Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Khamis Ali Vuai (1 total)

MHE. ALI VUAI KHAMIS aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Polisi Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ali Vuai Khamis, Mbunge wa Mkwajuni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika eneo la Matemwe lenye Shehia sita hakuna sehemu iliyotengwa kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi. Hivyo napenda kutumia fursa hii kumshauri Mheshimiwa Mbunge, aishirikishe Halmashauri ya Wilaya ya Kaskazini A ili itenge eneo kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi pamoja na nyumba za makazi ya askari katika eneo la Matemwe ili Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi itenge fedha kwenye bajeti kwa ajili ya ujenzi huo, ahsante.