Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon Kassim Hassan Haji (2 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020
MHE. KASSIM HASSAN HAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote na mimi nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa wingi wa rehema na kutujalia kuwa wazima wa afya njema na kutuwezesha sote kuwa pamoja siku ya leo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili nikushukuru wewe kwa kuweza kunipa nafasi ya kusimama katika Bunge lako tukufu kwa mara ya kwanza, pia nikishukuru chama changu Chama cha Mapinduzi kwa kuweza kunipa nafasi ya kuweza kuwakilisha wa Jimbo la Mwanakerekwe, naishukuru familia yangu pamoja na wananchi wa Jimbo la Mwanakerekwe kwa mashirikiano makubwa wanayonipa na nina wahaidi nitawatumikia Watanzania wote pamoja na wao kwa kuleta maendeleo mapana ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hotuba ya Mheshimiwa Rais ukitizama ukurasa wa 13 ameweka kipaumbele kikubwa katika miaka mitano kuendeleza, kulinda na kudumisha tunu za Taifa letu yaani amani, umoja na mshikamano wa nchi yetu, uhuru wa nchi yetu, pamoja na Muungano na Mapinduzi matukufu ya Zanzibar. Pia kuhahidi mashirikiano na Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi, na kusisitiza kuwa hata kuwa na mzaa kwa yeyote atakayetaka kukatisha uhuru wetu Muungano wetu na Mapinduzi matukufu ya Zanzibar, hali ambayo imefanya mpaka sasa hivi kuunda kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa katika Kisiwa chetu cha Zanzibar na kuleta maendeleo ya uchumi katika Kisiwa cha Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, ukurasa wa 14 wa hotuba hii Mheshimiwa Rais ameonesha kuonesha mashirikiano makubwa ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kuendelea kuleta maendeleo ya pande zote mbili za Muungano na kuahidi kuleta meli nne katika Kisiwa cha Unguja. Hii imekwenda kufanya kugawanya usawa, usawa wa meli nne ziwepo katika Tazania Bara na meli nne zije katika Kisiwa cha Unguja inakwenda kutimiza lengo la sera ya uchumi wa blue.

Mheshimiwa Spika, pia utoawaji tumeona juzi tu utoaji wa hati, utiahaji saini wa hati wa yamakubaliano ya maridhiano katika ujenzi wa bandari kuu ambayo itajengwa na mji wa kisasa katika Kijiji cha Manga Pwani kule Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa katika hotuba yake na mimi nimalizie katika ukurasa 36 niipongeze Serikali kwa kutunga sheria mpya kusimamia na kuendeleza uvuvi wa bahari kuu; hii imekwenda kutuongezea ajira zilizo rasmi na zisizo rasmi kwa vijana wetu ambao watakuwa wanajishughulisha na shughuli hizi na kufanya kwenda kuongeza Pato la Taifa letu la Tanzania, na mimi niunge mkono hoja na kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa mashirikiano yake makubwa ambayo ameyaonesha katika kisiwa chetu cha Zanzibar na kufanya mikataba ambayo inakwenda ili iwe haki, uhuru na sisi kufanya Kisiwa cha Zanzibar kiwe kiwe kinamabadiliko makubwa katika miaka mitano inayokuja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira
MHE. KASSIM HASSAN HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Awali ya yote, nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia uhai na uzima na kutuweka katika Mfungo wa Ramadhan tukiwa wazima na leo kushiriki katika Bunge lako hili Tukufu.

Mheshimiwa Spika, kwenye Ilani ya CCM, ukifungua kifungu cha 226 na 227 na ukurasa wa 276 – 277 inazungumzia mambo ambayo si ya Muungano lakini yanaleta faida katika kutatua changamoto za watu wetu zikishirikiana Serikali zetu mbili; yaani Serikali ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). Kwanza, niipongeze Wizara kwa kutatua baadhi ya changamoto kwa kuunganisha makampuni BRELA na BPRA. Memorandum ambayo wamefanya angalau inasaidia wafanyabiashara wakubwa wenye makampuni; mtu akiwa amesajili biashara yake Zanzibar, basi angalu wakija huku wanakubalika vile vibali vyao nao vinaweza kufanya kazi, niwapongeze kwa hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile, tukiangalia kwenye ZFDA na TBS wamefanya vivyo hivyo kwa kuwasaidia wafanyabiashara wadogo wadogo. Mtu akichukua biashara yake Zanzibar akija nayo Bara, basi nayo inakwenda bila usumbufu na cheti chao kinakubaliwa na jambo hilo linakuwa jema kwa wafanyabishara wetu wadogo wadogo. Niwapongeze kwa hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kidogo kuna shida moja, jambo hili tunaomba liende likafanyike katika TBS na ZBS. Tukizungumzia ISO kwenye standard katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tukienda kwenye codex inayotambulika ni moja tu; inatambulika TBS. Kwa hiyo, ZBS wanashindwa ku-recognize zile ISO ambazo wao wenyewe wanatakiwa waende wakazifanye kama ambazo wanazifanya TBS.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, kitu kimesajiliwa Zanzibar; TBS inatakiwa iwasaidie ZBS angalau kitu kile kikitoka nje ya Tanzania basi na wao kiende kikatambuliwe kiufasaha. Kwa hiyo, watu wetu ambao wanafanya biashara ndogo ndogo Zanzibar wanakosa fursa ya kupeleka bidhaa zao nje kwa sababu tu ya haya mambo madogo ambayo yapo na yanaweza kutatuliwa kwa kufanya memorandum ambazo wenzetu wa ZFDA na TBS walifanya lakini walifanya hao wa BRELA na BPRA. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama kauli yetu ya Muungano ya safari hii inavyosema, “Muungano wetu ni msingi imara katika mapinduzi ya kiuchumi” basi twende tukawasidie wafanyabiashara hao wadogo wadogo na wao waweze angalau kulipata soko la nje ya Tanzania kwa kuweza kufanya biashara zao zikawa zinakwenda na wakiwa wanapata kipato cha mtu mmoja mmoja. Si haya tu na taasisi nyingine ambazo zinakwenda kufanya mambo kama haya ya ushirikiano, basi tuwaombe sana wazifanye hizi memorandum angalau kuwafanya watu hawa wote wawili waweze kufanya biashara sehemu yoyote ambayo itakuwa ipo bila matatizo yoyote. Ahsante sana. (Makofi)