Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Questions to the Prime Minister from Hon. Saumu Heri Sakala (1 total)

MHE. SAUMU H. SAKALA:
Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, katika nchi yetu kumekuwa na baadhi ya wafanyabiashara wa mazao kuwalazimisha wakulima kufunga mazao yao kwa mtindo wa lumbesa jambo ambalo licha tu ya kumdidimiza mkulima huyu na kumnyanyasa lakini pia linaifanya Serikali inakosa mapato.Mheshimiwa Spika, sasa ni nini kauli ya Serikali juu ya suala hili ambalo limekuwa likiendelea kwa muda mrefu sasa licha ya makemeo mbalimbali yaliyokuwa yanatokea?
WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saumu, Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli wako wafanyabiashara hasa wa mazao wamekuwa na tabia ya kuwalazimisha wakulima kununua kwa gunia lililofungwa kwa mtindo wa kuwekwa kile kichuguu maarufu lumbesa, kwanza hilo ni kosa.
Mheshimiwa Spika, Serikali imeshatoa maelekezo kupitia Wakala wa Vipimo ambao ni wasimamizi wakuu wa kuhakikisha kwamba biashara yote ya mazao ya kilimo nchini yanauzwa kwa vipimo vya kilo na siyo kwa kufunga gunia likawa lumbesa. Lakini pia kwa mazingira ya vijijini ambako hakuna mizani imejitokeza sana hilo Mheshimiwa Mbunge la kwamba watu wanafunga gunia mpaka lumbesa ndiyo inakuwa kama gunia moja. Lakini gunia letu sisi limepimwa limeshonwa viwandani kwa vipimo sahihi na lazima lishonwe kwa uzi
juu ndiyo linakuwa gunia na wala siyo ile lumbesa.
Mheshimiwa Spika, sasa jukumu la Serikali ni kuendelea kusimamia na mimi nataka nitoe wito tena kwa Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya na Halmashauri zao za Wilaya na Maafisa Biashara walioko kwenye Halmashauri hizo kusimamia kwamba biashara hii haiwanyonyi wakulima wadogo wanaouza mazao ya mahindi, vitunguu, viazi na kitu kingine kwa kufunga magunia kwa njia ya lumbesa. Jambo hili wala siwaachii Wakuu wa Wilaya peke yao nawaagiza pia Wakuu wa Mikoa kupitia Kamati zao za Ulinzi na Usalama kwenye Mikoa, zisimamie agizo ambalo lilishatolewa na Serikali na leo
Mheshimiwa Mbunge umeliuliza inawezekana mambo hayo bado yanafanyika huko na Serikali isingependa ione mnunuzi anakwenda kununua kwa mkulima na kumlazimisha amfungashie kwa lumbesa halafu anunue kwa bei ndogo ya gunia na lumbesa siyo gunia kwa sababu gunia ni lile limeshonwa kiwandani, lina vipimo na linahitaji kushonwa pale juu.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge nikiri kwamba wako Wafanyabiashara wajanja wajanja na sisi Serikali tuko macho na sasa kupitia agizo hili kwa wafanyabiashara kwenye Halmashauri za Wilaya na maeneo yote lakini pia lishuke mpaka chini kwa Watendaji wa Vijiji na Watendaji wa Kata pale ambapo kuna biashara ya mazao kwenye maeneo
yao, waendelee kudhibiti kwamba ufungashaji wa mizigo hiyo na ununuzi haununui kwa kigezo cha lumbesa badala yake ununue kwa vigezo vya kilogram au kwa gunia ambalo ni
rasmi kutoka viwandani . (Makofi