Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon Salim Mussa Omar (4 total)

MHE. SALIM MUSSA OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Miezi mitatu iliyopita Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi alipokea ndege pale Zanzibar; moja ilikuwa na jina la Tanzanite na nyingine ilikuwa na jina la Zanzibar; na aliahidi kwamba wataongeza miruko hadi Pemba: -

Je, ni lini Wizara hii itasukuma Shirika hili ili kuweza kufika Pemba? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Salim Mussa Omar, Mbunge wa Gando kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekitk, kama Waziri alivyoahidi, ahadi hiyo ipo kwenye utekelezaji. Kwa hiyo, taratibu zote zitakapokamilika, ndege zitaanza kufanya safari kwenda Pemba.Ahsante.
MHE. SALIM MUSSA OMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ya kuweza kuuliza swali la nyongeza. Kumekuwa na malalamiko makubwa ya kukoseshwa fursa ZIC kama fursa inayopatikana na NIC huku Tanzania Bara: -

Je, Serikali inatuhakikishia vipi kwamba kuna mchakato sasa kuweza kuondoa malalamiko haya ili sasa Zanzibar insurance kwa sababu ipo katika mikoa zaidi ya mitano huku Tanzania Bara inaweza ikapewa fursa sawa kuweza kuingia katika miradi mikubwa ya Tanzania Bara?
NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mussa Omar Salim, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye jibu langu la msingi kwamba ZIC ni kampuni kama makampuni mengine. Kazi ya Serikali ni kuhakikisha kwamba inaweka mazingira rafiki ya kiushindani na kuhakikisha kwamba wanaweza kufanya biashara bila kuwa na changamoto yoyote.

Mheshimiwa Naibu Spika, naamini kabisa kwamba Serikali ikishaweka mazingira hayo, basi hata wao watajipima kulingana na mazingira ya kiushindani, kwa sababu kwa mujibu wa Sheria Serikali haiwezi kuingilia biashara ambazo wadau wanaweza kushiriki kwa pamoja. Ahsante.
MHE. SALIM MUSSA OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza kabisa nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali yenye kutia matumaini, lakini nimuulize swali la nyongeza.

Je, haoni kama ipo sababu ya kuweza kuweka kipaumbele au Wizara yake iko tayari kutoa kipaumbele kwa hili jambo ili kuweza kutatuliwa kwa haraka sana, kwa sababu Wapemba wanalaghaiwa na issue hii imekuwa kubwa sana. Sasa hivi ili Wapemba waweze kukupa dua ili uweze kutoboa katika mikeka ijayo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Salim Mussa Omar kwamba Serikali inafahamu na inatambua uzito mkubwa na umuhimu wa kupeleka ndege hiyo Pemba na ndiyo maana imeshaanza mchakato. Alichokifanya ni kutukumbusha, nasi tutajitahidi kuongeza kasi zaidi ili angalau ndugu zetu Wapemba waweze kusafiri kama inavyotakiwa. (Makofi)
MHE. SALIM MUSSA OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Nachukua fursa hii kuwaombea tu kwa Mwenyezi Mungu waweze kutimiza yale ambayo wananchi wana-wish. Nina swali lingine la nyongeza: Je, utaratibu huu ambao unafanyika kwa makampuni katika kujikadiria kodi yao kwa kufanya ukokotoaji wa kile ambacho wanaingiza, ni lini utaenda kwa maduka ya kawaida ya retails? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nina ushauri kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa nini sasa kutokana na sintofahamu kubwa iliyojitokeza ndani ya nchi yetu baina ya mlipa kodi na mtoza kodi, kwa nini sasa usiwepo mfumo wa kutengeneza activities za kimichezo baina yao hata kutengeneza ligi baina ya wafanyabiashara pamoja na TRA na viwanja tunavyo pale Kariakoo? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge. Kabla ya kujibu naomba nimpongeze sana kwa namna anavyojitahidi kutetea kampuni changa vile vile na wafanyabiashara wadogo wadogo. Swali lake anasema ni lini? Namwomba tu Mheshimiwa Salim awe na subira, mchakato huu unaendelea kufanywa na Serikali kwa nia safi. Mara tu baada ya kumalizika tutaleta katika Bunge lako tukufu, ahsante. (Makofi)