa nchi nzima tumeshafikia vijana 18,800. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna Program ya Mafunzo ya Ufundi kupitia vyuo vya Don Bosco na vyuo shirikishi. Takribani vijana 8,800 katika awamu ya kwanza wamenufaika na tunaendelea na awamu ya pili. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna program ambayo inaendeshwa DIT Mwanza ya Viatu na Bidhaa za Ngozi ambako vijana wanapata mafunzo na kuweza kunufaika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, program ziko nyingi sana kwa sababu ya muda, naomba niishie hapa lakini Mheshimiwa Mbunge atapata taarifa zaidi.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, nampongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri tena ya kina kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kuongeza jambo dogo tu, Mheshimiwa Tendega amelalamika hapa kwamba hakuna chochote kinachofanyika na haelewi chochote. Ili kumsaidia zaidi Mheshimiwa Mbunge akumbuke kwamba kila tunapopitisha bajeti za Serikali kila Wizara inaeleza program zote zitakazofanyiwa kazi kwenye bajeti ya Serikali.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuliweka suala hili, vizuri namwomba Mheshimiwa Tendega arejee kwenye bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, hizo program zote, utekelezaji wake kwenye ripoti ya Kamati upo na mambo yote yaliyofanyika yako wazi na yanaeleweka. Kwa hiyo, hatujaficha na siyo kwamba hakuna kinachojulikana. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda Ruaha National Park Iringa ni ahadi ambayo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Nne na Awamu ya Tano na mpaka sasa ni upembuzi yakinifu tu unaendelea kwa miaka yote hiyo kumi na tano. Ni lini sasa barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami ili kusaidia wale watalii wanaokwenda kule waweze kwenda kwa ufasaha? (Makofi)
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara anayoizungumza inaitwa jina Iringa - Msembe (km 104). Barabara hiyo ilikuwa imewekwa kwenye mafungu mawili; moja ni la ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Nduli ambao tumeshatangaza tenda na mkandarasi amepatikana wakati wowote tutasaini mkataba. Hizi km 104 tayari tumeshamaliza mpaka usanifu wa kina na tumeomba fedha kutoka Benki ya Dunia. Kwa hiyo, wananchi wa Iringa, tena ndiyo nimeoa kule, shemeji zangu wale, wala asiwe na wasiwasi barabara ile inajengwa.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Barabara ya kutoka Iringa Mjini kuelekea Ruaha National Park ambayo ni Jimbo la Kalenga imekuwa ni changamoto na ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne na Rais wa Awamu ya Tano. Ni lini sasa barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami?
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ile itajengwa pamoja na Uwanja wa Ndege wa Nduli na itajengwa kupitia fedha za Benki ya Dunia, taratibu za kupata hizo fedha zinaendelea itakapokamilika mradi utaanza.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, timu hii ya Twiga Stars ni timu ambayo imeweza kushinda michezo mingi nje ya nchi na ni timu ambayo kwa kweli ina makombe mengi kushinda hata makombe mengine ambayo yapo ya timu zingine za wanaume zilizopo hapa Tanzania. Sasa Serikali haioni haja sasa ya kuwatambua, kuwathamini na kuwekeza katika timu hii ya wanawake ili hawa wanawake waweze kupata ajira ndani na nje ya nchi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, michezo ni ajira na soka hili la wanawake limekuwa ni ajira sasa hivi. Tunaona watoto wengi wa kike wamependa michezo. Kule Kalenga sasa hivi nikienda badala ya watoto wa kiume kuomba mipira ni wasichana wanaomba mipira kwa ajili ya kucheza soka la wanawake na tunaona nchi za Ujerumani, Japan na West Africa nchi zao zimewekeza na timu za wanawake zimeweza kushinda katika soka kombe la dunia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa je, Serikali ina mkakati gani wa muda mrefu wa kujenga academy za soka la wanawake hata kwa kila kanda ili kuwawezesha hawa wanawake wakajengewa vipaji na kwa sababu michezo ni ajira. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa maswali mazuri lakini nikianza na swali lake la kwanza ambalo ametaka kujua kwamba mpango wa Serikali ni nini katika kuwekeza kwenye Timu ya Twiga Stars?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri kwamba ni kweli Timu ya Twiga Stars imekuwa ikifanya vizuri sana kwa miaka mingi na kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge umesema, kufanya vizuri kwa Timu ya Twiga Stars maana yake Serikali imefanya uwekezaji mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi nikuhakikishie kwamba kama ambavyo tumekuwa tukifanya uwekezaji katika Timu ya Twiga Stars, tunaahidi kwamba tutaendelea kufanya uwekezaji zaidi ili timu hii ifanye vizuri lakini si Timu ya Twiga Stars peke yake ni pamoja na timu nyingine kwa sababu tunazo timu nyingi sana ambazo zinafanya vizuri na ni timu za wanawake ikiwemo timu ya Kilimanjaro Queens inafanya vizuri lakini pia tunayo timu nyingine ya Mlandizi Queens pamoja na timu zingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, uwekezaji ni mpango ambao kama Serikali tunao na tunaendelea kuufanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lako la pili ambalo umetaka kujua kwamba Serikali tuna mpango gani katika kujenga academy. Nikuhakikishie kwamba sisi kama Serikali tumekuwa tukihamasisha sana kwa sababu tunatambua kwamba hatuwezi kuwa na timu kubwa za kitaifa kama hatujawekeza kwenye kujenga academy ambazo zitalea vijana. Kwa hiyo, sisi kama Serikali tumekuwa tukitoa hamasa kwanza kwa wadau kwa mashirikisho lakini vilevile hata kwa Waheshimiwa Wabunge tuweze kushirikiana katika kuhakikisha kwamba tunajenga academy.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nitumie fursa hii kuwapongeza wadau wote ambao wameshirikiana na Serikali lakini wameunga mkono jitihada za Serikali katika kujenga academy ikiwepo academy ya kule Kaitaba lakini tunayo academy ya pale Filbert Bayi pamoja na wadau wengine ambao wanafanya kazi vizuri katika kuhakikisha kwamba tunawekeza katika kuwakuza vijana wetu ili siku moja tuweze kuja kuwa na timu ambazo ni bora zaidi. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, majibu ya Waziri yameonesha kweli Kiswahili kimekua, lakini nchi ya Afrika Kusini wanafundisha Kiswahili na walitupa tender kama Tanzania ili tuweze kuwaandaa walimu wa kuwapeleka katika nchi ile. Lakini mpaka sasa hakuna jambo hilo limetekelezeka na hata nchi ya Kenya sasa wametupiku wamepeleka kule.

Je, Tanzania ina mkakati gani sasa wa kuhakikisha kwamba wana walimu wa kutosha wa kuwapeleka nchi hizo? (Makofi)
WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimhakikishie kwamba Serikali au nchi yetu ya Tanzania inao walimu wa kutosha wa Kiswahili ambao ni wabobezi, kwa hiyo suala la upungufu wa walimu wa kutosha ambao wanaweza kwenda kufanya kazi katika nchi za nje hamna tatizo lolote.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala la nchi kuamua kwamba inafanya kazi na nani hilo ni suala la hiyari ya nchi yenyewe, lakini kama Tanzania tuko tayari kupeleka walimu wetu wa Kiswahili mahali popote katika dunia hii kwa sababu tunao walimu wa kutosha mahiri na Serikali inaendelea kuimarisha ufundishaji wa somo la Kiswahili kwa sababu kama ambavyo tumeona lugha ya Kiswahili imeendelea kuheshimika na imeendelea kutumika sehemu mbalimbali katika Afrika na hata nje ya Bara la Afrika. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante pamoja na majibu ya Waziri naomba kuuliza maswali ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, afya ni jambo la msingi sana, Serikali ilikuwa imeshauri kwamba kila halmashauri iweze kutenga asilimia nne, wanawake; nne, vijana; na asilimia mbili kwa watu wenye ulemavu ili waweze angalau kujimudu kiuchumi, lakini halmashauri nyingi zimeshindwa kutenga fedha hizo kwa sababu vyanzo vingi vya mapato vimekwenda Serikali Kuu ikiwemo halmashauri yangu ninayotoka mimi ya Iringa DC. Swali la kwanza, je, Serikali sasa ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba hawa watu wenye ulemavu wanapata matibabu bila vikwazo ikiwemo wale wenye bima unakuta hata wakiwa katika bima vifaa tiba kama sun screen lotion inakuwa ni shida, haipatikani?

Mheshimiwa Spika, swali la pili ni lini sasa Serikali italeta huo Muswada wa Bima ya Afya kwa Watu Wote (Universal Health Coverage) ili tuupitishe na watu hawa wenye ulemavu waweze kupata huduma hii ya afya bila matatizo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali tuliweka utaratibu wa kuhakikisha kwamba tunatenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya vijana, wanawake na asilimia mbili kwa ajili ya walemavu na hili ni takwa kwa kila halmashauri ambalo wanapaswa wazingatie na kuhakikisha kwamba hii mikopo inafika na inapatikana pasipo kuwa na riba.

Mheshimiwa Spika, nikiongelea suala la matibabu, hakuna mwananchi ambaye anahitaji matibabu atayakosa kwa sababu ya hali yake ya maumbile. Kwa hiyo hilo nataka niliweke wazi na sisi kama Serikali tutaendelea kutoa matibabu kwa walemavu ambao wanastahili kwa mujibu wa taratibu ambazo tunazo.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ameongelea ni lini Serikali italeta Muswada wa mabadiliko ya sheria ama sheria inayohusiana na bima ya afya kwa wananchi wote, nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge mpango wetu sisi Serikali ni kuleta katika Bunge la Septemba.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Tatizo lililopo katika Jimbo la Mbulu Vijijini ni sawa kabisa na changamoto iliyoko katika Jimbo la Kalenga. Kata ya Kihanga, Ulanga, Ifunda katika Vijiji vya Mibikimitali na Kata ya Mgama iliyoko katika Vijiji vya Lupembewasenga, kuna changamoto ya mawasiliano.

Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha wananchi hao wanapata huduma hiyo ya mawasiliano ili waweze kufanya shughuli zao za kawaida?
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto tuliyonayo kwa sasa, labda nitoe maelezo kidogo. Ni kwamba kuna baadhi ya sehemu ambazo mawasiliano au minara ilipelekwa ambapo uhitaji wake inawezekana walikuwa watu 5,000 ambao walikuwa wanaweza kutumia huduma hiyo. Kwa sababu ya ongezeko la watu katika eneo husika, kwa hiyo, ile minara yetu inashindwa kuwa na uwezo wa kuhudumia watu wengi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi, kwa kugundua hilo, tumeagiza mobile operator wote wafanye tathmini, wafanye research za kutosha ili waongeze uwekezaji katika maeneo hayo, aidha kwa kuongeza minara au kwa kuongeza capacity katika minara ambayo tayari ipo katika maeneo husika ili kuhakikisha kwamba wananchi wote wanafikiwa na mawasiliano hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, imekuwa ni ahadi ya muda mrefu ya ujenzi wa sehemu za kujisubiria akina mama hasa wajawazito. Tumesema katika sera kwamba tutakuwa na Vituo vya Afya katika kila Kata na Zahanati katika kila kijiji; lakini katika Jimbo la Kalenga hii imekuwa ni changamoto kubwa sana. Akina mama wakijifungulia njiani wanatozwa Sh.50,000/= mpaka Sh.70,000/=. Ni lini Serikali itajenga majengo ya kujisubiria katika Jimbo hili la Kalenga? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, nini kauli ya Serikali kuhusu hizo tozo ambazo zinatozwa kwa akina mama ambao pia ni walipa kodi katika nchi hii na Serikali ndiyo yenye changamoto ya kutojenga hivyo Vituo vya Afya? (Maikofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Tendega, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tunahitaji kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto wachanga kwa kuboresha miundombinu ya huduma za afya. Ni kweli kwamba miradi ya ujenzi wa majengo ya kujisubiria kwa maana ya maternity waiting homes, imekuwa ni kipaumbele cha Serikali. Hata hivyo, majengo hayo yanajengwa ili kupunguza umbali wa wajawazito kufika kwenye Vituo vya Huduma za Afya. Kwa hiyo, ili ujenge majengo haya ni lazima uwe na Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Spika, sasa kupanga ni kuchagua. Ndiyo maana Serikali imepanga kwanza kujenga kwa wingi Vituo vya Afya ili viwe karibu zaidi na makazi ya wananchi na tuweze sasa, yale maeneo ambayo yana umbali mkubwa, kuweka mpango wa pili wa kuanza kujenga majengo ya kujisubiria wajawazito. Haitakuwa na tija sana ukiwekeza kujenga majengo ya kujisubiria wananchi sehemu ambayo ina umbali mkubwa sana kutoka kwenye vituo vya huduma za afya.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kipaumbele namba moja ni lazima uwe na kituo, ndiyo maana yale majengo yanajengwa karibu na kituo. Ndiyo maana katika miaka hii mitano tumejenga vituo vingi na tunaendelea na ujenzi wa vituo hivyo ili kusogeza huduma kwa wananchi, hatimaye tutakuja kujenga sasa majengo ya kusubiria wajawazito. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kipaumbele hicho bado kipo, lakini tunaboresha kwanza vituo na baadaye tutakenda kwenye awamu wa ujenzi wa majengo ya kujisubiria.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kauli ya Serikali kuhusu tozo, Serikali haijatoa maelekezo yoyote kwa watendaji na watoa huduma kutoza faini kwa wajawazito wanaojifungulia majumbani.

Mheshimiwa Spika, ni wajibu wa watendaji katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, ni wajibu wa watumishi katika vituo vya huduma kutoa elimu na kuhamasisha wajawazito kuona umuhimu wa kujifungulia katika vituo vya huduma badala ya kuwalipisha faini wakijifungulia nje ya vituo vya huduma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Serikali itaendelea kusimamia jambo hilo. Naomba nitoe wito kwa watendaji wote kuzingatia jukumu lao la kutoa elimu na kuhamasisha wananchi kujifungua katika vituo vya huduma.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Iringa Mjini kupitia Jimbo la Kalenga kwenda Kilolo kilometa 133 ambayo ina madaraja ni barabara ambayo ilikuwa ni ahadi ya hayati Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano, alipofika pale akatoa ahadi hiyo, ni miaka mitano sasa imepita haijafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni lini Serikali itaijenga barabara hii ili angalau kumuenzi hayati kwasababu alienda akaona wananchi wa kule wanavyohangaika katika kuuza mazao yao kwenda katika sehemu mbalimbali?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii yenye urefu wa km. 133 iliyoko Mkoani Iringa na ambayo ni ahadi ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Mheshimiwa Hayati, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli naomba nimhakikishie kwamba Serikali haitaacha ahadi zote ambazo zimeahidiwa na Mheshimiwa Rais. Nataka nimhakikishie kwamba barabara zote ambazo zimeahidiwa na Mheshimiwa Rais ikiwa ni pamoja na hiyo zitajengwa kwa kiwango cha lami awamu kwa awamu. Ahsante.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Kata hizo ambazo nimezitaja Kata ya Maboga, Kata ya Kalenga, Kata ya Ulanda, Kata ya Wasa wananchi ni wakulima ambao wanalima mali mbichi nyingi sana; viazi, njengere, maharage na mengine mengi na barabara imekuwa ni kikwazo katika kusafirisha hizo mali zao, na wamekuwa wakipata tabu mali zinaharibikia njiani. Mwaka 2020 pesa alizosema zimetolewa walikwangua sababu ilikuwa ni wakati wa uchaguzi, na sasa hivi baraba hazipitiki.

Je? Kwa nini Serikali haioni kwamba hii barabara sasa imekuwa ni kubwa na inahudumia watu wengi ambayo inaweza ikaenda mpaka ikatokea Madibila Mbeya ili iingie katika mpango wa TANROADS na itoke TARURA? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kuna barabara ambayo wananchi wametumia nguvu zao ambayo imetobelewa kutoka katika Kata ya Kihanga ikaja katika Kata ya Maboga ambako kuna Zahanati na kuna Hospitali ya Wilaya iliyoko Tosamaganga, wananchi wanashindwa kufika kupata hudama hizo.

Je, ni lini sasa Serikali itaifanyia kazi barabara hii ili wananchi hawa waweze kupata huduma hizo za afya na kuweza kufika katika maeneo hayo kwa urahisi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Victor Tendega Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza ameuliza kwamba kwa nini Serikali sasa isione umuhimu wa kuihamisha barabara ambayo inapita Maboga, Kalenga, Wasa, Kihanga mpaka kutokea Madibila kutoka TARURA kwenda TANROADS.

Mheshimiwa Spika, nimuhakikishie kabisa kwamba si barabara zote zinahitaji kupandishwa kwenda na kuhudumiwa na TANROAD, lakini jambo kubwa ambalo naweza nikamuhakikishia ni kwamba kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, Serikali itaendelea kuzitengea fedha barabara zote za muhimu.

Mheshimiwa Spika, na kikubwa ambacho alikuwa amekisema Serikali haifanyi kazi wakati wa uchaguzi peke yake, Serikali inafanya kazi muda wote, na katika bajeti hizi tumetenga fedha kwa ajili ya kazi hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo la pili ameuliza vilevile barabara ya kutoka Kihanga kwenda Maboga ambako amesema kuna kituo cha afya ni lini Serikali itahakikisha kwamba barabara hiyo inajengwa, nimeeleza hapa kwa kadri ya upatikanaji wa fedha na kwa sababu fedha tumetenga katika bajeti na kwa sababu bajeti tunakwenda kupitisha sisi sote hapa nikuombe Mheshimiwa Mbunge tupitishe hiyo bajeti ili barabara zetu zitengenezwe, ahsante.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika Ahsante sana kwa kuniona changamoto ya barabara katika Jimbo la Mwibara ni sawasawa kabisa na changamoto za barabara katika Jimbo la Kalenga Mkoani Iringa. Kumekuwa na changamoto kubwa sana na barabara ya kutoka Iringa Mjini kuelekea Kata za Muhota na Magulilwa kutoka Kijiji cha Kitayawa kwenda Nyabula ambako kuna Hospitali ya Misheni ambako wananchi wanatibiwa barabara imekatika kabisa haipitiki imekatika daraja limekatika.

Je! Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wananchi wa jimbo hili la Kalenga hususani wale wale wa…

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, taarifa kidogo.

MHE. GRACE V. TENDEGA: …Kata ya Mpota wanaweza wakapata mahitaji ya barabara.

SPIKA: Taarifa ya nini yuko wapi anayesema taarifa?

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Samahani unjuka ndio unaotusumbua Kiswaga hapa. (Kicheko/Makofi)

SPIKA: Ndio Mheshimiwa Kiswaga!

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Ni unjuka tu unatusumbua lakini kama unaniruhusu nitasema neno moja.
(Kicheko)

SPIKA: Karibu nakuruhusu.

T A A R I F A

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA, Mheshimiwa Spika, ahsante sana hiyo barabara ya kutoka Kitayao kwenda Nyabula tayari nimeshafanya mpango nimeongea na TARURA na sasa tumeshaweka mabomba hilo daraja linaanza kujengwa hivi karibuni ahsante sana tulipata fedha ya dharula nakushukuru. (Makofi/Kicheko)

SPIKA: Mheshimiwa Grace Victor Tendega unapokea hiyo taarifa? Halafu tuendelee na swali lako lipi sasa baada ya taarifa hiyo.

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, kwa uchungu kabisa ninazungumza hapa sipokei taarifa hiyo wananchi wale wanapata shida sana hakuna chochote anachokisema kimefanyika pale barabara imekatika na wananchi awapati huduma kwa hiyo naomba swali langu lijibiwe. (Makofi)

Ni lini Serikali itahakikisha wananchi hawa wanapata huduma ya barabara waweze kupata huduma zingine na matibabu na kiuchumi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumshukuru Mheshimiwa Kiswaga Mbunge wa Jimbo la Kalenga kwa juhudi kubwa sana anazozifanya kuhakikisha wananchi wa Jimbo la Kalenga wanapata barabara bora na hivyo wanaendelea na shughuli za kiuchumi na kijaamii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini nisema barabara hii ya kutoka Iringa Mjini kwenda Kata ya Maguliwa na maeneo haya kuna hospitali Serikali imeendelea kuhakikisha inatoa kipaumbele kwenye barabara ambazo zinapeleka huduma za jamii kwa wananchi, zikiwemo hospitali, shule na maeneo mengine yenye huduma za kijamii.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyotanguliwa kusema tumepata baraka ya mvua mwaka huu, lakini tunafahamu baraka hiyo imeambatana na uharibifu wa baadhi ya madaraja, ma-calvati na barabara zetu. Naomba nimuhakikishie kwamba Serikali inaendelea kuweka mipango ya haraka ikwezekanavyo kuhakikisha barabara ile aliyoisema inakwenda kutengenezwa na hilo daraja lifanyiwa matengenezo ili wananchi waweze kupita na kupata huduma hizo za afya na huduma nyingine. Kwa hiyo, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge jambo hilo linafanyiwa kazi na Serikali.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Changamoto za maji zilizopo katika Jimbo la Kalenga kwa Kata za Lumuli, Masaka, Kiwele, Luhota, Kalenga yenyewe na Magulilwa zimekuwa ni kubwa sana:-

Je, Serikali mna mkakati gani sasa wa kuhakikisha wananchi hawa wanapata huduma za maji safi na salama? (Makofi)
WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kilio hiki cha wananchi wake, lakini kubwa sisi kama Wizara ya maji, tumepewa maelekezo mahususi kabisa na Mheshimiwa Rais wetu kipenzi Mama Samia Suluhu Hassan; na akaenda mbali kabisa, kwamba tukizingua atatuzingua. Sisi hatupo tayari kuzinguliwa, tutakwenda kuhakikisha kwamba wananchi wako wanapata huduma ya maji. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda Pawaga kilomita 76 ambazo zilikuwa ni ahadi ya hayati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mbaya mno na wakulima wa pale wanalima mpunga lakini wanashindwa kusafirisha. Je, ni lini Serikali itakwenda kujenga barabara hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Iringa Pawaga ni kama barabara zingine ambazo zimepata changamoto kubwa katika kipindi hiki cha mvua. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hizi zipo kwenye ahadi na zitategemea na upatikanaji wa fedha. Pale ambapo fedha zitapatikana barabara hizo zitajengwa na ndioyo azma ya Serikali lakini kinachotukwamisha ni uwezo wa bajeti yetu. Kwa hiyo nimhakikishie fedha zikipatikana barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kila mwaka tumekuwa tunaongeza bajeti ya dawa katika Serikali yetu na tumekuwa tukiona bado zahanati na vituo vya afya havipati dawa. Swali langu: Je, mmefanya utafiti gani wa kuhakikisha kwamba hizo fedha, shilingi bilioni 270 na hiyo shilingi bilioni 140 ndizo zitakwenda kutatua changamoto ya dawa katika zahanati zetu na vituo vya afya?

Swali langu la pili; hivi tunavyozungumza wananchi wenye changamoto hizi wa kutoka Jimbo la Kalenga na wengine wengi wanaangalia; je, wananchi wategemee nini kuwa hizi dawa katika zahanati na vituo vya afya itakuwa ni historia?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama ambavyo Mheshimiwa Grace Victor Tendega ametangulia kusema, Serikali imeendelea kuongeza bajeti ya fedha kwa ajili ya ununuzi wa dawa, vitendanishi na vifaa tiba kwa takriban mara tisa ndani ya miaka mitano na hii ni kwa sababu Serikali inajali sana wananchi na inahitaji kuona wananchi wanapata dawa za kutosha ili kuhakikisha kwamba huduma za afya ni bora zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo ni kweli kwamba bado tuna changamoto ya uhitaji wa dawa na Serikali inatambua kwamba bado tuna kazi ya kufanya kuhakikisha tunaendelea kupunguza sana upungufu wa baadhi ya dawa katika vituo vyetu vya huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana katika jibu langu la msingi nimeeleza namna ambavyo Serikali imepeleka fedha mpaka sasa, zaidi ya shilingi bilioni 140 zimepelekwa katika vituo vyetu na mpaka mwisho wa mwaka huu wa fedha, ifikapo Juni, tutakuwa tumepeleka fedha zaidi kuhakikisha tunaendelea kuboresha upatikanaji wa dawa katika vituo hivyo na kwa makundi maalum na wananchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nimhakikishie kwamba Serikali imefanya tathmini kwamba kadri inavyoongeza fedha ndivyo upungufu wa dawa unavyopungua na ndiyo maana lengo la Serikali ni kuendelea kuongeza fedha. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutaendelea kuhakikisha tunatenga fedha kwa ajili ya kuboresha upatikanaji wa dawa na kuondoa kabisa upungufu wa dawa katika vituo vyetu.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini ukiangalia majibu yake yanasema kwamba bado wanafanya tathmini ina maana hawajaanza na robo tayari ya mwaka tumeshapita.

Sasa swali langu ni lini watakwenda kujenga shule hizo ili watoto wa kike wasiweze kupata adha hizo kwa sababu tumeona adha wanazozipata watoto wa kike hasa Mkoa wa Iringa wanapata changamotoo kubwa sana. Kwa hiyo, tunaomba majibu ni lini wanaanza, tumeshapitisha robo sasa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anasema kwamba robo ya kwanza ya mwaka imepita na bado inaonesha kama hatujafanya tathmini, kwa hiyo anachotaka kujua exactly ni lini? Ni kwamba Serikali ina mipango na mikakati yake na mimi nimwambie tu kwamba kabisa Serikali ya Awamu ya Sita hatutashindwa kukamilisha haya majengo kwa wakati. Moja ambacho hafahamu tunapojenga kwa mfano darasa ni muda wa miezi mitatu darasa linakuwa limekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunachokisubiri sasa hivi tu baada ya robo ya kwanza na mifumo ya fedha kufunguka kinachofuatia baada ya hapo ni fedha kuanza kuzitenga na kuzipeleka katika maeneo husika yaliyopangwa katika bajeti. Kwa hiyo, ninyi ondoeni wasiwasi Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan hii kazi tunaiweza na tutaimaliza kwa wakati. Ahsante. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, changamoto ya ajira kwa wahitimu wa Vyuo Vikuu wa sekta ya kilimo, zipo pia changamoto zingine kwa sekta mbalimbali. Tumeona kuna changamoto ya wahitimu wa Vyuo Vikuu kwa ajira za Ualimu;

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba hawa Wahitimu wa Vyuo Vikuu wa sekta ya elimu wanapata nafasi za kuajiriwa kwa sababu tumeona wananchi wanachangishwa kwa ajili ya kuweka Walimu katika sehemu mbalimbali, Walimu wa kati wapo wahitimu wengi wamekaa idle? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri ya awali.

Mheshimiwa Spika, maelezo yanayotoka katika Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Serikali inatambua mahitaji ya Watumishi katika sekta mbalimbali nchini. Naomba niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba Mheshimiwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita toka alipoingia madarakani aligundua mahitaji ya ajira mpya kwa ajili ya sekta mbalimbali na hivyo mara moja alifanya maamuzi ya kuanza kutoa ajira mpya na mpaka sasa kwa takwimu za mpaka mwezi Januari mwaka 2022 tayari tumekwishaajiri watumishi wapya 11,901 ambao wameshaingia katika sekta mbalimbali mtambuka.

Mheshimiwa Spika, tunajua kwamba ajira hizo 11,901 ni kati ya ajira 40,000 ambazo zilikuwa zimeahidiwa na Mheshimiwa Rais. Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge tunaendelea kufanya mazungumzo kuangalia Ikama, kuangalia jinsi fedha za ajira ambazo zimeweza kutengwa kwenye Wizara ya Fedha na kama tutakuwa kwenye position nzuri kabla ya kumaliza mwaka huu wa fedha tunataka kuhakikisha kwamba tunaongeza ajira nyingine mpya ili kukidhi mahitaji ya Watumishi katika sekta mbalimbali nchini. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Kasi ya kusambaza umeme kuwafikia wananchi imekuwa ikisuasua kinyume na ahadi tuliyokuwa tukiambiwa kwamba tutawafikia wananchi wote kwa wakati mmoja; na yote hii inasemekana ni ukosefu wa fedha: Je, ni lini Serikali itawapelekea umeme wananchi wa Jimbo la Kalenga Mkoani Iringa hasa vitongoji vya Irangi, Unyangwila, Wambi, Ilongimembe na Igawa pamoja na Kata za Magulirwa na Kihanga? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba wakazi wote wanapata umeme? Tumeona kwamba wakileta umeme katika Kijiji wanatoa kwa nyumba tatu au nne halafu wanaruka, wanakwenda sehemu nyingine, wanaruka. Sasa ni mkakati upi wa Serikali wa kuhakikisha kwamba nyumba zote ambazo zinahitaji umeme zinapata? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tendega kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kusema kwa niaba ya Serikali kwamba miradi yetu ya REA na upelekaji wa umeme vijijini haisuisui; na hizo rumors kwamba hakuna fedha, siyo za kweli. Katika awamu ya tatu mzunguko wa kwanza, miradi 28; jumla ya Lot 28 zilitekelezwa na asilimia kubwa zimekamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi hiki ambacho tupo, jumla ya Lot 39 tayari mikataba yake imesainiwa na takribani shilingi trilioni 1,250 zipo tayari kwenye mikataba na Wakandarasi wanaendelea na kazi katika maeneo mbalimbali. Kwa hiyo, suala la uhaba wa fedha halipo. Fedha ipo na umeme utafikishwa katika maeneo yote kwa kadri ya muda ulivyopangwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo la pili, ni kweli kwamba siyo kila anayehitaji umeme ameupata kwa sasa, lakini kama ambavyo tumekuwa tukisema hapa, Serikali ya Awamu ya Sita itajitahidi sana kuhakikisha kwamba fedha inapatikana; na mbinu nyingine za ubunifu zimekuwa zikitumika kuishauri Serikali. Tulisema juzi kwamba tunatarajia kufika 2025 kwa kadri tulivyojipanga, Serikali itakuwa imefikisha umeme katika vitongoji vyote kwa kutumia takriba shilingi trilioni 7,500 kama tulivyosema kwamba tutakwenda kutafuta sehemu ya kupata hizo fedha kwa ajili ya kupeleka umeme huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nimalizie kwa kumshukuru Mheshimiwa Kiswaga kwa sababu maeneo yote ambayo yamesemwa amekuwa akiyafuatilia pamoja na Mheshimiwa Mbunge aliyeuliza swali hilo kwa niaba ya wananchi wa Kalenga. Nashukuru. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vitongoji 42 vilivyobakia katika Jimbo la Kalenga, Mkoani Iringa?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, Iringa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kupeleka umeme katika vitongoji vyote nchini kwa jinsi upatikanaji wa fedha unavyoendelea. Hatua ambayo tunaendelea nayo sasa ambayo inatakiwa kukamilika ni hatua ya vijiji ambayo itakamilika Desemba mwaka huu na fedha zinavyozidi kupatikana, vitongoji vinapelekewa pia umeme.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuweza kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Wilaya ya Mkalama ina gari mmoja ambalo pia ni bovu.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba, wanapomaliza ujenzi wa kituo hicho wanawapa na nyenzo kama magari na pikipiki maalum?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika Jimbo la Kalenga pia kuna kituo cha Polisi cha Kata ya Ifunda lakini hawana nyumba Askari hao na pia hawana magari, je, ni mkakati gani wa Serikali unao ili kuhakikisha kwamba kituo hiko kinapata nyumba za watumishi pamoja na magari? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Tendega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja, kuhusu Kituo cha Mkalama baada ya kukamilika kupewa nyenzo za kutendea kazi ikiwemo magari, hilo ni wazi, gari lililopo kama ni bovu, kituo kitakapokamilika tutawapa gari ili waweze kutimiza majukumu yao vizuri. Kwa bahati nzuri tumeanza kupokea magari hayo na yameanza kugawiwa kule ambako kuna mahitaji makubwa sana.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Kalenga, hii Kata ya Ifunda, kuwa na kituo ambacho hakina nyumba wala magari; tutawasiliana na uongozi wa Polisi wa Mkoa, nadhani ni Iringa hii, ili kuona kama wanalo eneo la kutosha basi waingize kwenye mpango wa ujenzi waweze kufikiriwa kujengewa. Nashukuru. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda Kilolo ambayo ilikuwa ni kilometa 33, lakini inapita Jimbo la Kalenga kutoka Ipogolo kwenda Kilolo, lini itajengwa kwa sababu imekuwa ni muda mrefu haijajengwa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika,
ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge anahitaji tu commitment ya Serikali ya ujenzi wa barabara kilometa 33 kutokea Iringa kwenda Kilolo ambayo inapitia Kalenga ambayo muda mrefu haijajengewa. Ni kwamba barabara hii tumekuwa tukiitengea fedha za matengenezo; na kwa sababu, Serikali inazingatia umuhimu wa hayo maeneo, na ninafahamu katika mwaka unaokuja kuna fedha imetengwa kwa ajili ya kuhakikisha yale maeneo korofi yote yanatengenezwa. Ahsante sana.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Ilula, Mlafu, kuelekea Kilolo ni barabara ambayo ni mbaya sana. Ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami kwa sababu wakulima wa kutoka Kilolo wanatataka kusafirisha mazao yao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tendega Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara aliyoitaja iko katika hali mbaya lakini ni azma ya Serikali kwamba kabla ya kuanza kuijenga itaikarabati kwanza ili iweze kupitika wakati Serikali ikitafuta fedha kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza swali langu halijajibiwa. Naomba niulize maswali maeili kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama kuna mikataba mbalimbali ambayo tunaridhia katika nchi yetu, nini kilitokea mpaka tukajitoa katika OGP?

Mheshimiwa Naiibu Spika, swali langu la pili, kama alivyosema kwamba kuna vyombo mbalimbali ambavyo tunavitumia kama alivyoainisha. Sasa ni nini kinatufanya tusiridhie katika mikataba hiyo wakati sisi nchi yetu si kisiwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Tendega kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza, kwamba kwanini tulijitoa; tulikuwa tayari tupo na Mkataba wa Umoja wa Mataifa yaani UPRM, (Universal Periodical Review Mechanism) ambayo inafanyiwa review kila baada ya miaka minne, ambayo ni ya umoja wa mataifa. Wakati huo huo tulikuwa kwenye OGP ambayo ni CSO private sector.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu tayari nchi yetu ipo katika mikataba ya Umoja wa Mataifa kama vile UPRM. Nikienda kwenye swali lake la pili, why tusiridhie. Kama nilivyojibu kwenye swali la kwanza lakini kwenye majibu yangu ya msingi, tayari tuna mechanism zetu za ndani ya nchi, kama vile Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, tuna taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa. Tuna mechanism nyingi ambazo zinaangalia uwazi na utawala bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan imeweka wazi mbele taasisi zetu na mifumo yetu yote hii itafanya kazi kwa uwazi na uhakika.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Tarafa ya Kalenga katika Jimbo la Kalenga Mkoani Iringa?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli sasa hivi mwelekeo tumekwenda mpaka ngazi ya Kata tumepeleka maofisa wetu wakaguzi na wakaguzi wasidizi kwa ajili ya kusomamia Shughuli za polisi. Sasa iwapo Kata ya Kalenga haina tutaipa kipaumbele ili kata hii iweze kingatiwa hatimaye vijana wetu waweze kufanya kazi kwenye mazingira stahiki ya kutoa huduma za usalama wa raia na mali zao. Ahsante.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Barabara ya kutoka Irula katika Jimbo la Kilolo kwenda Image mpaka Kata ya Ibumu ni barabara mbaya sana, haijawahi kuchimbwa hata siku moja: Ni lini Serikali itajenga barabara hiyo kwa kiwango hata cha changarawe tu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Tendega ameainisha hii barabara ya kutoka Irula mpaka Ibumu kwamba ni bararaba ambayo haijajengwa, basi tutakwenda kufuatilia ili tuone kama imeanishwa kwenye bajeti ili tuweze kuifanyia kazi.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya Halmashauri zimekuwa kubwa mno na nyingine zimekuwa zina maeneo makubwa sana kijiografia, lakini nyingine zina Majimbo matatu, nyingine zina Majimbo mawili na kupata huduma wanapata katikati ambako ni Mjini.

(i) Je, serikali sasa haioni haja ya kufuata uhalisia na urahisi wa kupata huduma katika ugawaji wa Halmashauri hizo?

(ii) Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba katika utengaji wa fedha za maendeleo jiografia za Halmashauri zetu iwe ni mojawapo ya kigezo cha kuzingatiwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali wawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tuna Halmashauri ambazo zina maeneo makubwa kijiografia, lakini kuna Halmashauri ambazo zina Majimbo zaidi ya moja na ni kweli kuna changamoto ya umbali kutoka baadhi ya maeneo ya Halmashauri kufika kwenye Makao Makuu ya Halmashauri hizo. Serikali kwa sasa sote ni mashahidi kwamba mamlaka nyingi zimeanzishwa hazina majengo muhimu ya utawala, hazina miundombinu muhimu ya huduma za jamii. Kwa hiyo, kipaumbele cha Serikali kwa sasa ni kukamilisha kweye mamlaka zilizopo na baada ya hapo taratibu zitafuatwa ili kupata mamlaka nyingine na kusogeza huduma kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili; Serikali imekuwa ikipeleka fedha kwa kuzingatia jiografia kwa maana ukubwa wa maeneo, ndiyo maana hata kwenye Mfuko wa Jimbo, kigezo mojawapo ni ukubwa wa eneo la Halmashauri husika lakini hata kwenye fedha za barabra kwa maana ya TARURA kigezo mojawapo ni hicho. Kwa hiyo, Serikali inazingatia pia ukubwa wa kijiografia wa maeneo husika. Ahsante. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu ya Mheshimiwa Waziri ameonesha kwamba asilimia 88 ndio wameunda katika vijiji, kata na kwenye mitaa yetu. Hata hivyo Kamati hizi zimekuwa hazitekelezi majukumu yake ama hazifahamiki ipasavyo. Mimi nilitaka kujua, je, kamati hizi za ulinzi na usalama wa watoto zimeundwa na wajumbe gani ili tuwatatmbue tuweze kuwafuatilia?
NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swal la nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwongozo wa Kuanzishwa Madawati ya Ulinzi na Usalama kwa Watoto ulianzishwa Juni, 2022 na kuanzishwa madawati hayo machache. Hata hivyo wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Wizara ya Elimu pamoja na Mamlaka ya Jeshi la polisi tutaendelea kuimarisha Kamati hizi ifikapo mwaka 2023 basi tutahakikisha shule zote zina madawati. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, Mradi wa Umwagiliaji wa Izazi uliyopo Jimbo la Isimani una changamoto ya uchakavu wa miundombinu pia. Ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kukarabati miundombinu hiyo?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mirada yote ya umwagiliaji tuliyonayo hapa nchini hivi sasa tumeweka mpango mkakati katika mwaka wa fedha ujao kuhakikisha kwamba Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, inaipitia miradi yote nchini Tanzania, tufanye uhakiki, tujue miradi gani inafanya kazi, ipi haifanyi kazi na ipi inahitaji marekebisho ya kiwango gani?

Mheshimiwa Spika, katika uhakiki huo pia tutagusa na miradi ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Zahanati ya Kata ya Lumuli ambayo iko katika Jimbo la Kalenga, ziko mbili. Katika Zahanati hizi, wananchi walishapaua na wameshajenga majengo yako vizuri lakini hakuna samani, vitendanishi na vifaa tiba, ni lini Serikali itapelekea hivyo vitu ili wananchi waweze kupata huduma ya afya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza niwapongeze sana wananchi wa Iringa kwa kujenga zahanati hizi na kuzikamilisha. sasa niseme, kwamba vifaa tiba vinavyohitajika katika ngazi ya zahanati, gharama yake siyo kubwa sana ni imani yangu kwamba mkurugenzi wa halmashauri husika, wana uwezo wa kutenga kati ya ile asilimia 40 na 60 kununua vifaa tiba hivi. Kwa hiyo, naelekeza halmashauri, wakurugenzi watenge fedha, wanunue vifaa tiba zahanati hizi zisajiliwe ziweze kutoa huduma ahsante.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo tangu mwaka 2017, ilipitia taratibu na vigezo vyote vya kuweza kugawa jimbo. Lakini changamoto iliyorudishwa ni Kamba kuna idadi ndogo ya watu. Je, Serikali itakuwa tayari kuigawa hii halmashauri, baada ya sensa ya mwaka huu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Halmashauri ya Kilolo, ilikuwa imekidhi vigezo vingine isipokuwa ya idadi ya watu; na kinachosubiriwa ni kujua hiyo idadi watu. Mimi ninaamini kwamba kama vigezo vitafikiwa basi mapendekezo yatapelekwa huko mbele na mamlaka husika italiangalia. Kwa hiyo, tusubiri vigezo vikishakuwa vimekamilika, basi hatua hiyo inaweza kukubalika baadaye. Ahsante sana.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya kutoka Iringa Mjini kwenda katika Hifadhi ya Taifa Ruaha ambayo imetengewa fedha miaka mingi lakini hazitoshi na hazitoki na upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulishafanyika; je, ni lini sasa hii barabara itakwenda kujengwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Barabara ya Iringa – Ruaha (Iringa Msembe), kilometa 104, inafadhiliwa na World Bank na hivi tunavyoongea iko kwenye hatua ya manunuzi kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Wakati tunasubiri Musawada wa Bima ya Afya kwa wote.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba, watu wenye ulemavu wanapata bima ya afya wasio na uwezo?
NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kumuomba Mbunge mimi nayeye ili tusisubiri muswada wa bima ya afya, tuusukume kwa pamoja tuhakikishe unatokea. Lakini pia, ukweli ni kwamba kila hospitali yetu anakuwepo mtu wa ustawi wa jamii. Kazi yake ni kuhakikisha watu wa namna hiyo wanashughulikiwa na wanapata huduma. Hao walemavu hakuna ambaye hana uwezo ambaye amekosa huduma.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini kwanza kabla ya swali langu nitoe utangulizi, katika majibu ya Mheshimiwa Waziri anasema msamaha wa kodi uliotolewa ni baiskeli pamoja na magari mahususi kwa matumizi ya watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mlemavu wa macho au asiyoona hivi gari lake linafananaje? Naomba kuuliza swali la kwanza; Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba inatoa msamaha wa kodi kwa watu wenye ulemavu wa macho na vifaa vingine vyote wanavyoleta iwe sawa kama wale wenye ulemavu wengine waweze kupata msamaha wa kodi hiyo na kuleta unafuu wa maisha yao? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; kumekuwa na baadhi ya Watendaji wa Wizara hiyo ambao wanahusika na utoaji wa msamaha wa kodi wakiwatoza kodi wenye ulemavu na katika majibu ya Mheshimiwa Waziri ameonyesha msamaha wa kodi unatolewa. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari nimletee watu wenye ulemavu ambao wametozwa kodi wakati wanahitaji msamaha huo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa
Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tendega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kujibu maswali hayo, naomba nimpongeze sana kwa kiasi ambacho anawapigania ndugu zetu wenye ulemavu. Swali lake la kwanza kama nilivyojibu katika swali la msingi ni vifaa tu mahususi ambavyo wanatumia ndugu zetu wenye ulemavu ndivyo ambavyo vinapata msamaha, lakini maoni yake tunayachukua, tunaenda kuyaangalia kama yanaleta tija kwa pande zote mbili kwa walengwa na Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, siwezi kukataa kukutana na ndugu zetu, wananchi wenzetu wenye ulemavu na watu wengine wote mimi niko tayari kukaa nao, lakini naomba baada ya kipindi hiki cha maswali na majibu nikae na Mheshimiwa Mbunge tuone kwa kiasi gani tunaweza tukapata ufumbuzi wa suala hilo na kuwasaidia ndugu zetu hawa wenye ulemavu, ahsante. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wananchi wa Kata ya Lumuli ambayo iko Jimbo la Kalenga, Mkoa wa Iringa, walijenga maboma kwa ajili ya mabweni ya watoto wa kike, kwa miaka 13 sasa hayajamaliziwa. Ni lini Serikali itamalizia mabweni haya?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokuwa nimeshasema hapo awali, Serikali itamalizia mabweni haya, hata hili la Lumuli kule Kalenga, kwa kadiri ya upatikanaji wa fedha. Na tutaangalia katika mwaka huu wa fedha ambao tunakwenda kuuanza wa 2023/24 kama shule hii imetengewa fedha ili mabweni haya yaweze kukamilishwa na Serikali kuunga mkono juhudi za wananchi katika eneo hili.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa. Ni lini Serikali itajenga daraja la kutoka Itununu kwenda Igodi kafu ambayo ni Jimbo la Isimani kuhakikisha kwamba wananchi wanaweza wakapata huduma ya kwenda kwenye Hospitali ya Wilaya na wanafunzi wanashindwa kwenda shule?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itajenga barabara hii ya Itununu kwenda Igodi Kafu kadiri ya upatikanaji wa fedha. Na kwa sababu kuna huduma muhimu kama ya shule na vilevile kituo cha afya ambapo wananchi wanapata huduma basi tutaiangalia na kuiwekea kipaumbele ili barabara hii nayo iweze kutengenezwa.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu ya Serikali, Mbunge wa Mufindi Kusini Mheshimiwa David Kihenzile, amekuwa akipigania sana na akiomba ukarabati wa mradi wa Imayi, yaani Kata za Ihoanza, Malangali na Idunda; na ule wa Vijiji tisa wa Kata za Mbalamaziwa na Itandula, lakini mpaka sasa haujaanza: Je, ni lini Serikali itapeleka fedha? Pamoja na kwamba mmesema fedha zimetengwa, lini Serikali itapeleka fedha mradi huo uweze kufanikiwa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Mradi wa watumia maji wa Magubike, Kata ya Nzihi Jimbo la Kalenga umejengwa na wafadhili wa Marekani wanaoitwa WARIDI, lakini tayari walishajenga intake na tank lipo tayari, changamoto ni namna ya usambazaji wa maji kwenda katika vijiji sita pamoja na vitongoji vyake: Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ili kupeleka miundombinu hiyo wananchi waweze kupata maji safi na salama? (Makofi)
NAIBU WAZIRTI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Victor Tendega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Wizara tumejipanga vizuri, mradi huu wa Mbalamaziwa ambao unaenda kuhudumia vijiji tisa, tayari tumeshapata Mkandarasi na tunatarajia bajeti ijayo Mkandarasi huyu aanze kazi kwa sababu kila kitu kimeshakamilika. Mradi wa Malangali ni mradi mkubwa ambao tunatarajia utatumia zaidi ya Shilingi bilioni sita. Dhamira njema ya Mheshimiwa Rais ya kumtua Mama ndoo kichwani inaenda kukamilika kwa sababu bajeti ijayo tutahakikisha tunaleta fedha kwa awamu na kwa wakati ili mradi huu uweze kukamilika kwa wakati, na wananchi waweze kunufaika na maji safi na salama ya kitoka bombani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la intake na tenki kukamilika kwenye Jimbo la Kalenga, tayari tunaendelea na utaratibu kuona kwamba usambazaji wa maji tunakuja kuufanya ndani ya bajeti hii tunayoimalizia, pia kwa bajeti ijayo, tutakuja kuhakikisha maeneo yote ambayo yanapaswa kufikiwa na maji, yanakwenda kufikiwa. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Jimbo la Kalenga lina skimu 19 za umwagiliaji ambazo miundombinu yake yote ni chakavu.

Je, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba miundombinu hii inaboreshwa?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti yetu ya mwaka 2023/2024 tumetenga maeneo zaidi ya 80 ambayo yanakwenda kufanyiwa ukarabati zikiwemo skimu zilizo katika Jimbo la Kalenga. Kwa hiyo nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge, anaweza kupitia akaangalia orodha yetu na akaona kama maeneo yao yapona aweze kujiridhisha.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia watu wengi sana kwa sababu jiko barabarani pale, watu wa kutoka Mufindi wanahudumiwa pale lakini miundombinu yake ni chakavu;

Je, ni lini Serikali itakarabati miundombinu hiyo?
NAIBU WAZIRI, 0FISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itakarabati miundombinu hii chakavu pale katika Hospitali ya Mji Mafinga kadri ya upatikanaji wa fedha. Lakini nirudie tena kwamba Wakurugenzi wa Halmashauri wana wajibu wa kuhakikisha wanatenga fedha kwa ajili ya kuanza kutengeneza miundombinu mbalimbali kwenye halmashauri zao. Tayari Serikali kuu mmeona imefanya mengi chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka fedha nyingi kwenye halmashauri hizi. Ni wakati umefika kwa wakurugenzi, mabaraza ya madiwani nao kuweka kipaumbele cha kusaidia wananchi pale na kuujnga mkono juhudi ambazo Serikali hii ya awamu ya sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya kwa kupeleka fedha nyingi kwenye sekta hizi za elimu na afya.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Tumekuwa tukiona wanunuzi kutoka nje ya nchi wakija kununua mazao moja kwa moja wakiwa na magari yao ambayo yana namba za nje ya nchi; na tumekuwa tukiona wananchi wanauziwa kwa bei za chini sana, hasa mazao ya parachichi na mazao mengine kwa sababu hawana mtu anayewasimamia vizuri. Je, mnunuzi anapoenda kununua mazao hayo moja kwa moja kwa sasa hizo data wanazichukuwaje?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa Serikali imekiri kabisa inaendelea kuboresha huo mfumo wa ATMIS na TANCIS ni lini maboresho hayo yatakwenda kukamilika kwa sababu tumeona kwamba, bidhaa zinaenda nje ya nchi na tumekuwa hatujui mchango kamili wa kilimo kwa fedha za kigeni.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la kwanza, ni kweli kumekuwepo na baadhi ya wanunuzi ambao wanakwenda moja kwa moja mashambani, ndiyo maana Waheshimiwa Wabunge mtakumbuka tulileta utaratibu wa namna ya ununuzi wa mazao ili wale wote ambao wanataka kununua mazao nchini Tanzania wafuate utaratibu na mwisho wa siku sisi kama Serikali tupate takwimu sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali ni nini katika hili. Jambo la kwanza, katika eneo la mazao ya nafaka, hivi sasa tunataka kuboresha, kutengeneza masoko ili bidhaa zote zipelekwe katika masoko na wanunuzi wakanunue katika masoko yanayotambuliwa ili kupata takwimu sahihi.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, kwenye mazao ya mbogamboga na matunda, hivi sasa tunajenga common use facilities tatu za kuanzia katika eneo la Nyororo, Hai na Kurasini, ambapo kwa mfano parachichi yote itakusanywa, tutafanya grading, sorting na packaging ambayo itatupa pia uhakika wa kujua ni parachichi kiasi gani imekusanywa na kupelekwa nje ya nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, swali lako la pili kuhusu mifumo hii, kama mnavyofahamu Waheshimiwa Wabunge mifumo hii siyo jambo la siku moja. Tunaendelea kuiboresha kutokana na maendeleo ya teknolojia vilevile na ukuaji wa soko.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano kwa hivi sasa, tunao mfumo wetu ukiacha hii mifumo mingine wa kutumia mamlaka ya afya, mimea na viuatilifu, ambao wao wanawajibu wa kutoa phytosanitary kwa bidhaa zozote ambazo zinatoka nje ya nchi, cheti cha usafi wa mazao pia na wenyewe ni mfumo ambao tumewaunganisha kutupa takwimu sahihi. Kwa hiyo, hakuna mtu aliye na uwezo wa kusafirisha mazao nje ya nchi kama hajapata export permit na phytosanitary certificate ambayo pia inatupa nafasi ya kuweza kujua ni mazao kiasi gani yamesafirishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, tutaendelea kuboresha mfumo huu ili tupate takwimu sahihi ya mazao yetu.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika Awamu ya Tano ambayo kupitia RIGRO walipendekeza kwamba lengo kubwa ni kukuza utalii Kusini na walichagua Mkoa wa Iringa uwe ni makao makuu ya mradi huo. Sasa tumeshatenga eneo lipo na kila mwaka tunaadhimisha wiki ya utalii pale Mkoa wa Iringa.

Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha utekelezaji wa makao makuu haya unafanyika? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba wananchi walioko pembezoni mwa mbuga hii wanapata elimu, wanawezeshwa kielimu na kiuchumi kuhakikisha kwamba wao ndio watakaokuwa watangazaji wa mbuga hii?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza niendelee kuwapongeza Wabunge wote wa Iringa, pamoja na kuwa swali hili na Mheshimiwa Grace Tendega, lakini mara nyingi wanafuatilia sana kwenye mradi huu wa RIGRO na ujenzi wa information center ambayo itajengwa Makao Makuu Iringa uko kwenye hatua za kuanza. Tayari tulikuwa kwenye mkakati wa mkandarasi ambaye tayari tulikuwa tumeshatangaza kazi na tuko anytime kuanza kazi hii. Kwa hiyo, naomba niwataarifu tu kwamba Wana-Iringa na Watanzania wote kwa ujumla kwamba utalii na mkakati wa kukuza utalii Kusini mwa Tanzania uko mbioni kuanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala hili la kuwapa elimu wananchi wanaoishi pembezoni mwa hifadhi; kwenye Mradi wa RIGRO zimetengwa fedha kwa ajili ya kuwapeleka training wananchi mbalimbali waliozunguka katika maeneo yanayozunguka mradi huu, na ni shahidi tosha Wabunge wanaotoka katika maeeo hayo wanafahamu kwamba tumekuwa tukipeleka watoto ambao wanapelekwa shuleni kwa ajili ya kujifunza namna ya kuendeleza masuala mazima ya utalii na uhifadhi. Kwa hiyo, faida wameshaanza kuziona na wananchi wameshaanza kuona faida ya mradi huu.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Ninaomba sasa niulize maswali mawili ya nyongeza.

a) Je, ni kwa nini Serikali inachukua muda mrefu kutoa vitambulisho kwa Watanzania, hamuoni kwamba mnawakosesha fursa mbalimbali ambapo kitambulisho ndiyo takwa la fursa hizo?

b) Je, ni lini Serikali itaoanisha data zote za msingi ili ziweze kusomeka kwenye kitambulisho hicho cha NIDA?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru sana kwa maswali haya mawili ya nyongeza. Naomba kutoa majibu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Matiko, amekuwa mara kadhaa akifuatilia kuona namna ambavyo Watanzania wanaweza kupata vitambulisho ili kuweza kupata huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haijachukua muda mrefu sana kutoa vitambulisho kwa watu; na kama imechukua basi tulikuwa tuna changamoto. Changamoto ya kwanza tulikuwa na upungufu wa mashine za kisasa ambazo zilikuwa zinatoa vitambulisho kwa speed kubwa. Niwaambie wananchi na Watanzania; sasa tumeshapata mashine bora za kisasa na tunakwenda kuhakikisha Watanzania wote wanapata vitambulisho ili waweze kupata huduma, kwa sababu tunatambua sasa hivi kila kitu ni kitambulisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto nyingine. ninawomba Watanzania wote, wakamilishe taratibu ili tuweze kupata vitambulisho. Kuna watu wanashindwa kutoa baadhi ya particulars muhimu za kutengenezewa vitambulisho. Inakuwa ngumu kwetu kuweza kuwakamilishia.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona kwamba tunavyo vitambulisho vingi. Tuone namna ya kuviunganisha vitambulisho hivyo ili kiwe kimoja. Maana yake hicho hicho kiwe na uwezo wa kutumika benki, kwenye passport unaweza ukawa unakitumia kama NIDA au kitambulisho kingine. Tuko mbioni kuona namna ambavyo Serikali itapunguza changamoto hiyo, ninakushukuru.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; je, ni lini Serikali itafungua kituo cha afya cha Kata ya Lyamugungwe na kupeleka vifaa tiba?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutaangalia katika mwaka wa fedha unaofuata kama kuna fedha imetengwa, na kama bado haikutengwa basi tutatenga kwenye mwaka wa fedha wa 2024/2025.

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa. Je, ni lini Serikali itajenga daraja la kutoka Mlambalasi ambayo ni Kata ya Kiwere kwenda Kalenga ambako ndiko kwenye Makumbusho ya Chifu na wananchi wamekuwa wakipata shida sana? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, tutakaa na Mheshimiwa Mbunge kuweza kupitia bajeti ya TARURA ya mwaka 2023/2024 na kuona ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa daraja hili la Mlambalasi kuelekea Kalenga; na kama bajeti imetengwa tutahakikisha mara moja fedha hiyo inakwenda ili ujenzi huu uweze kuanza.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona:-

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Kalenga lina skimu ambazo ni chakavu sana. Nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba, skimu hizo zinafufuliwa na zinakuwa zinahudumia wananchi?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha miradi yote ya umwagiliaji inafanya kazi. Ninataka nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba, tunaendelea kuipitia miradi yote, tutakwenda pia katika Jimbo la Kalenga kuangalia na pia, wataalam wetu watafanya kazi tutahakikisha kwamba, miradi hiyo inafanya kazi na wakulima waweze kufanya kilimo cha umwagiliaji.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwanza nishukuru kwa majibu, lakini Serikali imesema itasimamia mikoa ili iweze kusimamia Halmashauri zisizo na utayari wa kuanza kutekeleza miradi.

Mheshimiwa Spika, lakini mikoa yenyewe imekuwa na chagamoto ya kuwa na fedha ambazo zinafanya ufatiliaji, tumekuwa tukiona tukienda ndio tunakwenda nao.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwawezesha kifedha Sekretarieti za Mikoa ili zitekeleze wajibu wao ipasavyo?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; fedha hizi hutolewa chini ya masharti ya Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa ya mwaka 1982; zipo Halmashauri zinapata fedha zaidi ya walichoomba na ziko Halmashauri zinapata pungufu ya walichoomba na zipo zinazocheleweshewa kabisa kupata kuanzia mwezi wa tano hadi wa sita, na Halmashauri zinazopata zaidi zinafanya ubadhirifu wa kutumia fedha zaidi nje ya matumizi ambayo walipanga na nyingine zinazopata kidogo hazitekelezi mikakati yao kikamilifu. (Makofi)

Je, Serikali ina mkakati gani na kauli gani tunaipata kutoka kwa Serikali kuhusu suala hili? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Victor Tendega kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na fedha zinazotakiwa kupelekwa katika mikoa nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, fedha zote zinazopelekwa katika maeneo yote kwa mujibu wa kanuni ambayo yeye mwenyewe amei–cite inayotoa miongozo ya fedha, inataka wahusika waombe fedha TAMISEMI ili wapelekewe na kama yako maeneo ambayo yametokea mapungufu hayo nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutafatilia na tungeomba taarifa hizo utupe za kina ili tuweze kuzifatilia.

Pili juu ya upendeleo; nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali haifanyi upemndeleo na kama nilivyoeleza kwenye jibu la msingi, miradi inayotekelezwa ndio ambayo inaielekeza Serikali ifanyeje, katika force account kinachofanyika ni kwamba Halmashauri husika inapokuwa tayari kutekeleza mradi inatoa taarifa kwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI, na fedha zinapelekwa na katika ilani ambayo inasimamiwa na wakandarasi Serikali inachofanya ni kwamba baada ya mkandarasi ku-raise certificate basi Serikali inapeleka pesa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nikuhakikishie na Bunge lako kwamba Serikali iko makini inaendelea kufanya kazi vizuri na kama yako mapungufu katika maeneo ambayo wewe Mheshimiwa Mbunge umewahi kupita, basi utupe taarifa tuweze kufatilia na kuyafanyia kazi. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi; ni lini Serikali itaiongezea nguvu minara ya TTCL iliyoko katika Kata ya Maguliwa, Jimbo la Kalenga, Kata ya Wasa na minara ya Airtel ambayo iko Kata ya Ulanda?
NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama iifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuelewa kuwa kuna haja ya kuongeza nguvu katika minara kadhaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa tuna zaidi ya minara 800 ambayo inahitaji kuongezewa nguvu. Serikali imeanza na awamu ya kwanza ya kuongeza minara 408 na mpaka sasa kwenye mradi wetu wa Tanzania ya Kidigitali ni minara 302 inakwenda kuingizwa katika utekelezaji na kuhakikisha kwamba minara hiyo inapata nguvu ya kutosha na kupata huduma za internet.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimuombe Mheshimiwa Mbunge awe na subira kidogo wakati Serikali inatafuta fedha ili tuhakikishe kwamba Tanzania yetu yote inakuwa ya kidigitali.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona, wananchi wa Mji wa Mafinga walishaanza kujenga Kituo cha Afya cha Upendo na kwa nguvu zao wenyewe.

Ni lini Serikali itapeleka nguvu za ujenzi katika kituo hicho?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itapeleka fedha katika Kituo hicho cha Afya Upendo ku-support nguvu za wananchi kadiri ya upatikanaji wa fedha. Vilevile nao wana uwezo wa kuanza kutenga bajeti kwa ajili ya ku-support jitihada hizi za wananchi hawa.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Hospitali ya Mji wa Mafinga inahudumia watu wengi sana pale, nini mkakati wa Serikali kuongeza vifaa tiba vya kisasa? (Makofi)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali hii ya Awamu ya Sita ni kuhakikisha kwamba vifaa tiba vya kisasa vinakuwepo katika hospitali zote za Wilaya na vilevile katika vituo vyetu vya afya vya kimkakati. Katika kuhakikisha hilo linafanyika Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 112 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba hivyo vya kisasa na tutahakikisha pia Hospitali ya Mji wa Mafinga nayo inaongezewa vifaa tiba kama ilivyofanyiwa katika mwaka wa fedha huu tunaomaliza sasa.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Halmashauri nyingi zinakosa fedha za kujiendesha zenyewe kutokana na Serikali Kuu kuchelewesha zile asilimia ambazo zinawekwa na zinatengwa kwamba, kwa kisheria asilimia 20 ndiyo inabaki asilimia 80 inakwenda Serikali Kuu.

Je, Serikali iko tayari kutengeneza mfumo ambao utafanya Halmashauri zinapokusanya fedha zile asilimia 20 zibaki moja kwa moja katika Halmashauri zake, badala ya kusubiri zirejeshwe kama ambavyo Serikali inakuwa hairejeshi wakati mwingine?

Swali langu la pili, kwa kuwa Halmashauri ndiyo watekelezaji wakuu wa sera na mipango ya Serikali Kuu kwa ngazi ya chini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kurejesha vyanzo vyote vya mapato ambavyo vinakusanywa katika Halmashauri ili viweze kuwasaidia kuendesha Halmashauri hizo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Tendega kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza la Serikali kuwa tayari kutengeneza mfumo kwa ajili ya kubakiza asilimia hizi kulekule kwenye Halmashauri ni wazo zuri na tunalipokea, tutakaa na timu ya wataalam kuona wamefikia wapi kwa sababu tayari pia wao walikuwa wanalifanyia kazi kwa ajili ya kutengeneza mfumo huo. Tutakaa kuona wamefika wapi na wenzetu vilevile wa Hazina kuona wamefikia wapi kwa ajili ya kuweza kutengeneza mfumo huu lakini ni wazo zuri.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili, tayari Serikali Kuu imeanza kuzirudishia Halmashuri vyanzo vile ambavyo wanakusanya. Mfano, katika mwaka wa fedha huu tunaoenda kuuanza wa 2023/2024 vyanzo vya makusanyo vile vya mabango ya matangazo vimerudishwa kule kwenye Halmashauri zenyewe ili ziweze kukusanya na tunaendelea kuangalia kama Serikali kwa ujumla wake ni vyanzo vipi viweze kuendelea kurudishwa kwenye Halmashauri zile ili kuziongezea uwezo.

Mheshimiwa Spika, vilevile Serikali kuu imekuwa ikipeleka fedha nyingi kwenye miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri hizi hata zile ambazo hazina uwezo kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya kuwasaidia katika ujenzi wa madarasa, katika ujenzi wa zahanati, katika ujenzi wa vituo vya afya na kadhalika ili kuwapunguzia mzigo Halmashauri hizi.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa; pamoja na tembo kuvamia maeneo mbalimbali hivi karibuni katika Kata ya Lyamigungwe na Kata ya Lupota simba wamevamia katika mifugo ya wananchi na wamekula mifugo ile na wananchi wana taharuki kubwa. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wanakuwa huru? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante, nimepokea maswali tisa ya nyongeza kwa Waheshimiwa mbalimbali na naomba niyajibu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la Mheshimiwa Londo; ameuliza ni nini kauli ya Serikali? Kama ambavyo nimejibu kwenye swali la msingi. Ni kwamba sasa hivi tunaangalia njia mbadala wakati huo huo tunaendelea kutatua migogoro hii ya wanyama wakali na waharibifu. Tunajenga vituo, tunaajiri VGS, lakini wakati huo huo tumeshaweka sasa mipango kwenye baadhi ya maeneo tuanze kuweka fence ya umeme ili kupunguza hii athari ya wanyama wakali na waharibifu.

Mheshimiwa Spika, kwenye suala la Mheshimiwa Anne Malecela, naomba niahidi mbele ya Bunge lako hili Tukufu kwamba baada ya Bunge hili tutaongozana naye katika maeneo yale. Lakini pia tumeshaanza kuongeza nguvu kwake, tumepeleka askari na tutaendelea kuajiri VGS katika maeneo hayo ili tuweze kushirikiana pamoja. Kwa hiyo, wananchi wa Same kilio chenu kimeshasikika Bungeni na tutaongozana na Mheshimiwa Mbunge (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye suala hili la Mheshimiwa Vita Kawawa, ni kweli Mheshimiwa Waziri alitoa ahadi ya ujenzi wa madarasa katika jimbo lake, na huu ulikuwa ni mpango wa CSR si kwa ajili ya fidia ya wanyama wakali na waharibifu. Ni kwamba Mheshimiwa Waziri alifanya ziara katika jimbo hilo na akatoa ahadi ya ujenzi wa madarasa ili kuwafanya wananchi wanaoishi katika maeneo hayo tushirikiane pamoja katika uhifadhi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niendelee tu kuahidi kwamba ahadi ni deni, Wizara itatekeleza. Na kwa kuwa ilikuwa ni kauli ya Mheshimiwa Waziri basi tutafuatilia ili ahadi hii iweze kutekelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Dunstan, Mbunge wa Mkinga, yeye ameongelea kuhusu kituo; niahidi tu kwamba katika mpango wa fedha wa 2023/2024 uliopitishwa katika Bunge lako hili, tutapeleka kituo katika Jimbo la Mkinga ili tuongeze nguvu ya kudhibiti wanyama wakati na waharibifu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Justin Nyamoga, madhara makubwa; naomba niahidi tu kwamba tutaendelea kufuatilia katika maeneo haya ili wananchi waweze kulipwa fidia inayotokana na wanyama wakali na waharibifu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Grace Tendega; naomba tu nilitaarifu Bunge lako, na kwa ridhaa yako, nipe tu nafasi kidogo nitoe ufafanuzi. Tumekuwa na changamoto nyingine imejitokeza katika Mkoa wa Iringa; kuna uvamizi wa simba kwenye baadhi ya maeneo, lakini naomba niwataarifu wananchi, nadhani wameona juhudi za Serikali toka uvamizi huu umejitikeza tumekuwa karibu na wananchi, tunatoa elimu.

Mheshimiwa Spika, naniendelee kutoa elimu kupitia Bunge lako hili, kwamba wakati huu ambapo tunawasaka hawa simba, wananchi wawe na tahadhari ya kutotembea usiku. Lakini pia wenye mifugo wawashe moto kuzunguka maeneo yale ya mifugo ili kuepusha simba wasisogee katika maeneo hayo tunajitahidi sana kulinda maisha ya Watanzania.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwaombe Wanairinga, Serikali iko kazini na tumeshapeleka helikopta inazunguka usiku na mchana kuhakikisha tunawasaka hawa simba. Tuendelee kushirikiana pamoja ili kuhakikisha zoezi hili tunalikamilisha na simba hawa tunawachukua na kuwarudisha katika maeneo yao.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la Mheshimiwa Charles, Mbunge wa Mwibara; kumekuwa na changamoto ya viboko na tembo. Naomba niendelee tu kuahidi, nakumbuka tuliwasiliana na Mheshimiwa Mbunge na tukaongeza nguvu ya askari katika maeneo hayo. Tuendelee tu kuwasiliana, nguvu tutaongeza lakini pia tutaendelea kuajiri VGS ili waweze kusaidia pale inapotokea dharura katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na ombi la Mheshimiwa Jimbo la Tunduru kwamba tuongeze VGS (askari wa vijiji). Tunaomba tulipokee hili na tutaweka priority katika eneo hili, tunajua hii changamoto ya wanyama wakali.

Mheshimiwa Spika, pia kulikuwa kuna shida moja ya mratibu ambaye alihamishwa. Nadhani maelekezo yameshatoka, atarudishwa katika eneo hilo ili aweze kushirikiana na wananchi kudhibiti wanyama wakali na waharibifu.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Matiko tayari nimeshalijibu, kwamba tuko kwenye process ya ku-review hizi sheria na kanuni kuangalia sasa angalau tusogeze kiwango fulani ili wananchi nao waweze kuona umuhimu wa namna ya uhifadhi.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwanza nishukuru majibu yake ni mazuri sana, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza, nina matarajio kwamba sasa kila Mkoa utapata kituo hiki cha One Stop Center. Swali langu, ni lini vituo hivi vitaanza?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Maafisa Ustawi wa Jamii ndio wanaotoa huduma za kisaikolojia; nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba mnaajiri Maafisa Ustawi wa Jamii wa kutosha ili waweze kutoa huduma hii?
NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Tendega kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuratibu uanzishaji wa vituo vya mkono kwa mkono hadi kufikia lengo la kuwa na angalau kituo kimoja kwa kila Mkoa. Hii ni kwa sababu ya kuwasaidia wananchi wetu pale wanapopata matatizo au changamoto ili waweze kwenda mahali ambapo watafanikiwa na kutatuliwa matatizo yao.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, Serikali itaendelea kuwaajiri Maafisa Ustawi wa Jamii kila tunapopata kibali ili waweze kusambazwa nchi nzima na kuhakikisha matatizo yote yanaondoka kwa wananchi na kupata elimu ambayo itawasaidia ili wasiathirike na msongo wa mawazo, ahsante. (Makofi)
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni lini Serikali itajenga Daraja la Itunundu kwenda Igodikafu Jimbo la Isimani ambako wananchi wanapata shida sana hasa wakati wa masika? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tendega, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba daraja alilolitaja litajengwa kama lilivyoainishwa kwenye ilani na hasa baada ya kufanyiwa usanifu wa kina.
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona daraja la Zihi – Mlambalasi kwenda Kiwele ambalo ni Jimbo la Kalenga ni daraja ambalo ni muhimu sana linatakiwa lijengwe kwa sababu linakwenda kwenye makumbusho ya Mkwawa.

Ni lini Serikali italijenga daraja hilo kwa sababu sasa hivi watu wanapita tu, ni kasehemu kadogo wanapita kwa pikipiki tu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunajenga madaraja ambayo yamekuwa sumbufu katika maeneo mbalimbali nchini. Kwa hiyo, niwaagize tu Mkandarasi wa TARURA Mkoa wa Iringa waweze kwenda kufanya tathmini na baada ya tathmini tutafute fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo. Ahsante.

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, nauliza maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, kutokana na uelewa wangu halmashauri zote zilizo nchini zinatofautiana mapato na Serikali imekuwa ikitangaza tu mafunzo ili halmashauri zijihudumie; je, hamuoni sasa kuna umuhimu wa Serikali kupeleka fedha kwa uwiano sawia?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kumekuwa na mfululizo wa hati chafu ambazo ni zaidi ya miaka kumi mfululizo; je, Serikali haioni kwamba inaendelea kupoteza fedha za wananchi kwa kutokuwa na watu wenye weledi au ufanisi mkubwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Grace Victor Tendega, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja ya lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba tunaongeza fedha kwa ajili ya mafunzo na tutazigawa kulingana na uwiano katika halmashauri moja na nyingine, kwa hiyo, hilo ndiyo lengo la Serikali, lengo letu ni kuhakikisha kwamba tunazuia wizi kwa kuwapa mafunzo ya kuweza kuzuia vitendo hivyo vya kihalifu katika halmashauri zetu.

Mheshimiwa Spika, lakini suala la pili kuhusu hati chafu katika maeneo mengi nchini, moja ya kazi kubwa ambayo tumeifanya sasa hivi ni kuhakikisha moja tunawaondoa watu wote wanaosimamia fedha katika maeneo hayo wakiwemo wahasibu, ma-DT pamoja na wakurugenzi. Kwa hiyo, hizo ni hatua ambazo tunachukua, lakini sasa hivi tutakkuwa tunaleta watu ambao ni waadilifu katika maeneo yetu na hatutakuwa tunahamisha kama ambavyo ilikuwa awali mtu anafanya tukio baya upande mmoja tunahamisha katika halmashauri nyingine. Ahsante sana.