MHE. STEPHEN L. BYABATO aliuliza: -
Je, lini Barabara ya Lake Oil - Ijuganyodo hadi Kyamunene itajengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. ZAINAB A. KATIMBA) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/2025 Barabara ya Lake Oil – Ijuganyodo hadi Kyamunene imetengewa shilingi milioni 40 kwa ajili matengenezo ya changarawe urefu wa kilometa 2.078 na ujenzi wa mifereji mita 800. Aidha, mkandarasi wa kazi hiyo ameshapatikana na anatarajiwa kuanza hivi karibuni. Katika mwaka 2025/2026 barabara hiyo pia imewekwa kwenye mpango wa bajeti kwa kutengewa shilingi milioni 33 kwa ajili ya matengenezo ya kiwango cha changarawe urefu wa kilometa mbili ili kukamilisha urefu wa kilometa 4.078.