Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Salum Khamis Salum (1 total)

MHE. SALUM K. SALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Tatizo la bwawa la Maswa linafanana kabisa na tatizo tulilonalo katika bwawa letu la Mwenyehina Meatu na aliyekuwa Waziri wa Maji alikuja kulitembelea na akatuahidi kutusaidia chujio kwa ajili ya kusafisha maji kwa ajili ya Mji wa Mwanhuzi. Nimwombe Waziri kwa sababu ndiye aliyekuwa Naibu Waziri, atuambie bwawa hilo limefikia wapi kwa sasa?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naona Mheshimiwa muuliza swali alichagua mtu wa kujibu, lakini nitajibu kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo la maji Meatu, aliahidiwa kujenga chujio, katika Bunge hili tumeelekeza kwamba tumetenga fedha kupitia kwenye Halmashauri zote. Halmashauri zote 181 tumezitengea fedha na tumeelekeza kwamba, kwanza wakamilishe miradi ambayo ilikuwa inaendelea, lakini pili wahakikishe kwamba miradi ya kipaumbele kama vile kukarabati chujio ambalo Mheshimiwa Mbunge anasema, basi ni vema ashirikiane na Halmashauri kuhakikisha kwamba wanaweka kipaumbele kutumia zile fedha tulizozitenga kwa ajili ya kufanya ukarabati wa hilo eneo husika. Kama hiyo fedha itakuwa haitoshi, namwomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane, tushirikiane ili tuangalie ni namna gani tunaweza tukaongeza fedha baada ya kufanya budget review mwezi wa Desemba.