Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Salim Hassan Turky (7 total)

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
MHE. SALIM HASSAN ABDULLAH TURKY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata fursa hii. Na mimi nachukua fursa hii kumshukuru Allah Subhanah-Wataallah kwa kutujaalia afya njema, tuko mjengoni tunafanya vitu vya uhakika, hatujui kutukana, tunahakikisha nchi yetu inaenda mbele, uchumi unakua na wala hatutatoka hata siku moja ndani ya mjengo huu tunahakikisha Tanzania inakuwa na amani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kumpongesa sana Rais wetu Bwana Magufuli na hali kadhalika Rais wetu wa Zanzibar Mheshimiwa Dkt. Shein kwa ushindi wake wa kishindo. Kwa sababu leo kama unavyojua, timu za mpira zikiitwa, timu kama haijahudhuria, timu iliyohudhuria inapewa kombe. Sasa sioni sababu ya watu kunung‟unika kwamba aah, kuna hili na lile. Umeitwa njo kwenye mechi, hujaja, shukuru Mungu jipange tena kwa mechi ijayo. (Makofi)
Mhesjimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo, nataka sasa nichangie katika uchumi wa nchi yetu. Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara na wewe nataka nikupongeze sana kwa sababu una nia ya dhati ya kutekeleza kauli aliyoitangaza mwenyewe mkubwa wa nchi hii kwamba hii safari itakuwa ni nchi ya viwanda. Na wewe umekuwa kweli askari wake wa kwanza wa kuhakikisha hili linakuwa na unajitahidi sana!
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mawazo ambayo nataka niyatoe; tutake, tusitake Mji wetu wa Dar es Salaam, ndiyo soko kubwa la wenye viwanda, wenye biashara na kila kitu ni Dar es Salaam na hasa wazalendo wamewekeza sana katika viwanda vyetu. Naomba sana Serikali nayo kama inataka viwanda basi ihakikishe pale Dar es Salaam inajipanga kutafuta eneo na kuwaita wawekezaji wetu wa nchini kwanza waulizwe kwamba wao wana shida gani na tuweze kushirikiana nao kuona kwamba uchumi huu tunakuwa pamoja tunaendeleza vipi nchi yetu kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili kama litawezekana Mheshimiwa Waziri, ninaamini kwamba Tanzania hii itabadilika. Vilevile nataka nizumgumze jambo lingine ambalo kwa kweli siyo Wizara husika hii, lakini nataka kusema kwamba Dar es Salaam ni mji wa biashara. Sasa hivi umefika wakati, na mimi naamini Rais wetu yule analiweza, Makao Makuu yahamie Dodoma, Dar es Salaam ubaki kuwa mji wa biashara. Pale ndiyo tutapata hali halisi ya uchumi wetu utakavyokuwa. Kwa hilo wala hatuna haja ya kutafuta fedha, majengo ya Serikali yote yale yaliyokuwepo kama utayabinafsisha kwa bei ya soko la dunia, basi pesa zile zinatosha kabisa kujenga Dodoma yetu mpya na Wizara zote zikahamia hapa. Kwa hiyo, hili nalo litazamwe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja katika uchumi wetu baina ya Bara na Visiwani. Nataka kusema kwamba Zanzibar mara nyingi sana katika Muungano wetu tunakuwa tunaitazama Zanzibar kama mshindani katika uchumi wa Tanzania. Hii fikra nataka tuiondoe. Tanzania ni moja, kwa sababu leo kama Zanzibar itakua kiuchumi, basi tujue kwamba na Tanzania imekua ka sababu Bank of Tanzania ni moja ambayo ndiyo inahimili fedha yetu. Kwa hiyo, uchumi unapokua kokote, sote wawili tunakuwa pamoja. Kwa hili, naomba sana kwamba Wazanzibar wao mashallah wamejaliwa kwamba ni bingwa wa kufanya biashara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mnavyojua Tanzania hii tuna wafanyabiashara wakubwa wawili, tuna Wachaga huku, tunao na Wazanzibar kule wakiongozwa na Wapemba. Sasa ninachotaka kusema ni kwamba lazima tupange uchumi ambao utakua kwa nchi yetu. Nimeshawahi kutoa wazo hapa, sasa hivi, vijana kama tunavyoona wanataka ajira; na ili ajira hizi zipatikane, basi Zanzibar tuitazame kama inakuwa center moja ya uchumi. Sisi sasa hivi ushindani wetu mkubwa ni Dubai. Kila kitu tukienda kununua, tunaenda Dubai. Watu wana ma-account Dubai, wana majumba Dubai, watu wanaenda kununua magari Dubai. Hii Dubai kwa nini tusiisogeze ikawa Zanzibar yetu pale? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Watanzania wote tusikubaliane kwamba sasa Dubai ya Tanzania ni Zanzibar na uchumi wote uje pale magari yaje pale bidhaa zote zikae pale na ugomvi wa kudaiana ushuru baina ya Bara na Visiwani utaisha. Kwa sababu kama Zanzibar itakuwa freeport leo ukichukua mzigo Zanzibar ukileta Bara unalipa kodi kama zinavyotakiwa. Isipokuwa ukisema leo bandari hii kwamba Bagamoyo au Mtwara iwe freeport, utajizonga mwenyewe, kwa sababu utakamata vipi watu wasikuibie katika nchi moja? Bahari utai-control mara moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili naomba sana Waheshimiwa Wabunge wenzangu tulisimamie kwa nguvu zetu, ikiwezekana mwaka huu tuweke azimio la kuhakikisha kwamba Zanzibar inakuwa Dubai ya Tanzania. Hili lazima tufanye kazi pamoja na hapo ndipo uchumi wetu utakapobadilika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine nataka kueleza, Mheshimiwa Waziri toka ameingia madarakani FCC (Fair Competition Commission) pale kuna Bodi ambayo toka mwaka 2015 haipo. Sasa hivi tuna viwanda, tuna makampuni kibao, watu wameuziana share na kila kitu. Hatuwezi kwenda mbele kwa sababu Bodi inatakiwa iwepo pale ndiyo iamue. Sasa hivi kwa kweli ni mwaka wa pili, kesi nyingi ziko pale hazipati maamuzi. Naomba sana wewe ni mtu wa speed, hili ulisamamie kwa nguvu sana liweze kukaa vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nataka niseme, na-declare interest, mimi ni mfanyabiashara. Sasa hivi nchi yetu ina ukata mkubwa sana wa sukari. Leo inasikitisha sana kuona kwamba nchi hii watu wanahangaika kutafuta sukari. Miaka 21 iliyopita nchi hii tulibinafsisha viwanda vyetu vya sukari na watu ambao tuliwapa viwanda hivi walituahidi kwamba katika miaka mitatu mpaka mitano, Tanzania itajitosheleza kwa sukari. Leo wenye viwanda hawa inabidi tuwaulize, ni kipi ambacho kimefanya mpaka leo hatujaweza kujitosheleza? Wawekezaji wapya wakija hapa, baada ya muda unaona hawapo, ni kwa sababu gani? Isije kuwa kuna mitikasi ambayo inafanywa kuweza kuendelea na mfumo huu wa kila siku ikifika sukari hamna Tanzania, haitoshelezi. Hapa nataka Serikali iwe macho sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hili jana nilikuwa na Mheshimiwa Adam Malima. Mheshimiwa Adam alipokuwepo hapa aliulizwa swali kwamba tunataka kujua cost of production ya sukari katika nchi yetu, mpaka ameondoka Wizara ya Kilimo jibu hilo halikupatikana.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara, nawe nakupa swali hili, naomba ukija hapa utupe majibu ya cost of production ya sukari yetu ndani ya nchi hii ni kiasi gani? Halafu lingine mara nyingi sana watu huwa wanazungumza lugha hapa kwamba nchi nyingine zina-subsidize, lakini je, ile figure ya subsidize ni kiasi gani? Pia hatuijui?
Mheshimiwa Mwenyekiti, subsidization wanayopata kule, utakuta ni mtu anapata 10 percent to 12 percent. Leo sisi hapa tunavilinda viwanda hivi kwa kuweka 100 percent protection. Kwa nini tunaweka ushuru wa kiasi hicho? Kwanini tusiweke ushuru wa asilimia 25 au 45 mpaka 50 ili wakati bei duniani ikishuka, basi mtu aweze kufanya biashara hiyo kuweza kuwalisha Watanzania. (Makofi)
Leo katika Tanzania yetu hii, nani anayemtetea mlaji? Hebu niambieni! Sisi tuko wakulima pengine labda milioni mbili, wafanyakazi pengine milioni mbili, lakini watu milioni 40, mfumuko wa bei unawaumiza. Mishahara ambayo kwa kweli iko chini na maisha haya yakipanda kwa kweli hatumtetei haki mlaji huyu, wala hatumlindi. Naomba sana hili litazamwe kwa nguvu zote.
MHE. SALIM HASSAN ABDULLAH TURKY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naunga mkono hoja kwa nguvu zote.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2015, Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. SALIM HASSAN ABDULLAH TURKY: Mheshimiwa Naibu Spika, hamu imenishika, fahamu imeondoka! Nashukuru sana. Mimi nina-declare interest ni mfanyabiashara mwenye viwanda kwa hivyo ninachotaka kuzungumiza ni uchumi wetu wa viwanda. Kwa masikitiko makubwa sana nasimama kwa huzuni kwamba Rais wetu anataka nchi hii iwe ya viwanda lakini nafikiri watu wanaoshauri Wizara hawashauri vizuri, mfano hai wa kwanza ninaotoa ni huu.
Kuna kiwanda kinazalisha pasta (macaroni), tambi, kiwanda hiki kiliomba msamaha wa kodi kwa sababu raw material inayotumia ni unga wa semolina ambao katika East Africa yote haipatikani na walikubaliwa na Serikali wakajenga kiwanda, uzalishaji umeanza miezi miwili iliyopita. Na hapo hapo waliahidi kwamba wataweka na kiwanda cha pili cha kusaga ngano inayotengeneza semolina. Kiwanda hiki kimechelewa kutokana na sababu zisizoweza kuepukika, kwa hivyo wenye viwanda wakaandika barua kuomba kwamba wanaomba waongezewe muda wa semolina kupewa msamaha huo, kilichotokea kwa masikitiko makubwa, kiwanda cha pasta sasa hivi kinazalisha kontena tano kwa siku yaani tani 96 kwa siku.
Mheshimiwa Naibu Spika, kinachojitokeza sasa hivi ni kwamba pasta tayari inazalishwa, kile kiwanda cha kutengeneza unga hakijawa tayari. Wameandika barua kuendeleza msamaha wa mwaka mmoja tena waongezewe, msamaha huo hawajapewa. Sasa matatizo yatakayojiyokeza kwenye kiwanda hiki ni kwamba semolina ndiyo inayotengeneza pasta (macaroni) maana yake mtu anayeagiza macaroni kutoka nje tayari anaweza akauza hicho kiwanda hakina kazi Tanzania, watu 156 wanakosa ajira hivi hivi! Kiwanda kile cha pili kinajengwa ili kusaidia kiwanda kile.
Mheshimiwa Naibu Spika, uwekezaji wa dola milioni 40, Serikali hii kwa uongozi huu uliyopo ndani ya Bunge hili, Waziri wetu wa Fedha jambo hili halioni? Nimemwambia, katia pamba kwenye masikio, halafu tunakuja hapa kujadili viwanda, kweli tunaifanyia haki Tanzania hii? Ninaomba sana Waziri wa Fedha jambo hili ukija utujibu kama kiwanda hiki kifungwe, kwa sababu ulishaniambia Watanzania wanakula muhogo pasta hawali! Uwekezaji huu unakuja kuwalisha pasta watu wote. Hivyo ninaomba sana, dakika zangu tano bado zipo?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Suala lingine ninalotaka kuliongelea ni kwamba Serikali yeyote unapotaka kuja kuwekeza katika nchi ni lazima sheria zako mwenyewe unazojiwekea uziheshimu. Kuna sheria hapa inasema kwaba mtu yeyote anayetaka kuja kuwekeza Tanzania basi aweke kiwanda, kiwanda kitatoa msamaha kwa mtu yeyote ambaye ataleta raw material katika nchi, kwa hiyo, anapewa zero. Mtu ambaye ataleta semi-finished product atapewa asilimia kumi na mtu ambaye ataleta finished product atalipa asilimia 25 ya kodi katika nchi yetu hii.
Sasa kinachojitokeza wawekezaji wameiamini Serikali yao, wamekuja wamewekeza, unakuja unabadilisha unasema sasa raw material tutatoza asilimia kumi na hiki kiwanda ambacho kinatumika kutengenezea raw materials na semi finished products ni viwanda viwili tofauti, uwekezaji wake ni mkubwa mno. Huoni kama unaanza kudumaza maendeleo ya viwanda hivi?
Mheshimiwa Naibu Spika, kauli yako mwenyewe unaanza kutia ulimi puani, kwa hivyo lazima tuheshimu maamuzi yetu. Serikali lazima iwe na kauli ya kuheshimu viwanda na kuendeleza viwanda. Kinachojitokeza sasa hivi mtu anakwambia kwamba mafuta yanayoletwa siyo mafuta ghafi, sasa tunataka Bunge hili watu waje wathibitishe kwamba toka tumeanza Bunge hili watu wangapi wamekamatwa hawajaleta mali ghafi wamedanganya Serikali hii tuletewe orodha yao hapa na wamepewa adhabu gani? Siyo tunakaa kwa kusema tu kwamba hapana, watu wanadangaya mafuta hivi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hiki kinachofanyika sasa ni kifo kwa wananchi wetu wa Tanzania. Mfumuko wa bei sasa hivi kama tunavyojua sukari bei yake ilivyoelekea huko na mafuta haya kwa kodi hii leo nataka muandike kwa kalamu tarehe ya leo na bajeti hii itakapoanza kufanya kazi kwa kutoza asilimia kumi mfumuko wa bei ya mafuta ya kula Watanzania mtapiga kelele humu humu. Naomba sana Wabunge wote tushirikiane, kodi hii tusiikubali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo naomba sitounga mkono hoja hii mpaka nipate majibu ya Waziri. Ahsante sana.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. SALIM HASSAN TURKY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi nashukuru kupata fursa leo ya kuweza kuchangia. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya, sote tu wazima na tupo katika Bunge hili tukijenga Taifa letu. Pia nachukua fursa hii kumpongeza Rais wetu kwa kufanya maamuzi magumu ya kuongoza Taifa hili na kwa kweli anastahili kila sifa kwa nia yake njema ya kutaka kuifanyia Tanzania ya leo iwe ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo sasa nataka niingie kwenye Mpango. Huu Mpango ni mzuri sana lakini kwa kweli heading yake ina matatizo tena ina matatizo makubwa sana. na matatizo yake Mpango unasema ni maendeleo ya Taifa lakini nikitazama tafsiri ya taifa siikuti Taifa bila ya Zanzibar. Katika mpango huu hakuna sehemu hata moja iliyotaja Wazanzibar na kwa kweli Mpango huu kwa njia moja au nyingine umetudhalilisha Wazanzibar kama vile hatustahili kupangiwa chochote katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, kama ni kosa basi nafikiri lirekebishwe kwa kuandikwa kwamba Mpango wa Maendeleo wa Tanzania Bara au uandikwe Mpango wa Taifa basi na Taifa la Zanzibar liwekwe katika Mpango huu lakini zero hakuna chochote. Hakuna mahali ilipoandikwa Pemba, Unguja wala Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hili sijui kama limefanywa kwa makusudi na kama limefanywa kwa makusudi basi naomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha awatazame sana watendaji wake kwa sababu yeye ni msimamizi wa sera pengine hakuwa na time nzuri ya kusoma, lakini kwa kweli hili limetuangusha sana Wazanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme kwamba kuna watendaji wa Serikali ambao kwa kweli hawaitendei haki Zanzibar na hasa katika mambo ya kufanya biashara baina ya Zanzibar na Bara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati zilizopita tulipata bahati ya kutembelea mipaka yetu, tulikwenda mpaka wa Sirari tukaona wafanyabiashara wadogo sana kila mfanyabiashara ana baiskeli ya rally nzuri madhubuti, lakini kazi yake yeye akiamka asubuhi anasukuma baiskeli kupita boarder anakwenda zake Kenya anachukua dumu la mafuta analeta, akimaliza kinachotakiwa Kenya anakichukua kwa baiskeli anaenda zake anapeleka na hakuna anayemuuliza kwa sababu ni mwananchi anayeishi maeneo yale, kwa hivyo, biashara hiyo inafanyika kwa baiskeli lakini unaweza kukuta ikifika jioni basi canter zima mtu kapenyeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi upande wa Zanzibar, leo miaka saba mimi nipo katika Bunge hili, kuna jambo moja dogo sana ambalo linatudumaza sisi Wazanzibar nalo ni lile la longroom pale Dar es Salaam. Wafanyabiashara wanaokuja sasa hivi kama mnavyojua Zanzibar inasifiwa kitalii, tuna utalii wa nje na wa ndani. Hawa watalii wa nje wakija kutembea Zanzibar mtu akinunua chochote Zanzibar akifika longroom pale akionesha risiti anaambiwa hapana tuoneshe na document ya importation ya kitu hiki, hivi kweli tunatendewa haki jamani Wazanzibari na Waziri wa Fedha upo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ninaomba sana lishughulikiwe kama wewe kweli ni muumini wa haki basi hili naomba ulisimamie Wazanzibar wasinyanyaswe pale. Mtu akija na tv moja ni biashara ni sawa sawa na mtu ambaye amenunua Morogoro akaja Dar es Salaam. Sasa leo ninashangaa leo watu wakienda wakinunua kitu kidogo Zanzibar akipita pale inakuwa kesi kubwa sana. Kwa hivyo, hilo ninaomba safari hii angalau tuhakikishe adha hii hii ndogo basi iishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiacha hilo, tunazungumzia uhusiano wa mapato baina ya wananchi kulipa mapato na Serikali kupokea mapato. Lakini TRA ilipoanzishwa kulikuwa na kauli mbiu inatumika kwamba sisi ni partners katika maendeleo ya nchi yetu, sasa hivi tafsiri hiyo inaondoka. TRA sasa hivi wamekuwa ni watu wa bunduki, watu wa kutumia nguvu, wanaingia kila mfanyabiashara anatafirika. Wewe mwenyewe ulitoa tafsiri katika mwaka uliopita ulisema maduka 4,000 yamefungwa, hiyo ni kwa sababu ya ukali wa TRA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mambo yanazungumzika, Serikali hii ilipoingia madarakani, Serikali iliyopita ililegeza mambo mengi sana, ninyi mmeingia mmekaza, mna haki ya kufanya hivyo, hakuna tatizo. Lakini kwa nini mnawaadhibu hawa kwa awamu iliyopita na awamu hiyo wewe Waziri, Rais wetu, sote tulishiriki, tulikuwemo katika Serikali iliyopita. Na sote kama kuna makosa yalitokea basi sisi pia ni wakosa wa Serikali iliyopita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Serikali hii ilishaamua kwamba twende vingine, basi tukubaliane kwamba twende kwa mwendo tunaotakiwa. Sasa tusiambiwe kwa makosa ya Serikali iliyopita, Serikali hii naiheshimu sana na tunataka tufanye kazi kwa pamoja na tuitekelezee kila wanachokitaka, tutakaza miguu tutafuata. Sisi private sector tunaamini kabisa mpango wa Rais wetu Dkt. Magufuli wa kutaka kuendeleza viwanda ni mzuri sana na utafuzu kwa nguvu zote, na yeye ana nia njema kabisa, lakini watendaji wetu wanatuangusha. Naomba Mheshimiwa Waziri hili ulisimamie kwa nguvu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nalo ni muhimu, wakati wa awamu zote zilizopita, biashara baina ya Bara na Visiwani, sisi Visiwani tunaitegemea Bara kwa asilimia 90 kwa maisha yetu ya kila siku Zanzibar. Unachosema wewe sisi tunanunua Bara ndiyo tunapeleka Zanzibar. Lakini awamu zote zilizopita kulikuwa na ulegevu fulani pale bandarini Wazanzibari waweze kuleta bidhaa zao ziuzike, sasa hivi awamu hii imetu-tag sisi Wazanzibari ni wezi, hatutaki kufanyiwa biashara, biashara yetu ni kuiba tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kutokana na fursa ambazo tulikuwa tukipewa na awamu zilizopita, naiomba awamu hii kwa sababu wamekaza kamba sasa wakubaliane na hii hoja ambayo naiomba kwako wewe Waziri kwa kupitia Mwenyekiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba mazingira ya kufanya biashara Zanzibar na Bara ni mawili tofauti kabisa katika East Africa nzima. Sisi leo kama tutaagiza mzigo kutoka nje, tukauleta Zanzibar, basi tutalipa kodi pale, tutaushusha mzigo Zanzibar, utaenda zake godown, atakuja mteja ataununua mzigo ule utapakiwa tena kutoka godown utakuja bandarini utapakiwa katika vyombo utakuja Bara, utapakuliwa, utakaguliwa, halafu upakuliwe tena ndiyo ufike sokoni, angalia safari zako hizi zote zilizopita, ni gharama mno kwa kufanya biashara Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Zanzibar kama tunavyojua, miaka yote nenda rudi ndicho kituo cha kufanya biashara na sisi sote nguvu zetu tuko katika kuendeleza Zanzibar iwe kituo cha biashara. Na hili nataka niombe sana Serikali yetu, tusione kwamba Wazanzibari ni wakorofi, tuone ni ndugu zetu ambao tunataka tushikamane nao, leo uchumi wa Zanzibar ukikua ndiyo uchumi wa Bara unakua. Haiwezekani uchumi wa Zanzibar ukawa mzuri wa Bara ukawa chini. Bado BOT ndiyo regulator wetu, haiwezekani uchumi ukawa wa upande mmoja na wa upande mwingine usiwe, uchumi wetu utakuwa chini tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kutokana na hilo, naomba sana hizi tozo za TRA kwa maana ya duty, sales tax na nini zilizoko katika Muungano wetu, kwa Zanzibar tufikiriwe angalau tushushiwe. Kwa Zanzibar, kama Dar es Salaam ni 25 percent, basi Zanzibar iwe 25 percent lakini database ile ile ikubalike. Mtu akishalipa kodi pale basi sawa iwe mzigo ule kutoka Zanzibar kuja Bara iwe ni rahisi wala hakuna matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hivi tunavyofanyiana ni sawasawa na mfanyabiashara mkubwa kumuua mdogo. Uchumi wa Zanzibar huwezi ukaulinganisha na uchumi wa Bara. Kwa maana hiyo, mtazame kwamba katika kutekeleza ni kwamba lazima kila mtu alipe kodi kwa uhakika wake na uhalali wake. Basi sasa tuangalie kodi zetu nazo ziwe rafiki kwa pande zote mbili. Hiyo inakuwa ni double taxation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo naomba sana Wizara ya Fedha ilitazame ni kwamba awamu iliyopita ukienda TRA kodi watu walikuwa wakilipa basi mara nyingi sana ni ile kodi ya chini kabisa mtu ndiyo bei anayotiliwa analipa, ukiingia sokoni bidhaa zinauzika, au analipa kodi bei ambayo hata katika database haipo, lakini inapitishwa watu wanalipa.

Awamu hii Ma Sha Allah imekuja vizuri sana mna- collect kodi vizuri sana, lakini kilichotokea, watu badala ya kutazama database bei za chini au za kati, wamekwenda kuzivamia za juu kabisa. Kilichotokea ni mfumuko wa bei kwa Tanzania nzima, vitu vyetu sisi vimekuwa ghali. Na kama unajua soko la Kariakoo ndiyo centre ya kulisha; Burundi, Rwanda na Kongo wote wananunua Kariakoo, bidhaa nyingi sana pale. Na ninaamini karibu asilimia 30 mpaka 40 ya kodi inatokana na Kariakoo. Lakini leo maduka yale yote yamekufa kwa sababu ya kodi kutozwa namna hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kwa Seriikali yangu ni kwamba hizi tozo tusitafute hiyo njia ya panya isiwepo, lakini hizi kodi angalau zitazame pale database bei ya chini. Kitakachofanya sasa hivi biashara hizi zinakuwa tena kwa nguvu sana, lakini sio Tanzania, watu wanakwenda kununua Kenya, soko hili la Rwanda, Burundi, Kongo, sasa hivi mambo yote watu wanakwenda kununua Mombasa, Nairobi, ndipo inapofanyika biashara hii. Tulioumia ni sisi Watanzania, biashara imeanguka kwetu, kwa hiyo hili nalo litazamwe.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. SALIM HASSAN TURKY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi nashukuru kupata fursa leo ya kuweza kuchangia. Awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya, sote tu wazima na tupo katika Bunge hili tukijenga Taifa letu. Pia nachukua fursa hii kumpongeza Rais wetu kwa kufanya maamuzi magumu ya kuongoza Taifa hili na kwa kweli anastahili kila sifa kwa nia yake njema ya kutaka kuifanyia Tanzania ya leo iwe ya viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo sasa nataka niingie kwenye Mpango. Huu Mpango ni mzuri sana lakini kwa kweli heading yake ina matatizo tena ina matatizo makubwa sana. na matatizo yake Mpango unasema ni maendeleo ya Taifa lakini nikitazama tafsiri ya taifa siikuti Taifa bila ya Zanzibar. Katika mpango huu hakuna sehemu hata moja iliyotaja Wazanzibar na kwa kweli Mpango huu kwa njia moja au nyingine umetudhalilisha Wazanzibar kama vile hatustahili kupangiwa chochote katika Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, kama ni kosa basi nafikiri lirekebishwe kwa kuandikwa kwamba Mpango wa Maendeleo wa Tanzania Bara au uandikwe Mpango wa Taifa basi na Taifa la Zanzibar liwekwe katika Mpango huu lakini zero hakuna chochote. Hakuna mahali ilipoandikwa Pemba, Unguja wala Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hili sijui kama limefanywa kwa makusudi na kama limefanywa kwa makusudi basi naomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha awatazame sana watendaji wake kwa sababu yeye ni msimamizi wa sera pengine hakuwa na time nzuri ya kusoma, lakini kwa kweli hili limetuangusha sana Wazanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme kwamba kuna watendaji wa Serikali ambao kwa kweli hawaitendei haki Zanzibar na hasa katika mambo ya kufanya biashara baina ya Zanzibar na Bara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati zilizopita tulipata bahati ya kutembelea mipaka yetu, tulikwenda mpaka wa Sirari tukaona wafanyabiashara wadogo sana kila mfanyabiashara ana baiskeli ya rally nzuri madhubuti, lakini kazi yake yeye akiamka asubuhi anasukuma baiskeli kupita boarder anakwenda zake Kenya anachukua dumu la mafuta analeta, akimaliza kinachotakiwa Kenya anakichukua kwa baiskeli anaenda zake anapeleka na hakuna anayemuuliza kwa sababu ni mwananchi anayeishi maeneo yale, kwa hivyo, biashara hiyo inafanyika kwa baiskeli lakini unaweza kukuta ikifika jioni basi canter zima mtu kapenyeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi upande wa Zanzibar, leo miaka saba mimi nipo katika Bunge hili, kuna jambo moja dogo sana ambalo linatudumaza sisi Wazanzibar nalo ni lile la longroom pale Dar es Salaam. Wafanyabiashara wanaokuja sasa hivi kama mnavyojua Zanzibar inasifiwa kitalii, tuna utalii wa nje na wa ndani. Hawa watalii wa nje wakija kutembea Zanzibar mtu akinunua chochote Zanzibar akifika longroom pale akionesha risiti anaambiwa hapana tuoneshe na document ya importation ya kitu hiki, hivi kweli tunatendewa haki jamani Wazanzibari na Waziri wa Fedha upo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ninaomba sana lishughulikiwe kama wewe kweli ni muumini wa haki basi hili naomba ulisimamie Wazanzibar wasinyanyaswe pale. Mtu akija na tv moja ni biashara ni sawa sawa na mtu ambaye amenunua Morogoro akaja Dar es Salaam. Sasa leo ninashangaa leo watu wakienda wakinunua kitu kidogo Zanzibar akipita pale inakuwa kesi kubwa sana. Kwa hivyo, hilo ninaomba safari hii angalau tuhakikishe adha hii hii ndogo basi iishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukiacha hilo, tunazungumzia uhusiano wa mapato baina ya wananchi kulipa mapato na Serikali kupokea mapato. Lakini TRA ilipoanzishwa kulikuwa na kauli mbiu inatumika kwamba sisi ni partners katika maendeleo ya nchi yetu, sasa hivi tafsiri hiyo inaondoka. TRA sasa hivi wamekuwa ni watu wa bunduki, watu wa kutumia nguvu, wanaingia kila mfanyabiashara anatafirika. Wewe mwenyewe ulitoa tafsiri katika mwaka uliopita ulisema maduka 4,000 yamefungwa, hiyo ni kwa sababu ya ukali wa TRA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mambo yanazungumzika, Serikali hii ilipoingia madarakani, Serikali iliyopita ililegeza mambo mengi sana, ninyi mmeingia mmekaza, mna haki ya kufanya hivyo, hakuna tatizo. Lakini kwa nini mnawaadhibu hawa kwa awamu iliyopita na awamu hiyo wewe Waziri, Rais wetu, sote tulishiriki, tulikuwemo katika Serikali iliyopita. Na sote kama kuna makosa yalitokea basi sisi pia ni wakosa wa Serikali iliyopita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Serikali hii ilishaamua kwamba twende vingine, basi tukubaliane kwamba twende kwa mwendo tunaotakiwa. Sasa tusiambiwe kwa makosa ya Serikali iliyopita, Serikali hii naiheshimu sana na tunataka tufanye kazi kwa pamoja na tuitekelezee kila wanachokitaka, tutakaza miguu tutafuata. Sisi private sector tunaamini kabisa mpango wa Rais wetu Dkt. Magufuli wa kutaka kuendeleza viwanda ni mzuri sana na utafuzu kwa nguvu zote, na yeye ana nia njema kabisa, lakini watendaji wetu wanatuangusha. Naomba Mheshimiwa Waziri hili ulisimamie kwa nguvu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo nalo ni muhimu, wakati wa awamu zote zilizopita, biashara baina ya Bara na Visiwani, sisi Visiwani tunaitegemea Bara kwa asilimia 90 kwa maisha yetu ya kila siku Zanzibar. Unachosema wewe sisi tunanunua Bara ndiyo tunapeleka Zanzibar. Lakini awamu zote zilizopita kulikuwa na ulegevu fulani pale bandarini Wazanzibari waweze kuleta bidhaa zao ziuzike, sasa hivi awamu hii imetu-tag sisi Wazanzibari ni wezi, hatutaki kufanyiwa biashara, biashara yetu ni kuiba tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kutokana na fursa ambazo tulikuwa tukipewa na awamu zilizopita, naiomba awamu hii kwa sababu wamekaza kamba sasa wakubaliane na hii hoja ambayo naiomba kwako wewe Waziri kwa kupitia Mwenyekiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba mazingira ya kufanya biashara Zanzibar na Bara ni mawili tofauti kabisa katika East Africa nzima. Sisi leo kama tutaagiza mzigo kutoka nje, tukauleta Zanzibar, basi tutalipa kodi pale, tutaushusha mzigo Zanzibar, utaenda zake godown, atakuja mteja ataununua mzigo ule utapakiwa tena kutoka godown utakuja bandarini utapakiwa katika vyombo utakuja Bara, utapakuliwa, utakaguliwa, halafu upakuliwe tena ndiyo ufike sokoni, angalia safari zako hizi zote zilizopita, ni gharama mno kwa kufanya biashara Zanzibar.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Zanzibar kama tunavyojua, miaka yote nenda rudi ndicho kituo cha kufanya biashara na sisi sote nguvu zetu tuko katika kuendeleza Zanzibar iwe kituo cha biashara. Na hili nataka niombe sana Serikali yetu, tusione kwamba Wazanzibari ni wakorofi, tuone ni ndugu zetu ambao tunataka tushikamane nao, leo uchumi wa Zanzibar ukikua ndiyo uchumi wa Bara unakua. Haiwezekani uchumi wa Zanzibar ukawa mzuri wa Bara ukawa chini. Bado BOT ndiyo regulator wetu, haiwezekani uchumi ukawa wa upande mmoja na wa upande mwingine usiwe, uchumi wetu utakuwa chini tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kutokana na hilo, naomba sana hizi tozo za TRA kwa maana ya duty, sales tax na nini zilizoko katika Muungano wetu, kwa Zanzibar tufikiriwe angalau tushushiwe. Kwa Zanzibar, kama Dar es Salaam ni 25 percent, basi Zanzibar iwe 25 percent lakini database ile ile ikubalike. Mtu akishalipa kodi pale basi sawa iwe mzigo ule kutoka Zanzibar kuja Bara iwe ni rahisi wala hakuna matatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hivi tunavyofanyiana ni sawasawa na mfanyabiashara mkubwa kumuua mdogo. Uchumi wa Zanzibar huwezi ukaulinganisha na uchumi wa Bara. Kwa maana hiyo, mtazame kwamba katika kutekeleza ni kwamba lazima kila mtu alipe kodi kwa uhakika wake na uhalali wake. Basi sasa tuangalie kodi zetu nazo ziwe rafiki kwa pande zote mbili. Hiyo inakuwa ni double taxation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo naomba sana Wizara ya Fedha ilitazame ni kwamba awamu iliyopita ukienda TRA kodi watu walikuwa wakilipa basi mara nyingi sana ni ile kodi ya chini kabisa mtu ndiyo bei anayotiliwa analipa, ukiingia sokoni bidhaa zinauzika, au analipa kodi bei ambayo hata katika database haipo, lakini inapitishwa watu wanalipa.

Awamu hii Ma Sha Allah imekuja vizuri sana mna- collect kodi vizuri sana, lakini kilichotokea, watu badala ya kutazama database bei za chini au za kati, wamekwenda kuzivamia za juu kabisa. Kilichotokea ni mfumuko wa bei kwa Tanzania nzima, vitu vyetu sisi vimekuwa ghali. Na kama unajua soko la Kariakoo ndiyo centre ya kulisha; Burundi, Rwanda na Kongo wote wananunua Kariakoo, bidhaa nyingi sana pale. Na ninaamini karibu asilimia 30 mpaka 40 ya kodi inatokana na Kariakoo. Lakini leo maduka yale yote yamekufa kwa sababu ya kodi kutozwa namna hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kwa Seriikali yangu ni kwamba hizi tozo tusitafute hiyo njia ya panya isiwepo, lakini hizi kodi angalau zitazame pale database bei ya chini. Kitakachofanya sasa hivi biashara hizi zinakuwa tena kwa nguvu sana, lakini sio Tanzania, watu wanakwenda kununua Kenya, soko hili la Rwanda, Burundi, Kongo, sasa hivi mambo yote watu wanakwenda kununua Mombasa, Nairobi, ndipo inapofanyika biashara hii. Tulioumia ni sisi Watanzania, biashara imeanguka kwetu, kwa hiyo hili nalo litazamwe.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. SALIM HASSAN TURKY: Mheshimiwa Spika,ahsante sana. Kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Rais wetu hasa kwa kufikiria vitu vikubwa na katika vitu hivyo, hivi viwili ni vya kiuchumi kabisa na leo hapa mimi na Mheshimiwa Bashe tunakaa pamoja lakini fikra zetu tofauti kabisa. Mimi nasema uchumi wetu tunatoka kwenye reli na kwenye ndege, tujipangeni; tunajipanga namna gani? Naomba sana, pesa ziko nje nje kwa kuendesha reli hii na ndege. Naomba Serikali itazame namna ya ku-float bonds katika national na international market. Tukitoa share hizi tukaziweka katika stock exchange yetu, tayari watu watanunua shares na shares hizi ndiyo pesa unazipata haraka haraka. Tena hili litakuwa na nguvu zaidi hata kesho Mheshimiwa Rais akimaliza muda wake maana yake sasa tunaingia partnership ya private na Government, tupo pamoja sasa. Kwa hivyo, hata ile management kesho itasimamiwa vizuri sana, mambo haya makubwa hayatofeli maisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo, naomba sana hili tulipokee kwa nguvu zote Mheshimiwa Waziri alifanyie kazi. Halafu reli ni moja ambayo haina hata mshindani, Government peke yake, ni monopoly yao, hakuna mtu anayeweza akajenga reli. Kwa hivyo, hii naamini akisema kesho tu atawapata shareholders sisi wengine wote humu tutanunua shares na watu wa nje wengine watakuja watajiunga pesa nje nje, hilo tumemaliza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili; nashukuru sana bandari inafanya kazi vizuri sana hasa ninavyozungumza Bandari ya Dar es Salaam pale, lakini kuna kitu ambacho kinatakiwa kiboreshwe, nacho ni mizigo inayotoka Zanzibar. Baina ya Bara na Zanzibar ni biashara ya tangu mababu na mababu, japo siku hizi imepewa majina ya ajabu ajabu lakini huwezi ukaamini ukweli kwamba Zanzibar ni kisiwa cha biashara na biashara hii itadumu sisi kama tupo hata tukiondoka naamini biashara hii itaendelea.

Mheshimiwa Spika, pale Dar es Salaam sasa hivi kuna congestion kubwa sana sana ya mizigo ya Zanzibar, nashukuru kwamba tumetoa ushauri kwa bandari kulikuwa na banda lilijengwa ukuta, namshukuru sana pale Port Director tumempa ushauri na ameufanyia kazi mara moja na jana nimepigiwa simu kwamba upo ukuta wa bati pale wa kuweka magari ya godauni umeshaondoshwa na watu wanashusha mizigo yao. Hata hivyo, bado kuna ukiritimba mmoja mkubwa sana ambao unafanyika; nao ni kwamba kuna ZFA, TBS na TRA wanagongana pale, mizigo haitoki ndani ya warehouse. Naomba hili lisimamiwe kwa nguvu sana chini ya bandari yake kwa sababu hawa wote hawana ofisi isipokuwa yeye mwenye bandari ndiyo anawakaribisha mle. Kwa hivyo, wakubwa wa bandari waangalie hilo na walisimamie kwa nguvu zote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la tatu; Mheshimiwa Rais wetu anataka nchi hii ikue kiuchumi, mimi nashangaa sana mnapokuja na mawazo ya kudumaza uchumi kwa kusema mtu mmoja awe na line moja ya simu au line mbili za simu, akitaka ya pili apate kibali; vitu hivi vya ajabu vinatoka wapi jamani? Huu uchumi leo sisi tunao mobile operators karibu watano kwa sita, kila mmoja anataka aingie sokoni; hapa kuna ajenda gani? Tunataka kumpandisha mtu mmoja, kama ilikuwa wana nia kila mtu awe na simu moja, basi hawa operators ilikuwa tuwanyime leseni hizo. Leo kila mmoja anataka soko, kwa nini anatubana tusiwe na simu? Leo mimi nataka simu ya jimboni kwangu na ya ofisini kwangu; hizi ni simu lazima kila mmoja apewe uhuru wake, huwezi ukanibania mimi ooh uwe na laini moja, kwa nini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa hivi uchumi huu unatakiwa ukue kwa kasi, huwezi ukabana hizi simu; simu nyingine mimi napokea simu za nje tu, sasa leo unaniambia aah usiwe. Hiyo nazungumza mimi kama Mbunge lakini kuna wafanyabiashara nje, wakulima na watu wote wanataka simu. Naomba hii sera ya kusema kwamba mtu mmoja laini moja, akitaka laini ya pili special pass sijui iende wapi, hiyo kitu inadumaza uchumi wa nchi hii. Naamini Rais akilisikia hili, hawezi akalikubali hata siku moja, tutakuja kuumbuliwa hapa bora tujiumbueni wenyewe, tujiwekeni sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya haya, sina la zaidi ila naipongeza sana Wizara na naunga mkono hoja na pia maendeleo yote yanatofanyika katika nchi hii nayapongeza kwa nguvu sana na naamini 2020 CCM itatisha sana. Ahsanteni sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Viwanda na Biashara
MHE. SALIM HASSAN ABDULLAH TURKY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Napenda niendelee kuwapongeza waumini wote wa Kiislam kwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Ramadhani zao ziwe njema, tufunge kwa raha mustarehe na wale wanaotusindikiza, tushirikiane vizuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kuchangia, nataka ni-declare interest mimi ni mfanyabishara mwenye viwanda. Napenda ku-declare interest kwa sababu hata kule Jimboni kwangu nilipogombania watu walinipa kura nyingi sana kwa sababu waliamini ni mfanyabiashara na mwenye viwanda. Kwa hivyo, leo nikisimama hapa naomba sana watu wasinitafsiri kwamba natetea viwanda vyangu, natetea viwanda vya Tanzania kwa ujumla wake. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme katika kukubali kauli ya Mheshimiwa Rais wetu, kampuni zetu sisi tumewekeza baada ya kuona Mheshimiwa Rais yupo tayari kupokea viwanda. Hivi sasa tumejenga kiwanda kikubwa sana East Africa nzima kiwanda cha kukoboa mpunga ambacho kiko Morogoro, kinakoboa tani 280 kwa siku na watu wa Morogoro wapo watakuwa mashahidi na baada ya miaka miwili kiwanda hicho kitakuwa kinakoboa tani 560. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama hilo halitoshi, Mheshimiwa Rais alikuwa anatuhimiza sana kiwanda cha dripu, nacho kiko tayari tukijaliwa mwezi Oktoba tutamwalika rasmi aje akifungue. Kama hilo halitoshi, hapa Dodoma tunawekeza kiwanda kikubwa kabisa cha sunflower kwa Afrika hii na tumepata hekari 90 Zuzu, tunategemea mwanzo wa mwaka ujenzi utaanza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini baada ya kumuamini Mheshimiwa Rais katika viwanda tunapata changamoto kubwa sana ambapo tunaamini kwamba kuna watu wanadumaza maendeleo ya viwanda vyetu. Kuna mfano halisi, sasa hivi kuna mafuta yako bandarini ya kampuni karibu tatu au nne ikiwemo na ya Burundi, mafuta haya yalipofika nchini na kawaida ya nchi yetu mafuta yakifika bandarini yanakaguliwa na TBS, TBS walipoyakagua walisema mafuta haya ni crude, tena mabaya sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, wafanyabiashara wale walipopeleka documents zao TRA, la kushangaza sana Kamishna anazungumza pale kwamba mafuta haya ni mabaya tunayataifisha. Neno taifisha sasa hivi katika juhudi za Mheshimiwa Rais wetu jamani linatoka wapi, litatutisha wafanyabiashara. Ikiwa mfanyabiashara mwenye kiwanda mafuta yake yanataifishwa Wamachinga mitaani wanaopiga kelele wana hali gani? Wanapopiga kelele kwamba TRA wanawasumbua, hili lina ukweli wake. Kwa hiyo, naomba Wizara husika waangalie suala hili wanali-control vipi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mafuta haya baada ya yeye kuyakataa yasitoke association ya wenye viwanda wakapeleka maombi Ofisi ya Waziri Mkuu, Waziri Mkuu kwa utaratibu wao wenyewe wakapeleka mafuta haya yakachunguzwe na Mkemia Mkuu. Mkemia Mkuu amesema mafuta haya ni crude. Sasa wametoka watu wameenda tena TRA, Kamishna anasema mafuta haya siyo crude ni semi- finished. Yale mafuta ambayo yalikuwa yanasemwa hayafai kuliwa na binadamu, watakufa, hayawezi yakaingia nchini, sasa anasema ni mazuri yaliwe na watu hawa, hapo ndipo tulipofika sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kumkamata hapo akadai sasa vifaa ambavyo anataka uwe navyo mafuta yakingia nchini. Anakudai wewe export originally document na documents zote originally zinatokea nchi ile. Sisi wanunuzi hata wasafirishaji wa korosho wa nchi hii, unapotengeneza export certificate hiyo ni mali ya exporter siyo ya importer, sisi tunazoletewa ni copy. Hiyo sheria alianza mwaka jana copy zilikuwa zinakubaliwa lakini kwa mzigo huu sasa anakwambia lete original, tunazitoa wapi huu mwezi wa saba?

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niwaambieni hili jambo sisi wenye viwanda vya mafuta bahati nzuri asilimia 90 ni Watanzania wazalendo, tunatokaje hapa? Hizi documents anazozidai kwa kweli hatuwezi tukazipata hata siku moja kwa sababu ni mali yao na sisi hapa tayari tumeshaleta copy certified ambazo ndizo zilikuwa zikitolea mzigo miaka yote hiyo, leo unaambiwa ulete originally tunatoa wapi originally? Kwa hiyo, mkae mkijua hili jambo linadumaza maendeleo ya viwanda vyetu. Leo viwanda vitano vya refinery vimefungwa, watu 280 wamekosa ajira kwa sababu …

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021
MHE. SALIM HASSAN TURKY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Sina budi kumshukuru Mwenyezi Mungu Subhana wa Taallah kwa kutujalia sisi tulioko humu wazima wa afya. Nachukua fursa hii kumpongeza sana Waziri wetu wa Mipango kwa kweli mpango aliouleta ni mzuri sana na madhubuti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuendelea na safari hii pia nataka nimpongeze sana Mwenyekiti wetu wa Chama cha Mapinduzi ambaye ndiyo Rais wa nchi hii, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayotufanyia ya kutaka kuhakikisha kwamba Tanzania tunaingia katika uchumi wa kati. Sitaki kutafuna maneno, wakati Mheshimiwa Rais anaingia madarakani na alipotoa matamko yake yale kwa kweli nilipigwa na butwaa nikasema hivi kweli mambo haya yanawezekana kwa kipindi hiki kifupi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ameweza kuthibitisha na mimi nachukua fursa hii kumpigia salute kabisa kwamba, kwa kweli anatupeleka kwenye maendeleo makubwa sana japo njia ni ngumu lakini dalili njema zimeshaanza kuonekana. Katika hilo wakati akiwa kama Waziri alikuwa akipiga kelele sana hapa kutaka madaraja yale ya ubungo pamoja na airport lakini nashukuru alipoingia madarakani tu alihakikisha daraja lile la pale njia ya airport TAZARA linasimama la Mfugale mara moja na limesimama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli kwa sisi ambao tunatoka Zanzibar kuja Dar es Salaam na Dar es Salaam Zanzibar, kwa kweli njia sasa hivi imekuwa ni ya muda mfupi sana. Kwa hiyo, hizi nia ambazo amezipanga, Mwenyezi Mungu azibariki na amjalie afya njema. Kwa wale wanaomtakia mabaya Mwenyezi Mungu amwepushe nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na-declare interest kwamba ni mfanyabiashara pamoja na viwanda, kwa hiyo, mada ambazo nitaongelea ni hizo na nitaanza na viwanda. Juzi moja tulirushiwa clip nzuri sana ya viwanda kutoka Ethiopia. Kwa kweli ukitaka kujifundisha jambo lolote, tushindane kwa mazuri. Katika Afrika yetu hii, Ethiopia ndiyo inaonekana kwamba ni nchi moja iliyojizatiti kweli kweli kutokana na umasikini na kuendelea mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, walichokifanya wao kama Serikali, wametafuta wawekezaji wakaingia nao ubia, wakajenga eneo kubwa sana la viwanda. Wamejenga eneo hilo na kuwakaribisha wawekezaji. Kwa hiyo, mwekezaji anapokuja nchini, hahangaiki tena kwenda kutafuta maeneo ya kuwekeza, kuanza kutafuta umeme na maji. Hayo yote yamepitwa na wakati katika dunia hii tunayokwenda nayo. Kwa hiyo, inatakiwa katika eneo hilo sasa hivi Serikali na labda Mheshimiwa Waziri wa Fedha akija katika mipango yake atueleze kwamba amejipanga vipi? Kwa sababu eneo hilo linafanya kazi vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba hata katika kurejesha pesa kwake kwa mradi ule, wao watazame zaidi kwamba ile miradi inapokuja nchini, wananchi wetu wapate ajira. Kwa mfano tu leo, Tanzania tuko nyuma sana katika viwanda vya nguo. Tuna pamba ambapo leo Mheshimiwa Waziri ametoa tamko hapa nimemsikia kwamba pamba inayotakiwa kwa viwanda vyetu ni nyingi kuliko tunayozalisha. Kwa hiyo, tayari zile kelele za watu wa maziwa kule kupiga kelele hilo jambo naona limeshapata ufumbuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ili tutoke hapa, tunafanyaje? Nakumbuka Mheshimiwa Waziri Mwijage alipokuwa hapa alisema kwamba anataka kila mtu awe anazalisha na kushona nguo. Vita vikubwa vya kushona nguo Tanzania ni kuruhusu mtumba. Mitumba inadumaza viwanda vya nguo. Kama hatutajipanga vizuri, naamini kwamba kuna nguo ambazo tunanunua China zinauzwa rahisi sana. Je, zikishonwa na pamba yetu wenyewe hapa Tanzania bila kusafirishwa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kuna haja ya makusudi kujipanga kuhakikisha kwamba hilo eneo la viwanda linasimamiwa kwa nguvu zote na ile kodi ikawekwa ndogo sana ili wananchi waweze kunufaika na ajira na mapato ya Serikali yatakuwa makubwa sana kwa kupitia huduma mbalimbali katika eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, mwanzo wa kipindi hiki cha tano tulikuwa tunasimama hapa Bungeni na kupiga kelele, nami wakati ule nilikuwa niko katika Kamati ya Viwanda na Biashara, tulifanya ziara bandarini na tukasema kwamba sasa hivi watu wote wamekimbia bandari yetu kutokana na tozo zilizopangwa kwa wakati ule; mambo ya VAT na nini yaliyowekwa pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana ziara ile ilizaa matunda; Waziri na Serikali ambayo ni sikivu waliona upungufu wakajirekebisha. Sasa hivi naweza kusema kwamba Bandari ya Dar es Salaam imechangamka mia kwa mia. Nampongeza sana Mkurugenzi Mtendaji wa TPA kwa kazi kubwa anayofanya pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli mwaka ule wa kwanza watu waliyachukua magari yale ya kusafirisha makontena wakapeleka nchi jirani. Hivi ninavyoongea na Bunge hili, kuna upungufu mkubwa sana wa magari ya kusafirisha container katika Bandari yetu ya Dar es Salaam, kwamba biashara imekubali Bandari ya Dar es Salaam. Naipongeza sana Serikali yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili biashara hiyo iwe nzuri zaidi, Serikali imejipanga kwa kujenga bandari kavu mbalimbali. Serikali hiyo hiyo ilitoa tamko kwamba zile ICD za watu binafsi zote ambazo ziko katika mji wetu wa Dar es Salaam zihame ziende katika umbali wa kilometa 35 nje ya Dar es Salaam ili kuondoa msongamano wa magari. Hilo ni jambo jema sana ambalo limepangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta binafsi iko tayari kujenga ICD mbalimbali nje ya Dar es Salaam. Serikali inapanga bandari kavu sehemu mbalimbali, ni jambo jema sana, lakini naomba sana TPA, hao watu wanaotaka kujenga ICD nje ya Dar es Salaam, walipoenda kuwaomba kwamba waweke wakaambiwa kwamba tutawapa ruhusa ya miaka miwili, baada ya hapo, kama Serikali ikiwa imeshajipanga, basi itakuwa wamefeli wao. Hilo jambo limewatisha private sector.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ajili hiyo, naiomba sana Serikali yangu itazame uwezekano kwa sababu sasa hivi tunachoongelea hapa kwamba Bandari ya Dar es Salaam inazidi kujengwa na ninaamini muda siyo mrefu nchi jirani zote mizigo yao itakuwa ikipitishiwa hapa na hasa reli itakapoanza. Kwa hiyo, makontena yatakuwa ni mengi mno. Nafikiri Serikali haina haja ya kuwa na hofu na private sector, hawa ni partners wetu, twende nao sambamba watatusaidia kama wanavyotusaidia sasa hivi. Sasa hivi mizigo tena imejaa katika ICD za private kwa sababu mzigo umeshakuwa mwingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, bora Serikali ikatoa tamko kuhakikisha kwamba tunapanga mipango mizuri ya kwenda pamoja. Tusitanguliane private na Government Sector ni partners, tutembee pamoja tutashinda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natokea Zanzibar na siku zote napendelea sana Zanzibar na Bara tuwe ndugu wa kupendana na kushirikiana na tusiwe washindni. Ila tunapoingia katika uchumi, tunaona kuna ushindani mkubwa sana. Ushindani gani?

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Turky, muda wako umekwisha. Kengele ya pili imeshagonga. Ahsante sana. (Makofi)