Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Questions to the Prime Minister from Hon. Hamida Mohamedi Abdallah (2 total)

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, lakini sasa nielekeze swali langu kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha kuwa Serikali inatekeleza lengo lake la sera za fedha na sheria kwa kupeleka maendeleo vijijini na hasa kwa kuwapelekea fedha za miradi ya maendeleo. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha fedha za miradi ya maendeleo, zinafika katika Halmashauri kwa wakati ili kuhakikisha wanatekeleza shughuli za maendeleo?
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali imeweka nia ya dhati ya kupeleka fedha zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo kwenye Halmashauri zetu, Wizara na Taasisi za Umma ili kufanya kazi za maendeleo. Waheshimiwa Wabunge ni mashahidi, mwaka huu kupitia bajeti yetu hii ambayo sasa tunaendelea nayo, tumefanya mabadiliko makubwa ya kutenga na kuongeza kiwango cha fedha za maendeleo kutoka asilimia 27 mpaka asilimia 40. Malengo yetu ni kuhakikisha kwamba miradi yote ya maendeleo, yale yote ambayo tunahitaji yafanyiwe maboresho, yanatekelezwa kama ambavyo imekusudiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweka mikakati kadhaa, moja ni kuhakikisha kwamba tunaongeza nguvu katika ukusanyaji wa mapato, lakini pia tunadhibiti mianya ya ukwepaji kodi ili kuweza kujiongezea pato zaidi, lakini kubwa zaidi ni kusimamia fedha hizi ambazo tunazipeleka kwenye Taasisi za Umma kwamba zinatumika kama ilivyokusudiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali bado tunaendelea kuwataka watumishi, pindi fedha hizi zitakapokusanywa na baada ya Bunge hili, tutaanza kupeleka fedha kwenye mamlaka zetu za Serikali za Mitaa na Taasisi na Wizara. Nataka nitumie nafasi hii kuwaambia Watumishi wa Umma waliopewa dhamana ya kupokea fedha na kusimamia matumizi, kuhakikisha kwamba fedha hii iliyotengwa inatumika kama ambavyo imekusudiwa; na kwamba hatutasita kuchukua hatua kali kwa yeyote ambaye atathibitika kupoteza fedha hizi nje ya matumizi ambayo tumeyakadiria.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni mkakati wetu pia kuhakikisha kwamba baada ya makusanyo tuzipeleke fedha zote. Wajibu mwingine ni kuhakikisha kwamba miradi inayotekelezwa inakuwa na thamani ya fedha iliyopelekwa kwa ajili ya matumizi ya maeneo hayo. Kwa hiyo, nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali itasimamia jambo hili, lakini pia tushirikiane Wabunge wote, nyie pia ni Wajumbe wa Mabaraza ya Madiwani kwenye maeneo yenu. Kwa hiyo, tusaidiane tukishirikiana, mkakati wa Serikali wa kupeleka fedha kwa wakati na mkakati wa Serikali wa kutaka kuongeza fedha ili kupeleka kwenye maendeleo uweze kufikiwa na hatimaye Watanzania waweze kuiona tija.
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH:
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, lakini sasa nielekeze swali langu kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha kuwa Serikali inatekeleza lengo lake la sera za fedha na sheria kwa kupeleka maendeleo vijijini na hasa kwa kuwapelekea fedha za miradi ya maendeleo. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha fedha za miradi ya maendeleo, zinafika katika Halmashauri kwa wakati ili kuhakikisha wanatekeleza shughuli za maendeleo?
WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali imeweka nia ya dhati ya kupeleka fedha zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo kwenye Halmashauri zetu, Wizara na Taasisi za Umma ili kufanya kazi za maendeleo. Waheshimiwa Wabunge ni mashahidi, mwaka huu kupitia bajeti yetu hii ambayo sasa tunaendelea nayo, tumefanya mabadiliko makubwa ya kutenga na kuongeza kiwango cha fedha za maendeleo kutoka asilimia 27 mpaka asilimia 40.
Malengo yetu ni kuhakikisha kwamba miradi yote ya maendeleo, yale yote ambayo tunahitaji yafanyiwe maboresho, yanatekelezwa kama ambavyo imekusudiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweka mikakati kadhaa, moja ni kuhakikisha kwamba tunaongeza nguvu katika ukusanyaji wa mapato, lakini pia tunadhibiti mianya ya ukwepaji kodi ili kuweza kujiongezea pato zaidi, lakini kubwa zaidi ni kusimamia fedha hizi ambazo tunazipeleka kwenye Taasisi za Umma kwamba zinatumika kama ilivyokusudiwa.
(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Serikali bado tunaendelea kuwataka watumishi, pindi fedha hizi zitakapokusanywa na baada ya Bunge hili, tutaanza kupeleka fedha kwenye mamlaka zetu za Serikali za Mitaa na Taasisi na Wizara.
Nataka nitumie nafasi hii kuwaambia Watumishi wa Umma waliopewa dhamana ya kupokea fedha na kusimamia matumizi, kuhakikisha kwamba fedha hii iliyotengwa inatumika kama ambavyo imekusudiwa; na kwamba hatutasita kuchukua hatua kali kwa yeyote ambaye atathibitika kupoteza fedha hizi nje ya matumizi ambayo tumeyakadiria.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ni mkakati wetu pia kuhakikisha kwamba baada ya makusanyo tuzipeleke fedha zote. Wajibu mwingine ni kuhakikisha kwamba miradi inayotekelezwa inakuwa na thamani ya fedha iliyopelekwa kwa ajili ya matumizi ya maeneo hayo. Kwa hiyo, nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba Serikali itasimamia jambo hili, lakini pia tushirikiane Wabunge wote, nyie pia ni Wajumbe wa Mabaraza ya Madiwani kwenye maeneo yenu. Kwa hiyo, tusaidiane tukishirikiana, mkakati wa Serikali wa kupeleka fedha kwa wakati na mkakati wa Serikali wa kutaka
kuongeza fedha ili kupeleka kwenye maendeleo uweze kufikiwa na hatimaye Watanzania waweze kuiona tija.