Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to Primary Questions by Hon. Amb. Liberata Rutageruka Mulamula (1 total)

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: -

Je, ni nchi ngapi zimeshafungua Ofisi zao za Ubalozi Jijini Dodoma baada ya zoezi la kuhamisha Makao Makuu ya Serikali Dodoma?
NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Pondeza Mbunge wa Chumbuni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hadi sasa nchi tatu zimeshafungua Ofisi Ndogo za Ubalozi Jijini Dodoma. Nchi hizo ni Uingereza, Ujerumani na China. Hata hivyo, Wizara inaendelea kuzishawishi nchi nyingine kufungua Ofisi zao hapa Jijini Dodoma.

Mheshimiwa Spika, katika hatua nyingine baadhi ya Mashirika ya huduma za jamii na maendeleo ya Umoja wa Mataifa yameshafungua Ofisi zake Jijini Dodoma. Mashirika hayo ni pamoja na UNDP, UNICEF, UN Women, WFP, WHO, UNFPA, FAO, IFAD, IOM, UNAID, UNCDF na UNIDO.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)