Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Rev. Peter Simon Msigwa (45 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2012, Mheshimiwa Mnyika alisimama hapa Bungeni akasema tumefika hapa tulipo kwa sababu ya udhaifu wa Bunge. Akasema tumefika hapa tulipo kwa sababu ya udhaifu wa CCM na tumefika hapa tulipo kwa sababu ya udhaifu wa Rais
Kikwete, mlimzomea, mkachukua Polisi mkamtoa. Leo wale wateule wa JK toka Magufuli ameingia amewaporomosha zaidi ya 30. Leo mnapiga makofi mnasema majibu yanatumbuliwa lakini miaka mitano iliyopita tulizungumza mambo ya safari za JK, mlitetea humu ndani na mkapiga makofi. Miaka mitano iliyopita tulizungumza sherehe, kofia, miavuli isiyo na tija mlipiga makofi, leo wengine mnajitoa ufahamu mnasema majipu yanatumbuliwa.
(Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunapozungumza hotuba ya Mheshimiwa Rais hii nchi ni ya wote. Mheshimiwa Rais tumempa kazi na Bunge hili lina wajibu wa kumsimamia, Tanzania ni yetu sote. Kwa hiyo, hatujaja hapa kumpambapamba, ana kazi anayotakiwa kuifanya kwa
Watanzania. Nikisema simuungi mkono katika mambo mengine anayofanya nitakuwa mwongo na nitakuwa mnafiki. Sisi kama Wabunge tunawajibu wa kutimiza wajibu wetu wa kuisimamia Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge lililopita lilikubali kutokuwa na meno na Mnyika alisema mkamzomea akatoka nje, tunataka turudie makosa yale yale ya kuwa na Bunge butu.
Wananchi wametutuma tuisimamie Serikali pamoja na kumwambia ukweli Mheshimiwa Magufuli. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Magufuli anasema anataka kubana matumizi, jambo ambalo ni zuri na Mbunge yeyote mwenye akili ataunga mkono. Hata hivyo, matumizi anayoyabana tumezungumza sana hapa, kuna idadi kubwa ya Wakuu wa Wilaya wanaendesha mashangingi hawana tija katika nchi hii akitaka kupunguza matumizi awatoe hao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, unamkuta Mkuu wa Wilaya naye ana chumba cha mikutano, kikao kikubwa anachoweza kufanya ni cha kuwa na wale walinzi na kazi yao ni kudhibiti mikutano ya CHADEMA. Hiyo kazi anaweza akafanya OCD, hatuhitaji Mkuu wa Wilaya. Wala Mkuu wa Mkoa hatumhitaji, kama ni kupunguza matumizi tumtoe huko. Kazi za Wakuu wa Wilaya wameishia kuomba hela kwa Wakurugenzi, abishe mtu kama haombi hela kwa Wakurugenzi hapa. Haya ndiyo mambo tunatakiwa tujadili kama tunataka tuisaidie Serikali ipunguze matumizi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunazungumzia masuala ya utawala bora, Mheshimiwa Mbarawa, wewe ni Mzanzibar na wenzako ambao hamjaapishwa, mnaondoka Zanzibar mnakuja kutaka kupiga kura Dar es Salaam, kuna utawala bora hapo? Hayo ndiyo majibu
mnatakiwa mumwambie Magufuli ayatumbue na muanze kutumbuliwa wenyewe. (Makofi)
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nina kaka yangu Maige kutoka Iringa, mwanadiplomasia, ameshiriki kwenye vikao vingi vya kutatua migogoro duniani hapa na yeye anaondoka mwanadiplomasia, Waziri wa Nchi za Nje, hajaapishwa anaenda kutaka
kupiga kura Kinondoni, huo ndiyo utawala bora? (Makofi/Kicheko)
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, hii ni hypocrisy of the highest order. Kama Rais anataka utawala bora haya ndiyo mambo tunatakiwa tujadili ili Taifa tuliweke katika misingi bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi kesho Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Nje kama ingemwagika damu Dar es Salaam angekwenda Rwanda kusuluhisha migogoro? Hebu tuwe wa kweli, tusijitoe ufahamu hapa. Hii nchi wote tunaipenda tuzungumze mambo ya msingi, hayo ndiyo mambo ya utawala bora?
Mheshimiwa Naibu Spika, jana Kilombero Mbunge mwenzetu anapigwa na kubebwa mzobemzobe na Polisi kwenye Jimbo lake mnakuja mnapiga vigelele hapa mnasema, utawala bora! Mbunge anazuiliwa kupiga kura kwenye Jimbo lake, haya ndiyo mambo tunayotakiwa
tuzungumze hapa lakini tunarudi kwenye mambo yale yale kwa akili ileile. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, mnasema utawala bora, rafiki yangu Kigwangalla anaondoka hata hafuati taratibu za Utumishi wa Umma unaenda kufungia watu kwenye ofisi. Najua nia nzuri ya Rais ya kutaka tulete mabadiliko lakini kama hatuja-change mindset za wafanyakazi wetu ni tatizo? Kama gari lako unaweza kuliendesha lina speed ya 120 hata unune, ukemee, haliwezi kwenda speed 200. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mmewajengea uwezo kiasi gani hawa watu? Human resources tuliyonayo ndiyo hii, hamjawajengea uwezo wa kufikiri vizuri, hamjawa-motivate, hamjawa-inspire, hamjajenga uwezo wa kwenda na kasi hii. Sasa hivi tunakwenda kwenye transformation hamjafanya hayo mambo kazi yenu ni kufukuzafukuza. Inawezekana nia ya Rais ni nzuri ya kutaka kuleta mabadiliko sasa wengine kwa sababu mmepewa vyeo siyo kwa merit mnataka muonekane eti mnafanya kazi, mnafungia watu milango, mnawafokea watu, anatoka hata Mkuu wa Mkoa anaenda kufokea watendaji wa mitaa ambao hawako chini yake wako chini ya Mkurugenzi, huo ni utawala gani bora wa sheria? Hebu tujihoji ndugu zangu.
(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tumekuja hapa tunapoanza hebu tuache kujitoa ufahamu. Tena nashukuru sasa hivi wengi mmekuja mnaufahamu, tuisimamie Serikali kama kweli tunataka maendeleo katika nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, akina Wassira wameondoka walikuwa hivyo hivyo, akina Malima walikuwa hivyo hivyo walikuwa kimbelembele, hebu tuwe wakweli tusijitoe ufahamu hapa. Kiukweli watu mnajitoa ufahamu matokeo ya Zanzibar yanaeleweka kabisa tunaanza
kuongea ngonjera na mashairi, tunaacha kusimamia ukweli. Kama tunataka tumsimamie Rais majipu ndiyo hayo, tuanze na majipu hayo, tusimame kiukweli tuitetee Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, unasema tunapunguza matumizi lakini matumizi yako pale pale. Wakuu wa Mkoa wana kazi gani? Mnasema msimamizi wa usalama kwani RPC hawezi kufanya? Ni kazi ipi ambayo hawezi kufanya RPC mpaka awepo Mkuu wa Mkoa, ndiyo kazi
kubwa wanayofanya. Hawa hawana kaz, kama kweli tunataka tupunguze matumizi ndiyo hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama hatutabadilika na hatutasimama kama Bunge ambalo wajibu wetu ni kuisimamia Serikali siyo kumpambapamba tu Magufuli na Serikali ya CCM, hizi ni kodi za wananchi na wananchi wametuleta hapa tuisimamie Serikali. Kwa hiyo, niombe tusijitoe ufahamu ndugu zangu. Tulizungumza haya mambo mkatuzomea, mkaimba ni walewale na Kinana aliwaambia muisimamie Serikali lakini leo Mbunge wa CCM unasimama hapa unaipamba, unajikombakomba kwa Rais baada ya dakika mbili barabara ni mbaya, maji
hayapo. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ninayezungumza pamoja na figisufigisu ambazo Chama cha Mapinduzi kilijaribu kuleta, nina barabara nzuri Iringa Mjini, nina maji asilimia 98, taa barabarani zinawaka, halafu wewe unakuja unajikombakomba hapa badala ya kuisimamia Serikali iwasaidie wananchi wako. Unajikomba kwa lipi, hiyo siyo kazi ya Kibunge! Wengine wamegeuka hapa wamekuwa Procurement Management Unit, siyo kazi yenu. Hata Halmashauri nimechukua pamoja na figisufigisu, nadhani Nape salamu anazipata hizi. Kwa
sababu nimefanya kazi ya kuwatumikia wananchi tuache unafiki, tuache kujikombakomba, tuisimamie Serikali.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naona naishiwa muda, Mungu akubariki sana. (Makofi/Kicheko)
Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa kwa kipindi cha Miaka Mitano kuanzia mwaka 2016/2017 – 2020/2021
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Nami naona nijaribu kushauri na kutoa mchango wangu kuhusiana na agenda iliyo mbele yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali kadhaa ambayo napenda kumuuliza Waziri wa Fedha kwamba katika Mpango huu, ni kwa namna gani mambo haya ameyazingatia?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Taifa letu toka tumepata uhuru, ni Taifa ambalo limekuwa tegemezi. Tumekuwa tukiendesha bajeti yetu na masuala mbalimbali ya kimaendeleo kwa kutegemea Wahisani au Wafadhili. Takwimu nilizonazo mpaka sasa ni kwamba kwa kipindi cha miaka 40, Jumuiya ya Ulaya imetoa zaidi ya Euro bilioni tatu kusaidia shughuli za kimaendeleo ambazo zimekuja kwa mfumo wa Kiserikali. Ukiacha mashirika kama Maria Stops na mashirika mengine kwa mfano kutoka Uingereza, hivi vyote vimekuja kuchangia na vimesaidia sana kukuza maeneo ya elimu, miundombinu na afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye eneo la afya, Marekani na mashirika yake mengi sana yamesaidia sana Sekta ya Afya kusaidia wauguzi wetu namna ya kutatua kero mbalimbali za afya. Vile vile Kiserikali, mashirika kama DFID kutoka UK, USAID, UNFPA inayoshughulika na idadi ya watu duniani, haya yote yametoa michango kwa ajili ya kuisaidia nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunataka Taifa ambalo linajitegemea na tumekuwa tukijinasibu sana kwenye vyombo vya habari kwamba tunataka Taifa liwe la kujitegemea, kitu ambacho ni kizuri. Napenda Waziri wa Fedha aniambie, ni namna gani mpango wake una-reflect kuachana na huu utegemezi wa muda mrefu ambapo toka tumepata uhuru tumekuwa tukiwategemea hawa watu? Katika kipindi cha miaka kumi tumepoteza watoto zaidi ya 600,000 ambao wamekufa kwa utapiamlo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Taifa letu sasa hivi kila saa moja mama mmoja mjamzito anakufa. Maana yake ni kwamba kwa mwaka tunapoteza akinamama wajawazito 9,000. Ni namna gani Mpango huu una-reflect kwamba tutahama kutoka kwenye hii hali ambapo tunapoteza watoto na akinamama wajawazito? Huduma ya afya kwa kiwango chote tunaitegemea kutoka nje!
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Taifa hili asilimia karibia 50 ya watoto wanaozaliwa ni stunts. Kuna mental retardation ya kutosha katika nchi; na wanasema pale anapokuwa mtu mmoja amedumaa, kuna watu wengine ambao wana mental retardation watano. Ni namna gani Mpango huu una-reflect kujaribu kuliokoa Taifa hili kwenye maeneo haya?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa ambalo Kambi ya Upinzani imezungumza, ni jinsi ambavyo Mpango uliopita ulitekelezwa kwa asilimia 26 tu. Mheshimiwa Waziri, kabla hatujaenda mbele, you know speed is useless if you don’t know where you are going or if you lost. Kabla hatujaenda mbele unapotuletea huu Mpango, ni kwa nini Mpango uliopita tumeshindwa, ulitekelezwa kwa asilimia 26? Vitu gani vilisababisha tushindwe? Ni hatua gani zimechukuliwa? Kwa nini tulishindwa? Kwa nini hatutashindwa katika Mpango huu? Ni namna gani yale ambayo yalitushinda miaka iliyopita tutayarekebisha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya kabla hatujaenda mbele ni lazima tuwe na majibu ya kutosha. Kabla hatujaparamia huu Mpango tuanze kuupitisha, tuambiwe ni kwa nini tulishindwa na kwa nini hatutashindwa kwenye Mpango unaokuja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi ya Upinzani imezungumza kwamba tunapopanga mipango lazima iwe inaendana na mazingira, kuna mipango mingine ni kweli huwa inakuwa imposed, haiendani na uhalisia wetu. Huu Mpango wako unasema nini kuhusu kuendeleza Sekta ya Utalii ambayo inachangia asilimia 25 ya fedha za kigeni? Vile vile asilimia 17 zisizo na kodi, yaani GDP Mpango wako unasemaje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa sababu gani? Kumekuwa na uvamizi na nashukuru sasa hivi Waziri wa Ardhi amekuja; kumekuwa na uvamizi wa mifugo, wafugaji wamevamia maeneo mengi ambayo ndiyo yanakuza Sekta ya Utalii ambayo kimsingi ndiyo yanatuletea pesa nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tena na Waziri wa Mifugo yupo hapa! Nchi yetu ina asilimia 10 kwa ajili ya ufugaji. Kwa bahati mbaya haya mashamba makubwa mengi ambayo tulitenga asilimia kumi kwa ajili ya ufugaji yamehodhiwa na watu wachache ambao kimsingi hayatumiki. Sasa maeneo haya yamesababisha hawa wafugaji waanze kuondoka sehemu ambazo tumezipima. Sasa zinaathiri kwenye hunting industry, zinaathiri kwenye National Parks wakati hii ardhi ipo, haijapangwa vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshangaa juzi Waziri wa Maliasili anahangaika na tumbili wale waliokamatwa KIA. Ni kweli sikubaliani wanyama wasafirishwe ovyo ovyo, lakini ukiangalia tumbili na athari zinazopatikana kwa wavamizi wafugaji wanaopeleka kwenye maeneo ya uhifadhi, ni athari kubwa sana kuliko tumbili ambao tunahangaika nao pale KIA. Ni sawa na nyumba inaungua moto, watu badala ya kuokoa vyombo, vinateketea, wewe unamshangaa binti aliyevaa sketi fupi. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ndiyo Serikali yenu! Hatuna priorities! Hii Sekta ya Utalii ndiyo inaiingizia Taifa asilimia 25 ya fedha za kigeni. Wafugaji najua wanapiga kelele sana, sio kwamba siwapendi, najua wengine watainuka hapa! Ufugaji katika nchi hii unachangia one point seven ya GDP, halafu mnaleta mchezo na inayochangia asilimia 17, hapa balance iko wapi? Naomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha anipe majibu, mmejipangaje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Iringa Mjini kwenye Sekta ya Utalii, hii Southern Circuit mlituambia katika Bunge hili kwamba tunataka na Southern Circuit kuwe na utalii, lakini Iringa Mjini pale ni mahali ambapo pamekaa kimkakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumelalamika sana miaka mitano hapa kwamba ule uwanja wa ndege uharakishwe, ujengwe vizuri na barabara ya lami ijengwe mapema iwezekanavyo kwenda kwenye Mbuga ya Ruaha ya National Park ambayo kimkakati ni hii Sekta ya Utalii. Sasa kumekuwa na maneno mengi, mara mnawapiga mkwala hawa wafadhili ambao wanatusaidia; Mheshimiwa Mpango umesema tunaweza kujitegemea, mmekejeli hata zile fedha za MCC.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekwambia hii ni nchi ambayo watoto wanakufa kwa utapiamlo. Tuambieni hii mikakati yote kwa miaka 40 tumetegemea fedha za kutoka Ulaya, mmejipangaje kujiondoa kwenye eneo hili? Naunga mkono tujitegemee, lakini tuwe realistic, tunaachanaje na kujitegemea? Tunatoa elimu ambayo ni spoon feeding! Ni elimu ya watu ambao wanamaliza shule lakini hawana mchango! Tunasomesha wachumi ambao hawana uchumi, wanataka wafundishe uchumi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi kwenda kujifunza uchumi, bora niende kwa Mangi kwenye kaduka kake atanifundisha uchumi kuliko nimpate mchumi mwenye degree kwa sababu hana uchumi yeye mwenyewe, hawezi kuleta chakula mezani. What kind of economics is that? Huo Mpango wako ni lazima tuwe na majibu haya, ni namna gani tutapunguza vifo vya akinamama wajawazito? Huu Mpango tunataka utupe majibu ni kwa kiwango gani tumeshidwa miaka mitano iliyopita?
Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia 26 ni ndogo sana. Utupe majibu ya kutosha! Nami najua, tulikwambia mapema kabisa, wewe sio mwanasiasa, lakini sasa hivi naona siasa imeanza kuingia, unatoa majibu ya kisiasa. Tunataka utupe majibu ya uhalisia! Kama kweli tunajifunga mkanda, tujue tunajifunga mkanda kwa kiwango kinachotosha. Tuambiane ukweli! Zama za kudanyanyana hazipo, tuambiane ukweli kwamba hela hii walikuwa wanatusaidia Wamarekani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema ukifuatilia hizi hela, afya ya nchi hii tumeikabidhi kwa Wamarekani, hatuna uwezo huo! Nimetaja haya mashirika yote ya Kiserikali, achilia mbali hizi NGOs ambazo zote zinaleta pesa kusaidia akinamama. Haya ndiyo mambo ambayo Bunge tunatakiwa tujadiliane na tuambiane ukweli hapa! Kinachonishangaza kikubwa, ni kwa kiwango gani tunacheza na Sekta ya Utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutengeneze Mpango in our context. Utalii ndiyo unaotuletea pesa nyingi katika nchi yetu, lakini matokeo yake, tunacheza na mifugo. Bahati mbaya wenzetu wa Kanda ya Ziwa, they speak a lot, wana influence. Akina Musukuma hawa wanaongea sana, wangependa hata hifadhi zile zote waingie wanyama tu. Nakubaliana kwamba mifugo ni ya muhimu katika Taifa letu, lakini hatuwezi! Hii inachangia one point seven GDP, tukaua inayochangia seventeen. Yaani tunaua uhifadhi kwa kiwango kidogo kwa sababu ya kufurahisha watu kisiasa. Naomba Mpango huu u-reflect ni namna gani tuta-boost uchumi wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunataka tuwe na uchumi wa kati, lakini ukiangalia idadi zote mlizotupa, wasomi tunaowaandaa katika sekta mbalimbali, kwa mfano, utalii una-boom katika nchi yetu. Sioni wale wanaohusika na industry hii tumewaandaa kwa kiwango gani; wale wanaohusiana na gesi tumechukua sababu za makusudi kiasi gani kuwaandaa kwa ajili ya uchumi wa baadaye badala ya kuleta siasa?
Mheshimiwa Waziri naomba haya maswali yangu niliyokuuliza kwenye Mpango wako, ina-reflect kiasi gani ili tuwe wahalisia, tusifanye vitu vya kubahatisha na siasa? Sasa hivi tumemaliza uchaguzi, hebu tuingie kwenye uhalisia, tusiende kwenye siasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi ninavyozungumza, bandari kwa taarifa zenu wenyewe, imeshuka kufanya kazi kwa kiwango cha asilimia 50. Wateja wengine kutoka Kongo wameondoka, wanakimbilia Beira. Haya mambo tutawezaje kuyafikisha kwenye uhalisia kama hatuambizani ukweli? Nasi kwenye Ilani yetu ya Uchaguzi tulisema angalau one third ya bandari ndiyo yangekuwa mapato ya Taifa. Sasa hivi tumeshashusha asilimia 50.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba uchumi pamoja na siasa mnazozifanya, hebu tu-balance kuwe na uwiano kati ya business na politics. Naona mizania ya siasa inapanda zaidi kuliko uchumi. Hebu tu-balance, kwa sababu mwisho wa siku, huu ni mtumbwi, tumepanda wote. Kama mwenzetu umeanza kutoboa, tutazama wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba haya majibu yasawazishwe ili kwa pamoja turidhiane, tuishauri Serikali. Waziri wa Ardhi unanisikia, Waziri wa Mifugo unanisikia, bahati mbaya Waziri wa Maliasili hayupo, naomba m-balance haya mambo; kwa sababu siku moja nimemsikia Waziri wa Maliasili na Waziri wa Mifugo, kulikuwa na sintofahamu kidogo katika eneo hili. Mimi wale tumbili hata mngeacha waende, hakuna shida. Ingekuwa tembo au faru, hiyo sawasawa. Wale Tumbili si sawa na Kweleakwelea! Wapo wengi tu, tungeuza tupate hela; lakini mnaacha uhifadhi, ng‟ombe wanakwenda kule, wanaharibu uhifadhi! Hii ni kwa ajili ya vizazi vyetu vya baadaye.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni hayo tu machache, nimejaribu kusaidiana kidogo katika hilo. Ahsante sana.
Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017- Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Na mimi nataka nitoe mchango wangu kuhusiana na Wizara hii ya Viwanda. Mheshimiwa Waziri nashukuru umekuwa unaongea sana na unapojibu maswali kama vile bado tuko kwenye kampeni. Tunatagemea sasa hivi hapa utupe data za uhalisia namna utakavyokwenda ku-earth majukumu yale ambayo Mheshimiwa Rais amekupa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua Mheshimiwa Rais amesema anataka nchi hii, jambo ambalo ni jema, iwe ni nchi ya viwanda kwa maana ya uchumi wa viwanda. Nchi hii wahitimu kwa mwaka ni 800,000. Katika majukumu ambayo Mheshimiwa Rais amekupa wewe kama Waziri amesema 40% ya wahitimu 800,000 anataka waende kwenye viwanda. Katika 40% ya hao watu 800,000 ni watu 320,000 maana yake hawa tunawaingiza kwenye viwanda. Kwa nchi hii kiwanda kikubwa ambacho kimewahi kuajiri watu wengi sana hawazidi 5,000. Sasa twende kwenye hesabu za haraka haraka maana ukija hapa unakuwa kama unafanya kampeni, twende kwenye hesabu za haraka haraka za kawaida tu. Ili lengo lako hilo la kuajiri watu 320,000 kwa mwaka lifikiwe maana yake unatakiwa uwe na viwanda 530 katika kipindi cha miaka mitano ya Ilani yenu ya Uchaguzi ambayo mnajisifu nayo. Hoja inakuja hapa mwaka huu sasa tunakwenda nusu una viwanda vingapi? Naomba utujibu hapo, una viwanda vingapi mpaka sasa? Utatutajia cha Dangote, alikiacha Mheshimiwa Kikwete ambaye sasa hivi mnamzomea, ninyi hamjatengeneza hata kimoja, una viwanda vingapi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii wafanyabiashara wanataka kuongea na Serikali yako, mnawakatalia, mnawa-frustrate, hamkai nao. Bado mnasema mna wawekezaji kutoka nje wakati hawa hawa waliomo ndani hamuwezi kuwa-handle vizuri. Ningekuomba Mheshimiwa Waziri hebu tuache mbwembwe tuwe realistic, hizi hesabu zinakataa, huna uwezo huo. Saa hizi hata viwanda viwili vipya huna! Ukinionesha viwanda vitatu umetengeneza nitakupa Land Cruiser yangu hapo nje kama unavyo, toka mmeingia Serikali hii, huna hivyo viwanda. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mnakuja hapa mnatupa takwimu za uongo, za kutuaminisha matumaini ambayo hayapo, hauna viwanda hivyo. Ukipiga hesabu hawa watu huwezi kuwapeleka, kiwanda kikubwa kinachoajiri watu sasa hivi ni Breweries inapeleka watu 3,000. Hawa watu 320,000 kwa mwaka where are you going to employ them, wapi utaenda kuwaajiri? Tunaomba unapokuja utuambie hesabu za uhalisia, hatuko kwenye kampeni, tunataka utuambie ukweli! Naomba hilo usije na majibu mepesi mepesi, hivyo viwanda hauna. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ndugu yangu hapa amezungumza, infrastructure ya umeme iko wapi, umeme wa uhakika uko wapi mpaka sasa unaowaita hao. Umetuambia Jumatatu tuje tugawane hapo, hatuwezi kugawana watu kama njugu wakati hakuna infrastructure yaani mimi nitaondoka na mwekezaji nasema naenda naye Iringa naenda naye wapi! Tukafanye nini? Mazingira yaliyoandaliwa yako wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri mimi ningeomba hebu tuambizane ukweli na ninyi ndio mtakaokwenda kumuangusha Mheshimiwa Magufuli kama mkija na mbwemwbwe ambazo hazina uhalisia. Mtupe mambo ambayo yanawezekana. Nimekupa hii takwimu uikatae! Unahitaji kuwa na viwanda 530 ndiyo uwapeleke hawa 40% kwenye hivyo viwanda unavyosema unakwenda kutupa na kuwaaminisha Watanzania kwamba nchi itakuwa ya viwanda, mambo yatakuwa mazuri, utupe figure ambazo ni za uhalisia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine amezungumza Mheshimiwa mwenzangu hapa kuhusiana na hawa wafanyabiashara wadogo wadogo ambao tumezungumza sana hata miaka mitano iliyopita tunawaona kama ni kero katika nchi yetu badala ya kuwaona ni fursa. Kwa hiyo, hebu tu-change, is a mindset thing. Change what you see by changing how you see. Tunapowaona wale watu ni kero ndiyo tunagombana nao na mabomu badala ya kuweka mikakati ya kuwafanya hawa watu wawe na tija kwenye maeneo yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa watu ni wengi sana wangetafutiwa maeneo. Tumezungumza sana na mwaka jana tulitoa mpaka na maazimio kwenye eneo hilo kuhakikisha miji yote yatengwe maeneo walao kila weekend maeneo yale yafunguliwe, haya mambo yamekuwa yakisuasua katika maeneo mbalimbali. Naona hapa kwa mfano Dodoma imeshaanza na maeneo mengine lakini tumekuwa tukiwapiga hawa Wamachinga, tumekuwa tukiwaonea, hatuwatengenezei mkakati mzuri. Kwa sababu wao kama alivyosema ndugu yangu hapa, ndiyo wako kwenye field wengine wote hapa tunaongea nadharia tu lakini wao wako kwenye field ndio wanaliona soko lilivyo.
Kwa hiyo, nikuombe Mheshimiwa Waziri, tungeomba hili tatizo nalo lipate ufumbuzi wa kudumu na wa moja kwa moja badala ya kuwaona hawa watu ni kero tuone kama ni fursa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikirudi kwenye suala la viwanda, kwa mfano Mwanza kuna kiwanda kilikuwa cha nyama ambacho kilikuwa cha Tanganyika Packers, wakaja wakawekeza wawekezaji hakikwenda vizuri. Wakaja watu wa nje, baadaye wakaja Wamarekani, Wamarekani baada ya matatizo yao ya uchumi, hakipo. Leo Mheshimiwa unasema kwamba watu waje, kile kiwanda kule tatizo ni nini? Vilivyopo vimeshindwa nini na sasa hivi unatuaminisha kitu gani kitasababisha hivyo viwanda vilivyopo kwenda mbele? Vile vilivyoshindwa vilishindwa kwa nini na sasa hivi kwa nini unatuaminisha kwamba hivyo vilivyopo tutasonga mbele? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hebu tuache mambo ya kampeni. Uchaguzi mlishashinda whether mlituibia kwa magoli ya mkono, it is fine, mlishinda, Serikali ni ya kwenu.
Sasa hapa hatuhitaji kampeni, tupeni vitu ambavyo mnakwenda ku-earth. Hatutaki mbwembwe! Mheshimiwa Mwijage acha mbwembwe, tupe vitu ambavyo ni practical. Mwalimu wangu alikuwa anasema how can you earth it?
Tuambie unawezaje kutuambia kwenye ground? Tuna viwanda vingi sana, Iringa tulikuwa na viwanda vingi vya akina-TANCUT vile vyote vimekufa. Ukienda Mbeya hivyohivyo, ukienda Morogoro hivyohivyo. Sasa hivi mnakuja na lugha nzuri sana, very testy lakini ukienda kwenye uhalisia, hii hesabu ni ndogo sana nimekupa, it doesn’t work brother. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba atakaporudi hapa atatupa majibu. Hii ni hesabu ndogo sana huhitaji kuwa na elimu ya Chuo Kikuu, ndogo tu. Utupe majibu namna gani hii kazi aliyokupa Mheshimiwa Magufuli ya kuhakikisha 40% ya wahitimu 800,000 wanaingia kwenye viwanda, ni viwanda vipi? Mpaka saa hizi huna hata kimoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka niliweke wazi hilo, tuache mbwembwe, tuambizane ukweli hapa ili tuisimamie Serikali. Nikushukuru sana kwa kunipa nafasi.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kwa mwaka wa Fedha 2016/2017.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi. Mimi nianze na Wizara kama ambavyo mchangiaji Mheshimiwa Lucy Owenya amesema, ili tupandishe uchumi wa Southern circuit lazima tufungue milango.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba sana Bunge lililopita tumezungumzia sana kuhusiana na uwanja wa Nduli Iringa pamoja na barabara inayotoka Iringa Mjini kwenda National Park. Ningeomba Wizara kama inawezekana hebu tushirikiane basi hata na TANAPA tutengeneze ile barabara kusudi tuweze kuzalisha pesa nyingi zinazotokana na hifadhi ambayo ni kubwa ya pili hapa Afrika, ningeomba hilo mlifanyie kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, ninataka nizungumzie kuhusu wanyama waliotoroshwa, hiki ni kiporo. Kwa bahati mbaya Wabunge huwa tunasahau tulikotoka, hiki ni kiporo. Bunge lililopita tumezungumza sana juu ya ujangili, lakini kuna wanyama waliokuwa wametoroshwa uwanja wa KIA. Bunge lililopita tulitoa azimio, AG wewe ni shahidi hapa tulikubaliana wote kwamba lazima ufanyike uchunguzi ni akina nani walitorosha wale wanyama, sasa hivi hakuna kesi, mwanzoni mlikuwa mnasingizia kuna kesi mahakamani, sasa hivi hakuna kesi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, iliingiaje ndege ya kijeshi? Jeshi lilionaje hapa? Usalama wa Taifa ulionaje? Hayo mambo bado hayajatolewa majibu. Serikali ya Qatar, nilibahatika kwenda Qatar walisema wamezoea kuchukua wanyama kwa style hiyo. Tulitoa Azimio kwenye Hansard inaonyesha Bunge lililopita. Ninaomba Waziri haya mambo hayawezi kulala kiporo kama tunataka tukomeshe ujangili, maana yake Serikali hii imesema inafukuwa makaburi, tuendelee kufukuwa makaburi hayo ni nani alihusika kutorosha hawa wanyama kuwapeleka Qatar, lazima turudishe na Bunge liliazimia. Naomba AG utasaidia Wizara hii namna gani tulifanye.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu ni hili suala ambalo Kambi ya Upinzani imezungumzia kuhusu Kampuni ya Green Miles. Kampuni ya Green Miles, amezungumza Mheshimiwa Mbunge Mzee wangu hapa, mimi nilkuwa miongoni mwa Kamati ya Wabunge wanne, tuliokuwa tunachunguza utoroshaji wa wanyama. Tulipochunguza kampuni ya Green Miles, kama alivyosema haikupewa vitalu vya uwindaji kwa sababu ilikuwa haina sifa. Kamati ya ushauri ilimshauri Waziri kwamba hii kampuni haina sifa, imesema uongo, lakini haihifadhi kwa sababu kwenye kuwinda kunahitaji uhifadhi, kwa bahati mbaya au vinginevyo mambo yalivyokwenda hii kampuni ikapewa. Ilivyopewa tukayashuhudia yale ambayo walivunja kanuni za uwindaji na kulikuwa na infringement zaidi ya 11.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 4 Julai niliweka CD hapa kuonesha jinsi ambvyo wanawinda vibaya! Hawa watu hawana sifa za uhifadhi na Waziri aliyepita aliamua kuifutia leseni ya uwindaji kwa sababu wanawinda vibaya, suala hili lilivuta hisia za Kimataifa katika masuala ya uwindaji, suala hili lilivuta hisia za Watanzania vituo karibu vyote vya televisheni vilionesha jinsi ambavyo hawa watu wanawinda vibaya wanyama, hawana sifa ya kuwinda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kushangaza Mheshimiwa Waziri umetoa barua tena. Hapa Mheshimiwa Maghembe, kwenya masuala ya uhifadhi niko na wewe, sikubaliani kwamba ng‟ombe waende kila mahali, lakini kwenye suala hili sikubaliani na wewe. Kwa sababu tunakubali kuwa uwindaji ni pamoja na uhifadhi, hunting is about conservation. Mwindaji yoyote ambae hawezi ku-conserve nature hatustahili katika nchi yetu! Sasa inawezekanaje hawa watu ambao hawana sifa, kuna infringement zaidi ya kumi na ngapi? Lakini Waziri aliyekutangulia alifuta, kulikuwa na makosa sita aliyaona. Walikuwa wanawinda ngedere hawaruhusiwi kuwinda ngedere.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtoto wa chini ya miaka 16 anawinda, sheria inakataa, walikuwa wanatumia bunduki ambazo zinaziba sauti, sheria inakataa, wewe mwenyewe unaijua kwenye sheria ya mwaka 2009 na regulations za mwaka 2010. Hawa watu wamevunja sheria, leo wanarudi wanarudi kwa mlango gani? Ninaomba Waziri utuambie hawa watu ambao hawana sifa za kuwinda wamerudije tena kwenye maeneo hayo? Tutakuwa tunaleta mchezo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niwaombe Waheshimiwa Wabunge hebu tuwe consistance kama tunataka tufanye uhifadhi. Wale waliokuja kuchukuwa wanyama wetu, watu walipiga kelele sana Bunge lililopita wakasema tunataka hata mifupa irudi. Nani alichukuwa hao wanyama? Hiyo ndege ya Qatar iliingiaje? Tulizungumza hapa kwamba mpaka na Ikulu ilikuwa inahusika, hatujapata majibu ya kutosha. Lakini hawa ambao walizuiwa wanarudi tena kwa mlango wa nyuma wamerudije? Naomba Mheshimiwa Waziri haya mambo utupe majibu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine kuna Mbunge, asubuhi amezungumza kwamba mpaka kwenye magazeti wanaandika kwamba kuna Wabunge wengine ni majangili. Hii ni kashfa kwa Bunge, hatuwezi kukaa kimya. Hili Bunge tumeambiwa kuna wala rushwa, Bunge hili wengine wanapiga mtindi, Bunge hili tena tunaambiwa kuna majangili. Tutakuwa na chombo cha umma kipi ambacho haya mambo kama hatuwezi kuyasemea? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu mtu kama kweli imeandikwa Jambo Mills gari yake hii hapa, kama ni kweli lazima tupate majibu na kwa bahati mbaya labda yeye hayupo na inasemekana, taarifa zinasemekana mpaka na gari lingine la Jambo Mills lilikamatwa na pembe za ndovu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama vile halitoshi, huyu mtu kuna leseni moja ya madini na yeye anahusika. Haya madini yako kwenye kitalu kule Meatu ambacho kuchimba madini hairusiwi kwenye hifadhi Waziri unajua Huyu mtu sijui amepataje kulikuwa hakuna EIA? Amepata, wanatumia wafugaji kuwaingiza eneo la uwindaji kwa kisingizio kwamba hawana malisho ili waweke pressure kusudi wakachimbe madini mpaka wamepata hiki kibali.
Nimshukuru Mkuu wa Mkoa alizuia hiki kibali na nimuombe Waziri wa Madini alifuatilie hili suala, ni nani alitoa kibali hiki, watu waingie kwenya hifadhi, sheria yetu inakataa kwamba wasiingie kwenye hifadhi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa huyu kama kweli haya mambo yanafanyika na yeye anahusika, Bunge lijisafishe, tujue kuna tatizo gani kama ni ya uongo asafishike, lakini vyombo vya habari vimeandika, vyombo vya habari vimetoa, anahusika, wanasema kuna Mbunge anahusika wamemtaja kwenye magazeti, ukienda kwenye mitandao na yeye hajakanusha. Lakini kuna wakati walivyokamatwa hawa watu waliachiwa, wakatoa fedha kidogo tu wakati wengine wanasota.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wanasafirisha tumbili, umewaweka ndani sasa hivi wanasota, lakini hawa watu wanatembea, inaoneka waliokamtwa wana nasaba na huyu mtu alyetajwa hapa, lakini wametoa faini wakaachwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanyama wanaonekana hapa hawakuchukuliwa hatua zozote, lakini wengine wamesafirisha tumbili tu wale tena wana haki, wale walikuwa wanasafirisha tumbili vizuri hawana makosa, akina Mzee Mlokozi wale wanalala tu kule ndani. Hawa wanatembea barabarani na wanatumia kisingizio, nikuombe hata hili suala la Toya Mheshimiwa Waziri hebu liangalie kwa upana wake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kwa bahati nzuri miaka yote mitano nimekuwa kwenye hilo eneo kidogo naelewa, watu wa Toya muwaangalie kwa jicho la karibu sana. Manyanyaso wanayoyapata na taabu wanayoipata kwa kweli haiwahusu. Tunajaribu kuwarudisha nyuma hawa ambao ni Watanzania wazawa, wanafanya biashara zao, tunawa-drag chini bila sababu. Niombe Watanzania wenzangu the fact sisi ni Wabunge hapa, tupo kwa ajili ya maslahi ya Watanzania na Taifa kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna msemo mmoja unasema: „it is not economical to go to bed early and save all the candles if the result is twins (siyo jambo la kiuchumi kwenda kulala mapema ukatunza mishumaa yote kama matokeo yake yatakuwa ni mapacha). Kama tutadhani ni uchumi kupeleka ng‟ombe kila mahali kusiwe na mipaka, tusidhani litakuwa jambo la kiuchumi, baadaye tutapata hasara ya Taifa hili, ni lazima tu-save nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii ni ya wafugaji, nchi hii ni ya wakulima, nchi hii ni ya wafanyakazi, nchi hii ni ya viwanda, kwa hiyo, lazima tutenge maeneo. Ndiyo maana China walivyoona nchi ni ndogo wakaweka sheria ya kuzaa mtoto mmoja. Kwa hiyo, hatuwezi tukasema ng‟ombe wawe kila mahali, hatuwezi kusema ufugaji uwe kila mahali, tukabaliane wote kama viongozi, tutenge maeneo maalum. Mheshimiwa Waziri, kuna asilimia 10 nchi hii ya ufugaji wa ng‟ombe, ambao ng‟ombe tulionao milioni 25, wakiwekwa vizuri tunaweza tukawatunza. Lakini hatuwezi kukubali kutumia mifugo tukaharibu uhifadhi, tukaharibu utalii ambao unatuletea fedha za kigeni asilimia 25 na GDP ya asilimia 17. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, badala ya kugombana hapa na wananchi wametuita hapa kama viongozi, kama watu wenye busara, badala ya kugombana hapa kuwa na mawazo madogo ya kuwaza Jimbo lako hebu tuwe na national interest, tukae wote kwa pamoja tukubaliane. Hii nchi ni yetu sote, tukubaliane mifugo ikae wapi, samaki wakae wapi, ng‟ombe wake wapi? Mheshimiwa Waziri tukiruhusu jazba zitutawale hapa tutaishia kugombana. Kama wananchi huko wakituona, mfugaji anagombana na mkulima, mkulima anagombana na mfugaji, huko nje tutaanzisha vita.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianzie hapo alipoishia Mheshimiwa Lema, Bunge kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linao uwezo wa kumu- impeach Rais. Sasa kama tuna uwezo wa kumu-impeach Rais halafu watu tukimtaja Rais hapa mnatetemeka maana yake tunataka tukiuke Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni Bunge pekee, ni chombo hiki pekee, waliotunga Katiba walijua kuna wakati Rais anaweza akakosea na hiyo mamlaka iko mikononi mwetu. Mimi nashangaa Wabunge tukimtaja Rais kama anakosea tutamui-impeach vipi kama anakosea anapoingoza nchi yetu? Kwa hiyo, hebu turudi kwenye senses zetu kwamba mamlaka hiyo tunayo na wala hatumuonei kama anafanya makosa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe sana Mheshimiwa Mpango, wengi wamezungumza mimi narudia na juzi nilisema na tunasema ukweli kwa sababu tunalipenda hili Taifa. Nikuombe sana unapoleta mambo yako hapa usilete kama vile upo kwenye lecture room kwamba unataka kutupa lecture. Sisi ni wawakilishi wa wananchi, wametutuma wananchi na ndiyo maana mnapoleta huu mpango hapa ni ili sisi Wabunge wote tuujadili vinginevyo msingekuwa mnaleta mngekaa nao huko Serikalini muendelee. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana ulipoleta, tena mimi tulikutana pale nje, mimi huwa nasema openly, tulikutana pale nje nikakuambia hizo kodi unazoleta kwenye VAT utaleta chaos, nikakuambia hizo kodi unazoleta bandarini utaleta taabu. Bandarini sikuwa na utaalam sana walau kwenye maliasili nilikuwa najuajua kidogo, lakini zimesababisha shida kubwa kwenye nchi yetu halafu hapa tunalindanalindana, tunafichamafichama kuelezana ukweli na mnamdanganya mfalme kwamba mambo yapo vizuri. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kitabu chake hiki najua kanuni zinaeleza kwamba hatuwezi ku-review bajeti iliyopita kwa sababu haijapita miezi sita, lakini haya mambo yote uliyoandika yame-based kwenye bajeti ile iliyopita ambayo hata wewe mwenyewe Waziri hukuwepo hapa Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu mpango unaouleta hapa haupo realistic kwa sababu Ilani ya Chama cha Mapinduzi aliyomaliza Mheshimiwa Jakaya Kikwete kipaumbele hakikuwa viwanda, hii sasa ya Mheshimiwa Magufuli inazungumzia viwanda. Huu Mpango wako umetuletea mambo ya DARTS na kadhalika ambayo ni mafanikio yaliyopita ya Mheshimiwa Jakaya Kikwete. Kwa hiyo, mpango huu haupo realistic, upo baseless, tunajadili kitu ambacho hakina miguu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Serikali hii kwa sasa tunapozungumza mipango Mheshimiwa Waziri Mpango lazima tuwe na watumishi ambao wana confidence. Amezungumza Mheshimiwa Lema hapa ukienda kwa watumishi wote wa umma hawana ujasiri katika nchi hii, mmewa-terrorize wote, hawana confidence, hawajiamini kila mtu akiamka asubuhi hajui kitu gani kitatokea. Haya mambo tunayopanga tutawezaje kuyatekeleza kwa watu ambao hawajiamini! Umma umeaminishwa kwamba watumishi wote wa umma ni wezi, wafanyakazi wote hawana ujasiri wa kukaa kazini, ile morale haipo kwa sababu kila mtu ni mwizi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, amezungumza vizuri sana Mheshimiwa Lema tukisema dhamira ya Mheshimiwa Rais ya kutaka kuleta mabadiliko na nidhamu katika nchi hii au ku-restore glory haipo tutakuwa tunasema uongo. Kuna mambo ambayo ameonyesha dhamira nzuri, wote tunakataa rushwa, wote tunakataa mambo mabaya ndani ya nchi lakini njia anazozitumia za kutisha watu na kuvunja sheria hizo ndiyo tunazozikataa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma Ripoti ya Utafiti wa Amani Duniani iliyotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya Institute of Economics and Peace ya mwaka 2015, Tanzania ni moja ya nchi 64 duniani zinazokaribia hatari ya kuvunjika kwa amani kwa sababu ya ukandamizaji wa kidemokrasia. Sasa tusipokuwa na amani na kuheshimu na mipaka na mipango tuliyojiwekea wenyewe tutawezaje kusonga mbele na mipango hii mizuri? Hii nchi ni yetu sote, pale Rais anapofanya vizuri tutakubaliana naye, lakini mazuri yake yote anayoyafanya yanaharibika pale alipozungukwa na watu ambao hawamwambii ukweli. Sisi hapa tutamwambia ukweli, mtukate vichwa tutamwambia tu, kama yupo uchi tutamwambia upo uchi, we are not scared of him. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Zitto amezungumza hapa Serikali hii haipo coordinated. Ukienda kwa mfano kwenye mipango yako hii hakuna mahali popote ambapo umezungumzia espionage (uchumi wa kijasusi). Wizara ya Mambo ya Nje ndiyo jicho la nchi ambapo mimi nashangaa katika mipango yako ya mwaka jana haikukuambia jinsi ambavyo Congo ni ya muhimu sana katika bandari yetu ya Dar es Salaam, Wizara ya Mambo ya Nje ilikuwa wapi? (Kicheko)
Leo Wizara ya Mambo ya Nje kama ni jicho, kama ipo coordinated ingeweza kusema unapopeleka mpango huu kwamba bandarini tutaongeza kodi kiasi hiki Mheshimiwa Mpango unakosea tutapoteza potential customers. Kama Serikali hii ipo coordinated ulipopandisha VAT kwenye mambo ya tourism Waziri wa Maliasili angekuambia you are wrong tunaenda kupoteza watalii. Hata hivyo, kwa sababu mkiamka kila mtu afanya la kwake, anawaza la kwake na mnashindana kwenda kujipendekeza kwa Magufuli matokeo yake ndiyo mnatuletea mipango ya ovyo ovyo. Tupo hapa kama Bunge, hampo coordinated ndiyo maana Mheshimiwa Kigwangalla anaweza akasema dawa zipo kidogo, Mheshimiwa Ummy anasema zipo za kutosha na Makamu wa Rais anasema hazipo, tumsikilize nani sasa, the same government! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri najua ni msomi, Mpango huu kuna tafiti nyingi ambazo hata rafiki yangu asubuhi amezizungumza hapa. Ukiangalia tafiti zilizofanywa na Taasisi ya Kimataifa ya GCI kuhusiana na mazingira bora ya uwekezaji Tanzania inashika nafasi ya 120 kati ya nchi 140 zilizotajwa kwenye uwekezaji huo. Ukiangalia moja ya matatizo tuliyonayo Tanzania nchi yetu imekuwa ni ya nne, mazingira ya uwekezaji hayajawa mazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, Tanzania inahesabiwa kwamba hatujawa wazuri katika matumizi ya teknolojia. Huu mpango hautafsiri ni namna gani tunapambana na hayo maeneo ili tutengeneze mazingira mazuri ya uwekezaji. Kwa hiyo, hizi tafiti zinaletwa halafu Mheshimiwa Mpango na wewe unaenda njia yako. Serikali nzuri na jasiri inaweza ikasimama na mimi ningekuwa wewe ningekuja hapa kwa sababu kimsingi hili joto tunaloliona mwezi wa sita mwakani litakuwa kubwa sana na inawezekana Bunge likaondoka na kichwa chako hapa. Inawezekana Mheshimiwa Waziri huu mpango labda ali-copy New Zealand au Australia, ni busara tu kuja hapa na kusema jamani this things it is not going to work here nili-copy mahali nika-paste hapa hai-work, tutaambizana ukweli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo ambayo ni kweli tumeshindwa kuyafanya kwa visingizio mnavyovileta, lakini kuna mambo we told you, ulishupaza shingo ukakataa. Kuna data nyingi zinaonyesha jinsi ambavyo Serikali yetu haina mazingira mazuri ya uwekezaji. Zimekuwa ni ngonjera nyingi hapa na kukandamiza demokrasia na kupiga wapinzani na yote yanayoletwa hapa yanakuwa hayatekelezeki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niwaombe Wabunge, hii nchi ni yetu sote na wala hatuitaji kugombana, tunahitaji kama Wabunge tuongee lugha moja lakini kwenye ukweli tumwambie mtu amefanya vizuri na kama amefanya vibaya tumwambie amefanya vibaya. Msingi wa kwanza lazima turudishe demokrasia katika nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii hali mnayotaka kuiweka kwenye Chama cha Mapinduzi ya kuogopa watu mnaitoa wapi? Hata Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alisema tusiogope watu, tuwaheshimu watu. Leo ndani ya chama chenu mmeanza kuogopa watu hicho chama chenu hakina wazee cha kuwaonya watu wasiogopwe? Hivi vyeo ni dhamana, alikuwepo Baba yetu wa Taifa na nataka niwaambie Serikalli ya Awamu ya Tano msidhani wale wa Awamu za Kwanza, ya Pili, ya Tatu na ya Nne hawajafanya mazuri na hata wapinzani hatusemi hivyo, kuna mambo mazuri ambayo Baba wa Taifa aliyafanya lazima tuyaenzi na kuyaheshimu, lakini kuna mambo mabaya aliyoyafanya tutayakataa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi kuna mambo mazuri aliyafanya na mabaya aliyafanya mazuri tutayaheshimu na alikosolewa, alisikiliza, tukampenda. Akaja Mheshimiwa Benjamin William Mkapa alifanya mambo mazuri tukampigia makofi, tulipenda hata hotuba zake za kila mwisho wa mwezi zilikuwa ni hotuba zilizoshiba siyo za vijembe za kutukana watu, lakini kuna mambo mabaya tulimsema. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, akaja mzee wetu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na kwamba tulim-challenge ni kweli, pamoja na kwamba kuna mambo hatukukubaliana naye lakini alisaidia nchi hii kwenda mbele. Kipindi chake aliweka mazingira walau watu duniani walianza kupenda kuja kuwekeza Tanzania na walau aliruhusu demokrasia. Tulimsema humu ndani lakini alihakikisha kila mtu kama Mtanzania anatoa mawazo yake, leo kwa nini Mheshimiwa John Pombe Joseph Magufuli asisemwe? Tulikuwa tunakaa naye pale kwenye kiti tunamfuata pale leo tunamuogopa ana mapembe? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe Wabunge wa CCM hebu tuweke itikadi zetu pembeni, tusimame kama Bunge, Rais akikosea tuwe na uwezo wa kusema no, wewe ni Rais wetu lakini hapa no. Hatuwezi tukawa waoga, anatisha kila mtu na kila mtu anajipendekeza kusema uongo. Hii nchi ina hali mbaya lazima tushirikiane. Ninyi mnaopeleka hiyo mipango kwa sababu mnamzingira akisimama kwenye vyombo vya habari anasema wale waliokuwa wanaiba pesa ndiyo wanapata taabu, hivi maskini wanaouza vitumbua kule…
T A A R I F A...
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa ya Mheshimiwa Simbachawene siipokei na haya ndiyo niliyoyasema ndiyo uoga tunaouzungumza huo. (Makofi)
La pili hayo maneno aliyoyazungumza Mheshimiwa Simbachawene wakaongee kwenye party caucus. Hapa tunaongea...
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ndugu zangu nimesema hapa hakuna mpinzani yeyote anayesema Serikali zilizopita hakuna mazuri yaliyofanyika, hakuna anayesema hivyo. Tunachosema mabaya tutakosoa na tutaendelea kukosoa. Kama ninyi mnamuogopa Mtukufu Rais sisi tutamsema, tutamkosoa ndani ya Bunge na nje ya Bunge na akifanya vizuri tutamwambia.
Niombe Wabunge wote tushikamane, tunapojadili mambo mazuri ya nchi wote tuwe pamoja uchumi uko vibaya, hakuna pesa mifukoni hakuna pesa kwa watu. Mheshimiiwa Rais mnam-mislead eti anasema waliokuwa wanapiga rushwa ndiyo wana shida huko mitaani mama ntilie kwenye majimbo yenu walikuwa wanapiga rushwa wapi?
Watu wana hali mbaya. Wanashindwa kulipiwa ada halafu mnakuja hapa mnasema wapiga rushwa walikuwa wanapiga rushwa wapi kwenye majimbo yenu. Hivi ninavyozungumza nyuso zenu zinawashuka kwa sababu mnajua ukweli huo kwamba hali ni mbaya. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba wote tuchangamke tumdhibiti Waziri wa Fedha alete mipango na bajeti inayoeleweka. Mawaziri wengine mnabeba mzigo sio wenu, wakati wa bajeti mwaka jana tulikuwa tukiwaambia pesa hazitoshi mnasema aah zinatosha hivyo hivyo. Sasa hivi kwenye Kamati mmerudi tena mnasema kwa kweli hazitoshi mtusaidie ninyi ninyi, sasa hivi mnasema hazitoshi. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, suala tumbane Waziri wa Fedha alete mipango inayoeleweka siyo mipango ya ku-copy na ku-paste sijui kutoka wapi iwe katika mazingira ya kwetu. Tuletee mipango in our context siyo mme-copy New Zealand au sijui Australia huko it doesn’t work here.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Taarifa ya Mwaka ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi, nianze kwa kusema kwamba na mimi ni Mjumbe wa Kamati hii, kwa hiyo ninaunga mkono hoja na nipongeze Wajumbe wenzangu wa Kamati pamoja na Mwenyekiti wa Kamati, ninaamini tumefanyakazi nzuri na tunaiomba Serikali ipokee ushauri ambao tumeishauri kwa ajili ya manufaa ya Taifa letu. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kama Mjumbe nilitaka nizungumze kwa ujumla mambo yanayohusiana na amani na utulivu wa nchi yetu. Ripoti ya utafiti iliyotolewa na Instituteof Economics and Peace inazungumzia na inaonesha kwamba Tanzania ni nchi ya 64 kati ya nchi 64 ambayo ipo hatarini kutoweka kwa amani. Kwa hiyo, Kamati yetu inahusika na mambo ya nje, ulinzi na usalama na ili ustawi wa amani katika nchi yetu ni lazima eneo hili liendeshwe kwa weledi, kwa utaalam, huku demokrasia ikishamiri katika nchi yetu. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ripoti hii imetaja ma-group manne ya nchi namna ambavyo yana-exercise utawala wake. Inasema pale ambapo kuna full democracy kunakuwa kuna amani ya kutosha na kunakuwa na maendeleo ya kutosha kwa sababu watu wanakuwa na uhuru wa kutoa mawazo yao, watu wanaweza waka-challenge na kukosoana kwa amani kwa sababu kuna full democracy. Kwa hiyo, katika ripoti hii inaonesha kwamba kukiwa na full democracy nchi huwa ina flourish. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ripoti hii imeeleza vilevile kuna frauddemocracy, democracy ya kiasi; kunapokuwa kuna democracy ya kiasi kunaanza kuwa na viashiria vya uvunjivu wa amani. Kipengele cha tatu kuna hybrid regime ambayo ndiyo Tanzania tunaangukia hapo kwamba tuna utawala wa kichotara ambapo kuna aina fulani ya demokrasia, lakini kuna aina fulani ya udikteta. (Makofi) Katika ripoti hii inasema nchi yoyote ambayo inaangukia katika eneo hili inakuwa kwenye hatari ya kupoteza amani na Tanzania tupo kwenye hatari ya kupoteza amani kwa sababu tupo kwenye hybrid regime. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho ni authoritarian regime ambayo hiyo ni ya kidikteta kabisa ambako bado hatujafika na tumeona madhara ya kuwa na regime za namna hii. Kwa hiyo, tunapozungumzia suala la ulinzi na usalama ni jambo la msingi na ni jambo la muhimu sana tukifuata taratibu, sheria na kanuni tulizojiwekea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeyazungumza yote haya kuweka kama msingi. Taifa letu ili tusiingie kuwa eneo la mwisho kabisa ambalo ni hatari, ni lazima tuzingatie sheria na taratibu ambazo tumejiwekea wenyewe. Kwa hiyo, ningeomba vyombo vya ulinzi na usalama na ningeomba watawala wanaohusika sheria ambazo tunazitunga hapa tukizifuata wote tutajikuta tunaiweka nchi yetu katika usalama na hatimaye uchumi wa nchi yetu utakua. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, nikiangalia Wizara ya Mambo ya Ndani nataka nimnukuu Mheshimiwa Kafulila jana ali-tweet, amezungumzia tuna chombo kwa mfano hiki cha National Drug Control Council ambapo ndani ya chombo hiki yupo Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Ndani, ambao hawa wote wanashughulika na chombo hiki kwa ajili ya kudhibiti pamoja na Waziri wa Afya naye yumo na wengineo. Hawa wote ni chombo ambacho kimeundwa kwa ajili ya kudhibiti dawa za kulevya na kipo kisheria. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nimezungumzia masuala ya ulinzi, kila Kiongozi ana mipaka yake na kila Kiongozi amepewa majukumu yake. Kuna chombo kama hiki nilitaka niulize Wizara ya Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Mwigulu upo hapa, kumetokea kitu gani badala ya hiki chombo kushughulika na masuala ya msingi kama haya ambayo sisi sote tunaunga mkono vita ya kupambana na dawa za kulevya, leo siwaoni Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Ndani na Waziri wa Afya mkishughulika na mkitoa matamko kwa sababu ninyi ndiyo wenye chombo hiki, tunamuona Makonda ndiyo amebeba bango la nchi nzima ambaye ni kiongozi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam sawa tu na Mheshimiwa Amina Masenza, Mkuu wangu wa Mkoa pale Iringa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Mheshimiwa Makonda yeye ndiyo abebe bango na chombo kikubwa ambacho kinatakiwa kifanye kazi hiki kikae kimya. Ningeomba haya mambo Serikali ijaribu kufafanua, kwa sababu haya ndiyo mambo ambayo yanasababisha utengamavu na utulivu wa nchi yetu upotee bila sababu. Mtoto aliyehongwa na mama yake huwa tunamuita mummy’s boy au mummy’s girl lakini inaonekana Makonda labda ningemuita daddy’s boy. Kwa sababu anaweza akasema chochote anachotaka wakati wowote hajui na mipaka yake, hii inaweza ikatuletea matatizo katika nchi yetu. Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Makonda siyo mtaalam wa mambo ya uchunguzi. Mwenyekiti wangu wa Kamati umekaa kwenye kitengo hicho utaweza kutusaidia. Polisi wamesomea, wanaweza kufanya investigation ya mambo haya, sasa watu wote tumekaa kimya nchi hii where are the lawyers? tuna Tanganyika Law Society,where are thelawyers, tunapoona mambo yanaenda vibaya tumekaa kimya. Where are thejudges hatuoni Majaji wakitoa matamko kuonesha kwamba kila mtu akae kwenye msimamo wake ili nchi yetu iweze kuwa na utulivu na amani, watu wote wamekaa kimya, tunalipeleka wapi Taifa ambalo kila mtu akiamka asubuhi anaamua kufanya jambo analolitaka na wachungaji wamekaa kimya, lakini wengine tunaona wakipewa zawadi wanasema at least mimi nasema hapa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana kuna checks and balance, wahenga/wataalam wa mambo ya utawala walivyoamua kuweka mihimili mitatu hawakuwa wajinga, waliona anaweza akatokea kichaa mmoja akaamua kufanya anavyotaka, Bunge letu hili lipo kwa ajili ya kazi hiyo mambo yanapokwenda hovyo lazima tusimame kama muhimili kumrudisha nyuma yule anaekwenda vibaya na maamuzi tuliyoyafanya. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, my question is where are the judges in thiscountry and where are the lawyers, tunawasomesha kwa gharama kubwa wanasoma sheria ili iweje? Lengo tunataka tukae katika nchi yetu kwa usalama na haki. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ripoti hii imezungumza vizuri sana juu ya jinsi ambavyo amani inaweza kutoweka. Lakini kwa sababu ya muda ninataka kusema Bunge hili kwa sababu ya kutokujua au kwa makusudi tulitoa maamuzi ambayo mengine ni ya hovyo katika nchi yetu, ni wakati sisi kama watunga sheria na muhimili ambao ni wa muhimu katika Taifa letu tufike mahali tujitafakari. Kwa mfano, tulipitisha sheria ambayo inaminya upatikanaji wa habari ambayo inawasaidia watu wachache, hii sheria tulipitisha hapa lakini mwisho wa siku itatugeuka ni kiashiria ambacho kinaweza kikasababisha tuvunje amani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile Bunge letu hili ambao ni muhimili muhimu katika taifa letu limekosa uhuru, limekuwa ni Bunge ambalo linaminywa, hatuwezi kuikemea Serikali tena, why are we here? Mheshimiwa Mwenyekiti, tupo hapa kufanya nini kama hatuwezi kuidhibiti Serikali na tunapoidhibiti Serikali siyo maana yake tunataka kuiangusha, tunataka itembee katika mkondo wake ili amani yetu itulie na ndiyo kazi ya Bunge. Kazi ya Bunge ni kuidhibiti na kuisimamia Serikali ienende kama inavyopaswa. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mwenzangu hapa ametoa mwongozo tunaye Katibu wa Bunge hapa anayetakiwa atuongoze tunapokaa hapa; sasa leo anaenda kwenye vyombo vya habari anasema Bunge limekosea. Na yeye anafanya kazi yetu ya Bunge hatujaajiriwa na yeye hapa with duerespect, anafanya kazi ya Bunge hajatuajiri yeye sisi hapa; anatakiwa afuate maagizo yetu. Na ana wataalam wanaotushauri anatakiwa atuelekeze where are we heading? Haya ni masuala tunahitaji tujadiliane siyo kwa kugombana ni kwa kujadiliana wote kwa pamoja. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine la pili ni Serikali kupiga marufuku vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara, huko ndiyo tunaweza kuona mambo mengi ambayo yanaenda hovyo, tukaongea kwa uhuru, tukaisaidia Serikali ienende vizuri. Haya mambo tunakaa kimya tunashangilia mtu mmoja anaamua halafu tunakaa kimya watu wote, where are we heading? (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine Asasi za Kiraia zikijaribu kuzungumza nazo zinazuiwa na zinakatazwa, haya ni masuala ambayo tunapaswa tujiulize tunakwenda wapi. Ni maoni yangu kwamba ni vizuri tukasonga mbele na ni vizuri tukatafakari kama Bunge, je, tunafanya wajibu wetu, tunatimiza wajibu wetu kama muhimili? MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa, dakika moja tu.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho niseme hii nchi yenye Bunge kibogoyo, TAKUKURU kibogoyo, vyombo vya habari bubu, NGO bubu na siasa bubu, polisi kibogoyo na National Drug Control kibogoyo, hatuwezi kuepusha michafuko katika nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe wote kwa pamoja na kwa kumalizia dakika ya mwisho kabisa mchungaji mmoja kule Ujerumani wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia aliwahi kusema; “Silence in the face of evil it is evil itself, God will not hold us guiltless not to speak is to speak, not to act is to act.” Kwa hiyo, hatupaswi tukae kimya katika haya mambo haya mabaya, ningewaomba Wabunge tushirikiane wote kwa pamoja tuulinde muhimili wetu, nashukuru sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Baada ya kumaliza uchaguzi wetu wa nchi mwaka 2015, mlishangilia kwa mbwembwe nyingi sana kwamba Serikali na Chama cha Mapinduzi mmeshinda kwa kishindo, mkawaaminisha Watanzania kwamba mnaweza kuongoza nchi hii. Watanzania wakawasikiliza, mkaunda Serikali yenu. Tukaja Bungeni hapa tukaapishwa. Siasa za nje tukazileta Bungeni na ndiyo maana hivi vipaza sauti vimewekwa hapa kwa ajili kuzungumza. It is about talking! Ni juu ya dialogue hapa Bungeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali mnakuja na hoja zenu mnaendelea kuwashawishi wananchi kwamba sisi tuna uwezo wa kuongoza nchi hii, mnaleta hoja. Nasi tuliowapinga tunakuja na hoja zetu kuwakatalia kwamba hizi hoja haziwezekani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa leo hii Serikali inayosema ni ya Hapa Kazi Tu, Wabunge 250 wa Chama cha Mapinduzi na Serikali yao inashindwa kujibu hotuba ya kurasa 34! Inataka kuwaambia nini Watanzania? Kama kurasa ya 34 Wabunge 250 wa Chama cha Mapinduzi wanaogopa isisomwe, ninyi ni mature wa kuongoza nchi hii? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yetu tunakuja hapa tuna-dialogue, sisi ndivyo tunavyoiona Serikali, tunaoliona Jeshi la Polisi linafanyaje? Mikataba ya hovyo ikoje? Mtazamo wetu wa pili kwenye view yetu, this is how we see. Njooni na hoja mwoneshe udhaifu wetu uko wapi? Muwaaminishe Watanzania kwamba we are not matured. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kabla hatujaendelea, hatujazungumza, mnaweka mpira kwapani, mnataka msaidiwe na marefa. Suala la kujiuliza, you guys are you fit to lead this country? Kama hotuba ya ukurasa 30 hamwezi kuijibu, nani asiyejua mizengwe ya nyumba zilizouzwa katika nchi hii? Nani asiyejua nchi hii ina mikataba mibovu?
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Ambaye anatakiwa ashangiliwe kama King Kanuti, hatakiwi kuguswa katika Bunge hili. Nirudie maneno aliyozungumza Mheshimiwa Sugu; huyu Rais Mwema mnamfanya wananchi wasimwelewe. Yeye siyo Mungu, ana hali ya ubinadamu anaweza akakosea. Lengo letu hapa tupo kuisaidia Serikali na ndiyo dhana nzima ya kuwa na mfumo wa vyama vingi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wamezungumza wenzangu hapa jinsi ambavyo mnawatumia Polisi, wakati wa uchaguzi mnawapa majina mazuri yote, lakini maisha wanayoishi ni ya shida sana. You are just using them! Mnawatumia wakati wa uchaguzi. Nawaomba ndugu zangu na niseme nyie mnaosema usalama wa nchi hii ni sababu ya ulinzi na usalama wa Jeshi la Polisi.
Mimi kama Mkristo na Mchungaji, Biblia inasema, Mungu asipoulinda mji, wakeshao wafanyakazi bure.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba utunze muda wangu tafadhali. Narudia tena, Bwana asipoulinda mji, wakeshao wafanya kazi bure! Biblia inasema mji haulindwi kwa wingi wa silaha anazokuwanazo mfalme. Ni Mungu ameamua ku-sustain amani ya nchi hii. Kama tutaendelea kucheza kwa kuamini kwamba bunduki na vifaru vitalinda amani ya nchi hii, tunapoteza muda. Ulinzi wa Muammari Gaddafi ulikuwa ni mkubwa kwa mbali kabisa kulinganisha na ulinzi wa nchi hii; lakini yuko wapi leo? Bwana asipoulinda mji, wakeshao wafanya kazi bure? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba Jeshi la Polisi, msitumike vibaya kisiasa, nchi hii ni ya mfumo wa vyama vyingi, sisi hapa hatujaja kwa fedha, tumekuja hapa kwa merit. Tuna haki hizo! Mnabambika watu kesi! Kama Mbunge, mimi nimebambikwa kesi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siku ya uchaguzi, kulikuwa kuna yule Mungi sasa mmempandisha cheo ameenda bandarini. Ameagiza Polisi wanakuja kunivamia, wamepiga watu, wamevunja miguu, mikono, mwisho wa siku, wiki mbili zimepita sipelekwi Mahakamani mpaka nikaanza kudai na Wakili wangu kwamba mmetupiga, wakatulaza kwenye bwalo wanawake na wanaume! Mimi ninayezungumza! Tunadai kwa nini hamtupeleki Mahakamani? Napelekewa charge eti wewe umemjeruhi Kamanda wa Field Force. (Makofi)
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mimi Msigwa namjeruhi Kamanda wa Fied Force; na la pili nimejeruhi gari la Polisi. Kesi imekwenda Mahakamani wiki mbili, imefutwa; haina mkia wala miguu. (Kelele/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaomba Jeshi la Polisi, hebu acheni kutumika kisiasa. Tupo kwenye nchi ya vyama vingi. Kazi yetu kubwa hapa ni kuiweka Serikali sawasawa mwone wenyewe, nanyi Makamanda wa Polisi mnaona jinsi gani Serikali inashindwa kujitetea hapa! Kurasa 34 wanashindwa kujibu, they cannot! Nchi imejaa hofu, watu mmejaa hofu, huyu Rais mwema sana amewatia hofu mnaogopa kujitetea na kusema. Why? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Plato anasema: “if you cannot die for something, you are not worth living.” Sisi tupo tayari kwa lolote kwa sababu tunataka tuinyooshe nchi kwa faida ya vizazi vijavyo; na wajibu wetu ni kuikosoa Serikali, kuiweka vizuri. Haya tunayoyashauri, mangapi tuliwashauri? Tuliwashauri jambo la Katiba, mkalichukua, ila kwa sababu hamna ubongo wa kuku, mkashindwa. Si mlishindwa! Tuliwashauri, mkachukua. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliwashauri suala la elimu bure, mmejikanyagakanyaga, mnashindwa na yenyewe. Mngetupa hapa, hiki ni kisima cha kupata hekima na busara tunataka tuwashauri. You are incapable of leading this nation. Hapa ni mahali pa ku-dialogue. Ambao hamjasoma historia, nendeni Ugiriki mkaangalie Wagiriki walikuwa wanafanyaje kule Heathen. Unakuja na hoja unazijenga! Tumehamisha siasa kule, hapa ndiyo tunajadiliana, njooni na hoja. Sasa mmetunua macho, hamwezi kujitetea, mnajaza hofu watu, wafanyakazi na watu wote wana hofu, tutaendeshaje nchi hii? Bunge mmelifunga, halisikikii, humu ndani mnataka kutu-paralyse, sasa hiyo siasa tutafanyaje?
MHE. PETER S. MSINGWA: Ila saa hizi ni watu ambao hawaaminiki hata huko msiwaamini, hawaaminiki, saa hizi wanajikosha kusema sema maneno mazuri hapa wanawadanganya, tulikuwa nao usiku, waongo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, muda ukifika muafaka tutawataja, walikuwa wanatuletea na hela za kampeni sasa leo hapa wanajifanya wanadanganya danganya wanatuzunguka waongo, ni wanafiki hawa, hawawafai hata ninyi na hawa hawaifai hata Serikali kuwepo kwa sababu wata… (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Msigwa.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu zinaonyesha kwamba toka mwaka 1980 mpaka 2010 Afrika pamoja na resources tulizonazo tumepoteza kiasi cha dola trilioni 1.4. Takwimu hizi zinaonyesha hii yote imesababishwa na uongozi mbovu katika Bara la Afrika. Mojawapo ya sababu ni
kutokuwepo mwendelezo wa viongozi wanapobadilishana madaraka. Nchi yetu katika Serikali hii ya Awamu ya Tano kumekuwa na changamoto kubwa sana ambazo takwimu hizi zina-cement kwamba na sisi kama Taifa tunaweza tukaendelea tena kupoteza mali tulizonazo kwa sababu ya tatizo la uongozi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Mtawa mmoja wa Kikatoliki aliishi miaka 1953 kule Marekani anaitwa Bishop Sheen, aliwahi kusema; “Civilization is always in danger when those who have given the right to command have never learned how to obey.” (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu iko kwenye kiza kinene kwa sababu kuna watu wengi sana ambao wamepewa mamlaka ya kuamrisha lakini wao wenyewe hawajawahi kujifunza namna ya utii. Nazungumza haya kwa masikitiko makubwa sana kwamba tatizo kubwa tulilonalo
katika Serikali ya Awamu ya Tano ni poor leadership skills ambayo hii inaweza ikatupelekea tukaingia kwenye matatizo makubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri amezungumzia sana masuala ya Chuo cha Uongozi, lakini nina wasiwasi sana kama hiki chuo kina mtaala wa namna ya kuwa-train hawa watu. Kwa bahati mbaya katika nchi yetu uongozi unakuwa defined kwa title au status badala ya
function. Uongozi wa sasa hivi tulionao wa Awamu ya Tano ni uongozi ambao ni bully, ni uongozi ambao ni una-scream, ni uongozi ambao una-shout, ni uongozi unao-intimidate badala ya kuonyesha njia. Kwa sababu ya uongozi huu umeparalyze civil service na tuki-paralyze civil service maana yake itashindwa ku-produce. Watu wako intimidated na uongozi huu hauko based kwenye merit kwa sababu watu hawajawa
trained.
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini utanitunzia muda wangu lakini na wewe mwenyewe umechanganya actually, sasa sijui hapo umesemaje, sijui ni Kiswahili hicho?
Mheshimiwa Naibu Spika, katika society ambayo nimeritocracy the blind cannot lead the sighted, uninformed cannot lead the wise and the unskilled cannot direct the skilled. Katika uteuzi wa Mheshimiwa Rais, amechukua makada wengi wa Chama cha Mapinduzi amewaingiza
kwenye civil servant ambayo hiyo ina-cripple utendaji wa kazi. Haya mambo hatuwezi kuyanyamazia kwa sababu hili Taifa ni la wote na ni kinyume kabisa na utaratibu. Ndugu zangu wote tukumbuke hapa tunapokwenda kwenye uchaguzi watu wote sisi tunakuwaga hatuna madaraka sisi wanasiasa, huwa wanabaki civil service, ukii-cripple civil service maana yake unaua utendaji kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nimshauri tu Mheshimiwa Rais ambapo wenzangu wengi wanaogopa sana hata kumshauri, maana yake Mheshimiwa Rais akisema mkikamata watu wanavunja sheria ng’oa matairi kuna watu wanapiga makofi kinyume cha taratibu. Mheshimiwa Rais akisema mimi sikuleta matetemeko wanapiga makofi.
Mheshimiwa Rais akisema mkikutana na jambazi huko hata kabla hajapelekwa mahakamani kinyume cha sheria watu wanapiga makofi, wanadhani kumsifu Mheshimiwa Rais kwa kile anachokifanya ni uzalendo. Tunatengeneza Taifa la waoga ambapo tuna cripple national kama hatuwezi kucriticise viongozi wetu. Tuko hapa kuwafanya viongozi wetu wawe accountable na ndiyo wajibu wetu, (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Thomas Jefferson, Rais wa Marekani aliwahi kusema ukiona wananchi wanaiogopa Serikali jua Serikali hiyo ni ya kidikteta. Ukiona Serikali inawaogopa wananchi jua Serikali hiyo ni ya kidemokrasia kwa sababu Serikali lazima iwe accountable kwa wananchi.
Sisi hapa kama Wabunge tuko hapa kuwawakilisha wananchi, the government must fear us. Serikali lazima ituheshimu sisi kwa sababu lazima iwe accountable kwetu.
Leo tunafika Bungeni tunanyamazishwa eti tusiikemee Serikali, why are we here? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi kama kiongozi, wewe kama kiongozi you are accountable to us, Serikali mko accountable kwa Bunge hili. Sasa kila kitu mna-protect, chochote mnachofanya mna-protect, Serikali ya Awamu ya Tano imekuwa ni ku-scream, shouting. Huwezi kujua leo ni msiba au leo ni harusi, huwezi kujua leo wako kwenye matatizo, leadership is about inspiring people, putting people to work is not about screaming and shouting. Tuna uongozi wa Awamu ya Tano ambao una-shout, una-scream unaintimidate everybody kwa hiyo ume-paralyze watu kufanya kazi. Halafu wengine wasomi hapa na ninyi mnakaa kimya mnapiga makofi mambo ambayo ni kinyume na utaratibu wa sheria ya nchi yetu, where we heading? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, the unskilled cannot direct the skilled. Tumekubali kuweka akili zetu mfukoni tunaongozwa na wale ambao ni unskilled. Leo tuna watu kama akina Bashite amesema Sheen hapa, those who have never learned how to obey they have given the right to
command, mtu kama Bashite anachokijua ni kuvaa shati la kijani na kumtukana Lowassa, ndicho alichoweza. Leo anakuwa Mkuu wa Mkoa anatoa amri kubwa halafu tunampigia makofi. Wale ambao ni incompetent wanawaongoza competent, kwa hiyo, utendaji kazi
unashuka wanaona sasa hata maana ya kusoma haipo. Kwa hiyo, mtoto yeyote anachoona ili niwe kiongozi ni kujua kumtukana mtu mmoja wa chama kingine, wapi tunakwenda jamani?
Mheshimiwa Naibu Spika, tuna wanasheria kwa mfano Mwanasheria Mkuu hapa, wajibu wake mkubwa yeye ni kuhakikisha Serikali inafanya kazi lakini na yeye amegeuka amekuwa Mbunge anatetea Serikali. Badala ya yeye kunyoosha akiona Serikali inakosea anasema Chief Whip
hebu ili jambo tu-withdraw tukajipange vizuri kwa sababu yeye ni kuweka mambo vizuri mwisho wa siku huu ni mtumbwi wa sisi wote lakini kilichotokea ni kati ya upinzani na sisi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mtaalamu mmoja anasema Taifa ambalo linazalisha soft minded people linanunua kifo kwa installment cha Taifa lenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu mnadiscourage criticism katika Bunge, mna-discourage dialogue mnataka tuwe tunapiga makofi, why are we here? Kama mngetaka tusije hapa mngetuzuia kule kule Iringa wakati wa uchaguzi, the fact kwamba watu wa Iringa wamenileta
hapa I will speak, I will talk.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo tuna TISS (Usalama wa Taifa) ambapo kazi yake kubwa ni ku-protect Chama cha Mapinduzi badala ya ku-protect nchi. Ukija kwenye Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi robo tatu utawakuta watu wa TISS wamevaa nguo za kijani, they are busy na Chama cha Mapinduzi. Tunazungumza hapa kuna mauaji, utekaji lakini ni kwa sababu wameacha mambo ya msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, in this country kila mtu anaweza akafanya jambo lolote. Jeshi linaweza likakusanya kodi na bunduki, leo tunakusanya kodi na bunduki (with guns). Hujui nani anafanya nini na kwa ajili ya nini ni kwa sababu nchi haina priority, poor leadership.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe ndugu zangu hebu tujipange Serikali ni ya kwenu, tuji-reorg, tujipange vizuri kwa sababu ni kama ubongo ambao uko scattered, you are every where, there is no priority. Mara tunaenda Dodoma, mara leo Bashite anakamata sijui watu gani, mara huyu ametumwa nini na kwa sababu hatuna priorities hatujui tunataka kufanya nini. Ni kama vile wataalamu hawapo katika nchi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunatoa mawazo yetu lengo ni kuifanya Serikali yetu iwe nzuri. Tume-discourage fikra ambazo zina criticize kwa sababu hakuna mtu ambaye hawezi kuwa challenged katika ulimwengu huu. Kuwa challenged ni sehemu ya uongozi ili ujipime, sisi ni mirror yaani sisi ni kioo chenu huwezi kwenda kwenye kioo nywele hujachana unakipiga ngumi kioo sasa utajionaje, mnatupiga sisi sasa mtajionaje?
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi ni kioo chenu tunawaona hivyo mnavyofanya, wote mmekuwa waoga (terrified). Mawaziri wote mko-terrified hapo, Wabunge mkoterrified tukitoka huko nje ndiyo mnatuambia ee bwana lakini hapa mnasema kweli na wengine nikitoka nje mtaniambia
lakini humu ndani hamsemi.
Mheshimiwa Naibu Spika, niombe Usalama wa Taifa wafanye kazi yao vizuri. Tumezungumza mauaji hapa sina muda wa kusema, baada ya Wabunge kusema kuna watu wako-tortured sana kule Mpingo wanafungiwa kwenye kachumba kadogo, wanakojoa humo humo, wanajisaidia
kwenye rambo wanateswa halafu wakionekana hawana hatia wanawadampo kwenye kituo cha mabasi pale wengine wako kwenye Jimbo langu toka Iringa wanaachwa na nauli tu. Hatuna muda wa kusema tu lakini haya mambo yapo watu wanakuwa totured tukisema hamtaki kusikia.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuturudisha tena Bungeni salama na ninaamini maneno ya Mheshimiwa Spika kwamba ulinzi utakuwa salama katika maeneo yetu ya Dodoma.

Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango nadhani kama Wabunge tumekushauri kuhusiana na jinsi ambavyo mliamua kutoa vyanzo vya mapato (own source) kwenye Halmashauri zetu ambavyo kimsingi vimeathiri sana maeneo mbalimbali. Kwa mfano, mlitoa ile property tax Manispaa yangu ya Iringa tulikuwa tukijiwekea bajeti ya kukusanya shilingi milioni 700 lakini hela iliyorudi kutoka TRA ni shilingi milioni 182 na hatujapata maelezo, TRA hawana hiyo capacity, hawana manpower ya kukusanya hiyo hela wakati sisi tulikuwa tunakusanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile mmechukua hela ya mabango ambayo tulikuwa tumejipangia kwenye bajeti kukusanya karibuni shilingi milioni 357, hiyo hela bado haijapatikana na kwa kukosekana kwa hela hii, tumeshindwa kutengeneza chumba cha uchunguzi katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Frelimo, tumeshindwa kujenga wodi ya wagonjwa katika eneo linaitwa Itamba katika Manispaa yangu, na hizi ni athari ambazo tulizisema toka mwanzo kwamba tulikuwa na uwezo wa kukusanya baada ya nyinyi kutoa hivi vyanzo mme-cripple maendeleo yetu kama Manispaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni mifano inawezekana na wenzangu kwenye maeneo yao kuna matatizo kama hayo, ningeomba kama inawezekana katika mpango huu mngerudisha hivi vyanzo vya mapato vibaki katika maeneo yetu. Ninavyozungumza Manispaa yangu ya Iringa ni moja ya Manispaa bora kabisa mpaka maeneo mengine wanakuja kujifunza namna ya usafi, namna ya kupanga Mji, lakini mkiendelea kutu–cripple namna hii mtaturudisha nyuma, nadhani hata Naibu Waziri alikuwa DC pale anajua jinsi Manispaa ya Iringa ilivyo nzuri, ikiongozwa na CHADEMA katika Mkoa wetu wa Iringa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite katika eneo moja kubwa, katika kitabu chako ulichotuletea ukurasa wa 35 umezungumzia kuhusu utawala bora. Kwangu hayo uliyoyazungumza kwenye utawala bora naweza kusema hii ni hardware hujazungumza software. Utawala bora niliotaka uzungumzie wewe umezungumzia kuhusu mahakama ambazo zitajengwa ambazo zinataka kujengwa, kwangu mimi hiyo ni hardware. Mimi nataka tuzungumzie component, characteristics za utawala bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili nchi yetu iweze ku-flourish lazima utawala bora uonekane kwa vitendo. Katika hotuba ya Kambi ya Upinzani ukisoma ukurasa wa tatu tumezungumza vizuri sana, naomba ninukuu: “Misingi ya uwajibikaji katika kutekeleza mipango ya maendeleo ipo kikatiba na kisheria. Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ya mwaka 1977 inalipa Bunge mamlaka ya kujadili na kuidhinisha mpango wowote wa muda mrefu au wa muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya Muungano na kutungia sheria.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kuwa na mipango mizuri kama Serikali yenyewe haiko accountable, inakwepa accountability. Kipindi cha nyuma Serikali ilikuwa inapaswa iwe inaleta namna inavyotekeleza bajeti kila baada ya miezi mitatu, juzi hapa tumepitisha sheria ambayo asubuhi leo tumeambiwa kwamba imeshapitishwa kwamba tutakuwa tunaletewa utekelezaji wa Serikali kila baada ya miezi sita, na sasa hivi tumeshaanza mpango wa mwaka unaokuja wakati utekelezaji wa Serikali muda uliopita hatujaupata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutakuwa hatuna uwezo wa kusema tunaisimamia Serikali kama Serikali yenyewe inakwepa accountability. Nasema hivyo kwa nini, mfano mzuri kama tunapanga vizuri matumizi yetu ya fedha Waziri wa Maliasili ambaye amebadilishwa juzi alikuja Iringa kule tulikuwa tunahamasisha mambo ya utalii huku Southern Circuit na mojawapo ya mambo ambayo tuliyajadili ilikuwa ni pamoja na kuuboresha uwanja wa Nduli kwa sababu Iringa imekaa ki- strategy.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mbuga ya wanyama ambayo tuna-attract watalii na maeneo mengine, tukazungumzia kuhusu barabara, lakini kwa sababu Serikali haitaki kuwa accountable, imechukua hela ambazo hazikuonekana popote kwenye vitabu vyako ulivyotuletea hapa ikaenda kupeleka Chato shilingi bilioni 39 mnajenga uwanja wa ndege Chato, mnaacha mahali kama Iringa ambapo pamekaa kimkakati na Wizara ya Maliasili wamesema pale pamekaa kimpango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano inaonekana ni ya ubinafsi mkubwa sana, Mwalimu Nyerere angekuwa mbinafsi..

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa yake naipuuza na kama ninavyompuuza mwenyewe, siichukui. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumzia Chato, nimezungumza mipango kama tuna-synchronize, Iringa imekaa kimkakati kwamba tukijenga kiwanja cha ndege kuna tija tutakayoipata kutokana na kiwanja cha ndege. Kujenga kiwanja cha ndege Chato tunataka tupate nini? Tulikuhoji muda uliopita hatukupata majibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Tano inaonesha ubinafsi wa hali ya juu, kama Mwalimu Nyerere angefanya hivyo Musoma ingekuwa Ulaya, lakini Mwalimu alikuwa anafanya mambo kimkakati, hatuwezi kusema tunataka tujenge, tupanue uchumi wa viwanja kwa upendeleo wa namna hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, hili la Serikali inatakiwa ilete matumizi ndiyo dhana nzima ya Wabunge kuwepo hapa, tukiua dhana nzima ya Bunge kuisimamia Serikali, Bunge linakuwa halina maana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jana nimezungumza kwenye briefing nimesema ukisoma historia kwa wale wanaosoma historia, nenda Ufaransa, nenda Uingereza, kwa nini waliwaua wale wafalme? Ni kwa sababu kodi yao walikuwa wanaitumia pasipo kusimamiwa, Bunge likaanzishwa ili liwe ni mlinzi wa Serikali. Sasa vifungu vyote hapa tumenyofoa kwa maana ya kwamba tunali-cripple Bunge, Serikali inaanza kujifanyia kama inavyotaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hazina ya nchi hii siyo mali ya mtu mmoja. Hazina ya nchi hii ni mali ya Watanzania na sisi ni tax payer representative, tukiacha kuisimamia Serikali ifanye inavyotaka tuna deceit the whole purpose ya kuwa na Bunge. Bunge siyo kuja kuvaa suti hapa, Bunge ni kuisimamia Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unapozungumzia good governance kuniambia kumejengwa mahakama, nimezungumza hiyo ni hardware, components za good governance kuna accountability. Serikali ya Awamu ya Tano inakataa accountability, haitaki kufuatiliwa, hamtaki tujue mmetumia kiasi gani na kuwepo kwa Bunge ni kutaka kujua Serikali imetumia kiasi gani na imetumia kama tulivyopanga kwa mujibu wa sheria. Kwa hiyo, hauwezi kuniambia good governance hapa kama hatuwezi kufuata sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Awamu hii ili tuzijue characteristics of good governance unaweza uka-google tusaidiane haya ninayoyasema, hii ni UNDP ilitoa mwaka 1997, inasema lazima kuwe na participation. Mme-cripple Halmashauri ambazo ndiyo hela zikienda kule chini wanashiriki watu kuanzia chini, sasa hakuna hela, wamekuwa crippled.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima kuwe na rule of law, good governance, human rights, democracy. Katika nchi hii hakuna democracy, watu wakitaka kuzungumza, wakitaka kuhoji wanakataliwa, tunawezaje kuutekeleza Mpango huu kama haya mambo hayapo? Ili Mpango uweze kutekelezwa ni lazima haya mambo yawepo nazungumzia good governance. Hii good governance it is not about Upinzani tu, good governance ni kwa wote, kwenye maeneo ya Manispaa zetu wote, haya mambo hayapo, ukienda mbele inasema hakuna upendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, asubuhi Naibu Waziri anajibu hapa maeneo mengine wanaambiwa kwamba ninyi kwa sababu mlinipa kura hamtabomolewa, maeneo mengine ma- bulldozer yanaenda yanabomolea watu, kutakuwa na good governance hapo?

KUHUSU UTARATIBU . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nasoma good governance, kuna utawala bora kwenye hiki kitabu, kwa hiyo nimejikita hapo na haya maneno ninayozungumza Waziri alisema hivyo, mimi nayanukuu maneno aliyosema Rais alipokuwa Kanda ya Ziwa alisema ninyi hamtabomolewa kwa sababu mlinipa kura. Nimesema kwenye characteristics za good governance lazima kusiwepo na upendeleo. Ukienda Kimara, ukienda Tabora huko bulldozer yanapita yanabomoa nyumba kwa nini tunajitoa ufahamu? (Makofi)

Kwa hiyo Mheshimiwa Mhagama anaongea kitu kingine mimi nazungumzia nukuu za Mheshimiwa Rais alizosema, jamani hamkusikia haya mambo? Ndiyo ninayoyazungumza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo la kunajisi Bunge nalitoa, lakini mtuambie kama hatuwezi kumnukuu Rais, Rais hatuwezi kumnukuu?

Mheshimiwa Rais alisema waliojenga kwenye mito wasiondolewe wakati Mwenyekiti wetu hapa mmebomoa kwake, sasa tusiseme haya maneno? Haya ndiyo nayasema good governance, hii hela tunayoitoa hapa ni pamoja na kuhakikisha Polisi wanafanya kazi vizuri, Usalama wa Taifa wanafanya kazi vizuri. Ninachosema, tulipata taarifa kwenye vyombo vya habari kwamba wale waliompa kura watasamehewa na wengine watabomolewa. Huo ndiyo msimamo wangu, hiyo haikataliwi.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri wa Mipango, kama kweli tunataka mipango hii itekelezwe lazima tuwe na good governance. Tuko kwenye nyakati ambazo usalama wa raia hauko vizuri, tuko kwenye nyakati ambazo watu hawana uhakika na maisha yao, kwa hiyo, tunapozungumzia kupanga mipango mwenzangu Mheshimiwa Bobali amezungumza hapa kwamba tusije na kauli tu kwamba sasa hivi tunasema viwanda. Utawala uliopita wa Awamu ya Nne ilikuwa Big Results Now ambayo imevunjwa juzi juzi na niliwahi kusema nilikuwa hapa hapa, nikasema Big Results haitatokea kwa sababu tu ya kubandika vibao kwamba Big Results, milango yote ya Halmashauri iliandikwa Big Results, lakini hiyo Big Results haikuonekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haikuonekana! Mbona ninyi wenyewe mnaiponda Serikali iliyopita! Leo tumekuja na kelele za viwanda, kuwa na viwanda ni jambo jema hakuna mtu anayekataa. Lakini kama alivyosema Mheshimiwa Bobali, hivi viwanda lazima tuwe na mipango mkakati, lazima tuwe na maeneo ambayo tunaamini yatatusaidia kuleta mipango mikakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia, nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kumlinda Mbunge mwenzetu ambaye alipata mateso makubwa sana kwa hawa watu wanaoitwa wasiojulikana. Kwa masikitiko makubwa wale wahalifu, wale ambao walikuwa wapo tayari kutoa uhai wa mwenzao kwa matakwa yao ambao hawajulikani mpaka leo ambao siyo mhimili huu, siyo Serikali, siyo Mahakama sijaona zimepiga kelele za kutosha kwa kitendo kibaya alichofanyiwa mwenzetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba Wabunge wote kwa umoja wetu tusikubali mateso aliyoyapata mwenzetu miongoni mwetu yeyote aje ayapate kwa sababu ni kitu ambacho Mungu hapendi. Sisi sote hapa ni ndugu, mwisho wa siku tunaijenga Tanzania, tusimame wote kwa pamoja kulaani. Waasisi wa nchi hii hawakutufundisha mambo yanatokea sasa hivi katika nchi hii. Kuona maiti kwenye viroba, kupigana, kuchukizana, kununiana, haya mambo hatukujifunza, tunayaona katika Awamu ya Tano haya mambo yanachipua, tuyakatae wote kwa pamoja kama Bunge ili kwa pamoja tushirikiane, tuhakikishe nchi ya viwanda tunayoitaka, tuweke mikakati ambayo tutakubaliana wote kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati nzuri nikiwa kama Waziri Kivuli nimefanya kazi na Mawaziri wanne. Nimefanya kazi na Mheshimiwa Maige na huyu ni Waziri wa nne. Nakumbuka mara ya mwisho nilivyochangia hotuba hii nilikuwa nimetoa ushauri kidogo kuhusiana na Wizara hii hasa Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla alipoingia kwa mara ya kwanza. Napoanza nina maswali machache sana ambayo ningeomba Waziri ayajibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Waziri alipochukua tu Wizara alituhumu watu kwamba walikuwa wanachukua fedha kwenye Kampuni ya OBC, kwenye migogoro ya Loliondo na kwamba yeye hapokei rushwa. Hata hivyo, hivi karibuni nimeona Wizara yake imepokea magari, nilitaka kujua yeye amepokea shilingi ngapi maana alisema wataondoka mwaka huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, Waziri alinituhumu na mimi mwenyewe kwamba mimi pamoja na Nyalandu ni mafisadi. Pia alisema katika Bunge hili ataleta hizo taarifa za ufisadi, ningeomba aziweke hapa maana tusiharibiane majina bila sababu ili anavyoongoza Wizara yake tuwe vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii naamini Mheshimiwa Rais alipompa Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla ambaye ni kijana na Bunge lililopita tulikuwa naye, aliona misukosuko mingi ambayo Wizara hii imepitia. Mheshimiwa Zakia Meghji ndiye pekee aliyekaa katika Wizara hii kwa muda mrefu wa miaka tisa, Mawaziri wengine wote wamekuwa wanakaa miaka mitatu, miwili au mmoja wanaondoka. Nilitegemea Waziri atamsaidia vizuri sana Rais lakini kwa bahati mbaya baada ya kuingia ofisini kumetokea migongano mingi sana ndani ya Wizara hii ambayo ni uhai wa Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachonisumbua, katika Kamati yetu ambapo mimi ni Mjumbe wa Kamati hii tumezungumza matamko ambayo umeyatoa hasa katika sekta ya uwindaji ambayo yameathiri sana sekta hii. Katika vile vitalu vya uwindaji ambapo 18 vimeondoka na sasa hivi ni zaidi ya vitalu 81 viko wazi. Ukiangalia toka vitalu hivi vimegawiwa tasnia hii imekuwa ikichangia pesa nyingi katika Taifa letu. Kwa matamko yako Waziri umeondoa confidence ya wawekezaji jambo ambalo lina athari kwa sababu Serikali haina pesa za kutosha za kutunza mazingira katika vitalu hivi. Serikali haiwezi kutengeneza barabara za kwenye vitalu, haina uwezo wa kuzia anti-poaching ambapo katika Awamu ya Nne baadhi ya Mawaziri nikimchanganya Mheshimiwa Kagasheki na Mheshimiwa Nyalandu walifanya kazi kubwa sana kuleta wafadhili kuzuia anti-poaching katika nchi hii. Matamko ya Waziri yamesababisha hawa watu waondoke na yanaleta tabu katika mapori hayo na kusababisha mapori yale yaingiliwe na watu wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kujua kuna mkakati gani wa makusudi wa kushughulikia matamko haya ambayo yalikuwa hayana uangalifu na yametuletea hasara katika tasnia hii? Waziri kijana ambaye tunategemea awe visionary atuambie hapa ana mipango gani zaidi kuliko matamko aliyoyatoa? Hilo ni suala la kwanza ambalo lazima liangaliwe vinginevyo kama Kamati ilivyosema tunaua tasnia hii.

Mheshimiwa Mwwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kuzungumza ni hawa wasafirishaji wa nyama. Takwimu ninazo hapa zinaonesha jinsi ambavyo Serikali inatumia pesa nyingi sana kwa mfano kuwaua ndege. Kila mwaka Wizara ya Kilimo huwa inaua ndege zaidi ya milioni 70, hawa kweleakwelea. Hawa watu huwa wanasafirisha ngedere na tumbili wanawapeleka huko nje. Nililalamika kwenye Wizara hii mpaka mtendaji mmoja mzuri sana katika Wizara alikuwa anaitwa Mulokozi aliwekwa ndani kimakosa mpaka akafariki, kuoneaonea watu tu kwa makosa ambayo hawakufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri amezungumza kwenye hotuba yake, time frame itakuwa lini ili hawa watu walipwe pesa zao kwa sababu wanaishi katika mazingira magumu. Hawaachi kuja hapa Bungeni kutaka wasaidiwe kwa sababu kwa kweli tumewa-cripple na Serikali haipo kwa ajili ya ku-cripple watu, hawa watu wa TWEA naomba hili suala lao liangaliwe kwa mapana kwa sababu kwa kweli wanapata tabu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo nataka nizungumze katika Wizara hii ni matangazo. TANAPA pamoja na Ngorongoro wamekuwa wakifanya kazi kubwa sana lakini Serikali imechukua kodi za matangazo ikapeleka Serikali Kuu ikayatoa kwenye maeneo yake, that is fine. Hata hivyo, Serikali hii imeamrisha, kwa mfano, ule utalii wa fukwe uende ukawe chini ya Wizara ya Mifugo, Mheshimiwa Mpina ana matatizo mengi sana ambayo hawezi kuyabeba hapa, Wizara hiyo haiwezi kutatua matatizo ya mifugo na uvuvi lakini bado Wizara imepelekewa kwamba ndiyo washughulike na utalii wa fukwe. Ningeshauri Serikali, ule utalii wa fukwe urudi tena kama ulivyokuwa kwenye TANAPA na Wizara badala ya kupeleka kwenye Mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kibaya zaidi kwenye masuala ya matangazo, Serikali imekuwa ikichukua matangazo na tuna-encourage TANAPA wafanye utalii wa ndani, watangaze zaidi, TANAPA wakijaribu kuweka mabango nchi nzima ili wa-encourage Watanzania waende kuangalia maeneo ya utalii utakuta bango moja la TANAPA lina-cost karibu shilingi milioni 4 kwa mwaka, kwa hiyo unakuta kwamba TANAPA au Ngorongoro hawawezi kulipia matangazo kama hayo. Kwa hiyo, ningeishauri Serikali iliangalie kwa umakini suala hilo kwamba watoe hizo tozo katika maeneo kama hayo kwa sababu tunataka tuingize pesa na tu-encourage utalii wa ndani ili uchumi uweze kukua. Naomba hilo liangaliwe kwa ndani sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa masikitiko makubwa naona Serikali imeamua kwa nguvu zote mradi wa Stiegler’s Gorge. Mradi wa Stiegler’s Gorge, ukiiangalia Selou, Selou is the one of the world heritage, ni urithi wa dunia, ni moja ya identity ya nchi yetu, huwezi kupata mahali pengine pazuri kama Selou. Hata hivyo, Serikali imeamua na inataka kwa nguvu zote, mpaka sasa hivi tumeomba Environmental Impact Assessment hapa tuoneshwe ni madhara gani yatapatikana lakini haya mambo hayajaletwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini taarifa tulizonazo ni kwamba mradi unasukumwa kwa nguvu na miti inataka kukatwa kule, tunataka tuharibu maeneo yale. Miti milioni tatu inataka iangushwe na wataalam wanasema maeneo yale ni mahali ambapo wanyama wanazalia, Wizara inasema nini kuhusiana na suala hilo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Selou ni kitambulisho cha nchi. Mara ya mwisho tulikwenda kule Urusi kwenye mkutano wanaisifu Selou inaitambulisha nchi yetu. Tutakapoweka hilo Bwawa faida yake ni ipi? Naunga mkono juhudi zinazofanywa kuwekeza utalii upande wa Kusini na Word Bank wanasema kama tukiwekeza vizuri Southern Circuit mapato tutakayoyapata ni dola karibu bilioni 16 ambazo zitatusaidia
kuongeza kipato katika nchi. Hili bwawa ukilitengeneza ambapo halitaanza kuzalisha mpaka baada ya miaka saba, mapato yake tutakayopata ni karibu bilioni 2 tukiuza umeme na kama tukipata wateja lakini ukiangalia nchi jirani zote, Malawi, Mozambique na Zambia nao wanatengeneza umeme wao, tutauza wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni mambo ambayo kama Taifa lazima tufikiri kwa pamoja, tusiende kwa kukurupuka. Nina wasiwasi kwamba kwa mara ya kwanza CCM mmeshindwa kuidhibiti Serikali, mmedhibitiwa na Serikali. Chama cha Mapinduzi mmeshindwa kuidhibiti Serikali kwa sababu mna wajibu wa kukaa kwenye vikao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kagasheki aliondoka hapa kwa Operesheni Tokomeza. Kuna watu waliuawa, walipigwa, walilazimishwa kufanya tendo la sex mbele ya watu, tulipiga kelele humu Bungeni akiwemo Mheshimiwa Pinda kama Waziri Mkuu hapa. Nilitegemea Waziri na Wizara hii itakuwa imejifunza na kuacha kuonea watu. Serikali inaoneaonea watu, inapigapiga watu hovyo, wapo wengine wanakufa, nilitegemea Wizara hii watakuwa wamejifunza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yanayozungumzwa sasa hivi, haya mambo ya vigingi, watu wanavyoonewa ina maana wakati ule wa Mheshimiwa Kagasheki hatukujifunza, hatukuwa na somo kwa sababu tunafanya yaleyale. Uendawazimu ni kufanya jambo lile lile, kwa njia ile ile halafu unategemea matokeo tofauti, huo ndiyo uendawazimu, hii ni simple definition ya uendawazimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Bunge tumezungumza sana suala hili, Serikali haipo kwa ajili ya kuonea watu, watu wanaonewa katika nchi yao wenyewe, wamejikuta wamezaliwa katika maeneo hayo, kwa nini hatuna njia ya kudumu ya kutatua matatizo? Mojawapo ni tatizo la Loliondo, nako kumekuwa na matatizo nenda, rudi. Waziri alikuja hapa kwa gear kubwa kwamba atatatua tatizo la Loliondo limefikia wapi mpaka leo? Juzi Waziri ulikwenda kupokea magari tena kule kule ulikosema watu wanapokeaga rushwa, wewe umepokea shilingi ngapi? Tuambie uko hapa tunakuona, umepokea shilingi ngapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanyama wameuawa, hawa askari tunawapenda sana wanalinda mapori lakini sasa tunawaona kwenye mapori ya akiba wana-shoot wanyama wa watu ambao ndiyo urithi na utajiri wao. Kwa kodi za wananchi zile risasi zimenunuliwa, wanawapiga bunduki ng’ombe kwa kodi ya wananchi. Yaani mtu analenga ng’ombe anasema piga hilo, lenga hilo, uchumi wa wananchi, hatuwezi kukubaliana na mambo haya. Wananchi wanavuliwa nguo katika nchi hii, nchi ambayo tumepata uhuru halafu tuseme hapa business as usual, hatuwezi kukubaliana. Haya ni mambo ambayo Waziri lazima atoe majibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hotuba ya Waziri sijaona mikakati yoyote, mnakimbilia mnasema mmenunua ndege, mlikuwa mnawaiga Rwanda sasa hivi ndege zinaporomoka. Wataalam wanasema hata Emirates ku-break even iliwachukua miaka 20. Hatukatai kununua ndege lakini hiyo shilingi trilioni 1 ambayo imewekezwa huko ingeweza kufanya vitu vya msingi halafu secondary itajichukulia yenyewe, tunafanya mambo kwa mihemko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshauri Mheshimiwa Waziri, sasa hivi naona kama kidogo ametulia, akae ajifunze Wizara vizuri, Wizara ina mambo mengi. Sasa hivi ametulia kidogo, Wizara ina mambo mengi na ni Wizara tunayoitegemea iinue uchumi katika nchi yetu.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Niseme tu katikati ya Bunge kwamba nasikitika tu kwamba, kwa sisi tuliokuwepo Bunge liliopita kabla ya Bunge halijaanza tulikuwa tumepewa semina elekezi pale Blue Peal Dar es Salaam, kutenganisha mihimili hii mitatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivi wakati mwingine sisi kama Wabunge tunasahau kabisa mhimili wetu una kazi gani dhidi ya Serikali. Kama Bunge lingekuwa linafanya kazi yake vizuri huu ndio wakati wa kuonesha power ya Bunge dhidi ya Serikali. Hii separation of power iliwekwa makusudi kwa sababu binadamu ana tabia ya ubinafsi, anataka yeye awe juu zaidi.

MheshimiMwenyekiti, kwa hiyo, ilivyowekwa Mahakama, Bunge na Serikali ni kuhakikisha yule anayeinuka zaidi avutwe mkia. Sasa kwa bahati mbaya Bunge letu tunadhani Serikali ina nguvu kuliko sisi. Ndio maana Wabunge wengi hapa wanapiga magoti na kuombaomba wakati Serikali kimsingi kupitia Waziri wa Fedha imekuja hapa kutuomba sisi tuidhinishe kutumia matumizi hayo. Ni wakati huu ambao Bunge lilitakiwa liiadabishe Serikali kwa matumizi ambayo Bunge halikuidhinisha. Sasa kwa sababu hatujui nguvu ya Bunge tumekuja hapa tunajibembeleza na naomba zahanati, naomba dispensary, naomba Kituo cha Afya wakati haya mambo ndio wakati wa Bunge kusema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wajibu wa Wabunge kujua what is our power, nguvu zetu ni zipi? Ndio maana CAG amekuja hapa ambaye ni jicho la Serikali, ni jicho la Bunge. Yeye ni Mkaguzi baada ya Serikali kuomba ruhusa ya kutumia pesa, sisi hatuna uwezo wa kwenda kukagua huko, CAG amekwenda kukagua kwa niaba yetu, anakuja anasema nimeona hili, nimeona hili halijapangwa vizuri, Wabunge wengine hapa wanamlaumu CAG. Ignorance ya kujua wajibu wetu kama Wabunge na hii tuna li-cripple Bunge tunasababisha watu wengine ambao ni wabinafsi wakue zaidi kuliko Bunge linavyotakiwa liwepo. Niwaombe ndugu zangu na nimpongeze Mheshimiwa Kadutu amefanya kazi ya Kibunge bila kujali itikadi za vyama kwa matatizo tuliyonayo kwenye majimbo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nakuja kwa Mheshimiwa Dkt. Mpango; mara tu alivyochukua Uwaziri alipoanza hapa alikuwa anahutubia kama yupo kwenye Lecture room, alikuwa kinadharia sana. Tulikwambia this is not a lecture room, sisi tupo kwenye ground. Tunakutana na watu, tunaishi na watu, hizi kodi ambazo leo amezitoa we told you three years back, kwamba hizi kodi zitaleta matatizo kwenye uchumi you never listen. Sasa hivi amerudi kwenye mgongo mwingine, halafu Wabunge hapa wanasema tunampongeza, tunaipongeza Serikali, yeye ndiye alitupeleka kule. Bado tunaendelea kusisitiza, huu utaratibu wa uchumi unaokwenda sasa hivi, huko mbele tunakwenda ku-crush na utaweka historia tunakwenda ku-crush kwa sababu uchumi tunaokwenda nao sio halisia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, asubuhi Mheshimiwa Sugu amesema hapa sisi tunaozungumza, najua Mheshimiwa Rais anasikia, actually sisi ndio tunaompenda Rais kuliko wengi wenu huko. Kwa sababu wanampaka Rais kwa mgongo wa chupa hawamwambii ukweli. They economy going crush kwa sababu huwezi kuniambia uchumi unakuwa, toka Serikali ya Awamu ya Tano nimeingia kwenye jimbo langu akinamama wale wengine wameuziwa fridge au wamenyang’anywa, wamenyang’anywa television na makochi kwa sababu hawawezi kulipa mikopo. Sasa utaniambiaje uchumi unakua kwa sababu hawawezi kufanya business, uchumi haukui.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka nimuulize swali Mheshimiwa Mpango, naomba anijibu honestly, Serikali ya Awamu ya Tano inaendesha hii nchi utadhania sisi ni Sudan ya Kusini, trial and error ambayo imezaliwa juzi. Serikali hii haina consistency kwa sababu nchi hii tokea tumepata uhuru ni Chama cha Mapinduzi kimekuwa kikitawala. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakubaliana wakati wa Mwalimu Nyerere kuna makosa mengine aliyafanya aliendelea kurekebisha kwa mfano hizi Serikali za Mitaa aliwahi ku-centralize akaona makosa akarudisha. Tunaweza tukamsamehe kwa sababu ndio kwanza tulikuwa tunapata Uhuru, lakini alivyokuja Mheshimiwa Mwinyi tukahama direction, tukahama mwelekeo, tukaacha mambo ya ujamaa, tukawa na free market katika nchi hii. Alivyokuja Mheshimiwa Mkapa naye akaanza, tukaanza kuweka wawekezaji akatengeneza mazingira ya wawekezaji tukaanza kuwa friendly kwa wageni ambao tuliwafukuza mwanzoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amekuja Mheshimiwa Dkt. Kikwete ametengeneza mazingira mazuri ya kuwa na marafiki wa nje, kuwafanya investors waje. Sasa swali kwa Mheshimiwa Dkt. Mpango aniambie namwona hapa wakati wa Mheshimiwa Kikwete alikuwa Katibu wa Tume ya Mipango ambayo sasa hivi unataka kuifuta. Wakati wa Rais Mheshimiwa Dkt. Kikwete, Mheshimiwa Dkt. Mpango alisimamia Kilimo kwanza, alisimamia SAGCOT, alisimamia Big Results Now, alisimamia Gesi, alisimamia PPP na wali- encourage D by D. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kwenye Awamu ya Tano amegeuka, ameenda kwenye mambo ya Stiegler’s Gorge, kwenye Standard Gauge ambayo mikopo yote hii anaichukua sio concessional loans, anachukua mikopo ambayo ni ya gharama kwa nchi hii, tell us wewe ni mchumi unayeamini nini? Atuambie hapa uchumi ule aliokuwa anaendesha Mheshimiwa Dkt. Kikwete ambaye alitengeneza mazingira mazuri ulikuwa na makosa au alimuingiza chaka? Sasa hivi ameweka u-turn, where are we heading as a Nation? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchumi wakati wa Serikali ya Kikwete ulikuwa una-embrace investors, ulikuwa una mazingira mazuri ya kuwaleta wawekezaji. Uchumi huu unagombana na wawekezaji, wanaonekana wote wizi katika uchumi huu ambao yeye ndiye Waziri. Wafanyabiashara wote wanaonekana ni wezi, wafanyabiashara wanaonekana hawalipi kodi, atuambie ni uchumi upi ambao anauamini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais wetu yeye sio mchumi, ni engineer, tunategemea Mheshimiwa Waziri ambaye ni Mchumi ampe maekelezo mazuri ambayo yatasaidia nchi yetu iende. Leo naongea kwa masikitiko makubwa kwa sababu tunaua Local Governments kwa uchumi wa namna hii, vyanzo vyote amechukua kwenye Local Government anavileta Central Government kuna maumivu makubwa ambayo yanapatikana kwenye Local Government. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Dkt. Mpango atoe majibu ni uchumi upi anauamini, what do you believe as an economics? Nani anamdanganya kati ya Mheshimiwa Dkt. Kikwete na Rais wa sasa? Kwa sababu Mheshimiwa Dkt. Kikwete alitengeneza mazingira pamoja na udhaifu wa Serikali ya Awamu ya Nne, alitengeneza mazingira mazuri ya kuwa na mahusiano na watu wa nje, alileta wawekezaji kulikuwa na mazingira mazuri, leo haya yoote umeyakataa, leo uko kwenye… (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namtaka Mheshimiwa Dkt. Mpango aniambie kichumi, nimesema wakati wa Mheshimiwa Dkt. Kikwete yeye alitu- encourage kwenye mambo ya SAGCOT, SAGCOT inazungumza kuhusu umwagiliaji kwamba tumwagilie, Stiegler’s Gorge inataka bwawa lile lijae. Sasa ni kwa namna gani tunaweza tukatekeleza SAGCOT na wakati huo huo tukaenda na Stiegler’s Gorge kwa maji yaleyale, ambayo upande wa SAGCOT tunataka tumwagilie kwenye kilimo cha umwagiliaji na wakati huo huo tunataka bwawa la umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ndio mambo ambayo kama Bunge tunatakiwa tujadiliane bila kujali itikadi za vyama. Nasema tutapigana makofi hapa lakini the economy is sinking na tunakwenda ku-crush sio muda mrefu kwa sababu tunakopa mikopo ambayo ni gharama kubwa. Makusanyo ni trilioni kumi na nne tu na bado tunaenda kwenye negative, hatuna hiyo pesa naomba Mheshimiwa Dkt. Mpango na juzi nilimuuliza kwenye Wizara yake kwamba ni kiasi gani cha pesa ambacho ni cha TRA. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, dada yangu Mheshimiwa Dkt. Sware amezungumza hapa hela zote ambazo wanadaiwa hizo ni kiasi gani ambacho wanakusanya kwenye TRA, lakini tukija hapa tunapongezana pongezan. Huu ndio wakati wa kuonesha the power of the Parliament. Tulitakiwa tushikamane kwamba ni kwa nini Serikali hii inalikosea adabu Bunge?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuuliza kwa nini Serikali inafungua miradi ambayo Bunge halijapitisha. Inaanza kuanzisha halafu tumekaa hapa tunapigania makofi kwa sababu Serikali ikileta maji kwenye jimbo langu is not a fever am the tax payer representative, mimi nawakilisha wapiga Kura wangu kule, kwa hiyo, siwezi kumpigia magoti Mheshimiwa Dkt. Mpango hapa. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekikti, Serikali ya Chama cha Mapinduzi is crying for my endorsement, am smart enough, nikitaka kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Magufuli naweza kuchukua TBC au ITV. Msiwe mnaviziavizia ndio nasema hapa simpongezi hapa ndio nasema sasa simpongezi kwa sababu ana washauri ambao mnampotosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi huko nje wanalalamika, there is no money kwenye mifuko, haya ndio ya kujadili kama Bunge, wengi huko mitaani kwenye majimbo yetu mimi saa hizi ukienda jimboni kwangu file la mahitaji liko hivi. Limekaa hivi, sijasoma nahitaji mtoto shule, ada, sijui nini, mafaili makubwa yamejaa hivi, hata mimi mwenyewe sina hela na nyie wenyewe ndio hayohayo, halafu tukija hapa tunadanganyana. Tuoneshe nguvu ya Bunge wewe mwenyewe Mheshimiwa Jenista unalalamika huna hela, tukikaa, saa hizi tuanze kukaa tunadanganyana tunapongezana, hakuna hela, huu uchumi Mheshimiwa Spika amezungumza asubuhi hapa uchumi kila mtu anao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisema juzi I am a theologian by profession, lakini huwezi kuniambia kwamba siwezi kuguswa kama hamna hela! Hata mama kule nyumbani anajua kama uchumi umekaa vibaya, uchumi haupo, tusidanganyane hapa, haukui! Wazimbabwe wanasema mtoto ambaye analia njaa leo huwezi kumwambia jana nilikupa chakula. Hakuna chakula huko mitaani tusidanganyane hapa hakuna chakula, hayo mambo ya ndege, kwanza ndege wametuletea disaster, wanapata hasara halafu hawasemi hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni mambo lazima tujadili kama Bunge na lazima tuoneshe power kwa Mheshimiwa Dkt. Mpango kwamba lazima awajibike. Hela ambazo ametumia bila kupata vibali vya Bunge anatakiwa awajibike. Sasa tumekaa hapa tunapongezana ametumia hela nyingi bila kibali cha Bunge, sasa Bunge lina kazi gani? Vinginevyo Bunge limemezwa, linawafanya wale watu wabinafsi wainuke zaidi.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 20 16/2017 - Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Utumishi na Utawala Bora
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi ningeanza kwa kuchangia utawala bora. Mtu mmoja aliwahi kusema, it takes a political consciousness and political will for the good governance to prevail. Utawala bora na utawala wa sheria hauanzi na bajeti, bajeti sio takwa la msingi la utawala bora. Kwa hiyo, inaanza political will kwamba tunataka tuwe na utawala bora ndiyo bajeti inakuja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini nazungumza haya? Toka Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani neno na dhana nzima ya utawala bora halionekani. Mtu mmoja pia naomba nimnukuu amesema, utawala bora ni kuongoza nchi kwa ufanisi na tija, kwa uwazi, uadilifu, uwajibikaji na ushirikishwaji wa watu kwa kufuata utawala wa sheria. Tangu Serikali hii imeingia madarakani, kuna mambo kadhaa ambayo imekanyaga huo utawala bora, halafu leo Waziri bila hata kuwa na uso wa soni anakuja kuomba hela zaidi ya shilingi bilioni mia nane hapa za utawala bora ambao haupo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze na la kwanza. Serikali hii imeanza kufanya kazi kienyeji. Mawaziri wote hawa wameanza kazi bila kupata instrument, huko ni kukanyaga sheria maana yake hawa Mawaziri ni sawa na sisi Mawaziri Vivuli walikuwa wanatoa maagizo wakati hawako kwa mujibu wa sheria, huo siyo utawala bora. Aidha, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumekaa kimya, hatusemi wakati wajibu wetu ni kuinyoosha Serikali, watu wote tumekaa kinafiki.
Hata Mawaziri wengine tukiwa kwenye chai mnalaumu utaratibu huu, mkija hapa mnageuka kama vinyonga, hamsemi na wakati hii ni kazi ya Bunge. Mkibisha tutataja mmoja mmoja ambao mnapinga utawala huu kwa taratibu hizo na wengine tumewarekodi kama Rais anavyosema amerekodi, kama mnabisha tuweke hapa. Hata ninyi hamkubali halafu tukikaa humu ndani ya Bunge hamsemi na kazi ya Bunge ndiyo hiyo tumekuja hapa kusema. Tunazungumzia utawala bora, mnafanya kazi bila instrument, that is wrong and thas is not good governance, shame with you.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, toka Bunge la Tisa…
KUHUSU UTARATIBU.....
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wakati wa kuchangia tunakuwaga na taarifa hatuna mwongozo, nashangaa huyu ameomba mwongozo umempa, Kiti bado kinayumba tu. Naendelea kuchangia, unayumba bado, hakuna mwongozo wakati wa kuchangia, sheria ndivyo inavyosema.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba muda wangu uzingatiwe. La kwanza nililokuwa nachangia ni Serikali kuongoza bila instrument.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, toka Bunge la Tisa la Mheshimiwa Sitta na utawala uliopita pamoja na kwamba kulikuwa na upungufu lakini utawala uliopita ulijitahidi kukuza demokrasia kwa kiwango fulani, Bunge lilikuwa linaoneshwa live, tumeona wakati wa madam Spika, Wabunge tulikuwa na uhuru. Kwa Wabunge wengine ambao ni washabiki Bunge halijaanza Tanzania, tusome kidogo kutoka Ugiriki, Wagiriki walifanyaje Bunge mpaka tukafikia hatua hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge ni mkutano wa wazi wa wananchi wote. Serikali hii inaanza kuminya inaweka siri, huu siyo mkutano wa unyago, tunaongelea matumizi ya hela za Watanzania, tunahitaji Watanzania waone kila kinachojadiliwa kwa manufaa yao. Serikali inayokandamiza uwazi ni Serikali ambayo ni oga, ni Serikali inayoficha madudu. Kama mnasimama hapa mnasema mnakusanya pesa za kutosha, mmevunja rekodi, haijawahi kutokea, mmeikuta Hazina tupu, mnaficha nini tusiwaoneshe Watanzania hayo mnayoyafanya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo la pili, mnakanyaga wenyewe sheria halafu mnakuja kuomba bajeti ya utawala bora ambao hamnao. Pamoja na udhaifu wa Serikali iliyopita lakini Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete alikuwa jasiri, aliruhusu humu ndani tuongee, tuikosoe Serikali kwa uwazi na hilo nampongeza bila aibu. Tulimsema, tulimkosoa na mambo mengine aliyafanyia kazi pamoja na kwamba mengine hakuyashughulikia. Leo mnakuja hapa kwa ujasiri mnasema Hapa Kazi Tu, kukosolewa hamtaki, kazi gani ambayo hamtaki kukosolewa?
Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wote bila aibu wakati ule tunamkosoa Kikwete hapa mlikaa kimya, mlituzomea lakini leo mnaufyata. Inaonekana Mheshimiwa Magufuli hata akidondosha kijiko ninyi mtapiga makofi kwa sababu ya uoga wenu. Wabunge hatuwezi kuwa waoga kwa kiwango hicho, wajibu wetu ni kuisimamia na kuikosoa Serikali. Waliosoma physics sasa imegeuka kama ile pendulum swing, Serikali iliyopita alikuwa upande huu, sasa hivi tumeendelea upande huu badala ya kukaa katikati, lengo letu ni kuinyoosha Serikali, huo ndio wajibu wa Bunge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la tatu, Waziri unapata wapi uhalali wa kutuletea bajeti hii wakati Serikali yako inakanyaga utawala bora wa sheria? Serikali inayoogopa uwazi ni Serikali isiyojiamini, ni Serikali ambayo inaficha uovu.
Tulitegemea demokrasia sasa inapanda ngazi kutoka pale tulipofika, kwa sababu mambo haya ni ya wazi, ni ya nchi, ni ya wananchi, tulitegemea sasa uwazi uwepo ili tukosoe, tudadisi, tuhoji kwa manufaa ya wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Sugu alizungumza hapa alisema numbers don‟t lie, imagine Serikali inayosema uwazi Dar es Salaam mmezidiwa, Mameya 11 lakini bado mnang‟ang‟ania, hata hiyo shule sasa imetusaidiaje kama hesabu tu inakataa, mmezidiwa, mnapiga danadana, mnakataa, huo ni uwazi gani mnaozungumza hapa?
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naikataa taarifa kwa sababu anasema uongo.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo na wewe umemwita bwege, kuna mtu kule Arusha alimwita Mheshimiwa Magufuli bwege akapelekwa Mahakamani na wewe utakwenda Mahakamani. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, mna dhana ya kusema tutumbuane majipu, ili Serikali ya Chama cha Mapinduzi ipone lazima tuwe na Bunge imara. Kama ni jipu linaanzia kwenye Bunge, Bunge hili ni jipu, limekuwa dhaifu, haliwezi kuikemea Serikali. Kuna maamuzi ya msingi na makubwa ambayo Bunge hili linayatoa na mimi kama Kamishna na Makamishna wengine hatushirikishwi, hili ni jipu, lazima tutumbuane humu ndani.
NAIBU SPIKA: Muda wako umekwisha,
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Niseme tu katikati ya Bunge kwamba nasikitika tu kwamba, kwa sisi tuliokuwepo Bunge liliopita kabla ya Bunge halijaanza tulikuwa tumepewa semina elekezi pale Blue Peal Dar es Salaam, kutenganisha mihimili hii mitatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivi wakati mwingine sisi kama Wabunge tunasahau kabisa mhimili wetu una kazi gani dhidi ya Serikali. Kama Bunge lingekuwa linafanya kazi yake vizuri huu ndio wakati wa kuonesha power ya Bunge dhidi ya Serikali. Hii separation of power iliwekwa makusudi kwa sababu binadamu ana tabia ya ubinafsi, anataka yeye awe juu zaidi.

MheshimiMwenyekiti, kwa hiyo, ilivyowekwa Mahakama, Bunge na Serikali ni kuhakikisha yule anayeinuka zaidi avutwe mkia. Sasa kwa bahati mbaya Bunge letu tunadhani Serikali ina nguvu kuliko sisi. Ndio maana Wabunge wengi hapa wanapiga magoti na kuombaomba wakati Serikali kimsingi kupitia Waziri wa Fedha imekuja hapa kutuomba sisi tuidhinishe kutumia matumizi hayo. Ni wakati huu ambao Bunge lilitakiwa liiadabishe Serikali kwa matumizi ambayo Bunge halikuidhinisha. Sasa kwa sababu hatujui nguvu ya Bunge tumekuja hapa tunajibembeleza na naomba zahanati, naomba dispensary, naomba Kituo cha Afya wakati haya mambo ndio wakati wa Bunge kusema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wajibu wa Wabunge kujua what is our power, nguvu zetu ni zipi? Ndio maana CAG amekuja hapa ambaye ni jicho la Serikali, ni jicho la Bunge. Yeye ni Mkaguzi baada ya Serikali kuomba ruhusa ya kutumia pesa, sisi hatuna uwezo wa kwenda kukagua huko, CAG amekwenda kukagua kwa niaba yetu, anakuja anasema nimeona hili, nimeona hili halijapangwa vizuri, Wabunge wengine hapa wanamlaumu CAG. Ignorance ya kujua wajibu wetu kama Wabunge na hii tuna li-cripple Bunge tunasababisha watu wengine ambao ni wabinafsi wakue zaidi kuliko Bunge linavyotakiwa liwepo. Niwaombe ndugu zangu na nimpongeze Mheshimiwa Kadutu amefanya kazi ya Kibunge bila kujali itikadi za vyama kwa matatizo tuliyonayo kwenye majimbo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nakuja kwa Mheshimiwa Dkt. Mpango; mara tu alivyochukua Uwaziri alipoanza hapa alikuwa anahutubia kama yupo kwenye Lecture room, alikuwa kinadharia sana. Tulikwambia this is not a lecture room, sisi tupo kwenye ground. Tunakutana na watu, tunaishi na watu, hizi kodi ambazo leo amezitoa we told you three years back, kwamba hizi kodi zitaleta matatizo kwenye uchumi you never listen. Sasa hivi amerudi kwenye mgongo mwingine, halafu Wabunge hapa wanasema tunampongeza, tunaipongeza Serikali, yeye ndiye alitupeleka kule. Bado tunaendelea kusisitiza, huu utaratibu wa uchumi unaokwenda sasa hivi, huko mbele tunakwenda ku-crush na utaweka historia tunakwenda ku-crush kwa sababu uchumi tunaokwenda nao sio halisia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, asubuhi Mheshimiwa Sugu amesema hapa sisi tunaozungumza, najua Mheshimiwa Rais anasikia, actually sisi ndio tunaompenda Rais kuliko wengi wenu huko. Kwa sababu wanampaka Rais kwa mgongo wa chupa hawamwambii ukweli. They economy going crush kwa sababu huwezi kuniambia uchumi unakuwa, toka Serikali ya Awamu ya Tano nimeingia kwenye jimbo langu akinamama wale wengine wameuziwa fridge au wamenyang’anywa, wamenyang’anywa television na makochi kwa sababu hawawezi kulipa mikopo. Sasa utaniambiaje uchumi unakua kwa sababu hawawezi kufanya business, uchumi haukui.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka nimuulize swali Mheshimiwa Mpango, naomba anijibu honestly, Serikali ya Awamu ya Tano inaendesha hii nchi utadhania sisi ni Sudan ya Kusini, trial and error ambayo imezaliwa juzi. Serikali hii haina consistency kwa sababu nchi hii tokea tumepata uhuru ni Chama cha Mapinduzi kimekuwa kikitawala. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakubaliana wakati wa Mwalimu Nyerere kuna makosa mengine aliyafanya aliendelea kurekebisha kwa mfano hizi Serikali za Mitaa aliwahi ku-centralize akaona makosa akarudisha. Tunaweza tukamsamehe kwa sababu ndio kwanza tulikuwa tunapata Uhuru, lakini alivyokuja Mheshimiwa Mwinyi tukahama direction, tukahama mwelekeo, tukaacha mambo ya ujamaa, tukawa na free market katika nchi hii. Alivyokuja Mheshimiwa Mkapa naye akaanza, tukaanza kuweka wawekezaji akatengeneza mazingira ya wawekezaji tukaanza kuwa friendly kwa wageni ambao tuliwafukuza mwanzoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amekuja Mheshimiwa Dkt. Kikwete ametengeneza mazingira mazuri ya kuwa na marafiki wa nje, kuwafanya investors waje. Sasa swali kwa Mheshimiwa Dkt. Mpango aniambie namwona hapa wakati wa Mheshimiwa Kikwete alikuwa Katibu wa Tume ya Mipango ambayo sasa hivi unataka kuifuta. Wakati wa Rais Mheshimiwa Dkt. Kikwete, Mheshimiwa Dkt. Mpango alisimamia Kilimo kwanza, alisimamia SAGCOT, alisimamia Big Results Now, alisimamia Gesi, alisimamia PPP na wali- encourage D by D. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kwenye Awamu ya Tano amegeuka, ameenda kwenye mambo ya Stiegler’s Gorge, kwenye Standard Gauge ambayo mikopo yote hii anaichukua sio concessional loans, anachukua mikopo ambayo ni ya gharama kwa nchi hii, tell us wewe ni mchumi unayeamini nini? Atuambie hapa uchumi ule aliokuwa anaendesha Mheshimiwa Dkt. Kikwete ambaye alitengeneza mazingira mazuri ulikuwa na makosa au alimuingiza chaka? Sasa hivi ameweka u-turn, where are we heading as a Nation? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, uchumi wakati wa Serikali ya Kikwete ulikuwa una-embrace investors, ulikuwa una mazingira mazuri ya kuwaleta wawekezaji. Uchumi huu unagombana na wawekezaji, wanaonekana wote wizi katika uchumi huu ambao yeye ndiye Waziri. Wafanyabiashara wote wanaonekana ni wezi, wafanyabiashara wanaonekana hawalipi kodi, atuambie ni uchumi upi ambao anauamini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Rais wetu yeye sio mchumi, ni engineer, tunategemea Mheshimiwa Waziri ambaye ni Mchumi ampe maekelezo mazuri ambayo yatasaidia nchi yetu iende. Leo naongea kwa masikitiko makubwa kwa sababu tunaua Local Governments kwa uchumi wa namna hii, vyanzo vyote amechukua kwenye Local Government anavileta Central Government kuna maumivu makubwa ambayo yanapatikana kwenye Local Government. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Dkt. Mpango atoe majibu ni uchumi upi anauamini, what do you believe as an economics? Nani anamdanganya kati ya Mheshimiwa Dkt. Kikwete na Rais wa sasa? Kwa sababu Mheshimiwa Dkt. Kikwete alitengeneza mazingira pamoja na udhaifu wa Serikali ya Awamu ya Nne, alitengeneza mazingira mazuri ya kuwa na mahusiano na watu wa nje, alileta wawekezaji kulikuwa na mazingira mazuri, leo haya yoote umeyakataa, leo uko kwenye… (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namtaka Mheshimiwa Dkt. Mpango aniambie kichumi, nimesema wakati wa Mheshimiwa Dkt. Kikwete yeye alitu- encourage kwenye mambo ya SAGCOT, SAGCOT inazungumza kuhusu umwagiliaji kwamba tumwagilie, Stiegler’s Gorge inataka bwawa lile lijae. Sasa ni kwa namna gani tunaweza tukatekeleza SAGCOT na wakati huo huo tukaenda na Stiegler’s Gorge kwa maji yaleyale, ambayo upande wa SAGCOT tunataka tumwagilie kwenye kilimo cha umwagiliaji na wakati huo huo tunataka bwawa la umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ndio mambo ambayo kama Bunge tunatakiwa tujadiliane bila kujali itikadi za vyama. Nasema tutapigana makofi hapa lakini the economy is sinking na tunakwenda ku-crush sio muda mrefu kwa sababu tunakopa mikopo ambayo ni gharama kubwa. Makusanyo ni trilioni kumi na nne tu na bado tunaenda kwenye negative, hatuna hiyo pesa naomba Mheshimiwa Dkt. Mpango na juzi nilimuuliza kwenye Wizara yake kwamba ni kiasi gani cha pesa ambacho ni cha TRA. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, dada yangu Mheshimiwa Dkt. Sware amezungumza hapa hela zote ambazo wanadaiwa hizo ni kiasi gani ambacho wanakusanya kwenye TRA, lakini tukija hapa tunapongezana pongezan. Huu ndio wakati wa kuonesha the power of the Parliament. Tulitakiwa tushikamane kwamba ni kwa nini Serikali hii inalikosea adabu Bunge?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuuliza kwa nini Serikali inafungua miradi ambayo Bunge halijapitisha. Inaanza kuanzisha halafu tumekaa hapa tunapigania makofi kwa sababu Serikali ikileta maji kwenye jimbo langu is not a fever am the tax payer representative, mimi nawakilisha wapiga Kura wangu kule, kwa hiyo, siwezi kumpigia magoti Mheshimiwa Dkt. Mpango hapa. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekikti, Serikali ya Chama cha Mapinduzi is crying for my endorsement, am smart enough, nikitaka kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Magufuli naweza kuchukua TBC au ITV. Msiwe mnaviziavizia ndio nasema hapa simpongezi hapa ndio nasema sasa simpongezi kwa sababu ana washauri ambao mnampotosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi huko nje wanalalamika, there is no money kwenye mifuko, haya ndio ya kujadili kama Bunge, wengi huko mitaani kwenye majimbo yetu mimi saa hizi ukienda jimboni kwangu file la mahitaji liko hivi. Limekaa hivi, sijasoma nahitaji mtoto shule, ada, sijui nini, mafaili makubwa yamejaa hivi, hata mimi mwenyewe sina hela na nyie wenyewe ndio hayohayo, halafu tukija hapa tunadanganyana. Tuoneshe nguvu ya Bunge wewe mwenyewe Mheshimiwa Jenista unalalamika huna hela, tukikaa, saa hizi tuanze kukaa tunadanganyana tunapongezana, hakuna hela, huu uchumi Mheshimiwa Spika amezungumza asubuhi hapa uchumi kila mtu anao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisema juzi I am a theologian by profession, lakini huwezi kuniambia kwamba siwezi kuguswa kama hamna hela! Hata mama kule nyumbani anajua kama uchumi umekaa vibaya, uchumi haupo, tusidanganyane hapa, haukui! Wazimbabwe wanasema mtoto ambaye analia njaa leo huwezi kumwambia jana nilikupa chakula. Hakuna chakula huko mitaani tusidanganyane hapa hakuna chakula, hayo mambo ya ndege, kwanza ndege wametuletea disaster, wanapata hasara halafu hawasemi hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni mambo lazima tujadili kama Bunge na lazima tuoneshe power kwa Mheshimiwa Dkt. Mpango kwamba lazima awajibike. Hela ambazo ametumia bila kupata vibali vya Bunge anatakiwa awajibike. Sasa tumekaa hapa tunapongezana ametumia hela nyingi bila kibali cha Bunge, sasa Bunge lina kazi gani? Vinginevyo Bunge limemezwa, linawafanya wale watu wabinafsi wainuke zaidi.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Niungane na Mheshimiwa Nsanzugwanko kuhusiana na barabara ya Nyakanazi tokea nimekuwa Mbunge hapa nasikia Kigoma-Nyakanazi toka nimekuwa Mbunge kipindi cha kwanza, kwa kweli watu wa Kigoma mnaonewa inabidi tuwasaidie, mpigiwe debe, mpo porini sana, mmetengwa. Nadhani Wizara watasaidia kidogo, ilikuwa mara ya kwanza kufika Kigoma kwa kweli mko nje ya Tanzania.

Mheshimiwa Spika, nikirudi kwenye Wizara hii; naamini Wizara hii ya Fedha na Mipango ni Wizara ya Fedha na Mipango, lakini kwa mtazamo wangu naona wamejikita zaidi kwenye fedha kuliko kwenye mipango na kwa kuwa wao ni Wizara ya Fedha na Mipango walipaswa wawe ni Dira kubwa ya Taifa ili kuliongoza namna gani ya kupata hizo fedha halafu kisha wakusanye, lakini Wizara hii katika utendaji wao wamekuwa kama vile ambavyo wanataka wamkamue ng’ombe ambaye hawamuandalii mazingira mazuri ya kutoa maziwa.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ndiyo inayosimamia Dira ya Taifa, Wizara hii ndiyo inasimamia Mpango wa Miaka Mitano wa Taifa, lakini kwa bahati mbaya toka Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani kuna mipango mingi ambayo inatekelezwa na Wizara hii ni ile ambayo haipo kwenye Mpango wa Miaka Mitano wa Taifa.

Mheshimiwa Spika, sasa mimi siyo Mchumi, I am Theologian by professional, inanichanganya kidogo kwamba sasa hiyo mipango ni ipi wanayoisimamia kwa sababu tunakuwa na priorities, tunaweka mikakati, lakini mwisho wa siku tunapokuja kwenye utekelezaji wanaleta vitu vingine kabisa ambavyo havikuwepo kwenye mpango wa nchi, wanaanza kufanya vitu ambavyo havipo.

Mheshimiwa Spika, mfano mzuri, hakuna mtu anayekataa move ya kuhamia Dodoma, lakini haikuwepo kwenye Mpango wa Miaka Mitano, it was more of a political than economical, imetulete shida, tunahangaika, hatukuwa na Ofisi, imechanganya mambo mengi sana katika kuendesha nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, nirudie tena, hatukatai kuhamia Dodoma lakini hatukuwa na mpango huo, hela tumeitoa wapi? Natoa mifano kama hiyo.

Mheshimiwa Spika, mpango mwingine ambao naweza kusema, mipango hii ambayo inafanywa ambayo haikuwepo kwenye mpango wa nchi, inaleta tabu katika nchi yetu. Nitoe mfano mmoja wa haraka haraka, kwa wastani TRA wanasema kwa sasa hivi wanakusanya wastani wa trilioni 1.3 mapato kwa mwezi. Hata hivyo, mapato haya ukiangalia wao wamekuwa kama Wakala tu, hela nyingi wanazokusanya siyo za kwao.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, wanachukua wharfage, wanachukua hela zote za halmashauri, property tax kwa mfano za majengo wamechukua, wamechukua zile VAT refundable, wamechukua mpaka zile levy za korosho, wamechukua hela nyingi ambazo siyo za kwao halafu wanapita mitaani, barabarani kwa wananchi kisiasa wanasema sasa hivi tumedhibiti mapato yanakuwa mengi. Wakati huo huo hizo hela walizotunyang’anya kwenye halmashauri zetu mnazi-ground halmashauri, hazifanyi kazi vizuri, yaani hadi hela za REA nazo wanasema za kwao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wamezi-ground halmashauri, sasa leo hiyo mipango una-match vipi mipango na jinsi ambavyo wanakusanya hizo pesa. Matokeo yake katika halmashauri wameshindwa kupeleka wataalam wazuri, wameamua tena ku-centralize ambapo ni mipango iliyoshindikana toka tumepata uhuru, tulijaribu tukakwama.

Mheshimiwa Spika, kwenye Majukwaa wanasimama kwamba wanakusanya pesa nyingi, lakini zile pesa ambazo wametunyang’anya kwenye halmashauri hazirudi kwa sababu hakuna mipango mizuri. Nilitegemea Mheshimiwa Waziri katika mipango yake angeishauri Serikali hii kwamba kupeleka watendaji katika halmashauri ambao hawana weledi, ambao wameenda kisiasa kunaharibu utendaji wa kazi kwa sababu nchi hii mtu akiwa Mwanasiasa anaaminika kwamba anajua kila kitu.

Mheshimiwa Spika, nakumbuka siku moja Katibu aliyeondoka Dkt. Kashilillah alisema hapa Wabunge tukianza hapa kuzungumzia masuala ya nuclear tutataka tuchangie hata kama hatuyajui. Pia tunaamini kwamba mtu akiwa mwanasiasa anajua kila kitu na nategemea Wizara ya Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Dkt. Mpango ingekuwa ndiyo dira ya kuishauri Serikali hii. Tumekuwa na mipango mingi ambayo iko nje ya bajeti.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia wakati wa Dkt. Kikwete, Dkt. Kikwete ameondoka hapa tunakusanya 900.0 billion 900.0 ambazo hakukusanya hizi hela za wengine. Inaonesha yeye system zake zilikuwa zinafanya kazi vizuri lakini wao wame-intefere maeneo mengine yote, wanataja pesa kubwa hii lakini bado utekelezaji haupo. Sasa wanatangaza hizo pesa zote zipo zinakusanywa, kwa nini kwenye pesa za maendeleo pesa hazirudi kwenye maeneo yetu tunapotoka kama hizi pesa zote wanazikusanya? Mfano mzuri, kwenye kitabu cha Kamati wamezungumza mpaka Disemba, 2017 Serikali ilikuwa imekusanya 7.6 trillion na mpaka Februari, 2018 walilipa deni la nje trilioni 5.5 maana yake tulibakiwa na trilioni mbili.

Mheshimiwa Spika, sasa tunaendeshaji hii nchi kwa utaratibu huo kama hela zote tunazokusanya tunalipa madeni na bado kwenye kitabu cha hotuba cha Mheshimiwa Waziri ukisoma ukurasa wa 96 amezungumza na hawa wamesema, anasema kwamba deni bado linahimilika lakini mzigo mkubwa bado anabeba mwananchi wa Tanzania. Wakitoka nje kisiasa wanasema kila kitu kipo safi, tunapongezana hapa, mtumbwi unazidi kuzama, kiuhalisia tuna-suffocate, hakuna oxygen katika nchi hii bado tunazama. Kila mtu anaamua anavyotaka, tutapigiana makofi hapa lakini hela hamna. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukienda kwenye kila Wizara kama ni Wizara zipo zimepata pesa zaidi ya asilimia 50 na kitu ni chache sana, zote ziko chini ya kiwango. Kama tunakusanya mapato hayo Waziri, Mheshimiwa Dkt. Mpango, kwa nini Wizara zote zinapata pesa chini ya kiwango? Haya ni masuala ambayo anatakiwa atujibu na ningeomba katika suala hili anijibu hela halisi ambayo anakusanya kodi ya TRA bila kuchanganya na hizi nilizomtajia, wharfage zile za Halmashauri, sijui VAT refundable za watu wengine ambazo wanashika ni shilingi ngapi? Tujilinganishe na Serikali iliyopita na ya sasa kama tunakwenda pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine kama nilivyozungumza, mipango mingi anayotekeleza sasa hivi Mheshimiwa Waziri haikuwepo kwenye Mpango wa Miaka Mitano. Hatukuwa kwenye mpango wa miaka mitano kwamba we will move from Dar es Salaam to Dodoma, kwenye mpango wa miaka mitano hatukuwa na standard gauge, where are we getting the money?

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, hizi hela ukiangalia kiutaratibu wamekopa mikopo ya commercial ambayo ni very expensive. Tunakopa mkopo kwa sababu commercial unakopa mkopo, unaanza kulipa mkopo huo mapema kabla ya ule mradi wa longterm haujaanza kuzalisha sasa ku- service huu mkopo tuta-service kupata hela, itatoka wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri atupe majibu hapa. Ukiangalia Ethipoia au Kenya wao walipata concession loan ambayo ukikopa wale watu watamaliza ule mradi, halafu wakishamaliza ule mradi, unapoanza kufanya kazi ndipo unaanza kulipa. Ni kitu gani kimesababisha wasiende kwenye mikopo hiyo, wameenda kwenye mikopo hii ya commercial loan? Mheshimiwa Waziri, Dkt. Mpango ningeomba anijibu. Kwa hiyo, kuna mipango mingi ambayo tunafanya lakini haikuwepo kwenye utaratibu.

Mheshimiwa Spika, tumeenda kwenye mambo ya Stiegler’s gorge hapa, tatizo la Tanzania siyo kwamba tuna tatizo la umeme, tatizo ni kuuhamisha umeme ulipo kwenda kwa walaji. Hizo megawatts zote tunazozitaka tunataka tuzifanyie nini? Ambapo tutachukua hela ya sasa, kwenye longterm loan ambazo zinakuwa ni mzigo kwa Watanzania wakija hapa wanasema mkopo bado unabebeka. Haya ni mambo siyo suala tuje tushangiliane hapa. Bado nam- challenge Mheshimiwa Mpango yeye ndiye dira ya nchi yetu. Hii mamlaka inatoka wapi ya kwamba wanaleta mipango ambayo haipo kwenye mipango ya miaka mitano? Haya ndiyo yanayotuchanganya, yanatuchanganya kama Taifa hatuelewi tushike lipi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yote yaliyofanyika, sasa hivi nimezungumza hapo mwanzo kwamba, tumefika mahali tuna-centralize kila kitu ambapo hayo mambo yalishindikana hapo mwanzoni, sasa hivi halmashauri zote tumezi-ground tunarudi kule kule ambako tulishindwa. Ilitumika pesa nyingi sana kuunda Serikali za Mitaa, kuzi-empower Serikali za Mitaa tulitumia pesa nyingi sana hizi D by D leo tena tumerudi kule kule kitu kinafanyika Dar es Salaam, kila kitu wanataka kifanyike sijui Dodoma ambako tumezi-ground Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, hii mipango inekuwa ina-empower watu wa kule chini inge-empower watu wa chini waone kama wana-own, wame-complicate. Naamini na elimu yangu ndogo hii niliyonayo, elimu hai-complicate mambo, elimu ina-simplify mambo, lakini ukiangalia mipango yote tunapiga mapambio mengi kwenye vyombo vya habari. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jana wakati nasoma report hapo nimesikia kwenye report wenzangu walifanya siwa-challenge lakini nilishangaa wanashangaa mtu analipwa milioni 96 (Dola 40,000) tunashangaa mtu analipwa eti Dola 40,000, this is poverty mentality. Yule mtu kwanza ameingia mkataba na wale watu, zile hela siyo za kwetu, akilipwa milioni 96 kwanza atalipa kodi milioni 30 si zitakuja hapa nchini, tuna hasara gani sisi? Kodi milioni 30 zitakuwa hapa nchini, tutawaaminisha Watanzania kwamba mtu akilipwa milioni 40 kama ni laana, that is poverty mentality.

Mheshimiwa Spika, watu wangelipwa hela zaidi ya hizo ilimradi hawavunji sheria, sasa kwa mfano, waki-import expert ambaye huwezi kumpata tena ni wa gharama utamlipa Sh.200,000 tunazolipana lipana hapa? Wachezaji wa mpira wanalipwa hela nyingi kwa sababu ya professionalism walizonazo, sasa tusifike mahali tunakuwa sadist, tunawachukia watu wanapolipwa hela nyingi badala ya ku-encourage watu walio chini walipwe zaidi, sisi tunasema analipwa zaidi, kwa hiyo ashuke chini, are we serious?

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka niseme kwa ujumla, I am Theologian anyway I am not an economist lakini nataka kusema Mheshimiwa Mpango atuongoze, atusaidie.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa uzima tena tumerudi mahali hapa kama kawaida. Bila kusahau, nampongeze Msemaji wa Kambi ya Upinzani, Mheshimiwa Halima Mdee kwa hotuba iliyosheheni mawazo pevu ambayo naamini Mheshimiwa Dkt. Mpango atayafanyia kazi. Sisi kama Wapinzani tumekuwa tukitoa ushauri mwingi, kwa manufaa ya Taifa hili na Serikali hii namshauri Waziri apitie kitabu cha Sera Mbadala za CHADEMA zitamsaidia katika kuandaa mpango kwa sababu tunapenda kulisaidia Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, tumekuwa tukitoa mpango wa mwaka mmoja mmoja kutoka kwenye mpango wa miaka mitano. Kwa experience ambayo imeonekana sasa hivi, hasa hii miaka miwili ya karibuni, kuna miradi mingi imeingizwa ambayo haikuwepo kwenye mpango wa miaka mitano, jambo ambalo linatufanya tuonekane kama Taifa hatujui tunakotaka kwenda lakini ni wakati muafaka wa kujitafakari kama Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mdee katika hotuba amezungumzia sana kuhusiana na suala la Katiba, kwamba ni kipaumbele na kilio cha wananchi na amesema kwamba mipango yote mizuri hii kama hatutaangalia kilio cha wananchi itakuwa haina maana. Kwa kuongezea hapo, Mheshimiwa Dkt. Mpango nataka tujiulize maswali kama manne kama Taifa tunapoendelea na mipango hii, vinginevyo tutakuwa tunapoteza muda na tunapoteza kodi za wananchi. Hebu tujiulize kama Taifa, tunapopanga mpango huu nchi yetu kidiplomasia ikoje as we speak? Mahusiano yetu na mataifa mengine yakoje? Wanatuonaje kama Taifa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mkapa aliwahi kusema, Tanzania inauhitaji ulimwengu kuliko ulimwengu unavyoihitaji Tanzania. Ni maneno ya hekima ambayo tunatakiwa tuyatafakari, watu wanatuonaje kwa sasa? Katika historia haijawahi kutokea, tunamkuta hata Balozi wa EU anaitwa kujadili mahusiano na Taifa letu, kuna nini? Tunatakiwa tujiulize, tunazungumza masuala ya kujipanga, lazima tujue Taifa letu limekaaje Kimataifa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, tujiulize foreign investors wanaionaje nchi yetu, are they comfortable kufanya biashara katika nchi yetu? Hatuwezi kukaa kimya tukajipongeza hapa tukawa na sifa nyingi na pambio lakini hatujiulizi haya maswali. Wawekezaji wanajionaje kuwepo katika nchi hii? Wako salama, wanaweza wakafanya biashara zao? Takwimu zinaonesha kwamba foreign investors wanafunga virago wanaondoka katika nchi yetu kwa sababu wanaona hawako salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, wawekezaji wa ndani wako salama? Hiyo purchasing power kwa watu wetu ipo? Haiingii akilini matajiri wa nchi hii wote hawana raha. Kama tajiri mkubwa, bilionea, anaweza akakamatwa katika nchi hii, akatekwa, akafichwa, akarudishwa, mambo yakaendelea kama yalivyo, nani atakuwa na raha ya kutaka kuleta hela katika nchi hii akafanya biashara? Serikali haisemi chochote, hatujui nani amemkamata, amerudishwa, alivyokamatwa hajapewa hata nafasi ya kusema alikuwa wapi, nani atakuja kuweka biashara hapa ndani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo hatuwezi kufumba macho kwamba hayapo katika nchi. Bado mnataka tukuze uchumi, haya ni masuala ambayo kama Wabunge lazima tujadili. Serikali lazima iwe accountable, usalama wa wafanyabiashara wetu ukoje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumza mambo ya kidiplomasia. Kuna clip moja ilikuwa inatembea, kuna Wanaigeria wawili walikuja hapa nchini wameitangaza dunia nzima jinsi ambavyo hatuko friendly kwa wageni. Kuna clip moja inamwonesha mtu wa Denmark/Danish alikuja kuwekeza, anamwomba Rais aingilie kati, hatuko friendly kwa hawa wawekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi Mheshimiwa Dkt. Mpango Serikali haieleweki inaendesha uchumi wa aina gani? Ni uchumi wa ujamaa na kujitegemea hundred percent ambao Mwalimu Nyerere alishindwa wakati ule au ni uchumi wa aina gani, tufafanuliwe. Kama ni uchumi tufafanuliwe watu wanakuja kuwekeza katika uchumi wa aina gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la nne, tujiulize, mazingira ya civil servants, katika Awamu ya Tano kila mtu amekuwa intimidated, kila mtu ametishwa. Tumezungumzia masuala ya Katiba, Taifa letu kwa sasa haliko united. Tunatakiwa tuwe na kitabu kimoja, tuwe na Katiba ambayo inatu-unite Watanzania wote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunapigana Vita ya Uganda, Mwalimu Nyerere alituunganisha wote, tuliona umuhimu wa kupigana Vita ya Uganda, lakini leo vita ya uchumi ni kubwa ambapo wote kwa pamoja tunatakiwa tushikane na kitu kinachoweza kutushikanisha ni Katiba. Hivi tunapozungumza maofisini watu wako timid, wana hofu, culture of impunity imekuwa ya hali ya juu sana, kila mtu anafanya anavyotaka halafu watu hawachukuliwi hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati mbaya sana Mheshimiwa Waziri Mkuu yuko hapa, hasa wateule wa Rais, wanaonekana wanamtii Rais peke yake, hakuna chain of command, kila mtu ni kambale. Utakuta Ma-DC hawaheshimu Mawaziri, Wakuu wa Mikoa hawaheshimu Mawaziri, kila mtu anafanya anachokitaka. Hii imesababisha kusiwe na discipline katika utendaji kazi katika ofisi za umma. Ni wakati muafaka kama Taifa kuji-unite pamoja, tuwe pamoja; upinzani ndani ya Serikali, watendaji wa umma na watu wote tushikamane pamoja ili tulijenge Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii culture of impunity, mfano mzuri ni bwana mkubwa mmoja hapa kila siku anatoa mambo ya ajabu. Ametoa matamko ambayo tumesikia hata watalii hawataki kuja nchi hii. Utakuzaje utalii kwa namna hii? Halafu Serikali mnasimama mnasema aliyoyasema ni ya kwake yeye, siyo msimamo wa Serikali. Sasa anawezaje mtu kusema mambo yake kwa kutumia instruments za Serikali? Amekaa kwenye ofisi na bendera ya Serikali na Polisi wa Serikali wanamlinda halafu mnasimama mnasema aliyoyasema ni ya kwake mwenyewe. Kama yake mwenyewe mbona hamjamchukulia hatua? Unatumiaje ofisi ya Serikali halafu mnasema ni ya kwake mwenyewe? Hatuwezi kujenga uchumi katika Taifa ambalo liko scattered, Taifa ambalo limetawanyika na halina umoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wa Utalii naye anasimama bila kuangalia madhara ya vile anavyo-twit; ana- twit, saa hiyo hiyo London nao wanarudi na majibu kwamba tuna-cancel trip na mnajua utalii unachangia fedha ya kigeni asilimia 17. Sasa tutajengaje uchumi wa namna hii Mheshimiwa Mpango na unapimaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapaswa tuweke mambo ya msingi. Tukianza na mambo ya msingi mambo ya juu yatajijenga yenyewe lakini kuna matatizo, wafanyakazi hawako comfortable…

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, we are in a serious business, tunazungumzia masuala ya uchumi na masuala ya uchumi yakiyumba tutayumba wote hapa. Hizi mbinu ambazo Serikali ya Awamu ya Tano inazitumia ni mbinu ambazo zilitumika karne ya 17 hazifanyi kazi leo. Katika jamii hii watu wanatishwa, hakuna usalama ndani, utajengaje uchumi ambapo hakuna demokrasia, hakuna uhuru wa mawazo na watu hawawezi kujieleza? Humu humu ndani watu tunashindwa kujieleza, tunajengaje uchumi wa hivyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona Serikali ya Awamu ya Tano imeleta kongamano kujipima namna ya utendaji kazi. Waliokwenda kwenye kongamano ni hao hao watendaji akina Mheshimiwa Kabudi. Ni hao hao wanaofanya kazi, ni hao hao wanaojipima, ni hao hao wanaojisifu. Hamtaki hata kusikia sisi tunawaonaje? Humu ndani we are not intruders, sisi ni part and parcel ya development ya nchi hii. You don’t want to hear sisi tunawaonaje. Mnafanya kazi wenyewe, mnajipima wenyewe, mnajipongeza wenyewe, halafu mnajitekenya wenyewe. Hiki ni kipimo gani mnachofanya? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo niliyoyasema lazima tujitafakari, mahusiano yetu na Kimataifa yako wapi? Tunahusiana vipi kwa sababu sisi siyo kisiwa. Rais wetu mpendwa mnampa kazi kubwa sana, lakini hamumshauri, ameshindwa kwenda… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nijaribu kutoa maoni yangu kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania siyo kisiwa. Tanzania ni miongoni mwa nchi nyingi zilizoko duniani na kwa kuwa Tanzania siyo kisiwa kwa hiyo ni taifa ambalo tunategemeana na mataifa mengine. Muda siyo mrefu sana na miaka ya nyuma kama Wabunge na kama Kambi ya Upinzani tumetoa ushauri mwingi sana, sana, sana hasa kwa Mheshimiwa Mpango. Kabla sijaendelea kuchangia nilitaka nipate majibu kwa sehemu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujua Mheshimiwa Mpango, tumekuwa tukiambiwa mara kwa mara kwamba uchumi unakua, ukiangalia exchange rate kwa sasa hivi (ukwasi) kati ya Shilingi na Dola, ameondoka Mheshimiwa JK hapa Dola moja tunalipa kwa Sh.1,600 na tukawa tunakusanya shilingi bilioni 800 lakini leo tunaambiwa uchumi umekua makusanyo yako shilingi trilioni 1.3 mpaka 1.4 lakini exchange rate kwa mfano jana ilifika mpaka Sh.2,400. Hii inamaanisha nini katika masuala ya uchumi wakati tunambiwa uchumi unakua?

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kwenye masuala ya mapato, tumeambiwa mapato tunakusanya sana na suala la GDP kwamba linaongezeka. Nilitaka nijiulize au tujiulize wote kwa pamoja tunapojadili haya masuala, masuala ya revenue, ni kweli hiki tunachokusanya ni revenue kwa wafanyabiashara wetu? Vyanzo vya mapato ni vipi ambavyo tunakusanya hii pesa? Au tunakusanya tozo na faini? Kwa sababu kuna uwezekano mkubwa…

T A A R I F A

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujua Mheshimiwa Waziri haya mapato tunayoyakusanya ni tozo au kweli ni vyanzo vya biashara tulivyonavyo? Kwa sababu takwimu zinazoonyesha kwamba biashara nyingi katika nchi yetu zinafungwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi navyozungumza kwa mfano Arusha Mjini kuna watu zaidi ya 650 wanafunga biashara, hawafanyi biashara. Sasa hizi tunazitegemea ni tozo au ni revenues na ni sustainable kwa siku zinazokuja au tunapiga kelele tu kwamba uchumi unakua? Mnatoza faini nyingi kwa wavuvi halafu tunasema tunakusanya kodi, hivi ni vitu ambavyo siyo sustainable. Lazima haya mambo tutafakari kama Wabunge na kama Silinde alivyosema tusiletewe taarifa ambazo ni za kubumba hazitusaidii kama Taifa ili tuweze kulishauri Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ni kweli uchumi unakua? Hilo ndiyo suala la kujiuliza. Kwa nini kuna tofauti kati ya economic growth na development growth? Kwa sababu kama kuna economic growth tungeona development growth inakuwa reflected lakini katika maisha ya watu hatuoni hayo mabadiliko pamoja na pambio na nyimbo nyingi za kwamba uchumi unakua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbona vyumba vya madarasa mashuleni hakuna kama uchumi unakua? Sasa hivi tunahangaika kwenye Halmashauri zetu vyumba vya madarasa tunashindwa kupeleka watoto kama huo uchumi unakua kwa nini hatupeleki hizo pesa? Kwa nini huduma za afya zinadidimia kama uchumi unakua? Haya ni mambo ambayo yanatugusa moja kwa moja. Kwa nini matatizo ya maji yameendelea kuwepo kama uchumi unakua? Haya masuala lazima tujiulize kama wawakilishi wa wananchi. Uchumi unakua kwenye makaratasi lakini kwenye mazingira ya uhalisia hauonekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la lingine tunaambiwa kwamba uchumi unakua kama ambavyo nimesema Mheshimiwa Mpango tumemshauri sana miaka iliyopita, twende kwenye Halmashauri zetu ndugu zangu Wabunge sijui wengine, mimi kwenye Halmashauri yangu ya Iringa pesa inayokuja ni ile ya kusukumasukuma elimu bure lakini pesa zote za maendeleo hazirudi. Mheshimiwa Mpango tulikukataza hapa usichukue mabango tuliyokuwa tunayategemea kwenye Halmashauri, tulikukataza hapa usichukue property tax, mlisema hapa kwa mbwembwe nyingi kwamba tunachukua vyanzo vya mapato, property tax, mlisema mnachukua mabango, mkasema hiyo hela itakuwa inarudi saa hizi hamjarudisha hiyo hela. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, TRA tuliwaambia hapa hata mimi nilisema hawana capacity ya kukusanya hizo pesa, hawawezi kukusanya pesa, hela hairudi, mmerudisha mara moja. Haya ni mambo tunatakiwa tujadiliane sasa huo uchumi unakuaje na hiyo hela hamrudishi kule? Utaratibu huu una-cripple D by D, Halmashauri zinashindwa kujiendesha halafu tunafichama hapa tunapongezana pongezana kitu gani? Huo uchumi unaokua unakuaje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema mwanzoni kwamba sisi siyo kisiwa tunahitajiana duniani. Haya yote tunayapata ni kwa sababu tumeshindwa kuwa na mahusiano ya kimataifa. Haya ni matokeo ya kutokuwa na mahusiano mazuri, diplomacy yetu imeporomoka kwa kiwango kikubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti yetu ya Taifa asilimia 40 tumetegemea wafadhili ambao mara nyingi kwenye chama chenu na kwenye tv yenu mmekuwa mkiwabeza, mkiwaita mabeberu lakini asilimia 40 ya bajeti yetu tunategemea mabeberu. Jambo analolifanya Mheshimiwa Rais la kusema tujitegemee ni jambo jema lakini tunajitegemeaje? Tunajitegemeaje wakati muda wote tumekuwa tukiwatukana na kuwakebehi wafadhili.

T A A R I F A

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, donors wetu ambao toka tumepata uhuru nchi za Ulaya zimetusaidia sana katika maeneo mbalimbali ya elimu, afya ambao kwa sasa hivi wametoa masharti kwamba nchi yetu haina masuala ya kidiplomasia, nchi yetu haina utawala bora na demokrasia katika nchi yetu haipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba mnasema sisi tunataka tujitegemee nakubaliana lakini ushahidi kuonyesha kwamba hatuwezi kujitegemea na matusi mnayowapa wafadhili na kila siku Waziri wa Mambo ya Nje hapa akisoma bajeti yake huwa anataja nchi wafadhili, wahisani waliotusaidia katika nchi hii, sipingi kujitegemea lakini namna gani tunahama kutoka kutokujitegemea kwenda kujitegemea. Hawa wahisani ambao wamekuwa wakitusaidia leo tunasema mabeberu lakini demokrasia haifanyiki, nani atakuwa na ujasiri wa kuja kuwekeza katika nchi yetu. Serikali ambayo haiwezi hata kumheshimu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani ambaye ana kura milioni sita inamweka ndani kwa ajili ya bail, ni mwekezaji gani kutoka nje atakuwa na confidence ya kuja kuwekeza katika nchi hii? Anayekuja kuleta mamilioni kama bail ya mtu mwenye wafuasi milioni sita anawekwa kienyeji kienyeji ndani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo mnaongea kwa ujasiri hapa, mtuambie ni kwa nini Waziri wa Mambo ya Nje, Profesa Kabudi na Dkt. Slaa walienda kupiga magoti kule nchi za Ulaya kama mnaweza kujitegemea? [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

Kama tunaona tunaweza kujitegemea, tumesema masharti hatuwezi, hawa ni watu ambao tunatakiwa…

KUHUSU UTARATIBU

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisema nasema uongo unanionea. Vyombo vya habari vimesema na hawajakanusha na kanuni zinataka kwanza yeye aseme kama mimi nasema uongo. Yeye athibitishe kama mimi nasema uongo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachosema, uchumi wa nchi hii tutaimba pambio hapa, tutapongezana, TBC itawasifu sana, lakini duniani kote nimesema Tanzania siyo kisiwa. Ili uchumi wetu uweze kukua tuimarishe demokrasia, na utawala bora…

KUHUSU UTARATIBU

MWENYEKITI: Mheshimiwa Peter Msigwa kwa vile huna ushahidi na hilo naomba ufute kauli yako.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Dkt. Kabudi, Dkt. Slaa na Mheshimiwa Mahiga walisimama walipokwenda Ulaya kuomba misaada, hawakupiga magoti. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoweza kusema…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Peter Msigwa.

Kwa hiyo kauli yako ya mwanzo umefuta? Haya sema nimefuta kauli yangu ile ya kupiga magoti.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Hiyo ya mwanzo nimefuta, imebaki ile ya kusimama. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mpango, Mheshimiwa Silinde hapa amezungumza hapa kwamba atayekuwa wa kwanza kwenda gerezani ni Katibu wa Hazina, lakini hata wewe Mheshimiwa Mpango hakitakukosa kikombe hiki kwa sababu mambo mnayoyafanya nje ya utaratibu katika Serikali hii yamekithiri kuliko kawaida na jinai huwa haifi. Msishangilie tu mambo haya kama hatuwezi kufuata utaratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe hii bajeti mnayohangaika na kusema haiendi vizuri, naomba nikuulize Mheshimiwa Mpango, kama wafadhili wanatoa hiyo asilimia 40 wanaotuletea pesa mnawaita mabeberu na huko barabarani ukipita unaona barabara kwa hisani ya watu wa Marekani, ukikuta daraja kwa hisani ya watu wa Marekani, UKIMWI kwa hisani ya watu wa Marekani, condom hisani ya watu wa Marekani, malaria hisani ya watu wa Marekani, mama na mtoto hisani ya watu wa Marekani, kama wafadhili wakiondoa asilimia 40 kwa moyo mweupe kabisa, hiyo asilimia 40 kwa mpango wenu wa Serikali mnaitoa wapi ili tuweze kujitegemea? Kweli tujitegemee hamna mtu anayekataa lakini mnajitegemea, mnaondoka kwa mbwembwe na matusi wakati uwezo huo wa kupata asilimia 40 hatuna. (Makofi)
Mkataba wa Ubia wa Uchumi baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. In principle, nakubaliana na mawazo ya Serikali kwamba mkataba huu tusiusaini, lakini kuna mambo ambayo kama Wabunge na kama wawakilishi wa wananchi lazima tuyajadili kwa pamoja tuone faida na hasara. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, napingana sana na wenzangu wanaofika hapa wanasema kwa sababu Mheshimiwa Mkapa amesema, Mheshimiwa Magufuli amesema, kwa hiyo, hatuusaini.
Mheshimiwa Spika, wajibu wetu sisi kama Wabunge hapa na hii ndiyo tabia ya Watanzania wengi, hatupendi kuhoji, hatupendi kudadisi, hatupendi kubishiwa. Hiki kitu kimekuja hapa, tuna haki ya kuhoji, kudadisi na kuuliza ili tukubaliane. Sisi siyo nyumbu kwamba tuingie tu mtoni, kwa nini mnataka tusidadisi? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, huu mkataba wataalam walipokuja juzi hapa, Profesa Kabudi alifafanua vizuri sana, lakini katika article 140 na kitu, alizungumza article karibu 20 au 15. Alizijadili hapa vizuri sana kwa weledi. Sisi kama Taifa amezungumza vizuri sana dada yangu hapa, tuna tabia ya ku-complain, tuna tabia ya kulialia! Complainers attract complainers. Kila wakati tunalalamika. Nakubaliana kabisa kwamba hii ni vita. Kila mtu anataka kupata hii keki ya uchumi duniani; kwa nini mnadhani Kenya wakubaliane na sisi kama wao hawapati maslahi? Kwa nini mnafikiri Europeans waje hapa kufanya mikataba kama wao hawana maslahi?
Mheshimiwa Spika, ni wajibu wetu sisi kama Taifa kutengeneza mazingira ambayo na sisi tuta-capitalise kupata faida. Siyo kila saa tunakuja hapa tunalialia, Kenya wametuzidi, Kenya wametuzidi. Kama wewe ni mpumbavu, upumbavu wako hauwezi kutoka kwa sababu unamchukia mwenye akili. We are responsible kujifunza kwa nini Kenya kila siku wanakuwa pro-active na sisi tunachelewa ku-capitalise huko mbele? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, wenzetu tunalia nao hapa kwamba wana mazingira mazuri. Sisi hapa tunalalamika; Mzee wa sound hapa kila siku ana viwanda vya kwenye mabegi. Sasa kama tuna viwanda vya kwenye mabegi, tutaenda kuuza nini Ulaya? Kutokuwa na kitu cha kuuza Ulaya is that their problem or is our problem? Badala ya kwamba sisi tukae hapa tujadiliane ni kitu gani tutapeleka Ulaya, tunalaumu kwa sababu hatuna kitu cha kuuza Ulaya. Is that their fault? That is our fault. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tumezungumza kwenye bajeti iliyopita, tumelalamika sana jinsi ambavyo Wizara ya Mambo ya Nje, imekuwa dhaifu katika masuala ya diplomasia ya kiuchumi. Ni kwa sababu hatuna wataalamu ambao wanaangalia mbele kuangalia Tanzania tunahitaji nini.
Mheshimiwa Spika, amezungumza dada yangu hapa, ukianza kujiuliza kaka yangu Mwijage hivi tunahitaji nini? Kwenye East Africa tunataka kupata nini? Tunataka kufanya biashara ipi? Iko kwenye makaratasi hapa halafu mnataka kutuambia Waheshimiwa Wabunge tukienda kwa wananchi...
Taarifa...
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Nakushukuru kwa taarifa, lakini wazungu sio watawala wa Kenya. Kenya inatawaliwa na Uhuru Kenyatta ambaye ni Mswahili.
Mheshimiwa Spika, ninachotaka kusema hili suala la blame shift, kila siku tuna-blame wengine tunashindwa kuwa responsible kwa uchumi wetu, hebu tuliache. Kwa sababu Wizara ya Mambo ya Nje ina udhaifu mkubwa sana katika nchi hii katika masuala ya diplomasia ya kiuchumi.
Mhemiwa Spika, nimemuuliza ni kitu gani tunataka kama Taifa upande wa Afrika Mashariki, ni kitu gani tunataka SADEC? Tunakuja hapa tunalialia tu, lakini hatujui tunataka nini. Hebu tuambie kwa mfano Wabunge tunataka tufanye biashara vipi na Afrika Mashariki, Ulaya, Marekani, Afrika ya Kusini au na Brazil? Tunataka tufanye biashara gani? Tunayo mikataba.
Mheshimiwa Spika, la pili, tumezungumza juzi kwenye ripoti ya …
Mheshimiwa Spika, naomba unilinde kwenye muda wangu, naona wanani-disturb sana.
Mheshimiwa Spika, kwenye ripoti ya GCI imezungumza sana jinsi ambavyo mazingira hata ya kufanya biashara katika nchi yetu ni magumu sana; mojawapo ya mazingira magumu ni kwamba Tanzania hatuna utaalam hata wa TEHAMA.
Mheshimiwa Spika, nchi za nje zinashindwa kufanya biashara na sisi kwa sababu hatuna utaalam huo. Mazingira ya rushwa, ufisadi na urasimu katika kufanya biashara, haya mambo hatu-deal nayo, matokeo yake tunaanza kuwalaumu Kenya, tunailalamikia Kenya, Kenya wanatuzidi, wametutangulia. Is that their problem or our problem?
Mheshimiwa Spika, pamoja na haya mambo yote ambayo Serikali ilileta wataalam hapa ambayo nakubaliana nayo kwamba lazima tuwe waangalifu, lakini lazima tuji-position mahali ambapo tuwe na uwezo wa ku-compete Kimataifa, siyo kulialia. We are like babies, every time tunalia, Kenya wametutangulia. Kwani wewe kutanguliwa unaona tatizo gani? Tulipata uhuru kwa pamoja; kila siku tunalialia Kenya wajanja, Kenya wajanja. Hapa Tanzania tunalalamika, Kenya wajanja; ukienda kwenye aviation, Kenya wanatuzidi; hata hapa Tanzania, wao wako zaidi.
Mheshimiwa Spika, ukienda kwenye tourism, Kenya wametuzidi. Tunalialia. Hatuandai watu wetu, hamweki mipango madhubuti ya kuandaa watu wetu kwenye mazingira ya kibiashara, tunabaki kulialia, mwisho wa siku tunakuwa kwenye mkia.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Kaijage.
Si Kaijage jamani!
MBUNGE FULANI: Mwijage!
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwijage, nakushauri, hivi viwanda vyako vya kwenye mabegi na kwenye mifuko ni kweli hatutapeleka bidhaa Ulaya, haiwezekani. Ni lazima tutengeneze mazingira. Mnalalamikia Kenya eti viwanda vya Wazungu viko Kenya, kwa nini nyie msilete viwanda vya wazungu hapa? Kwani si Watanzania wataajiriwa? Hiyo Dangote ni ya Mtanzania? Si ni Mnaigeria amekuja hapa Watanzania wanaajiriwa? Tusitafute visingizio tunashindwa kujipanga wenyewe, tunashindwa kutengeneza mazingira mazuri, halafu inapokuja mikataba hii tunaanza kulaumiana.
Mheshimiwa Spika, kubwa zaidi, nimemwona Mheshimiwa Hawa Ghasia hapa, mazungumzo mengine anayozungumza siyo ya kidiplomasia; ya kusema watu wengine tuna- support kwa sababu ya ushoga, hii siyo lugha za kidiplomasia. Tanzania siyo kisiwa, tunahitajiana vizuri sana.
Mheshimiwa Spika, la pili ambalo tunatakiwa tujue, kwa nini Kenya wamesaini? Lazima tujue kwa nini Kenya wamesaini? Haya masuala ya kidiplomasia ni vizuri tukatoa michango ya kidiplomasia kwa sababu tunahitajiana na watu wengine. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, leo wakenya wamesaini, Watanzania tunakaa pembeni; lakini kumbuka kuna siku kutakuwa na jambo ambalo Watanzania tutakuwa na faida nayo kubwa, lakini kuna uwezekano tukamhitaji Kenya au Rwanda. Wao watakapochomoa, itakuwaje? Kwa hiyo, haya ni mambo ambayo ni lazima tujadiliane kama Taifa, siyo tukiwa blind; lazima tujadiliane tu-dialogue.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Mheshimiwa Mpango, wakati anatuletea Mpango wa Miaka Mitano mara tu baada ya Serikali kuingia madarakani, mojawapo ya mambo ambayo Serikali ilikuwa imetutangazia na kutuahidi kwamba itayafanya ni pamoja na masuala ya demokrasia na utawala bora ambayo yanapatikana katika ukurasa wa 111 katika kitabu hiki cha Mpango wa Miaka Mitano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mojawapo ya mambo ambayo aliyasema alisema kuhakikisha usawa wa kiuchumi, demokrasia na uvumilivu wa kisiasa katika jamii. Ukomavu wa demokrasia na ushiriki wa wananchi utazidi kuimarishwa kupitia, akaelekeza mambo gani yatapitia jinsi gani itakavyoimarishwa. Mojawapo alisema kuwekeza zaidi katika kuboresha mfumo wa uchaguzi na kufanya kuwa wa kisasa zaidi pamoja na kuzidi kupanua uhuru wa kujieleza, uwazi, upatikanaji wa habari; kuna mambo mengi sana alizungumza katika mpango wa miaka mitano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunapozungumza tunakwenda kumaliza kipindi chetu kama Wabunge, Madiwani na kama Mheshimiwa Rais, lakini haya mambo yote ambayo Mheshimiwa Mpango alikuwa ameahidi katika mpango, Serikali ilituhakikishia kwamba itaimarisha demokrasia tukianza moja baada ya jingine katika kipindi cha miaka mitano, kila kitu hapa kimedorora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna uwazi wa vyombo vya habari, hakuna mfumo mzuri wa uchaguzi, hakuna mfumo wa kidemokrasia. Mara tu tulipoingia Bungeni hapa, kitu cha kwanza tulizuiwa mikutano, tukazuiwa Bunge live. nataka nimuulize Mheshimiwa Mpango huko ndio kuimarisha ambako alikuwa anatuambia wakati akituambia miaka mitano? Kwa sababu wamezuia Bunge Live, wamezuia mikutano wakasema Wabunge sehemu tunazotoka tutaruhusiwa kufanya mikutano na yenyewe wamezuia. Kibaya zaidi walisema wataimarisha chaguzi na hiki tunachokiona sasa katika nchi yetu ya Tanzania ambacho hakijawahi kutokea ni ishara tosha kwamba Serikali yenu haina mpango wa kuimarisha demokrasia na chaguzi huru katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kwa bahati mbaya Mheshimiwa Jaffo hayupo hapa, kinachofanyika sasa hivi kwenye Serikali za Mitaa kimsingi Chama cha Mapinduzi wanakunywa sumu. You are just drinking poison, inawezekana isiwaue leo lakini itawaua kidogo kidogo. Hamuwezi kusimama hapa mka-claim kwamba ninyi ni ma-champion and you don’t want to compete; victory inatokana na ushindani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanajiitaje washindi na hawataki kushindana? Katiba yetu inasema kila baada ya miaka mitano tutapambana uwanjani na viongozi bora wanapatikana baada ya ku-compete, hawataki competition, huo ni utawala bora wa aina gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tunapozungumza, Wenyeviti wa Mitaa wote karibu nchi nzima wamefunga ofisi wamekimbia, hawataki kupokea mapingamizi, watendaji wote wamekimbia kwenye ofisi za umma, tunasema tunataka tuzungumzie utawala bora, hawapo wanakimbia... (Makofi)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Waitara.

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa mchangiaji kwamba hili jambo limezungumzwa jana na leo. Mheshimiwa Spika jana alitoa maelekezo, leo wewe umetoa maelekezo na hapa tunapozungumza Mheshimiwa Waziri hayupo hapa lakini amekwenda Singida akakuta mambo sio kama walivyozungumza humu ndani, ameenda Manyara; tumetuma maafisa wetu wamekwenda kule Moshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nampa taarifa kwamba Mheshimiwa Msigwa tunayo kuanzia jana tarehe 5 na tarehe 6 ya mapingamizi, tunayo tarehe 6, 7 mpaka 9 ya Kamati ya Rufaa; maelekezo yaliyotolewa na Serikali ni kwamba kuna mtu amelalamika kama inavyozungumzwa waandike barua za malalamiko na malalamiko yatafanyiwa kazi, tunao muda mpaka tarehe 9. Kwa hiyo, usianue kwanza matanga kabla msiba haujaisha. Ahsante. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa unaipokea taarifa hiyo?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hii taarifa siipokei, inaonekana Mheshimiwa Waziri anataka kupotosha na hana information. Mimi kwenye Jimbo langu nina mitaa 192, wameenguliwa watu 185, sasa hivi wapo kwenye Ofisi za Kata zote zimefungwa; what are you talking about? Halafu mnataka kusema mnashinda, mnashindaje? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitoe mfano, wakati wa segregation kule Marekani Malcom X anatoa hotuba moja naomba ukaisikilize, kulikuwa kuna field negro na house negro. Humu ndani inawezekana wengine ni house negro hawajui tunacho-feel sisi ambao ni field negro kwenye field. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hamjui madhira tunayoyapata, kufanya siasa katika nchi hii imekuwa ni criminal, unahesabiwa kama ni mhalifu kufanya siasa ya nchi hii wakati Katiba inanipa mamlaka/uhuru wa kujieleza (freedom of expression). Ninyi mmekuwa ni house negro kwa sababu ni beneficiary wa mambo haya ndio maana hamuwezi kuyaona. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kuongea na wapiga kura wangu kwenye Jimbo langu na Wabunge wengi wenzangu wa upinzani ni uhalifu katika nchi hii. Tunaambiwa sisi lazima tuombe ridhaa ya kufanya mikutano, wengi wenu ninyi huwa mnaenda kufanya mikutano huko wala hamuulizwi na mtu yeyote. Kwa hiyo, tunaongea mambo ambayo tuna-feel.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nchi hii mnasema tushindane, Katiba inataka kila baada ya miaka mitano tushindane na nyie mnasema chama chenu kimeimarishwa; miaka minne hatujaongea, hatujafanya mkutano, Wenyeviti wa vyama vyetu hawajasafiri, mmesafiri ninyi peke yetu. Television mmezishika nyinyi peke yenu, unasema utawala bora; huo ndio utawala bora mnaotuambia hapa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, television, radio, mikutano ninyi, tunakuja kwenye mikutano seven days, you are running away, halafu mnakuja hapa mnasema tunatengeneza demokrasia, what kind of democracy is this? Mkifika uchaguzi mnakimbia mnasema kuna democracy, what democracy is this?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapokuja hapa kama tunataka tutengeneze nchi yetu tukubaliane kama tumeamua kufuta mfumo wa vyama vingi its well and good, mpo wengi, leteni Muswada wa Sheria hapa kwamba tumefuta mfumo wa vyama vingi tutabanana hukohuko si itakuwa ni sheria, tutabanana hukohuko kwenye majimbo yenu maana yake itakuwa ni sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Katiba ya nchi yetu inatupa uhuru kwamba, mtu ana mawazo tofauti na mwingine wala hatugombani, wewe una mawazo yako na mimi nina mawazo yangu, tunashindana kwa hoja, baadaye tunaenda kwa wananchi, huo uhuru uko wapi katika maelezo ya Mheshimiwa Mpango aliyoandika hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kitabu hicho hicho Mheshimiwa Waziri amesema kuhikisha kuwepo kwa mgawanyo wa madaraka na ufasaha wa mipaka baina ya mihimili mitatu ya Serikali kwa kuimarisha uwezo wa taasisi na rasilimali watu kwa kila mmoja kuwezesha ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, democracy ilivyoanza, separation inahitaji balance, tunahitaji ku-balance, mhimili unaojitegemea wenye mamlaka na nguvu. Tunapozungumza, nimezungumza hapa leo Bunge Live lilizimwa, huu ni mkutano wa wananchi wa Tanzania, tunakuja kutunga/ tunapoingia Bungeni hapa tunapanga bajeti ya wananchi milioni 50 waliotutuma tuje tuwatenge hela zao katika bajeti hii, tunazungumzia kuhusu afya zao, kilimo, shule na afya zao, leo tunapozungumza Wabunge tuliotumwa tunakuja hapa tupo gizani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wenzetu Kenya ambapo Mheshimiwa Spika alikwenda, wao mpaka kamati zipo live. Tunazungumza separation of powers, nguvu ya mhimili wa Bunge, hawa tunaowasemea mimi sijaja peke yangu na kila mmoja hajaja peke yake, anawawakilisha watu wake. Tumekuja hapa ili wananchi wale waliotutuma wasikilize tunachosema, tunafanya gizani; hiyo ndio separation of power?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanasiasa tunashinda mahakamani kwa kosa la kufanya siasa, sisi sio wezi, hatujavunja nyumba. Ninyi Serikali ya Chama cha Mapinduzi mnapata wapi legitimacy ya kusema watu wasiwe wezi kama nyie wenyewe mnaiba kura, where do you get that? Kama nyie wenyewe mna-rob kura mnapata wapi kwamba watu wasiibe mitihani, mnawaambia watoto wasiibe mitihani kama ninyi wenyewe hizi kura mnanyang’anya kwa nguvu, mnapata wapi kwamba watoto wasiibe mitihani? (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu utaratibu.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, where do you get that, where do you get that power?

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WATU ENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu utaratibu.

MBUNGE FULANI: Wanatengeneza hao.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, mnapata wapi hiyo nguvu?

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa. Mheshimiwa Jenista Mhagama, Utaratibu Kanuni.

KUHUSU UTARATIBU

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nitumie Kanuni ya 68 lakini naomba niende 68(1) lakini niende Kanuni ya 64(1) Kanuni ndogo ya
(a) hiyo inakataza kabisa ndani ya Bunge mtu kutokutoa taarifa ambazo hazina ukweli lakini nitakwenda mpaka Kanuni ya 65. Naomba Mheshimiwa Mbunge kwa kweli asiendelee kulipotosha Bunge kwamba uwepo wetu sisi hapa ndani na uwepo wa Serikali yetu unatokana na vitendo vya wizi wa kura na ndivyo vinavyotufanya tuendelee kuwepo madarakani.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuhuma hii, ni tuhuma kubwa na ni tuhuma ambayo sisi tunaojua Sheria na taratibu ushindi wa mgombea yoyote unatawaliwa na Sheria tulizonazo, Sheria za uchaguzi Katiba ya Nchi yetu na hapa ndani ya Bunge tunatawaliwa na Kanuni katika kuyaeleza hayo. Mgombea yoyote ambaye hajashinda ana uhuru wa kwenda Mahakamani na kwenda kueleza Mahakamani na kule Mahakamani wanaweza wakatoa nafasi ya mgombea yoyote kuthibitisha ama kuweka wazi kile kinachomkera. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, si kweli na nadhani anataka kutudhalilisha anapotutuhumu sisi wote, Serikali nzima, Wawakilishi wote wa Wananchi na hasa kupitia Chama cha Mapinduzi kwamba uwepo wetu hapa ni uwepo ambao si halali jambo hili si sahihi na anavunja Kanuni za Bunge. Kwa hiyo, tunamuomba sana Mheshimiwa Msigwa ama afute kauli hizi ama ajielekeze katika mjadala bila ya kuwa na tuhuma ambazo si za sahihi na hazina ukweli kwa mujibu wa Sheria tulizonazo kwa mujibu wa Kanuni na kwa mujibu wa Katiba.

MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge alikuwa akichangia Mheshimiwa Msigwa, ametoa maelezo marefu ambayo Mheshimiwa Waziri wa Nchi amesimama kuhusu utaratibu akataja Kanuni ya 68 na akataja Kanuni iliyokuwa ikivunjwa na Mheshimiwa Msigwa Kanuni ya 64(1)(a) ambayo Kanuni ya 64 kwa ujumla wake inazungumzia mambo yasiyoruhusiwa Bungeni na (1)(a) inazungumzia kutokutoa ndani ya Bunge taarifa ambazo hazina ukweli.

Mheshimiwa Msigwa kwa muktadha wa Kanuni zetu ukisoma hii kanuni ya 64 ukiizungumzia taarifa ambazo hazina ukweli itatupeleka kwenye Kanuni ya 63 inayozuia kusema uwongo Bungeni. Sasa kwa muktadha wa Kanuni hizo hizo zinataka hizo taarifa kama hazina uwezo wa kuthibitishwa basi Mbunge apewe fursa ya kufuta hayo maneno yake ili aendelee kuchangia. Kwa hiyo, na wewe nitakupa hiyo fursa ya kufuta hayo maneno yako halafu tutaangalia utaratibu mwingine kama utakubali kufuta, utakuwa umefuta kama hukukubali maana yake nitasimama tena.

Mheshimiwa Msigwa!

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumza suala hilo ukienda Ndarambo kule kwenye Jimbo la Silinde kura ziliibiwa kabisa mpaka tukaenda…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa, hapo unataka kueleza maelezo mengine, umepewa fursa ya kufuta kauli uliyokuwa ukizungumza, kama hukubali kufuta hiyo kauli uliyokuwa unasema, wewe sema ili nitoe maamuzi, umepewa fursa ya kufuta kauli uliyokuwa ukizungumza kama hukubali kufuta unao ushahidi, wewe utasema, mimi nitaendelea na utaratibu wetu wa Kikanuni. (Kicheko)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ushahidi wa kuibiwa kura tunao, ninao.

MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, Waheshimiwa Wabunge kwa mujibu wa hizi Kanuni zetu na mambo ambayo tunaweza kuzungumza humu ndani na sasa tunaelekea kukamilisha hili Bunge letu nataka kuamini kila mtu anaelewa Kanuni zetu matakwa yake ni yapi?

Kwa kuwa Mheshimiwa Msigwa unao ushahidi wa kuibiwa kura, na kwa kuwa huo ushahidi mimi hata ungeniletea hapa sina uwezo wa kujua kama ni wa kweli ama siyo utaenda kwenye Kamati ya Haki na Maadili ili ukathibishe kule hiki ulichokisema hapa. Kwa hiyo, kwa mchango wako wa sasa hayo maneno ya kuibiwa hutarudia mpaka utakapoenda kuthibitisha kule ile Kamati italeta taarifa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa.

MWENYEKITI: Nadhani tumeelewana vizuri, maneno ya kuhusu kuibiwa kura utaenda uthibitishe kule kwenye Kamati.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachosema tunapata wapi legitimacy kama sisi wenyewe hatuwezi kuishi yale tunayoyasema, Mheshimiwa Mpango kwenye Mpango wako.

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Taarifa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, democracy…

MHE. DKT. GODWIN O MOLLEL: Taarifa …

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Democracy ni kitu cha msingi ambacho…

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Taarifa …

MBUNGE FULANI: Taarifa ya nini?

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa kuna taarifa. Mheshimiwa Dkt. Mollel.

T A A R I F A

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, kiongozi mwenzangu hapa anajaribu kuzungumzia legitimacy ya kuzungumza mambo ya kiadilifu na kufanya mambo ya kiadilifu. Lakini yeye kwenye Kambi yake, kwa maana ya Chama cha Chadema Wabunge wote sasa hizi wamegoma kuchangia chama kwa sababu ya Mwenyekiti wao kuiba milioni mia sita akiwa yeye ni mbeba mkoba, akiwa yeye ni mmoja wapo wa wabeba mkoba kwenye wizi huo na hata ruzuku haionekani na siasa ndani ya chama chake, ndani ya chama chake haiwezekani kwa sababu hakuna resources na watu wote wamegoma kuchangia na kusaidia chama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa anasema hata huo wizi alitumwa na Chama cha Mapinduzi ufanyike na kwenda kununua hizo shamba Morogoro na vitu vingine ambavyo ni vya kibadhirifu vilivyoumiza chama chake.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa unaipokea taarifa hiyo?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitegemea utasema naye athibitishe kwa sababu anatuhuma watu kwamba wameiba.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa unazifahamu Kanuni ametoa taarifa, Kanuni inayohusu taarifa ni Kanuni ya 68 na uzuri tumeletewa na Mheshimiwa Spika hapa huna haja ya kubeba makaratasi, fungua Kanuni yako soma ya 68 amesimama kuhusu taarifa, unaipokea taarifa hiyo?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, siipokei, his house kneegrow anyway.

MWENYEKITI: Eeeh! Halafu Mheshimiwa Msigwa, unajua tangu mwanzo nilikuwa nimekuacha na wewe unafahamu hayo maneno huko kwenye nchi unayoisema yana maanisha nini. Na wewe unasoma vizuri huwezi kuita Mbunge mwingine kama kneegrow, kama wewe unataka kujiita kneegrow ni suala lako wewe.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Haja-complain.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa…

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Haja-complain

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa…

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Ehehe! Hamna aliyelalamika.

MWENYEKITI: Natoa maelezo kuhusu jambo unalotakiwa kulifanya ndio ninacho…

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Haja-complain…

MWENYEKITI: Naomba ukae, naomba ukae. Siyo suala la yeye ku-complain kazi yangu mimi kusimamia utaratibu hakuna Mbunge anayeweza kuitwa kneegrow humu ndani hayupo.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kasema Mbowe mwizi, kasema Mbowe mwizi, kasema Mbowe mwizi, umenyamaza,

MBUNGE FULANI: Mwizi.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, si umenyamaza alivyosema Mbowe mwizi…

MWENYEKITI: Mheshimiwa, Mheshimiwa Msigwa tusibishane, nimesema nakuelekeza utaratibu, kama unataka kuusikiliza, sikiliza usijibizane na mimi. Nasema hizi maneno hayo kule yanakotumika yana maanisha kitu kibaya sana na wala hakuna mtu anataka kuitwa hayo maneno. Humu ndani hawezi kuitwa Mbunge mwingine hayo maneno kama mtu amelalamika, ama hajalalamika kazi yangu kusimamia utaratibu na nilikuwa nimekuacha tangu mwanzo ili umalize mchango wako halafu nije niseme mwisho ana maanisha nini, sasa kwa kuwa unaendelea kuyasisitiza hakuna Mtu anayeitwa jina hilo humu ndani, naomba uendelee na mchango wako. (Makofi)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mpango ninachokisema kwenye kitabu chako ulituambia utasimamia democracy, tunaongea miaka mitano sasa tunamaliza kipindi chetu democracy ya nchi hii sasa hivi iko ICU, uhuru wa Vyombo vya habari ni disaster, waandishi wa habari wamekamatwa, wengine wamepotea, wengine hawawezi kujieleza, vyombo vingine vimekamatwa, Wabunge hawawezi kufanya mikutano kwenye majimbo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kubenea kwa mfano miaka miwili hawezi kufanya Mkutano, Mheshimiwa Halima hawezi kufanya Mkutano, Mheshimiwa Sugu hawezi kufanya Mkutano, Wabunge tunakatazwa, hii ndiyo democracy inayosema kwenye Mipango ya miaka yako mitano, na ulivyokuwa unazungumza Bajeti ya mwisho hapa ulinukuu mpaka maneno ya Mungu, ukasema Mungu atusaidie, ukanukuu na vifungu vya Biblia, halafu ukasema wananchi wakachague wagombea wa Serikali za Mitaa wanaotokana na Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo huu uchaguzi ambao unasema wakachague huu wa kupora, wa kupora kwa nguvu, katika nchi ya kidemokrasia, hebu vaeni vitu vyetu nimesema mna hiari mko wengi, leteni Muswada hapa kwamba tunafuta mfumo wa Vyama vingi tusijidhalilishe Duniani kwamba tuna democracy wakati hakuna democracy. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnaogopa, mnaweka mpira kwapani halafu mnashangilia, tumeshinda, tumeshinda… Unaweza kuwa champion bila kushindana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, the finishing line is for the winners, you cannot be a winner without competition, ingizeni mpira hapa, tuweke Wagombea wetu na ninyi muweke, tuone mziki wananchi wanamtaka nani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka mitano mmetuzuia, mmetuzuia muone tutakavyocheza mpira uwanjani, how do you call you self that you’re a champions. Watu wa Turkey, Waturuki wanasema when the fish is rocking it is start from the head. Hizi zote vurugu za Watendaji wa Mitaa na nini, ni matatizo ya Wizara, ni matatizo ya Serikali yenyewe, hiki kiburi cha kufunga Ofisi cha kufanya nini, msitudanganye, ni kwamba mmeona huko nje hali ni mbaya mlisema tumekufa, hatujafa, we are still standing. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mnajiaminisha mnaweza njooni uwanjani tucheze mpira, ili hayo uliyoyasema yathibitike tuweze kuendesha nchi nzuri ambayo Mungu ametupa, tusidanganye hapa, nakushukuru sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niungane na wenzangu. Kwamba Wizara hizi ni Wizara nyeti kama alivyosema Mheshimiwa wa Bukoba; ni Wizara Mtambuka ambazo ni muhimu sana kwa uchumi wetu.

Mheshimiwa Spika, lakini mimi leo sitakuwa na huruma kwa Mawaziri. Asilimia kubwa ya Mawaziri tulionao katika Serikali hii wanafanya kazi ambazo ni ad hoc au wanashughulika na kero wanaacha suala la msingi na majukumu ya Kiwaziri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, majukumu ya Kiwaziri ni kushughulika na Sera, usimamizi na tathmini, lakini muda mwingi utawakuta Mawaziri hawa wako barabarani. Utamkuta Waziri huyu anachukua ruler anapima samaki; wanafanya kazi za operational ambazo inaonekana kwamba mifumo ya nchi hii imefeli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Waziri anapoanza kufanya kazi za operation maana yake mifumo imefeli. Unamchukua Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi naye anaenda mahali na camera kutatua mgogoro wa Kiwanja sijui cha Juma na Hadija, maana yake mifumo imefeli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, unamkuta Waziri wa Kilimo naye anahangaika sijui nani ameuza nini wanaenda kwenye kazi za operational wameacha majukumu yao ya kazi na hii inamuwia Rais kazi ngumu sana, inafika mahali na yeye mpaka anaanza kusuluhisha na ndoa barabarani. (Makofi/Kicheko) [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

Mheshimiwa Spika, hatuwezi kuendesha nchi kwa namna hiyo kwa sababu kazi zenu Mawaziri mmeacha kushughulika na masuala ya Sera; na mimi nataka nijikite zaidi Maliasili kwa sababu mimi ni Waziri Kivuli wa Maliasili, lakini mnashughulika zaidi na kutatua migogoro na mnapenda sana kutatua migogoro kwa sababu mnaunda Kamati, ikiisha Kamati mnaunda nyingine, kwa sababu kuna hela huko; mmeacha majukumu yenu ya kutengeneza Sera. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hatuwezi kutoka kwenye maendeleo kama hamsimamii Sera zenu; kazi za migogoro kuna watu wanaofanya kazi hizo; na hatuwezi kuwaonea huruma lazima tuwaseme ndiyo kazi yenu mliyoitiwa hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ya Maliasili pamoja na kwamba ina vivutio vingi katika nchi yetu lakini bado haiko katika tano bora za kuwa destination ya watalii katika nchi hii; hilo ni tatizo kubwa kwa sababu tumeyaacha masuala ya msingi. (Makofi)

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, leo unamkuta Waziri anapiga kelele kwamba anataka kurogwa ameacha kuleta ideas za kutuhamisha kutoka hapa tulipo twende hapo mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwenye mitandao kila wakati anasema wanataka kumroga badala ya kukaa chini.

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, apate ideas namna gani ya kukuza watalii katika nchi hii. (Makofi)

SPIKA: Mchungaji kuna taarifa unapewa.

T A A R I F A

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Spika, nashukuru nilikuwa naomba nimkumbushe Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa mfumo wa kiutawala nchini Mawaziri wetu ni Wabunge pia ni Parliamentarians; na kama ambavyo sisi Wabunge hatuna mipaka kwenye kufatilia kero za wananchi basi ni hivyo hivyo Waheshimiwa Mawaziri ambao pia ni parliamentarians kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hawana mipaka kwenye ku-implement nafasi zao za Kibunge; ahsante sana.

SPIKA: Mheshimiwa Msigwa unapokea taarifa hiyo ya Mheshimiwa Mboni.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, kama Waziri ni Mbunge achague kimoja anaweza akakataa Uwaziri afanye kazi ya Kibunge. Sisi ni back benchers, hawa wanatakiwa watupe majibu na wafanye majukumu ambayo wamepewa kwa mujibu wa kazi; lakini wewe unapoteza kodi ya wananchi tena usinipotezee muda kwanza tufanye kazi ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ya Maliasili ina majukumu mawili; kutunza Maliasili na kutangaza utalii. Kuna majukumu makubwa sana ya kutunza Maliasili, nalo ni jukumu kubwa sana. Wako watu wa TANAPA, Ngorongoro, kazi yao ni hiyo. Tunategemea Waziri asimamie sera. Narudia tena, operational si kazi yake, kama ni kutangaza wako watu wa TTB wanatangaza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo kazi ya kuleta watalii hapa imebaki kuwa ya travelling agents si ya kwake tena, wao sasa wanaingia kwenye operational na wanaacha kazi zao; ndiyo maana kumekuwa na migongano mingi katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano takwimu zinaonyesha watalii wengi wanaokuja nchini kama nilivyosema wanaletwa na travelling agents lakini Waziri hasimamii zile sera ili kuhakikisha tu-boost huu utalii uje. Hawa wanaosema wameongezeka wengi wao ni wale ambao hata hao akina Esther na akina Heche wakipita pale Serengeti nao wanajumuishwa kwamba ni watalii, nao wanaongezwa kwenye idadi; halafu mnajaza idadi hapa kwamba watalii wameongezeka kwa sababu hatufanyi kazi ambayo tunatakiwa tufanye. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano Waziri ambaye ni makini kama tunataka tukuze utalii katika nchi yetu…

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: …Mheshimiwa Spika, China peke yake mwaka jana….

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

T A A R I F A

SPIKA: Taarifa Mchungaji unapewa.

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Spika, naomba nimpe taarifa mzungumzaji kwamba kuna watalii wa ndani na kuna watalii wa nje. Sasa kama hawatambui watalii wa ndani labda ni tafsiri ya kule Iringa.

SPIKA: Taarifa unapewa Mchungaji.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nampuuza huyu, angekuwa Mbunge nampuuza, angekuwa Mbunge makini angejua utalii wa ndani unaingiza shilingi ngapi katika nchi hii. Sasa kwa sababu hujui pamoja na kwamba unatoka Serengeti tusipoteze muda. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano naishauri Wizara ya Maliasili, mwaka jana China peke yake watalii kutoka China kuja duniani kote kutembea sehemu nyingine walikuwa milioni 150, lakini waliokuja Tanzania walikuwa karibu 11,000 tu. Kwa Waziri makini, hayo ndiyo masuala ya kukaa na kujadiliana na ku-capturise katika watu milioni 150 hawa Wachina, Tanzania nifanye nini ili hawa watu milioni 150 wangapi watakuja Tanzania. Lakini badala yake unawachukua akina Steven Nyerere mnaenda Mlima Kilimanjaro sijui unamtangazia nani. Alisema Mheshimiwa Lema juzi hapa, unaenda nao kule unafanya kazi za operation, mnapiga picha sijui unamtangazia nani? (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, mwaka huu China ilitegemewa kutoa watalii milioni 180 duniani kote, lakini huoni Wizara ikikaa kwamba hapa pana mtaji mkubwa tunataka Wachina waje, hakuna mkakati wowote. Bahati mbaya sasa hivi imekuja hili gonjwa labda watapungua, lakini hakuna mkakati wowote ambao kama Wizara inapanga, kwamba kwenye eneo hili hebu tu-capturise tunawaleta watalii wangapi, badala yake unaenda kutatua mgogoro wa Loliondo sijui na nani.

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, taarifa.

T A A R I F A

SPIKA: Taarifa!

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, mwenzetu kwanza amejikita kwenye kulalamika haoneshi solution, lakini yeye ni mojawapo wa pioneer wanaopinga ununuzi wa career zetu kwa sababu ameonesha watalii wa China ni zaidi ya 50,000 lakini waliofika Tanzania ni wachache. Maana yake wenzetu ambao wana career zao ndio hao wanapeleka watalii wengi wanaishia kwenye nchi zao. Yeye anatakiwa sasa afike mahali ile pioneering yake ya kupinga Tanzania kuwa na ndege zake kwa ajili ya kuboresha utalii, aanze kuanzia leo kuunda na kutupa mawazo mengine yatakayotufanya tuende mbele. (Makofi)

SPIKA: Pokea taarifa hiyo.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, Waziri makini angefanya projection kwamba Tanzania nataka nifanye iwe destination Africa watalii waje wengi wanatoka wapi? Waziri makini angefanya projection kama hivyo angweza ku-capitalize kutoka China kuna watalii wangapi. Sasa hivi wanaongoza kuja Tanzania ni watalii toka Marekani. Waziri makini asingehanganika na kina Steven Nyerere, Waziri makini angewachukua watu kama wakina Roger Federer, sijui kama unamjua wewe Roger Federer. Unawatangaza duniani kama wenzetu Rwanda wameandika visit Rwanda hapa unamchukua…

MBUNGE FULANI: Kuhusu utaratibu

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, unamchukua wachezaji wazuri wa tennis au unamchuku huyu wa basket LeBron James unatangaza nchi yako…

SPIKA: Kuhusu utaratibu.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Spika, kwa Mujibu wa Kanuni ni marufuku Mbunge kujielekeza katika jambo ambalo halipo mezani na…

SPIKA: Tumsikilize tupe kanuni gani halafu uweze kuendelea. (Makofi)

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Spika, Kanuni ya 28.

SPIKA: Hebu isome, naomba tusikilizane Waheshimiwa twende kwa utaratibu. (Makofi)

Naomba tusikilizane, Waheshimiwa tusikilizane kanuni 28 amesema.

WABUNGE WENGINE: Aaaah!

MBUNGE FULANI: Kwa kuheshimu muda asisome.

SPIKA: Naam!

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Spika, kwa kuokoa muda na sijafungua tablet naomba nisisome.

WABUNGE WENGINE: Aaaah!

SPIKA: Unaweza ukakaa tu Mheshimiwa, Mchungaji malizia dakika zako.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, kama tupo serious na kuongeza utalii lazima tuwe serious. Rwanda baada kusema inavyotangazwa mpira duniani kule ime-double watalii kuja kwenye nchi yao. Kwa hiyo, unaita watu, unatangaza na watu wanojulikana kama vile akina Serena Williams. Unatangaza, unachukua watu wakina hawa wakina Steven Nyerere nani anawajuwa? Hata hapo Blataya ya Malawi hakuna anayewajua lakini Waziri ndio anaenda nao kuwatangaza nani anawajua? We are not serious, anapanda mlima hata hatua mbili hafiki unamtangazia nani? (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kama tupo serious na biashara hii nimshauri Waziri tumieni pesa watafuteni watu ulikuwa haupo, watafute kama watu akina Roger Federer, akina Djokovic wanajulikana akipiga tennis pale wanaandika visit Tanzania dunia nzima inaona. Na usiogope kurogwa hamna atakaye kuroga tangaza nchi vizuri. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Msigwa unaniacha hoji. Kuroga roga ndio kitu gani? Maana yake unaonge vitu ambavyo Spika havielewe. (Kicheko)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, vilikuwa kwenye mitandao Mheshimiwa. Sera, sera ya utalii ilikuwa ni low volume high yield ambayo ni mwaka 1976. Lakini ukienda katika utendaji na jinsi Waziri anavyofanya sasa hivi ina-contradict. Sasa hivi wanataka mass tourism, lakini ukiangalia wanavyo practice hii ya low volume na high yield na hii ya mass tourism katika implementation yao kuna contradiction fukwe hamjaziandaa, hakuna vitanda ukingalia maeneo mengine…

SPIKA: Hiyo kengele ya pili Mchungaji.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, wamenikatisha katisha Mheshimiwa.

SPIKA: Kengele ya pili.
Itifaki ya Nagoya ya Kusimamia Upatikanaji na Mgawanyo Sahihi wa Faida zitokanazo na Matumizi ya Rasilimali za Kijenetiki.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, in principle sina tatizo na itifaki zilizoletwa, lakini nilitaka tu tujitafakari kama Bunge. Hili Bunge letu la Bajeti ni Bunge la muda mrefu na Bunge huwa linajua ratiba itakuwaje. Lakini kumekuwa na mazoea kila siku mnapoleta itifaki hizi mnatuletea siku hiyo ya kupitisha hizo itifaki. Hii inaonesha jinsi gani ambavyo Bunge linaonekana halitimizi wajibu wake na kwamba Serikali inatuchukulia poa tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi vifungu ukiwauliza Wabunge unavipitia saa ngapi, kila wakati itifaki zinapokuja zinaletwa siku hiyo hiyo, hivi vifungu unavipitia saa ngapi? Unasoma saa ngapi? Unapewa dakika tano kuchangia wakati ingegaiwa mapema kwenye Kamati watu wangepitia tunapojua ratiba inavyokwenda tuje tusome, lakini imekuwa business as usual tunapiga makofi na Bunge tunakubaliana mikono yetu na nguvu yetu ya Bunge inapungua nguvu kwa mambo kama haya ya kuridhia mambo ambayo hayawezekani, kwa sababu ni mambo ya msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Watalaam wanasema the past is where you have learn the lesson and the future is where you apply the lesson. Asubuhi hapa tumejaribu hata kuomba miongozo, mambo ya Hati za Dharura tunarudia tena kana kwamba mambo ya nyuma hatujajifunza kwa sababu tunaenda haraka haya mambo! Wabunge hebu tujiulize, hivi wananchi huko wakituona tunaondoka tumebeba mavitabu haya, tunasoma saa ngapi? Tunasoma saa ngapi hivi vitabu! Tunaletewa muda mfupi! (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, hii ni kulifanya Bunge liwe crippled, Bunge ambalo haliwezi kuisimamia Serikali, kwa hiyo hapa sisi tumekuja ku-rubber stamp. Tukubaliane kwamba, Bunge hili linaongozwa na Serikali, Bunge haliwezi kuisimamia Serikali kwa sababu tunakuja hapa tuna-rubber stamp… (Makofi)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoomba hili Bunge letu, Serikali iwe inafanya vitu kwa utaratibu, kwa sababu Serikali zote duniani huwa zinapenda


kulifanya Bunge liwe kibogoyo ili zifanye mambo yake vizuri. Na sisi kama Wabunge tuna wajibu wa kuhakikisha tunachukua role yetu kuisimamia Serikali. Hatuwezi kuchukua role kama tunauziwa mbuzi kwenye magunia. Huku ni kuletewa mbuzi kwenye magunia, halafu tunashangilia katika vitu ambavyo hatujasoma, na ni kukwepa wajibu wa Bunge. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, tunaposema mikataba na sheria ziletwe Bungeni hatumaanishi iletwe kama hivi itupwe hapa! Tuna maana iletwe tupate muda wa kuisoma na kuitafakari ili tuone ni jinsi gani tunawawakilisha wananchi ambao wametutuma, lakini ikiletwa tu hapa inakaa mezani, inaletwa hapa, halafu wanasema tunaazimia, watu tunapiga makofi, tunasema ililetwa Bungeni, hiyo siyo maana halisi ya kuletwa Bungeni. Hakuna kati yetu hapa aliyesoma hapa tukisema lipi ambalo tunaazimia hapa, waliosoma ni wachache sana kwenye Kamati idadi kubwa ya Wabunge hatujasoma. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, hilo ndiyo naliomba tuliinue Bunge letu kiwango. The more tutakuwa na Bunge dhaifu, the more tutakuwa na Serikali dhaifu. Hawa Mawaziri lazima tuwashughulishe wafanye kazi. Hawa Mawaziri hawatafanya kazi kama Wabunge tutakuwa weak. Ni lazima tuwe after them, watakuwa na nguvu ili kuishauri Serikali na ndiyo wajibu wetu. (Makofi)

Mheshikiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi, dakika tano na mimi nitakwenda brief, hazitoshi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mtaalam mmoja na mwalimu wa mambo ya kidini anasema; “the greatest mistake in life is being busy but not effective na the greatest challenge in life is knowing what to do”. Kwa bahati mbaya sana Serikali ya Chama cha Mapinduzi hii ya Awamu ya Tano inaonekana iko busy sana, lakini haiko effective. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niungane na Mheshimiwa Mnyika kama kweli tuko serious, kuna Wabunge hapa wanasimama kwamba kwenye Majimbo yao upatikanaji wa maji ni asilimia 16 na bado wanapiga makofi wanaunga mkono bajeti hii. Mheshimiwa Mnyika amependekeza hapa tuunde Kamati Teule kama ambavyo na Mheshimiwa Esther Matiko amesema, kama ambavyo Mabunge huko nyuma yamefanya kwa ajili ya kutatua tatizo la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ndugu zangu tatizo la maji ni kubwa sana kama Serikali hii ina-syncronise utendaji wake kazi, mojawapo ya kikwazo kikubwa cha watalii kuja Tanzania ni pamoja na mambo ya hygenic. Inaonesha Tanzania kuna uchafu mkubwa hakuna maji, sasa usafi utapatikanaje bila maji? Hiyo ndiyo inatuangusha duniani kwamba kuna uchafu Tanzania, kuna kipindupindu, maana yake watu wanakula kinyesi na maji yanasababisha watu wasiugue. Sasa tunaleta utani katika masuala ya maji, jukumu pekee ambalo tunalo Watanzania ni kuondokana na bla bla za Chama cha Mapinduzi ambazo zimefanyika muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivi ndugu zangu kama kweli Wabunge tunavaa na suti hapa, inaingiaje akilini kwamba matatizo ya maji kijijini mpaka Mheshimiwa Rais apige simu amuambie Katibu Mkuu wa Wizara anamuunganisha na Mtendaji wa Kijiji, tunaona ni jambo la kawaida kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Katibu wa Wizara ambaye juzi nilisema hapa wajibu wake mkubwa kusimamia hizi sera na utendaji, amekazana kwenye mitandao anagombana na maaskofu, this is a serious business, haijawahi kutokea katika nchi hii Katibu wa Wizara ana majukumu makubwa ya Wizara, badala ya kushughulika na matatizo ya maji, hivi akilini inaingiaje kwamba Katibu wa Wizara unamuunganishaje na Mtendaji wa Kijiji wakati hiyo shughuli iko kwenye Local Government? Inaonesha kwamba system ime-fail, haifanyi kazi. Tunafanya majukumu mazito tunashindwa utekelezaji wa kazi. Hili suala la maji ni serious business.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Mbele yetu ni Wizara nyeti katika Taifa letu na hasa katika shughuli nzima za kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara hii ni kama kufanya business. Na ili ku-operate business kubwa lazima uwe na investiment kubwa, kuwe na brain kubwa ambayo unaiweka katika business unayotaka kuifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu sana nimekuwa Mbunge sasa wa miaka tisa, lakini katika Wizara hii imekuwa ni kutatua migogoro ya Loliondo na wafugaji, kutatua migogoro ya watu wa Ngorongoro na wafugaji, kutatua migogoro ya TANAPA na wananchi, mipaka ni tatizo. Imekuwa ni kutatua migogoro ya maeneo chepechepe, kwa mfano kule Kilombero, Ihefu na wananchi. Kwa hiyo, badala ya kufanya business tunajikuta kama Taifa tuko busy kutatua migogoro badala ya kusonga mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani ni wakati muafaka kama Serikali tufike mahali tuseme enough is enough, tufanye biashara inayotokana na Wizara hii, kwa sababu, migogoro imekuwa mingi hatutoi suluhisho la kudumu katika masuala ya mipaka, kwenye maeneo oevu, kwenye maeneo ya hifadhi, hatujatoa suluhisho la kudumu. Hatuwezi kuendelea kama tunaendelea kukaa chini na kutatua migogoro badala ya kufanya business na kushindana kimataifa namna gani tuweze kufanya hii biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo napenda nizungumze kwa upana sana eneo moja. Kumekuwa na biashara ya viumbe hai, wanyama hai ambao wamekuwa wakisafirishwa. Biashara hii imekuwa ikifanywa toka wakati wa mkoloni na wakati wa mkoloni ni wazungu tu walikuwa wanasafirisha, mpaka mwaka 1974 ikabadilishwa wakawa wanafanya wazawa peke yao. Sasa kwa bahati mbaya sana hawa watu wamefanya biashara na wamefanya kwa mujibu wa sheria, lakini kama hotuba yetu ilivyosema ghafla wakati wa Mheshimiwa Maghembe biashara hii ilisitishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ilisitishwa wakati watu hawa wameshafanya maandalizi, wamekamata wanyama wamewaweka kwenye holding grounds, wamekopa mikopo, wamefanya contact na wateja wao duniani kote, ikaja hii biashara ghafla ikasitishwa. Watu hawa hii biashara hawafanyi wanyama ambao wako kwenye National Parks, kwenye Game Reserves, wanafanya biashara ya huku porini ambako kuna nyani, kuna ngedere, kuna spiders, kuna konokono na nyoka na mijusi, vitu ambavyo havitumiki kwa biashara nyingine katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hawa watu baada ya Serikali kusitisha wameingia katika umasikini mkubwa sana, wengine mpaka juzi nimesikia wamekufa. Ningeomba Mheshimiwa Waziri hebu tutoe jibu kwa hawa watu ni kwa namna gani tutawalipa fidia, hawa ni Watanzania. Ukiangalia biashara hii ilikuwa inaongeza pato la Taifa, fedha yake inayotumika asilimia 100 Serikali haiingii hasara na tunapata fedha ya kigeni, hawa watu wamefanya kazi kubwa sana kulikuwa na wakamataji, kulikuwa na mahoteli, ikasitishwa na wengine mpaka walikufa, wale watu waliopelekwa Mahakamani mpaka leo walishinda kesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa watu wameendelea kuwatesa, tumewa-cripple, ningeomba Serikali itoe jibu lake; wametoa malalamiko kwako Waziri, Waziri aliyepita, wametoa kwa Rais, naomba hawa watu Mheshimiw Waziri awaangalie kwa jicho la huruma. Muda mwingi tumezungumza watu wengine sana, hawa ni wafanyabiashara wadogo wadogo na ni Watanzania wazawa ambao walikuwa wanajitahidi kujitokeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kibaya zaidi Serikali huwa inatumia pesa nyingi kuangamiza ndege kama kwelea kwelea. Kwa mfano kuna wakati waliuwa ndege karibu milioni 70, sasa unapoua wale ndege dawa zile wanaposhusha kuwaua wale ndege, dawa zile zinaua na mijusi na hao nyoka ambao wale watu wangewasafirisha tukapata hela. Sasa haya ni mambo ambayo hebu tuangalie namna gani tunaweza tukafanya biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimezungumza hapo mwanzoni hii biashara ni business na namshukuru Waziri ni mfanyabiashara, lazima ana business mind. Wizara hii tukiichukulia kama Wizara nyingine bila kuwa na upeo wa kibiashara hatuwezi kusonga mbele, hatuwezi kuingia kwenye ushindani, lazima kuwe na fikra za kibiashara. Katika maeneo mengine Mheshimiwa Waziri amefanya vizuri, siwezi kumkandamiza katika kila eneo; alitoa kwa mfano ile Tanzania Unforgetable, nilitamani sana ingetumika hata wakati wa Timu yetu ya Taifa, Tanzania Unforgetable, kuliko ile tuliyotumia “Sasa hivi ni Zamu Yetu”, tukienda nchi sasa hivi ni zamu yetu haiwezi kutusaidia, ingetusaidia kutangaza utalii, lakini tungelitumia hilo neno ni neno zuri ambalo linaitangaza nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ambalo wamefanya vizuri ni kwenye masuala ya ujangili. Wizara imefanya vizuri, hatuwezi kuwalaumu, nimekuweko kwenye Wizara hii ujangili kweli umeporomoka, lazima tuwapongeze katika hilo; lakini ninachosema kwenye eneo hili la hawa watu ambao wana shida, tumewatesa kiasi cha kutosha naomba Waziri atakaporudi atoe tamko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni suala la sheria zinazokinzana; kuna sheria nyingi zinakinzana, Sheria za Ardhi, Sheria za Mazingira, Sheria za Maliasili, zinakinzana maeneo mengi kiasi kwamba, hazitekelezeki, Sheria za Madini, kuna maeneo mengi ambayo hizi sheria zinakinzana kila eneo. Ningeomba hili suala limalizwe ili tuache kukaa muda wote tunagombana na kutatua migogoro, tuwe tunafanya biashara tunashindana na watu wengine duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, success is attracted, you don’t pursue success, ni lazima tutengeneze mazingira ambayo yata-attract mafanikio katika nchi yetu, lakini hatuwezi kutengeneza mazingira kama tuna watu wa aina ileile. Ili tu-attract success katika nchi yetu lazima tuwe na watu ambao wanavutia hayo mafanikio. Ni sawa na mbegu ya mahindi, mbegu ya mahindi ukiiweka kwenye simenti haiwezi kuota mpaka uitengenezee mazingira uweke maji, uweke udongo mzuri, uweke mwanga na oxygen, hewa, maana ndio itaota. Sasa tukiwa na watu ambao hawafikiri kibiashara, tukiwa na watu ambao hawafikiri Kitaifa, we have to think globaly and act local, lazima tubadili namna ya kufikiri katika namna nzima ya kuiendeleza Wizara hii ya Maliasili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba Mheshimiwa Waziri, najua wamefanya kazi kwa sehemu ambayo wanaenda mbele, kwa mfano wamefungua Television ambayo inatangaza nchi yetu, tutakuwa hatufanyi vizuri kama tusiposema mambo haya, hayo ni mambo mazuri ambayo lazima tuyapongeze kwa sababu tunataka tu- attract watalii zaidi. Hata hivyo, bado tunahitaji urithi tulionao na resources tulizonazo, it is highly time kwamba, tuchague, ni kwa kiasi gani Ngorongoro inatusaidia na tuna faida nayo. Tuchukue maamuzi ambayo yatatufanya Ngorongoro itusaidie, ni kwa namna gani maeneo oevu kama Kilombero yanatusaidia kama Taifa? Tufike mahali tuamue tunataka watu wachunge ng’ombe au tuache maeneo oevu ambayo yanasaidia mpaka kule Selou? Ni wakati muafaka tuangalie mipaka tuliyoipanga katika nchi yetu, tutaendelea kuwa na migogoro mpaka lini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kupata vitu ambavyo ni standard kama tuna fikra ambazo ni sub- standard. Kuna watu wako under average wanataka wapate mshahara ambao ni above average, haiwezekani. Kwa hiyo, tunashindana na Mataifa mengine kama Botswana, tunashindana na Mataifa mengine kama South Africa, hatuangalii ni brain kiasi gani wame-invest katika tasnia hizo, ili wapate return kubwa. Huwezi ku-invest brain ndogo ukategemea upate return kubwa in terms of money, in terms of mipango, mambo mengi hayo yana-involve mipango mizuri, tumezungumza sana kuhusiana na masuala ya migogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mambo matatu ambayo nimeyazungumza Mheshimiwa Waziri ni suala la viumbe hai wanaosafirisha ambalo kwa kweli wamewa- cripple, jambo ambalo sio sawasawa, lakini bado suala la pili nimezungumza kuhusiana na sheria ambazo zinakinzana ziko nyingi na kanuni ambazo ziko kwenye uwezo wao. Afadhali sheria labda zitachukua muda, lakini kanuni nyingi ziko kwenye uwezo wao wanaweza wakazileta hapa tukazirekebisha kuondokana na migogoro ili tufanye business.

Kwa hiyo, nimwombe sana Mheshimiwa Waziri, Wizara hii ni Wizara ambayo inategemewa kuleta mapato mengi katika nchi yetu, tufike mahali waache legacy katika Wizara hii, imekuwa ni Wizara ya kufukuza watu wengi, ya kubadilisha watu wengi, hapo nyuma tumegombanagombana, lakini kwa namna moja au nyingine sasa hivi kuna mwanga unaonekana, kuna kazi inafanyika. Wanasema mara nyingi hatusifu, leo Mheshimiwa Dkt. Kigwangala nisifu kidogo kuna sehemu ya kazi inafanyika, mambo madogo madogo yarekebishwe. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, wakati Mheshimiwa Rais akifanya mabadiliko kwenye Baraza la Mawaziri akimtoa aliyekuwa Waziri wa Viwanda alisema moja ya kazi aliyowapa ni kufanya biashara na sio kupeperusha bendera tu. Mheshimiwa Rais ninaamini amewateua Mawaziri kwa ajili ya kumsaidia na kumpa ushauri, ili kuweza kuhakikisha Taifa letu lina-flourish, tunasonga mbele kiuchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, niliwahi kusema mahali hapa kwamba if you are lost, speed is useless (ukiwa unakimbia mwendokasi na umepotea, ule mwendokasi hauna maana). (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mpango ni miaka minne sasa hivi tunajadili kuhusu maendeleo ya nchi yetu na toka bajeti ya kwanza mfumo na mpango mzima mliokuja nao humu ndani Wabunge wengi kwa wingi wetu tulipinga namna ya uendeshaji uchumi na mipango mliyokuwa mmepanga. Na nimesema Rais anapowachagua anataka mka-add value na ndio maana alisema sikuwachagua kupeperusha bendera tu. Kwamba ninyi ni wachumi, mnazijua kanuni za uchumi, mnajua mki-violate kanuni a uchumi ita-backfire. Kodi jinsi mlivyokuwa mnakusanya tulitoa ushauri kwenye bandari hamkutusikiliza, tulitoa ushauri kwenye watalii hamkutusikiliza, tulitoa ushauri namna ya ukusanyaji kodi kwa bunduki, kwa task force hamkutusikiliza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa leo miaka minne mmebadilisha lugha sasa hivi mmekuwa laini as if sio ninyi. Mimi nilitaka Mheshimiwa Mpango kama mchumi, mmoja wa watu wanaoheshimika katika nchi hii, hebu tuambie ule ushauri ambao Bunge na Wabunge wengi humu ndani tulishauri kwamba hiyo njia unayokwenda sio sahihi kwa nini mlikuwa mnakataa? (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Msigwa ongea na Kiti. Ongea na Kiti.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, niliomba Waziri wa Fedha aseme kwa nini walikuwa wanakataa na walikuwa wanataka ku-achieve nini?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu, yote tuliyozungumza sasahivi wamegeuka kwa mlango wa nyuma wanatekeleza yaleyale baada ya kulitumbukiza Taifa kwenye matatizo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi mimi nailinganisha na timu inayocheza mpira kwenye uwanja ambao hauna magoli, mnapiga mashuti makubwa ambayo huwezi ku-major, you are going no where kwa sababu ya miradi mikubwa ambayo mmeweka... (Makofi)

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Msigwa kuna Taarifa. Mheshimiwa Julius Kalanga

T A A R I F A

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Naibu Spika, moja ya kazi kubwa ya Bunge ni kuishauri Serikali. Bunge hili limekuwa likiishauri Serikali mambo mengi ikiwepo kuondoa VAT kwenye umeme wa Zanzibar na maeneo mengine, kwa hiyo, Serikali imechukua ushauri wa Bunge ambao ni ajnibu wake kwa hiyo, Mbunge hana sababu ya kuhoji kwa nini Serikali inatekeleza yale ambayo Bunge limeshauri ni kazi ya Bunge. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Msigwa unaipokea taarifa hiyo?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru, kumbe ili Serikali isikie inachukua miaka minne, yaani mnakuwa mmemaliza muda wa miaka minne ndio mnasikiliwa. Nachukua uchauri wako kwamba, ni kuishauri, lakini tumewashauri four years, mambo ya miaka minne ndio wanasikiliza leo na mwakani ni uchaguzi na mkataba wenu na wananchi ni miaka mitano, yani mnashauriwa miaka minne ndio mnasikiliza, thank you. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema miradi mikubwa na ukilinganisha kiukweli Waziri wa biashara amekaa karibu siku mia mbili na kitu, ametumbuliwa kwa maana ya kwamba hajamsaidia Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukiniuliza mimi watu ambao kwa weledi wao na heshima kubwa ambayo Rais aliwapa, waliotakiwa kutumbuliwa ni pamoja na Mheshimiwa Mpango na Waziri Kabudi. Kwa sababu kwa nini nasema? Nitatoa sababu kwa nini nasema hivyo? (Makofi/Kicheko)

MHE. AMINA S. MOLLEL: Taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Msigwa kuna taarifa nyingine. Mheshimiwa Amina Mollel.

T A A R I F A

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda tu kumfahamisha Mheshimiwa Msigwa kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana imani kubwa na Dkt. Mpango na ndio maana mpaka sasa Waziri Mpango bado yupo akitekeleza majukumu yake kama Waziri wa Fedha.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Msigwa unapokea taarifa hiyo?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, wala sipotezi, ananipotezea muda tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema waliotakiwa kutumbuliwa ambao wameleta shida ya kutunigiza kwenye matatizo ni Mheshimiwa Mpango pamoja na Mheshimiwa Kabudi. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Kabudi alitoa ushauri kwenye masuala ya madini, leo kama Taifa we are stuck, yamebaki machimbo madogo madogo, machimbo makubwa ukienda Bulyankulu kume-stuck, we are not going anywhere tumekaa haturudi nyuma, hatuendi mbele, akatuambia kutakuwa na kishika uchumba, wala kishika uchumba hakionekani mpaka leo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati wa report ya Profesa Osoro kulikuwa na ngoma na ngonjera na praise and worship kila mtu alikuwa anashangilia. Leo tunataka mtuambie what is it going on? Mheshimiwa Kabudi where is our money? Mheshimiwa Kabudi alisema haya mambo, ametuletea hasara na amemshauri Rais vibaya. (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Taarifa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, mtu wa pili ambaye nasema ni Mheshimiwa Mpango…

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, hii itakuwa taarifa ya mwisho kwa Mheshimiwa Msigwa. Mheshimiwa Stanslaus Nyongo.

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpe taarifa tu Mheshimiwa Msemaji kwamba sekta ya madini anavyosema ime-stuck, naomba nimtaarifu tu kwamba, sekta ya madini haija-stuck, unless otherwise unazungumza kitu kingine.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, sekta ya madini kwa taarifa yako ni kwamba, sasahivi imekuwa ndio iliyoongeza mchango wa Taifa. Na tumechangia zaidi, tumekusanya maduhuli zaidi ya bilioni mia tatu na kumi na kitu ambayo imetokea kwa mara ya kwanza toka tumepata uhuru wa nchi yetu. Masuala ya kishika uchumba anayoyazungumza huyu Mheshimiwa ni kwamba, hiyo commitment kweli ipo na mazungumzo yanaendelea…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU WAZIRI WA MADINI: …tuendelee kusubiri pale taarifa rasmi itakapokuja.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni kwamba sekta ya madini inaendelea kukua na hata sasa hivi ni kwamba watu wanaona ni jinsi gani sekta ya madini ilivyoweza kuingiza kipato cha Taifa katika nchi yetu, asipotoshe aananchi. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Msigwa unaipokea taarifa hiyo?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru Serikali imekiri kwamba, kishika uchumba bado kinajadiliwa, ndio nilichokuwa nazungumza kwamba wameendelea kwamba, kishika uchumba mpaka leo. Ndio maana nimesema Mheshimiwa Kabudi anamshauri vibaya Rais na kwa bahati mbaya amekuwa sasa kwenye masuala ya kidiplomasia ameendelea kuwa arrogant, wala haisaidii nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mpango toka umekuwa Waziri wewe Makamishna wanazidi kuondoka na wewe ndio msimamizi, there must be something wrong. Aidha, una-violate principle za uchumi wewe mwenyewe huzifanyi na watu waungwana wana-step down kama principle zile walizosoma za uchumi hazifanyi kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunasifu na kuabudu hapa kwamba uchumi unakua, economics. Economies obout the walfare of people, the well being of people, kuhusiana na uchumi wa watu, hatuwezi tukawa tunaimba mnachozungumza takwimu mnasema uchumi unakua, takwimu zenu zinakwenda hivi wananchi wanakwenda kushoto, sasa hizo ni takwimu gani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yani tukubaliane kwamba, wale IMF ni waongo, uchumi unakuwa kwa asilimia saba kama mnavyosema ninyi maana mtatufunga tukisema zingine. Sasa maisha ya Watanzania yakoje? Ni kwa nini maduka yanafungwa? Kwa nini watu wanashindwa kusomesha watoto shule? Kwa nini kunywa chai maeneo mengine imekuwa luxury? Wananchi huko chini wanataka waone maisha ya kawaida, mnaweza mkatangaza kwamba uchumi unakua kwa asilimia 15, that is fine, lakini kule nyumbani hayo ndio maisha? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, ushauri mnaotoa, purchasing power ya mwananchi wa Tanzania iko chini kwa kiwango kikubwa sana. Mheshimiwa Mpango hasara aliyoileta Mheshimiwa Kakunda, wewe na Mheshimiwa Kabudi ni kubwa zaidi kwa sababu ninyi ndio mnamshauri Rais kwa karibu kuhusiana na uchumi wa nchi hii. Yale yote tuliyosema mliyakataa miaka minne iliyopita, halafu hapa tunabaki kusifu na kuabudu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie kidogo suala la korosho; suala la korosho kwa kawaida korosho msimu ukifika wale wanunuzi wa nje huwa wanaleta makontena wakinunua korosho zinaingizwa kwenye makontena zinasafirishwa kwenda nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, mara nyingi zimekuwa zikisafirishwa kwenda nje kwa sababu sisi hatuna uwezo wa kutunza korosho. Watu wa nje wakinunua hizo korosho kule kwao wana ma-godown ambayo yanaweza yaka-regulate temperature. Sasa ninyi washauri wa Mheshimiwa Rais mlimshauri Rais, mkapeleka Jeshi kwenda kukusanya korosho, mkaziweka kwenye ma-godown ambayo mengine yananyeshewa na mvua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nimesea mwanzoni kwamba, if you are lost, speed is useless na tumepotea mnaendelea ku-accelerate, tunaenda kwenye chaka ninyi mnaendelea kuongeza mafuta, uchumi unakua, uchumi unakua, huku mnapotea njia. Tusipokuwa waangalifu hizi korosho tutavuruga hata msimu unaokuja watu wa nje watashindwa kununua korosho zetu kwa sababu taarifa nilizonazo, watanisaidia watu wenye maeneo hayo, korosho asilimia kubwa zimeanza kuharibika na zinaoza maeneo mengine na zikioza hizi korosho maana yake wateja wa nje wanakuwa na wasiwasi kuja kununua korosho kwenye nchi yetu na zinashuka thamani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunakaribia kwenda msimu mwingine. Mimi nishauri jambo moja, aidha korosho zile ziuzwe kwa bei ya chini ili tuziondoe kwa sababu Trade World Organisation ina maswali mengi kuhusiana na korosho zetu. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru. Nami nianze kuzungumzia ambapo ameishia Mbunge mwenzangu wa Iringa kuhusiana na ugonjwa wa CORONA.

Mheshimiwa Spika, kiukweli mimi pamoja na mambo mengine mazuri ambayo Waziri Mkuu ameyasema lakini katika hotuba yake sijaridhika kabisa na jinsi ambavyo amelizungumzia suala la huu ugonjwa wa Corona, amelizungumza kwa kifupi sana. Jana wakati ulitupa nafasi ya kujadiliana hapa tulisema kwamba tuko vitani na tunapokuwa vitani lazima tujiandae kwa kiwango kikubwa sana. Tukiwa wa kweli kama Watanzania na kama Wabunge suala la kunawa mikono ambalo Serikali inajua imechukua hatua, suala la hygiene, masuala ya kunawa mikono wenzetu Ulaya, Marekani, ni kitu cha kawaida kabisa. Sipingani kabisa na hatua zilizochukuliwa na Serikali za kunawa mikono, lakini kama tunataka tudanganyane hapa tu kwa kunawa mikono na visabuni vile tumeweka kwenye maduka kwamba tunapambana na Corona wenzetu Ulaya suala la kunawa mikono sio swali. Ndiyo maana unawakuta wanakula bila kunawa wakati mwingine lakini suala la kunawa mikono haliko kwenye akili kwa sababu wakati wote wananawa mikono. Kwa hiyo, mimi nadhani…

SPIKA: Katika watu ambao hawanawi mikono Wazungu namba moja.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, hapana, sio kweli. Sio kweli, tabia ya kunawa mikono Wazungu ni ya kawaida kabisa, ni maisha yao.

MBUNGE FULANI: Hamna!

(Hapa baadhi ya Waheshimiwa Wabunge waliongea bila utaratibu)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, mimi naomba nipewe nafasi nizungumze. (Kicheko)

SPIKA: Waheshimiwa namlinda Mheshimiwa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, naomba unilinde, inategemeana, mimi nimekaa na Wazungu sana, nimeishinao.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Kwa hiyo, huwezi kunidanganya, suala la kunawa mikono sio suala la kufundishana.

SPIKA: Mchungaji, Wazungu hawanawi wala hawaogi. (Kicheko)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, wananawa.

SPIKA: Mzungu anaoga mara moja kwa wiki. (Kicheko)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, kwa hilo nitawapinga.

SPIKA: Namlinda, namlinda jamani, endelea.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nachoweza kusema kama tunadhani kukabiliana na CORONA ni kunawa mikono tu peke yake tutakuwa tunajidanganya, kuna hatua za zaidi kama nchi tunatakiwa tuzichukue. Huu ndiyo wajibu wetu sisi kama Wabunge kui- task Serikali kwamba ni mipango gani ya dharura ambayo Serikali imeifanya.

Mheshimiwa Spika, takwimu nilizonazo mimi Tanzania nzima pamoja na kuwa na watu milioni 58 tuna ICU 38 in case tukipata matatizo, haya ni masuala ya kujadiliana hapa tupewe ripoti. Kama nchi nzima tuna ICU 38 …

MBUNGE FULANI: Vitanda.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, vitanda 38, kama ugonjwa huo…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri Afya nimekuona.

T A A R I F A

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Spika, nalazimika kusimama kwa sababu mchangiaji ambaye anachangia sasa hivi anapotosha sana na nataka nimpatie taarifa za kitaalam tu kabisa. Corona Virus ambaye ni COVID19 ukuta wake umetengenezwa na mafuta na sababu ni silaha ya kutosha ya kuki-destroy kirusi hiki. Hatutoi hizi taarifa kwa ajili tu ya kuudanganya umma, sabuni na maji tiririka ni silaha ya kutosha kabisa kukiuwa kirusi cha Corona. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini la pili, muongeaji ambaye ametoka kuongea sasa hivi anasema Tanzania tuna vitanda 38 vya ICU. Hospitali ya Muhimbili peke yake ina vitanda zaidi ya 40, hizo taarifa anazitoa wapi? (Makofi)

SPIKA: Ni taarifa tu hiyo Mchungaji kukuweka sawa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nadhani tunajaribu kukimbia hoja ya msingi tunayoijenga hapa. Nimesema sipingani na masuala ya kunawa na sabuni zilizowekwa barabarani na kwenye maeneo mengi. Nimesema kama tunadhani tutaondoa Corona kwa sabuni tunazonawa tunajidanganya. Hoja ya Corona ni zaidi ya tunavyodhani na ndiyo maana nchi za wenzetu zimeamua kuwatoa watu wake Barani Afrika. Jana nilikuwa nasikiliza Al- Jazeera wanasema ndani ya wiki tatu ugonjwa huu tutaanza kuyaona matokeo yake katika Bara la Afrika kwa sababu measures tunazochukua haziendani na tatizo tulilonalo, hili ni tatizo kubwa. Bunge saa hizi hapa tunajadili bajeti as if hakuna chochote kitakachotokea.

Mheshimiwa Spika, Spain na Italy walipuuza kwa sababu waliona hilo suala halitawafikia, lakini mtu yeyote mwenye busara anajiandaa kabla ya vita. Tunachozungumza hapa ni kutaka kufahamu ni kwa kiwango gani tumejipanga. Wakilipuka wagonjwa laki moja hapa tutawalaza wapi? Hayo mambo tunatakiwa Serikali ituambie. Haya masuala ya kusema kuna vitanda 40, nyumba za ICU ziko 38, huwezi kukataa hiyo hatuna ICU za kutosha hapa. Mimi ndiyo nasema Serikali ituambie incase wakizuka wagonjwa laki moja tutawaweka wapi kama nchi? Serikali muwe na majibu hapa, hamna majibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini la pili, consenquences za ugonjwa huu zina athari za kiuchumi. Wewe ni shahidi, sekta ya utalii kuna direct employment zaidi ya milioni moja na laki tatu au laki nne ambao sasa hivi hawana kazi na wengine wanaathirika, sekta ya utalii karibu watu milioni mbili hawako kazini kwa sababu hamna kazi. Hoteli zimefungwa, Zanzibar kule zaidi ya hoteli za kitalii 250 zimefungwa, Bara zaidi ya hoteli 250 zimefungwa, these are the issues tunatakiwa tu- discuss hapa, revenues mtakusanya kutoka wapi? Utalii unaingiza 25% ya forex, hiyo forex inatoka wapi? 25% ya forex katika nchi siyo kitu kidogo, haya ndiyo mambo tunatakiwa tuyajadili hapa, sio stories. Serikali ituambie ina mpango gani tuweze kuishauri. Hili ndiyo Bunge tushauriane hapa.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MBUNGE FULANI: Anza wewe kutoa ushauri.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, kuna watu katika industry hiyo wamekopa…

T A A R I F A

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika,
taarifa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Serikali haijatuambia ime-negotiate vipi na mabenki…

SPIKA: Mheshimiwa Mchungaji, namwona Mheshimiwa Waziri wa Nchi amesimama.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika,
naomba tu kumpa taarifa Mheshimiwa Msigwa kwamba, kwanza anapoona hali hii ya mwenendo wa Corona tunavyokwenda nayo inaonesha dhahiri shahiri ni kwa namna gani Serikali imejitahidi na iko kazini. Naomba tu nimwambie Mheshimiwa Msigwa ili tuweze kuwa pamoja, huu ndiyo muda muafaka nadhani badala ya kuendelea kulaumu ilikuwa ni fursa kwake…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika,
ilikuwa ni fursa kwake na yeye kutushauri kwa sababu tumeshapokea maagizo yako kwamba hata sisi tutakuja kama Serikali na umetuambia tutoe taarifa mbili; taarifa ya mwenendo mzima wa tatizo la Corona na tatizo la mafuriko nchini. Sasa anaposimama ajue sio kwamba Serikali imekaa tu ila tungefurahi sana Mbunge atushauri kuliko kulaumu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba tu nimpe taarifa kwamba tunajiandaa, hili ni tatizo la dunia. Hata huko anakosema Ulaya hata ICU za Ulaya hazitoshi na wao wana shida hiyohiyo. Kwa hiyo, kila mtu anapambana na Corona kwa mazingira aliyonayo na kwa namna anavyoweza kukabiliana nayo. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Msigwa unapokea taarifa hiyo?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, mimi hapa silaumu. Serikali yoyote duniani ipo kwa ajili ya kulinda uhai wa raia wake, that is a paramount, hicho ni kitu cha kwanza. Wao hapa waje na mpango kwamba jamani wakilipuka wagonjwa elfu hamsini tumepanga hivi, Wabunge mnatushauri nini? Waje na plan, tuko vitani hapa. Waje na plan Wabunge tuwashauri, wamekaa kimya muda unaenda, tunavyoviona tu ni visabuni huko barabarani, ndiyo hicho nachozungumza.

Mheshimiwa Spika, tunazungumzia uchumi hapa, kuna wafanyabiashara wamekopa benki, Serikali haijatuambia…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Muswada wa Sheria ya Upatikanaji wa Habari wa Mwaka 2016
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi nami nichangie kwa kifupi. Niseme tu tuliku-miss wewe Mheshimiwa Chenge, karibu tena tunafurahi kukuona. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti…
MWENYEKITI: Hebu acha matani yako, ulini-miss mimi? (Kicheko)
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu ni ya kidemokrasia na naomba ninukuu maneno machache, Novemba 1883, aliyekuwa Rais wa Marekani wakati huo, Abraham Lincoln aliwahi kutoa hotuba moja maarufu sana inayoitwa The Gettysburg Address ambayo alisema Serikali ya watu, inayotokana na watu, kwa ajili ya watu. Sisi kama Tanzania tumeamua kwenda kwenye mfumo wa vyama vingi, mfumo wa kidemokrasia. Nikirudi kidogo kwenye historia, dunia imepitia hatua mbalimbali, mifumo ya kidikteta, mifumo ya kichifu mpaka tumefika kwenye mfumo wa kidemokrasia ambapo Serikali ya watu, kwa ajili ya watu, haiwi mali ya mtu mmoja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nayasema haya kwamba kama Taifa tunajitungia utaratibu ambao kila mtu ataufuata kwa mujibu wa Katiba yetu ambayo tumeiweka wenyewe. Napata ukakasi sana kwa kaka yangu, Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe anapouleta huu Muswada, niwe mkweli kabisa naona una agenda ya siri. Ni Muswada ambao tunatengeneza sheria ambapo tunaangalia kipindi chetu cha utawala na wengi wetu hata lifespan ya maisha inakwenda ukingoni, ndiyo tunateremka hatuliangalii kama Taifa kwa siku zinazokuja baadaye. Napata ukakasi kwamba hivi hizi sheria tunazozitunga na tunazileta, mmeshaleta bills nyingi, zipo kwa ajili ya kufurahisha kwamba tuna Bunge la kutunga sheria na tunaweka bills nyingi, kwa sababu sheria tulizozitunga zilizopita hazifuatwi, hazizingatiwi, hazifuatiliwi, kwa nini tunaleta sheria tena? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mihimili yetu mitatu hii, sasa hivi Bunge ndiyo mhimili ambao hauna heshima katika nchi hii. Ni kwa sababu Wabunge tumekosa heshima, tunaamua mambo ya hovyohovyo, mambo ya kipuuzi ambayo hatutafakari. Nimekuta Wabunge wengine wanalalamika jinsi ambavyo hata polisi wanatudharau kwa sababu Wabunge tumeshindwa kusimama kwenye nafasi zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema haya? Mimi binafsi nasikitika kwamba huu Muswada unakuja, tunaye Mwanasheria wa Serikali na Waziri, tunaamini hawa ni wasaidizi hata wa Mheshimiwa Rais, hawa ndiyo wanatakiwa wamwoneshe Mheshimiwa Rais awe anang‟ara Tanzania na nje ya Tanzania. Hata hivyo, kuna mambo ambayo nasema nasikitika Miswada kama hii inakuja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe kwamba napata ukakasi na Muswada huu, wakati ule tulikuwa hatuko humu Bungeni, Mheshimiwa Nkamia alisimama hapa ana-challenge hukumu ambayo mhimili mwingine umetoa kule Arusha na Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe, huyu ni mtaalam, msomi, anadiriki kusema ule mwenendo wa kesi atam-task DCI aulete wakati taratibu hazisemi kama mtu hajaridhika kwenye mahakama anakata rufaa kwenye mhimili mwingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napata ukakasi ni nini agenda ya Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe kwenye Muswada huu ambapo haya aliyoyaeleza humu ndani kwa mfano hizo haki za kupata habari za hao Madiwani, Wenyeviti wa Mitaa, hizo excess zipo, wote si tupo kwenye council kule, nani anamzuia mtu kupata habari hizo kwenye Councils zetu kule, wote wanakuja wanapata hizo habari. Napata tatizo, naanza kujiuliza, hivi nchi yetu inafika mahali, kwa wale walioiona ile movie ya Gods must be Crazy, yule bushman, ametoka porini haelewi kwamba watu huwa wanafuga mbuzi anachukua kamshale kake anapiga mpaka wanampeleka mahakamani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli nchi hii sheria hazifuatwi kiasi hicho, Mwanasheria wa Serikali amekaa kimya, Waziri amekaa kimya, anadiriki kutokutafsiri, sasa mimi nauliza hizi habari mnazoleta zitakuwa practiced wapi? Ndiyo hoja ambayo naiuliza, hii miswada uliyoileta itakuwa practiced wakati Katiba inakanyagwa kabisa. Tulitegemea Waziri asimame aseme this is not right, kama hii haikubaliki mimi na-step down, AG anafanya nini ofisini kwa sababu vitu vya hadharani vinakiukwa! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nasema Bunge hili linadharauliwa. Leo katika nchi hii mtu anaona kwamba hata kumpa mtu mafao ya kisheria ni kama favour, AG hasemi, Waziri husemi, halafu leo unatuletea Muswada mwingine tutunge ukatekelezwe wapi sasa? Kwa watu civilized na dunia iliyopevuka kama mambo hayafuatwi kwa mujibu wa sheria wana-step down, sasa hivi mngekuwa mmeficha nyuso zenu. Ndiyo maana nasema napata ukakasi, mnatuletea huu Muswada utakwenda kutekelezwa wapi wakati Katiba inakanyagwa lakini hamsemi na ninyi ndiyo mnatakiwa mseme Mheshimiwa Kwamba this is not right, tumekaa kimya, sasa Bungeni tunafanya nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa hatusemi, tutapataje hiyo heshima huko nje kwamba sisi ni watunga sheria na hizo sheria tunataka zisimamiwe? Hao polisi wana haki kabisa ya kutuburuza na kututania kwa sababu hatuna hiyo hadhi, tulitakiwa tuulinde mhimili huu. Leo mnaleta huu Muswada na kuwazuia whistleblowers. Kwa mfano, Bunge lililopita tulizungumza kuhusu wale wanyama waliotoroshwa. Hivi kwa Muswada huu mnaouleta hapa yule mwandishi aliyeandika atakuwa na uwezo wa kuandika hizi habari.
KUHUSU UTARATIBU.....
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, dakika zangu nane naomba utanitunzia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na wewe kumuunga mkono Mheshimiwa Mhagama lakini when you talk about Sweden ni watu wako civilized, demokrasia iko wazi siyo kama hapa. Ukimwona Waziri wa Sheria wa Sweden anaji-behave anafuata taratibu, ukimwona AG wa Sweden anaheshimu nchi anafuata Katiba, kwa hiyo, tukilinganisha Sweden na hapa tunakuwa tunajidanganya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tunajilinganisha na Rwanda, ndiyo tunachojilinganisha hapa. Hizo reference zote wanazozichukua hizo ni kujificha, it’s just political gimmicks, reference wanazozitoa siyo kwa nchi hii hakuna civilization. Nimesema kwa nchi nyingine yanayotokea na sintofahamu katika nchi hii, Waziri wa Sheria na AG walitakiwa wawe wame-step down kwa sababu ni aibu kwa dunia!
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaikanyaga Katiba halafu watu tunachekacheka hapa, ndiyo maana nasema napata ukakasi kwamba tunaleta sheria wakati Katiba inakanyagwa na hii sheria inatokana na Katiba. Leo anasimama mtu mmoja anasema watu wote wanyamaze halafu tunapiga makofi halafu unasema I am a Member of Parliament, kwa nini polisi wasikudharau? Haya ndiyo ninayoyazungumza, watu hawataki kuzungumza hapa, wote tuko kwenye mess na ndiyo tunatakiwa tujadili hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napata ukakasi kwamba Waziri na AG wanaleta huu Muswada wanao uwezo wa kusimamia hii sheria, ambao nasema kuna kitu kimefichwa nyuma yake. Kwa hiyo, ukiniambia tufuate kifungu cha ngapi, hiyohiyo sheria inanipa uhuru, mimi sijasoma sheria lakini being a theologian najua mme-copy mambo mengi kutoka kwenye mosaic law, namna ya kutafsiri, walau naijua context, principle ambayo interpret scripture na ninyi mnafuata, Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe huwezi kuikata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sheria za nchi hii kama tunafuata tafsiri, Waziri anasimama kutetea kitu ambacho kiko wazi atawezaje kutetea hii? Anatetea kitu cha uwazi kabisa hata mtu asiyesoma sheria anaona kuna makosa. Ndiyo hoja yangu kwamba what is it behind, Wenyeviti wa Mitaa ndiyo wanaitaka hii? Hii ndiyo kazi ya sisi Wabunge tutoe vitu vya maana. Vilevile mimi kutoa mchango wangu sidhani kama natakiwa nipangiwe na wewe na wewe toa mchango wako. Kwa nini usubiri mimi niseme uanze kunisema mimi? Toa mchango wako hapa tukusikilize. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo. Kwa hiyo, suala langu ninalolizungumza, inakuwa haina maana kuendelea kutuletea bills hapa ambazo hazitekelezwi. Ina maana mawili na mimi nawa-challenge hawa wakubwa wawili, AG pamoja na Waziri, aidha kwenye ofisi hiyo viatu ni vikubwa mno wanatupotezea muda hapa, maana yake hawawezi kufuatilia hizi sheria au hawatoi ushauri au wanaogopa, lakini vyote hivyo viwili wangesema watoke hadharani kwa sababu lazima tulinde Katiba ya nchi, ndiyo hivi vitu vingine vifuatwe. Sasa Katiba ya nchi haifuatwi halafu watu wote mnakaa kimya mnachekelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue hekima zake Shibuda, aliwahi kusema siku moja maabara ikisema Mheshimiwa Mfalme anaharisha usibomoe maabara unatafuta dawa. Hii yote ni kuviziba vyombo vya habari, vyombo vya habari vinasaidia kusema mfalme anaharisha, mfalme anatakiwa atafutiwe dawa ili apone. Sasa mnaziba, hamtaki watu waseme, mnataka tuje hapa tupongezane tu. Humo sisi hatumo na tunaongea kwa nia nzuri Tanzania ipone, wote tufuate Katiba hii si ndiyo imetuleta humu ndani. Wote tufuate Katiba hii hakuna mtu ambaye yuko juu ya Katiba sasa tunaogopana, watu wanajificha, wanakuwa kwenye uvungu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka kwenye Biblia wakati wa Gideoni walikuwa wanakwenda kwenye mapango kule wanajificha, everybody is hiding, wengine wanajibembeleza kutaka vyeo, tufanye kazi zetu. Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe nashindwa sana kujadili kipengele baada ya kipengele kwa sababu naona dhana iliyoko nyuma siyo nzuri kwa ajili ya Taifa letu. Niwaombe Wabunge tuache ushabiki, tuchukue nafasi yetu kama Wabunge tulisaidie Taifa. Mwisho wa siku tunamaliza vipindi wengine hawakuwepo wapo barabarani, wengine hizi sheria zinawatafuna saa hizi wamekwenda huko mbali, tuweke sheria ambazo kila mtu ata-comply na kila mtu ataishi kwa raha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba wengine hawayapendi haya, lakini lazima tuyaseme. Anafika mtu mmoja, hivi kwa sheria za nchi kweli Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe, Sheria Na.5 ya 1992 ya Vyama vya Siasa ndivyo inavyotafsiriwa vile, seriously?
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya. Nilikuwa nasema, namshangaa AG anasimama anatetea, hivi sheria za Tanzania ndiyo zinavyotafsiriwa vile? Hizo ndiyo principles za kutafsiri sheria? Kweli kabisa wanasheria wakubwa tumesomesha anasimama anasema, eeh, hiyo ndiyo hivyohivyo.
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi wa Mwaka 2018
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru na mimi kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kwa utangulizi kabisa kama Wabunge na kama Taifa tunapaswa tukumbuke usemi huu; “the past is where we have learned the lesson and the future is where we apply the lesson.” Kwenye masuala haya mengi ya mikataba kuna mambo mengi ambayo tumejifunza huko nyuma, ni wajibu wetu baada ya Serikali kuleta muswada huu wote kwa pamoja tungeangalia ni namna gani huko nyuma tumepata masomo ambayo sasa tunapokwenda kuandika miswada mingine inayoletwa kama hii tu-apply yale masomo tuliyojifunza.

Kabla sijaendelea ninaunga mkono kwa dhati kabisa hotuba ya Kambi ya Upinzani na mambo mengi ambayo Mheshimiwa Halima ameyazungumza kwenye hotuba na ninaamini Mheshimiwa Mpango atakwenda kuyafanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo kubwa ambalo napenda kujiuliza ni kwamba tunapoleta sheria hapa ndani ya Bunge huwa kunakuwa na jambo ambalo tunataka kulitatua, tunataka ku-solve nini? Tumekuwa na matatizo gani? Sheria iliyokuwepo ilikuwa na shida gani? Ni kwa nini tunaleta amendments? Ni lazima tuwe na majibu hayo kwamba tunataka tutatue nini. Hakuna anayepinga hapa kwamba tunahitaji PPP, lakini naiomba Serikali haijatoa clear definition ni uchumi wa aina gani tunaotaka kuuendesha katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, toka Awamu ya Kwanza Mwalimu Nyerere ali-define ni aina gani ya uchumi, lakini baada ya Mwalimu Nyerere kushindana na Ndugu Edwin Mtei akaamua kung’atuka, mfumo wa uchumi ukabadilika. Tungependa Awamu ya Tano ituambie ni aina gani ya mfumo wa uchumi inayotaka kutupeleka kama Taifa. Kwa sasa hivi tukiwa wakweli tukianza kuangalia ni kama chombo, ni kama space ship ambayo ipo angani haijui inataka kutua wapi, kwa sababu mnatuambia uchumi wa viwanda, mnatuambia PPP lakini mambo mnayoyafanya na mnayotuletea hapa hayaendani na PPP.

Mheshimiwa Mpango investors wote wanapotaka ku- invest, wanapokuja katika nchi yoyote huwa wanazingatia vitu vitatu vya msingi na ninaomba utanichambua hapa au utanipinga kama nasema uongo, najua wewe unayajua haya mambo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu cha kwanza wanachoangalia ni contract sanctity. Sanctity yaani utakatifu, utukufu wa huo mkataba mnaokubali. Wanataka waone ni namna gani hii nchi inaheshimu mikataba tunayokubaliana ili wawe na uhakika wanapokuja kwenye nchi. Neno sanctity linatokana na Latin word, kitu holy (kitakatifu). Kama Taifa lazima tujiulize huwa tunaona mikataba tunayoingia na watu wengine au tunaamua kuivunja kwa vile tunavyotaka? Sasa tunapotengeneza hizi Katiba lazima tujiulize ni kweli huwa tunaona hiyo mikataba ambayo tunafanya au tunafanya kisiasa? Hakuna investor yoyote ambae atakuja mahali ambapo hatuheshimu mikataba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka wakati wa makinikia ambayo sasa hivi mmeingia, mmejificha uvunguni Mheshimiwa Lissu alizungumza hapa, alisema report ya Osoro ni rubbish. Watu walimrushia maneno mengi hapa, mkatangaza kwenye vyombo vya redio, kukawa na kelele nyingi na ngoma nyingi, mkasema tutapata karibu trilioni 425 ziko wapi mpaka leo? Mkavunja mikataba bila utaratibu, bila kuheshimu mikataba tuliyoifanya ambao ni sisi wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Halima Mdee amezungumza asubuhi hapa, amesema tatizo letu hatuwezi
kuwalaumu hawa wanaokuja humu ndani, ni namna tunavyoandika mikataba wenyewe, halafu tukiandika mikataba tunaanza kuwalaumu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo investors wanaheshimu ni regulatory framework (clarity), mfumo mahsusi wa kudhibiti makubaliano ambao bado katika nchi yetu hatufuati hayo mambo, kila mtu anaamua. Mwingine amezungumza hapa asubuhi, anavyo-behave Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ni tofauti kabisa anavyo-behave Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Ni investor gani atakayekuja katika nchi kila mtu anatoa matamko yake? Mkuu wa Wilaya anataka achukue kodi, anataka adai kodi, sasa ni investor gani atakayekuja atasikiliza mambo kama hayo? Tuna ukosefu mkubwa wa clarity, ni namna gani hii mifumo tunaisimamia kama Taifa.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu ni international arbitration, ambayo nimeshangaa sana kwenye muswada wako Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Dkt. Mpango unasema kwamba, unatoa wazo kwamba eti kama ikitokea kutokuelewana basi mahakama zetu ndiyo ziamue. Nikuulize swali Tanzania ni member wa MIGA, inawezekanaje member wa MIGA tuwaambie hao investors wanaokuja katika nchi yetu waje wafanyie kesi zao kwenye mahakama zetu? Nitaomba uje unijibu hili swali rahisi kabisa, inawezekanaje member wa MIGA au tumejitoa kwenye MIGA? Wanawezaje kuja sasa, unawaambia investors ambao wanaleta pesa zao kwa risk kubwa halafu unasema tufanye kwenye mahakama zetu! Kwa bahati na Mahakama zetu hizi ambazo mtu anakaa ofisini anapiga simu kwamba funga akina Msigwa miaka mitano, nani atakubali kuleta mitaji yake? Mahakimu na Majaji wanapigiwa simu funga huyo miaka mitano uhakikishe anafungwa Sugu ndani, nani atakuja kwenye mahakama za namna hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshuhudia kwenye Mahakama hizo anaambiwa Jaji Mkuu kwamba hizi kesi zikiisha nitawapa bilioni kadhaa, nani ata-trust mahakama za namna hiyo halafu ulete investment hapa? Ukiangalia spirit
ya Wabunge wengi humu wananong’ona wengine hawataki kusema, actually wanaishangaa hata Kamati kuuleta huu Muswada humu ndani, kwa sababu huu Muswada unaua PPP na mtuambie kabisa kwamba hamna mpango wa PPP. Serikali ya Awamu ya Tano ilitengeneza mazingira mazuri. Mfano mzuri, baada ya ile Sheria ya Rasilimali zetu mambo ya gesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya ile Sheria ya Rasilimali ambayo tuliileta hapa tulianza kubadilisha sheria za mchezo katikati ya game. Makampuni makubwa, kwa mfano, Exxon Mobil iliondoka. Wote mnajua kwamba mojawapo ya watu wa ile Kampuni ni Rex Tillerson huyu aliyekuwa State Secretary wa Marekani maana yake mnadhani amepeleka meseji gani kule Marekani kwa ajili ya investors? Utasema hao ni Wamarekani, makampuni ya Norway yameondoka, makampuni ya Brazil yameondoka, sasa hao investors mnaosema waje wanatoka wapi? Tunapeleka picha gani huko ulimwenguni tunaposema tunaleta hao investors, wako wapi? Tunaongea lugha nyingine na tunatekeleza kitu kingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni mambo ambayo kama Bunge tunatakiwa tujadiliane. Mambo mengi hapa tumeyazungumza wakati mwingine tunatolewa kwa kushikwa na maaskari, vigelegele vinapigwa, mwisho wa siku muda ukifika tunaanza kutoana macho, tunaanza kuoneana aibu hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni wajibu wetu kama Bunge, mimi ningesema, ningekuwa ni Mjumbe wa Kamati ningelazimisha hii sheria irudi kwa sababu kimsingi sheria iliyokuwepo nyuma ni bora zaidi kuliko hii. Kwa hiyo, kwa kifupi, Serikali ya Awamu ya Tano inaturudisha kwenye enzi za ujamaa na kujitegemea, enzi za Awamu ya Kwanza
ambayo mfumo wa ujengaji wa uchumi ulishindwa, sasa mnataka turudi tena kule kwa kisingizo cha Ujamaa kwamba tunapenda watu wakati hatuwezi kuwaajiri tunapoua sekta binafsi, hatuwezi kujenga viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiwa Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani nimezungumza sana kuhusu Economic Diplomacy lakini huoni hizi sheria zinaonesha Economic Diplomacy, hauzioni Economic Diplomacy katika masuala haya. Sasa mnawezaje kutunga sheria ambazo actually zinawafukuza investors? Ningeomba kama Bunge tuwatendee haki wananchi, kwa sababu mwisho wa siku mtumbwi huu ukitoboka sote tutashuka chini, tutatumbukia wote kwenye maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, amendments zako ulizozileta siungi mkono hoja kwa sababu zinaua PPP, hazitatusaidia na Serikali hamtaweza kufanya biashara. Tumetoka huko hata maandazi Serikali ilikuwa inauza, ilishindikana! Tulikuwa tunapanga foleni kwenye maduka ya RTC, foleni imeshindikana. Niambieni jambo moja ambalo mmelilete hapa Awamu ya Tano, mmesema mnajali wanyonge, yote yamegota ukuta, lakini mkija hapa wengine mpaka sasa hivi wame-back off hawataki kuzungumza lakini huu ndiyo ukweli kwa sababu tunaua sekta binafsi kushirikiana na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, amezungumza dada yangu hapa kwenye eneo la unsolicited, nalichukulia kama mchonga kinyago, whatever you got the message. Mimi nalichukulia kama mchonga kinyago. Mchonga kinyago akiliona gogo, wewe unaliona gogo yeye anaona sura ya kinyago, sasa amekuja hapa yeye ameona kinyago, ameona potential wewe hujaona, anakuja na hela zake, anataka kufanya investment wewe bado unambana, unamsumbua halafu aziweke pesa Benki Kuu, kwa misingi gani, nani ateleta hela zake aweke hapa, mtampata wapi mtu wa namna hiyo? Halafu ni nchi gani inayo practice haya mambo mnayoyafanya. Mtupe mfano mmoja ni nchi gani ina-practice hayo mabo mnayoyafanya ambayo mnaamua kujifanyia mnavyotaka as if investment inatakiwa iwekwe tu Tanzania. Hawa ma-investors tunawagombania, tunawakata waje lakini mnafanya mambo kwa mashinikizo.
Hali ya Uchumi wa Taifa Kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru. Nianze na ugatuzi mikoani, jinsi sasa hivi Serikali inavyo-treat masuala ya Serikali za Mitaa ni kama vile Serikali za Mitaa hazitakiwi. Ningemwomba Mheshimiwa Waziri Serikali hii inachotaka kukifanya ni kile ambacho Mwalimu Nyerere aliwahi kukifanya, kikashindikana na akaanza tena ku-empower Local Government. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mawaziri wa TAMISEMI wote hapa kila jambo likifanyika wanaelekeza kwamba kwenye Local Government nyie Wabunge ni Madiwani, mkakusanye hela, mhakikishe mambo yanafanyika lakini wakati huo huo mnanyang’anya vyanzo vyote vya mapato kwenye Local Government, kwa hiyo, mnasema jambo lingine na huku mnatenda jambo lingine.

Mheshimiwa Spika, kwa kifupi ni kwamba bajeti ya Mheshimiwa Waziri muundo wa ukusanyaji kodi una-cripple utendaji wa Local Government. Mlitoa Property Tax, marejesho yanayorudi kwenye Local Government yamekuwa ni kidogo sana ukilinganisha na jinsi tulivyokuwa tunakusanya. Kwa mfano, Iringa Mjini tulikuwa tunakaribia kupata karibu shilingi bilioni moja sasa hivi mmetuletea kama shilingi milioni 200 na bado main power watu wa TRA wanahitaji kutoka huko kwenye Local Government kitu ambacho hakina sababu mngetuachia tukusanye wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini jambo lingine kubwa ambalo tunalijadili wote na ambalo nami nataka niliseme kuhusiana na suala ambalo kama Taifa tunataka tupasuke lakini wakati huo huo hatutaki kwenda kwenye kina kuhusiana na suala hili la madini. Hili suala la madini mimi bado narudia approach, hawa wawekezaji waliokuja hapa nchini is unfair to call them ni wezi, mimi sikubaliani kuwaita kuwa wao ni wezi.

Mheshimiwa Spika, nasema hivyo kwa sababu mwaka 1997 na 1998 kuna sheria zililetwa humu ndani Bungeni na zikapitishwa. Chama cha Mapinduzi mlikuwa na sera yenu na mkanadi kwenye Ilani, Rais anapochaguliwa nyuma anasukumwa na policy ya chama, mtuambie sasa hivi policy ya madini ya chama chenu ni ipi. Policy ya madini ya chama chenu mkaleta, zikapitishwa humu ndani na haya mambo yote ambayo hawa wawekezaji waliingia nchini yalipitishwa kwa mujibu wa utaratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Wabunge tusishabikie hivi vitu bila sababu kwa sababu mambo haya kabla mikataba haijafanyika, kuna timu za wataalam zinakaa, zinajadiliana baadaye Makatibu wa Wizara wanakaa, wanapitisha baadaye Mawaziri mnakaa ndipo Rais anasaini. Vinginevyo mtuambie hata Mheshimiwa Magufuli hizi nyumba za Serikali aliuza peke myake na kama aliuzam peke myake mna yeye tumchunguze aliuzaje nyumba za Serikali.

SPIKA.... Kidogo tu Mchungaji....

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nimekusikia, naomba ninukuu kidogo, nikumbushe zile sheria ambazo Bunge hili lilizipitisha na policy ya Chama cha Mapinduzi ilisimamia sheria hizi. Sheria ambazo zilitungwa na Bunge hili, namba moja, Sheria ya mwaka 1997 iliwapa wawekezaji wa kigeni ulinzi mkubwa wa manufaa mengi kama vile kuondosha nje fedha na faida yote wanayoipata kwa uwekezaji wao nchini na mikataba ilikuwa siri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kitu cha pili, Serikali hii hii ilikuwa inaongoza, Sheria ya Uwekezaji ya Tanzania ya mwaka 1997 iliwapa wawekezaji wa kigeni ulinzi mkubwa na manufaa mengi kama vile kuondosha fedha nje na faida yote wanayoipata kwa uwekezaji wao nchini, wanaondosha vyote sheria inasema hivyo, sasa tunawaitaje wezi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kingine, mwaka 1997 Bunge lilipitisha Sheria ya Madini ambayo ilitamka kwamba mwenye miliki ya madini na fedha yote itokanayo na mauzo ya madini ni mwenye leseni ya kuchimba madini hayo…

T A A R I F A......

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, mjadala ungekuwa mzuri kama tungepeana uhuru wa kuzungumza kwa sababu wenzetu wanazungumza mpaka wanaongezewa na dakika, you got to see our views, smooth water never develop a skillful sailor. You guys you are looking for smooth water, ukitaka upate baharia mzuri akumbane na maji magumu, hebu mpate maji magumu ili muonekane umahiri wenu basi, mbona mnaogopa tukisema? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninachokisema, hizo sheria zilikuja kwa Hati ya dharura hapa, tunachogaombana hapa, Serikali inafanya kazi kwa kuwajibika wote, lakini Mheshimiwa Rais mnalosema tumshangilie na tumuunge mkono, hakuna mtu anayekataa kuzuia wizi unaoonekana lakini Mheshimiwa Rais alikuwa miongoni mwa Baraza la Mawaziri. Wakati Zitto anazungumza na Karamagi hapa alikuwa ni miongoni mwa waliosema Zitto asulubiwe wakamtoa Zitto nje kuzungumza hii mikataba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa leo haya masuala ya madini…

T A A R I F A

Mheshimiwa Spika, lakini nimeipokea. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, alichokuwa anasema wajina wangu Peter Serukamba nakubaliana kabisa, lakini mimi siyo mtu ambaye napenda ku-embrace mediocrity. Kwa nini nasema hivyo? Let us be honesty, hakuna mtu anayekataa tusiibiwe lakini kama Chama cha Mapinduzi, Mheshimiwa Spika unasema kwamba siwezi kutoa ushahidi, Chama cha Mapinduzi ndiyo mmekuwa majority humu ndani, kwa hiyo, sheria yoyote hapa ndani haiwezi kupita bila ninyi kuipitisha. Kwa hiyo, sheria zote ziwe nzuri, ziwe mbovu zilipitishwa na Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Spika, sasa tunachotaka kukisema kama Rais ni muungwana, anajua hawa hawa akina Tundu Lissu ambao leo mnawatukana walipambana na haya mambo toka zamani, asimame kwenye television aseme kwamba mimi nimegundua wezi hawana Chama, wanaweza kuwa CCM wanaweza kuwa CHADEMA na mimi nimegundua ndani ya Chama cha Mapinduzi kuna majizi. Kwa sababu ndani ya Chama cha Mapinduzi kuna majizi naomba tushikane wote mikono tung’oe wezi CHADEMA na tung’oe wezi CCM. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nawashangaa sana wenzangu wa Chama cha Mapinduzi, kimsingi Rais anachokifanya Sera ya Chama cha Mapinduzi ameweka pembeni anaongoza kama vile ni Mgombea Binafsi. Hiyo mimi namuunga mkono kwa sababu sera yenu kuhusu madini ni hiki kilichofanyika, sasa leo mnageukaje? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana tunasisitiza kama kweli Mheshimiwa Magufuli ana dhamira ya kweli ya kuleta mabadiliko katika nchi hii hapa, alete mabadiliko kwenye Katiba ili Marais waweze kuhojiwa. Hiyo ndiyo dawa pekee kwa sababu vinginevyo hata yeye ameuza nyumba za Serikali kitu ambacho siyo kweli asingeuza bila Mkapa kusaini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumeshangilia Muhongo kuondoka wakati sheria hizi mbovu maskini hata Muhongo hakuwepo wala hii sera hakuwepo, leo tunashangilia Muhongo kaondoka hakuwepo, he was not here.

KUHUSU UTARATIBU.....

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Vilevile tunatakiwa tuwe skillful tunapo-deal na hawa tunaowaita wezi. These are not intruders, we invited them in this country. Sasa kwa sababu tuliwa-invite siyo kwa sababu tu tuko vitani hatuendi blindly lazima tuwe skillful. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunachokizungumza hapa hata haya mambo unayosema yalikuwa ya World Bank hata madini ni World Bank hivyo hivyo, tuko-pushed hivyo hivyo lakini sisi hatukulazimishwa kula, hawatukushikia, tulisaini hapa wengine wakaenda usiku, mkapiga mayowe hapa, mkaunga mkono. Bunge lililopita kwa Mheshimiwa Spika Makinda nakumbuka mara ya mwisho hapa zililetwa sheria tatu za dharura, Mnyika alikuwa anaomba…

Kwa siku moja, tukalazimika tukatoka nje, tukazomewa, tukafukuzwa humu ndani sasa leo mnasema twende mbele tu, tulitoka humu ndani wote, mnasema twende mbele tu tusikumbuke nyuma, why? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hii tunayosema kama mpo sincere mnataka tupigane hii vita kwa sababu kwanza hii vita mlikuwa hamuitaki, sasa kwa sababu Mheshimiwa Rais, yeye ameamua kutofuata...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2017/2018
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi siwapongezi Wizara hii kwa sababu kwanza wanatimiza majukumu yao na pesa wanazozitumia ni kodi ya wananchi. Ila ninachoweza kusema Jimbo langu limekaa vizuri kwenye miundombinu ya maji na umeme tuko vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kusema kinachofanyika humu ndani ya Bunge ni sawa na baba ambaye anaenda sebuleni anajisaidia halafu watoto na mama wanamchachamalia kwamba atoe uchafu aliojisaidia sebuleni, halafu anapoutoa anasema mnishangilie nimefanya kazi kubwa. Hiki ndio kinachofanyika na nyie Wabunge wa Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana, Bunge la Kumi.......

TAARIFA ....

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge la 10 wakati wa saga la Escrow tulikaa katika Bunge hili mpaka saa sita za usiku na Waheshimiwa Wabunge wote tulikubaliana kuhakikisha Mheshimiwa Profesa Muhongo na watu wengine waondolewe. Pamoja na Mheshimiwa Kigwangalla wote mnajua kwenye kumbukumbu alisema hajawahi kuona Profesa muongo kama Mheshimiwa Muhongo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wa CCM na sisi hapa kwa wingi wetu wote mkapiga makofi mkashangilia Mheshimiwa Profesa Muhongo aondoke na kwa sababu, Mheshimiwa JK alikuwa anaheshimu maamuzi ya Bunge, Mheshimiwa Profesa Muhongo na wenzake waliondoka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, alivyokuja Mheshimiwa Magufuli, alivyoanza kuteuwa Baraza la Mawaziri hakujali kwamba Bunge liliona nini, lilifanya nini, akasema hapa kazi, mnamuonea wivu, namchagua Mheshimiwa Muhongo; mkapiga makofi mkasema jembeee! Huko ng’ambo huko, kwa sababu ya wingi wenu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, juzi baada ya huu mchanga amemtumbua, tena mnashangilia mnasema jembee! Ninyi, ninyi! Hebu tufike mahali tuone wajibu wetu wa Bunge ni nini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, amezungumza Mheshimiwa Tundu Lissu ambaye walau katika Bunge hili ana historia ya migodi na jinsi ambavyo watu wameonewa, amefungwa mpaka ndani na mikataba iliyowekwa. Kweli, amekuwa akitetea na hajaacha kutetea wachimbaji wadogo, lakini leo tunaanza kujitoa ufahamu! Wataalam wanasema when you are lost speed is useless; ukipotea spidi haina maana! Ukipotea unarudi unasoma ramani....

T A A R I F A ......

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, this is just a joke, tunazungumza Bunge hatuzungumzi mambo ya Lowassa hapa. Tunazungumza Bunge na wajibu wa Bunge, na tunaowazungumzia humu ndani ni wale waliopewa madaraka ya kuongoza nchi hii. Leo mnajitoa ufahamu mnashangilia Magufuli utadhania ni Columbus anagundua kisiwa cha Australia huko bara la Australia. Anachokifanya Magufuli si kitu cha kwanza.

MWONGOZO.....

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba unitunzie muda wangu. Ninachokisema alichokifanya Mtukufu Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli si kipya, maana mnashangilia hapa utadhania ni Columbus amugundua Bara la Australia. Tume ya akina Maige hapa wapo akina Zito. Haya mambo waliyazungumza. Alipoingia Ikulu tulitegemea angeona mafaili, kitu gani kifanyike kuhusiana na matatizo ya tasnia hii na kwenye Baraza la Mawaziri naye alikuwepo. Sasa hapa mnabeba ngoma mnashangilia kama tumevumbua bara lingine wakati ni mambo yenu wenyewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ninyi CCM ni waungwana mngewaomba radhi Watanzania, kwamba tumechafua sebule. Sebule tumeiweka katika hali mbaya ya hewa tunawaomba radhi tumewakosea. Sasa mnazunguka hapa kwa mlango wa nyuma kama vile sisi wote ni watoto. Eti tumpongeze Mheshimiwa Rais, hii nchi ni ya wote. Siku zote mnasema hapa ndiyo!, iweje nchi ya wote hapa kwenye mambo yasiyokuwa na maana? Tunajitoa ufahamu, ndiyo. Tume ya akina Maige hawa walienda walizunguka nchi nyingi duniani na walilipwa hela nyingi sana Tume na wenzake walizunguka dunia mzima, sasa leo mnakuja hapa tumpongeza Mheshimiwa Rais na nataka niwaambie Watanzania, hizi lugha tunazozungumza hapa kuhusu investors unajua kuna mtu mwingine anadhani investors hawa wa madini wana–invest kama kibanda chako unachouza mkaa huko nyumbani.

Mheshimiwa Naibu Spika, wengi hapa mnazungumza kwa sababu hamjaenda kwenye migodi mkaona heavy investments walizoziweka kule ndani. Kwa hiyo si kitu cha dakika moja; unadhani kwamba unaweza ukawaambia toka leo ingia leo? It is a heavy, ni hela nyingi. Muwaulize wenzenu waliotangulia tulifanya nini kwenye Dowans tulivyojaribu kutaka kuwapeleka mahakamani. Mnasimama tu hapa mnasema tuwapeleke mahakamani, sawa tutaenda lakini hiki tunachocheza nacho hapa si kitu kidogo; na kuwapoteza investors si kitu kidogo. Hakuna mtu wa upinzani anayetaka tuibiwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi tunachozungumza ni juu ya method iliyotumika na namna ya kufanya haya mambo. Tumezungumza miaka mingi tangu wakati wa Mheshimiwa Rais Ally Hassan Mwinyi; kwamba watu wanaingia vibaya mkabisha na ndiyo tabia yenu. Tulivyokuja na suala la Katiba, likiwa linatoka kwetu mkalivamia mkashindwa kulimaliza; tulipokuja na suala elimu bure mkashindwa kulimaliza; tuliwaambia haya madini nayo mnakosea, narudia, narudia tena, When you are lost speed is useless; ukipotea huongezi accelerator, hukanyagi mafuta bali unasoma ramani na ramani pekee ambayo mngechukua ni ile ya Tume ya Bomani, soma anasema nini, ndicho ambacho tungetakiwa kukifanya ndugu zangu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunawatukana wawezekaji kama vile invaders kama vile wametuvamia. Hawa watu tukiwaambia kesho tu wanaondoka. Leo tunawaambia wezi hii mikataba tumefanya wenyewe, Sheria tumetunga wenyewe, leo tunawaita wezi eti tumekamata makontena mia saba, kwani yameanza kusafiri leo? Vyombo vya usalama havikuwepo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunachokisema sisi kama Watanzania mbinu mnayotumia si sahihi. Njia mnayotumia si sahihi kwa sababu inatuingiza chaka zaidi. Niwaombe kama Bunge, tunachotakiwa kufanya hapa ni kuiomba Serikali i-engage, tuingie kwenye majadiliano badala ya kufikia kwenda mahakamani. Kwa sababu nawa- guarantee, kama wakitupeleka Mahakamani we are going to lose big time, whether you like or not. Cha msingi Bunge tungetoa ushauri badala ya kuwafukuza investor na kuwatuna. Ma- investors wale wanaweka heavy money…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila mpangilio)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Kama tumehongwa hela nyie mikataba mliingia wenyewe na mmeifanya hii nchi ya trial and error halafu leo mnasema eti tuwe wazalendo. Katika Bunge liloisha kuna mikataba mingi Sheria nyingi zimetungwa kwa hati ya dharura na hizi Sheria nyingi tumekuwa tukizipinga tukijaribu kuwashauri lakini huwa hamsikii. Niwaombe Waheshimiwa Wabunge hebu tuache kujitoa ufahamu. Wengi wenu hapa mnapiga kelele hata hiyo Sheria ya Madini hamjasoma, hamjui hata hiyo migodi, mmekuwa washangiliaji tu kama Mheshimiwa Tundu Lissu anavyosema mmekuwa washangiliaji hamjasoma hata Sheria unakuja hapa hufanyi research huwezi kuuliza maswali, wewe walichosema tu unashangilia shangilia tu hapa, hili ni Bunge la aina gani? Hebu tuache kujitoa ufahamu turudi kwenye nafasi, tuache kujitoa ufahamu; na wengi wenu mnapiga kelele tu kwenye majimbo yenu hakuna lami, maji, umeme mnatetea mambo ya ovyo tu. Tunachozungumza hapa tunazungumza mustabali wa Taifa letu siyo ushabiki. Siyo ushabiki wa kupiga piga makofi hujaletwa kupiga piga makofi hapa. Kasome Sheria za madini chimba visima hakikisha unatetea maslahi ya nchi yako.

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani hii dozi inatosha nitarudi kidogo kwenye ufahamu.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nami nawashukuru Wenyeviti wote wa Kamati waliowasilisha, lakini na mimi najikita zaidi kwenye Wizara ya Ardhi, Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sisi wengine tuliotoka Bunge liliopita na wakati ule Bunge la Tisa tulipokuwa tukiangalia kwenye television, Bunge kama hili lilikuwa Bunge lenye uhai, Bunge ambalo Serikali inasikiliza hoja ambazo baada ya Waheshimiwa Wabunge kutembea maeneo mbalimbali wanajaribu kuishauri Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni tofauti sana na Bunge hili ambalo kwa kweli limepooza, unakuta hata Kiongozi Mkuu wa Serikali hayupo hapa, Wabunge wanajaribu kutoa maoni yao na kuishauri Serikali, Mawaziri wanachelewa kama hivi Mheshimiwa Waziri wa Maliasili ni hoja yake hapa, ndio anafika saa hizi. Kwa hiyo, hizi ni hoja ambazo tunakiwa tujitathmini kama kweli Bunge tunatimiza majukumu yetu. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo taarifa siipokei. Labda ni Awamu ya Tano ndiyo utaratibu wake. Nimezungumza Bunge la nyakati za nyuma, Spika akiwa Marehemu Mheshimiwa Sitta au Mheshimiwa Anna Makinda, tulikuwa tunamwona Waziri Mkuu anakuwa hapa, tunampa taarifa jinsi tunavyofanya kazi huko. Utaratibu wa sasa hivi toka Bunge limeanza Waziri Mkuu hayupo, Mawaziri wenyewe wanakuwa hawapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ndiyo hiyo, Serikali haitilii maanani hoja ambazo sisi kama Wabunge tunataka kuishauri Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachonisumbua ni jinsi ambavyo haya mambo tumekuwa tukitoa ushauri miaka nenda rudi, lakini tunarudia kila mwaka kuyazungumza yale yale. Kamati ya Maliasili katika kitabu chao ukurasa wa 33, wamesema, Kamati ilikutana na Mkutano wa Wadau na Uwindaji wa Kitalii nchini na kupokea malalamiko yao kuhusu hatua ya Waziri ya Maliasili na Utalii kufuta leseni zote za umilikaji vitalu kwa kipindi cha miaka 2018 na 2022. Sitaki niendelee sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, industry hii ya uwindaji kwa muda mrefu, kwa namna moja au nyingine ndiyo imekuwa inaibeba Wizara hii. Mheshimiwa Waziri anapotoa matamko ya mihemko ya haraka haraka anai-disturb industry. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri anaposema anafuta hizi leseni, naomba nimshauri, kwa sababu kuna vitalu 61 ambavyo havina watu. Kama angetaka vifanyiwe minada anayoitaka, angeanza na hivyo vitalu ambavyo havina watu mpaka sasa huko maporini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tasnia hii uwekezaji wake ni mkubwa sana. Anataka wakafanyie vitalu ambavyo wawekezaji wameweka pesa nyingi sana katika vile vitalu. Miaka mitatu ilioyopita, miaka mitano watu wamewekeza, wengine wamelea simba, halafu unasema wakafanye minada! Ni kuvuruga hii industry. Namshauri Mheshimiwa Waziri, hii tasnia inatakiwa achukue muda kui-study. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, binafsi nimefanikiwa kwenda katika maeneo mengi ambayo nimeona wame-invest hao wawekezaji. Kwa hiyo, tukianza ku-disturb kwa mihemko haitatusaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashauri hawa Mawaziri vijana, fursa au opportunity is attracted by talent skill performance and ability. Show your talent and ability, people will love you. Be humble! Hao Mawaziri wa zamani kwa mfano, akina Lukuvi na Tizeba, tunawaona; wakijibu hoja, wanajibu hoja siyo za kimihemko. Unaridhika hata Mheshimiwa Waziri akikujibu, unapenda. Vijana wengi mnaonekana kama mnataka kufanya Serikali hii kiasi kwamba Serikali inayokuja mtakuwa hamna use. Kwa sababu mna mihemko sana. Onesheni ability na performance mnapofanya kazi zetu ili tuitunze Serikali...


T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S.MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukiilaumu Serikali kwamba inaonekana kila mtu anafanya kivyake, hamja-synchronize. Wakati natoa hotuba yangu ya mambo ya nchi za nje mwaka 2017 nilizungumza, naomba ninukuu mahali nilisemaje?

Nilisema diplomasia ya uchumi pamoja na mambo mengine inahusu kuvutia fursa za wawekezaji wa kigeni (foreign investment), utalii (tourism) na biashara huria (free trade) kwa kufanya ushawishi wenye kufungua masoko mapya ya kuuza bidhaa za Kitanzania kupunguza au kuondoa masharti ya kodi na kusaidia wafanyabiashara na wawekezaji wa Kitanzania kuzitumia kikamilifu fursa za kiuchumi zinazopatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii tasnia; utalii huu umejengwa kwa muda mrefu sana. Akitokea mtu mmoja anaamua kufanya tu kwa kutaka cheap popularity atauvuruga kwa muda mfupi sana. Utalii unaingiza GDP kwa asilimia 20 na forex kubwa inatokana na utalii. Kwa hiyo, hicho siyo kitu kimoja ambacho mtu anaweza akaamka leo akasema nimeharibu. Hii diplomasia ya kiuchumi inategemea sana na kutabirika. Wawekezaji wanataka waone kwamba kunatabirika, tukienda tutafanya biashara zetu. Haiwezekani huyu Waziri, huyu huyu Waziri anatoa amri mpaka na mapolisi wanamkataa, anashindwa hata kuwasiliana na Waziri wake wa Mambo ya Ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu huyu Waziri anatoa amri, anapingana na Waziri wa Ardhi, huyo huyo mmoja! Huyu huyu Waziri anapingana na Waziri wa Uvuvi, huyu huyu Waziri mmoja. Hatuwezi kuwa na Mawaziri ambao wanafanya kazi kwa mizuka. Lazima wote kama

tunaliopenda Taifa letu tufanye kazi kwa kupendana na kuheshimiana katika mipaka. Ndiyo maana nimesema, kama Serikali hamja-synchronize kwamba vipaumbele vya nchi hii ni vipi? Kama vipaumbele hivi, tunataka tutekeleze diplomasia ya uchumi, maliasili ina-fit wapi? Foreign wako wapi? Uvuvi wako wapi? Tunataka tuuze wapi? Sasa kila mtu akiamka asubuhi ana mzuka wake, mara amebebe waandishi wa habari aondoke na makamera, akaseme anayoyataka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana nimesema Waziri Mkuu anatakiwa awe hapa. Waziri wa Maliasili ndivyo tunavyomwona sisi kama Wabunge. Anai-disturb industry. Full time yuko kwenye twitter, kila wakati, utadhania Trump! (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja nyingine ambayo nilisema ambayo nasema kama Serikali hamja-synchronize, nilisema Tanzania haina ajenda ya Taifa juu ya diplomasia ya uchumi wala mipango mikakati inayopimika (strategic plans) ambayo inabeba vipaumbele mahususi yaani specific priority. Tungekuwa na vipaumbele na mipango, maana yake tunge- synchronize. Waziri wa Maliasili anapoona mambo yake ya kiuchumi kuhusu wawekezaji lazima ashirikiane na Waziri wa Ardhi, atashirikiana na Waziri wa Kilimo, atashirikiana na Waziri wa Mifugo, lakini Waziri amekuwa na mihemko, anafanya mambo yake peke yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe ndugu zangu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
Sheria ya Fedha ya Mwaka 2019
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kunipa nafasi. Nina mambo mawili, matatu nitaongea kwa kifupi na kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijazungumza nilitaka nitoe ushauri kwa Serikali kwa sababu tunapokusanya kodi lazima tuwe na jicho pana namna ya ukusanyaji kodi. Kwa mfano, mwaka jana au mwaka juzi tuliongeza kodi kwa watu wanaokuja kidini, kwa mfano, tukatoza dola 500 kwa ajili ya residence permit, labor permit dola 500 ambayo inafika karibu dola 1,000. Sasa ukiangalia jicho la Serikali ni kuangalia tu ile pesa ambayo wanaiingiza wanapoingia lakini hawamuangalii huyu mtu anapokuwa nchi ni kiasi gani cha pesa anakiacha ndani ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, huyu mtu anakuwa na watoto ambao watakwenda kusoma atapeleka pesa shuleni, tayari ni hela tunazipata sasa Serikalil haioni katika jicho hilo. Huyu mtu atakwenda kwenye super market ataacha pesa Serikali haioni kwa jicho hilo. Huyu mtu atakwenda kwenye clubs atakutana na watu mbalimbali wata-socialize wanatafanya manunuzi yapatikane katika nchi, Serikali haikuangalia hivyo inaangalia tu ile kodi ya mwanzo matokeo yake tumekimbiza watu wengi sana nchi za jirani zinawachukua kwa sababu wao wanalipa kidogo. Kwa mfano, Rwanda hapa wa-missionary wengi ambao ni rafiki zangu wameondoka hapa wameenda Rwanda wakati sisi tunatoza dola 1,000 pale wanatozwa equivalent na dola 110 na process ni siku tatu wakati hapa nchini it take ages. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba Serikali tunapotafakari masuala ya kodi na kuzuia hizi permit watu kuja nchini tuangalie ni matumizi kiasi gani yanaweza kutumika baada pale kwa sababu tukiji-limit kwenye hela ile wanaotoa mwanzoni ni ndogo sana matokeo yake tunapoteza maeneo mengi, shule zinafungwa, hoteli zingine ziliajiri watu zinafungwa kwa sababu watu wa nje waliokuwa wana-accommodate maeneo hayo wameondoka. Kwa hiyo, naishauri Serikali mnapofanya mambo muwe mnaangalia kwa mapana.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jambo lingine ambalo nataka kuzungumza katika Muswada huu, Serikali imekuwa ikisema inamjali mnyonge na kimsingi mtu mnyonge kwa Tanzania ni mkulima.

Mheshimiwa Naibu Spika, huyu mkulima anafanya kazi usiku na mchana, ndiyo wanaolisha Taifa letu, wanafanya kazi kwa tabu sana. Kwa bahati mbaya Serikali yenu ya CCM siyo siri mmewavuruga wakulima wa korosho. Mmewaleta adha katika maisha yao lakini kama vile haitoshi sasa tena mnataka mvuruge wakulima wa pamba. Bei ya pamba soko limeshuka duniani na mkulima sasa hawezi kuuza pamba yake lakini nilitegemea mnapoleta sheria hizi walau mngepunguza hizi kodi.

T A A R I F A

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Si uvumilie?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Msigwa, kuna taarifa, Mheshimiwa Innocent Bashungwa.

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpa taarifa Mheshimiwa Msigwa, Serikali haijavuruga wakulima wa korosho bali Mheshimiwa Rais alilazimika kuingilia kati baada ya mfumo mzima wa mnada kutoa bei ya unyonyaji. Baada ya kuapishwa mimi mwenyewe nimeenda ghala kwa ghala kuangalia hali ya koroshona kuona korosho yetu bado ni bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulichokifanya, sasa hivi tumeandaa catalogue ambayo inaonyesha quality ya korosho ni nzuri na sasa tunajiandaa kutumia mfumo wa TMX kuiambia dunia kwamba korosho ya Tanzania bado ni bora. Hata hivyo, kupitia wapotoshaji wachache kama Mheshimiwa Msingwa anavyofanya, dunia imelazimika kuamini kwamba korosho ya Tanzania si bora. Wewe ndiyo unawavuruga wakulima wetu wa korosho si Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nilipenda kumpa taarifa hiyo, tutangulize uzalendo kwanza. Nakushukuru sana. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Msingwa, unaipokea taarifa hiyo.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa yake siipokei kwa sababu yeye amesema walikuwa wanazuia bei za kinyonyaji lakini sasa nyie ndiyo mmepeleka bei za kiporaji kwa sababu wananchi hamjawalipa pesa zao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Waziri wa Viwanda nikushauri na ukamshauri Mheshimiwa Rais, hizi korosho bora mkachome kwa sababu mtaathiri hata korosho zinazokuja kwa sababu hazina soko, mmeziharibu, zinaoza. Sikutaka tufike huko lakini kama mna nia nzuri na nchi yetu hizi korosho zichomwe moto, muwalipe fidia ili tuanze upya kwa ajili ya future reference ili watu waone korosho ni bora. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Serikali hii inasema inawapenda wanyonge hawa watu wa ginneries wana kodi kibao na hawa ndiyo wateja wa wakulima wa pamba. Kwa mfano, kuna baadhi ya kodi anatozwa huyu mtu wa ginneries, anatozwa fire, service levy, leseni ya manispaa na viwanda, weight na management, OSHA, kodi ya mapato hizi zote zinaenda kwake.

KUHUSU UTARATIBU

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu utaratibu

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Sasa Mheshimiwa Inno itakuwa Bunge gani hilo?

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Msingwa kuna Kanuni inafunjwa, Mheshimiwa Innocent.

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesimama kwa Kanuni ya 63(4), Mheshimiwa Msigwa amesema kwamba korosho ya wakulima wetu imeoza na mimi nimetoka kwenye maghala yote tumefanya cutting taste tuna catalogue ambayo inaonyesha kila lot ya korosho ipo katika hali ya namna gani, korosho yetu bado ni bora. Sasa ningependa Mheshimiwa Msigwa athibitishe kama korosho imeoza kweli.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, kama korosho haijaoza basi kwa kutumia Kanuni za Bunge Mheshimiwa Msigwa achukuliwe hatua. Kwa sababu korosho ya wakulima wetu bado ipo katika hali nzuri na mimi nina ushahidi naweza nika-print hiyo catalogue nikakukabidhi sasa hivi na yeye kusema kwake kwamba korosho imeoza athibitishe kama kweli korosho imeoza. Nashukuru. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, wakati akiichangia Mheshimiwa Msigwa amesimama Mheshimiwa Innocent Bashungwa kwa mujibu wa Kanuni 63 (4). Kanuni hii ya 63 inakataza kusema uongo. Kwa muktadha wa kanuni hii nzima ukiisoma inamtaka Mbunge anayesema Mbunge mwingine anasema uongo anapaswa kuthibitisha yeye kwanza kwa mujibu wa fasili ya (5) na nyingine zilizopo hapo ili sasa Mbunge yule aliyekuwa anachangia kabla ya yeye kusimama kuhusu utaratibu aweze kupewa fursa ya kuthibitisha yale aliyoyasema ama vinginevyo.

Waheshimiwa Wabunge, lakini niseme hivi, kwa muktadha huo huo wa Kanuni ya 63 nadhani Mheshimiwa Msigwa na natumia neno ‘nadhani’ Mheshimiwa Msigwa hoja yake ilikuwa kwenye korosho kwamba bado zipo maghalani zinunuliwe. Sasa baada ya kupewa taarifa ndiyo ameenda huko kwenye korosho kuoza. Kwa hiyo, Mheshimiwa Msigwa nyoosha machango wako vizuri ili tusizipungukie Kanuni zetu namna zinavyotutaka. (Makofi)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kutoa mwongozo vizuri na ningeomba tu ieleweke sisi ni Wabunge na hapa tupo kuwatetea wananchi dhidi ya government. Kwa hiyo, hatuko hapa kitu chochote kinacholetwa na Serikali tukiamini. Ndio maana huwa inaundwa Kamati ya Bunge kwenda kuchunguza, I don’t trust what you are talking, vinginevyo iundwe Kamati ya Bunge ikathibitishe hayo unayoyasema, why do you what me to trust what you are saying?

Mheshimiwa Naibu Spika, niko hapa kwa niaba ya wananchi, mimi napata ripoti kwa wananchi, tupo hapa kuwasemea wananchi verses the government ili government iwatumikie wananchi inavyopaswa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nilichokuwa nasema hizi kodi zinamfanya mkulima apunjwe kwa sababu hawa watu wanachajiwa kodi zote hizi hapa mwisho wa siku hizi kodi kwenye pamba zinamfanya mtu anayeumia wa mwisho awe ni mkulima. Kwa hiyo, nilitegemea Muswada huu utakapokuja hapa kama kweli mnawajali wanyonge mngewakumbuka hata wanyonge wa pamba, mahindi ambao mara nyingi wakilima mahindi yao mnazuia hayauzwi matokeo yake wanapata hasara, wanakuwa hawaondoki kusogea mbele kimaendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana kwenye michango yetu tumesema mngepunguza kodi za mabati, za nondo, hivi vitu vya kujengea wananchi hawa wanyonge mnaowasema ingewasaidia.

Sasa mmevuruga wananchi wapo stacked, it is obvious wananchi wa Mtwara wapo stacked, hii haihitaji rocket science kuelewa kwamba shughuli ya korosho imewashinda na mngekuwa waungwana mngesema we blue it, tungewaona mna busara lakini bado mnabumbabumba tu, mnatudanganya hapa, you blue it brother. Mngetuambia tumeshindwa tuanze upya, what is the way forward. Sasa tusipokuwa waangalifu msimu wa korosho unaokuja tutaharibu tena kwa sababu ya ubishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, juzi nilisema if you are lost you don’t have to accelerate you stop and you read the map, unatafuta njia inaenda wapi. Tusipokuwa waangalifu, kama suala lenyewe ndiyo hiyo pamba ime-stack mbona hajampeleka Jeshi kwenye kununua pamba? Kama Jeshi ina- work, kama hiyo methodology mliyotumia it is working kwa nini hamja deploy makanda kwenda huko kwenye pamba si hainunuliwi sasa hivi hapa?

MBUNGE FULANI: Na kahawa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Na kahawa. We told you kwamba haya mambo yanahitaji negotiation, tunajadiliana, tunakuwa na mutual understanding na ndiyo maana tupo hapa kushauriana tunataka taifa letu liende mbele.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kumpongeza Mwenyekiti wa Kamati pamoja na Kamati nzima kwa kazi nzuri ambayo tumeifanya kama Kamati, lakini kwa usimamizi mzuri wa Mwenyekiti wa Kamati.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika ukurasa wa kwanza kwenye kitabu chetu, Kamati katika aya ya tatu imesikitishwa kwa kitendo cha kupigwa risasi Mbunge mwenzetu Mheshimiwa Tundu Lissu. Jambo hili lilisikitisha, lilistua, vilevile nimeshtuka sana wakati Wabunge wengine wakipongeza kitendo cha Kamati kusikitishwa na jambo hili niliona Wabunge wengine wamenuna, isipokuwa tu walipotajwa Wanajeshi 15 ndiyo watu wakapiga makofi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwangu binafsi imenisikitisha sana, ubaguzi wa wazi. Mbunge mwenzetu ameumizwa watu wamekaa kimya, hili jambo hatupaswi kulifumbia macho. Kwa sababu ya muda mdogo wengine watalizungumza, lakini hili ni jambo baya sana. Ninaiomba Serikali, sasa ni zaidi ya miezi mitano hakuna suspect hata mmoja! Tumeomba Vyombo vya Kimataifa vitusaidie kuwapata hao watu, Serikali inakataa. Ni lini Serikali itatuambia kuhusu tatizo hili ambalo lilifanyika mbele ya macho ya watu juu ya mwenzetu aliyepigwa risasi. Hili ni jambo la aibu na hatupaswi kulifumbia macho katika Taifa letu, ni jambo la hovyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, Mheshimiwa Heche juzi alizungumza hapa, mimi ni Mjumbe wa Kamati hii ambayo tunachangia, kuhusiana na suala e-passport ambalo Waziri wa Mambo ya Ndani, Mheshimiwa Mwigulu alizungumza kwamba kilichozinduliwa siku ile ni e- immigration. Nataka nipate majibu halisi kwamba siku ile Mheshimiwa Rais alizindua e-immigration au ni e-passport?

Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima tujue jambo hilo kiundani. Kwa sababu Serikali hii imekuwa ikijipambanua kwamba ni Serikali inayokomesha ufisadi, lakini kiundani kama Kambi ya Upinzani tunazo nyaraka za kutosha, ambazo tutaziweka wakati muafaka. Nyaraka za kutosha ambazo hazina mashaka juu ya ufisadi na harufu kubwa ya ufisadi ndani ya jambo hili katika Serikali hii ambayo inayojipambanua kwamba ni Serikali inayopingana na ufisadi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano; katika mkataba ambao waliingia kwenye Memorandum of Understanding, bei ya passport moja ilikuwa inagharimu Pound za Uingereza 6.84, lakini hii e-passport iliyozinduliwa inagharimu Dollar 68 na ndiyo maana bei ime-shoot kutoka Sh.50,000 mpaka Sh.150,000. Mkurugenzi anasema kwamba hii ni ya miaka 15 hata ya Sh.50,000 tuliyokuwa tunatoa ilikuwa ni ya miaka 15 anyway. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, wananchi wa Watanzania hebu tuione hii Serikali inayojipambanua inakomesha ufisadi wakati kuna harufu kubwa na kwa kichaka cha Usalama wa Taifa. Pia niseme haya mambo ya kusema hela inayoenda Usalama wa Taifa Wabunge tusijue, hiyo siyo kweli.

Mheshimiwa Naibu Spika, tufuatilie nchi kama Israel, tufuatilie nchi kama Uingereza, Bunge tunayo haki ya kujua hela inayokwenda Usalama wa Taifa, isipokuwa hatuna haki ya kujua wanafanyaje ndani ya Usalama wa Taifa. Hata hivyo, kutudanganya kwamba tusijue hela inayokwenda Usalama wa Taifa ndiyo wizi unakopigiwa huko kwa kigezo cha kwamba haya ni mambo ya siri, masuala ya passport siyo mambo ya siri.

Mheshimiwa Naibu Spika, kulikuwa na watu waliopewa kazi Memorandum of Understanding ni kwa nini walitolewa akaja akapewa mtu mwingine kinyemela nyemela? Hii ni hoja ya Mheshimiwa Heche….

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ukicheza na nguruwe kwenye matope mtachafuka wote, lakini nguruwe atachekelea. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nataka nilizungumze …

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili nataka nizungumze Polisi wamekuwa wakisema kwamba tutii sheria bila shuruti, lakini Polisi ndiyo wa kwanza wenyewe kuvunja sheria. Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, inamtaka Polisi akimkamata Mtuhumiwa ampeleke Mahakamani ndani ya masaa 24, lakini mimi ni shahidi nimekuwa mhanga wa kuingia mara nyingi Kituo cha Polisi.

Mheshimiwa Naibu Spika, I am not criminal, I am a Politician, lakini kuna watu ambao wameomba niwasemee na Mheshimiwa Waziri unasikia hapa, wamekaa ndani ya Kituo cha Polisi kwa mfano Iringa Mjini, kabla ya Christmas miezi miwili wako ndani, hawatoi maelezo, hawapelekwi Mahakamani. Kwa nini tunawatesa watu?

Mheshimiwa Naibu Spika, mmezungumza hapa asubuhi nimeuliza swali la kupiga watu, Polisi wanapiga watu wanawavunja mpaka miguu, wanawaonea! Anakamatwa mtu hana makosa, amekamatwa mzima akifika ndani ya Kituo cha Polisi anapigwa, akipelekwa hospitali wanawaambia wasiwaandikie hata matibabu. Hii nchi tunaipeleka wapi?

Mheshimiwa Naibu Spika, wengine humu ndani tunapozungumza masuala ya Polisi mnaona kama vile hakuwahusu, wengine hata hamna legitimacy ya kuongea masuala ya Polisi. Kwa sababu you have never been there, hujawahi kwenda Magereza, hujawahi kwenda Polisi, unajaribu kuchangia, unadhani labda hakukuhusu! Hata kina Mramba walidhani hakuwahusu, lakini siku moja walienda.

Mheshimiwa Naibu Spika, mazingira ya kule ndani ni ya hovyo, Mbunge ambaye sina makosa nimechaguliwa na wananchi, natimiza majukumu yangu ya Kibunge …

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji).
Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi. Na mimi nichukue fursa hii kuwapongeza Mawaziri wote watatu wa TAMISEMI, pamoja na changamoto tulizonazo lakini unaiona ile sense ya utendaji kazi na kufika kwa haraka kwenye maeneo ambayo tunafanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hilo tutakuwa tunafanya makosa tusipowapongeza, hasa Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Selemani Jafo, amekuwa msikivu na anajitahidi, pamoja na kwamba vitendea kazi vinaweza visiwepo, lakini niwapongeze kwa ujumla wenu, pamoja na Mzee wangu, Mheshimiwa Kapteni Mkuchika katika eneo lake la mambo ya Utawala Bora ambalo mimi ndiyo nitajikita zaidi na nitakupa vidonge kidogo Mheshimiwa Kapteni Mkuchika kwenye eneo lako. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika nchi yetu suala la utawala bora, ambalo kwenye hotuba yake Mheshimiwa Kapteni Mkuchika, amegusagusa tu mambo mengine lakini mambo ya msingi hujayagusa. Ndugu zangu Taifa hili ni letu sote, kwa bahati mbaya kuna watu wengine wana notion kama Wapinzani ni intruders na kwamba kuwepo kwetu hapa ni kama fadhila fulani ambazo tunapewa na mtu fulani. Sisi hapa ni Watanzania halisi, hii ni nchi ya kwetu na tulifanya chaguzi, tumekuja hapa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tunazo haki na Katiba yetu inaturuhusu kuwepo kwetu hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali iliyofikia kwa sasa hivi kwa mazingira ya utawala bora ni hali ya hovyohovyo sana katika nchi yetu. Tatizo kubwa katika Taifa letu tuna-embrace mind ndogo na tunapuuza big mind. Taifa ambalo halitaki big mind, watu wenye uelewa mkubwa hawatakiwi, watu wanaohoji, wanaodadisi hawatakiwi katika Taifa letu. Tukitaka kujenga Taifa lenye nguvu, lenye uchumi mpana ni lazima tuwe na hoja zinazokinzana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa na Bunge ambalo linapenda kushangilia vitu vya hovyohovyo na hii inatokana kwenye Taifa letu kunapofanyika promotion au appointment au placement kwenye eneo lolote, haitegemeani na merit. Unapomchagua Katibu Mkuu wa Wizara unamchagua kwa vigezo gani, unataka aka-add value gani? Unapomchagua Mkuu wa Mkoa unamchagua kwa kigezo gani, anaenda ku-add value gani kwenye ule Mkoa? Unapomchagua Mkuu wa Wilaya unamchagua kwa kigezo gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulilalamika wakati Serikali hii inaingia madarakani kwamba mmewatoa ma-DED waliokuwa wazuri, wanafanya kazi, wana weledi kwenye ofisi zao, wakaletwa watu ambao kwa sababu tu walivaa uniform za CCM, leo tumeona jinsi ambavyo Halmashauri zetu zinavyoshindwa kufanya kazi. Kumekuwa na nepotism ya hali ya juu sana, kumekuwa na upendeleo wa hali ya juu sana kwa sababu hawa wote wanaochaguliwa hawaendani na kazi walizopewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano ofisi ya Katibu Mkuu ni ofisi serious kabisa, unamwona mtu kama Profesa Kitila Mkumbo, badala ya kushughulikia na namna ya kumtua mama ndoo kichwani yeye amekazana anaandika kuwajibu Maaskofu ambao wanashughulika na roho za watu mitaani, badala ya kukaa kwenye ofisi haya ndiyo ninayosema mtu hajui anaenda kuongeza value gani na nimezungumza mambo ya placement haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unamchukua mtu kama Profesa Kitila anayezungumzia mambo ya elimu unampeleka kwenye mambo ya maji, anakaa ofisini badala ya kuzungumza mambo ya kumtua mama ndoo ambalo ni wazo zuri, yeye anakazana anataka amjibu Askofu kwa sababu ya mawazo waliyotoa kwamba hakuna demokrasia nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, dola karibu milioni 500 za India zimerudi huko kwa sababu ya utendaji wa hovyo kabisa wa Serikali zetu…

KUHUSU UTARATIBU . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ndiyo mambo ninayozungumza. Dada yangu namheshimu sana na ni Engineer huyu, anashindwa kuelewa, yaani anashindwa kuunganisha utawala bora ninaouzungumza na natoa kwa mifano. Sasa hizi ndiyo appointments ambazo zinatolewa, haelewi kabisa hapa ninapozungumza. Nimezungumza kuanzia uteuzi wa Katibu Mkuu, ukienda kwenye Wakuu wa Mikoa watu kama akina Mnyeti, anasimama kinyume kabisa na utaratibu wa sheria, Mkuu wa Mkoa kabisa anagawa kadi za Chama cha Mapinduzi barabarani. Mtumishi wa umma, tunazungumzia masuala ya utawala bora, anagawa kadi na anasema sitashirikiana na Wapinzani, halafu mtu kama huyu bado yuko kwenye ofisini, halafu mnakuja hapa mnasema kuna utawala bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, analipwa kodi ya nchi hii, halafu…

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna-embrace vitu vidogovidogo; huyu kijana mdogo, msomi, anashindwa kutofautisha kazi ya Mkuu wa Mkoa na kwenye vikao ndani ya Chama cha Mapinduzi, this is very sad, hawezi kuelewa tofauti hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu kama Mnyeti hapaswi kuwa kwenye ofisi ya Umma ya Serikali, mambo ya CCM akayafanye kwenye ofisi ya CCM huko. Unamchukua mtu kama Makonda, kila siku anaharibu, alianza madawa ya kulevya, leo…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

T A A R I F A . . .

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii hotuba ya Serikali imeandaliwa si chini ya miezi sita na haijaandaliwa na Waziri, imeandaliwa na timu kubwa, leo mnataka sisi tuandae kwa dakika moja kwa sababu mnaamini tunafanya mchezo hapa, nakupuuza wewe, sijui Daktari wa wapi wewe. Sasa narudi kwenye hoja yangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tumekuwa tukiishauri Serikali hii na tutaendelea kuishauri. Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliwashauri juu ya makinikia ni aibu kubwa mkagonga ukuta kwa sababu ya utawala bora ambao hauendani. Tuliwashauri juu ya sukari, tuliwashauri juu ya Bombadia ni kwa sababu ya kuweka watu ambao hawaendani kwenye ofisi, hili ni suala la utawala bora ambalo nazungumiza. Leo mnakosa hoja hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunapozungumzia utawala bora, wengi hapa tunapozungumza tumekuwa tukishauri na ndiyo wajibu wetu, tumetoa ushauri mkapiga kelele hapa kwamba tutapewa trilioni 490 ziko wapi leo? Leo kuna watu wanapitapita hapa kuwaambia Wabunge wa CCM msizungumze masuala ya makinikia kwa sababu ni aibu, hakuna hela hizo. Akaja Dokta yule akawaambia atawapa hela, bilioni 300, ziko wapi? Mheshimiwa Dokta Mpango atuambie ziko wapi kwenye bajeti kwenye vyanzo vyake, kwenye mpango wake ziko wapi hizo hela za Acacia? Mambo yote yamekuwa ni aibu kwa sababu hamtaki ushauri na unakosekana utawala bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kipaumbele cha nchi hii ni kipi katika masuala ya utawala bora?

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwambie Mbunge; mama nataka nikwambie niko vizuri sana, kama mnataka suala la DNA niko vizuri, labda kama mnahitaji vitu vingine, napo niko vizuri kabisa, anayetaka kuja aje tu. Kama mnadhani hiyo ni kiki mnapoteza muda niko vizuri kabisa na nina watoto saba. Mawaziri wote tutawapima DNA humu ndani, si mnataka tupimane, haina shida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachozungumza ndiyo haya, tunaacha kuzungumza mambo ya maana tunazungumza mambo ya kipuuzi kwa sababu tuna-embrace akili ya kijingajinga, tunaacha kuzungumza mambo ya uchumi wa nchi hii unahangaika na DNA yangu, ya nini? Au unanitaka? Hapa we are talking about serious matters... (Makofi)

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza masuala ya uchumi katika nchi hii…

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza masuala ya barabara mbovu katika nchi hii, tunazungumza masuala ya utawala bora, watu wanakufa, watu wanauawa, unahangaika na DNA ya kwangu, haya ndiyo mambo ninayoyazungumza… Bunge ambalo linatakiwa…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mchungaji Peter Msigwa muda wako umekwisha, inatosha. Ahsante sana.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Kumi na Kumi na Moja wa Bunge
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru, kwanza kabisa naunga mkono maoni ya Kamati na niwapongeze sana kwa kufanya kazi nzuri sana ambayo kimsingi imekuja wakati muafaka jinsi ambavyo tunaona watu wengi wanaoumia huku chini ni wananchi wanyonge ambao Serikali ya Awamu ya Tano imesema inashughulika nao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria ipo kwa ajili ya kumfanya binadamu awe bora, haipo kwa ajili ya kumkandamiza binadamu. Ukiangalia hizi sheria nyingi, hata kwenye Halmashauri zetu ni sheria ambazo zimekuwa kandamizi na zinazidi kuleta ugumu kwenye maisha ya huyu Mtanzania. Kwa hiyo, niseme Mheshimiwa Chenge pamoja na Kamati yako nikushukuru sana kwa kazi kubwa mliyofanya ya uchambuzi ambayo tukienda kwa kina kama wabunge tutaweza kuwasaidia watu wetu wasiteseke sana huko chini ambako kimsingi ndiko wanakoumia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiangalia sheria mama kwa mfano ya BASATA ambayo ilisainiwa na Baba yetu wa Taifa, Mwalimu Julius K. Nyerere mwaka 1985, kifungu cha pili kimeorodhesha kabisa ni nini sanaa, imefafanua nini ni sanaa, lakini kwenye kanuni alizotuletea Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe hapa ukisoma ukurasa wa 59 ameingiza pamoja na ukumbi nayo ni sanaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa unashangaa ukumbi unakuaje nao ni sanaa, hata ukimuuliza mtoto wa darasa la pili; nina mtoto wangu anaitwa Simon, mtoto wa darasa la pili, ukisema taja kitu ambacho hakihusiani na sanaa azungushie pale, nadhani ukumbi ukiweka miongoni mwake atasema hakipo, sasa sielewi Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe amewekaje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, angalia sasa kwenye mambo aliyoyataja yanayohusiana na ukumbi. Anasema gharama za kibali kwa kumbi za maonesho sanaa na burudani zenye ukubwa wa kukaa watu wasiozidi 350 yaani unapokwenda kufanya maonesho hayo ukalipe shilingi 350,000 unapeleka BASATA, siyo unalipia ukumbi, unapeleka BASATA, bado ukumbi hujalipia, watu 350 unalipa shilingi 550,000 unapeleka BASATA. Ukumbi unahusianaje na sanaa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nikizingalia hizi kanuni za Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe zinakwenda kinyume kabisa na hii sheria mama ambayo Baba wa Taifa aliisaini. Hii inaonesha jinsi ambavyo Serikali ya Awamu ya Tano iko desperate, inatafuta hela kwa gharama yoyote ambazo hazihusiani kabisa na masuala ya sanaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kumbi zenye ukubwa wa watu 750 na kuendelea mtu analipa 1,050,000 kupeleka BASATA, what is this? Hapo bado hujalipia ukumbi. Sasa hizi ni sheria kandamizi ndiyo maana narudia tena kwamba niwapongeze sana Kamati, mmefanya kazi kubwa kuangalia sheria kama hizi. Bado kuna kodi mbalimbali na siyo ukumbi tu, sasa haya ni mambo ya kuwanyonya na kuwakatisha tamaa hawa wanyonge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na kwamba Mheshimiwa Dkt. Mwakyembe ame-withdraw hiki kitu, lakini bado nasema hii sheria tungetoa maamuzi kwamba isifanye kazi, isimame kwanza kwa sababu ina mapungufu mengi, BASATA bado wanaitumia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, ni sheria hii hii ilimzuia msanii ambaye amejaribu kuiweka Tanzania kwenye ramani, Diamond, wamemzuia anataka kwenda nje, vijana hawa wako talented, wanajaribu kutafuta pesa lakini kwa sheria mbovu kama hii tumemzuia asiende kutafuta pesa. Bado hata wasanii wadogo ambao wanajitahidi wanaambiwa wanapotaka kwenda kwenye matangazo watoe shilingi milioni tano, huku ni kuwakandamiza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye maelezo yenu yote mmesema mnataka mkuze vipaji, tutakuzaje vipaji kwa kanuni kama hizi. Kwa hiyo, niseme tu kwamba sheria kama hizi zinakandamiza wananchi, zinaonea wananchi, ni wakati muafaka kwamba tufafanue kwa pamoja na ni vizuri sheria kama hizi zisiwe zinaanza kufanya kazi kabla hazijaja tukazipitia humu na wataalam vizuri ili ziwe zinafanya kazi, itasaidia kupunguza matatizo kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo linaendana na hili, kuna wakati mwingine kuna sheria hizi ndogo ambazo zimeainishwa kabisa kwa mujibu wa sheria. Kwa mfano tuna sheria za Serikali za Mitaa, nikichukulia mfano wa kesi ya Mheshimiwa Haonga. Mheshimiwa Haonga alifanya makosa kwenye kikao cha Halmashauri kwa mujibu wa mashtaka aliyopelekewa Mahakamani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa bahati mbaya Maafisa wa Mahakama wamekwenda kumshtaki kwa sheria nyingine tofauti na mahakama ambayo mpaka hakimu anasema mmemleta kwenye mashtaka haya wakati huyu makosa yake alitakiwa ahukumiwe na sheria ndogo ya ndani ya Manispaa. Kwa hiyo, maafisa wanapotosha, badala ya kuisadia mahakama kufafanua vizuri hizi sheria ndogo zinavyotumika, wanajikuta wanapotosha umma, wanatumia sheria nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni sawa na hapa Bungeni. Hapa tukikoseana kwa makosa ya kimaadili hauwezi kuchukuliwa hapa ukapelekwa mahakamani kule, ndiyo maana kuna Kamati ya Maadili hapa inakuita inakuonya. Lakini matokeo yake huko mitaani kwenye Halmashauri zetu watu wakifanya makosa ya kimaadili utakuta watu wanatumia madaraka yao vibaya wanawapeleka mahakamani kwa sheria zile mnaita criminal procedure, si ndiyo? Sheria za Makosa ya Jinai, wakati watu wamekosea. Kwa hiyo, hata hizo sheria ndogo zipo haziheshimiwi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba wale maafisa wa Serikali tusaidiane tuwaelimishe wananchi, tusaidiane kuelimisha mahakama tuiongoze mahakama vizuri kwa sababu wao ni Maafisa wa Mahakama.

Kwa hiyo, Mheshimiwa Chenge na Kamati yako nikupongeze sana kwa kazi nzuri ambayo kwa pamoja tutakwenda kuwasaidia wananchi wetu.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia kwenye mjadala ulio mbele yetu. Kabla sijasahau, Mheshimiwa Sware amezungumza sana kuhusiana na Ruaha mto mkuu kukauka, lakini nataka tukumbushane kama Wabunge kuna mwandishi wa kitabu anasema: “The Politicians don’t care about economics, and the economists don’t understand politics.”

Mheshimiwa Spika, ni kweli watu wamepongeza nia njema ya Rais ya kutaka wale watu walionyanyaswa kwenye maeneo mbalimbali jinsi ambavyo wametendewa vibaya, lakini vilevile kama viongozi ambao tunalitakia mema Taifa hili tusije tukaziacha faida za kiuchumi ambazo zinatokana na kutunza mazingira. Kwa hiyo, natamani wote kwa pamoja kama Wabunge hayo tuyaangalie, tusipige kelele tu watu wanapovamia maeneo ya utunzaji, hatuwezi kusahau eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, takwimu za mwaka 2009 katika sekta ya utalii zinaonesha mapato duniani, yaliyotokana na shughuli za utalii yalikuwa dola za Kimarekani bilioni 852, watalii waliosafiri duniani kote walikuwa zaidi ya milioni 800 na sekta hii ilitoa ajira zaidi ya milioni 255 duniani kote, hii ilikuwa ni asilimia 11 ya ajira duniani.Hii inaonesha jinsi gani sekta hii ilivyo na umuhimu na inaajiri watu wengi na inazalisha shughuli mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, kumbuka wakati huo Serikali ilijaribu kupanua wigo, lakini kama dunia nzima toka wakati huo, miaka kumi sasa imepita watu walikuwa milioni 800 wanaotalii, wakati huo nchi yetu ilikuwa na uwezo wa kuvutia watalii laki nane na kitu, Mahiga atanisaidia, alikuwa Waziri wakati huo.

Mheshimiwa Spika, lakini mpaka leo, pamoja na fursa nzuri tulizonazo katika nchi yetu, hatujaweza kufikisha watalii 1500, tunahangaika hangaika kwa sababu hatuna mipango endelevu, milioni moja na nusu hatujafikisha, tunahangaika kwa sababu hatuna mipango endelevu. Hatuna mipango endelevu kwa sababu hatu-plan kama Taifa.

Mheshimiwa Spika, katika Wizara hii, Waziri aliyekaa muda mrefu katika historia ya nchi hii ni Mheshimiwa Zakhia Meghji na huyu Waziri inasemekana alikaa muda mrefu katika Wizara hii kwa sababu alikuwa anawasikiliza wataalam. Nchi yetu ni miongoni mwa nchi ambazo zina vivutio vingi sana, tungeweza kuwa-attract kwa sababu hawa watalii tunanyang’anyana na nchi zingine, lakini kwa bahati mbaya Wizara hii imekuwa ikibadilishwa Mawaziri ambao wanaenda wanakuwa kama ni wajuaji kuliko uhalisia.

Mheshimiwa Spika, tuna fukwe nyingi, katika nchi yetu hatuja-utilize, tuna maeneo mbalimbali hatujaya-utilize, wakati ule takwimu hizi zinatokea wataalamu walikuwa wamejua kwamba na World Bank ilikuwa imesema kwamba kwa sababu sekta hii inaajiri watu karibu laki tano kama tukikuza utalii, upande wa kusini tutakuwa mara mbili, kwa sababu kaskazini ndio iko zaidi. Kwa hiyo tukikuza kusini itakuwa mara mbili.

Mheshimiwa Spika, nazungumza kwamba Wizara hii, tumekuwa hatuko consistency watu wanaoingia, kwa sababu tumeenda kwa pamoja mradi wa REGROW alikuja Makamu wa Rais alikuja Iringa, akauzindua lakini kwa taarifa nilizonazo kama Mbunge na Mjumbe wa Kamati, huu mradi wa REGROW unaonekana unasua sua na kuna dalili kwamba World Bank wame-pull off hata hiyo hela tena, haipo tena. Kwa hiyo ile mipango yote mizuri, ambayo tulitakiwa tukuze Mikumi, tukuze Ruaha tuuokoe mto Mkuu Ruaha mipango hii yote inakufa tena.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tunaanza kulalamika katika suala la Utalii kwa sababu mipango tunayopanga inakuwa sio endelevu, kila anayeingia kwenye Wizara ni kama yeye ndio anaanza anaacha mipango mizuri ambayo wengine wameanza. Mfano mzuri rafiki yangu Mheshimiwa Kigwangalla amekuwa na matamko mengi ambayo ni matamko ambayo yanaleta madhara, Twitter zake zinaleta madhara. Juzi ameenda kwenye TTB amevunja Bodi, tumesikia tena hiyo Bodi haijavunjika bado ipo. Kwa hiyo masuala haya wanafanya mambo ambayo hawafanyi utafiti, yana-disturb industry.

Mheshimiwa Spika, industry hii ni very delicate, hawa watalii waliokuzwa kutoka laki nane mpaka tulipofika imefanyika kazi kubwa sana ya kutangaza utalii huu. Sasa tunapokuwa hatuko consistency, hatufanyi kama ambavyo tume-plan, tunasababisha industry iyumbe na inaingiza uchumi mkubwa sana katika nchi yetu. Kwa hiyo niiombe Wizara itafakari kwa makini, ni namna gani inaweza kuiendeleza sekta hii.

Mheshimiwa Spika, tuna matatizo ya hospitality tunapozungumza masuala ya hospitality ina-involve mambo ya customer care, ina-involve mambo ya customer service, ina-involve hoteli zetu nyingi ziko sub-standard watalii hawaendi tu kwa sababu ya kwenda hotelini na kwao kuna hoteli nzuri, hoteli ziko sub-standard, watu hatujawa-train, watu wakifika hapa wanapata shida. Sasa hao watalii wataongezekaje? Watalii wakija hapa kwetu watakwenda kulala wapi, watakaa wapi, kama hiyo competition hatulingani na watu wengine duniani. Hilo nilitaka nizungumze kwa mapana.

Mheshimiwa Spika, takwimu ambazo zimetolewa na Wizara yenyewe, tatizo lingine kubwa ambalo limesababisha watalii Tanzania isionekane ni nzuri zaidi mambo ya usafi, hygine kunaonekana kuna uchafu, watalii wanalalamika, ni takwimu za Wizara yenyewe, kuna mambo ya usalama, kuna mambo ya infrastructure, haya mambo yote wanayolalamika yanasababisha utalii uwe wa hovyo.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine nataka kuzungumza ambalo kwa masikitiko makubwa niseme katika Kamati tulipokuwa tuna-windup jana tulilipanga nalo lingeweza kuzungumzwa katika Kamati hii, kwa bahati mbaya halijazungumzwa, ambalo katika Kamati yetu tulipata malalamiko kuhusu unyang’anywaji wa mashamba makubwa. Hatuna tatizo na mashamba makubwa kunyang’anywa kwa mujibu wa sheria, lakini kuna mashamba makubwa katika Wizara ya Ardhi, pamoja na sifa nyingi ambazo Mheshimiwa Lukuvi hata mimi nimeshiriki kumpa, lakini suala hili la mashamba makubwa lina harufu fulani ya ukakasi, lazima tuelezane ukweli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika mashamba makubwa haya, kwa mfano Mheshimiwa Sumaye…

T A A R I F A

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, sasa mimi nimemchafuaje hapa anavyosema? Nadhani anaenda haraka, kwani nimesemaje sasa, anasema nimemchafua, wapi? (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nimezungumza kwamba sina tatizo kabisa na mashamba makubwa kunyang’anywa kwa mujibu wa Sheria na taratibu kwa kufuata procedure. Nimetoa mfano mmoja, mimi sijagusa mashamba ya Jimboni kwake, nimetoa mfano kwamba Mheshimiwa Sumaye, alikuwa na shamba lake, alilipata kihalali, ameliendeleza mpaka wana-revoke lile shamba lake alikuwa na ng’ombe 200 kwenye shamba, alikuwa na kondoo 350, nyumba kubwa ya umwagiliaji, visima, go-down. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ameambiwa hajaendeleza, nasema unyang’anyaji huu, Rais kubadilisha hati ana mamlaka hayo, Rais anaweza akabadilisha sio tatizo, lakini ninachosema...

SPIKA: Aaah, muda umekwisha Mheshimiwa, dakika kumi zimekwisha.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, dakika nane mpaka sasa hivi nikisoma hapa, ziko dakika nane….

SPIKA: Malizia sentensi yako basi.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, mpaka sasa hizi ukiangalia jinsi ambavyo mashamba hayo yamechukuliwa, akina MO, wameendeleza mashamba lakini wamenyang’anywa, ndio maana sisi, lazima, bila ubaguzi…….

(Hapa baadhi ya Waheshimiwa Wabunge walizomea)

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Lazima bila ubaguzi, tulitaka Kamati ya Uchunguzi iundwe, kwa nini mnakataa kuunda Kamati ya Uchunguzi? Lazima Kamati ya Uchunguzi iundwe ili tuone uhalali wa mashamba hayo kunyang’anywa. (Makofi)
Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Dhana nzima ya uhifadhi wa mazingira yaani Flora pamoja na Fauna wote kama Watanzania tunapenda sana, lakini masuala kadhaa katika mambo ambayo nimeyazungumza muda uliopita ni lazima kama Taifa tuwe tumejiuliza na kujihoji.

Mheshimiwa Spika, Serikali yetu imekuwa na mipango mingi sana na hasa Wizara hii, lakini kuna wakati mwingine mipango hii huwa haifiki mwisho. Kupandisha hadhi mapori ni jambo jema, lakini kabla hatujapandisha ni lazima tujihoji masuala ya msingi sana. Ni kweli kama wenzangu ambao tuko nao kwenye Kamati wamepongeza utendaji mzuri sana wa TANAPA, namna ya uhifadhi na kwa kweli TANAPA wanafanya kazi kubwa sana ya uhifadhi na kama Bunge tunapaswa tuendelee kuwaunga mkono, lakini bado nauliza swali lile lile ambalo wenzangu wameuliza.

Mheshimiwa Spika, TANAPA tunazidi kuiongezea mzigo kwa sababu haya mapori yalikuwa TAWA, TAWA tumeipa mamlaka, sasa TANAPA ambayo ni hifadhi zake tano tu ambazo zinaendesha hifadhi zingine 11. Swali ambalo tunapaswa kujiuliza kama Serikali na kama Taifa; pamoja na kwamba tunaongeza hizi hifadhi lakini lazima tuwe na mikakati ambayo itasababisha hifadhi hizi ziweze ku-generate income. Kama TANAPA ina hifadhi tano zinaendesha hifadhi 11 ni dhahiri kwamba mapato mengi ambayo yangeweza kuleta shughuli nyingine za kimaendeleo tunajikuta yanakwenda kuendeleza hifadhi zingine.

Mheshimiwa Spika, sasa niombe Mheshimiwa Waziri atakapokuja hapa ajaribu kutupa picha ni namna gani hizi hifadhi zingine ambazo hazija-break even kwa muda mrefu, ni nini mkakati za Wizara kwa hizi hifadhi zingine 11, time limit ni kwa kiwango gani hizi hifadhi zitaendelea kuwa tegemezi kwa hifadhi zingine au tutaendelea kuchukua kiwango kile kinachopatikana kwenye hifadhi zingine na kuendelea kutunzwa kwenye maeneo mengine. Hili ni jambo ambalo tunapaswa tujiulize kabla ya kwenda haraka haraka kufanya maamuzi tunayokwenda kuyafanya.

Mheshimiwa Spika, jambo kubwa ambalo tunapaswa tujiulize; kwenye Bunge la Bajeti Mheshimiwa Waziri alikuja hapa na tukapanga mipango mizuri sana ya kukuza utalii Kusini mwa Tanzania na mipango ilikuwa mizuri sana, Serikali ikaenda World Bank ikakopa pesa Dola bilioni 150 kuhakikisha maeneo ya Mikumi, Ruaha, Selou yote tunaiimarisha ili tukuze utalii upande wa Kusini. Ni maeneo machache tu, lakini kabla kabla hatuja-take off tumeanza tena maeneo mengine. Tunapenda Tanzania tuiunganishe yote kwa pamoja, lakini hatuwezi kufukuza sungura wawili kwa wakati mmoja. Waziri hajatoa maelezo ya kina ni kwa kiwango gani REGROW inaendelea mpaka sasa.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema tuna taarifa kwamba World Bank wame-pool out kwa sababu Serikali haiku consistency kwenye maamuzi yake. Wananchi wa Kusini wametutamanisha, wametupa imani, wakazi wangu wa Manispaa ya Iringa walikuwa na matumaini makubwa kwamba tunakwenda kuinua utalii sasa, wakazi wa Mbeya, wakazi wa Mikumi, hata Selou waliaminisha Taifa hili. Nakuwa na wasiwasi isije ikawa kama wakati ule wa gesi watu waliimba hapa gesi, gesi, gesi, gesi ikaenda, baada ya muda ikapotea tena.

Mheshimiwa Spika, napata tabu kwamba inaonekana hata hii REGROW inaweza ikawa kiini macho. Nimwombe Mheshimiwa Waziri atupe maelezo ya kina ni kwa kiwango gani na kwa namna gani kuboresha Southern Circuit. Haitaathirika na mipango mingine sasa tunayokwenda tena upande mwingine kabla huku hatujamaliza. Serikali ya Chama cha Mapinduzi imekuwa ni bingwa sana wa kuanzisha miradi na kuachia njiani kama ambavyo wanataka kufanya sasa hivi. Uwanja wa Nduli kwa mfano pamoja na kuongeza runway lakini bado tunahitaji kuwa na jengo la wageni, la wasafiri hatujaimarisha, bado tunahitaji kuwa na barabara kutoka Iringa Mjini kwenda Ruaha National Park. Wajumbe wa Kamati wataniambia ni tabu kweli kweli kusafiri kutoka Iringa Mjini kilomita 104 kutoka Iringa Mjini kwenda Ruaha National Park, haya mambo hayajafanyika.

Mheshimiwa Spika, tulizungumza mradi huu ulikuwa ukatengeneze barabara nzuri za kwenda Selous kwenye mahoteli na hela tumeshapata. Tumeanza ku-service mkopo, lakini sasa ghafla tumeongeza mambo mengine ambayo wakati bado hatujaimarisha. Niseme siwezi kusema naunga au napinga, lakini kuna maswali mengi yanaleta ukakasi, kwa nini hili jambo lije kwa haraka na haya mapori tunayo?

Mheshimiwa Spika, jambo lingine; wenzangu wanasema itasaidia kupunguza migogoro. Wote hapa ni mashahidi zimetokea kampeni mbalimbali mara tokomeza, mara nyingi, kugombana na wananchi, wafugaji hasa wanapoingia kwenye hifadhi na tumekuwa tukii-task Serikali kwamba lazima itenge maeneo ya wafugaji na uhifadhi. Sasa leo watu wanasema kwa kuongezewa hifadhi tutapunguza migogoro, sasa hii migogoro mingine yote iliyoko kwenye hifadhi imetokana na nini? Kwa sababu wananchi huwa wana-intrude kwenye maeneo ya hifadhi. Sasa ni kwa kiwango gani Serikali imeweka utaratibu ambao hatutaingia kwenye matatizo kwa sababu hifadhi zote za nchi hii ukienda karibu zote kuna ugomvi kati ya wafugaji na wahifadhi, kuna watu wanavamia maeneo ya uhifadhi.

Mheshimiwa Spika, sasa tusije tukawa tunakuja hapa kwa haraka haraka, halafu baadae tena tukaingia kwenye shida ambayo kimsingi tusipofanya vizuri tunaingiza gharama kwa TANAPA yenyewe kuijendesha, kwa sababu kwanza itaanza kugombana tena na watu. Tunaifanya TANAPA iwe adui kwa wananchi kwa sababu hatujapanga mipango vizuri. Watu wakiona magari ya TANAPA wanawachukia, watu wakiona mavazi ya TANAPA wanawachukia kwa sababu wanaona kama wanaumiza, wakati tulitakiwa tuweke utaratibu mzuri wananchi waone faida ya uhifadhi huu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo naomba Mheshimiwa Waziri lazima atuambie ni namna gani mpango huu hautaathiri mpango mzuri ambao umeanza upande wa Kusini. Kusini kuna maeneo, isiwe sifa tu kwamba Ruaha ni kubwa lakini uwekezaji mdogo. Naamini tukienda huku
TANAPA sasa, watahamisha pesa nyingi sana kuanza kubeba mzigo mkubwa huu wa Magharibi wakati Kusini hatuja-take off, hatuja-take off kwenye miundombinu, hatuja-take off kwenye mambo ya mahoteli, mambo ya customer service, mabo ya customer care, hospitality kwa ujumla iko chini, badala hizi pesa tungeweka kwenye vitu vya msingi ambavyo vingesababisha vitu vya juu vijichukulie vyenyewe, tunaongeza mzigo mkubwa.

Mheshimiwa Spika, nadhani kama Bunge kwa pamoja tungetafakari tusifanye haya mambo kishabiki, wote tunahitaji maendeleo, tunahitaji uhifadhi kama nilivyosema, siko kinyume na uhifadhi kabisa, lakini kama Taifa na kwa pamoja tunatakiwa haya masuala tuyaangalie wka upana, tuone yataleta tija gani. Kwa hiyo kwa ujumla, sikatai au siungi mkono ila nataka kwanza wote tutafakari kwa ujumla tuone ina tija gani hasa kwa kuzingatia REGROW naomba nipate majibu ya Mheshimiwa Waziri ili niweze kuwa comfortable kama mwakilishi wa Kusini. Ahsante sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kwa kunipa hizi dakika tano. Mara nyingi tumeambiwa kwamba upande huu hatusifu, nianze sasa kwa kutoa sifa zifuatazo. Kwanza, nimshukuru sana Mheshimiwa Mkuchika alikuja akatoa Semina nzuri ya Maadili ya Utumishi wa Umma ambapo vijana wengi pale Iringa waliifurahia. Sijui nani watakaorithi kuendelea na utaratibu ambao Mheshimiwa Mkuchika aliufanya maana wafanyakazi wengi waliufurahia. Hayo ni mambo mema ambayo tunapenda yatokee katika nchi kwa sababu ni mazuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, nimshukuru sana Waziri wa Afya na Naibu wake pale ambapo Mkuu wetu wa Mkoa ali-demoralize spirit ya watendaji kazi katika Manispaa ya Iringa, alim-harass sana Daktari wetu ambaye ni Bingwa ambao tumewasomesha vizuri, lakini walihakikisha yale mambo wameyaweka calm yakaenda vizuri na Daktari anaendelea vizuri. Hilo niwashukuru sana ni mambo mema mnayoyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la tatu ambalo napenda nishukuru tena katika Manispaa ya Iringa ni pale ambapo Mkuu wa Mkoa alivyofika tulikuwa na machinjio; Kamati ya LAAC walifika na waliona tuna machinjio nzuri sana, ilikwama kwa sehemu na wakaiona, wakatutia moyo. Ilipaswa iwe imeanzishwa miaka mitatu, minne iliyopita lakini kukawa na vikwazo vya kisiasa, wakatupa ushauri lakini kuna mambo mengi tulivyotaka kuanza kulikuwa na taabu sana, Mkuu wa Mkoa kajiapiza kwamba akiwa yeye Mkuu wa Mkoa hataruhusu hela yoyote ije. Niwashukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu pamoja na Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo, jana Meya wangu wamesaini, Serikali imekubali ku-release shilingi bilioni 1 ambayo itasaidia kufanya hayo machinjio iweze kufanya kazi. Haya ni mambo mema ni lazima tupongeze na kama mwakilishi wa watu ni lazima niyapongeze. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niombe Wizara kama nilivyomsifu Mheshimiwa Mkuchika tufanye kazi kwa utaratibu na Maadili ya Umma kutokana na sheria inavyosema. Hawa Wakuu wa Mikoa wengine kwa kweli wanapagawa sana, hawamjali mtu yeyote. Naomba kama inawezekana kwa mujibu wa utaratibu Mheshimiwa Waziri Mkuu na Waziri wa TAMISEMI, tuendelee kusaidiana, muendelee kuwalea hawa vijana wenye mihemko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haya mambo ya kuwekaweka watu ndani ina-demoralize utendaji wa kazi. Lile wiki alilokuja Ndugu Hapi Iringa Mjini wafanyakazi wote walikuwa down lakini kwa sababu na mimi nilikuwa na misuli ya kutosha, nilihakikisha napandisha ile morale ya utendaji kazi ili turudi kwenye utendaji kazi na kufuata masharti ya utumishi wa umma. Watendaji hawa wateule, Wakuu wa Wilaya, wanatumia vibaya madaraka yao. Hili ni Taifa la wote, tunatakiwa tufuate taratibu, kanuni na miongozo.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa, nilishamuona Mheshimiwa Waziri Mkuu, kuna Bwana mmoja alikuwa ni Mkurugenzi wetu aliondolewa Iringa kwa siasa, Iringa kuna siasa nyingi sana. Hata hivyo, tunafanya kazi kama nilivyosema tunaongoza kwa kukusanya mapato, tunaongoza kwa usafi na tunapata hati safi mfululizo. Misingi hii aliyetuwekea ni Bwana mmoja anaitwa Ahmed Sawa, mmeenda kum-dump sijui wapi huko Mkoani kwa kosa ambalo hana. Watumishi kama hawa hata asiporudi Iringa mtafutieni sehemu nyingine afanye kazi kwa sababu ni mchapakazi, ni mbunifu, haya mambo tunayoyapata leo ni kwa sababu ya utendaji wake mzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana, nimeona nitoe haya kwa sababu mimi ni mwakilishi wa watu na watu wengine hawayajui, watu wengine wanaonewa sana katika nchi hii kwa makosa ambayo hawajayafanya.

Mheshimiwa Spika, Nikushukuru sana.

T A A R I F A

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nilitaka nipokee tu taarifa yake kwamba haya matatizo ya Wakuu wa Wilaya na Mikoa yako maeneo mengi. Kwa hiyo, Waziri Mkuu na Serikali mnasikia, sisi Wabunge tunataka tufanye kazi na wateule wa Rais kwa kupendana siyo kwa kushindana. Mtu anakuja ametukuta pale tunafanya kazi, haya mambo hayakuzuka kuna watu walifanya kazi.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru sana kwa kunipa nafasi lakini nalidhani Serikali ingekuwa inavumilia ikatujibu kwenye hoja, sisi ndivyo tunavyoona, hayo ni maoni ya Kambi ya Upinzani. Naona mnaogopa kivuli chenu wenyewe huku mnasema mmejipanga na tupo tayari kutoa ushahidi. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Msigwa, jambo likishafanyiwa maamuzi usilete ushabiki ambao hauna maana. (Makofi)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Toka Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani imefanya maamuzi makubwa matatu na maamuzi madogo madogo mengi ambayo kwa ujumla wake siyo chini ya 10. Serikali ya Awamu ya Tano ilifanya maamuzi ya Kikokotoo, korosho, Muswada wa Habari, Muswada wa Takwimu, kutokufanya kazi na CAG, Muswada wa Vyama Siasa, Stiegler’s Gorge, SGR, ununuzi wa ndege na kuhamia Dodoma. Is a major decision toka Serikali ya Awamu Tano imeeingia madarakani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya sifa za viongozi duniani ni pamoja na kufanya maamuzi (decision making), sina tatizo na hilo lakini tunapaswa tujue kama Taifa kwamba consequences are more important than decisions. Matokeo ya maamuzi tunayoyafanya ni ya muhimu zaidi kuliko maamuzi tunayoyafanya. We don’t live by decisions we live by consequences, hatuishi kwa maamuzi tunayoyafanya dakika moja tunaishi kwa matokeo ya maamuzi tunayoyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kabla ya kufanya maamuzi watu wenye busara, wenye hekima wanaoongoza lazima wajifunze consequences. You have to study the consequences before you make decisions. Unafanya research, unatafuta information, unatafuata historical data, unatafuta watu wengine wamefanya maamuzi gani katika mambo unayokwenda kuyafanya na unajifunza kwa watu wengine katika maamuzi unayokwenda kuyafanya. nimezungumza tumefanya maamuzi makubwa sana kama Serikali na Serikali tunazungumzia masuala ya utawala bora na Serikali za Mtaa, haya mambo yote lazima yawe synchronized ili tupate matokeo yaliyo bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tukienda kwenye Kikokotoo, Mheshimiwa Jenista anahusika. Mlikuja hapa na nyimbo nyingi sana kuhusu Kikokoto na kwa mujibu wa taratibu ili sheria ije Bungeni inapitia hatua mbalimbali. Inaanza kwenye Wizara husika, inakuja kwenye Cabinet Secretariat, inakuaja kwenye MMC, Makatibu, inaenda kwenye Baraza la Mawaziri, inaenda kwa wadau inakuja Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa baada ya kufanya maamuzi ya Kikokotoo tukapitisha kwa nyimbo nyingi sana hapa na tuliwaambia humu ndani, baada ya miezi mitatu mkaweka U-turn. Swali la kujiuliza, are we capable to lead this country? Kama kupitia hatua zote hizi mmefanya haya mambo yote ndani ya miezi kadhaa Kikokotoo kikageuka, mkarudi na ngonjera zingine za kukipinga Kikokotoo ninyi wenyewe hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais, ameteua wengine hapa Maprofesa, Madaktari, degree holders wanaoweza ku-scrutinize vitu, kuona kama vina hoja; think tank ya Ikulu, nasi Wabunge tunaowawakilisha wananchi hapa, tukaimba ngonjera nyingi bila kuangalia consequences. Tunaitumbukiza nchi kwenye matatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hiyo haitoshi, lilikuja suala la Korosho hapa, tunasema tunataka tuwe na maendeleo, mkaondoka mpaka na azimio la kusifu maamuzi ya Korosho. Baada ya muda mfupi, leo tunaambiwa kangomba hawana makosa. Tuliitwa Kangomba sisi huku. You guys did you study the consequences of the decision you are making? (Makofi)

MHE. JOHN W. HECHE: Mnaita mhindi anunue kilo ngapi...

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi ambao mnasema mko fit kuiongoza nchi hii, did you study the consequences? Kama hiyo haitoshi, Muswada wa habari, nilitegemea maswali; kama nilivyosema inapitia maeneo yote hayo; Muswada wa Habari, mnataka kuniambia Mawaziri walikuwa hawajui kwamba unakinzana na Jumuiya ya Afrika Mashariki? Mmekuja hapa mmelazimisha, mnataka kusema mlikuwa hamjui, kama unakinzana na Jumuiya ya Afrika Mashariki! (Makofi)

MHE. JOHN W. HECHE: Na mli-ratify wenyewe.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi wenyewe Baraza zima la Mawaziri, mlileta hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, mkaleta takwimu, tukapitisha na azimio la kusema hatufanyi kazi na CAG. Leo vitabu vyake viko hapa na sahihi iko hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu kwenu, ninyi mnapofanya maamuzi, huwa mnajifunza consequences? Do you do research? Maprofesa mko hapa, huwa mnafanya research ili mfanye hayo maamuzi. Leo tumefanya maamuzi makubwa. Nia na dhamira nzuri ya Stiegler’s Gorge na Standard Gauge ni mambo mazuri ya kuhamia Dodoma na kununua ndege, vyote ni vitu vizuri. Ila consequences zinazotokea sasa hivi kwa maamuzi hayo makubwa ambayo tulikuwa hatuna priorities, ndiyo maana tunaona hamwezi kuajiri wafanyakazi wapya. Those are the consequences na hamkuliandaa Taifa kwamba hatutaajiri wafanyakazi wengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna increment kwa wafanyakazi, mishahara haiongezeki, hakuna motisha. Halafu haya mambo makubwa mnategemea staff wataleta positive result katika mambo haya ambayo hamkufanya study? Asimame mtu hapa atuambie what are the consequences na tuta-suffer kipindi hiki bila kuajiri wafanyakazi wapya for how long? Leo mnasimama hapa mnasema, ukisikiliza hotuba za Mheshimiwa Rais, ni contrary kabisa na ninyi Mawaziri mnavyofanya kazi hapa, zote! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kuna Wizara moja tu ambayo mimi naiona Mheshimiwa Rais hazungumzi ni Wizara ya Ulinzi. The rest, kwenye mikutano yake huko, Wizara karibu zote, tulizungumza na Mheshimiwa Mpango, hayupo hapa leo; tulimwambia utaratibu wa kodi unaofanya haufai, leo Mheshimiwa Rais anasema yale yale tuliyosema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulizungumza mambo ya msingi mengi hapa hamkutusikiliza. Leo mnasema wawekezaji. Tuliwaambia mnafukuza wawekezaji, leo Mheshimiwa Rais ndiye analalamika kwamba wawekezaji wanakimbia. Why do you expect wawekezaji waje katika nchi ambayo hakuna democracy, hakuna good governance, hakuna kuelewana! Mnataka kupuuza kwamba sisi wote hatuna social capital katika nchi hii? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnataka kupuuza Kiongozi wa Kambi ya Upinzani kwamba hana social capital katika nchi hii? Hatuna wafuasi katika nchi hii? Nani atakuwa na confidence ya kuleta mitaji hapa nchini aweze kuwekeza kwenye nchi hii ambapo hakuna uhuru wa mawazo, hatuwezi kuji-express? Nani ataleta mitaji katika nchi ili mambo yaende vizuri mahali ambapo Wakurugenzi, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, kila mtu anaenda njia yake? Mheshimiwa Rais anatoa maagizo haya, Mkurugenzi anatoa haya, Waziri anasema haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kuleta mabadiliko na tabia za kama Manaibu Waziri akina Mheshimiwa Waitara hapa, ambao kila saa anadhani tuko kwenye Mikutano ya Siasa. Changamoto tulizonazo zinahitaji big brain. Tanzania tuna matatizo makubwa kutoka hapa tulipo. Hatupo kwenye Mikutano ya Kisiasa hapa ndani. Uliondoka CHADEMA, is over. Do the job, mwonyeshe Mheshimiwa Rais kwamba you are capable. Show your talent! Show your ability. (Kicheko/ Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa mambo ya kusema nilikuwa CHADEMA, mipasho, haitusaidii. Mheshimiwa Rais amewapa hiyo kazi, hebu tuonyesheni uwezo wa kututoa hapa tulipo. Nchi hii haina mashimo ya vyoo sasa hivi, mnasema huko, vyanzo vyote kwenye hotuba yetu tumezungumza, vimehamishwa vyote vimekuja Serikali Kuu, lakini hela hiyo hairudi kwa wananchi.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Reverend Msigwa. (Makofi)

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Nimemaliza! (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kuisoma nukuu hii inayosema; “Udikteta wa wengi wape. Udikteta wa wengi wape ni ile hali ambapo Serikali au mamlaka nyingine inayoungwa mkono kidemokrasia na wafuasi wake wengi walio katika vyombo vya maamuzi wanapoamua kutengeneza sera au kupitisha maamuzi yenye kufaidisha maslahi yao lakini bila kujali haki wala ustawi wa watu wengine wote walio chini ya utawala wao.”

MWENYEKITI: Niambie source yake.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, source yake ni kwenye dictionary.

MWENYEKITI: Niambie dictionary ipi.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni Oxford Dictionary.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi ni wawakilishi wa walipa kodi na kuna myth inataka kutengenezwa katika Bunge hili kwamba sisi wapinzani hatuwapendi polisi. duniani kote polisi wanasimamia law and order na tunahitaji Polisi hakuna mtu ambaye hawataki Polisi, hiyo ieleweke kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wanataka kupotosha hapa na kujipendekezapendekeza kana kwamba sisi hatuwataki polisi, hata sisi tukichukua nchi tutawataka polisi. Kuna mambo Jeshi la Polisi linafanya kazi vizuri na ndiyo maana kwenye Utawala Bora Mheshimiwa Mollel alisimama hapa kuwatetea wafanyakazi wa umma ambao ni pamoja na polisi wapate mishahara yao. Kwa hiyo, hiyo myth iondoke kwamba sisi hatuwataki Polisi, tunawataka polisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja kubwa tunayojenga dhidi ya polisi ni pale ambapo hawafuati sheria. Kuna Police General Order (PGO) lakiniPolisi hawaifuati na sisi hapa ni wajibu wetu kama Wabunge kuhakikisha inafuatwa. Sisi tunasema wafuate sheria ninyi hamtaki, sasa mnataka waendesheje Jeshi, tunataka wafuate sheria kwa sababu hazifuatwi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijasahau, Mheshimiwa Kangi, nina maswali kadha ambayo lazima uwaambie Watanzania na Mheshimiwa IGP ananisikia hapa. Mheshimiwa Rais hivi karibuni aliliambia Jeshi la Polisi kwamba Watanzania siyo wajinga, ile move ya MO, haieleweki. Tunataka uwaambie Watanzania exactly what happened? Kwa sababu polisi kazi yao ni kulinda raia na mali zao, full stop. Mimi kama Mtanzania Polisi ana wajibu wa kunilinda, exactly tunataka tujue movehiyo na Rais alisema, kama mnapinga maamuzi ya Rais sijui, alisema Watanzania siyo wajinga na IGP akasema baada ya siku tatu atatoa taarifa, sasa hivi muda umepita hiyo taarifa haijatoka, we want to know that. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, number two, polisi bado hawajatuambia, what exactly, ni kitu gani kilimtokea Roma Mkatoliki, bado tuko gizani hatuna majibu hayo, tutakuwa Wabunge wa hovyo sana kuliruhusu Jeshi la Polisi mambo ya hovyo yanatokea halafu eti tuseme polisi wang’atwa na mbu, hawalali si ndiyo kazi ya polisi, yaani mwanajeshi akienda vitani tuanze is not doing as a favor that is his job. Utuambie Roma Mkatoliki kilitokea kitu gani nchi haijui. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, polisi haijatambua kuvamiwa kwa Clouds, hamjatoa maelezo yoyote Clouds ilivamiwa kilitokea gani? Nani alihusika nani alikamatwa hatuwezi kukaa kimya halafu tukasifu tu Jeshi la Polisi hapa. Polisi haijasema kuhusu Azory na jana nimesikitika sana kumsikia Mheshimiwa Mwakyembe hapa anasema eti mtu mmoja tu tunaangaika naye. Uhai wa mtu mmoja ni wa thamani sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwenzangu ame-quote Biblia out of context lakini Biblia inasema tumeumbwa kwa image ya Mungu, mtu mmoja akipotea Taifa lazima linununike, watu wanaokufa siyo inzi ni binadamu. Polisi hamjasema kitu gani kimetokea kwa Ben Saanane mnabumba bumba mpaka leo. You must tell us nani alimuuwa Mawazo polisi mmekaa kimya, Jeshi la Polisi halijasema Mheshimiwa Kangi, polisi hamjasema mpaka leo dunia nzima mnasema (Makofi)

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. MCH. PETER S.MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Tundu Lissu anawabagaza Polisi hamjasema nani alimpiga risasi kwa Tundu Lissu…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpe taarifa huyu.

MHE. MCH. PETER S.MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna uchunguzi tutakaaje kimya tuseme Jeshi la Polisi tunalishangilia matukio makubwa kama haya, dunia inaona, Polisi hawatoi ripoti sasa kazi yao nini? Kazi ya Polisi ni kulinda raia na mali zao ndiyo kazi ya Polisi. Polisi anawajibu wa kulinda raia na atoe ripoti kwa nini raia wameuwawa tuende wapi, wao ndiyo wana mabomu, wao ndiyo wana vitendea kazi, tumewakabidhi watulinde na wapo kwa ajili ya hiyo. Nani alimnyooshea bunduki Mheshimiwa Nape we are quite, polisi hawajatoa ripoti nani alionesha bunduki pale amechukuliwa hatua gani? Sasa tukae hapa tuseme hoo wanang’atwa na mbu sasa wana kazi gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma historia duniani wenzetu Marekani ambapo demokrasia imeshamiri George Washington alivyokuwa anaunda Serikali walitaka kumfanya awe mfalme akasema lazima tuwe na Serikali ambayo itakuwa na nidhamu kwa wananchi. Leo vyombo vya dola tunaonekana kama sisi ni watumwa swali la kujiuliza; are we captive or we are citizen in this county? Kwa sababu maonezi yanayofanywa kwenye Vituo vya Polisi ni makubwa sana sisemi Jeshi la Polisi lote. Kama mimi Mbunge nimesingiziwa kesi ya kuchoma nyumba, nimesingiziwa kesi ya kubomoa nyumba hawa raia wa kawaida na siyo Mbunge fala, lakini nimesingiziwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kesi zimeenda Mahakamani within a minute zimefutwa kwa sababu ni uovu, RCO wa Iringa amehamishiwa sasa hivi Pemba anatengeneza kesi za uongo kabisa nimelala mahabusu kwa kuonewa na wengine wenu hapa hamna legitimacy ya kuongelea mambo ya custody wala huko kwenye cell, you have never been there! Hamjui ukienda central pale how it looks like? We have been there. Hamjaenda Segerea mnasema tu hapa hamjaona watu wanavyoteswa kule ndani, hamna hiyo legit. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaongea haya mambo kwa sababu tuna experience, anasimama leo, leo Kikatiba mtuambie kama Katiba haifuatwi hii, nchi ni ya utawala wa sheria, Katiba inatupa haki ya kuandamana, anasimama RPC, mtumishi wetu, mtumishi wa umma sisi siyo captive, we are not captive we are citizen anasimama and we pay them na wamekuja hapa kuomba hela ili tuwalipe…

MWENYEKITI: Ongea na Kiti.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, yes sir, anasimama kwenye vyombo vya habari anasema nitawatandika nitawachakaza who he think he is? Nataka niwaambie Polisi kuna watu ambao walifanya makosa katika Vita vya Pili vya Dunia… (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa ongea na Kiti, huwezi kuwaambia Polisi ni-address mimi.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu ambao walifanya makosa katika Vita Vikuu vya Pili vya Dunia leo wanalipa gharama you never go away pale ambapo mlipaswa msimamie sheria mkafunika mkadhani sheria haitawafuata; somewhere in the future tutakuja tutakukamata kwa sababu sheria inakutaka ufuate sheria, watu wanaoza kwenye vituo, wanakamatwa raia, sheria inasema wakae masaa 48 wanakaa miezi miwili, wanakaa miezi mitatu, tumekuwa na torturing chamber katika nchi hii watu wanapigwa, kuna yule mzungu amevunjika miguu, anateswa na mabinti wengine wa kike wanamwambia aoneshe uchi wake wanamtesa, “how can we live in this county. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, halafu tuseme tusikemee haya mambo haya tutasemea wapi? Raia wanakufa kwenye mikono ya Polisi kila wakati halafu tusiseme halafu tuseme wapi. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kumwomba Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi Mheshimiwa Mengi ambaye amekuwa na mchango mkubwa katika Taifa letu. Pia niwashukuru Madaktari wote nchini, Manesi na Wauguzi wote nchini, kwa kweli wamekuwa wakifanya kazi kubwa, kazi ngumu, kazi ya wito, kazi ya kujitolea. Niwashukuru wote kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la iringa Mjini kwa kazi kubwa ambayo wamekuwa wakiifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, niseme mawili matatu yanayohusu jimbo langu na mengine nitaangalia yanayohusiana na Taifa. Amezungumza Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum hapa kuhusiana na Hospitali yetu ya FRELIMO ya Manispaa ya Iringa, asubuhi nimeuliza swali hapa, nashukuru Waziri amejibu lakini niombe wizara wasaidiane na TAMISEMI, wilaya zingine zote zilipewa fedha zile karibu bilioni moja kusaidia vifaa, hospitali yetu ile ni ya muhimu, ikiwezeshwa itasababisha hospitali ya rufaa ipunguziwe mzigo. Niombe sana tusaidiane kuhakikisha haya mambo yanafanyika kama Waziri alivyosema wa TAMISEMI.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa Mheshimiwa Ritta hajasema sana, hospitali ya mkoa kwa sasa hivi hakuna bingwa wa mifupa, Daktari wa Mifupa wala Bingwa wa surgery. Hii yote aliyoisababisha ni Mkuu wa Mkoa katika ziara yake aliyosema Iringa mpya. Katika Iringa yake mpya imekuwa ni ya kubomoa. Sasa hivi pale Hospitali ya Rufaa kuna matatizo makubwa sana, wagonjwa wanategemea Walimu wanaokuja kuwafundisha wanafunzi wa UDOM kuja kufanya upasuaji, kwa hiyo imekuwa ni ngumu sana. Niombe sana Wizara na Serikali kwa ujumla, hebu tuangalie viongozi wasiwe wana-demoralize wafanyakazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hao Madaktari wanasomeshwa na nchi kwa gharama kubwa sana na wanafanya kazi kubwa sana, kama kuna matatizo ya management, ya kiutendaji, zifuatwe procedures za namna ya ku-deal nalo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakumbuka Mkuu wa Mkoa alimdhalilisha Daktari Nyakioto, ni bingwa, amefanya kazi kubwa sana, pia kuna Daktari Rehema naye ameondoka lakini hawa watu wote wamekimbia Iringa ni kwa sababu ya utendaji wa hovyo wa wanasiasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Wizara iji-commit kwa sababu Wakuu wa Wilaya wala Wakuu wa Mikoa siyo ngazi za kutoa adabu kwa watendaji. Naomba mnapotoa majibu hapa mtangazie Tanzania kwamba wao wala viongozi wa chama kama kule Arumeru, kiongozi wa kata tu anampa maagizo daktari eti dakika 15 umefika. Naomba Serikali itangaze kwamba wao siyo ngazi za kuwawajibisha, madaktari hawa wanafanya kazi kubwa sana. Niombe hilo mlifanyie kazi ili madaktari na manesi wetu wafanye kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, madaktari na wauguzi wetu wanahitaji kutiwa moyo, ni watu ambao wanashika vinyesi, mikojo na mautumbo yetu, lazima tuongee hizo ni kazi za kujitolea. Viongozi wa kiserikali na wenye vyeo tunatakiwa tuwape moyo, tusiwa-demoralize, tuwape moyo wafanye kazi vizuri kama ambavyo tuna mategemeo mazuri kutoka kwao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hotuba yetu ya Kambi ya Upinzani, Mheshimiwa Esther ameorodhesha viongozi wengi wa kisiasa na amewataja. Namba hili suala mlitolee maamuzi ya msingi kabisa ili utendaji kazi uende sawasawa kama sheria na taratibu zinavyotaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine ni hili ambalo na Mheshimiwa Sakaya amelizungumza ni la wazee kwenye masuala ya pensheni, mliahidi kabisa kwamba mtawaongeza kutoka Sh.50,000 kwenda Sh.100,000, wale waliokuwa PPF wameongezwa wengine wamekuwa wakidai hawajapata. Ni lini sasa fedha zao ambazo wanatakiwa waongezewe watapewa? Hawa ni wazee ambao wamefanya kazi kubwa katika Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna wataalam wengine wanasema we are just dwarf standing on the shoulder of the giants. Sisi ni matokeo ya hao wazee waliotangulia. Tutakuwa ni taifa la namna gani tusipowaenzi wazee. Tukumbuke na sisi tuta-phase out, tutazeeka. Hiyo nafasi uliyonayo hapo Mheshimiwa Waziri na Naibu wako kuna wengine walikuwepo wameondoka. Hata mimi nafasi yangu ya Ubunge niliyonayo hapa kuna wengine walikuwepo wameondoka. Tunapofika mahali kama taifa wazee hatuwaheshimu, hatuwatunzi kwa kweli hatuwatendei haki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri katika maeneo haya ya kutunza wazee, hebu tusilaaniwe na Mwenyezi Mungu tunapokuwa tumewasahau wazee. Tupange bajeti za kutosha kuwasaidia hawa wazee. Wazee wengi ukiwakuta katika maeneo mbalimbali wanalalamika.

MBUNGE FULANI: Akina Mzee Lubeleje.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Wanalalamika hawapati huduma zinazotakiwa. Ndiyo maana wakati mwingine tunalazimika kurudi Bungeni humu kwa sababu hali ni ngumu huko mitaani.

MBUNGE FULANI: Usituseme bwana.

MBUNGE FULANI: Akina Mzee Lubeleje.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati mbaya bajeti ya Wizara hii imeendelea kushuka, sasa hawa wazee tunawasaidiaje? Wizara hii ni nyeti, amezungumza Mheshimiwa Lwakatare hapa, kweli kuna vifo vingi ambavyo kimsingi siyo Bwana ametwaa, ni kwa sababu hazijapatikana huduma za msingi ambazo zingeweza kuokoa maisha ya watu wengi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, watoto wengi wanakufa kwa sababu hawajapata huduma zinazostahili. Akina mama wajawazito wengi wanakufa kwa sababu hawakupata huduma zinazostahili. Watu waliopata ajali wengi wamekufa si kwa sababu walitakiwa kufa, ni kwa sababu hawakupata huduma zinazostahili. Tumekuwa hatuna vifaa vya kutosha, hatuna madaktari wa kutosha lakini hata hao madaktari wachache walioko bado tuna wa-frustrate. Naomba sana katika eneo hili Mheshimiwa Ummy na kweli wengine wamesema mara nyingi ukipigiwa simu umekuwa una-respond pamoja na Naibu wako…

MBUNGE FULANI: Wanachapa kazi.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Una-respond na unajibu kwa wakati, ningeomba hii ishuke mpaka huku chini na madaktari hao walindwe. Wana chama chao, wana namna yako ya kuwalinda, walindwe hawa madaktari kama wana makosa mimi siwatetei lakini hatuwezi kuwaadhibu madaktari wetu kwenye mikutano ya hadhara, hatuwezi kuwaumbua madaktari wetu kwenye vikao vya kisiasa. Wahukumiwe, waadhibiwe kwenye proper channel, inaumiza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mkutano mmoja wa siasa umeathiri hospitali yangu hakuna madaktari bingwa, ina maumivu makubwa sana. Nikuombe Mheshimiwa Ummy Mwalimu, hili linaniumiza sana kwa sababu hapa napata meseji Iringa kama unavyoiona, tumeitengeneza Southern Circuit ili tukuze utalii, tunahitaji tuwe na hospitali za kutosha. Iringa ni mahali pazuri, pana hewa nzuri, tuna mazingira mazuri lakini inapofika mahali tunakosa madaktari tunaongeza matatizo yasiyokuwa ya lazima katika Manispaa yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambvyo Waziri amekuwa aki-respond nimwombe katika suala hili alisaidie taifa zima kwamba tuheshimu madaktari wetu ili wafanye kazi kwa weledi. Anafika Mkuu wa Mkoa anasema, eti sasa hivi daktari ni marufuku kumwekea drip mgonjwa kabla hujampima. Sasa Mkuu wa Mkoa amesomea wapi kazi hiyo?

MBUNGE FULANI: Na mgonjwa kama anaharisha?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Ndiyo, kama mgonjwa anaharisha daktari si ndiyo anajua kazi yake? Leo Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya anajua utaratibu huo, pamoja na kwamba mnasema Chama cha Mapinduzi, ina maana chama ndiyo kinatuma watu wawaambie hivyo madaktari? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni mambo ambayo kama Bunge lazima tukemee, madaktari wetu walindwe, waheshimiwe, wasikoselewe kwenye mikutano ya hadhara. Hii Mkuu wa Mkoa wa Iringa anisikie, imeleta shida safari hii, ziara yake ya Iringa mpya imekuwa matatizo katika Mkoa wa Iringa, hatukuwa na mazoea haya. Najua Mheshimiwa Kabati ameogopa kusema kwa sababu ya mambo ya ki- protocal lakini Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ametuletea tatizo katika Mkoa wetu wa Iringa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze mambo mawili. Jambo la kwanza ni kuhusu kilimo cha parachichi; naomba niishauri Serikali, Nyanda za Juu, hasa Iringa ni corridor ya parachichi duniani na naomba tafiti zilizofanyika wahakikishe wanazifanyia kazi kubwa kwa ajili ya kuhakikisha wakazi wa Iringa na maeneo mengine wananufaika na zao la parachichi. Naomba sana wasifanye business as usual kwa sababu wanatumia methods zilezile, ulimwengu ume-change, wanafikiri vilevile, change namna ya kufikiri kulingana na ulimwengu unavyokwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, katika kitabu cha hotuba yetu ukurasa wa 24 tumezungumza jinsi ambavyo Mheshimiwa Profesa Kabudi na Gavana wa Benki walisimamia kwenye kuandika ule mkataba wa wanunuzi wa korosho. Profesa ni authority, profesa ni mtu ambaye inatarajiwa kwamba anajua mambo mengi, anajua namna ya kufikiri na Mheshimiwa Rais katika Serikali ya Awamu ya Tano amefanya kazi nzuri sana ya kuwaleta wasomi, Maprofesa na Madaktari, tunategemea Madaktari na Maprofesa wanapofanya maamuzi lazima wanakuwa wamepanuka sana ili wasilipotoshe Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo la kutia aibu mahali ambapo mtu kama Mheshimiwa Profesa Kabudi amekaa, wamekuja na ile kampuni ya kitapeli kabisa, Rais amewaamini kampuni ya kihuni wanalitangazia Taifa kwamba kila kitu kitakuwa safi, korosho itanunuliwa, halafu korosho haijanunuliwa. Hili ni jambo la aibu, hatuwezi kulifumbua macho, lazima Mheshimiwa Profesa Kabudi ajiuzulu kwa kulipotosha Taifa. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni jambo la aibu sana hili. (Makofi)

MWENYEKITI: Hebu ngoja. Mheshimiwa Mchungaji Msigwa, wewe ni term yako ya ngapi Bungeni?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Naam?

MWENYEKITI: Muhula wa ngapi huu?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Wa pili.

MWENYEKITI: Ahaa, kwa hiyo unajua sana mambo.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Ndiyo.

MWENYEKITI: Haya.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimem-single out Mheshimiwa Profesa Kabudi alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria, kwa hiyo we expected kwamba yeye angetu-guide na angem-lead Rais katika njia iliyo sahihi, he was responsible for that Ministry, hatuwezi kum-spare. Amelipeleka Taifa kwenye sintofahamu kwa ku-mislead nchi, ni wajibu wake kusimama hapa na kusema kitu gani kilifanya aingie kwenye mkataba wa hovyo na nchi hii, lazima… (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu Utaratibu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mchungaji Msigwa nimeshaliamulia, sasa unarudi hukohuko, usinilazimishe niangukie kwenye Kanuni ya 73. Haya.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwamba Serikali imekubali kwamba inawadanganya wananchi wa Mtwara na korosho, ina- mislead Taifa la Tanzania na kuwapa ahadi hewa… (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: …kwa sababu inaingia kwenye mikataba ambayo haitekelezeki.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ninayoijenga hapa, Serikali ina wajibu wa welfare za wananchi. Serikali imesababisha tuko foreign, forex imeshuka kwa sababu ya mipango ya hovyo ya Serikali kuhusiana na korosho. For the first time ninyi Mawaziri, amesema hapa Kaimu Kiongozi, walimshauri Rais wakaamua kutumia Jeshi kuchukua korosho, anakuja Waziri hapa anasema eti anayeleta mkataba amekuja na ndege, anashangaa na ndege, mbona ana caravan hapa, what is ndege? Wanamshangaa eti kwa sababu amekuja na ndege ndiyo wanaingia kwenye chaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii Serikali lazima wasimame waombe radhi kwa wananchi, mnaharibu kilimo, wamewa- cripple wananchi kwa sababu ya mikataba ya hovyo, watu wengine kule Mtwara wameshindwa kupeleka watoto wao shule. Walikusanya korosho zao halafu wanasema hapa tuwapigie makofi. Mawaziri waliohusika na Waziri wa Katiba anatakiwa a-step down, amei-mislead nchi. Kuna wengine wamekufa watoto wao wameshindwa kupeleka shule halafu wanasema hapa tusiseme, tumekuja kufanya nini hapa, shame on you Government. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, binafsi nianze kwa kuipongeza kwa sehemu Kamati kwa kazi nzuri ambayo wameifanya, na kazi kubwa ya Kamati hii, hii ni oversight committee, hasa baada ya kupata ripoti ya CAG ambaye ndio jicho letu la Bunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pamoja na mambo mengi ambayo mmetupa Kamati Mwenyekiti, kuna mambo mengi ya msingi ambayo sisi kama Wabunge na kama wasimamizi wa rasilimali za Taifa hili tunataka tuyapate majibu kama Wabunge. Na wajibu wetu sisi kama Bunge ni kuisimamia Serikali na kwa bahati nzuri sana Serikali hii imejipambanua sana kwamba haitaki fedha zitumiwe hovyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nina maswali kadhaa ambayo ninamini kwamba Kamati yako haijatutendea haki kama Wabunge. Baada ya Ripoti ya CAG kuna mambo mengi sana ambayo CAG aliyaona. Kwa mfano kwenye ripoti yako sijaona masuala ya flow meter; ripoti ya CAG ilionesha kwamba haifanyi kazi, na Mheshimiwa Rais pamoja na Waziri Mkuu wamekwenda mara kwa mara na inaonekana flow meter hii kule bandarini haifanyi kazi; kwa nini kwenye Kamati yako hujatupa ripoti hii tukaweza kujua kuna kitu gani kinachoendelea?

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Ripoti ya CAG, CAG alihoji masuala ya uniform za polisi, na kwenye ripoti yake CAG alisema kukosekana kwa nyaraka za kuthibitisha uletaji wa mzigo, niliomba hati ya kupokelea shehena ya mizigo bandarini ukurasa wa 311, Mheshimiwa Waziri aliyekuwa Waziri wa Mambo ya ndani hapa aliweka rehani mpaka Ubunge wake. Nilitegemea Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati hii, hizo gharama za ripoti na ile sintofahamu…

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu utaratibu.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana. Ninashangaa kwa kweli kuona Serikali inashindwa kujibu hoja, hizi hoja ni kitabu cha Serikali, tunafanya kazi ya Umma, nikushukuru kwa kutoa uamuzi ambao ni sahihi kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja yangu niliyokuwa naizungumza ni kwamba haya ni mambo ya msingi, nimezungumza hii flow meter ilionekana kuna wizi mkubwa, na Rais alizungumza. Kwa nini Kamati haijatuambia Wabunge tuone huo wizi umedhibitiwa vipi?

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nilienda kwenye hoja nyingine kuhusiana na CAG alidai documents zinazohoji nani aliagiza sare za polisi. Hizo bilioni 16 zinalipwaje, mlipwaji ni nani, tenda ilikuaje? Ninahoji ni kwa nini Kamati – bilioni 16 siyo hela ndogo – kwa nini Kamati haijaleta hapa tuone huyo mtu alilipwajelipwaje kwa sababu CAG alionesha haya mambo. Haya mambo ni kama yanapotea gizani, ni mambo ya msingi ambayo Serikali inataka tutunze hela na ni kweli ni haki yetu kusimamia hela, haya ni mambo ya msingi hayahitaji kufichwa. Watanzania wanapaswa wajue, Bunge hili linapaswa lijue.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Lugola alisema ataweka rehani Ubunge wake hapa. Mwenyekiti naomba atuambie hivyo vitu vyote CAG alivyovidai vimepatikana? Na juzi hapa tumesikia Rais anasema amelipwa sijui bilioni 10; amelipwalipwaje? The Government moves on paper, amelipwaje huyu mtu, kwa namna gani? Kamati haijatuletea.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, kwenye masuala ya TPA kule bandarini; TPA inataka kuvunja mkataba wakati mkandarasi yule ameshalipwa zaidi ya asilimia 70 na walimleta mtaalam kutoka nje asimamie, ni kwa nini wanataka kuvunja mkataba? Tunataka tujue haya mambo ili Bunge tusimamie vizuri Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine, watu wa NIDA; CAG alishasema vile vifaa vya BVR havifanyi kazi, vilikuwa sio compatible na windows ili vitoe vitambulisho vya uraia pamoja na vya kupigia kura lakini inasemekana sasa hivi vile vitu havifanyi kazi na wameagiza vitu vingine tena vipya hivi vingine vyote vinatupwa nje. Hizi ni hela za Watanzania tunataka tujue haya mambo yanakwendaje, yanafanyikaje haya mambo kienyejikienyeji na hili ni Bunge na Mheshimiwa Rais amesema watu wanafanya mikataba bila Bunge kujua. Haya masuala sisi hatujui yanafanyikaje? Masuala ya e-passport tulizungumza sana hapa Bungeni mauzo ya passport wakati mwingine yanaonekana kwamba kuna faida inaonekana. Hii passport chanzo chake kilikuwaje, tuliingia mkataba na nani? Tulitumia kiasi gani? Tunalipaje, tender ilikuwaje? Passport moja gharama yake ikoje? Sasa litakuwa Bunge la aina gani ambalo haliwezi kuhoji mambo kama haya.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati ni oversight committee ambayo inapaswa isimamie pesa za walipa kodi, wana wajibu wa kutuambia mambo makubwa kama haya ndani ya Bunge lazima tuyajadili, hatuwezi tukawa tunashughulika na mambo ya Simba na Yanga hapa tunaacha mambo ya msingi haya ya hela ya wananchi. Hatukuja kwenye Simba na Yanga pamoja na kwamba mimi mpenzi wa Simba. Tumekuja hapa kuhakikisha tunasimamia kodi za wananchi, hela ya wananchi, si ndiyo mtazamo wa Mheshimiwa Rais kwamba hela ya nchi isiibiwe, haya mambo makubwa Kamati inaweza kuachaje ili yasijadiliwe kwa upana wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ningeomba Mwenyekiti anapokuja kuhitimisha hapa, kuna mambo ya msingi ambayo ni lazima Bunge lijue, hizi ni hela nyingi, mabilioni ya Watanzania ambayo yanapaswa tuyajadili kwa kina ili Bunge lichukue nafasi yake. Hii mikataba mingi imeenda kimyakimya, kiholela holela Wabunge tunapita tu tunaondoka na sasa hivi tunamaliza muda wetu, tukienda kuulizwa kwa wananchi tutaenda kusema nini. Naomba Mheshimiwa Mwenyekiti atakaposimama hapa atuambie kwa nini kwenye ripoti yao hawajatuambia masuala ya e-passport, masuala ya NIDA, masuala ya nguo za Polisi; na nasikia kuna baadhi walienda wakachungulia tu watuambie walipata hizo documents, walienda kuchungulia tu makontena, kama walioneshwa mlangoni tu kule ndani labda kulikuwa na baiskeli tutajuaje sisi, kama walidanganywa zimetoka China inasemekana zimetengenezwa hapa hapa Tanzania, tunataka hayo mambo tujue, ndiyo wajibu wa oversight committee. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ningeomba Mheshimiwa hoja yangu ni kwamba pamoja na kazi nzuri waliyoifanya na mambo mengine, lakini kuna mambo ya msingi ambayo Taifa la Watanzania wanataka wayajue na yapatiwe majibu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Kulitangaza Jiji la Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi wa Mwaka 2018
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru na mimi kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, nianze kama alivyosema Mheshimiwa Saleh, dhana nzima ya kuifanya Dodoma iwe Makao Makuu ni nzuri na hatuwezi kusema ni jambo baya. Hata hivyo, kuna tofauti kubwa sana kati ya kufanya jambo zuri na jambo sahihi. Linaweza likawa ni jambo zuri lakini lisiwe jambo sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi kama Wabunge hapa kazi yetu kubwa ni kusimamia kodi za wananchi. Kwa hiyo, masuala
mengi ambayo Serikali inatuletea mezani ni wajibu wetu kutafakari kwa pamoja kama Taifa kwamba hili suala tunalokwenda kulifanya is it economical? Ni suala la kiuchumi, lina tija gani kwa wananchi wetu, ni priority, lilikuwa limepangwa? Sasa tunaangalia kile ambacho tunacho kwenye hazina kama Taifa, tunaangalia vipaumbele vyetu ni vipi, vitaleta tija gani, sisi kama Wabunge ni wajibu wetu kuchekecha.

Mheshimiwa Spika, tukiwa wakweli na tukijitathmini kiundani kweli kweli, amezungumza Mheshimiwa Saleh hapa wengi wanakuja na hoja kwamba Mwalimu Nyerere alishasema, Mwalimu Nyerere kasema mambo mengi sana, alishawahi hata kusema kwamba chama kinachofaa kutawala baada ya CCM ni CHADEMA, hilo mbona hamlitekelezi? Hatuwezi tukasema mambo yote aliyosema Mwalimu Nyerere lazima tuyatekeleze hapa lakini mnachukua yale machache aliyosema Nyerere mnapindisha msumeno. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nachotaka kusema wajibu wetu ni kutunza kodi ya wananchi. Nchi hii ina matatizo mengi na makubwa sana. Ukiangalia kwa mfano kwenye masuala ya afya kuna matatizo makubwa sana, policy ya nchi yenu imezungumza mambo mengi sana kuhusu kuboresha afya ya mama na mtoto, tuna matatizo ya maji na kuna mambo makubwa ya msingi. Sasa tukipima kama Wabunge tukitafakari hapa wote tukiwa na sober mind, tuna-reason, tunakuja na evidence kwa sababu argument hapa ni kuhamia Dodoma kama tuna reasoning ukipima mizani is this our priority? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tulipoingia Bunge hili, suala hili halikuwa kwenye Mpango wa nchi wa Miaka Mitano, it was unplanned; halikuwa kwenye mpango wa mwaka mmoja, it was unbudgeted. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa leo tunakuja na…

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, nimeomba haya masuala tuyajadili tukiwa na sober mind. It’s not about Chama cha Mapinduzi au CHADEMA, tunazungumzia kuhusu masuala ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, labda nikurudishe kidogo; simple understanding, mkiwa na argument yoyote kuna mambo matatu ya kuzingatia ambayo ni premises, inference na conclusion. Premises tuliyojenga hapa tunazungumzia kuhamia Dodoma lakini kwenye inference tulete hoja, tuwe na argument za hoja, tuwe na mifano, kwa nini tunahamia Dodoma na kwa nini tusihamie Dodoma?

Mheshimiwa Spika, mimi najenga hoja, ukiniambia hapa Ilani ya Chama cha Mapinduzi, hatutekelezi Ilani ya Chama cha Mapinduzi hapa, tunatekeleza Mpango wa Taifa. Tukishamaliza uchaguzi na kuja humu ndani tunaubadilisha unakuwa Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano na inakuwa Mpango wa Taifa wa mwaka mmoja mmoja; sasa Chama cha Mapinduzi kinatoka wapi hapa, vinginevyo si mngejadili kwenye caucus muamue wenyewe? Mimi nazungumzia Mpango wa Miaka Mitano wa Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa nimezungumza tuwe na sober mind, tuangalie is this our priority? Siku moja niliwahi kusema hapa, Botha kwenye hotuba yake maarufu aliwahi kusema, an African person can only plan for one year. Nimezungumza hiki kitu, tumekuja hapa it was unplanned; ilikuwa-planned wapi, kwenye Mpango wa Miaka Mitano iko wapi?

Mheshimiwa Spika, usi- spin. Sijasema namuunga mkono Botha lakini nasema anaweza akatu-prove right kama tunafanya makosa yale yale. Kwa sababu hii nchi haijapata uhuru jana ndugu zangu, hii siyo Sudan ya Kusini ambayo wanahangaika kutafuta majengo. Leo hata wewe mwenyewe Mheshimiwa Jenista ofisi yako ni mgogoro hapa Dodoma. Ofisi zote hapa ni mgogoro, ukienda kwa mfano Zimamoto kwa Wizara ya Mambo ya Ndani kuna majengo makubwa tulikuwa tume- plan kule Dar es Salaam, yalikuwa yanainuka, sasa hivi tumesimamisha tunakuja hapa Dodoma. Narudia kusema, it was unplanned, unprepared, unbudgeted, uneconomical. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumekuja hapa tunataka ku- popularize tu, tunatafuta political mileages kuleta hapa lakini haya mambo tukikaa chini, nimezungumza tuna matatizo makubwa sana ya vituo vya afya, vifo vya akina mama na watoto, hatujayaweka mbele; magonjwa mengi yanayosababishwa na…

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, haya ni matatizo ya kukimbia shule. Nimezungumza mambo ya inference, nadhani haelewi hata ninaposema inference ni nini. Anazungumzia vituo 200, nchi hii tunahitaji vituo 4,600 wewe unazungumzia vituo 200. Hizo data gani anazoniambia?

Mheshimiwa Spika, tunahitaji vituo 4,600 na magonjwa mengi tunatumia pesa nyingi kwenye dawa yako related na maji, watu wanakunywa maji machafu. Dodoma hii inaongoza kwa kutokuwa na maji, sasa priority ni kuhamia Dodoma, tuseme tu tumehamia Dodoma au tunapanga hela zetu chache tulizonazo tuangalie priority yetu ni ipi, tufanye nini? Watoto hawana vifaa madarasani, hawana madarasa; is it our priority? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali haijatuambia hapa how much money you are using moving from Dar es Salaam to here, halafu tunakuja hapa tushangilie tu. Huu si wajibu wa Bunge, Bunge siyo rubber stamp, we are here to reason, tuje na evidence. Njooni na hoja zenu kwamba faida ya kuhamia Dodoma ni hii, tukikaa Dar es Salaam ni hii, tusipokwenda Dodoma tutapata hasara moja, mbili, tatu nne, tukikaa Dar es Salaam tutapata hasara moja, mbili, tatu nne. Mnakuja hapa na siasa mnatuambia Ilani ya Chama cha Mapinduzi, who cares? Inatusaidia nini hapa? We are all in the same boat. Chama cha Mapinduzi kikiwa dhaifu wote tunakuwa dhaifu hapa, mnahitaji strong political party ili muwe na nguvu, sasa mnakaa mnajilegeza hapa mnapiga makofi tu, mnataka tusi-reason? Mahali hapa ni pa ku-reason. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa bahati mbaya duniani kote, ndiyo maana mihimili mitatu ilianzishwa. Mtawala, Serikali yoyote huwa inataka Bunge liwe rubber stamping, lisijadili, watu wapige makofi, kwa sababu mtawala yeyote duniani anataka mambo yake yawe mteremko. Bunge lipo kwa ajili ya ku-balance na tuko hapa kusema Serikali mmeleta mpango huu, huu mpango unatia hasara kwa Taifa, haya lazima tujadiliane hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa tunakuja hapa mnaanza kusema Serikali, Ilani ukurasa, mimi I haven’t even read your Ilani. Tulikuja tukajadili kama Wabunge hapa tumeondoka na Mpango wa Miaka Mitano wa nchi, hiyo ndiyo dira ya nchi yetu. Hivi vitu havikuwa planned, havipo, tukiwaambia mnashindwa kutekeleza hayo mambo mnaanza kusema tunahama hoja. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, binafsi hata sijamuelewa. Nachoweza kusema kwa kifupi kwa sababu mmekuwa mnani-interrupt sana, it is very dangerous to do a good thing at the expense of the right thing. Kama ninyi mnaona kuhamia Dodoma ina tija zaidi kuliko kuboresha vituo vya afya, kuliko kuwa na maji ya kutosha katika nchi hii ili tupunguze magonjwa, wananchi watatu-judge na historia itakuja kuzungumza. Nimesema kuja Dodoma ni jambo zuri lakini it was unplanned, it is not economical, we were not prepared, it is unbudgeted.
Muswada wa Sheria ya Serikali Mtandao wa Mwaka 2019
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nianze kwa kusema, dhana nzima ya Serikali Mtandao ni jambo jema ambalo kimsingi litarahisisha mambo mengi katika nchi yetu. Niseme tu kwamba Muswada wenyewe kwa mtazamo wa Kambi na mimi vilevile nauona ni Muswada njiti (premature). Nasema ni premature kwa sababu hizi ntakazozieleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, picha halisi ukitaka kujua access ya internet katika nchi yetu ni hata leo tulivyoanza kuletewa Order Paper kwenye Simu Janja mikononi mwetu. Wabunge wengi hapa wamehangaika hawajapata hii Order Paper. Hii inaonyesha ndiyo picha halisi ya namna gani ndiyo tunaweza tukawafikia watu huko nje.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiwa wakweli, Watanzania wengi wameanza kuziona computer wanavyofika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Wanaanza darasa la kwanza, wanasoma shule za mwanzoni computer hawazijui, kwa hiyo uwezo wa kutumia computer na kujua computer katika nchi yetu uko kwa kiwango cha chini sana. Serikali masuala ya umeme ndiyo tunahangaika sasa hivi na REA lakini elimu ya computer bado haijawafikia Watanzania walio wengi na hata hizo computer ambazo ziko katika Ofisi zetu za Serikali, Watendaji wengi wa Serikali wanajua kutumia program za Word na Excel kwa hiyo computer zenyewe tulizonazo ndani ya Ofisi zetu za Serikali hatuja-utilize kiasi cha kutosha. Kwa mtazamo wangu tumeanza na secondary tumeacha primary tuki-assume kwamba tukimaliza secondary huku chini tutaweza kufanyakazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Bill Gate wakati anaanzisha Microsoft mwaka 1975 walipingana na IBM. IBM waliamini kwamba dunia inahitaji computer tano lakini Bill Gate alisema nataka kila nyumba ya mtu duniani awe na computer. Ni miaka 43 sasa hivi imepita leo ukiangalia ni Watanzania wangapi wana Simu Janja, kwa maana kwamba hatukuweza ku-catch wave dunia inakwenda wapi. Wataalam wanasema “if you want to be a head you got to know things that other people don’t know”, lazima uvijue vitu ambavyo watu hawavijui ndipo utakwenda kwenye mafanikio. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Serikali tumekuwa tuna-slow halafu tuna-assume kwamba tukijua haya mambo ya juu tukaacha mambo ya primary mambo yatakwenda vizuri. CHADEMA tumefanya ni msingi, tumezunguka karibu Kata nzima, kuna Kata zingine kumpata mtu mwenye smartphone hayupo na ukimpata ni wa CHADEMA naye amekosa ajira amerudi kijijini! How are we going to implement this? Huu ni ukweli tunataka tusaidie.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda kwenye Serikali yetu mpaka leo kuna watu wanaondoka na Ma-file hapa anatoka nalo File Dodoma anampelekea Katibu Mkuu Dar es Salaam akasaini, sasa hii tuna-implement vipi? Wakati hata hizi organization binafsi zilishaacha hayo mambo muda mrefu sisi kama Serikali tunasuasua.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili; kwenye faida za huyu Muswada ambazo nakubaliana nazo, mmesema “transparency, accessibility, efficiency na cost” kwamba tunapunguza cost, sasa kama ni wakweli tunataka tupunguze cost kwanini hamja-incorporate Sheria ya Uchaguzi humu ndani tupunguze cost ili kuwe na transparency, kuwe na accessibility, kuwe na efficiency, ili haya mambo yote ya uchaguzi tuyaingize humu ndani mbona hamjayafanya? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hii sheria ni nzuri, inatamanisha lakini utekelezaji wake ni mgumu kweli. Hatujaambiwa hapa uwezekano wa internet, Watanzania wanaofikiwa na internet wangapi, yaani internet itafika wapi kama nilivyosema umeme haupo ni kwa kiasi gani lakini inaonyesha ni less than five percent! Hizi WiFi zinafika wapi, less than five percent tunawafikia sasa tunakuja na huu Muswada, ndiyo maana nimesema Muswada huu ni njiti pre- mature pamoja na kwamba ni mzuri na dhana nzima mimi naiunga mkono. (Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, Muswada huu vilevile Msemaji wa Kambi ya Upinzani amezungumza jinsi ambavyo Tanzania tulijitoa kwenye OGP sasa kwenye Muswada hatujabadilisha hizi sheria ambazo tulijitoa, hatujasema lakini sasa hapa tutashirikianaje na Kimataifa. Kuna watu watafanya biashara tutaingiliana nao lakini hatujasema ni namna gani baada ya kujitoa katika mambo ya uwazi tutalinganishaje. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili ni suala la Miswada ambayo tuliipitisha hapa na tulilalamika hizi Sheria haziendani na ulimwengu unavyokwenda, masuala ya Cybercrime Act kwa mfano, masuala ya Statistics Act, masuala ya Media Service Act, haya mambo yote yanaingiliana na Muswada huu.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Serikali imeuleta Muswada ambao ni pre-mature, tulitakiwa tujiandae, tujipange vizuri, tuwe na weledi wa kutosha, watoto wetu tuwafundishe. Wenzetu Rwanda walianza wakafundisha kwanza watoto mashuleni, watu wakawa na weledi wa computer, wakajifunza wanapokuja kwenye internet na kutengeneza e-Government kinakuwa ni kitu ambacho kinawezekana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mliahidi wakati wa uchaguzi kwamba mtaleta computer za Walimu hamjaleta mpaka leo. Mfano mzuri kuna Halmashauri moja huko Moshi imejiongeza inataka kununua iPad kwa ajili ya Madiwani ili waingie kwenye hiki tunachokifanya na hii imefanyiwa siasa haiwezekani. Kwa hiyo ni kwamba mlikuwa hamjajipanga vizuri, mmeuleta huu Muswada pre-mature ningeomba Mheshimiwa Waziri tafakari vizuri, dhana nzima ni nzuri tunaunga mkono lakini tumeanza mambo ya secondary tumeacha mambo ya primary.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana. (Makofi/ Kicheko)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali (Na.8) wa Mwaka 2019 (Toleo la Kiingereza)
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Mimi nataka nizungumzie kifungu cha 31 cha muswada kinarekebisha kifungu cha 190(1) cha sheria mama kinachotaka mtu akitaka kuishtaki Halmashauri (Local Government), badala ya kutoa notice ya siku 30 atoe notice ya siku 90.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimekuwa nikijiuliza swali Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu duniani kote sasa hivi ulimwengu unataka sheria ambazo ni rafiki kwa raia sio kandamizaji na sheria zilivyotungwa zinatungwa lazima zi-relate na uchumi. Sheria kama hii ni sheria ambayo inataka raia waogope Serikali, waone ni dudu fulani sio la kuliuliza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kukwepa jinsi ambavyo wananchi wana-interact na Serikali yao. Ukienda kwenye Local Government kule kuna watu wanazika, watu wanafanya biashara, wanaiuzia Local Government, wakandarasi wanafanya shughuli zao. Sasa Serikali mara nyingi imeshindwa kulipa fedha kwa mfano watu wanaidai Serikali. Sasa badala ya kupunguza muda namna ya hawa watu kupata haki zao Serikali inaongeza muda zaidi kuwapa ugumu hawa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, raia wengi wana madeni, wamekopa benki, wanataka wafanye biashara zao, uchumi ukue, Serikali inaweka mazingira magumu ili hawa watu wasipate haki zao. Ulimwengu wa leo unataka vitu vinavyokwenda haraka haraka.

Mimi sielewi Mwanasheria Mkuu hii sheria unayotuletea mabadiliko haya yanaturudisha nyuma, tunaenda backward kimsingi na nakumbuka hapa mlipoleta Sheria ya Takwimu ilikuwa sio computable kimataifa ndio maana mkabanwa tena mkaja mkairudisha hapa. Ni sawa na sheria hii sasa katika ulimwengu wa leo wa kiuchumi mnapowabana hawa watu maana yake mnawatengenezea mazingira magumu. Mtanzania wa kawaida hakwepi kui-interact na Halmashauri yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ili wawekezaji waje katika nchi, ili watu wafanye biashara lazima waone kwamba kuna urahisi wa kupata haki zao na kwa bahati mbaya katika nchi hii mtu akiipeleka Serikali mahakamani anaonekana sio mzalendo na ndio maana mnaweka hizi sheria nzito ili mtu aonekane kwamba haieshimu Serikali, mnaweka mazingira magumu siku 90, lakini ukienda hata kwenye Serikali Kuu mwanzoni walikuwa wameweka zile siku 90 Mheshimiwa Chenge utakubaliana na mimi kabla ya hapo ilikuwa lazima uripoti/utoe taarifa kwa Waziri. Baadaye mkabadilisha kwa sababu mazingira hayo yalikuwa magumu kwamba kwa nini mtoe ripoti kwa Waziri ili kuishtaki Serikali lakini bado sababu nyingine State Attorney walikuwa wachache sasa hivi hawa State Attorney wako kila mahali kwa nini tunaweka mlolongo huu wa kuongeza shida kwa wananchi kuishtaki Serikali yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kibaya zaidi hiyo Local Government ikitaka kumshtaki mtu binafsi kesho tu inamshtaki, lakini Serikali inataka ipewe muda wa siku 90 huu ni ukandamizaji na ukandamizaji ambao unawaonea raia wa kawaida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi hii sio monarchy, tukumbuke dunia inaenda mbele, dunia hairudi nyuma, dunia imekuwa ikikua ikipevuka hii nchi sio monarchy. Wakati wa utawala wa kifalme mfalme hata watu wanakuwa ni mali yake, mfalme anataka watu wamuogope, hii ni republic kwenye republic kuna liberty. Ukisoma Thomas Jefferson anasema; “When the people fear the Government there is tairan when the Government fears the people there is liberty.” Ulimwengu wa leo tunazungumzia liberty unapokuwa na liberty maana yake watu wanafanya kazi kwa raha, kwa haki, bila uonevu na kama kumetokea dispute waone kuna uharaka wa kwenda kupata haki zao na ndio maana kama haki zao hazipatikani kwa urahisi watu huwa wanaamua kuchoma watu moto, watu wanachukua sheria mikononi kama vyombo vya haki havitendi haki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mnapotoa kutoka siku 30 kupeleka siku 90 maana yake mnaweka mazingira magumu ya watu kudai haki zao na bado hata kama hizi msingeweka Serikali bado ina nafasi ukipeleka hizo 90 bado ukienda mahakamani kama hujajiandaa unaweza ukamwomba Jaji kwamba akuongezee muda na bado unapewa siku 21, ukipewa siku 21 tena anakupa muda mwingine kwa nini tunaweka mazingira magumu ya namna hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini linalofanana na hili ni hili la Chama cha Wanasheria; pamoja na maelezo mazuri ambayo yanazungumzwa sio siri Serikali mnataka kuwadhibiti wanasheria ambao hawa ni Maafisa wa Mahakama ambao wanatakiwa wasaidie wananchi kujua haki zao kuna ubaya gani wananchi wakijua haki zao, wanapojua haki zao wananchi wanaweza kuiadabisha Serikali na maana yake watumishi wa umma wanakuwa na nidhamu kwa wananchi wao wanafuata taratibu, kanuni na sheria tulizojiwekea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawahitaji hawa wanasheria wasiingiliwe katika mambo yao. Kwa nini tunataka kuwabana, kwa nini tunataka kuwaminya? Tunataka kuwaminya kwa sababu tunataka Serikali iwe ni lidude fulani linaloogopwa, linalotisha ambalo… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Msigwa.
Muswada wa Sheria ya Usuluhishi wa Mwaka 2020 (Toleo la Kiingereza)
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru, na mimi nitoe mchango wangu kidogo kuhusiana na suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, takwimu zinaonyesha kwamba afrika inachangia zaidi ya asilimia 40 ya migogoro duniani lakini wataalamu wa kusuluhisha migogoro hii wako Ulaya. Kwa bahati mbaya sana sheria hii ilitungwa tangu wakati wa mkoloni na ina zaidi ya miaka 85 imekuwepo hapa nchini. Wenzangu wamezungumza hapa kumekuwa na gap kubwa sana la mabadiliko dunia ime-change kwa kiwango kikubwa; na kwa bahati mbaya sana Serikali imekuwa ikikaa kimya kuhusiana na suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu nalotaka kujiuliza, ni kwa nini Serikali ina tabia ya kuleta mabadiliko kama haya kwa dharura? na tumepata somo ambalo mara ya mwisho wakati zinaletwa hizi sera za madini kwa mbwembwe zililetwa kwa mbwembwe na vigelegele humu ndani. Lisu alizungumza sana hapa sisi ni member wa Miga hayo mambo mnayoyafanya hayatakwenda kufanya kazi; humu ndani watu wote mlituzomea wengine wakasema tulikuwa Morena kupokea hela za mabeberu. Leo mmeleta amendment hizi mnataka ku-fit in kwa sababu wamewa- squeeze hao mabeberu wamewaweka kwenye kona ambao mwanzoni mlisema sisi tunatumiwa nao. Sasa mnakuja kwa mgongo wa nyuma wenzangu wamesema kichaka, mnakuja kwa mbwembwe nyingi kwa muswada wa dharura tena ule ule; ni kwa nini hampendi kusikia?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye west minister parliament role ya upinzani ni kuongea maovu mliyonayo ambayo ninyi kwenye chama chenu hamwezi kuzungumza kwa sababu mnaogopana; kwa hiyo sisi hapa tuko kuwasaidia pengine mnamwogopa mtu kusema sisi hapa tunasema. Sasa mnatuminya tusiseme hamuwezi kurekebisha wakija mabeberu kuwabana tena mnarudi hapa. Wazungu wanasema you have thrown in the toe; yaani mmeona kwamba hii haifanyi kazi sasa wenzenu tulijua three years back, sasa nani anafaa kuendesha nchi hii? We knew this three years back na ninyi mko kwenye role mnashindwa kuona vitu vidogo vidogo kama hivi. Ninachoweza kusema muswada huu mnajaribu kutoroka, mna-justify kwamba sheria na mambo mliyotuletea hapa hayafanyi kazi tena pamoja na kwamba mlitunga kwa mbwembwe nyingi mwaka 2017.

Mheshimiwa Naibu Spika, mmegundua kwamba miswada na sheria mlizozileta hapa zimeshindwa kuzuia arbitration kimataifa, yaani Tanzania pamoja na miswada mliyoleta bado tunashitakiwa kimataifa na inatuletea shida. Kwa hiyo mnakuja kwa mlango wa nyuma ili muondoe aibu mliyokuwa nayo. Hatujauliza wadau hii inaonyesha kwamba you‟re not visionary viongozi wazuri wanakuwa proactive yaani hamuangalii mbele mpaka mgonge ukuta ndio mnarudi mnatakiwa kuona mapema. Mara nyingi tumesema kwa nia nzuri hata masuala ya kusema sijui kifungu kiondoke mnafanya makosa yale yale ya jinsi tulivyonunua ndege.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumenunua ndege kubwa hapa marubabi hawana uzoevu wa kutosha mlilazimisha ndege kubwa kutembea nchini ili waongezewe millage wakubalike kimataifa how do we do that tunaendeshaje nchi kwa hivyo? Yaani tunaanza na kufanya mambo kabla ya ku-plan na kujiandaa. Tukisema hivi, tuna nia nzuri, tunaishauri nchi. Mlianzisha wakaanza kuruka kwenda Mwanza, Bombadier mnairusha ili milleage ziongezeke, wa-fit Kimataifa kwamba wanaweza kuendesha ndege, ndivyo mnavyofanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mmeenda kujifungia huko, mmeingia mkataba na Barrick, baada ya kuwa-squeeze halafu sasa ndiyo mnakuja kusema tunaleta marekebisho, mnatuona kama sisi hatuelewi. Tunawashauri kwa nia nzuri, achene role ya Upinzani ifanye kazi yake that‟s why we are here! Tulipoingia kwenye mfumo wa vyama vingi, role ya upinzani ni jicho! Sio siri kuna mambo mengine ukiangalia wengi hapa mnajitetea, yaani mko so defensive mkiguswa kidogo mnajificha, hili lisizungumzwe, mtazungumzia wapi, sisi tunawafanya mpumue. Tupeni nafasi hiyo mpumue. Tunajua hata ninyi wenyewe hampumui huko, tupeni nafasi. (Makofi)