Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Miza Bakari Haji (1 total)

MHE. MIZA BAKARI HAJI: Mheshimiwa Spika, asante na mimi nina swali moja la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani mbadala ya kuwaepuka Wakandarasi wa aina hii ambao wanaleta usumbufu mkubwa kwa wananchi na hasara kubwa kwa Taifa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Miza Bakari Haji kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuifuatilia kwa ukaribu sana sekta hii ya ujenzi, naomba nimhakikishie kwamba Serikali yetu iko makini kuhakikisha inafuatilia utekelezaji wa mikataba. Kwa sasa tunahakikisha mikataba yote inaziba mianya yote ya kumpa mtu unafuu wa kuja kuharibu baadaye na akaja akadai analindwa na mikataba. Kwa hiyo, tuna hakikisha mikataba tunaiweka sawasawa na tutakapogundua yeyote ambaye uwezo wake, tatizo siyo mikataba tatizo ni uwezo wake huwa tunamzuia hapati miradi tena mingine.