Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Mustafa Mwinyikondo Rajab (1 total)

MHE. MUSTAFA MWINYIKONDO RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninaishukuru Serikali kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kituo hiki kimejengwa kwa muda mrefu hivi sasa na kwa kuwa katika eneo hili kuna wananchi wamezunguka na sasa hivi wameshaanza ujenzi;

Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kufuatana nami kwenda kuhakiki mipaka ya ukubwa wa eneo hili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na napenda kumueleza Mheshimiwa Mbunge kuwa niko tayari. Tutaongozana ili kwenda kutatua tatizo la mipaka lililopo, ahsante sana.